
Baadhi ya simu za kisasa zaidi kwa mfano Samsung Galaxy S5 tayari zina app hiyo, na hakuna haja ya ku-download upya.

Hatua ya kwanza ni ku-download Google Cloud Print kisha 'add new printer'

Baada ya kuchagua 'add new printer' utapalekwa kwenye ukurasa wa Google wa Cloud Print, au kwenye akaunti yako ya Google iwapo hujasaini.

Japo ukurasa wa Cloud Print haupo bayana sana kimatumizi, zoezi la ku-'set up' si gumu. Fata maelekezo kutoka kwa printer yako,iwe ni offline model au Cloud ready model.

Sasa nenda kwenye faili unalotaka ku-print kutoka katika simu yako, na utaona chaguo la kulichapisha.
Iwapo unahitaji ku-print SMS,njia nyepesi ni kutumia app iitwayo SMS Backup& Restore. App hii ina-backup SMSzako kwenye simu yako,email au huduma za 'cloud' kama vile Dropbox na Google Drive. Ukisha-backup,nenda mahala ulipohifadhi SMS hizo,kisha chagua 'print'

CHANZO: Andoidpit
Natumaini makala hii itakuwa na msaada na manufaa kwako pindi utapohitaji kuchapisha dokumenti au SMS zako. Usikose makala nyingine za teknolojia katika blogu hii,ambazo utazipata kirahisi kwa kubonyeza hapo juu kwenye blogu palipoandikwa TEKNOLOJIA
0 comments:
Post a Comment