Showing posts with label JOHN MAGUFULI. Show all posts
Showing posts with label JOHN MAGUFULI. Show all posts

27 Oct 2020



Pengine umeshawahi kusikia jina la Profesa Allan Lichtman wa Marekani ambaye ana rekodi ya miaka 30 ya kutabiri kwa usahihi kabisa matokeo ya urais katika nchi hiyo. 



Pengine utabiri uliompatia umaarufu zaidi ni wa mwaka 2016 ambapo takriban kila kura ya maoni ilionyesha kuwa mgombea wa chama cha Democrats, Hillary Clinton, angemshinda mpinzani wake wa chama cha Republican, Donald Trump.

Profesa huyo anatumia vipengele 13 vinavyopatikana kwenye kitabu chake kiitwacho "The Keys To The White House" (funguo za kuingilia Ikulu ya Marekani).

Katika vipengele hivyo 13 ni kauli zenye mrengo wa ushindi kwa mgombea aliyepo madarakani. Kwa muktadha wa Tanzania, vipengele hivi hapa chini vinamhusu Rais John Magufuli wa chama tawala CCM anayechuana vikali na mpinzani wake mkuu, Tundu Lissu wa Chadema.

Endapo majibu ya SI KWELI (FALSE) ni matano au pungufu kwa vipengele hivyo, basi mgombea aliyepo madarakani anatabiriwa kushinda. Lakini endapo majibu ya SI KWELI (FALSE) yatakuwa sita au zaidi, basi mgombea huyo ataanguka kwenye uchaguzi husika.

Naomba nitahadharishe kuwa hii ni mara ya kwanza kwa kanuni hii kutumika kutabiri matokeo ya urais nchini Tanzania. Hata hivyo nimejiridhisha kuwa japo Profesa Lichtman alilenga chaguzi za rais wa Marekani, zaweza pia kutumika kwa muktadha wa Tanzania.

1 May 2020


Kituo cha runinga cha NTV cha nchini Kenya kiliripoti jana jioni kwamba idadi ya vifo vya korona jijini Dar es Salaam pekee kwa jana vilikuwa 50. Kutokana na unyeti wa maradhi haya, yayunkinika kuamini taarifa hiyo kwa sababu sio rahisi kwa chombo cha habari cha kitaifa kama hicho kutoa taarifa nzito kama hiyo bila kujiridhisha. 

Lakini kwa upande mwingine takriban kila anayefuatilia kinachoendelea huko Tanzania anafahamu fika kwamba serikali ya Rais Magufuli sio tu inaficha takwimu kuhusiana na maambukizi na vifo bali pia inafanya mzaha mkubwa dhidi ya jana hilo.

Taarifa nilizopatiwa alfajiri hii zinaeleza kuwa serikali imetoa mwongozo wa siri kuhusu jinsi ya kuwashughulikia wagonjwa wa korona. Kwa mujibu wa mwongozo huo, mgonjwa atakaa hospitalini wak siki tatu tu. Endapo hali ya mgonjwa haitogeuka kuwa mahututi, atarudishwa akaugulie nyumbani. Mtoa taarifa ananiambia kuwa waraka huo ni sehemu ya utekelezaji wa "herd immunity," mkakati hatari ambao kwa lugha nyepesi ni kuruhusu korona iangamize maelfu hadi mamilioni ya Watanzania kwa matarajio kuwa watajenga kinga dhidi ya ugonjwa huo. 

Licha ya uwezo wake mkubwa kiuchumi, Uingereza iliamua mapema tu kuachana na wazo hilo la herd immunity ambapo japo hadi muda huu idadi ya vifo imezidi 20,000 kwa kufuata herd immunity idadi hiyo ingeweza kuwa kubwa zaidi. Kadhalika, herd immunity ni sawa na kuangamiza watu bure kwa nchi kama Tanzania ambayo ina idadi kubwa ya watu wenye magonjwa kama ukimwi, pumu, kisukaribi, shinikizo la damu, nk ambayo yamethibitika "kuwa na ukaribu na korona" ambapo wenye maradhi hayo wamekuwa waathirika wakuu wa janga hilo. 

Endelea kutembelea blogu hii mara wa mara uweze kupata updates mbalimbali hususan kuhusu janga la korona.

Chukua tahadhari, jikinge na uwakinge na wenzio. Na heri ya Mei Mosi.

29 Feb 2020


Somo: Kuvuliwa uanachama Bernard Membe, Waziri Wa Zamani wa Mambo ya Nje, Mbunge wa zamani, kada mkongwe na mmoja wa wana CCM walioingia "tano bora" ya kutafuta mgombea urais kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015

Key subject(s)

  1. Bernard Kamilius Membe
  2. John Pombe Magufuli
  3. Jakaya Mrisho Kikwete
  4. Modestus Kipilimba
Dhana ya kwanza: Membe "anakubali matokeo," anaamua kuachana na siasa. 

Dhana ya pili: Membe "anafanyiziwa."

Dhana ya tatu: Membe "anakubali matokeo," anaamua kujiunga na chama cha upinzani

Dhana ya nne: Membe hakubali matokeo, anaamua "kutafuta haki yake" CCM.

Dhana ya tano: Membe hakubali matokeo, anaamua "kutafuta haki yake" nje ya CCM

Ushahidi: Hadi muda huu Membe hajatoa tamko rasmi kuhusu mustakabali wake. Kwahiyo dhana zote nne zinasimama kama zilivyo kwa vile hakuna ushahidi wa kupelekea kuziondoa.

Kipimo/Vipimo: Haipo muda huu mpaka Membe atoe tamko rasmi. Dhana zote zinaendelea kubaki hai.

Mchujo: Kwa kuzingatia kuwa Membe hakuomba msamaha alipoitwa kwenye vikao husika, na kwa kuzingatia "damu mbaya" (bad blood)kati yake na Rais John Pombe Magufuli, tangu mwanzo wa Awamu ya Tano, yayumkinika kuamini kuwa uwezekano wa Membe "kutafuta haki yake" CCM ni hafifu.
Vigezo hivyo vinafanya uwezekano wa Dhana Ya Nne kutimia kuwa ni hafifu. Kwa mantiki hiyo, dhana hiyo inaondoshwa (yaweza kurejeshwa huko mbeleni)

Walakini: Hakuna

Unyeti: upo katika maeneo yafuatayo
  1. Membe ni mmoja wa makada zaidi ya 40 wa CCM waliojitokeza kuwania kupitishwa na chama hicho kwenye nafasi ya urais wa JMT.
  2. Membe alikuwa mpinzani mkuu wa Edward Lowassa kada aliyekuwa anapewa nafasi kubwa ya kuwa mrithi wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, na ambaye baada ya kutopitishwa CCM alihamia Chadema, japo baadaye alirudi tena CCM.
  3. Membe alikuwa miongoni mwa "tano bora" pamoja na Magufuli, January Makamba, Amina Ali na Asha Rose Migiro
    Migiro
  4. Membe ni swahiba mkubwa wa Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete
  5. Membe ni mwanachama wa kwanza wa CCM "mwenye hadhi ya kitaifa"kufukuzwa uanachama.
Uchambuzi:

Uzito wa dhana ya kwanza kwamba Membe atakubali matokeo na kuachana na siasa upo kwenye hoja kwamba kutokana na uzoefu wake ndani ya CCM, anafahamu kuwa jaribio lolote la kuendelea na "maisha ya kisiasa" litakumbwa na upinzani na vikwazo vingi kutoka kwa Magufuli na CCM kwa ujumla.

Kadhalika, kama shushushu wa zamani, Membe anafahamu kuwa yeye sasa ni "high value target" huko Idara ya Usalama wa Taifa, ambapo kila nyendo yake sio tu itafuatiliwa kwa karibu bali pia anaweza "kuchanganywa akili" kwa kufanyiwa "overt surveillance" (kumfuatilia mlengwa bila kificho, lengo likiwa kumjulisha kuwa anafuatiliwa. Mbinu hii hutumika zaidi "kumchanganya akili" mlengwa).

Mapungufu ya dhana ni ukweli kwamba Membe ni "high value target" pia kwa vyama vya upinzani, na kwa kuzingatia kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi, anaweza kupewa fursa ya "kulipa kisasi dhidi ya Magufuli kwa kupitishwa kuwa mgombea wa chama cha upinzani."

Mapungufu mengine katika dhana ya kwanza  ni "dalili za awali" kuwa "huu sio mwisho wa Membe kisiasa."

Uzito wa dhana ya pili upo katika ukweli kwamba Magufuli " hana mshipa wa aibu." Kama aliweza "kuamuru Lissu afanyiziwe," hashindwi kutoa maagizo kama hayo dhidi ya Membe.

Uzito mwingine upo kwenye ukweli kwamba shushushu wa zamani Membe nje ya CCM anabaki kuwa tishio kuliko alipokuwa mwanachama "anayebanwa na taratibu za chama."

Uzito mwingine ni ukweli kwamba Membe ni swahiba na watu wawili muhimu kwenye siasa za Tanzania, na ambao huenda wakawa na influence kwenye uchaguzi mkuu ujao, Rais Mstaafu Kikwete na Mkurugenzi wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa, na sasa balozi wa Tanzania Namibia, Dkt Modestus Kipilimba. Japo watu hawa wawili, kama ilivyo kwa Membe sasa, nao ni "high value targets" ambao sio tu wanafuatiliwa na mawasiliano yao kusikilizwa (uwepo wa walinzi unarahisisha zoezi hilo), lakini wanaweza kuwa nguzo muhimu kwaMembe "kulipa kisasi."

Kwa vile Kipilimba yupo nje ya nchi, na Kikwete huwa safarini mara kwa mara, kuwafuatilia kwa utimilifu wa asilimia 100 ni kugumu, na ikizingatiwa kuwa Membe ni shushushu wa zamani, anaweza kufanikisha mawasiliano nao na kuepa "surveillance" (kufuatiliwa) na "bugging" (kunasa mawasiliano).

Mapungufu ya dhana yapo kwenye ukweli kuwa japo "Magufuli hana mshipa wa aibu," na hivyo anaweza "kumfanyizia" Membe, lolote litakalomtokea Membe kati ya sasa na Oktoba litatafsiriwa moja kwa moja kuwa ni "mkono wa Magufuli." Na hilo linaweza kuwafanya "mabeberu kumrukia kama mwewe."

Na ikumbukwe kama Waziri wa Mambo ya Nje kwa miongo miwili, Membe atakuwa na "connections" kubwana nzito huku ughaibuni. Akidhuriwa na Magufuli, yawezekana kabisa "mabeberu" wakaamua kuharakisha utekelezaji wa mkakati wa kumng'oa kiongozi huyo.

Uzito wa dhana ya tatu ni ukweli kwamba kujiunga na chama cha upinzani sio tu kunaweza kumpatia fursa ya "kulipa kisasi kwa Magufuli, kwa kuwa mpinzani wake kwenye uchaguzi mkuu ujao (kwa kuamini kuwa atapitishwa kuwa mgombea urais katika chama chochote atakachohamia)," pia itakuwa nafasi adimu kwake kufanya jaribio jingine la kuwania urais wa Tanzania.

Uzito mwingine wa dhana hii ni kauli za Kiongozi Mkuu wa chama cha Wazalendo (ACT),Zitto Kabwe baada ya tangazo kuhusu kufukuzwa kwa Membe huko CCM, Kauli hizo zilikuwa na harufu ya "karibu kwetu."




Mapungufu ya dhana hii yapo kwenye ukweli kwamba hata kama Membe ataamua kujiunga na chamacha upinzani, vikwazo na usumbufu kutoka kwa Magufuli kupitia Idara ya Usalama wa Taifa vinaweza kumfanya "atamani ardhi immeze."

Kingine ni ukweli kwamba "Membe sio msafi kihivyo," na hiyo inaweza kumrahisishia Magufuli "kumzulia kesi ya utakatishaji fedha na/au uhujumu uchumi." 

Vivilevile, Idara ya Usalama wa Taifa inaweza kumshurutisha Membe asijiunge na chama kingine, hasa ikizingatiwa kuwa Magufuli amekuwa akiitumia taasisi hiyo kuwatisha na kuwahujumu wapinzani wake au/na wakosoaji/wanaharakati.

Kadhalika, licha ya Zitto kuonyesha dalili za awali za uwezekano wa "Membe kuhamia ACT-Wazalendo," kwa kuwa hatujui Maalim Seif na "ACT-Zanzibar" wana mtazamo gani kuhusu "ujio wa Membe," na ukweli kuwa wanaweza kumkataa, yawezekana Membe kuhamia chama hicho kusitokee.

Uzito kwenye dhana ya tano upo kwenye ukweli kwamba endapo atatumia vema ujuzi wake kama shushushu mstaafu, na endapo atapata sapoti kutoka kwa Kikwete na Kipilimba, Membe anaweza kuwa tishio nje ya CCM bila hata kujiunga na chama kingine cha siasa. 

Ukweli kwamba kuna wana-CCM wengi tu wanaotamani Magufuli aondoke hata kesho unaweza kumsaidia Membe kupata "marafiki" wengine muhimu ndani ya chama hicho, ambao pamoja nao wanaweza kuanzisha harakati za kumng'oa Magufuli.

Mapungufu ya dhana hii ukweli kwamba kwa nchi ambayo "ili nguvu za kisiasa shurti uwe mwanasiasa," uwezekano wa Membe kuwa na "nguvu" nje ya mfumo wa kisiasa ni mdogo.

Mchanganuo: Kwa upande mmoja, uamuzi wa Magufuli kumfukuza Membe unaelezea zaidi kuhusu yeye kuliko kilichompata Membe. Ukweli kwamba jina la Membe limekuwa likitajwa mara kadhaa kuhusiana na kinyang'anyiro cha urais mwaka huu, uamuzi huo wa Magufuli unatafsiriwa kuwa ni UOGA. Kwa kifupi, Magufuli amemuogopa Membe akiwa ndani ya CCM na ndio maana akashinikiza afukuzwe chamani.

Hofu ya Magufuli kwa Membe haina mashiko. Membe hakupaswa kushika nafasi ya tano kwenye "tano bora" ya kumtafuta mgombea urais kwa tiketi ya CCM, huku akiambulia kura 120 tu, nyuma ya JanuaryMakamba (124), Migiro (280),Amina Ali  (284) na Magufuli (290). Hakupaswa kushika nafasi hiyo kwa sababu kuu mbili. Kwanza, yeye ndiye alikuwa "front runner," kwa kuzingatia kuwa ndiye alikuwa mpinzani mkuu wa Lowassa.Na pili ni uswahiba wake na Kikwete na familia yake. Kingine cha kuongezea hapo ni ukaribu wake na maafisa mbalimbali wa Idara ya Usalama wa Taifa ambayo aliwahi kuitumikia huko nyuma.

Membe hakuwa na sababu moja ya msingi ya kutoibuka mshindi kwenye kinyang'anyiro hicho. Sasa sijui hiyo hofu ya Magufuli inatoka wapi. 

Ubashiri: Endapo Magufuli "hatomfanyizia" Membe, kuna uwezekano mwanasiasa huyo akajiunga na ACT- Wazalendo. Lakini kujiunga huko kutategemea endapo Maalim Seif na "ACT - Zanzibar) wataridhia. Hata hivyo, intelijensia sio sayansi timilifu, na matokeo ya ubashiri huu yanaweza kuwa tofauti.

Hitimisho: Suala hili lina sura mbili. Moja ni ukweli kwamba udikteta wa Magufuli sasa umepiga hodi ndani kabisa ya CCM.Pili, mpira upo mikononi mwa Membe. Akipanga karata zake vizuri, anaweza kutoa upinzani japo kidogo kwa Magufuli hapo Oktoba. Anaweza kuwa Rais ajaye wa Tanzania? Uwezekano huo ni hafifu japo wanasema "never say never in politics."

Uchambuzi huu ni endelevu. Utakuwa updated kadri kunapotokea maendeleo mapya.









16 Apr 2018






Africa Confidential Toleo la 28 Machi 2018


27 Machi 2018

Hatua za kidikteta za Magufuli zinakumbana na upinzani unaoongezeka lakini ndio Ameshika uelekeo huo na anatishia wanaomkosoa

Katikati ya muhula wake wa kwanza, Rais John Magufuli anakabiliwa na shinikizo. Huku akikabiliwa na tishio kubwa kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), vikundi vya kiraia, viongozi wa kanisa, na sasa vijana kwenye mitandao ya kijamii, anaonekana kufurahia mapambano hayo. Dola pia inatishiwa na makundi yenye silaha yaliyokuwa viongozi wa serikali na chama mkoani Pwani (MKIRU). Majibu ya serikali kukabiliana na changamoto hizo yametawaliwa na ukatili ambao haujawahi kuonekana kamwe, na kupelekea kulaaniwa kutoka kila upande.

Kuongezeka kwa vurugu za kisiasa, hasa wakati wa uchaguzi mdogo wa jimbo la Kinondoni, kulipelekea lawama dhidi ya utawala wa mabavu wa Magufuli. Ubalozi wa Marekani ulitaka kufanyike uchunguzi kuhusu utekaji na mauaji ya kiongozi wa upinzani jijini Dar es Salaam wakati wa kampeni. Umoja wa Ulaya baadaye ulionyesha wasiwasi wake kuhusu "mwenendo wa hivi karibuni unaotishia kanuni za demokrasia" baada ya polisi kutumia risasi katika maandamano ya Chadema katika mkesha wa siku ya kupiga kura Februari 17, hali iliyopelekea majeruhi watatu na kuuawa kwa mpita njia.

Wiki mbili baada ya matamko hayo, Wizara ya Mambo ya Nje ilijibu kwa taarifa yenye kurasa tatu na nusu ikiyahusisha matukio ya huko MKIRU na "vikundi vya ndani na nje ya nchi vinavyochukizwa na jitihada za Magufuli kuondoa ufisadi, biashara ya mihadarati, ujangili, ukwepaji kodi na kujenga uwajibikaji."

Vikundi hivyo vyenye silaha, ambapo baadhi vinadaiwa kuwa na mahusiano na Al-Shabaab ya Somalia, vimewauwa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na baadhi ya watendaji wa serikali. Tatizo hilo lilianza tangu mwaka 2014 lakini likafikia kilele mwaka 2017 baada ya operesheni ya kikatili ya vyombo vya dola kushambulia. Serikali inajaribu kuushawishi umma kwamba maandamano ya amani dhidi ya haki za kiraia na mauaji hayo ya MKIRU ni pande mbili za kitu kimoja. Ni watu wachache tu wanaoshawishika kuamini.
Katika ujumbe wao kwa msimu wa Kwaresma, maaskofu wa Katoliki walionya kwamba kuendelea kwa ukandamizaji wa kisiasa kutapelekea migawanyiko itakayohatarisha misingi ya kitaifa ya umoja na mshikamano. Walieleza kwamba kuzuwia shughuli za kisiasa sio halali na kunakiuka katiba. Kituo ch Demokrasia (TCD), ambacho huvileta pamoja vyama vya siasa kilitoa tamko la pamoja na viongozi wa Kikristo na Kiislamu kudai mapitio ya Katiba. Hii ilifuatiwa na kauli ya kuunga mkono ya vikundi zaidi ya 100 vya kiraia.

Jumapili ya Majivu Machi 25 ilishuhudia maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (ELCT) wakitoa tamko kali wakiilaani utekaji watu, utesaji watu, upoteaji watu, mashambulizi ya silaha dhidi ya wanasiasa, mauaji yanayotokana na itikadi za kisiasa, vitisho, kesi za kubambikizwa, na unyanyaswaji wa raia unaofanywa na vyombo vya dola. Pia walitaka katiba mpya iwepo kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. "Taifa huongozwa na katiba ambayo ndio msingi wa sheria zote", walisema. "Haiongozwi na ilani za vyama."

Pia kuna changamoto za kisheria. Mahakama Kuu inatarajiwa kusikia kesi mbili za kikatiba zilizoletwa na watetezi wa haki za binadamu ikiwa ni pamoja na Chama cha Wanasheria TLS, Umoja wa Watetezi wa Haki za Binadamu (the Tanzania Human Rights Defenders Coalition), na Taasisi ya sheria na haki za binadamu (the Legal and Human Rights Centre). Kesi zote zinaongozwa na Fatma Karume wa kampuni ya uwakili ya IMMA, ambayo ofisi zake zilichomwa moto Agosti mwaka jana. Akiwa anatoka kwenye familia yenye nguvu ya Karume, amekuwa mwiba kwa utawala uliopo madarakani. TLS inaongizwa na mmoja wa wateja wake, kiongozi wa Chadema Tundu Lissu, ambaye bado yupo Ubelgiji anakopata matibabu ya majeraha ya risasi kufuatia jaribio la kumuuwa.

Kumekuwa na ukosoaji ndani ya CCM pia. Nape Nnauye, mbunge aliyetimuliwa uwaziri mwaka jana, ametoa wito wa kuifanyia marekebisho Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) akieleza "kwa macho makavu" kuwa kama ambavyo taasisi hiyo imekuwa ikifanya kazi kwa manufaa ya dola, pia imekuwa ikiitumikia CCM, inaendeshwa kisiasa.

Mbunge mwingine wa CCM, Hussein Bashe, ambaye awali hakufahamika kuwa na mtazamo huru, na aliongoza kampeni ya Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwania urais, naye ametokea kuwa mtetezi wa uhuru wa kujieleza na mawazo mbadala.

Haya na matamko mengine yanaashiria demokrasia ya Tanzania ipo katika kipindi kigumu. Akiongea kwenye shughuli ya TCD ambayo ilipelekea wito wa katiba mpya, Askofu Benson Bagonza wa Kanisa la Kilutheri alitanabaisha kuwa kamwe hajawahi kuona polisi wakitumia risasi dhidi ya waandamanaji. "Nini kimebadilika?" aliulizwa.

Moja ya majibu kwa swali lake hilo ni "hakuna kikubwa (kilichobadilika)." Kunapokuwa na upinzani mkali kwenye chaguzi zilizopita, dola na chama tawala vimekuwa vikikimbilia kwenye ukatili. Kufanya vema kwa Chadema katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kulipelekea angalau miaka miwili ya ukatili. Ilianza Januari 2011 ambapo polisi walitumia risasi dhidi ya maandamano ya wafuasi wa Chadema Arusha.
Februari 2012, wanaharakati 16 wa haki za binadamu walikamatwa kwa kuunga mkono mgomo wa madaktari. Agosti mwaka huohuo, polisi walimuua kwa risasi muuza magazeti huko Morogoro wakati wa maandamano ya Chadema. Mwezi uliofuata, mwandishi wa habari Daudi Mwangosi aliuawa na polisi kufuatia kupigwa na bomu la kutoa machozi huku akiwa amekandamizwa chini na polisi. Katika mwezi huohuo, kiongozi wa maandamano ya madaktari, Steven Ulimboka alitekwa, akateswa na kuachwa ajifie mwenyewe kwenye msitu nje ya jiji la Dar es Salaam, tukio linalodhaniwa kufanywa na maafisa wa TISS. Baadaye mwaka huo huo, na pia Mei 2013, njia za kikatili zilitumika kukabiliana na maandamano yaliyoambana na wimbi kubwa la machafuko katika historia ya Tanzania.

CCM inakabiliwa na changamoto kubwa kudumisha utawala wake. Kwa kutoongelea suala la ufisadi mkubwa (katika kampeni zake za uchaguzi mkuu wa) mwaka 2015, ilitoa fursa kwa Chadema kupata mafanikio (ya kuridhisha) katika uchaguzi huo. Wimbo la ukandamizaji linaloendelea hivi sasa, linailenga Chadema, na pia linachangiwa na hofu kuhusu vikundi vyenye msimamo mkali vyenye silaha (kama ilivyokuwa huko MKIRU).

Sintofahaumu hiyo inaweza kueleza ukatili mkubwa uliotumika kukabiliana na kilichokuwa kikijiri katika mkoa wa Pwani. Miili kadhaa iliyofungwa kwenye 'viroba' iliyokutwa inaelea maeneo ya (Msasani) Peninsula jijini Dar es Salaam inaashiria jinsi hali ilivyokuwa.

Wizara ya Mambo ya Nje ilitoa tamko masaa tu baada ya tovuti ya African Arguments ya Royal African Society kuchapisha habari iliyoeleza kuhusu matumizi ya silaha za moto dhidi ya waandamanaji huko wilayani Rufiji katika ofisi za halmashauri ya mji.

Kwa kuunganisha vitendo vya vikundi hivyo vilivyokuwa vinavyotumia silaha (huko MKIRU) na upinzani dhidi ya mageuzi yanayofanywa na Magufuli, inatoa kisingizio kwa dola kutumia nguvu dhidi ya makundi yote mawili (vikundi vya MKIRU na upinzani dhidi ya Magufuli).

Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo aliwataka Watanzania kuwa wazalendo dhidi ya tishio kwa amani, umoja, uhuru na mshikamano. Kichekesho ni kwamba aliyasema hayo katika maadhimisho ya viongozi waliopambana na utawala wa mkoloni mwaka 1907 katika Vita ya Maji Maji. Jinsi dola inavyopambana na vurugu na upinzani inarejesha kumbukumbu za jinsi serikali ya mkoloni ilivyopambana na upinzani dhidi yake.

Mafanikio yoyote ya kuelezea kuhusu tishio linaloukabili demokrasia nchini Tanzania yatategemea zaidi makundi mbalimbali ndani ya CCM na tabaka tawala. Wanaoonekana kama wapinzani ndani ya CCM kama Nape na Bashe watabaki ndani ya chama hicho kwa gharama yoyote, wakicheza mchezo mrefu wa subira hadi uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ambapo inatarajiwa Magufuli atamaliza muda wake.

Viongozi wa dini – Magufuli anajitambulisha kama Mkatoliki mcha Mungu – wanaweza kufanikiwa kumshawishi kupunguza matumizi ya vyombo vya dola dhidi ya upinzani. Lakini wanaharakati na wanasiasa wa upinzani wanafahamu fika kuwa kudhibitiwa kwa asilimia 100.

MHALAKI (SOCIALITE) AONGOZA MAPAMBANO KUPITIA MTANDAO WA KIJAMII WA INSTAGRAM

Mashtaka yanayofunguliwa na taasisi za kiraia na matamko ya viongozi wa dini ni kitu kimoja, lakini wito wa kufanyika maandamano unaotolewa na bloga mwenye makazi yake Los Angeles (Marekani), Mange Kimambi, ni changamoto tofauti kabisa kwa Magufuli. Kimambi amekuwa sura ya hadharani ya wito wa maandamano ya nchi nzima tarehe 26 Aprili dhidi ya Magufuli.

Akifahamika zaidi kwa masuala ya fasheni na habari zinazohusu watu maarufu, akaunti ya Instagram ya Kimambi imekuwa ikihamasisha na kuyapa umaarufu maandamano hayo, yanayotarajiwa kufanyika siku ya Muungano, ambayo ni kumbukumbu ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar.

Kimambi anayedhaniwa kuwa anashirikiana na wanaharakati nchini Tanzania, anachukuliwa kwa uzito mkubwa na mamlaka za nchi hiyo. Akiongea kwenye tukio moja Machi 9 kijijini kwake Chato, Magufuli alisema "tusubiri na tuone wakiandamana, na watanitambua." Siku chache kabla, Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba aliwatuhumu waandaaji wa maandamano hayo kuwa wanapanga kuuwa watu na kisha kuvitupia lawama vyombo vya dola. Maonyo mengine yametolewa na angalau makamanda wa polisi wa mikoa saba. Inafahamika kuwa viongozi wa serikali na chama (tawala) wameelekezwa kuhamasisha upinzani dhidi ya maandamano hayo na tayari watu kadhaa wameshakamatwa.

Kimambi ni mwanaharakati ambaye haingekuwa rahisi zamani kumtarajia. Alipata umaarufu mwaka 2009 kupitia blogu yake ya 'U-Turn' ambayo ilikuwa ikisimulia kuhusu maisha yake kama mhalaki huko Dubai. Baadaye alihamia katika makazi yake ya sasa, Los Angeles, kabla ya kuanza kuiteka Instagram mwaka 2015, ambapo alimpigia Magufuli kampeni yenye ufanisi, licha ya yeye kushindwa kuteuliwa kugombea ubunge jimbo la Kinondoni.

Alimgeuka Magufuli takriban Mei 2016 ambapo alipinga vikali kusitishwa kwa matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya bunge. Anachanganya upinzani wa kisiasa na nguvu yake kama mhalaki anayeweza kumjenga au kumbomoa mtu kwa kutumia mitandao ya kijamii. Awali ilikuwa kuhusu picha zake binafsi na "selfies" lakini baadaye mabadiliko yakajitokeza. Kufikia mwishoni mwa mwaka 2016, akaunti yake ikawa sehemu kuu ya harakati za mtandaoni za upinzani dhidi ya serikali, na sehemu ya kuona nyaraka mbalimbali zilizovuja.

Akaunti yake imechukua nafasi ya Jamii Forums, jukwaa la maoni mtandaoni lililokuwa kitovu cha upinzani mtandaoni, na ambalo waanzilishi wake wanakabiliwa na kesi mahakamani na wamekuwa wakisumbuliwa na mamlaka kwa muda mrefu.

Huku akiwa na wafuasi zaidi ya milioni 1.4* kwenye Instagram, uwezo wa Kimambi kuwafikia watu unawazidi wanasiasa wote wa Tanzania, japo kuna shaka kuhusu maandamano ya April 26. Kujitokeza kwa watu wengi kwenye maandamano hayo kutategemea uwezo wa waandaaji wake wa maandamano hayo nchini Tanzania, ambao wanaokabiliana na utawala usio na huruma – polisi watamwaga risasi kwa ajili ya kuuwa, kama ambavyo wamefanya huko nyuma.

Haitojalisha hata kama hakuna mtu atayejitokeza kuandamana Aprili 26. Kutoka umbali wa kilomita 26,000, Kimambi tayari ameweza kufanya zaidi ya kutikisa mkia wa chui kwa kutumia simu ya mkononi tu. Na laiti ikitokea asalimisha yeye mwenyewe, mara moja kukamatwa kwake kutakuwa tukio kubwa kabisa litakaloiweka Tanzania kwenye macho na masikio ya dunia nzima.

MAELEZO YANGU: Makala hii ni tafsiri ya neno kwa neno ya makala ya gazeti maarufu la duniani la habari za kuchunguza kuhusu bara la Afrika la AFRICA CONFIDENTIAL Toleo laMachi 28, 2018 lililokuwa na kichwa cha habari "Enemies Without And Within."

Nimejitahidi kadri nilivyoweza kufanya tafsiri ya karibu kabisa kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili. Ni vigumu kufanya tafsiri timilifu kwa asilimia 100 hasa pale mwandishi na mtafsiri ni watu wanaoongea lugha mbili tofauti. Ni rahisi kwa mtu aliyeandika mwenyewe kufanya tafsiri ya alichoandika kuliko kazi hiyo kufanywa na mtu mwingine.
* Idadi ya "followers" kwenye akaunti ya Mange kwa sasa ni watu milioni 1.8.






18 Feb 2018


Nianze makala hii kwa kutoa salamu zangu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Daniel John, ambaye hadi alipouawa kinyama alikuwa Katibu wa Chadema kata ya Hananasifu, na pia kwa familia, ndugu,jamaa na marafiki wa marehemu Acqulina Akwilin (samahani kama nimekosea jina).

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, mwili wa marehemu Daniel uliokotwa kwenye ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam ukiwa na majeraha. Alieleza kuwa awali marehemu alichukuliwa na Land Rover nyeupe na watu waliohifanya askari polisi, lakini tangu wakati huo Polisi hawakuwa na taarifa zozote za kiuchunguzi, na hata jitihada za kupatikana mwili huo zilifanywa na Chadema wenyewe.




Kwa upande wa marehemu Acquilina, kifo chake kilisababishwa na kasumba hatari inayozidi kuzoeleka kwa watumishi wa vyombo vya dola kufanya mzaha katika matumizi ya silaha za moto, ambapo katika tukio husika, polisi waliokuwa wakizuwia maandamano ya wafuasi wa Chadema, walitumia risasi za moto,na moja kati ya risasi hizo ilipelekea kifo cha binto huyo, ambaye hadi mauti yanamfika alikuwa mwanafunzi katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) akisomea shahada ya ununuzi na ugavi.
Ni muhimu kutambua kuwa vifo vyote hivi viwili vingeweza kuepukika laiti utu na ubinadamu wetu ungewekwa mbele ya chuki za kisiasa. Huhitaji kuwa mjuzi wa uchunguzi wa mauaji kufahamu kuwa vifo hivyo ni matokeo ya chuki, hujuma, uonevu na kila aina ya baya dhidi ya chama kikuu cha upinzani, Chadema, kuhusiana na kampeni za uchaguzi mdogo katika jimbo la Kinondoni, ambalo kama ilivyo kwa jimbo la Siha, ni "piga ua" kwa CCM ishinde. Yaani chama hicho tawala kilitarajiwa kutumia kila mbinu kuhakikisha inashinda katika majimbo hayo mawili.

Lakini kabda sijaingia kwa undani katika mada hii - ambayo lazima nikiri kwamba inanipa wakati mgumu sana kuiandika kwa sababu nimebanwa na mchanganyiko wa majonzi na hasira, sambamba na hofu ya kuona taifa langu likisukumwa kuelekea kwenye upotevu wa amani na mshikamano wetu – naomba kuweka wazi masuala matatu ya msingi kunihusu mie mwandishi wa mwakala hii.

Kwanza, mimi licha ya kuwa na makazi nje ya Tanzania kwa takriban miaka 15 sasa bado no Mtanzania. Utanzania wangu ni haki nilioirithi kutoka kwa wazazi wangu, na itabaki hivyo milele. Naeleza hili kwa sababu kuwa wabaguzi wanaopenda kutuhukumu Watanzania tunaoishi huku ughaibuni, na kutaka tuonekane kama Utanzania wetu sio kamili. Kwa mantiki hiyo, kama Mtanzania, nina kila haki ya kutoa maoni yangu kuhusu mustakabali wa taifa letu, hususan katika nyakati hizi ambapo kuna dalili za wanaotaka kulipeleka kubaya taifa letu.

Pili, mwaka 2015 nilishiriki kikamilifu katika kampeni zilizomwingiza madarakani Rais John Magufuli. Kwa upande mmoja nililazimika kumkampenia Magufuli kwa vile nilikuwa nina "sababu binafsi" dhidi ya aliyekuwa mpinzani wake mkuu, mgombea urais wa tiketi ya UKAWA, Edward Lowassa. Wanasema "adui ya adui yako ni rafiki yako."Kwa upande mwingine, nililipwa kutoa huduma ya ushauri wa kitaalamu (usadi, yaani consultancy kwa kimombo) hususan kwenye mitandao ya kijamii. Natanabaisha hili ili asije akakurupuka mtu na kusema "ah ulishiriki kutupigia kampeni kwa vile tulikupa pesa."

Tatu, huko nyuma nilikuwa mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa. Na kabla ya kuanza utumishi katika taaluma hiyo muhimu na nyeti, nilikula kiapo kwa nchi yangu, kiapo ambacho nitaishi nacho hadi ninaingia kaburini. Kiapo hicho sio cha kukitumikia chama flani au viongozi wake bali Tanzania yetu. Nchi ni muhimu  kuliko vyama vya siasa au wanasiasa.

Mtu aliyepikwa na kuiva kwenye taaluma ya uafisa usalama wa taifa, katika nchi yoyote ile, anapaswa kubaki kuwa mtiifu kwa nchi yake bila kujali yupo ndani au nje ya ajira ya taasisi inayohusika na usalama wa taifa wa nchi husika.

Wanasema hata nje ya ajira rasmi, kila mtu aliyewahi kuwa afisa usalama wa taifa anaendeshwa na "sense of public duty born in their previous lives" yaani wajibu kwa umma uliozaliwa katika maisha yao huko nyuma. Jasusi mmoja mstaafu anaeleza “...I have obligations, professional obligations. If there’s a national security emergency or possible national security issue, I should report it."


Kwahiyo, hata kama "maafisa wenzangu wa zamani" wataamua kukaa kimya kwa sababu moja au nyingine – wengi wanahofia usalama wa maisha yao – sie wengine hatuwezi kukaa kimya, hasa kwa vile baadhi yetu tumeshalipa gharama kubwa kwa kelele zetu. Kukaa kimya ni sawa na kuafiki uhuni unaoendelea ambao ni tishio kwa usalama wa taifa.

Lakini licha ya wajibu huo unaotokana na utumishi wetu kwa nchi huko nyuma, Rais Magufuli amefanikiwa kuvifunga mdomo vyombo vya habari kiasi kwamba haviwezi kusema lolote kuhusu "mabaya" yake, na amefanikiwa kuvijengea nidhamu ya uoga vyombo hivyo vya habari kiasi kwamba habari pekee zenye umuhimu kwao ni za kumtukuza na kumpamba "mungu-mtu" huyo. Kwahiyo na sie tuliopikwa na kuiva kuhusu ujasiri, kujitoa mhanga na kutokuwa waoga tukiufyata na kukaa kimya - ilhali media zetu ndio zishapigwa kufuli - hali itazidi kuwa mbaya.


Baada ya kuweka wazi nafasi yangu, sasa tuangalie kwa kina kinachoendelea huko nyumbani hasa kuhusiana na uchaguzi mdogo kwenye jimbo la Kinondoni na Siha na kuuawa kwa Daudi na Acquiline.

Ni muhimu kutambua kwamba ukandamizaji dhidi ya vyama vya upinzani sio kitu kilichoanza chini ya utawala wa Magufuli bali hali hiyo imedumu mfululzo tangu kuanzishwa kwa mfumo wa siasa za vyama vingi mwaka 1992. Labda kilicho tofauti kwa zama hizi ni "ujasiri" wa Magufuli kutoficha chuki yake dhidi ya vyama vya upinzani. Yaani angalau akina Mwinyi,Mkapa na Kikwete walikuwa "wanauma na kupuliza." Kwamba angalau walikuwa na "mshipa wa aibu" na walijitahidi japo kutowaonea Wapinzani waziwazi.

Kwa wanaojua "yanayojiri nyuma ya pazia" watakwambia kuwa hujuma dhidi ya vyama vya upinzani ni miongoni mwa vipaumbele vikubwa kwa CCM na serikali zake, na hiyo imepelekea kujengeka "symbiotic relationship" kati ya chama hicho tawala na taasisi za dola, ambapo kila mmoja anategemea uhai wa mwenzie.

Lakini kama kuna kitu kinachokera zaidi kuhusu hujuma dhidi ya demokrasia ni pale CCM na taasisi zake hasa za dola wanapoweka mbele maslahi yao mbele ya utu na uhai wa Watanzania. Na hili halijaanza jana au katika kampeni za chaguzi ndogo katika majimbo ya Kinondoni na Siha.

Uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 ulihusisha matukio mengi tu ambayo kwa makusudi hayapo kwenye kumbukumbu za wazi (japo yamehifadhiwa mahala flani).

Lakini kama wanavyosema "amekula asali sasa anachonga mzinga," baada ya hujuma za kimyakimya za mwaka 1995 kuzaa matunda, CCM na taasisi zake ikanogewa, na matokeo yake ni kwamba uchaguzi mkuu uliofuata, mwaka 2000 uliweka doa kubwa kwa historia ya Tanzania yetu ambapo kwa mara ya kwanza nchi yetu ilizalisha wakimbizi kufuatia unyama uliofanyika huko Zanzibar na kupelekea vifo kadhaa (idadi halisi ya vifo haijawahi kuwekwa hadharani japo "wenyewe" walisema zaidi ya watu 19 ndio waliokufa kwenye machafuko hayo. Wasichosema pia ni idadi ya watu waliobakwa, kuteswa na kuwekwa kizuizini.

Kwamba hujuma hizo za CCM dhidi ya demokrasia zilipelekea vifo na majeruhi ni kitu kibaya kabisa. Lakini kitu kingine kibaya ni ukweli kwamba hakuna mtu hata mmoja aliyechukuliwa hata kutokana na unyAma waliofanyiwa Wazanzibari hao.

Kwa namna ya kipekee, CCM ikawa kama imepewa ruhusa ya kutumia vyombo vyake vya dola kufanya lolote itakalo ili ifanikishe hujuma zake dhidi ya Wapinzani na demokrasia kwa ujumla, kisha iibuke na ushindi.

Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 ulikuwa na "uchafu kupindukia." Kundi lililofahamika kama "mtandao" lilijipenyeza katika kila sekta, kuanzia kwenye vyombo vya habari, taasisi za dola hadi kwenye taasisi za dini. Yayumkinika kabisa kuhitimisha kwamba yaliyojiri wakati "mtandao unafanya jitihada za kumwingiza mtu wao Ikulu" ni mabaya zaidi ya haya tunayoshuhudia sasa tangu Magufuli aingie madarakani.

Kwanini basi hayo yaliyojiri kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 hayajulikani? Jibu ni kwamba, wakati mbinu iliyotumika mwaka 1995 na 2000 ilitegemea zaidi vyombo vya dola, uchaguzi wa mwaka 2005 na 2010 ulitegemea zaidi nguvu ya fedha, nyingi zikiwa fedha haramu. Na sehemu ya fedha hiyo ilitumika "kununua ukimya" wa wanahabari wengi tu. 

Lakini si fedha tu bali pia kuna hujuma mbalimbali – nyingine chafu na za kuchefua – zilizotawala safari za ushindi wa chama tawala kwenye chaguzi hizo.


Image result for lowassa kikwete 2005

Labda tofauti nyingine kuhusu mwaka 2005 na 2010 ni ukweli kwamba wakati chaguzi hizo zilihusisha "kikundi binafsi" yaani hicho cha wanamtandao ambacho hakikuwa taasisi ya serikali au chama.

Lakini muda wote huo, CCM ilikuwa kama imepwa ruhusa na Watanzania kuendeleza hujuma zake dhidi ya Wapinzani na demokrasia kwa ujumla. Hakujawahi na utashi miongoni mwa Watanzania kutaka kukabiliana kwa dhati za uhuni/uhalifu wa kisiasa. Na kwa bahati mbaya, kwa vile vipaumbele vya Watanzania wengi ni kwenye "ubuyu" na "kubeti/mkeka" basi habari mbaya ni uwezekano wa CCM kuendelea kufanya itakavyo kwa muda mrefu sana.

Sio kama kwa kubashiri kuwa unyanyasaji wa CCM utaendelea muda mrefu sana ninamaanisha kuwa nimekata tamaa. Hapana. Ninakuwa mkweli tu. Tatizo ni zaidi ya CCM na uhuni wake. Watanzania wenyewe ni sehemu ya mfumo unaowezesha CCM kufanya uhuni/uhalifu huo.

Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ulihusisha pia matuki kadhaa yaliyojiri "nyuma ya pazia." Na ukitaka kufahamu kuwa Tanzania yetu haijawahi kuhangaishwa na mauaji ya kisiasa – kuanzia yale ya mwaka 2001 huko Zanzibar hadi haya ya Daudi wa Hananasifu na dada Acquilina – ni kifo cha Mchungaji Christopher Mtikila.


Kwahiyo, na ninaandika haya kwa uchungu mkubwa uliochanganyika na hasira, kuuawa kwa Daudi na Acquilina kutaishia kuwa moja tu ya matuko yaliyowahi kutokea katika Tanzania yetu. Tutawasikia wanasiasa wetu wa vyama vya upinzani wakiongea kwa hisia kubwa. Tutashuhudia pia wanafiki wengi tu miongoni mwa wasanii wetu nao wakijifanya kuguswa na vifo hivyo, lakini wakiwa makini kuepuka kumuudhi "Bashite na baba yake" au kuitibua CCM. Tutashuhudia pia kundi la wanafiki hatari ndani ya CCM wakijifanya kuumizwa na mauaji hayo, na kutaka uchunguzi ufanyike, ilhali nao ni kondoo waliojivika ngozi ya mbwa mwitu.



Kama ambavyo "mauaji mengine ya kisiasa" yalivyoruhusiwa kupita kimyakimya, ndivyo unyama huu uliofanywa dhidi ya Daudi na Acquilina utakavyoruhusiwa uishe kimyakimya.

Kwa upande mmoja tusitarajie Rais Magufuli awajibike – sio kwa yeye binafsi kujiuzulu kwa sababu hilo litakuwa kutarajia zaidi ya muujiza – kwa kumtimua Waziri husika na watendaji katika jeshi la polisi. Kwa upande mwingine, hakuna wa kumshinikiza Rais Magufuli achukue hatua stahili dhidi ya wahusika.

Na nisingependa kuuma maneno hapa. Yeye Magufuli mwenyewe ni chanzo muhimu cha siasa hizi za uhasama zinazoendelea kuitafuna Tanzania yetu. Huyu ni mtu ambaye wala hapati shida kuonyesha chuki zake za waziwazi dhidi ya Wapinzani, Upinzani na demokrasia kwa ujumla.


Kama ilivyo kwa madikteta wengine duniani, Magufuli amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutumia ajenda yake ya ufisadi kama kisingizio cha kusigina haki za binadamu nchini Tanzania, na kubinya kila fursa ya haki za kidemokrasia na uhuru wa habari. Kama nilivyoeleza awali, amefanikiwa kuviziba midomo vyombo vya habari na ndio maana hata habari za kusikitisha kuhusu mauaji ya Daudi na Acquiline hazijaripotiwa vya kutosha.

Kwa kuviziba midomo vyombo vya habari Magufuli amefanikiwa kuzuwia "habari asizozipenda" na ndio maana hadi muda huu ni Watanzania wachache tu wanaofahamu kilichojiri huko MKIRU katika kilichoitwa "operesheni dhidi ya ugaidi." Kuna siku yaliyojiri huko – na ambayo yamechangia "kupotea" kwa mwandishi wa gazeti la Mwananchi Azory Gwanda – yatajulikana hadharani. Haijalishi itachukua miaka mingapi.


Lakini "yaliyojiri MKIRU" ni uthibitisho mwingine wa hicho nilichoeleza hapo juu kuwa Watanzania wenyewe ndio wanaopaswa kubeba lawama nyingi katika kasumba ya CCM kutojali uhai katika harakati zake za kukandamiza demokrasia. Kwamba kama yaliyojiri MKIRU yameachwa yaishe kienyeji, kwanini tutegemee hali tofauti kwa vifo vya Daudi na Acquiline?

Kama ndugu zetu wa Chadema (na kila mpenda haki) "wamekubali yaishe" kuhusu kifo cha Kamanda Mashaka, "kupotea" kwa kada Ben Saanane (hata zile kampeni za #BringBackBenAlive zimejifia kifo cha asili), na hawasumbuliwi na serikali ya Magufuli kupuuzia jaribio la mauaji dhidi ya Tundu Lissu, kwanini tutarajie jipya katika mauaji yaliyofanywa dhidi ya Daudi na Acquiline?

Yaani Mnadhimu Mkuu wa upinzani anamwagiwa risasi hadharani wakati mkutano wa bunge unaendelea huko Dodoma, na tunaambiwa kuwa tukio hilo lilitokea katika eneo lenye ulinzi mkubwa na lenye CCTV, kwanini basi wanaosumbuliwa na tukio hilo wasitafute njia stahili za japo kuifanya serikali ione aibu na kufanya japo "uchunguzi wa kizushi"?

Kuhusu hujuma "za kawaida" za uchaguzi, kama kila aina ya uhuni uliofanywa na CCM kwenye chaguzi ndogo za madiwani katika kata 43 uliofanyika Novemba mwaka jana uliruhusiwa upite "kimya kimya" – kwa maana kwamba hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya uhuni huo – kwanini basi chaguzi hizi ndogo katika jimbo la Siha na Kinondoni zilitarajiwa kuwa tofauti?

Na katika hili, inapaswa wana-Chadema wajiulize kuhusu busara za viongozi wao kuamua kushiriki katika chaguzi hizo ndogo Siha na Kinondoni ilhali mazingira yaliyokuwepo yalikuwa yaleyale yaliyopelekea chama hicho kususia chaguzi nyingine ndogo tatu katika majimbo ya Longido, Singida Kaskazini na Songea Mjini uliofanyika mwezi uliopita.

Hadi wakati ninaandika makala hii, tayari Tume ya Uachaguzi ilikuwa imeshamtangaza mgombea wa CCM jimbo la Siha, Godwin Mollel kuwa mshindi kwa tofauti kubwa tu ya kura dhidi ya mgombea wa Chadema. Hata kama CCM wameiba kura, ukubwa wa tofauti kati ya kura za mgombea wao na huyo wa Chadema zinaashiria kuwa chama hicho kikuu cha upinzani kilipitisha mgombea fyongo.


Na kama ilivyotarajiwa mgombea wa CCM jimbo la Kinondoni, Maulid Mtulia, naye ametangazwa mshindi.


Mie mtumishi wako nilishabashiri mapema tu kuwa chama hicho tawala kingeshinda majimbo hayo, "iwe isiwe."

Ushindi kwa wagombea hao wa CCM ulipaswa kupatikana kwa gharama yoyote kwa sababu laiti wangeshindwa, kinachoelezwa kama "mkakati wa Magufuli kuua upinzani kwa kununua wabunge na madiwani wa Upinzani"  kingemfanya achekwe hata huko kwenye chama chake.

Na kwa vile hadi sasa wabunge na madiwani waliohama upinzani na kujiunga na CCM wamefanikiwa kurudi madarakani baada ya chama hicho tawala kuwapa fursa ya kuwa wagombea wake kwenye chaguzi ndogo, na kuwasaidia kwa hali na mali washinde, tutarajie wabunge na madiwani wengin zaidi kuhama vyama vya upinzani na kujiunga na CCM. Kisa? "Dili hilo linalipa," kwa CCM na kwa wanasiasa hao wanaohama.

Na unadhani mbunge au diwani "mwenye moyo mwepesi" akiona jinsi chama chake "kilivyochukulia poa" yaliyowasibu akina marehemu Mashaka na Daudi, na yaliyowasibu Ben Saanane na Lissu, kwanini iwe ngumu kwake kushawishika kuhama?

Ningetamani sana kuhitimisha makala hii kwa kushauri nini kifanyike lakini itakuwa kupoteza muda wangu na muda wako msomaji. Ni vigumu mno kuwashauri watu waliokubali kwamba mgao wa umeme ni stahili yao kwa zaidi ya miaka kumi sasa, na ambao kila mara umeme unaporudi wanashangilia kana kwamba wamepewa upendeleo flani.

Kama Watanzania wameshindwa kuilazimisha Tanesko iache mgao wa umeme, wataweza kweli kuilazimisha CCM iache hujuma dhidi ya vyama vya upinzani na demokrasia kwa ujumla? Ndio maana bila utu wala aibu, chama hicho tawala kinapata ujasiri wa kukifanyia mzaha kifo cha Acquiline ambapo kwa kudai polisi (haohao waliomuua binti huyo) wachukue hatua dhidi ya Mbowe. Utterly disgusting!


Na kama mauaji mbalimbali ya kisiasa huko nyuma yameachwa yapite na kusahaulika, kwanini tutarajie miujiza kwenye mauaji haya ya sasa dhidi ya wapendwa wetu Daudi na Acquline?

Na ukweli mchungu ni kwamba Magufuli ataendelea kuwapelekesha Watanzania atakavyo ka sababu si watangulizi wake -Mwinyi, Mkapa na Kikwete – wenye jeuri ya kumwambia "Ee bwana ee, huku unakoipeleka nchi siko." Hawawezi kwa sababu nao ni kama "mateka." Madhambi waliyofanya kwenye tawala zao yanawafanya wahofie hatma yao pindi wakimkosoa "mungu-mtu" aliyepo madarakani.

Na wakati wastaafu au watumishi wa zamani wa Idara za Usalama wa Taifa kwenye nchi kama Marekani wamekuwa mstari wa mbele kukemea kila tendo linalotishia usalama wa nchi hiyo – kwa mfano 'ndoa' kati ya Rais Donald Trump na Russia – wastaafu wetu sie hawana jeuri ya kufungua mdomo sio tu kwa vile wanahofia kuathiri posho na marupurupu yao bali kwa vile nao ni mateka wa "madudu" waliyofanya walipokuwa madarakani. Ukiwa mchafu unajinyima uhuru wa kukemea uchafu.


Basi niishie hapa kwa kurejea tena salamu zangu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Daudi na Acquiline. Ni vigumu kuwaambia maneno yanayotosha kuwaliwaza lakini la muhimu ni kuendelea kuzikumbuka roho za marehemu hao, hasa katika kipindi hiki cha Kwaresma ambapo sisi Wakristu tunaadhimisha mateso ya Bwana Yesu Kristo. Pumziko la Milele awape Bwana, na Mwanga wa Milele awaangazie, wapumzike kwa amani. Amen


30 Sept 2017

Mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka juzi nilipata ujumbe kutoka kwa watu kadhaa wakinieleza kuwa kwa namna moja au nyingine niliwasaidia kufanya maamuzi ya kumpigia kura aliyekuwa mgombea wa CCM, John Magufuli.

Unajua, moja ya makosa makubwa waliofanya wana-UKAWA kwenye kampeni za uchaguzi huo ni kutojihangaisha kulifikia kundi muhimu la wapigakura nchini Tanzania: wananchi wasiofungamana na chama chochote.

Ili kulielewa vema kundi hili, inabidi kuangalia idadi ya wanachama wa CCM na UKAWA (kwa kuzingatia uchaguzi wa mwaka 2015). Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa CCM ina wanachama milioni 8. Makadirio ya idadi ya wanachama wa UKAWA ni angalau milioni 5. Kwahiyo makadirio ya jumla ya wapigakura wenye kufungamana na vyama vya siasa ni takriban milioni 13. Tanzania ina watu zaidi ya milioni 50, tukitoa hao milioni 13 tunabakiwa na watu milioni 37. Tukienda kwenye idadi ya waliojiandikisha kupiga kura walikuwa milioni 23 hivi. Kwahiyo, kimahesabu, takriban watu milioni 10 (milioni 23 waliojiandikisha kutoa milioni 13 wenye ufuasi wa vyama vya siasa) walikuwa wapigakura wasiojihusisha na chama chochote.

Tofauti na UKAWA ambayo viongozi na wanachama wake walielemea zaidi kuhamasishana wao kwa wao, wenzao wa CCM waliwalenga hao takriban milioni 10 wasiofungamana na chama chochote.

Na kimsingi, mie japo sikuwa mpigakura, nilikuwa katika kundi la watu wasio na vyama. Mara ya mwisho kuwa mwanachama wa chama cha siasa ilikuwa mwaka 2005, na takriban miaka 15 baadae, sheria ilinizuwia kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa.

Mwaka 2006 nilianza kufuatilia skandali ya Richmond iliyokuwa ikimhusisha aliyekuwa Waziri Mkuu wa wakati huo, Edward Lowassa. Naweza kwa uhakika kuwa nilikuwa bloga pekee niliyevalia njua suala hilo, sambamba na kuliandikia makala mbalimbali katika magazeti ya ‘Kulikoni’ na baadaye ‘Mtanzania’ na hatimaye Raia Mwema. Ufuatiliaji huo ulinigharimu mno lakini hilo si la muhimu kwa sasa.

Kutokana na bughudha niliyopata kuanzia mwaka 2006 na kuendelea, haikuwa ajabu kwa mie kuunga mkono harakati za Chadema kupambana na ufisadi. Na mwaka 2010 nilishiriki kikamilifu kumnadi mgombea urais wa Chadema, Dkt Wilbrord Slaa. Hata baada ya uchaguzi huo, niliendelea kuunga mkono sera hiyo ya ufisadi ya Chadema. Hata hivyo, sikuwahi kuwa mwanachama wa chama hicho.

Mwanzoni mwa mwaka 2015 nilikuwa miongoni mwa watu waliopiga kelele kwenye mitandao ya kijamii kuwataka UKAWA watangaze mgombea wao wa kiti cha urais mapema hasa ikizingatiwa kuwa CCM walikuwa na safari ndefu ya ‘kung’oana macho’ kugombea kuteuliwa na chama chao kuwania urais. Hata hivyo, kelele hizo hazikuzaa matunda, na utetezi mkubwa ulikuwa “UKAWA inajibidiisha kushughulikia daftari la wapigakura sambamba na kuhamasisha wapigakura watarajiwa kujiandikisha.” Hatimaye tulikuja kufahamu kuwa mbinu hiyo ya “kununua muda” ililenga kumwandalia nafasi Bwana Lowassa endapo asingepitishwa huko CCM. Muungano wa vyama makini vinne vya upinzani unasubiri ‘kapi’ kutoka chama tawala!

Kufupisha stori, mara baada ya UKAWA kumtangaza Lowassa kuwa mgombea wao, kwa sie wengine ilikuwa haiwezekani tena kuunga mkono umoja huo uliojumuisha vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD.

Kwa vile wagombea wakuu katika uchaguzi huo walikuwa Lowassa na Magufuli, ilikuwa vigumu kumpinga Lowassa bila kumsapoti Magufuli. Kwahiyo japo awali nilijaribu kuepuka kumnadi mgombea wa CCM, Magufuli, mazingira yaliyokuwepo – pamoja na mkataba wa kutoa huduma ya usadi (consultancy) – ilipelekea nami nianze kumnadi Magufuli. Haukuwa uamuzi rahisi hasa kwa kuzingatia serikali ya CCM ilivyonitenda kuanzia mwaka 2006 nilipoanza kufuatilia skandali ya Richmond.

Ushiriki wangu kwenye kampeni haukuwa rahisi. Katika maisha yangu yote sikuwahi kutukanwa kiasi nilichotukanwa katika kampeni za uchaguzi huo. Jitihada zangu za kuwaelewesha watu kwanini nimelazimika kumuunga mkono Magufuli hazikusaidia kitu. Pengine kibaya zaidi ni kwamba wakati wa kuelekea uchaguzi huo nilifiwa na baba yangu, marehemu Mzee Philemon Chahali. Baadhi ya watu bila utu walitumia msiba huo kuingiza uhasama wa kisiasa.

Pamoja na mvua ya matusi ya kila aina, niliendelea na jukumu la kumnadi Bwana Magufuli. Nadhani mchango wangu mkubwa zaidi ulikuwa kwa wapigakura waliokuwa hawajafungama na chama chochote. Na nilifahamu kuhusu hilo baada ya uchaguzi ambapo baadhi yao walinieleza bayana kuwa ushawishi wangu kwao ulipelekea kufanya uamuzi wa kumpigia kura mgombea huyo wa CCM.

Lakini tukiweka kando ‘sababu zangu binafsi,’ Magufuli alionekana kama mgombea bora zaidi ya mpinzani wake Lowassa. Pamoja na sababu nyingine, wakati Magufuli alikuwa ‘mgombea wa CCM kutoka CCM,’ Lowassa alikuwa mgombea wa UKAWA kutoka CCM.

Hatimaye uchaguzi ukafanyika na Magufuli akaibuka mshindi. Kama kuna kitu kilichonipa matumaini sana kuhusu urais wa Magufuli ni hotuba yake aliyoitoa wakati wa uzinduzi wa bunge la Jamhuri ya Muungano. Katika hotuba hiyo, Magufuli alionyesha kuwa mtu anayezielewa vema shida za Watanzania hususan janga la rushwa na ufisadi, na akaapa kushughulikia kwa nguvu zake zote. Na alipoomba Watanzania wamwombee katika vita hiyo ngumu, naamini hata miongoni mwa wale ambao hawakumpigia kura waliitikia wito huo wa kumfanyia maombi.

Kisha zikaja ziara ya kushtukiza na taratibu tukaanza kuingiwa na matumaini mapya ya “mrithi halisi wa Nyerere/Sokoine.” Na dunia pia ikaungana nasi kusherehekea kiongozi huyo adimu, na ikaibuka alama ya reli #WhatWouldMagufuli Do iliyotamba kila kona ya dunia. Na haikupita wiki bila kushuhudia “tumbua majipu.”

Kwa kufurahishwa na kuridhishwa na utendaji wake, mie ‘nikajipinda’ na kuandika kitabu cha tathmini ya urais wa Magufuli, siku 55 tu baada ya yeye kuapishwa kuwa Rais wa tano wa Tanzania. Watu kadhaa walinikosoa kwamba haikuwa sahihi kwangu kufanya tathmini hiyo mapema kiasi hicho. 


Kwa wakati huo niliona walionikosoa kuhusu suala hilo kama watu wenye chuki binafsi dhidi ya ‘mkombozi’ Magufuli.

Dalili ya kwanza kwamba huenda kuna walakini katika utawala wa Magufuli ni pale alipotangaza baraza lake la mawaziri ambalo ilituchukua wiki kadhaa kulisubiri. Lilipotangazwa, sio tu lilikuwa kubwa kuliko ahadi yake kuwa angeunda serikali ndogo tu ili kupunguza gharama za uendeshaji wa serikali, bali pia lilijumuisha baadhi ya sura ‘zenye utata.’ Miongoni mwa sura hizo ni Profesa Muhongo, ambaye alilazimika kujiuzulu katika serikali ya Awamu ya Nne kutokana na kuhusishwa na skandali ya Tegeta Escrow.

Kuna tuliouona uteuzi wa mtu kama Nape Nnauye kuwa ni wa kisiasa zaidi, huku sura kama Simbachawene, Lukuvi na Profesa Maghembe zikijenga ishara kuwa huenda mambo hayajabadilika kama tulivyotarajia.

Kisha kukafanyika uteuzi wa mabalozi ambao ulionekana bayana kama kutumia nafasi hizo nyeti kuwaondoa watu flani kwenye nyadhifa zao huko CCM. Baadhi yetu tukaanza kujiuliza, “hivi hatujayashuhudia haya huko nyuma?” Lakini tukaendelea kuwa na matumaini.

Dalili ya kwanza kabisa kuwa pamoja na mazuri yake yaliyowavutia Watanzania wengi na kona mbalimbali duniani, Bwana Magufuli ana mapungufu yake ni pale serikali yake kupitia ‘shujaa wa sasa’ Nape Nnauye ilipozuwia haki ya mamilioni ya Watanzania kusikiliza matangazo ya moja kwa moja ya Bunge. Niwe mkweli, wanaomwona Nape shujaa huwa siwaelewi kabisa. Ningemwona shujaa laiti angetumia ukongwe wake ndani ya CCM kumweleza bosi wake Magufuli kuwa wazo la kuzuwia matangazo ya bunge live ni fyongo, na laiti Magufuli angemomea basi angejiuzulu kishujaa badala ya kusubiri kufukuzwauwaziri kwa kupambana na ‘kimeo kingine cha Magufuli’ yaani Daudi Albert Bashite.

Baadaye likaja zuwio dhidi ya mikutano na maandamano ya vyama ya siasa. Awali baadhi yetu tulijipa matumaini kwamba “ah huu ni muda wa kuchapa kazi. Hayo maandamano na mikutano ni ya nini muda huu?” Kwahiyo kwa wakati huo ili-make sense.

Mara tukakumbwa na janga la tetemeko la ardhi huko Kagera. Ikategemewa Rais angekwenda kuwafariji wahanga hasa ikizingatiwa kuwa anatoka Kanda ya Ziwa. Hakwenda hadi baadaye. Na alipokwenda akatoa hotuba isiyopendeza kuisikiliza. Maneno kama “serikali haikuleta tetemeko la ardhi” sio ya busara hata kidogo. Pia akaongopa kwa kudai hakuna serikali duniani inayotoa misaada kwa wahanga wa majanga ya asili. Sijui muda huu anajisikiaje akiona kwenye runinga jinsi serikali ya Marekani inavyowahudumia wahanga wa vimbunga.

Baadaye kukusikika taarifa mbalimbali za tishio la uhaba wa chakula, lakini badala ya kuwafariji wananchi, Magufuli akawaropokea kwamba serikali yake haitotoa chakula kwa vile serikali haina shamba.
Na wakati mmoja alipita sijui Nzega au Urambo, mwananchi mmoja akamwambia “njaa Mheshimiwa.” Hilo jibu alilotoa utadhani ugomvi. Pamoja na majibu mengine ya ngebe akasema “njaa, kwani mnataka niingie jikoni kuwapikia?” Ovyo kabisa.

Likatokea tukio la maaskari polisi wanane kuuawa huko Kibiti lakini Amiri Jeshi Mkuu akaenda kufungua mabweni chuo kikuu cha Dar es Salaama badala ya kwenda kuaga miili ya askari hao.

Pia kulijitokeza tukio la ‘kupotea’ kwa kada wa Chadema Ben Saanane ambaye hadi ‘kupotea’ kwake alikuwa akihoji kwa nguvu kubwa kuhusu PhD ya Magufuli. Baadhi tulimsihi awe makini (kwa sababu dalili zilishaanza kujionyesha kuwa Magufuli ni mtu wa aina gani) lakini bahati mbaya hakusikia ushauri wetu. Hadi leo haijulikani nini kimemsibu kijana huyo japo Chadema nao hawawezi kukwepa lawama katika poor handling ya suala hilo. Kumekuwa na kauli zinazokinzana kutoka kwa baadhi ya viongozi wa chama hicho kama ile ya mwenyekiti Mbowe kuwa Ben alitekwa huku Mbunge wa chama hicho Saeid Kubenea akidai kuwa kada huyo anaonekana vijiweni. Kwanini chama hicho hakijawabana viongozi hao kufafanua kauli zao, only God knows!

Lakini kama kuna tukio lililompotezea heshima kubwa Bwana Magufuli ni lile la Mkuu wa Mkoa Paul Makonda kuvamia stesheni ya redio na runinga cha Clouds  akiwa na askari wenye silaha. Siku chache baadaye huku baadhi ya watu wakitarajia angemtimua Makonda, Magufuli akatufanya sote mabwege kwa kumtetea Makonda huku akidai yeye hapangiwi kazi, yeye ndo Rais, na kumwita Makonda mchapakazi. Yaani Mkuu wa Mkoa amevamia kituo cha habari, kitendo ambacho ni kosa la jinai, halafu Rais anamsifu kuwa ni mchapakazi?
Uswahiba wa Magufuli na Makonda umechangia mno ugumu wa kuchunguza tuhuma kuwa mkuu huyo wa mkoa amefoji jina analotumia pamoja na cheti cha kuhitimu kidato cha nne. Laiti Magufuli angekuwa mwajibikaji kama tunavyoamini basi angeamuru uchunguzi kuhusu suala hilo.

Na kwa wanaofahamu yanayoendelea ‘nyuma ya pazia,’ inadaiwa kuwa vetting aliyofanyiwa Bashite ilionyesha bayana mapungufu yanatajwa kumhusu yeye, na ‘Bwana mkubwa’ akashauriwa kuchukua hatua stahili lakini hakufuata ushauri huo.

Hili la Bashite limeendelea kuwakera watu wengi sana, hasa ikizingatiwa kuwa mtu huyo anatumia ipasavyo upendeleo anaopewa na Magufuli, na kufanya dharau za wazi kama ile ya kupigiwa saluti na vingozi wa ngazi za juu wa jeshi la polisi huku amevaa kapelo. Hiyo ni dharau ya hali ya juu kwa vyombo vyetu vya dola.



Na Magufuli ataingia kwenye vitabu vya historia kwa serikali yake kulifungia gazeti la kila wiki la Mwanahalisi kwa miaka mitatu, na siku 10 baadaye akalifungia gazeti jingine la kila wiki la Raia Mwema kwa siku 90. 

Na kama kuna gazeti lilijitahidi mno 'kumnadi' Magufuli ni Raia Mwema. Nakumbuka makala nyingi katika gazeti hilo wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi zilisheheni habari 'nzuri' kuhusu Magufuli.

Pengine si vibaya nikitumia fursa hii kueleza kuwa sababu hasa iliyonifanya niache uandishi wa makala katika gazeti hilo ni kwamba lilihojiwa na 'vijana wa Magufuli' kuhusu mie lakini wahusika hawakuona umuhimu wa kunieleza wala kuandika kuhusu habari hiyo.


Na kilichopelekea bwege huyo kudadisi kuhusu mie ni TWEET...Yes, just a tweet, a #FutureTweet to be precise. 

Kanuni muhimu katika chombo cha habari ni kwamba unyanyasaji wa taasisi yoyote ile dhidi ya mwenzenu ni unyanyasaji dhidi yenu nyote. Gazeti hilo lilipaswa kunijulisha kuhusu kilichotokea au kukiandika kama habari gazetini. Lakini bahati nzuri mie mzoefu wa 'dark arts' nikafahamu mapema kilichokuwa kinaendelea.

Hata hivyo, kitendo cha gazeti hilo nilikiona kama usaliti, nikaamua kuachana nao. Hata hivyo, mie sina kinyong'o nao na ndio maana jana nililaani na kupiga kelele kuhusu hatua hiyo ya serikali.

Haya yanatokea wakati Tanzania bado ipo kwenye mshtuko kufuatia jaribio la kumuua mwanasiasa ambaye amekuwa mpinzani mkubwa wa Magufuli, mbunge wa Chadema Tundu Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria cha TLS. Chuki inayopandikizwa dhidi ya wapinzani imepelekea takriban asilimia 99 ya viongozi wa CCM kuogopa kwenda kumjulia hali Lissu huko Nairobi alikolazwa.

Lakini pengine kipimo halisi cha mambo kwenda kinyume na matarajio ya baadhi yetu kuhusu Magufuli ni kwamba tangu aingie madarakani, zaidi ya viongozi na wanachama 400 wa Chadema wamekamatwa na polisi. Imefika mahala, wakuu wa wilaya wanakamata viongozi wa Chadema kila wanapojisikia. Na pengine kibaya zaidi ni ukweli kwamba taratibu jamii inaanza kuzowea kuona viongozi na wanachama wa upinzani – hususan Chadema – wakidhalilishwa na kukamatwa kiholela.

Jambo jingine la kusikitisha kuhusu utawala wa Magufuli ni utitiri wa sheria kandamizi kuhusu uhuru wa habari. Licha ya sheria ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015 ambayo ni kazi ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, tayari kuna sheria ya Huduma za Habari, ambayo ‘shujaa Nape’ alihusika kwa kiasi kikubwa, na sasa kuna kinachoitwa ‘Kanuni za Maudhui ya Mitandao ya Kijamii,’ ambayo laiti zikipitishwa zitakuwa balaa kubwa.

Na huku Chadema ikishuhudia viongozi na wanachama wake wakinyanyaswa ovyo ovyo, kuna kila dalili kuwa mgogoro unaoendelea ndani ya chama cha CUF una mkono wa serikali hasa kwa kuzingatia mwenendo wa ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (taasisi ya serikali) kuibeba waziwazi kambi ya mwanachama aliyejiuzulu kwa utashi wake Prof Lipumba, ambaye from nowhere alirudi chamani na kudai yeye bado mwenyekiti.

Majuzi, Magufuli katumwagia siri kwamba kuna siku aliombwa ushauri na Spika Ndugai kuhusu uteuzi wa wajumbe wa kamati ya bunge. Hiyo ina maana kuwa bunge limewekwa mfukoni na mhimili wa serikali. Kadhalika, kauli za Jaji Mkuu ‘mpya’  baada ya jaribio la mauaji dhidi ya Tundu Lissu zinajenga taswira ya mhimili wa mahakama nao kuwekwa mfukoni na mhimili wa serikali.

Katika kuhitimisha makala hii ndefu ninarudia swali lililobeba kichwa cha habari: nini kilichomsibu Magufuli hadi kubadilika kiasi hiki? Kauli yake kuwa alisukumwa kuchukua fomu ya urais inazidi kuleta mkanganyiko kwamba labda alikuwa anafahamu fika hana uwezo wa kuongoza taifa letu lakini akakubali tu kutokana na shinikizo hilo, ambalo hata hivyo hatujui limetoka kwa watu gani.

Dalili kwamba ‘Magufuli atabadilika’ (kurejea kuwa yule tuliyemwona ni mkombozi wetu) ni finyu. Kwa vile maamuzi yake mengi yanamtengenezea maadui zaidi ya waliopo, kuna kila dalili kwamba atazidi kuwa mkali ili ‘kujilinda.’ Tutegemee uhuru wa kujieleza/habari uendelee kubinywa zaidi kadri bwana mkubwa anavyozidi kutukumbusha yeye ndio Rais, asiyeambiwa nini cha kufanya, anayejua siri zote na nchi yetu, na vitu kama hivyo.

Nimalizie kwa kuwakumbusha Watanzania wenzangu kuhusu rai ya mara kwa mara ya Rais Magufuli kuwataka Watanzania tumwombee. Na tufanye hivyo kwa bidii kubwa ili Mwenyezi Mungu amwonyeshe njia sahihi ya kuliongoza taifa letu kwa kuzingatia haki na usawa. Tumwombee aondokane na 'fear of the unknown,' apate muda wa kupumzika badala ya kukesha macho akihofia 'the unknown.' Aachane na chuki dhidi ya kila anayemkosoa hata kama kukosoa huko ni kwa nia njema. Tumwombee awe na busara ya kutokitumia 'kitengo' kama kampuni yake binafsi. Ajiulize, kwanini licha ya ulinzi wake wa 'kufa mtu' bado siri zinavuja? Jibu jepesi: ukiwafanya watu wazima tena wenye utaalamu nyeti kuwa kama watoto, inakuwa 'mwaga ugali nimwage mboga.' Na asije kukasirishwa na makala hii...

Ni wazi kuwa ndoto za kuikomboa Tanzania yetu kiuchumi haziwezi kufanikiwa katika hali ya sasa ya siasa za vitisho, kunyanyasa wapinzani, “watu wasiojulikana,” na vitu kama hivyo. 

Mungu ibariki Tanzania


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.