19 Jul 2011




Kama kuna kosa ambalo Watanzania watalijutia kwa muda mrefu sana ni lile walilofanya mwaka 2005 na kisha kulirudia mwaka jana kumchagua Jakaya Kikwete kuwa Rais wa nne wa Tanzania.Tusiume maneno,mengi ya matatizo yanayoikabili nchi yetu kwa sasa ymesababisha,yanasababishwa au yamechangiwa au yanachangiwa na ubabaishaji wa Kikwete.

Ni nani mwenye akili timamu asiyefahamu kuwa wakati kelele dhidi ya ufisadi zinaelekezwa kwa "mapacha watatu" waliobaki wawili (ie Lowassa na Chenge,na Ristam aliyejiuzulu),Kikwete ni sehemu muhimu kabisa ya tuhuma zinazoelekezwa kwa wanasiasa hao.Hapa simaanishi kuwatetea mafisadi hao bali ninachojaribu kupigia mstari ni ukweli kwamba Kikwete hana tofauti na Lowassa,Chenge au Rostam.Na hilo halihitaji ufafanuzi.Yeye anajua,mapacha watuatu waliobaki wawili wanajua,na kila Mtanzania mwenye akili tiammu anajua.Kwanini hadi leo Kikwete bado ni Rais wetu ni swali gumu kulijibu just like lile la kwanini alichaguliwa mara ya kwanza mwaka 2005 na baadaye 2010 ilhali wanamjua walikuwa wanatambua bayana kuwa hana sifa za kushika wadhifa huo mkubwa kabisa katika nchi yetu.

Anyway,lengo la makala hii sio kujadili ubabaishaji wa Kikwete katika utendaji kazi wake bali lengo ni kukemea kwa nguvu kubwa uhuni uliofanywa na Kikwete wa kufanya harusi ya mdogo wake kwenye Ikulu ndogo ya Bagamoyo.Hivi kwa kuwa Rais,Kikwete anadhani kuwa Watanzania wametoa urais kwa ukoo wake mzima?Kwanini asikodi ukumbi kwa fedha zake kisha akamfanyia sherehe mdogo wake?

Kama huelewi kwanini ninalamika,Ikulu iwe ile ya Magogoni au hizo ndogo za wilayani na mikoani ni mahala patakatifu-kama alivyowahi kusema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.Si mahala ambapo kila Tom,Harry and Dick anaweza kufanya atakalo.Lakini licha ya utakatifu huo wa Ikulu,ifahamike kuwa mahala hapo panaendeshwa kwa fedha za walipakodi.Kwa mantiki hiyo,kufanyia sherehe mahala hapo ni sawa na kuwabebesha gharama Watanzania kwa ajili ya harusi ya ndugu wa Kikwete.Sidhani hata waliompigia kura mwaka jana au 2005 walitamani kuona kura waliyompigia Jakaya inageuzwa kuwa mithili ya kuupigia kura ukoo wake mzima.

Huu ni uhuni unaopaswa kukemewa vikali.Rais anaweza kuzurura nje ya nchi atakavyo (inaelekea kama hakuna namna ya kumwelewesha kuwa safari zake za mara kwa mara nje ya nchi ni mzigo mkubwa kwa Watanzania) lakini kamwe tusiruhusu nafasi ya Urais ikageuzwa kuwa kama cheo cha kifamilia.

Madhara ya kumwacha Kikwete aendelee na madudu yake ni kwamba anaweza kumaliza muda wake hapo 2015 na kuiacha Tanzania ikiwa jina tu-haina maadili,haina raslimali,na kibaya zaidi,nafasi ya urais ikaishia kuwa na heshima ndogo kuliko ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa.

PICHA: Kwa hisani ya Global Publishers

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.