30 Aug 2014

Watanzania watatu, Hemedi Dendengo Sefu, Hassan Mohamed Nduli na Abdou, jana walitiwa hatihani na mahakama moja nchini Afrika Kusini kwa kosa la kula njama za kumuua aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Rwanda Jenerali Faustin Kayumba Nyamwasa mwezi Juni mwaka 2010.

Watanzania hao walikuwa miongoni mwa watuhumiwa sita, ambapo wawili walikutwa hawana hatia, na mmoja, raia wa Rwanda, alitiwa hatiani. Watahukumiwa mapema mwezi ujao.

Hakimu aliyeendesha kesi hiyo alieleza kuwa lengo la mauaji hayo lilikuwa ni la kisiasa. Jenerali Kayumba alikimbilia uhamishoni Afrika Kusini baada ya kutibuana na rafiki yake wa zamani, Rais wa sasa wa Rwanda, Paul Kagame. Hata hivyo, Rwanda imekanusha kuhusika na mpango wa mauaji hayo.

Mwandishi wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) alieleza kuwa Mkuu huyo wa zamani wa Majeshi ya Rwanda alikuwepo mahakamani wakati hukumu hiyo inatolewa. "Mahakama imeeleza kwa usahihi kuwa mpango wa kuniua ulikuwa na malengo ya kisiasa," alisema Nyamwasa.

Mmoja wa Watanzania hao, Sefu, alitajwa kuwa ndiye aliyepangiwa kumpiga risasi Jenerali huyo.

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka vynazo mbalimbali mtandaoni




0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.