19 Sept 2014

Alex Salmond
Waziri Mkuu wa Uskochi Alex Salmond amejiuzulu wadhifa huo kufuatia kushindwa kwa kura ya maoni ya 'uhuru wa Uskochi.'

Salmond, mwanasiasa machachari, ameeleza kuwa ataondoka madarakani rasmi mwezi Novemba. Alieleza kuwa amemwandikia barua Katibu Mkuu wa chama anachokiongoza cha Scottish National Party (SNP) kuwa hatogombea uongozi.

"Baada ya kura ya uongozi ndani ya SNP hapo Novemba, nitaondoka madarakani kama Waziri Mkuu ili kuruhusu kiongozi atakayechaguliwa katika mkutano huo kuchukua wadhifa huo kwa mujibu wa kanuni za Bunge."

Alipoulizwa na mwandishi wa Shirika la Utangazaji wa Uingereza (BBC) kwa atafanya shughuli gani baada ya kung'atuka Uwaziri Mkuu, ikizingatiwa kuwa 'unri haujamtupa mkono,' Salmond alitanabaisha kuwa ataendelea kujihusisha na shughuli za siasa. "Sintojitoa moja kwa moja katika siasa." Alisema kuwa anaweza kushiriki chaguzi zijazo kwa minajili ya kuwa mwanasiasa wa kawaida. "Huhitaji kuwa kiongozi wa SNP au Waziri Mkuu ili uweze kushiriki katika siasa."

Waziri Mkuu wa Uingereza 'nzima' David Cameron alimpongeza Salmond, na kumwelezea kama mwanasiasa nguli, hata kama walitofautiana kimsimamo kuhusu Muungano wa Uingereza."

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka vyanzo mbalimbali mtandaoni

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.