Showing posts with label UTAWALA WA JAKAYA KIKWETE. Show all posts
Showing posts with label UTAWALA WA JAKAYA KIKWETE. Show all posts

24 May 2013










HEBU JIULIZE, LINI ULISHUHUDIA HALI KAMA HII IKITOKEA TANZANIA?

BADALA YA KUSAKA CHANZO, OUR DEAR LEADER DOKTA KIKWETE ANADAI "ATAKATA MAPEMBE" YA ANAYESABABISHA VURUGU. WELL, YEYE MWENYEWE NI PEMBE PIA KWANI UTAWALA WAKE UMEZIDI KUISUKUMA TANZANIA YETU KUELEKEA MAHALA KUSIKOFAA: UFISADI UMEKUWA KAMA SEHEMU YA MAISHA YA MTANZANIA, UDINI SIO TU UMEONGEZEKA BALI PIA UMEANZA KUWAFARAKANISHA WATANZANIA HUKU BAADHI YA WENZETU WAKIPOTEZA MAISHA YAO, UHUNI USIOELEZEKA MIONGONI MWA WATU WALIOCHAGULIWA NA KUPEWA DHAMANA YA KUWAKILISHA WATANZANIA (WABUNGE), MGAO WA UMEME USIOISHA LICHA YA AHADI KEDEKEDE KUTOKA KWA KIKWETE...MENGINE ONGEZEA MWENYEWE MSOMAJI.

NASEMA HIVI, IFIKE MAHALA KIKWETE AAMBIWE UKWELI KUWA KAMA KWELI ANA LENGO LA KUKATA PEMBE BASI AJIWEKE KANDO YEYE MWENYEWE KWANI YEYE NDIYE PEMBE KUBWA ZAIDI.

15 Jan 2013


Haya ndio matokeo ya kumkabidhi mtu mbabaishaji kuongoza nchi.Naam,namzungumzia Rais Jakaya Kikwete.Wengi wanaomfahamu vizuri wanatambua kwanini nchi yetu inazidi kupoteza mwelekeo.Majambazi waliojivika joho la uongozi wanazidi kufilisi nchi yetu, Na sasa kila Mtanzania amebebeshwa deni la takriban shilingi laki tano kila mmoja kutokana na zigo zito la misumari la deni la ndani la taifa la shilingi 22,000,000,000,000 (TRILIONI 22). Na hilo ni deni la NDANI TU.

Wakati tunakabiliwa na mzigo huo wa deni hilo kubwa,serikali ya Kikwete imelipa takriban SHILINGI MILIONI 100 kugharamia makazi ya Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt CHARLES TIZEBA (Ni muhimu kujikumbusha Waziri KAMILI wa Uchukuzi ni yule anayetajwa kama kuwa mfano wa viongozi safi wachache ndani ya CCM, Dkt Harrison Mwakyembe).

Uchunguzi wa gazeti la Kiingereza la Guardian umefukua uhuni huo unaotokea katika Hoteli ya Kitalii ya New Africa jijini Dar,ambapo gharama za makazi ya Dkt Tizeba zimeendelea kuchajiwa hata pale anapokuwa nje ya jiji la Dar.

Gharama za malazi katika hoteli hiyo zinaangukia katika makundi matatu: vyumba vya kawaida dola 160 kwa usiku mmoja; vyumba vya klabu dola 180 kwa usiku mmoja; na vyumba maalumu (suites) dola 300 kwa usiku mmoja.Dkt Tizeba anaishi kwenye chumba maalumu (suite) lakini hoteli hiyo imekubali kupunguza gharama hadi dola 250 kwa usiku mmoja.

Hadi kufikia Jumamosi iliyopita (Januari 12, 2013) Naibu Waziri huyo angekuwa ameishi hotelini hapo kwa sangalau siku 247,na hivyo kufanya gharama za malazi yake hotelini hapo kufikia dola 61,750 (sawa na SHILINGI MILIONI 98.8)

Hata hivyo jumla hiyo ni ya malazi na kifungua kinywa tu ( bed and breakfast), ikimaanisha kuwa gharama za jumla zinaweza kuwa kubwa zaidi ikijumlishwa na zile za mlo,ambapo mlo mmoja (buffet) unagaharimu angalau shilinhi 21,000.

Kadhalika,kwa vile Naibu Waziri huyo ana familia,gharama hizo zinaweza kuwa kubwa zaidi.Hivi karibuni Naibu Waziri Tizeba alitembelewa na wanawe wawili walioishi hotelini hapo kwa zaidi ya wiki kwa gharama ya dola 100 kwa kila usiku.

Alipotafutwa na gazeti hilo,Dkt Tizeba ambaye ni Mbunge wa jimbo la Buchosa kupitia CCM, alishauri suala hilolielekezwe kwa mamlaka zinazohusika na makazi ya mawaziri na viongozi wengine wa umma.

"Siwezi kujipangia makazi mie mwenyewe...kuna mamlaka zenye jukumu hilo,kwahiyo tafadhali ongea nao na upate tamko rasmi.Hata hivyo,vyanzo vya gazeti hilo vimeeleza kuwa gharama za makazi ya Naibu Waziri huyo hotelini hapo zinabebwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Hta hivyo,Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Paniel Lyimo alikataa kuzungumzia suala hilo,hususan haja ya kupunguza gharama kwa kumpatia Dkt Tizeba makazi ya kudumu badala ya kuishi hotelini na hivyo kuongeza gharama.

Katibu huyo Mkuu alimtaka mwandishi kumtumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS), akidai maongezi kwenye simu hayakuwa sawia.Lakini masaa mawili baadaye,mwandishi alipokea ujumbe kutoka kwa mtu aliyedai kuwa ni Naibu Katibu Mkuu katika Wizara hiyo akisema:

"Kuhusu taarifa ulizokuwa ukisaka kutoka kwa Lyimo,Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, ningependa kukufahamisha kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri wa Uchukuzi ameshapangiwa nyumba kitambo sasa."

Hata hivyo kuna taarifa kuwa Dkt Tizeba amekataa kuhamia kwenye nyumba hiyo,ambayo awali ilikuwa ikitumiwa na mtangulizi wake, Athuman Mfutakamba. kwa madai kuwa "haiendani na hadhi yake."

Lakini alipotakliwa kutoa msimamo wake, Dkt Tizeba 'aliponda' tuhuma hizo akidai zinasambazwa na maadui zake.ambao walikuwa wakipambana na harakati za Wizara yake kuweka mambo sawa (kupambana na ufisadi).

Gazeti hilo limepata taarifa kuwa Naibu Waziri wa Fedha, Saada Mkuya, naye aliishi hotelini hapo kwa angalau miezi miwili baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo.

HII NDIO SERIKALI YA RAIS KIKWETE AMBAYO IAN DENI LA NDANI LA SHILINGI TRILIONI 22 NA DENI LA NJE (HADI KUFIKIA AGOSTI MWAKA JANA) LA DOLA BILIONI 10.35 (SHILINGI 16,050,000,000,000),YAANI ZAIDI YA SHILINGI TRILIONI 16.KWAHIYO KIMSINGI JUMLA YA DENI LA NDANI NA LA NJE NI TAKRIBAN SHILINGI TRILIONI 40 (40,000,000,000,000) AMBALO LINAMFANYA KILA MTANZANIA KUDAIWA TAKRIBAN SHILINGI MILIONI MOJA KILA MMOJA (NI WASTANI WA SHS 888,888,.89 )

LAKINI LICHA YA UZITO WA DENI HILO BADO SERIKALI YA KIKWETE HAIJALI KUMLIPIA NAIBU WAZIRI TAKRIBAN SHILINGI MILIONI 100 KWA MAKAZI YA HOTELINI (MNAZIKUMBUKA ZILE NYUMBA ZA MAWAZIRI PALE VICTORIA JIRANI NA KAMBI YA USALAMA WA TAIFA NA HOSPITALI YA KAIRUKI?)

SIJUI HALI YA NCHI YETU ITAKUWAJE HAPO 2015 KIKWETE ATAKAPOONDOKA MADARAKANI.ILA MOJA LILILO WAZI NI KUWA DENI HILI LA MATRILIONI YA SHILINGI LITAKUWA LIMEZALIANA KWA KASI PENGINE ZAIDI YA KASI YA KUZALIANA KWA MAFISADI HUKO NYUMBANI.



31 Dec 2011

Kikwete's smile says it all
Vyombo mbalimbali vya habari leo vimebeba picha ya Rais Jakaya Kikwete akiwa na Katibu Mkuu Kiongozi mpya,Balozi Ombeni Sefue na mtangulizi wake Philemon Luhanjo ambaye amestaafu.Sidhani kama kuna Mtanzania asiyefahamu uhusika wa Luhanjo katika sakata la ufisadi uliofanywa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,David Jairo.Bunge lilishamshauri Kikwete awawajibishe wahusika wote wa ufisadi huo,ikiwa ni pamoja na Jairo na Luhanjo.

Lakini kama ilivyokuwa katika sakata la ufisadi wa Richmond ambapo Bunge lilishauri wahusika wachukuliwe hatua,lakini tukaishia kuona watu kama aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Johnstone Mwanyika walistaafu kwa heshima (bila kusahau marupurupu ya kustaafu),Kikwete amerejea tena udhaifu wake kwa kumwogopa Luhanjo na hatimaye kumwokoa kwa kumruhusu astaafu badala ya kumwadhibu kwa ufisadi wake na Jairo.

Kwa vile leo ni siku ya mwisho kwa mwaka huu 2011,picha ya Kikwete na Luhanjo ni kama kuwakumbusha Watanzania jinsi Rais wao alivyo dhaifu na mbabaishaji wa hali ya juu katika kushughulikia ufisadi.Na japo wengi wenu mtajipa matimaini kuwa mwaka 2012 utakuwa wa matumaini,ukweli mchungu ni kwamba kwa mwenendo huu wa Kikwete kuwaogopa na kuwalea mafisadi,viumbe hao hatari watazidi kuzaliana kwani wanajua fika hakuna wa kuwadhibiti au kuwaadhibu.

Samahani Mheshimiwa Rais,lakini uzembe wako katika kuwashughulikia mafisadi ni sawa na tusi kwa taasisi takatifu ya Urais.Ni lini utaamka na kuyatumia madaraka yako ipasavyo kupambana na ufisadi?

Salama zangu za mwaka mpya kwako si za kupendeza kwani namwomba Mungu aharakishe siku ili umalize muhula wako na ubaki historia isiyo na manufaa kwa Watanzania.Can't wait to see you gone!

6 Aug 2011




JK: Nawajua wala rushwa kwa majina
By Richard Williams | Published  02/22/2006 | Habari za Kitaifa |Rating:
.Asema tabasamu lake lisipotoshe watu
.Maamuzi yake si nguvu ya soda




RAIS Jakaya Mrisho Kikwete amesema anawajua kwa majina wala rushwa katika wizara na kwamba nguvu anayokwenda nayo siyo ya soda.

Alikuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika jana katika uwanja wa michezo wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga, mkutano ambao lengo lake lilikuwa ni kuwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa ushindi wa kishindo waliompatia yeye na Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu wa Desemba 14, mwaka jana.

Rais Kikwete ambaye mkoa wa Rukwa ulikuwa ni wa nne katika ziara zake za kuwashukuru wananchi, amesisitiza kwamba kauli mbalimbali ambazo amekuwa akizitoa katika ziara zake za kutembelea wizara mbalimbali na idara za serikali ni kauli ambazo hazitoi kwa kutania, bali ni kauli za mambo anayoyafahamu vyema na kwamba mengine ameyaweka akiba. 

"Sizungumzi kwa utani nayajua ninayoyasema. Nilichoweka akiba ni kuwataja watu kwa majina, wasidhani nikienda wizarani nikasema watu hawa wanakula rushwa wasidhani siwajui kwa majina, ninawajua, bali kwa sasa ninatoa muda kwa watu hao wajisahihishe. Mwenye masikio nadhani atakuwa amesikia," alisisitiza.

Katika mazungumzo yake na wananchi hao ambayo mara kwa mara yalikuwa yakikatishwa na vigelegele na nderemo; Rais alirudia tena kauli yake kwamba Mwenyezi Mungu amemuumba akiwa na sura ya tabasamu jambo alilosema kuwa hawezi kulibadili, lakini tabasamu hilo lisiwapotoshe watu, kwani yanapokuja mambo ya msingi huwa hana mchezo na mtu. 

Alisisitiza kuwa kila kiongozi katika nafasi wajibu wake ni kuwatumikia wananchi na kwamba wananchi wanayo haki ya kupata huduma kutoka kwa kiongozi huyo. 

"Ikifika mahali Mtanzania akitaka huduma kutoka kwa mtumishi wa serikali anayelipwa mshahara, basi ni lazima kwanza kabla ya kupewa huduma hiyo, amlipe mtumishi yule, tukifika huko basi huo ni ukiukwaji wa maadili ya kazi na mtu kama huyo hastahili kuwa mtumishi wa umma.

"Tumejipanga vizuri ndani ya serikali katika kuwatumikia wananchi, na hii siyo nguvu ya soda, ukisimama mbele yetu utasukumwa," alisema na kushangiliwa na wananchi.

Rais amebainisha kuwa wale watumishi ambao wamekuwa wakidhani kuwa kutokana na unyeti wa taaluma zao basi hata wakinyanyasa wananchi hawataondolewa katika nafasi zao, wakidhani hivyo wanajidangaya.

"Anayedhani kuwa ataendelea kuharibu kwa sababu katika taaluma yake itachukua muda kuwafundisha watu wengine, anajidanyaganya, tuko tayari kuanza upya. Bora tabu kuliko kuwa na mtu wa aina hiyo ambaye badala ya kuwatumikia wananchi yeye anawatesa," alisema.


Alisema maamuzi mbalimbali ambayo serikali inayachukua hivi sasa na hapo baadaye yanalenga katika kuurejesha utumishi wa umma katika mstari ulionyooka na kwa sababu hiyo amewataka watumishi wa serikali kuu na serikali za mitaa kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia maadili ya kazi na viapo walivyokula



Alisema mfanyakazi atakayetekeleza kazi zake kwa kuzingatia maadili ya kazi yake, hata nishani anaweze kupewa na serikali, lakini kwa yule ambaye atafanya kinyume chake serikali haitakuwa na muda naye.



"Hatuna ugomvi na mtu wala hatuna chuki na mtu, tunachotaka kutoka kwako ni utumishi wako uliotukuka kama ulivyoapa kufanya kazi kwa kuzingiatia maadili," alisisitiza Rais na kuufanya umati wa wananchi wa Sumbawanga kumshangilia.



Alisema kuwa anachotoa ni ilani na kukumbushana kama gari lilikuwa linapita kwenye majani, basi sasa lirejee barabarani ili kule lilikokuwa linapita lisije kuwakanyaga watu.



Kikwete alisema uwajibikaji huo wa watumishi wa serikali kuu na mitaa unawahusu vilevile wakuu wa mikoa ambao tayari alishazungumza nao, na atarudia tena kwa wakuu wa wilaya na wakuregenzi wakati atakapokutana nao mara baada ya kukamilisha kazi ya kuwateua.



Akiwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa kumpatia ushindi wa asilimia 86, Rais alisema kuwa ahadi ya serikali ya kuwajengea barabara ya lami kutoka Sumbawanga hadi Tunduma, iko palepale na kwamba kazi ya uchoraji imekwisha kamilika na zabuni za kutafuta kandarasi ili kazi ianze inaendelea. 



Kuhusu mvua zinazoendelea kunyesha katika mkoa huo, Rais amewaomba wananchi hao kuzitumia vizuri ili waweze kuzalisha chakula cha kuwatosha wao na ziada itumike kuwalisha Watanzania wengine ambao mikoa yao imekosa mvua.



Rais Kikwete alishindwa kuhutubia jana mjini Iringa kwa sababu ya mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na radi na hivyo atahutubia leo na baadaye atakwenda kutembelea mabwawa yanayotoa umeme ya Kihansi na Mtera.



Mikoa ya Rukwa na Mbeya ambayo hivi sasa mvua zinanyesha, ingawa zilichelewa kuanza, hali ya mashamba na mazao ni ya kuridhisha hali inayoashiria kuwa kama mvua hizo zinataendelea basi kuna uhakika wa kupata chakula kwa wingi.



Mkoa wa Rukwa hauna matatizo ya njaa isipokuwa katika wilaya ya Mpanda ambako bei ya mahindi imepanda hadi kufikia sh. 10,000 kwa debe, kupanda kwa bei huko kumetoka na wananchi wa maeneo hayo kuuza kwa wingi mahindi yao za ziada 
katika nchi jirani ambako kuna njaa.



Mkoa huo wa Rukwa unatarajia kuzalisha tani milioni 1.2 za mahindi wakati mahitaji halisi ya mkoa ni tani 500,000.


Kutoka gazeti la Uhuru
ISSN 0876-3896 NA.19240
Na Maura Mwingira, Sumbawanga

HABARI HII ILICHAPIHSWA KWENYE MTANDAO WA HABARI TANZANIA

25 Jul 2011


Nchi ipo kizani,Rais Kikwete yupo bize kuzurura nje ya nchi,na akirejea ni kama hayupo.Binafsi sielewi kwanini huyu mtu aligombea urais mwaka 2005 na baadaye 2010.Je ni kuweka historia tu hata kama historia yenyewe ni ya kukinai?Je ni kutopima kina kabla ya kujitosa bwawani?

Kitu kimoja cha wazi ni kwamba kama kuna mtu anayetegemea Kikwete na CCM yake wataleta ufumbuzi wa matatizo ya Tanzania,basi anaweza pia kutarajia kugema damu kwenye jiwe.Kulalamika peke yake hakuwezi kuleta ufumbuzi wa matatizo.Mkoloni,Makaburu,Nduli Idi Amini hawakuondoka kwa vile tuliwatukana au kuwalalamikia,bali tulijiunga kwa umoja wetu na kupambana nao (hata kwa nguvu ilipobidi).

Anyway,soma habari hii hapa chini inayodhihirisha kuwa wababaishaji hawa (Kikwete na chama chake cha Magamba) wapo too busy katika vita vyao vya kimaslahi to care about matatizo ya Watanzania 

Gamba laivuruga CCM 
Monday, 25 July 2011 08:47


Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Benno Malisa

WENYEVITI MIKOA WALIPINGA, BARAZA KUU UVCCM LAUNGA MKONO ZIARA ZA KINA NAPE
Waandishi Wetu
MPANGO mkakati wa kujivua gamba kwa lengo la kurejesha uhai ndani ya CCM unaelekea kuwa bomu la maangamizo kwa chama hicho, baada ya baadhi ya wenyeviti wa mikoa kuupinga huku wakiagiza wafuasi wao kuwashusha majukwaani makada wanaoupigia debe.
Wakati wenyeviti hao wakiupinga, Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), jana limetoa tamko rasmi la kuunga mkono ziara hizo zinazofanywa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa chama hicho, Nape Nnauye za kutekeleza mkakati huo.

Mpango huo wa kujivua gamba ulitangazwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho kikongwe barani Afrika, lakini jana baadhi ya wenyeviti wake wa mikoa akiwamo, John Guninita wa Dar es Salaam na Hamis Mgeja wa Shinyanga, waliupinga wakisema unamwaga sumu kali dhidi ya chama.

Msimamo wa UVCCM
Baraza Kuu la UVCCM limetoa msimamo wake kuunga mkono ziara za mikoani zinazoongozwa na Nnauye za kujivua gamba huku likiweka bayana kuwa huo ni msimamo wa Halmashauri Kuu (Nec) ya chama na si wa Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi.

Mbali na Nape, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wamekuwa wakifanya ziara mikoani hasa katika mwisho wa wiki ambazo pamoja na mambo mengine, wamekuwa wakifanya mikutano ya kukipa uhai chama huku wakitangaza uvuaji gamba.

Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Malisa alisema UVCCM ilipongeza uamuzi wote wa NEC: "Kila kinachofanyika ni sahihi na sisi tunaunga mkono kabisa."

Guninita awatangazia vita
Wakati vijana wakiuunga mkono ziara hizo, juzi Guninita aliwaambia wanaCCM wa Tawi la Sinza kwamba watakapomuona kiongozi yeyote mkubwa wa chama hicho anakikiponda katika wasisite kumshusha jukwaani.
Guninita alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wanachama hao kuhusu matatizo mbalimbali ya chama hicho na kusisitiza kwamba Waziri Sitta asipojibiwa kauli zake atajiona kuwa ni mkubwa zaidi.

Wiki iliyopita Mwenyekiti huyo alimtupia kijembe Sitta akidai kwamba waziri huyo ana mpango wa kuhakikisha kuwa Serikali ya chama hicho inaondolewa madarakani kwa kuwa bado ana hasira za kupoteza wadhifa wa Spika wa Bunge.

“Chama chetu kinazidi kupoteza sifa, hii ndiyo sababu ya mimi kufanya ziara katika majimbo ambayo yalishindwa katika ngazi zote kukipatia chama ushindi wakati wa uchaguzi. Kumekuwa na viongozi wakubwa wa chama hicho wanaozunguka nchi nzima na kuchochea ili Serikali iondolewe madarakani, nawaambieni mkiwaona viongozi hao wanakiponda chama washusheni majukwaani, wanataka kujiona wao ndiyo wakubwa zaidi ya wengine.”

Alisema chama hicho kinajipanga kikamilifu ili kuhakikisha uchaguziwa mwaka 2015, kinashinda kwa kishindo ikiwa ni pamoja na kupambana na tatizo la rushwa lililokitawala.

Guninita ambaye amekuwa akipingana hadharani na wapambanaji hao wa ufisadi ndani ya CCM, alisema katika uchaguzi huo hawatahitaji ushahidi kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) na kuwa mtu atakapobainika anajihusisha na rushwa atachukuliwa hatua hapohapo.

“Tatizo la rushwa katika chama lipo hasa wakati wa uchaguzi. Ninachotaka kuwahakikishia ni kwamba tunajipanga na katika uchaguzi ujao hatutahitaji ushahidi wa PCCB (Takukuru), tutakapombaini mtu tutampeleka mahakamani wenyewe. Hatutaki aibu ya mwaka huu itukumbe tena.”

Alisema tayari chama kimewabainisha viongozi wote walioingia madarakani kwa rushwa na kuwa wanaendelea kujadiliana hatua za kinidhamu dhidi yao.

Guninita alisema katika uchaguzi wa mwaka 2015, chama hicho hakitapeleka majina ya watu watakaobainika kutoa rushwa kwa ngazi za juu ili wakubalike katika kura za maoni.

Mgeja atoa tahadhari
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja alisema juzi kwamba licha ya kuwakaribisha wapambanaji hao na mkakatio wao wa kujivua gamba katika mkoa wake, waende na majibu ya kero za wananchi.

Alisema viongozi wa chama chake wanatakiwa kwenda na majibu ya kero zilizopo katika mkoa huo za wakulima kuuziwa dawa feki za pembejeo, rushwa, umasikini na rasilimali kama madini kushindwa kuwanufaisha, badala ya kutumia ziara hiyo kuwapaka matope wenzao.

“Ziara za kusafisha chama siyo mbaya, kama zitatumika vyema, lakini hali ambayo imeanza kujitokeza ni wazi haijengi chama, bali inaendelea kumwaga sumu,” alisema.

Millya, Porokwa waponda ziara hizo
Mbali ya Guninita na Mgeja, Mwenyekiti wa UVCCM, mkoani Arusha, James Ole Millya naye ameziponda ziara hizo za kujivua gamba akisema hazina tija kwa chama na Serikali kwa kuwa Sitta, ni waziri ndani ya Serikali hiyohiyo anayoituhumu na kueleza kwamba anaona kuna uchafu ndani yake ni vyema akatoka.

Millya aliwatuhumu Sitta, Nape, Ole Sendeka na Dk Mwakyembe kuwa wamekuwa wakitumia mwanya wa ziara hizo kuichafua Serikali na chama tawala huku akisisitiza: "Kama wanaona Serikali hiyo haifai ni bora wangeondoka. Sitta ni waziri, Mwakyembe ni waziri na wengine wako ndani ya Serikali na chama hawa wote ni viongozi, sasa kitendo cha wao kuzunguka na kuisema vibaya Serikali na chama tawala hakifai.”

Alisema viongozi hao wameamua kuanza mashambulizi dhidi ya Serikali kwa kuwa ni wabinafsi, huku akikitahadharisha chama hicho kuwa makini na ziara hizo kwa kuwa huenda zikakiingiza katika hatua mbaya.

Naibu Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Daniel Porokwa naye aliziponda ziara za viongozi hao akisema zimejaa unafiki kwa kuwa Sitta na Nape walikuwa waanzilishi wa Chama cha Jamii (CCJ) na kuwaita wasaliti ndani ya CCM.

Alisema pamoja na kutoa tuhuma mbalimbali dhidi ya viongozi hao kuwa ni waasisi wa CCJ, anashangaa hadi leo uongozi wa chama chake haujawahi kumwita au kumwomba udhibitisho juu ya madai aliyoyasema.


Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Nape akutana na mabango Moshi
Ziara ya Nape, juzi mkoani Kilimanjaro ilikumbana na upinzani mara baada ya kiongozi huyo kupokewa kwa mabango mbalimbali wakati akishuka kwenye gari lake katika Kituo cha Mabasi Moshi Mjini tayari kwa kuhutubia mkutano wa hadhara katika eneo hilo.

Hata hivyo, tofauti na mikutano mingine kama ule wa mkoani Mbeya, huo ulihudhuriwa na watu wachache huku wengine walionekana wakishuka kutoka kwenye mabasi uwanjani hapo.

Nape aliyefika kituoni hapo mnamo a saa 9:00 mchana akitokea Mwika katika ufunguzi wa Tawi la CCM Chuo Kikuu cha Tumaini (Smmuco), alikutana na mabango yaliyokuwa yameshikiliwa na vijana wa CCM wilayani Moshi ambayo yalikuwa yamebeba ujumbe mbalimbali.

Baadhi ya mbango hayo yalikuwa yakisomeka: ”CCJ nao wajivue gamba,” “Hatutaki makundi ndani ya CCM,” ”Vijana tumechoka na wana CCJ, wana CCJ ondokeni mtuachie CCM yetu.”.

Wakati vijana hao wakibeba mabango hayo mbalimbali yaliyolenga kufikisha ujumbe kwa Nape, vijana wa ulinzi wa CCM maarufu kama “Green Guard,” iliwabidi kutumia nguvu za ziada kuzima juhudi za vijana hao waliobeba mabango hayo na waliyakamata na kisha kuyachana baadhi yao huku mengine yakiwasilishwa katika Ofisi ya Katibu wa CCM wilayani Moshi.

Akimkaribisha Nape jukwaani, Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi Mjini, Amos Shimba aliyaponda vikali mabango hayo huku akisema vijana walioyabeba siyo wakazi wa Mji wa Moshi, bali wanatoka mkoani Arusha huku akiwaonya, kamwe wasithubutu kuleta mambo hayo mkoani Kilimanjaro.

“Kuna vijana wanaotaka kutuletea vurugu na tunajua wanatoka tu Arusha, tunawaambia tafadhali sana msituletee mambo yenu ya vurugu za Arusha hapa mkoani kwetu,” alionya Shimba.

Akihutubia mkutano huo, Nape alisema lengo la ziara yake mkoani Kilimanjaro ni kuleta matumaini kwa wanachama wa CCM sanjari na kufafanua falsafa ya kujivua gamba ambayo alidai inapotoshwa na watu wachache hapa nchini.

Alikishambulia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) hususan viongozi wake kwamba wanapenda vurugu na maandamano huku akionya kwa kutumia mifano na nahau mbalimbali ya kuwa kamwe Serikali ya CCM haitakubali amani ya nchi ichezewe.

Aliendelea kumshambulia vikali Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akidai kuwa ameamua kukishinikiza chama chake kumlipa kiasi cha Sh7 milioni ihali alikuwa kinara wa kupinga mishahara minono na marupurupu ya wabunge.

“Namtaka Dk Slaa aishi kama anavyoongea, alinituhumu nahusika na EPA mkiniangalia mimi sura yangu inafanania na EPA? Mbona yeye amekishinikiza chama chake kimlipe Sh7milioni wakati alikuwa akipinga mishahara na marupurupu ya wabunge? Huyu ni mnafiki,” alisema Nape.

Alisema falsafa ya kujivua gamba ndani ya CCM imekuwa ikipotoshwa na baadhi ya watu hususan wapinzani na kuuita kuwa ni dhana ya kishetani kwa kuwa imetumia mfano wa nyoka na kuwabeza watu hao kwa kuwataka wasome biblia na msaafu na kuwaeleza kuwa nyoka ametajwa ndani ya vitabu hivyo.

Akizungumzia kauli za wanaCCM wanaoipinga dhana hityo, alisema asingependa kujibizana na watu wanaouzungumza barabarani kwani chama kina vikao ambavyo vitawahukumu.

Alichokisema Sitta
Akizungumza Dar es Salaam juzi, Sitta alisema Serikali makini lazima ikiri mapungufu kutokana na makosa yake: "Nilichokisema Mbeya ni kuwaambia Watanzania ukweli na nitaendelea kuwaambia ukweli."

Alisema serikali makini haiwezi kuwadanganya wananchi wake na kusisitiza, "Watanzania wa leo ni watu wenye akili huwezi kuwambia habari nzuri za umeme wakati umeme ni tatizo."

"Kule Mbeya nilieleza ule umati ukweli kuhusu upungufu wetu serikalini na wananchi walituelewa. Kuna upungufu tumeukiri na tunajipanga kuupatia ufumbuzi. Umeme ni tatizo kubwa huwezi kueleza uongo kwa Watanzania wakakuelewa, waambie wananchi ukweli watakuelewa. Sasa huu ndiyo upungufu wetu, lakini wanatokea baadhi ya watu wenye upeo mdogo ndani ya CCM wanaoendekeza siasa za ufuasi, wanakaa na kuzungumza mambo ya hovyo."

Imeandaliwa na Ramadha Semtawa, Minael Msuya, Dar, Habiel Chidawali, Dodoma, , Moses Mashalla, Moshi

Chanzo: Mwananchi 

19 Jul 2011


Rais Kikwete kutembelea Afrika Kusini 
Monday, 18 July 2011 21:28

Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, jana alianza ziara ya kihistoria ya kidola nchini Afrika Kusini, ikiwa ni ziara ya kwanza ya aina yake, kufanywa na Rais wa Tanzania katika nchi hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Kikwete anafanya ziara hiyo kwa mwaliko wa Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ambaye utawala wake umekuwa uhusiano wa karibu na Tanzania, tangu aliposhika madaraka ya kuongoza taifa hilo kubwa kiuchumi kuliko mengine, katika Afrika.

Rais Kikwete na ujumbe wake unaojumshia pia mkewe, Mama Salma Kikwete, uliondoka nchini jana mchana kwenda Pretoria, kwa ziara hiyo ya siku nne.Pamoja na kwamba marais wa Tanzania waliomtangulia Rais Kikwete wametembelea Afrika Kusini mara nyingi kwa shughuli mbalimbali, lakini hakuna kiongozi aliyepata kualikwa kufanya ziara rasmi, ya kiserikali ama ya Kidola, tangu nchi hiyo ilipoingia katika mfumo wa demokrasia mwaka 1994.

Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, Rais Kikwete na ujumbe wake, watapokelewa rasmi leo asubuhi katika Jumba la Serikali, mjini Pretoria.Tayari Rais Zuma na mkewe walikwishajipanga kwa sherehe za makaribisho zitakazofuatiwa na mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Tanzania na Afrika Kusini.

Mazungumzo hayo, yatafuatiwa na utiaji saini wa mikataba na makubaliano katika nyanja mbalimbali kati ya nchi hizo mbili.Baadaye, viongozi hao wawili watahutubia mkutano wa waandishi wa habari na baada ya hapo, Rais Kikwete atatembelea Uwanja wa Uhuru akiandamana na Rais Zuma.

Mchana viongozi hao watahudhuria chakula cha mchana kikiwashirikisha pia wafanyabiashara wa Tanzania na Afrika Kusini ambao watazungumza na kuelezea umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.Jioni, Rais Zuma ataandaa dhifa ya kitaifa kwa ajili ya Rais Kikwete na ujumbe wake .

Keshokutwa, Rais Kikwete na ujumbe wake watakwenda Cape Town, ambako miongoni mwa mambo mengine ujumbe huo utatembelea Kisiwa cha Robben ambako wapigania uhuru maarufu wa Afrika Kusini, akiwamo Rais Mstaafu Nelson Mandela, walifungwa kwa miaka mingi na makaburu. Rais Kikwete atarejea nyumbani keshokutwa asubuhi.

CHANZO: Mwananchi 

LABDA AKIREJEA KUZURURA TATIZO LA UMEME LITAKUWA LIMEPATA UFUMBUZI. 




Kama kuna kosa ambalo Watanzania watalijutia kwa muda mrefu sana ni lile walilofanya mwaka 2005 na kisha kulirudia mwaka jana kumchagua Jakaya Kikwete kuwa Rais wa nne wa Tanzania.Tusiume maneno,mengi ya matatizo yanayoikabili nchi yetu kwa sasa ymesababisha,yanasababishwa au yamechangiwa au yanachangiwa na ubabaishaji wa Kikwete.

Ni nani mwenye akili timamu asiyefahamu kuwa wakati kelele dhidi ya ufisadi zinaelekezwa kwa "mapacha watatu" waliobaki wawili (ie Lowassa na Chenge,na Ristam aliyejiuzulu),Kikwete ni sehemu muhimu kabisa ya tuhuma zinazoelekezwa kwa wanasiasa hao.Hapa simaanishi kuwatetea mafisadi hao bali ninachojaribu kupigia mstari ni ukweli kwamba Kikwete hana tofauti na Lowassa,Chenge au Rostam.Na hilo halihitaji ufafanuzi.Yeye anajua,mapacha watuatu waliobaki wawili wanajua,na kila Mtanzania mwenye akili tiammu anajua.Kwanini hadi leo Kikwete bado ni Rais wetu ni swali gumu kulijibu just like lile la kwanini alichaguliwa mara ya kwanza mwaka 2005 na baadaye 2010 ilhali wanamjua walikuwa wanatambua bayana kuwa hana sifa za kushika wadhifa huo mkubwa kabisa katika nchi yetu.

Anyway,lengo la makala hii sio kujadili ubabaishaji wa Kikwete katika utendaji kazi wake bali lengo ni kukemea kwa nguvu kubwa uhuni uliofanywa na Kikwete wa kufanya harusi ya mdogo wake kwenye Ikulu ndogo ya Bagamoyo.Hivi kwa kuwa Rais,Kikwete anadhani kuwa Watanzania wametoa urais kwa ukoo wake mzima?Kwanini asikodi ukumbi kwa fedha zake kisha akamfanyia sherehe mdogo wake?

Kama huelewi kwanini ninalamika,Ikulu iwe ile ya Magogoni au hizo ndogo za wilayani na mikoani ni mahala patakatifu-kama alivyowahi kusema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.Si mahala ambapo kila Tom,Harry and Dick anaweza kufanya atakalo.Lakini licha ya utakatifu huo wa Ikulu,ifahamike kuwa mahala hapo panaendeshwa kwa fedha za walipakodi.Kwa mantiki hiyo,kufanyia sherehe mahala hapo ni sawa na kuwabebesha gharama Watanzania kwa ajili ya harusi ya ndugu wa Kikwete.Sidhani hata waliompigia kura mwaka jana au 2005 walitamani kuona kura waliyompigia Jakaya inageuzwa kuwa mithili ya kuupigia kura ukoo wake mzima.

Huu ni uhuni unaopaswa kukemewa vikali.Rais anaweza kuzurura nje ya nchi atakavyo (inaelekea kama hakuna namna ya kumwelewesha kuwa safari zake za mara kwa mara nje ya nchi ni mzigo mkubwa kwa Watanzania) lakini kamwe tusiruhusu nafasi ya Urais ikageuzwa kuwa kama cheo cha kifamilia.

Madhara ya kumwacha Kikwete aendelee na madudu yake ni kwamba anaweza kumaliza muda wake hapo 2015 na kuiacha Tanzania ikiwa jina tu-haina maadili,haina raslimali,na kibaya zaidi,nafasi ya urais ikaishia kuwa na heshima ndogo kuliko ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa.

PICHA: Kwa hisani ya Global Publishers

16 May 2011


Rais wetu mpendwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kushangaa hajambo.Sasa anashangaa kwanini kuna utitiri wa mabango yenye ujumbe dhidi ya rushwa lakini rushwa inaendelea kutawala katika wizara mbalimbali bila uoga.

Tell you what Mr President,jibu la kinachokushangaza ni rahisi sana.Kama wewe mwenye kila nyenzo ya kukabiliana na rushwa,na ambaye ulitangaza hadharani kuwajua wala rushwa ila uliwapa muda wa kujirekebisha-na wakagoma kujirekebisha,lakini unaogopa kuwachukulia hatua-unasuasua katika kutekeleza ahadi uliztoa mwenyewe,unatarajia nini kutoka kwa watu wasio na uwezo wala mamlaka ya kupambana na rushwa?

Wewe unashangaa na sie tunakushangaa pia.One thing for sure,rushwa haiwezi kumalizwa kwa Rais kushangaa.Kinachohitajika ni vitendo na sio kubembelezana katika semina elekezi zinazozidi kuwatwisha mzigo walipa kodi masikini.

Jaribu kuwa mkali kidogo,punguza kushangaa,fanya vitendo.

Habari kamili ni hii hapa chini

Kikwete ataka vita vya rushwa kwa vitendo

na Danson Kaijage, Dodoma

RAIS Jakaya Kikwete, ameagiza mabango yote ya kupambana na rushwa yanayobandikwa katika wizara na taasisi za serikali na za umma yaendane na matendo yanayofanywa na maofisa katika ofisi husika.

Alitoa agizo hilo jana alipokuwa akifunga semina elekezi kwa viongozi na watendaji wakuu wa serikali iliyofanyika mjini Dodoma kwa siku saba.

Alisema wananchi wangependa kuona ukusanyaji wa mapato unaimarika na nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za umma inakuwa bora zaidi badala ya kujaza mabango mengi yasiyokuwa na faida.

Alisema wananchi wanatarajia kuona juhudi za mapambano ya kweli kwa kudhibiti mianya ya rushwa badala ya kuona mabango mengi bila kuwepo na juhudi za makusudi.

Rais Kikwete alisema kinachoshangaza ni kuona wingi wa mabago katika kila kona wakati rushwa inaendelea kutawala ndani ya wizara mbalimbali bila woga.

Aidha, alisema kutokana na kuwepo kwa rushwa kuanzia ngazi ya juu ni wazi kuwa rushwa itaendelea kutendeka hadi ngazi ya chini kwa kuwa misingi ya rushwa inaanzia ngazi ya juu na kushuka ngazi ya chini.

Aliwataka vingozi na watendaji wakuu hao, kuonyesha ujasiri mkubwa juu ya kupiga vita masuala ya rushwa badala ya kuoneana aibu na kufichiana siri.

Rias Kikwete alisema semina hiyo ambayo ilikuwa na mikakati ya kuimarisha utendaji ndani ya serikali inapaswa kuzaa matunda hasa katika mapambano dhidi ya rushwa.

Hata hivyo, alisema wananchi wanatazamia kuona viongozi wa ngazi ya juu wakiwa mfano mzuri wa utawala bora, kuheshimu Katiba, utawala wa sheria na nidhamu ya kazi na uwajibikaji.

Naye Katibu Mkuu Kiongozi, Philimon Luhanjo, alisema waliazimia mazimio 14 ambayo viongozi hao wanatakiwa kuyatekeleza na kuyawasilisha katika ofisi yake kila baada ya miezi mitatu.

Semina hiyo iliwashirikisha mawaziri, makatibu wakuu, manaibu makatibu wakuu na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.



10 May 2011



Ama kweli chozi limepata mliaji.Kila mara tunasikia Rais wetu kalia na watendaji hawa,au kasikithswa na watendaji wale.Kichekesho ni kwamba watendaji hao hawakujiteua wenyewe kuwa madarakani bali waliteuliwa na huyhuyo anayelalama.

Binafsi,nadhani tatizo sio watendaji dhaifu wanaopelekea Rais "kulia" nao kila mara bali tatizo la msingi ni Rais mwenyewe.Kiongozi dhaifu haishiwi visingizio.Kiongozi dhaifu haishiwi lawama.Na kiongozi dhaifu hakawii kudai hili limeshindikana kwa vile yule hakufuata maagizo.Kwanini asiwatimue?

Hizi semina elekezi ni mzigo mwingine kwa Watanzania,ambao hawastahili kubebeshwa gharama za posho za waheshimiwa hao kwa ajili ya semina kama hizo ilhali aliyawateua ana kila sababu ya kuwatimua,lakini hana nia wala uwezo (wa kibinadamu,sio uwezo anaopewa na Katiba).

Yaani hadi tutapofika hapo 2015 sijui hali itakuwaje.Lakini moja ambalo tuna uhakika wa kulikumbuka kuhusu Kikwete ni hivi "vilio" vyake dhidi ya watendaji aliowateua yeye mwenyewe.

Enewei,soma habari husika hapo chini:

Kikwete alia na mawaziri mizigo 
Monday, 09 May 2011 21:54


Habel Chidawali, Dodoma
RAIS Jakaya Kikwete amewataka mawaziri na makatibu wakuu kujiamini katika utendaji wao wa kazi badala ya kutegemea maelekezo ya mamlaka zilizo juu yao.Alisema hayo jana alipokuwa akifungua semina elekezi kwa viongozi na watendaji wakuu wa Serikali iliyofanyika katika Ukumbi wa St Gasper nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma.“Hadi leo sijui kwa nini hasa watu (mawaziri) wanashindwa kuzungumza mambo yaliyofanywa na Serikali na kuwapa uwanja mpana wenzetu wa upande wa pili (wapinzani) ambao wanajua kweli kuvitumia vyombo vya habari. Sisi tunaendelea kulalamika kila siku kwamba hatuandikwi, nani atakuandika wakati hutoi taarifa,” alisema Kikwete.

Kuna wakati waziri mmoja aliwahi kunipigia simu na kusema 'Mheshimiwa Rais habari hii tuikanushe?' Nilichokifanya nilimwambia pima wewe baada ya hapo nikakata simu,” alisema

Rais Kikwete alisema kitendo cha mawaziri kukataa kutoa habari na kuwafanya maofisa habari wa wizara kuwa kama waandishi wa habari ni hatari kwa serikali.

Katika hotuba yake, Rais Kikwete aliwataka watendaji hao kufanya kazi kwa kufuata misingi ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu ili kukwepa hasara inayoweza kutokana na uamuzi usiofuata kanuni na kuiaibisha Serikali.
"Ni muhimu kwenu kama viongozi mkajielimisha juu ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu mbalimbali zinazoongoza utendaji kazi katika sehemu zenu za kazi. Uhalali wa maamuzi mtakaoyafanya hupimwa na sheria," alisema Kikwete na kuongeza:
"Ukifanya uamuzi unaokinzana na sheria utahojiwa wewe binafsi lakini pia utaibebesha Serikali mzigo wa hasara na fedheha itakayotokana na uamuzi huo. Uamuzi usiofuata sheria unaweza kuwa na madhara kwa wananchi.

"Heshimuni Katiba na fuateni sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika utekelezaji wa majukumu yenu. Katika semina hii masuala hayo yatafafanuliwa na kuzungumzwa. Kadhalika, uhusiano wa Serikali na mihimili mingine ya dola yaani, Bunge na Mahakama utafafanuliwa."

Rais Kikwete pia aliwataka watendaji hao kuepuka kauli na vitendo vinavyoweza kuwafarakanisha na kuleta mgawanyiko katika Serikali ili kulinda dhana ya uwajibikaji wa pamoja.

"Viongozi na watendaji wakuu wa wizara hamna budi kujenga uhusiano mzuri na uwajibikaji wa pamoja. Haifurahishi kuona waziri na katibu mkuu au waziri na naibu waziri; naibu waziri na katibu mkuu au katibu mkuu na naibu katibu mkuu hawaelewani."

"Wanasemana na hata wanapingana hadharani, yaani mbele ya wafanyakazi. Baya zaidi ni pale wanapopingana katika vyombo vya habari kuhusu uamuzi au utendaji wa wizara au serikali kwa jumla. Hayo si maadili mema katika taasisi yoyote.

"Kama unaona vigumu kuuafiki ni bora kutoka. Hairuhusiwi kupinga taasisi ambayo wewe umo ndani kama mmoja wa viongozi wake. Ni vyema hili likaeleweka. Msitupe tabu ya kuulizana maswali na kuwasemea."
Rais Kikwete pia aliwataka watendaji hao kuwa mstari wa mbele kuzungumzia mafanikio ya Serikali ili kuziba midomo ya wapinzani wanaopita kila kona nchini na kuwaeleza wananchi kuwa haijafanya chochote.

"Sijui kwa nini hatuwi wepesi kuyasemea mafanikio mengi tuliyoyapata tukaacha wasiotutakia heri wanaosema hatukufanya kitu wasikike mpaka waonekane wanasema kweli," alisema.

Alisema hajui na hana majibu mazuri ya kwa nini Serikali imekuwa ikishindwa kuzungumza mambo mazuri yaliyofanywa katika kipindi cha miaka mitano na hata wakati mwingine kushindwa kuzungumza jambo hadi wampigie simu, kitu ambacho ni aibu.

Alisema kuna udhaifu katika kujipanga kwa wasemaji kutokana na kuchelewa kutoa taarifa au kukanusha habari ambazo zimekuwa zikitolewa na upinzani, jambo linalowafanya wananchi waamini kuwa ni kweli, kwani uongo ukizungumzwa mara nyingi hugeuka na kuwa ukweli.

“Unajua mimi sijui hadi leo ni kwa nini hasa watu wanashindwa kuzungumza mambo yaliyofanywa na serikali na kuwapa uwanja mpana wenzetu wa upande wa pili ambao wanajua kweli kuvitumia vyombo vya habari huku sisi tunaendelea kulalamika kila siku kwamba hatuandikwi, nani atakuandika wakati hutoi taarifa,” aliuliza Kikwete.

Alikanusha madai kuwa baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika habari za upinzani na kuacha habari nzuri za serikali na badala yake akasema woga na urasimu uliowajaa wasemaji katika serikali, ndilo tatizo hasa kwa kuwa hawajui kuwa vyombo vya habari vinatafuta habari na kama wao hawatoi habari ni lazima waandike zile zinazotolewa na upande wa pili.

Katika hatua nyingine, Kikwete alisema kuwa anategemea kuona Serikali yake ikifanya kazi kwa umoja na ushirikiano mkubwa katika kipindi hiki cha miaka mitano na kwamba kushirikishana na kupeana habari iwe ndiyo dira ya maendeleo yao.

Sikuteua mawaziri wa kusoma mafaili ofisini
Aliwataka viongozi hao kuacha umangimeza, badala yake watoke ofisini kujionea matatizo ya wananchi.
"Mawaziri na makatibu wakuu lazima mtoke. Hiyo ndiyo njia bora zaidi ya kujua mambo yahusuyo wizara zenu na ndiyo njia bora ya kuongoza: kuona wenyewe na kutenda," alisema Rais Kikwete na kuongeza: "Hii itawafanya mjiamini kuelekeza na pia mnaposimama mbele za watu na kusema. Msiwe mamangimeza. Tokeni, tembeeni kuona shughuli zenu. Tembeleeni wananchi muwafahamu, wawafahamu, mjue shida zao muwatatulie."

Alikemea tabia ya viongozi hao kushinda kwenye mitandao kila siku na kusoma ujumbe badala ya kwenda kuwatumikia wananchi vijijini.Alisema tabia hiyo haipaswi kuvumiliwa hata kidogo na akaonya viongozi wa namna hiyo wataishia kuwa wababaishaji na hatakwenda nao katika kipindi chake cha uongozi.

Mimi sikuteua mawaziri wa kusoma mafaili ofisini, bali niliteua watu wanaoweza kukimbizana kwa kasi zaidi, ari zaidi pamoja na nguvu zaidi, kwani nataka kuwasikia mkichakarika huko kwenye miradi mlikopeleka fedha, siyo kupokea taarifa ofisini bila ya kujua fedha za walipa kodi zinatumikaje huko.”

Dawa ya mawaziri hawa ipo jikoni
Rais Kikwete pia aliwatahadharisha mawaziri ambao wamekuwa wakipinga kauli na miswada ya mawaziri wenzao, huku wengine wakiwa wanatoa siri za Serikali.Alisema kuwa watu wa namna hiyo dawa yao iko jikoni kwa kuwa kitendo wanachokifanya si kizuri ndani ya Serikali.

Alisema anayo mamlaka ya kuchagua na ya kumwondoa waziri wakati wowote akiamua, hasa kama haoni umuhimu wa kuendelea na mtu wa aina hiyo.

“Katika hili nawaambia mapema kabisa kuwa waziri anayeishi kwa kupinga miswaada ya Serikali ajue kuwa anaipinga Serikali na hivyo sitakuwa tayari kufanya kazi na mtu wa aina hiyo. Sehemu kubwa ya kazi zenu mawaziri nataka ziwe za Serikali na zile za jimbo mtajua namna mtakavyojipanga bila ya kuharibu kazi za Serikali,” alisema.

Pato la Mtanzania litakua miaka mitatu ijayo
Rais Kikwete alisema kasi ya kukua kwa pato la Mtanzania ni ndogo na kwamba kunahitajika juhudi za makusudi katika kuongeza pato hilo. Hata hivyo, alitamba kuwa pato la Mtanzania litaongezeka katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa kutokana na baadhi ya nchi wahisani kuahidi kuongeza misaada kwa Tanzania.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake, umaskini umepungua kwa asilimia mbili tu hivyo, akaahidi kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya awamu ya pili ya uongozi wake, umaskini utapungua kwa kiasi kikubwa.

Alisema mkakati uliopo hivi sasa serikalini ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025, Tanzania inakuwa nchi yenye uchumi wa kati pato la Mtanzania wa kawaida likitarajiwa kufikia Dola za Marekani 2,500 hadi 3,000. Sasa ni Dola 600. Kuhusu kipindi cha miaka mitatu, alisema kuwa, ipo mipango mizuri kutoka kwa wahisani, ikiwamo Benki ya Dunia ambayo imekubali kuisaidia Tanzania kiasi cha Dola 2.8 milioni ambazo zinaweza kusaidia katika kutengeneza ajira na kupambana na umaskini.

Semina hiyo ilihudhuriwa na watendaji wote wa Serikali wakiwamo Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, mawaziri na manaibu waziri, makatibu na naibu makatibu wakuu, Mwanasheria Mkuu na naibu wake, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na viongozi wastaafu, akiwamo Spika wa zamani na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya

CHANZO: Mwananchi

20 Oct 2010


Baadhi ya wazazi wa watoto wanaugua ungonjwa wa malaria wakiwa nje ya Kituo cha Afya Nyamongo Wilayani Tarime

Anthony Mayunga, Tarime

KITUO cha Afya Nyamongo wilayani Tarime hakijapata dawa ya mseto inayotibu malaria kwa kipindi cha miezi mitatu hadi sasa.

Tatizo hilo linakwenda kinyume na kampeni za kupambana na malaria kwa kuwatibu wagonjwa ambayo inasisitiza kwamba Watanzania watapata vyandarua na dawa sahihi za kutibu malaria.

Uchunguzi wa uliofanywa na Mwananchi katika kituo hicho kilichoko katikati ya eneo la mgodi wa dhahabu wa North Mara ,ulibaini ukubwa wa tatizo hilo na wananchi kuonyesha kukata tamaa juu ya
mikakati inayonadiwa na viongozi kutokomeza malaria nchini. Marwa Ryoba mkazi wa Nyangoto alisema wanalazimika kutumia dawa za krolokwini,metakefilini na SP ambazo zilikwishapigwa marufuku na serikali kwa kushindwa kutibu ugonjwa huo.

“Tunashangaa ahadi na tambo nyingi za serikali kuwa watatokomeza malaria wakati hatupati dawa , hivi kupewa vyandarua na Wamarekani bila dawa inatusaidia?”alihoji kwa uchungu.

Mganga mfawidhi wa kituo hicho Dk George Marwa alikiri kuwa hawajapata
dawa mseto licha ya kutoa taarifa kwa zaidi ya miezi mitatu. “Hapa tunapambana na matatizo makubwa maana jamii haijui tatizo la Msd badala yake lawama zinaelekezwa kwetu,maana kama hakuna Alu unadhani huko wanatumia nini,”alisema. Kuhusu kadi za kiliniki hakuna na wajawazito na wenye watoto
wanalazimika kununua mitaani inadaiwa wananunua Sh2,000= maana hatuna,na hilo linawakatisha tamaa wasiokuwa na fedha kuhudhuria
kiliniki.
“Hapa tunahudumia zaidi ya watu laki moja kutoka kata zaidi ya nne za Tarime na Serengeti, glovu unapewa pc 50 kwa miezi mitatu ,wakati hizo ni kwa wiki moja,wanalazimika kununua, na ni tatizo la mfumo.

Awali mwanamke aliyekutwa katika kituo hicho akisubiri huduma jina tunao ,alisema kuwa wanachofanya ni kwenda kuandikiwa tu kisha wanakwenda kununua dawa kwenye maduka ya watu ambao pia si wataalam.
“Wengi tunatumia panadol wakati unaumwa malaria na hata kwa watoto
,matokeo yake panapotokea vifo inakuwa vigumu kujua nini tatizo ,maana wapo wanaoishiwa damu, lakini tunashindwa watibiwe na nini,”alisema.

Alikwenda mbali na kudai kuwa matatizo ya wananchi kwa huduma za afya yamegeuka kuwa mtaji kwa wanasiasa wanafiki,kwa kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki,”suala la dawa limeshindikana sasa wanadai malaria
itakuwa historia kwa kuua ama nini?”alihoji kwa masikitiko.Baadhi ya wajawazito na wenye watoto waliokuwa hapo kituo
cha afya walisema mbali na dawa ya malaria pia wanalazimika kununua kadi na glovu kwa kuwa hazipatikani hapo kituoni .

“Pembeni wanasema huduma kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano bure ,lakini hapa tunanunua dawa,mipira ya mikononi(Gloves)na kadi za kiliniki,wengi wanajifungulia majumbani na hawaleti watoto
kiliniki akiugua malaria wananunua panadol na dawa za kienyeji,”walisema.

CHANZO: Mwananchi

NAAMINI TATIZO LA KUDAIWA MALIPO KWA HUDUMA ZINAZOPASWA KUTOLEWA BURE NI KARIBU KILA MAHALI NCHINI.NDIO MAANA CCM HAWATAKI KUSIKIA AHADI YA CHADEMA KUHUSU  ELIMU BURE.

20 Aug 2010

Pamoja na kumtetea mwanaye,JK alisema (namnukuu)"...hata kama aliyegombea hakuridhishwa na mazingira ya namna aliyeshinda alivyoshinda, ndiyo ameshapata,hivyo jambo la msingi ni kuacha makundi yaliyokuwepo wakati wa kura za maoni, bali wajielekeze katika kutafuta ushindi wa kishindo huku wakijiandaa kwa kugombea kipindi kingine..."SWALI.Je kama kutoridhishwa huko kunatokana na matumizi ya rushwa?Au kwa vile Awamu ya Nne ilikuwa na huruma kwa mafisadi basi wagombea waliofisadiwa nao waige mfano wa serikali hiyo?Soma habari kamili HAPA.

5 Aug 2010

Natoa wito kwa wanachama walioomba nafasi lakini wakakosa, jamani msiwe chanzo cha mifarakano ndani ya chama, KAZI ZIPO NYINGI,TUNAWEZA KUTEUANA, fanyeni kazi ya ushindi kwa chama chetu,” .Hayo si maneno yangu bali ya Rais Jakaya Kikwete aliyoyatoa siku alipochukua fomu za kuogombea tena urais kwa tiketi ya CCM.Ni kweli kazi zipo nyingi ikiwa ni pamoja na kilimo au biashara lakini haiingii akilini kwa watu waliokataliwa na wananchi kupewa nafasi kwa mlango wa "kuteuana".

Hili ni tatizo sugu katika siasa za Tanzania.Utakuta mtu ameboronga sehemu moja kisha anahamishiwa sehemu nyingine.Yayumkinika kusema kuwa kuteua "rejects" hao sio tu matumizi mabaya ya ruhusu inayotolewa na katika kufanya teuzi mbalimbali bali pia ni dharau ya moja kwa moja kwa wananchi.

Haiwezekani kwamba nchi yenye watu zaidi ya milioni 40 iwe na kikundi kidogo tu cha watu wenye uwezo wa kuwa viongozi.Na kibaya zaidi kikundi hicho kikijumuisha watu waliokataliwa na wananchi katika chaguzi au maombi yao ya kutaka wachaguliwe kuongoza.

Na ukiingia kiundani zaidi kuangalia tabia hii isiyopendeza,unaweza kuyumkinisha kuwa hata uteuzi wa Dkt Gharib Bilal unaangukia kwenye eneo hilohilo.Bilal alitaka ridhaa ya vikao vya CCM kuwa mgombea wa Zanzibar lakini "kura hazikutosha".Hata hivyo,katika kile kinachoelezwa kama kujenga mshikamano miongoni mwa wana-CCM,Bilal aliteuliwa na JK kuwa mgombea mwenza wake.Kwa maana nyingine,mtu aliyekataliwa na kikundi kidogo (kikao cha CCM kilichpiga kura kumpata mgombea urais wa Zanzibar) anaweza kuwa Makamu wa Rais wa Watanzania milioni 40 na ushee pindi JK akishinda katika uchaguzi ujao.

Tumekuwa tukishuhudia teuzi za mabalozi wetu nje ya nchi,wenyeviti wa bodi za wakurugenzi wa taasisi mbalimbali,wakuu wa mikoa na wilaya na nafasi mbalimbali zinazojazwa kwa teuzi zinazofanywa na rais zikijazwa na "rejects"-watu walionyimwa ridhaa ya kuongoza na wananchi lakini wanaishia kuwa viongozi kwa mlango wa nyuma.Yaleyale ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa UWT,Hasna Mwilima.Kikundi kidogo katika jumuiya hiyo ya akinamama wa CCM kilimkataa,huku sababu kuu ikitajwa kuwa ni uongozi mbovu.Lakini siku chache baadaye,Rais akamteua mwanamama huyo kuwa Mkuu wa Wilaya.Busara kidogo tu zinaweza kubainisha kuwa kuwa mtu alokataliwa kuongoza UWT hawezi kuwa "rais wa wilaya" (DC) lakini kwa vile Katiba inamruhusu Rais kuteua yeyote amtakaye,analotaka liwe litakuwa.

Ni katika mazingira haya ndio maana tetesi kuwa Lowassa,Waziri Mkuu aliyelazimishwa kujiuzulu kutokana na ufisadi wa Richmond,atarejea madarakani pindi JK akishinda hapo Oktoba zinazidi kupata nguvu kwa vile Rais akiamua iwe na itakuwa.Na kwa vile Watanzania wanasifika kwa upole wao,hakutokuwa na "kelele" za kupinga uteuzi huo.

Nguvu anazopewa Rais kwenye Katiba hazimaanishi ajifanyie mambo anavyotaka bali ni kwa minajili ya kuwatumikia Watanzania kwa ufanisi.Lakini kwa upande mwingine,lawama zinaweza kuelekezwa kwa taasisi zinazomshauri Rais kuhusu teuzi mbalimbali (ikiwa ni pamoja na kuchunguza 'usafi' na uwezo wa wateuliwa watarajiwa) kwa sababu inaelekea kwa wao,kila jina linaloletwa na Rais ni 'safi'.Professionalism na ethics zinawekwa kando kwa minajili ya kumfurahisha mkuu wa nchi.

20 Jul 2010

SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete kueleza umma wa Watanzania kwamba ongezeko la magari na kero ya msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam ni dalili ya maisha bora, wanazuoni na wanasiasa nchini wameikosoa kauli hiyo na kuilaani vikali.

Wamesema kauli hiyo ni dalili tosha kwamba CCM imekosa mwelekeo halisi ya maendeleo ya nchi hivyo haistahili kuendelea kutawala kwa kuwa haina dira ya kubali maisha ya Watanzania.

Mhadhiri katika kitivo cha Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bw. Bashiru Ally aliliambia Majira kuwa ni aibu kwa kauli hiyo kutolewa na kiongozi wa nchi aliyebeba dhamana ya taifa zima.

Alisema ongezeko la fedha, majumba ya kifahari kwa watu wachache na foleni za magari jijini Dar es Salaam hakuwezi kuchukuliwa kama kipimo cha maisha bora kwa kuwa hivyo si vigezo vinavyopaswa kutumiwa kupima kiwango cha maendeleo katika nchi yoyote duniani.

Alisema maisha bora na maendeleo yoyote katika nchi yanapaswa kupimwa kwa kuzingatia ongezeko la watu, upatikanaji wa ardhi, siasa safi na uongozi bora mambo ambayo bado ni ya taabu na yanayozua migogoro mikubwa nchini.

"Kauli hii inanikumbusha kauli ya hayati Korimba (Horance), kuwa CCM haina dira wala mwelekeo, huwezi kupima maisha bora ya mwananchi wa Masasi au Kagera kwa kuangalia foleni za magari Dar es Salaam, laiti kama Mwalimu (Nyerere) na Sokoine (Moringe) wangekwepo leo kauli hii ingewapandisha presha," alisema Bw. Bashiru.

Alisema ni vema Rais Kikwete akaangalia uwiano wa ngezeko la foleni hizo na uboreshaji wa miundombinu hususan barabara, shule na mfumko wa bei za bidhaa na thamani ya fedha ambavyo vimekuwa vikiporomoka kwa kasi katika kipindi cha uongozi wake.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bw. Freeman Mbowe, alisema kauli hiyo inaonesha jinsi serikali ya CCM isivyokuwa na jambo la kujivunia kwa wananchi katika kipindi chote cha miaka mitano iliyopita.

Alisema kimsingi msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam inasababishwa na ukosefu wa miundombinu ambayo chimbuko lake ni uongozi mbovu ulioko madarakani.

Alisema kinachotokea Dar es Salaam si kuboreka kwa maisha ya wananchi bali ni ongezeko la tabaka kati ya walionacho na wasio nacho hasa masikini walioko vijijini hali ambayo inasababisha ongezeko la watu mijini wasiokuwa na ajira wala mahali pa kulala.

"Foleni za magari Dar es Salaam si dalili ya maisha bora, na kama ukifanya utafiti utagundua kuwa foleni kubwa ni katika baadhi ya barabara zinazoelekea kwa matajiri wachache ambao baba, mama na watoto kila mmoja ana gari lake, sasa maendeleo ya watu wachache huwezi kuyatumia kupima kiwango cha maisha ya Watanzania wengine," alisema Bw. Mbowe.

Naye Mhadhiri Mwandamizi katika Kitivo cha uchumi na Biashara Chuo Kikuu cha Dar Salaam, Profesa Humphrey Moshi, alisema si sahihi kwa rais wa nchi kupima maisha ya Watanzania wachache wengi kwa kutumia mfano wa watu wachache wenye uwezo wa magari.

Alisema licha ya ukweli kuwa ongezeko la idadi ya watu wanaomiliki magari linaweza kutumika kuonesha ongezeko la kipato kwa wananchi lakini haikuwa sahihi kwa kiongozi wa nchi kupima maisha ya Watanzania kwa kuangalia wenye uwezo wachache walioko Dar es Salaam.

Alisema Dar es Salaam ni mji wa kibiashara wenye viwanda, mashirika na taasisi karibuni zote za serikali ambazo katika shughuli za kawaida zinahitaji usafiri wa magari, hivyo kuna uwezekano kuwa foleni kubwa husababishwa na magari ya taasisi, hizo lakini si mabadiliko ya maisha ya Watanzania.

"Magari mengi si ya watu binafsi, idara nyingi za serikali ziko hapa, kuanzia ikulu, bunge, wizara zote, taasisi binafsi, mashirika ya dini, viwanda na wafanyabiashara mbalimbali ambao ndio wamiliki wa magari, sio wananchi wa kawaida, sasa huwezi kusema kuwepo kwa foleni za magari ya idara hizi ni maisha bora kwa wananchi," alisema Prof. Humpherey.

Alisema maendeleo yanapimwa kwa kuangalia maisha ya jumla si ya mwananchi mmoja mmoja, ikiwa ni pamoja na kuangalia uwezo wa kuzalisha mali wa wananchi, thamani ya fedha, kiwango cha elimu na uimara wa sekta za viwanda na kilimo, na si kuangalia msongamano wa magari yaliyokosa barabara za kupita.

Akihutubia wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam katika mkutano wa kuwatambulisha wagombea urais, mgombea mwenza na Rais wa Tanzania Visiwani katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Rais Kikwete alisema ongezeko kubwa la magari na kusababisha msongamano wa magari ni mijawapo ya dalili za maisha bora.

CHANZO: Majira

19 Jul 2010

Foleni za magari ni maisha bora-JK
Monday, 19 July 2010 05:33
*Asema watakakamatwa kwa rushwa CCM haitawatetea

Na Peter Mwenda

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Kikwete ametamba kuwa chama hicho kwa miaka mitano iliyopita kimeinua maisha ya Watanzania akitoa mfano wa Jiji la Dar es Salaam kuwa foleni za magari zinatokana na wananchi kuwa na maisha bora.

Alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na CCM Mkoa wa Dar es Salaam kwa ajili ya kumpongeza Rais Kikwete kuchaguliwa kuwa mgombea pekee wa urais kwa asilimia 99.16, Dkt. Ali Mohammed Shein kuchaguliwa kuwa mgombea wa Urais Zanzibar na Dkt. Mohamed Gharib Bilal kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais.

"Hapa Dar es Salaam taabu ya msongamano wa magari inaonesha hali ya maisha ni bora, sasa tunahangaika jinsi ya kuondoa msongamano, kuanzia mwakani tutaanza kujenga barabara za juu," alisema Rais Kikwete.

CHANZO: Majira

Hivi kumbe maendeleo yanapimwa kwa msongamano na foleni za magari!Vipi kama foleni hizo ni matokeo ya mindombinu isiyoendana na mahitaji?Vipi kama wingi wa magari hayo ni matokeo ya ufisadi-aidha ya wizi na ubadhirifu wa mali ya umma na ukiukwaji wa taratibu mbalimbali eg ukwepaji kodi stahili bandarini na TRA?

Na je,foleni hizo za magari zinaendana vipi na idadi ya Watanzania wanaumudu mlo wao kila siku?Je wingi wa magari unaendana na idadi ya wamiliki wa magari?Nauliza hivyo kwa sababu wengi tunafahamu kuwa wakati kuna wachache wenye msururuwa magari na majumba ya kifahari kuna wengine wengi tu ambao hata fedha ya kununulia baiskeli hawana,achilia mbali uhakika wa nauli ya daladala.

Na je inawezekana Rais hajafahamishwa na wasaidizi wake kuhusu ongezeko la 'TZ ELEVEN' i.e. watembea kwa miguu ambao hawafanyi hivyo kama sehemu ya mazoezi ya viungo mbali ukosefu wa nauli?Au hawajamwambia kuhusu idadi ya 'mikweche' ambayo licha ya kusababisha foleni inachangia uwezekano wa ajali?Na inawezekana pia wasaidizi wake hawajamfahamisha kuwa mingi ya 'mikweche' hiyo iko barabarani baada ya wamiliki kutoa 'kitu kidogo' kwa askari wa usalama barabarani?

KAMWE MAJIBU RAHISI KWENYE MASWALI MAGUMU HAYAWEZI KULETA UFUMBUZI WA MATATIZO YETU!SINTOSHANGAA TUKISKIA HATA KUONGEZEKA KWA WENYE VITAMBI (INCLUDING WALE WENYE VITAMBI VYA KWASHAKOO) NAKO NI DALILI YA MAISHA BORA!

20 Jun 2010

RAIS Jakaya Kikwete ameliponda Shirika la Haki Elimu kwa kusema ni waongo, wazushi na wanafiki.

“ Ukweli siku zote hujitenga na uongo Haki Elimu ni waongo, wazushi na wanafiki wanapodiriki kuwatangazia umma wa watanzania eti kuna uhaba wa nyumba za walimu zipatazo 22,000 nchini na kwamba Serikali ya Nne kwa kipindi chote cha utawala wake kimemudu kujenga idadi ya nyumba za walimu zipatazo 300 tu haya ni matusi kwetu….kweli akutukanae hakuchagulii tusi…..watu wazima ovyoo” amesema Rais

---------------------------------------------------------------------------------------------------------
RAIS Jakaya Kikwete amesema Serikali ya Awamu ya Nne imetekeleza kwa vitendo ahadi zote za uchaguzi ilizowaahidi wananchi ukiwamo ujenzi wa miradi mikubwa mitatu ya barabara kuu za mkoa wa Rukwa zenye urefu wa kilometa 657.5 kwa kiwango cha lami.

“Tuliyowaahidi wananchi tumeyatekeleza kwa hakika tumefanikiwa vizuri sana katika ujenzi wa barabara, elimu na afya,”

Alisema hayo juzi wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kiwanja cha michezo cha Nelson Mandela mjini hapa, huku akishangaa wanaobeza safari zake za nje ya nchi.

Alisema watu hao hawamnyimi usingizi hata kidogo na alihoji kama asingekwenda Marekani kuonana na Rais George Bush (mstaafu) nani angefadhili ujenzi wa mradi mkubwa wa barabara ya Tunduma – Laela – Sumbawanga yenye urefu wa kilometa 224.5 kwa kiwango cha lami.

LAKINI NI MAJUZI TU GAZETI LA HABARI LEO LILIMNUKUU RAIS AKISEMA YAFUATAYO

AHADI ambazo hazijatekelezwa na Serikali ya Awamu ya Nne zitatekelezwa katika Bajeti hii ya mwaka 2010/11, imeelezwa.

Akizungumza jana mjini hapa katika kikao cha kazi na wakuu wa mikoa na wa wilaya pamoja na makatibu tawala wa mikoa yote Tanzania Bara, Rais Jakaya Kikwete aliwataka viongozi hao kusimamia shughuli za Serikali kikamilifu.

Aliwataka kutokwenda likizo katika kipidi hiki cha kuelekea uchaguzi na wasimamie kazi kama wanavyofanya wakati wote.
Rais Kikwete alisema katika kipindi cha miaka mitano tangu Serikali yake iingie madarakani mengi waliyoahidi yametekelezwa.

“Juzi kabla ya Bajeti hata kwenye Baraza la Mawaziri, tulizungumzia ahadi zetu na nyingi tumeshazitekeleza, lakini zilizobaki na majukumu tuliyojipangia kwa miaka yote hii tutatekeleza katika Bajeti hii … tulipoingia mwaka wa kwanza, tulitekeleza ya Awamu ya Mzee Mkapa (Rais mstaafu Benjamin) sasa tunaendelea na kutekeleza yetu,” alisema.

SASA KAMA AHADI ZOTE ZIMESHATEKELEZWA,HIZO ZINAZODAIWA KUTEKELEZWA KATIKA BAJETI HII YA 2010/11 NI AHADI ZIPI TENA?

NA SOTE TUNAKUMBUKA THE MOTHER OF ALL PROMISES,ILE YA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.HIVI KWELI RAIS KIKWETE ANATAKA KUTUAMBIA KUWA KILA MTANZANIA HIVI SASA ANA MAISHA BORA?

KADHALIKA JK ALITAMKA BAYANA KUWA ANAWAFAHAMU WALA RUSHWA KWA MAJINA NA KUSEMA ANAWAPA MUDA WAJIREKEBISHE VINGINEVYO ANGEWACHUKULIA HATUA.JE RAIS ANAPOTUAMBIA KUWA AHADI ZOTE ZIMESHATEKELEZWA ANAMAANISHA TATIZO LA RUSHWA NALO LIMEKWISHA?AU ANAMAANISHA WALA RUSHWA ALOSEMA ANAWAFAHAMU KWA MAJINA WAMEAMUA KUJIREKEBISHA?

-----------------------------------------------------------------------------------------------
RAIS Jakaya Kikwete amewataka wanaume wasiwe 'mafataki', wawaache watoto wa kike wasome.

Kikwete amesema, wanaume wanapaswa kuwafuata wanawake wakubwa wenzao na si watoto, na kwamba, wanawake wapo wengi.

“Ninachowaomba wanafunzi wa kike washuhulike na masomo, mambo ya mimba yaacheni… kina baba waacheni watoto wa shule kina mama watu wazima wamejaa tele acheni kupiga ufataki” Rais Kikwete ameyasema hayo wakati anajibu swali la mtoto Rehema Abbas wa Dar es Salaam.

HAYA NI MAENDELEO MAPYA BAADA YA KIKWETE HUYUHUYU KUSEMA YAFUATAYO HIVI KARIBUNI

JK: Mimba kwa wanafunzi ni kiherehere chao

Monday, 07 June 2010 07:33
Rais Jakaya Kikwete amesema matukio ya mimba kwa wanafunzi wa kike nchini yanasababishwa na viherehere vya wanafunzi wenyewe.

Aidha, Rais Kikwete amekiri kwamba matukio ya mauaji ya vikongwe pamoja na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), yanalidhalilisha taifa.

Rais Kikwete alitoa kauli hizo katika kijiji cha Kisesa wilayani Magu jana wakati akihutubia wananchi kwenye ufunguzi wa mashindano ya ngoma kwa kabila la Wasukuma; ngoma ambazo zinajulikana kama 'Bulabo'.

" Kila anayepata Ukimwi anaufuata mwenyewe na wengine ni viherehere vyao; kwa mfano watoto wa shule," alisema Rais Kikwete wakati akijibu risala ya Mkurugenzi wa Makumbusho ya Bujola, Fadha Frasince Sandhu, ambaye alisema ujumbe wa mashindano hayo mwaka huu ni vita dhidi ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete, suala la zinaa kwa bianadamu, siyo la lazima hivyo binadamu anaweza kujizuia ama kujikinga kwa kutumia kondomu.
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.