Nianze
makala hii kwa kuwashukuru ndugu nyote mlionitumia salamu za upendo,kunipa pole/kunipa
moyo baada ya jina langu kutajwa miongoni mwa watu 9 wanaodaiwa kuwa hatari kwa
usalama wa Tanzania.
Orodha
hiyo ilitajwa na mtu mmoja anayejiita Cyprian Musiba japo taarifa nilizonazo ni
kwamba jina hilo lina walakini kama lilivyo jina la rafiki yake – na miongoni
mwa watu waliofanikisha press conference yake – Daudi Albert Bashite. Waingereza
wanasema "birds of a feather flock
together."
Kichekesho
ni kwamba mara ya kwanza kumfahamu mtu huyo ni wakati flani aliponitumia ujumbe
kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akinifahamisha kuwa wana gazeti lao
linaitwa 'Tanzanite' na kuniomba niwe nawatumia makala. Nilipuuza ombi hilo kwa
sababu kutoka level ya kuandikia gazeti kubwa kama Raia Mwema kwenda kuandikia
kijigazeti kipya kama hicho cha Tanzanite ingekuwa kujishushia heshima yangu.
Kwa
upande mmoja,tuhuma za huyo mtu hazijanishangaza kwa sababu kadhaa. Kwanza,
tunafahamu fika ugumu wa maisha huko nyumbani, na sio suala la ajabu kuona
baadhi ya watu wakiuza utu wao ili mradi tu "njia ya kwenda msalani isiote
nyasi."
Lakini
pili, kuna jitihada kubwa za kuigeuza Tanzania kuwa kama wilaya ya Kanda ya
Ziwa. Huyo mtoa tuhuma ana asili ya maeneo hayo, na kuna hali inayozidi kuota mizizi
kwa baadhi ya wahuni wanaotoka eneo moja na Magufuli kujiona wana hatimiliki ya
Tanzania yetu.
Jingine
ambalo lilinifanya nipuuze hizo tuhuma za huyo bwege ni ukweli kwamba safari
yangu kimaisha hadi hapa nilipo imepshapitia vilima na mabonde. Nimeshaeleza
mara kadhaa kuhusu janga lililonisibu Februari 2, 2013 ambapo chombo kimoja cha
usalama hapa kilinifahamisha kuwa kuna tishio dhidi ya uhai wangu, tishio from
Tanzania. Na kwa zaidi ya mwaka mzima tangu wakati huo, nikawa ninaishi maisha
ya kutambua kuwa muda wowote ule naweza kudhurika. Licha ya ugumu mkubwa, hali
hiyo ilinipa uzoefu wa kuishi na vitisho.
Lakini
pia, hiyo hatua tu ya huyo mzembe kunituhumu naona kama tusi flani kwangu. Mie
sio wa kutuhumiwa na mtu asiyejulikana kama yeye. Ilipaswa labda awe kigogo
flani wa Usalama wa Taifa, ndo ningeweza kuchukulia suala hilo seriously.
Wanasema "usiongee na mbwa bali ongea na mwenye mbwa."
Hata
hivyo, japo sikushangazwa na tukio hilo la kihuni, nilikerwa na vitu vikuu
vitatu. Kwanza, wakati nina uhakika wa asilimia 100 kuwa huyo bwege ametumwa tu,
nilikerwa mno na uongo wa mchana kweupe uliokuwemo kwenye tuhuma zake. Uongo
huo ni pamoja na kudai kuwa FBI ni shirika la ujasusi la Marekani. Hivi hao
wapuuzi waliomtuma hawakufanya research japo kidogo ya kuwaelewesha kuwa
shirika la ujasusi la Marekani ni CIA na sio FBI?
Halafu
huyo bwege akachapia tena kwa kudai kuwa chama cha Kansela Angela Markel ni CDP
ilhali chama chake ni CDU. Halafu sijui ni mie tu na "macho yangu ya
kishushushu" niliyeona huyo jamaa akiongea kwa kuhema kana kwamba
anakimbizwa, huku amejawa na uoga mkubwa. Hizi njaa zitakuwa watu mwaka huu.
Seriously!
Kingine
kilichonikera ni jinsi huyo bwege alivyopewa umuhimu mkubwa asiostahili. Hivi
kwa mfano hiyo video ya press conference yake ingepuuzwa, nani angejua kuwa
kuwa mwendawazimu flani kuitisha press conference kutuhumu watu kadhaa wenye
heshima zao katika jamii? Kuna nyakati ukimya una nguvu zaidi ya kupigiana
kelele na mtu. So far, huyo mhuni amefanikiwa kufikisha ujumbe wake kwa watu
wengi mno kutokana na sie wenyewe – including tuliotuhumiwa -kumsaidia
kusambaza ujumbe wake muflis. Anyway, by muda huu hizo 15 minutes of fame
zimeshaisha muda wake.
Lakini
pia nilikerwa na ukweli kwamba uhuni wa aina hii ukiachwa tu bila kuchuliwa
hatua unaweza kusababisha madhara makubwa huko mbele. Maana tumeshaona jinsi Bashite
alivyoweza kuvamia studio za Clouds kisha Rais Magufuli bila aibu akamtetea
hadharani na kumsifia kuwa ni mchapakazi. Kwa kifupi, huko ni kusherehesha
uhuni.
Sasa
huyu bwege si mara ya kwanza kuibuka na press conference za kiendawazimu.Last
time aliitisha press conference na kutishia kumfungulia mashtaka shujaa Tundu
Lissu. Katika tukio hilo nilikerwa zaidi na ukweli kwamba kuna viumbe wenye
roho mbaya kama wachawi, ambao hawajatosheka na mateso aliyepitia Lissu baada
ya karibio la kutaka kumuuwa. Mie nimesoma"War Studies" na miongoni
mwa kanuni za vita ni kwamba pindi adui yako akiwa chini basi unatarajiwa kutomdhuru.
Kwahiyo hata kama Lissu ni adui yao, basi angalau wangesubiri apone kwanza
kabla ya kuanza kumwandama namna hiyo
Kwa
taarifa nilizonazo, press conference ya huyo bwege inamhusisha Bashite ambaye
bila shaka ana baraka za baba yake, lakini pia watu wa Kitengo nao wamehusika.
Ni vigumu kujua "kitengo kipi" maana kwa sasa ni kama tuna "Idara
mbili" – hiyo tunayoifahamu na hiyo "kampuni binafsi ya ulinzi wa
JPM/Bashite."
So who is this man Cyprian Musiba?— Evarist Chahali (@Chahali) February 26, 2018
Surely someone was behind his press conference: Is it @MagufuliJP? Bashite or TISS?
I'll have answers soon
| Je mtu huyu Cyprian Musiba ni nani? Kwa hakika ametumwa: Je ametumwa na Magufuli? DAB au Kitengo?
Nitakuwa na majibu karibuni pic.twitter.com/WFsQSi4u0I
Lakini
kubwa zaidi, na hasa ndio lengo la makala hii ni kuwafahamisha Watanzania
wenzangu kwamba tafsiri halisi ya tuhuma zilizotolewa kwenye hiyo press
conference ni kuwafanya ninyi Watanzania hamna akili ya kuweza kubaini nani
hasa ni tishio kwa usalama wa taifa lenu.
Twende
hatua kwa hatua japo kwa umbali mfupi tu.Hivi katika ya hao watu tisa ni yupi
alishiriki kupanga na kutekeleza shambulio la kinyama dhidi ya Lissu? Kibaya
zaidi, Lissu nae yumo katika orodha hiyo.
Je
ni yui kati ya hao tisa alitoa ruhusa kwa askari kumpiga risasi na kumuuwa
binti asiye na hatia Akwilina? Je ni nani kati yetu aliyehusika na mauaji wa
Katibu wa Chadema Kata ya Hananasifu marehemu Daniel na Diwani wa Kata ya Namwawala
Marehemu Luena? Maana kwa matukio haya matatu tu, na pengine la nne ni la
Lissu, inatosha kuonyesha kuwa kuna pattern ya mauaji dhidi ya raia wasio na
hatia. Na kwa vile hakuna jitihada zozote za vyombo vya dola kuwasaka wahusika
na kuwatia nguvuni, yayumkinika kuhisi ushiriki wa serikali ya Magufuli katika
matukio yote hayo.
Sasa
yule bwege kuwaona ninyi Watanzania hamnazo, kwamba "anamudu kuwalisha matango
pori" kwa kudai kuwa huyo na huyu ndiyo tishio kwa usalama wa nchi yetu,
ilhali kila mwenye akili timamu anafahamu bayana kuwa tishio kubwa zaidi kwa
sasa linatoka kwa WATU WASIOJULIKANA.
Je
sie tisa tuliotajwa ndo tumegeuka kuwa "watu wasiojulikana" ambao
sote wenye akili timamu twatambua ndio tishio kwa usalama wa Tanzania?
Ni
rahisi kulitazama suala hilo kama ni uhuni wa huyo mbwa dhidi yetu lakini
kiukweli mbwa huyo kawanyea Watanzania wote wenye akili timamu. Kawafanya hamna
uwezo wa kutofautisha pumba na mchele. Huyu mtu ni adui yenu zaidi ya adui wa
sie aliotutuhumu.
Sasa
je hasira yako dhidi ya mtu huyu na waliomtuma unaionyeshaje? Mie ushauri wangu
ni mwepesi tu: kama una uwezo wa kuwasomea dua mbaya, itakuwa vema. Kama una
utaalamu wa masuala ya asili, basi ni vema pia. Hata ukitukana kimoyomoyo ni
vema pia. Lakini ukipata wasaa wa "kumpa a uso" popote pale – iwe mtandaoni
au mtaani – tafadhali fanya hivyo.
Naamini
kabisa kati ya sie tisa tuliotajwa na huyo bwege, tuna watu walio tayari
kutafuta haki kwa ajili yetu.Na haki si lazima ipatikane mahakamani. Na
mahakama zenyewe hizi zinazoendeshwa kwa rimoti na Magufuli hadi kumfunga Sugu
wala hazina maana. Ombi langu kwenu ni kila aina ya laana dhidi ya mtu huyo, si
kwa sababu labda ana umuhimu flani bali ukweli huo niliyotanabaisha hapo juu
kuwa amewaona ninyi Watanzania kama hamnazo hadi kufikia hatua ya kutuzushia
sie tusio na hatia tuhuma hizo za kuhatarisha usalama ilhali sote tunafahamu
vema akina nani wanaohatarisha usalama wa Tanzania yetu.
Kama
ukinitumia picha wakati unamfanyia kisomo huyo mbwa basi itakuwa vema sana haha
Natamani kama huyu jamaa angepuuzwa from the start. Kick aliyoipata hakubadili kabisa. Tatizo la power ni kulevya. Wamelewa madarakani sasa hivi mning'inio utapata.
ReplyDeleteTatizo lingine kubwa ni vyombo vya habari vinampa fame mtu asiye stahili kabisa,mtu kuongea hawezi anakodoa macho kama amekalia sindano anakuja kupewa airtime kiasi hicho
ReplyDelete