Showing posts with label SOCIAL MEDIA. Show all posts
Showing posts with label SOCIAL MEDIA. Show all posts

21 Aug 2014

Naomba kukiri hadharani kwamba katika mitandao yote ya jamii, Twitter ndio namba wani kwangu. Mtandao huo sio tu umeniwezesha kufahamiana na watu muhimu kabisa, bali pia ni moja ya vyanzo vyangu vikuu vya habari na uelewa. Nitaanda makala maalum ya kukufahamisha msomaji jinsi ninavyoitumia Twitter kwa ufanisi, na jinsi inavyoweza kukidhi mahitaji yangu.

Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekuwa wakiilaumu kwa mapungufu wanayokutana nayo. Kwa mfano, nimesikia kwa watu kadhaa wakiilaumu Instagram kwamba imegeuka uwanja wa matusi. Jamani, tatizo sio Instagram, Twitter, Facebook au mtandao mwingine wowote ule wa kijamii bali tatizo ni mtumiaji. Kama ilivyo mtaani, ukikaa kijiweni utaambulia ya kijiweni. Ukitumia muda wako mwingi maktaba, utaweza kupata vya kupatikana maktaba. Uki-hang out na walevi, well, twajua ni utapata. Ukipendelea kuwa na watu wa Neno la Mungu, utapata Neno la Mungu. Ukijiweka karibu na wasomi, utafaidika na uelewa (knowledge). Ukifuatilia vyombo vya habari, utahabarika. 

Msanii maarufu wa muziki na filamu nchini Marekani, Tyrese Gibson, anatoa ushauri huu 

Employees hanging out with employees is just going to further your career as an employee. You start hanging out with bosses, you eventually become one. (Mwajiriwa anayetumia muda mwingi na waajiriwa wenzie wa kawaida, atadumisha ajira yake kama mwajiriwa wa kawaida tu.Ukianza 'kujichanganya na mabosi, basi nawe waweza kuishia kuwa bosi)
Naam, watu unaojihusisha nao wanachangia kukufanya kuwa mtu wa aina flani. Na kanuni hiyo ina-apply pia kwenye mitandao ya jamii. Uki-follow watu wenye kuendekeza matusi au majungu, utaishia kukutana na matusi au majungu. 

Basi hapa chini ninakupatia orodha ya maprofesa waliobobea katika fani zao ambao wapo Twitter, na waweza kuwa-follow au  kuwaingiza katika LIST yako (nitaandaa makala ya jinsi ya kutumia 


Uongozi (Leadership)
Bill GeorgeHarvard Business School, @Bill_George

Adam GrantWharton School of Finance, @AdamMGrant
Monique ValcourEDHEC, @MoniqueValcour
Karl MooreMcGill University, @ProfKJMoore
Gianpiero PetriglieriINSEAD, @GPetriglieri
Stew FriedmanWharton School of Finance, @StewFriedman
Sir Cary Cooper, Lancaster University, @ProfCaryCooper
CV HarquailHowe School of Business, @CVHarquail
Bret SimmonsUniversity of Nevada-Reno, @DrBret
Mark EspositoHarvard University, @Exp_Mark
Ian McCarthyBeedie School of Business, @Toffeemen68
Gautum MukundaHarvard Business School, @GMukunda
Thomas RouletUniversity of Bath, @ThomRoulet
Terri GriffithSanta Clara University, @TerriGriffith
Patrick J. MurphyDePaul University, @ProfPJM

Ubunifu (Innovation)

Richard FloridaRotman School of Management, @Richard_Florida
Clayton ChristensenHarvard Business School, @ClayChristensen
Calestous JumaHarvard University, @Calestous
Alf RehnÅbo Akademi University, @AlfRehn
Marcel BogersUniversity of Southern Denmark, @Bogers
Cyndi BurnettBuffalo State College, @CyndiBurnett
Diego RodriguezStanford University @Metacool
Bob SuttonStanford University, @Work_Matters
Karim R. LakhaniHarvard Business School @KLakhani
Tim KastelleUniversity of Queensland, @TimKastelle
Tor GronsundUniversity of Olso, @Tor
Frank PillerRWTH Aachen University, @MassCustom
Tina SeligStanford University, @TSeelig
Bill FischerIMD Business School, @Bill_Fischer
Gary HamelLondon Business School, @ProfHamel

Mikakati (Strategy)

Michael PorterHarvard Business School, @MichaelEPorter
Estelle MetayerMcGill University, @Competia
Ioannis Ioannou, London Business School, @iioannoulbs
Rita McGrathColumbia Business School @RGMcGrath
Teppo FelinUniversity of Oxford, @TeppoFelin
Roger Martin, Rotman School of Management, @RogerLMartin
Peter G. KleinUniversity of Missouri-Columbia, @PeterGKlein
Mislek Piskorski Harvard Business School, @MPiskorski
Kevin BoudreauLondon Business School, @KevinJBoudreau
Sheen S. LevineColumbia University, @SSLevine
Freek VermeulenLondon Business School, @Freek_Vermeulen
Marion Debruyne, Vlerick Business School, @MarionDebruyne
Robin TeiglandStockholm School of Economics, @RobinTeigland
Dan Elfenbein, Washington University, @OrgStratProf
Sydney FinkelsteinTuck School of Management, @SydFinkelstein

Watajwa wa heshima (Honorable Mentions)

Terry Linhart, Bethel College,@ TerryLinhart
Teresa AmabileHarvard Business School @TeresaAmabile
Terri ScanduraUniversity of Miami, @TerriScandura
Michael RobertoBryant University, @MichaelARoberto
Nadia KazimHigher Colleges of Technology @Nadiakazim

Wasomi hawa mahiri duniani ni visima vya uelewa (knowledge). Na kama sote tunavyoelewa, ili uweze kuchota maji kutoka katika kisima shurti uende kisimani.

Basi endelea kutembelea blogu hii kwa habari mbalimbali, ikiwa ni pamoja na hizi za teknolojia. Bonyeza TEKNOLOJIA hapo kwenye menu juu upelekwe moja kwa moja kwenye habari hizo.


3 May 2010

Waziri Mkuu wa Australia,Kevin Rudd,amekuwa akifuatilia tovuti za ngono (porn sites),kwa mujibu wa kituo cha runinga cha Sky. 


Rudd,hata hivyo,amekuwa 'mfuatiliaji' wa tovuti hizo kutokana na mapungufu katika nyenzo za usalama/udhibiti (setting) katika akaunti yake ya Twitter.Kutokana na mapungufu hayo,kiongozi huyo amekuwa akifuatilia watu kama bloga wa mambo ya ngono,duka linalouza bidhaa za ngono,mwanamama aliye kifua wazi huku amjifunga pingu,na kadhalika.

Msemaji wa Waziri Mkuu ameeleza kuwa tatizo hilo lilitokana na akaunti ya Twitter ya Rudd kufuata wale wote wanaomfuata (auto-follow those who follow him)."Japo Waziri Mkuu anajitahidi kutoa majibu kwa wale wanaosema chochote kwake,kazi hiyo ni ngumu ukizingatia idadi ya watu ni 900,000", alieleza msemaji huyo.

Japo inamhitaji mtumiaji wa Twitter kuangalia kwanza wasifu wa mtu anayeomba kukufuata,kuna kipengele kinachoiwezesha akaunti imkubali moja kwa moja mtu anayeomba kumfuata pasipo haja ya mwenye akaunti kufanya hivyo.Uwezo huo unaonekana kuwa muhimu kwa watumiaji wa Twitter wenye wafuasi (followers) wengi.Katika akaunti yake KevinRuddPM,Waziri Mkuu huyo ni mfuasi wa wana-twitter wengine 200,000.

Wataalam wa teknolojia wanatahadharisha kuwa nyenzo za habari kwa jamii (social media)zinaweza kuhatarisha usalama wa mtuamiaji kama hataokuwa makini."Kuna imani kwamba kwenye vitu kama Twitter unaweza tu kufungua akaunti na mambo yakaenda mwanana",anasema Handsley,makamu mwenyekiti wa kampuni ya Young Media Australia."Tunapaswa kufahamu kwa undani kuhusu usalama wa chanzo husika cha habari kwa jamii kabla ya kuamua kukitumia",aliongeza alipoongea na gazeti la Herald Sun.

Kwa mujibu wa gazeti hilo,baadhi ya wengine 'waliofuatiliwa' na Waziri Mkuu Rudd ni pamoja na tovuti ya kamera-mtandao (webcams) za ngono na mmiliki wa kiota cha watenda ngono wa jinsia moja (gay resort) cha Phuket,Thailand.

Rudd amekuwa mtumiaji mzuri wa teknolojia ya habari huku nyakati nyingine akitumia nyenzo kama Twitter kubainisha sera zake.

Imetafsiriwa kutoka Sky News

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.