27 Feb 2018




Nianze makala hii kwa kuwashukuru ndugu nyote mlionitumia salamu za upendo,kunipa pole/kunipa moyo baada ya jina langu kutajwa miongoni mwa watu 9 wanaodaiwa kuwa hatari kwa usalama wa Tanzania.

Orodha hiyo ilitajwa na mtu mmoja anayejiita Cyprian Musiba japo taarifa nilizonazo ni kwamba jina hilo lina walakini kama lilivyo jina la rafiki yake – na miongoni mwa watu waliofanikisha press conference yake – Daudi Albert Bashite. Waingereza wanasema "birds of a feather flock together."


Kichekesho ni kwamba mara ya kwanza kumfahamu mtu huyo ni wakati flani aliponitumia ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akinifahamisha kuwa wana gazeti lao linaitwa 'Tanzanite' na kuniomba niwe nawatumia makala. Nilipuuza ombi hilo kwa sababu kutoka level ya kuandikia gazeti kubwa kama Raia Mwema kwenda kuandikia kijigazeti kipya kama hicho cha Tanzanite ingekuwa kujishushia heshima yangu.

Kwa upande mmoja,tuhuma za huyo mtu hazijanishangaza kwa sababu kadhaa. Kwanza, tunafahamu fika ugumu wa maisha huko nyumbani, na sio suala la ajabu kuona baadhi ya watu wakiuza utu wao ili mradi tu "njia ya kwenda msalani isiote nyasi."

Lakini pili, kuna jitihada kubwa za kuigeuza Tanzania kuwa kama wilaya ya Kanda ya Ziwa. Huyo mtoa tuhuma ana asili ya maeneo hayo, na kuna hali inayozidi kuota mizizi kwa baadhi ya wahuni wanaotoka eneo moja na Magufuli kujiona wana hatimiliki ya Tanzania yetu.

Jingine ambalo lilinifanya nipuuze hizo tuhuma za huyo bwege ni ukweli kwamba safari yangu kimaisha hadi hapa nilipo imepshapitia vilima na mabonde. Nimeshaeleza mara kadhaa kuhusu janga lililonisibu Februari 2, 2013 ambapo chombo kimoja cha usalama hapa kilinifahamisha kuwa kuna tishio dhidi ya uhai wangu, tishio from Tanzania. Na kwa zaidi ya mwaka mzima tangu wakati huo, nikawa ninaishi maisha ya kutambua kuwa muda wowote ule naweza kudhurika. Licha ya ugumu mkubwa, hali hiyo ilinipa uzoefu wa kuishi na vitisho.

Lakini pia, hiyo hatua tu ya huyo mzembe kunituhumu naona kama tusi flani kwangu. Mie sio wa kutuhumiwa na mtu asiyejulikana kama yeye. Ilipaswa labda awe kigogo flani wa Usalama wa Taifa, ndo ningeweza kuchukulia suala hilo seriously. Wanasema "usiongee na mbwa bali ongea na mwenye mbwa."

Hata hivyo, japo sikushangazwa na tukio hilo la kihuni, nilikerwa na vitu vikuu vitatu. Kwanza, wakati nina uhakika wa asilimia 100 kuwa huyo bwege ametumwa tu, nilikerwa mno na uongo wa mchana kweupe uliokuwemo kwenye tuhuma zake. Uongo huo ni pamoja na kudai kuwa FBI ni shirika la ujasusi la Marekani. Hivi hao wapuuzi waliomtuma hawakufanya research japo kidogo ya kuwaelewesha kuwa shirika la ujasusi la Marekani ni CIA na sio FBI?

Halafu huyo bwege akachapia tena kwa kudai kuwa chama cha Kansela Angela Markel ni CDP ilhali chama chake ni CDU. Halafu sijui ni mie tu na "macho yangu ya kishushushu" niliyeona huyo jamaa akiongea kwa kuhema kana kwamba anakimbizwa, huku amejawa na uoga mkubwa. Hizi njaa zitakuwa watu mwaka huu. Seriously!

Kingine kilichonikera ni jinsi huyo bwege alivyopewa umuhimu mkubwa asiostahili. Hivi kwa mfano hiyo video ya press conference yake ingepuuzwa, nani angejua kuwa kuwa mwendawazimu flani kuitisha press conference kutuhumu watu kadhaa wenye heshima zao katika jamii? Kuna nyakati ukimya una nguvu zaidi ya kupigiana kelele na mtu. So far, huyo mhuni amefanikiwa kufikisha ujumbe wake kwa watu wengi mno kutokana na sie wenyewe – including tuliotuhumiwa -kumsaidia kusambaza ujumbe wake muflis. Anyway, by muda huu hizo 15 minutes of fame zimeshaisha muda wake.

Lakini pia nilikerwa na ukweli kwamba uhuni wa aina hii ukiachwa tu bila kuchuliwa hatua unaweza kusababisha madhara makubwa huko mbele. Maana tumeshaona jinsi Bashite alivyoweza kuvamia studio za Clouds kisha Rais Magufuli bila aibu akamtetea hadharani na kumsifia kuwa ni mchapakazi. Kwa kifupi, huko ni kusherehesha uhuni.

Sasa huyu bwege si mara ya kwanza kuibuka na press conference za kiendawazimu.Last time aliitisha press conference na kutishia kumfungulia mashtaka shujaa Tundu Lissu. Katika tukio hilo nilikerwa zaidi na ukweli kwamba kuna viumbe wenye roho mbaya kama wachawi, ambao hawajatosheka na mateso aliyepitia Lissu baada ya karibio la kutaka kumuuwa. Mie nimesoma"War Studies" na miongoni mwa kanuni za vita ni kwamba pindi adui yako akiwa chini basi unatarajiwa kutomdhuru. Kwahiyo hata kama Lissu ni adui yao, basi angalau wangesubiri apone kwanza kabla ya kuanza kumwandama namna hiyo

Kwa taarifa nilizonazo, press conference ya huyo bwege inamhusisha Bashite ambaye bila shaka ana baraka za baba yake, lakini pia watu wa Kitengo nao wamehusika. Ni vigumu kujua "kitengo kipi" maana kwa sasa ni kama tuna "Idara mbili" – hiyo tunayoifahamu na hiyo "kampuni binafsi ya ulinzi wa JPM/Bashite."


Lakini kubwa zaidi, na hasa ndio lengo la makala hii ni kuwafahamisha Watanzania wenzangu kwamba tafsiri halisi ya tuhuma zilizotolewa kwenye hiyo press conference ni kuwafanya ninyi Watanzania hamna akili ya kuweza kubaini nani hasa ni tishio kwa usalama wa taifa lenu.

Twende hatua kwa hatua japo kwa umbali mfupi tu.Hivi katika ya hao watu tisa ni yupi alishiriki kupanga na kutekeleza shambulio la kinyama dhidi ya Lissu? Kibaya zaidi, Lissu nae yumo katika orodha hiyo.

Je ni yui kati ya hao tisa alitoa ruhusa kwa askari kumpiga risasi na kumuuwa binti asiye na hatia Akwilina? Je ni nani kati yetu aliyehusika na mauaji wa Katibu wa Chadema Kata ya Hananasifu marehemu Daniel na Diwani wa Kata ya Namwawala Marehemu Luena? Maana kwa matukio haya matatu tu, na pengine la nne ni la Lissu, inatosha kuonyesha kuwa kuna pattern ya mauaji dhidi ya raia wasio na hatia. Na kwa vile hakuna jitihada zozote za vyombo vya dola kuwasaka wahusika na kuwatia nguvuni, yayumkinika kuhisi ushiriki wa serikali ya Magufuli katika matukio yote hayo.

Sasa yule bwege kuwaona ninyi Watanzania hamnazo, kwamba "anamudu kuwalisha matango pori" kwa kudai kuwa huyo na huyu ndiyo tishio kwa usalama wa nchi yetu, ilhali kila mwenye akili timamu anafahamu bayana kuwa tishio kubwa zaidi kwa sasa linatoka kwa WATU WASIOJULIKANA.

Image result for watu wasiojulikana

Je sie tisa tuliotajwa ndo tumegeuka kuwa "watu wasiojulikana" ambao sote wenye akili timamu twatambua ndio tishio kwa usalama wa Tanzania?

Ni rahisi kulitazama suala hilo kama ni uhuni wa huyo mbwa dhidi yetu lakini kiukweli mbwa huyo kawanyea Watanzania wote wenye akili timamu. Kawafanya hamna uwezo wa kutofautisha pumba na mchele. Huyu mtu ni adui yenu zaidi ya adui wa sie aliotutuhumu.

Sasa je hasira yako dhidi ya mtu huyu na waliomtuma unaionyeshaje? Mie ushauri wangu ni mwepesi tu: kama una uwezo wa kuwasomea dua mbaya, itakuwa vema. Kama una utaalamu wa masuala ya asili, basi ni vema pia. Hata ukitukana kimoyomoyo ni vema pia. Lakini ukipata wasaa wa "kumpa a uso" popote pale – iwe mtandaoni au mtaani – tafadhali fanya hivyo.

Naamini kabisa kati ya sie tisa tuliotajwa na huyo bwege, tuna watu walio tayari kutafuta haki kwa ajili yetu.Na haki si lazima ipatikane mahakamani. Na mahakama zenyewe hizi zinazoendeshwa kwa rimoti na Magufuli hadi kumfunga Sugu wala hazina maana. Ombi langu kwenu ni kila aina ya laana dhidi ya mtu huyo, si kwa sababu labda ana umuhimu flani bali ukweli huo niliyotanabaisha hapo juu kuwa amewaona ninyi Watanzania kama hamnazo hadi kufikia hatua ya kutuzushia sie tusio na hatia tuhuma hizo za kuhatarisha usalama ilhali sote tunafahamu vema akina nani wanaohatarisha usalama wa Tanzania yetu.

Kama ukinitumia picha wakati unamfanyia kisomo huyo mbwa basi itakuwa vema sana haha


2 comments:

  1. Natamani kama huyu jamaa angepuuzwa from the start. Kick aliyoipata hakubadili kabisa. Tatizo la power ni kulevya. Wamelewa madarakani sasa hivi mning'inio utapata.

    ReplyDelete
  2. Tatizo lingine kubwa ni vyombo vya habari vinampa fame mtu asiye stahili kabisa,mtu kuongea hawezi anakodoa macho kama amekalia sindano anakuja kupewa airtime kiasi hicho

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.