Showing posts with label AdelPhil Consultancy. Show all posts
Showing posts with label AdelPhil Consultancy. Show all posts

9 Dec 2015

Siku ya leo ninaadhimisha birthday tatu kwa mfululizo, mbili zangu binafsi na moja pamoja na Watanzania wenzangu. Wakati Tanzania inatimiza miaka 54 tangu ipate uhuru, nami ninatimiza miaka kadhaa tangu nizaliwe, nikiwa mtoto wa tano wa familia ya watoto wanane ya marehemu baba yangu mpendwa Philemon Chahali na marehemu mama yangu mpendwa Adelina Mapango.

Lakini leo pia ni siku ambayo kampuni yangu ya huduma za ushauri wa kitaalamu (consulting services) inazaliwa rasmi, Kampuni hii ni matokeo ya uamuzi wangu wa kutafsiri ujuzi na uzoefu wangu wa muda mrefu katika maeneo kadhaa na kuufanya kuwa kazi rasmi. 

Jina la kampuni, yaani AdelPhil, ni kumbukumbu ya marehemu mama ADELina na marehemu baba PHILemon,. Imesajiliwa hapa Uingereza lakini itatoa huduma za kimataifa katika maeneo ya Intelijensia na Usalama, mikakati ya siasa (political strategies), na masoko kupitia mitandao ya kijamii (social media marketing). Lengo hasa la kampuni hii ni kuliunganisha eneo la Maziwa Makuu (Great Lakes region) yaani Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Zaire na Jamhuri ya KidemOkrasia ya Watu wa Kongo (DRC) na dunia kwa ujumla. Awali, msisitizo utakuwa kati ya Tanzania na Uingereza. 

Pamoja na sababu nyingine, kuanzishwa kwa kampuni hii ni katika kuunga mkono jitihada za serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi uliotukuka wa Rais Dkt John Magufuli, ambaye tangu aingie madarakani amekuwa akifanya jitihada kubwa kuipeleka Tanzania yetu mahali inapostahili. AdelPhil itawasaidia Watanzania - kwa maana ya taasisi za umma na binafsi na watu binafsi - kulifikia soko la huduma na bidhaa hapa Uingereza (kwa kuanzia) na wakati huohuo kuwezesha wateja wa hapa Uingereza kulifikia soko la hudma na bidhaa nchini Tanzania. Baadaye wigo utatanuliwa ili kufikisha huduma hizo kwa nchi zote za Maziwa Makubwa na dunia kwa ujumla (hususan Ulaya Magharibi).

Basi nitumie fursa hii kumshukuru Mungu kwa kunijaalia mwaka mwingine. Japo mwaka huu ninaomaliza ulikuwa mgumu kwangu kutokana na kumpoteza baba yangu mpendwa, Marehemu Philemon Chahali, miaka 7 baada ya kumpoteza mama yangu mpendwa, Marehemu Adelina Mapngo, na sasa kubaki yatima.

Hata hivyo, japo nusu ya pili ya mwaka huu ilianza kwa kifo cha baba, hatimaye nilipata nguvu na kushiriki kikamilifu katika kampeni za uchaguzi mkuu huko nyumbani ambapo hatimaye Rais Dkt Magufuli aliibuka mshindi. Ushiriki huo umechangia sana wazo la kuanzishwa kwa kampuni ya AdelPhil baada ya kupata ushauri kutoka kwa watu kadhaa.

Uchungu mkubwa katika siku hii ni kutokana na ukweli kwamba kila mwaka, siku yangu ya kuzaliwa iliambatana na Marehemu baba kuniimbia happy birthday, kwa simu niwapo mbali na nyumbani, lakini hii ni birthday ya kwanza ambapo nitakosa upendo huo mkubwa wa baba kwa mwanae. Lakini yote ni mipango ya Mungu, na ninaamini wazazi wangu wapendwa huko walipo wanapata faraja kuona mtoto wao naanzisha kampuni ambayo nime-dedicate jina lake kwao.

Kwa Watanzania wenzangu, wito wangu mkubwa kwenu ni kuendelea kuunga mkono jithada za Rais Dkt Magufuli kwa sababu tuna malima mrefu wa kupanda na anahitaji kila aina ya ushirikiano wetu. Mie ndo mchango wangu wa kwanza ni huo wa AdelPhil Consultancy, kampuni ambayo japo inafanya biashara lakini pia ni ya kuwatumikia Watanzania wenzangu na nchi yetu kwa ujumla. Katika siku zijazo nitaelezea kwa undani ni jinsi gani waweza kunufaika na huduma za kampuni hii.

Nimalizie kwa kusema HAPPY BIRTHDAY TANZANIA, HAPPY BIRTHDAY ME, na HAPPY BIRTHDAY ADELPHIL CONSULTANCY

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.