18 Jul 2011


BRILLIANT BUDGET SPEECH, HONGERA SANA! 
Nd. Mnyika,
Nimesoma hotuba yako bungeni hapa chini kwa makini sana na kupata faraja kubwa – hongera nyingi, na kama wasemavyo wataliano – BRAVISSIMO!  Pia nimefurahi zaidi baada ya kuona baadhi ya yale ninayoandika na kushauri, hususan maswala ya urani (uranium), kupewa hisa watanzania, STAMICO na TPDC, maswala ya kulinda na kuhufadhi vizuri mazingira ya nchi wakati wa uchumbaji wa madini, haja ya kuchunguza na kubadilisha mikataba mibovu ya madini ikiwa ni pamoja na ulaghai wa kampuni kama Williamson Diamonds, TanzaniteOne, uzembe uliofanyika kuingia mikataba mibovu ya gesi asilia n.k., haya mambo yote umeyachambua ipasavyo na hata kwenda mbele zaidi kwa kuweka bayana baadhi ya mambo mengine ambayo mimi kama mtaaalamu sikuwa nayafahamu kuwa yanatendeka Tanzania hivyo kuweza kunipa habari ambazo zitanisaidia kuyachambua kitaalamu, tena kwa kina. Nimepaka rangi baadhi ya sehemu kwenye hotuba yako kuonyesha yale ambayo yamenigusa zaidi na mambo ambayo niliwahi kuyakemea na kusisitiza yachunguzwe na kubadilishwa kwa muda mrefu.
Nadhani utakuwa umesoma barua zangu za hivi karibuni zinazohusu maswala ya madini nchini Mongolia na Sudani Kusini – ziko hapa. Ni matumaini yangu mtazichambua barua hizi pamoja na wenzako wa kambi ya upinzani Bungeni na muangalie namna gani mnaweza kuhakikisha yale muhimu kwa taifa letu yanaweza yakatekelezwa Tanzania. Ndani ya barua hizo utaona pia maoni yangu kuhusu mauaji ya Tarime uliyoniuliza hapo awali ingawa msimamo wangu kuhusu hili jambo niliwahi kuzungumzia vikali kwenye baadhi ya barua zangu zikiwezo hizi hapa: 1 (soma kuhusu mamillionea wa kimya kimya - Silent Millionaires – walivyowadanganya watu wetu Bulyanhulu. Baadhi ya hawa mamillionea ni/au walikuwa wafanyakazi wa serikali). Soma pia hapa 2, pamoja na hapa 3.
Pia hapa chini nakutumia tovuti za makala kadhaa ambazo nadhani ni muhimu kuzisoma hasa baada ya kuona kuwa ni mambo ambayo uliyazungumzia kwenye hotuba yako na mimi pia nimekuwa nikisisitiza kwa muda mrefu yafanyiwe kazi na serikali. Ni matumaini yangu utaendela na msimamo wako imara wa kuibana serikali ifanye marekebisho pale ambapo inaonekana kuwa rasilimali za taifa haziwanufaishi watanzania, na wale waliongia nchini kama wawekezaji wa kigeni, na hata raia na makampuni yetu ya Tanzania, wanakiuka na kuvunja sheria za sekta ya madini. Ni muhimu makosa makubwa tunayoyafanya kwenye sekata ya madini, gesi asilia na petroli yarekebishwe, tena haraka sana. Kama ulivyoeleza kwenye hotuba yako, hakuna sababu yeyote ya msingi watanzania waishi kwenye umaskini wa kutupwa huku wakiwa na utajiri mkubwa wa madini kama tulionao, utajiri ambao serikali yetu inautoa, hata niseme, kuutupa kwa wageni – hii si sahihi hata kidogo. Nitashukuru kama utakuwa unaniarifu mara kwa mara maendeleo ya jitihada zenu kufanikisha azma hii.
Ahsante, na pongezi nyingi kwa ujasiri na uimara wako Bungeni.
Shaaban
Moscow, Urusi.     

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.