28 Aug 2013

Woman caught with Dhs3 million of drugs blames husband for...

Mwanamke wa Kitanzania aliyekamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akiwa na madawa ya kulevya yenye thamani ya Dirham milioni tatu (takriban shilingi bilioni 1.3 za Kitanzania) amedai kuwa alifanywa 'punda' na mumewe.

Mwanamke huyo ambaye hata hivyo hajatajwa jina alikamatwa na kilo 3 za 'unga' (cocaine) akitokea nchini Brazil, ambapo alipita transit Dubai, kwa madhumuni ya kuja Tanzania.

Kwa mujibu wa Polisi wa Dubai, mwanamama huyo alieleza kuwa alitibuana na mumewe, na mumewe akaamua kumpeleka Brazil kwa mapumziko, na wakati anarejea kutoka huko alikabidhiwa suitcase ambayo baadaye iligundulika kuwa ina madawa hayo ya kulevya.

Polisi hao wanasema kilichopeleka mwanamke huyo kushtukiwa na hali yake ya kutia mashaka wakati akiwa airport hapo.

Kesi yake imewasilishwa kwa waendesha mashtaka kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria

iMETAFSIRIWA KUTOKA TOVUTI YA 7 Days in Dubai



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.