14 Oct 2010


Awali nilitundika taarifa ifuatayo baada ya kuiona huko Jamii Forums kabla ya post husika kufutwa.Mzembe mmoja akanitumia email akidai mie ndio mtunzi wa taarifa hiyo.Mchumia tumbo huyo alikuwa na kila sababu ya kukasirika just like mafisadi wanavyokasirika kusikia uwezekano wa Dokta Slaa kuingia Ikulu baada ya Uchaguzi hapo Oktoba 31.Anyway,naiwasilisha tena kama ilivyo (lengo sio kumridhisha huyo mzushi aliyenituhumu bali kusambaza ujumbe husika)

Taarifa ya Siri-Mikakati ya Kuiba Kura Inavyoendelea
From:
From:
To Journalists   


To:Yahya Mkombe ; Yahya Charahani ; Waziri Kindamba ; Tobias Nsungwe; Thisday [The Editor] ; Theodatus Muchunguzi ; Tanzania Daima ; Tanzania Daima ; Sweya ; Stephen Ernest Kasambo ; Stella Mchiwa ; Stanslaus Kirobo ; Sosthenes Paulo Mwita ; Sofia Machagga ; Siyovelywa Hussein; Sisa Suzy ; Simon Mkina ; Simbaulanga ; Siahanna; Sherbanu Mussa ; Sauli Giliard ; Sarah Mwaga ; Sani; Samson Mwigamba ; Salehe Mohamedi ; Said Michael ; Saed Kubenea ; Rusibamayila ; Ruhazi Ruhazi ; Rookie ; Robert Nyimbo ; Richard Lupembe ; Reginald Simon Miruko ; Ramadhani Semtawa; Raia Mwema ; Prudence Karugendo ; Privatus Karugendo ; Peter Nyanje ; Patien Celkanah ; Paschally Mayega ; Othman Juhudi; Oscar Mkoma ; Oneo Yolazi ; Omari Kaseko ; Omar; Nthelezi Nesaa ; Nombo ; Nkwanzi Nkuzi ; Nikita Naikata; Ngwada ; Ngowe ; News Editor [Thisday] ; News [The Citizen]; Ndyesu ; Ndimara Tegambwage ; Ndesanjo Macha ; Nathan; Nadra Mussa ; Mzee Mwanakijiji ; Mwitete ; Mwesigwa; Mwenyekiti wa Baraza ; Mwankemwa ; Mwanahalisi; Mwachapite ; Mutahungurwa ; Musa Ngarango ; Mumba Mabu; Mum China ; Mtoha ; Matinde Nyagonda ; Mary Fwaja; Martin Malera ; Makwaia wa kuhenga ; Majid Mjengwa ; Mabala wa Mabalaa; Lusungu Hemed ; Lula wa Ndali Mwanzela ; Lukawe ; Ludger Bernard Nyoni ; Lucy Ngowi ; Lucy Mchiwa ; Leo Jasson ; Lawrence Kilimwiko; Laumbe ; Latrix ; Kyembe ; Kwariko Mahmoud ; Kumburu ; Kobelo ; Kiwango ; Kitambo Robert: Padre ; Kililui; Kiangosekazi wa nyoka ; Kevin Makyao ; Kaselema Luhanga; Kambi Mbwana ; Kally ; Kagomba ; Kady Fanny; Julius Samwel ; Joseph Petro ; Joseph Moses Ndumbaro ; Joseph Mgullo; Joseph Kulangwa ; Joseph Kulagwa ; Johnson Mbwambo ; Johnson Mbwambo ; John Mnyika ; Jeff Msangi ; Ipimilo ; Innocent Mwesiga; Ibrahim Lipumba ; Hoja ; Hilda Super ; Herry Gasp ; Henry Kimani ; Hellen [Mama] ; Haruna Sauko Mohamed ; Haruna Sauko Mohamed; Haruna Sauko Mohamed ; Happines Katabazi ; Halifa Shabani ; Hakielimu ; Habibu Miradji ; Habib Miradji ; Godfrey Mogellah ; Gloria William; Gervas Zombwe ; Freddy Macha ; Fred Macha ; Financial Times; Financial Times ; Ezekiel Kamwaga ; Evarist Chachali Uskochi ; Endakig ; Emmanuel Elias ; Elias Mhegera ; Edward Kinabo; Edison Kamukara ; Duhu Daniel ; Deusdedit Jovin ; Deus Bugaywa ; Deogratius Temba ; Dawson Mongi ; David Mhando ; Dattani ; Daniel Mwaijega ; Coster ; Chesi Mpilipili ; Che Chenjah; Charles Semiono ; Charles Nkwabi ; Charles Mullinda ; Charles Kayoka; Charles G. Mnyeti ; Changamoto ; Changamoto ; Chacha Nyakega ; Catherine Justus ; Carol Njiro ; Bwire ; Bwire; Business Times ; Bollen Ngetti ; Beatrice Kawanara ; Beatrice Kallaghe ; Balinangwe Mwambugu ; Bai ; Ayub Rioba ; Asubuhi Njema; Ansbert Ngulumo ; Angetile Osiah ; Angela Semaya; Angel Tenga ; Amina Emmanuel ; Amani ; Alloyce Komba; Alli Gilla ; Alfred Chonya ; Aghan Daniel ; Adam Lusekelo; Absalom Kibanda ; Abdulhamid Njovu ; Abass Juma Msahaury 
Kama nilivyoipokea nami nawatumia. Napenda kuwajulisha mikakati michafu ya kupora na kuzuia maamuzi ya umma yanayofanywa na ccm kwa uratibu wa usalama wa taifa. Baada ya kubaini dalili za kuanguka vibaya katika uchaguzi wa mwaka huu idara ya usalama wa taifa imeandaa mikakati ya kuiba kura ili kuzuia CHADEMA msiingie ikulu. Mikakati hii inaeleweka vizuri kwa tume ya taifa ya uchaguzi ambayo inashirikiana bega kwa bega na idara ya usalama wa taifa kumtengenezea jk ushindi bandia wa 80%.
Wana hakika watanzania watagundua wizi huo na watakataa matokeo ndiyo maana kwanza waliwatumia viongozi wa dini waliotembelea makao makuu ya CHADEMA wawasihi CHADEMA wakubali matokeo yatakapotangazwa na juzi wamelitumia jeshi kutisha wananchi watakaoamua kupinga matokeo ya kupikwa yanayoandaliwa na NEC/Usalama wa taifa. MAJID KIKULA ambaye ni Government Security Officer ndiye mratibu wa zoezi la kuiba kura, ni mtaalamu aliyebobea katika kazi za aina hii aliratibu vizuri zoezi kama hilo mwaka 2005.
Pia mwaka 2007 alitumwa kenya kwenda kumsaidia Kibaki kupora ushindi wa Odinga. Kikula ww.yahooanatumia muda wake mwingi hivi sasa ofisi za tume ya uchaguzi kwa ajili ya uratibu wa uvurugaji daftari la kudumu la wapiga kura akiifanya kazi hiyo kwa karibu na baadhi ya watendaji wa NEC na maafisa kadhaa wa usalama wa taifa kutoka Kurugenzi ya IT ya idara ya Usalama (DITA) ambao wako ndani ya NEC kwa zaidi ya miezi sita sasa, nitawapatia majina yao.
Pia kuna vijana wataalamu wa IT waliochukuliwa kutoka maeneo mbalimbali wamepewa nyumba upanga mtaa wa Undali. Shughuli kubwa wanayofanya ni kuandaa utaratibu wa ku-access remotely daftari la kudumu la wapiga kura. Hawa wanafanya kazi chini ya SALVA RWEYEMAMU na MINDI KASIGA kutoka Kurugenzi Ya Mawasiliano Ikulu. Wapo vijana kadhaa leo nawapa majina ya wawili; MAHARAGE CHANDE ambaye ni mfanyakazi wa VODACOM na EDGAR MASATU wanafanya kazi kwa karibu na NZOWA wa Idara Ya Usalama ambaye ndiye aliyeratibu shambulio la kumwagiwa tindikali KUBENEA. Pia kuna kundi linalojumuisha wataalamu wa printing wa kiwanda cha uchapaji cha usalama wa taifa kilichopo MALINDI ambao hivi karibuni walikuwa mjini TANGA kwa semina fupi ya jinsi ya kughushi kura kupitia fake ballot paper, timu hii inaongozwa na Ndg. SINYAU.
Kwa hiyo utaona kwamba imeandaliwa mikakati mingi kuufanikisha uovu huo ili mmoja ukikwama basi mwingine utatumika ila wameamua ni lazima JK ashinde kwa 80%.
Ndani ya Idara Ya Usalama Wa Taifa maafisa wengi wamechoshwa na uongozi mbovu wa CCM hivyo wanataka mabadiliko ya uongozi idara imechukua hatua kadhaa kuhakikisha maafisa wote wa idara wanampigia kura JK, wote wameagizwa kuwasilisha vitambulisho vyao vya kupigia kura ili vinakiliwe namba ili atakayepigia upinzani afukuzwe kazi baada ya uchaguzi.
Fuatilieni kwa karibu haya niliyowaeleza nimeyapata kwa nafasi yangu ndani ya TISS. Huyu KIKULA mfuatilieni kwa karibu ni hatari. HAKIKISHENI DUNIA NA WATANZANIA WOTE WANAJUA MAPEMA HILA HIZI. Jambo la kujiuliza maafisa Usalama Wa Taifa wanafanya nini ndani ya Tume Ya Uchaguzi wakati huu
.

1 comment:

  1. Kaka Chahali, Kuna habari imekosekanasana hapo kkwenye display yako kama inavyonesha baada ya maneno haya,,,,
    Taarifa ya Siri-Mikakati ya Kuiba Kura Inavyoendelea
    From:

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.