30 Dec 2014



Nesi mmoja aliyekwenda Sierra Leone kusaidia harakati za kukabiliana na janga la ugonjwa wa Ebola, amerudi Uingereza akiwa ameambukizwa ugonjwa huo, na hivi sasa amelazwa kwenye kituo cha maradhi ya kuambukiza cha Browlee katika Hospitali Kuu ya Gartnavel, hapa Glasgow.

Nesi huyo anatarajiwa kuhamishiwa London kwenye hospitali maalum ya Royal Free Hospital.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu wa Uskochi, Nicola Sturgeon, amewahakikishia wakazi wa Glasgow na Uskochi kwa ujumla kuwa uwezekano wa kusambaa kwa ugonjwa huo kutokana na maambukizi ya nesi huyo ni 'sawa na sifuri.'

Hata hivyo, bado kuna maswali ilikuwaje nesi huyo aliyepimwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow, London, kabla ya kuunganisha ndege na kuja Glasgow, hakugundulika kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo hatari usio na kinga wala tiba.

Profesa Jonathan Ball, mtaalam wa 'molecular virology' katika Chuo Kikuu cha Nottingham, ameeleza kuwa kesi hiyo inaashiria ugumu wa mkakati wa kupima wasafiri kutoka nchi zilzoathirika na Ebola wanapoingia Uingereza.

Chini ni baadhi ya picha zinazohusiana na habari hii ambayo waweza kuisoma kwa kirefu HAPA

A female health worker who returned from Sierra Leone last night is being treated for Ebola at Glasgow's Gartnavel Hospital (pictured), the Scottish Government confirmed
Hospitali ya Gartnavel

Safari ya nesi aliyeambukizwa Ebola, kutoka Sieera Leone hadi Glasgow.



The health worker was admitted to hospital early yesterday morning after feeling unwell and was placed in isolation 

The ebola patient is being treated at the specialist Brownlee Unit for Infectious Diseases at Gartnavel Hospital
Kituo cha maradhi ya kuambukiza cha Brownlee

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.