
Naomba kukiri hadharani kwamba katika mitandao yote ya jamii, Twitter ndio namba wani kwangu. Mtandao huo sio tu umeniwezesha kufahamiana na watu muhimu kabisa, bali pia ni moja ya vyanzo vyangu vikuu vya habari na uelewa. Nitaanda makala maalum ya kukufahamisha msomaji jinsi ninavyoitumia Twitter kwa ufanisi, na jinsi inavyoweza kukidhi mahitaji yangu.
Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekuwa wakiilaumu kwa mapungufu wanayokutana nayo. Kwa mfano, nimesikia kwa watu kadhaa wakiilaumu Instagram kwamba imegeuka uwanja wa matusi. Jamani, tatizo sio Instagram, Twitter, Facebook au mtandao mwingine wowote ule wa kijamii bali tatizo ni mtumiaji. Kama ilivyo mtaani, ukikaa kijiweni utaambulia ya kijiweni. Ukitumia muda wako mwingi maktaba, utaweza kupata vya kupatikana maktaba. Uki-hang out na walevi, well, twajua ni utapata. Ukipendelea kuwa na watu wa Neno la Mungu, utapata Neno la Mungu. Ukijiweka karibu na wasomi, utafaidika na uelewa (knowledge). Ukifuatilia vyombo vya habari, utahabarika.
Msanii maarufu wa muziki na filamu nchini Marekani, Tyrese Gibson, anatoa ushauri huu
Employees hanging out with employees is just going to further your career as an employee. You start hanging out with bosses, you eventually become one. (Mwajiriwa anayetumia muda mwingi na waajiriwa wenzie wa kawaida, atadumisha ajira yake kama mwajiriwa wa kawaida tu.Ukianza 'kujichanganya na mabosi, basi nawe waweza kuishia kuwa bosi)

Naam, watu unaojihusisha nao wanachangia kukufanya kuwa mtu wa aina flani. Na kanuni hiyo ina-apply pia kwenye mitandao ya jamii. Uki-follow watu wenye kuendekeza matusi au majungu, utaishia kukutana na matusi au majungu.
Basi hapa chini ninakupatia orodha ya maprofesa waliobobea katika fani zao ambao wapo Twitter, na waweza kuwa-follow au kuwaingiza katika LIST yako (nitaandaa makala ya jinsi ya kutumia
Uongozi (Leadership)
Bill George, Harvard Business School, @Bill_George
Adam Grant, Wharton School of Finance, @AdamMGrant
Monique Valcour, EDHEC, @MoniqueValcour
Karl Moore, McGill University, @ProfKJMoore
Gianpiero Petriglieri, INSEAD, @GPetriglieri
Stew Friedman, Wharton School of Finance, @StewFriedman
Sir Cary Cooper, Lancaster University, @ProfCaryCooper
CV Harquail, Howe School of Business, @CVHarquail
Bret Simmons, University of Nevada-Reno, @DrBret
Mark Esposito, Harvard University, @Exp_Mark
Ian McCarthy, Beedie School of Business, @Toffeemen68
Gautum Mukunda, Harvard Business School, @GMukunda
Thomas Roulet, University of Bath, @ThomRoulet
Terri Griffith, Santa Clara University, @TerriGriffith
Patrick J. Murphy, DePaul University, @ProfPJM
Ubunifu (Innovation)
Richard Florida, Rotman School of Management, @Richard_Florida
Clayton Christensen, Harvard Business School, @ClayChristensen
Calestous Juma, Harvard University, @Calestous
Alf Rehn, Åbo Akademi University, @AlfRehn
Marcel Bogers, University of Southern Denmark, @Bogers
Cyndi Burnett, Buffalo State College, @CyndiBurnett
Diego Rodriguez, Stanford University @Metacool
Bob Sutton, Stanford University, @Work_Matters
Karim R. Lakhani, Harvard Business School @KLakhani
Tim Kastelle, University of Queensland, @TimKastelle
Tor Gronsund, University of Olso, @Tor
Frank Piller, RWTH Aachen University, @MassCustom
Tina Selig, Stanford University, @TSeelig
Bill Fischer, IMD Business School, @Bill_Fischer
Gary Hamel, London Business School, @ProfHamel
Mikakati (Strategy)
Michael Porter, Harvard Business School, @MichaelEPorter
Estelle Metayer, McGill University, @Competia
Ioannis Ioannou, London Business School, @iioannoulbs
Rita McGrath, Columbia Business School @RGMcGrath
Teppo Felin, University of Oxford, @TeppoFelin
Roger Martin, Rotman School of Management, @RogerLMartin
Peter G. Klein, University of Missouri-Columbia, @PeterGKlein
Mislek Piskorski Harvard Business School, @MPiskorski
Kevin Boudreau, London Business School, @KevinJBoudreau
Sheen S. Levine, Columbia University, @SSLevine
Freek Vermeulen, London Business School, @Freek_Vermeulen
Marion Debruyne, Vlerick Business School, @MarionDebruyne
Robin Teigland, Stockholm School of Economics, @RobinTeigland
Dan Elfenbein, Washington University, @OrgStratProf
Sydney Finkelstein, Tuck School of Management, @SydFinkelstein
Watajwa wa heshima (Honorable Mentions)
Terry Linhart, Bethel College,@ TerryLinhart
Teresa Amabile, Harvard Business School @TeresaAmabile
Terri Scandura, University of Miami, @TerriScandura
Michael Roberto, Bryant University, @MichaelARoberto
Nadia Kazim, Higher Colleges of Technology @Nadiakazim
Wasomi hawa mahiri duniani ni visima vya uelewa (knowledge). Na kama sote tunavyoelewa, ili uweze kuchota maji kutoka katika kisima shurti uende kisimani.
Basi endelea kutembelea blogu hii kwa habari mbalimbali, ikiwa ni pamoja na hizi za teknolojia. Bonyeza TEKNOLOJIA hapo kwenye menu juu upelekwe moja kwa moja kwenye habari hizo.
0 comments:
Post a Comment