Showing posts with label BIG BROTHER. Show all posts
Showing posts with label BIG BROTHER. Show all posts

4 Jun 2009


Sophie Reade, 20
Glamour model from Cheshire
Sophie, whose bra size is 30GG, has been working as a glamour model for two years, posing nude for UK Playboy magazine and appearing at motorbike shows - but has never told her parents.
Charlie Drummond, 22
Customer service advisor from Newcastle
Charlie is a former Mr Gay UK contestant who won the Newcastle heat back in 2007. He has worked as a model but now works in customer service for the Job Centre which he loves
Karly Ashworth, 21
Unemployed and from Fife
A part-time glamour model and one of FHM's "high street honeys", Karly says her job defines her 100% as she loves to show off, knows how to work the camera, and loves looking good. Her proudest achievement was being accepted to study art and design at Dundee University, though she left after only three weeks. Karly is passionate about women's rights, empowering women and stopping domestic violence. She believes in God but would not class herself as a proper Christian as she has had sex before marriage....
Rodrigo Lopes, 23
A student from Brazil
Rodrigo is half Italian, half Brazilian and came to the UK to study and to search for a better life... Before he came to the UK he wasn’t interested in men but now he thinks he might be gay, although on average he dates an equal amount of men and women...Once, after a night out, he couldn’t afford the taxi home so paid the taxi driver by giving him his shoes.
Saffia Corden, 27
Beauty consultant from Nottingham
A mother of two, Saffia hates people who stereotype her as a single mum and strives to be just the opposite...Single Saffia said she considered turning lesbian because she is sick of men.
Cairon Austin-Hill, 18
A student from Florida
Cairon was born in London but moved to Florida when he was a year old. He returned two years ago and now lives in London with his dad...He says that people perceive him as a joker or a ‘sarcastic prick’ and that his dad calls him Cassanova as he used to be a ‘player’ but not so much anymore.
Lisa Wallace, 41
Unemployed and from Birmingham
Lisa has worked in various factories throughout her life and says she has learned to go without and is not greedy. She was a geeky teenager who came out as a lesbian to a teacher after being teased about it .
Marcus Akin, 35
A window fitter from London
Something that Marcus has not done for 20 years is share a house with someone, let alone 15 fellow housemates. He describes himself as a big kid in a man’s body... A porn star or toy designer would be his ideal job.
Sophia Brown, 26
Private banking assistant from London
Sophia, who is 4ft 11in and has suffered from lupus since she was young, describes herself as fun, fierce and feisty. Her proudest achievement was getting an A* in GCSE English...
Siavash Sabbaghpour, 23
An events organiser, formerly from Iran
Siavash grew up in Iran but moved to the UK when he was a child. He lives with his mum but mostly stays with friends. He has never paid a rent bill in his life.Siavash dropped out of studying fashion at university, saying he hated it because he was surrounded by people without money....He is sure he will be a millionaire in ten years time. His biggest regret in life is not having a bigger penis...If he could make a law it would be for ugly people not to be allowed to have children.
Noirin Kelly, 25
Retail manager from Dublin
A former All-Ireland athletics champion who describes herself as a "girly girl", Noirin says she believes education is the answer to everything. She is a self-assured straight talker, though she says she has a bad habit of speaking before she thinks, so could end up insulting people unintentionally.
Noirin is a practising Catholic

Freddie George Fisher, 23
An entrepeneur from Market Drayton
Oxford University graduate Freddie describes himself as a polymath: a free spirit for whom 2009 is about blossoming, which is why he decided to go into the Big Brother house....He gets annoyed when people put his achievements down to the wealth of his parents...Freddie was a member of the young Conservative association although says he is an anarchist at heart...Freddie doesn’t own a TV and claims that he doesn’t really have a clue how Big Brother works.
Angel McKenzie, 35
Professional boxer and artist from south London
Originally from Russia, Angel is an ex-rock star who moved to England 12 years ago and now runs a gym owned by her adopted "father", a former British and European boxing champion.
She is passionate about boxing and fitness, neither smokes nor drinks alcohol and says she will approach the Big Brother experience as if it were a boxing bout.
Angel left home at 24 to pursue a career as a rock star, and was well known in Russia.
Kris Donnelly, 24
A visual merchandiser from Shrewsbury
Kris says he dropped out of University after the girls stopped doing his work for him. When he was younger he never had any job aspirations....Single Kris says he doesn’t have a girlfriend, through choice, because he is waiting for The One, although he does admit that he pulls someone every time he goes out.
Beinazir Lasharie, 28
Study support assistant from London
Beinazir's family were forced to flee their native Pakistan and seek asylum in the UK when she was one year old after her father - a supporter of Benazir Bhutto after whom she was named - received death threats over his political views.
Sree Dasari, 25
Student union elected president from India
Sree grew up in India, and left the country for the first time when he came to England to study for a masters degree in business....Sree says that girls tend to love him as he can flatter anyone. Sree intends to stay a virgin until he meets the right girl. He is looking for someone that is patient, committed and honest and says his ideal woman is Beyonce.

18 Nov 2007

Soma makala nyingine mbili hapa

Asalam aleykum,

Moja ya mambo nayopendelea kufanya pindi muda unaporuhusu ni kuangalia runinga.Lakini naweza kusema kwa kujiamini kabisa kwamba mahaba yangu kwa runinga yamekuwa ni sawa na mithili ya kuingia darasani kwani ni nadra kwangu kupitisha siku nzima pasipo kujifunza kitu kipya kwenye runinga.Hiyo haimaanishi kwamba kila kipindi nachoangalia kina jambo jipya au la maana,bali najitahidi kuwa makini katika uchaguzi wa kile nachoangalia.Halafu nimejenga desturi ya kuangalia runinga huku laptop yangu ikiwa pembeni.Hiyo huwa inanirahisishia kufanya “reference” ya kitu nachokiona kwenye runinga lakini pengine hakijafafanuliwa vizuri.Inapotokea hivyo basi huwa naingiza neno husika kwenye mtambo wa kusaka habari kwenye mtandao ujulikanao kama “Google” au nakimbilia kwenye tovuti nyingine maarufu kwa maelezo ya watu na vitu ijulikanayo kama “Wikipedia”.

Kitu kimoja nilichojifunza kuhusu vipindi vya televisheni hapa Uingereza ni namna mashindano ya kupata watazamaji yalivyo juu.Kutokana na mashindano hayo,vituo vya televisheni hujitahidi kuja na ubunifu wa kila namna,wa maana na wa kipuuzi.Na miongoni mwa ubunifu huo ni hivi vipindi vinavyojulikana kama “reality tv” ambavyo kwa tafsiri isiyo rasmi ni vipindi vinavyoonyesha maisha katika uhalisi wake.Sintoingia kwa undani sana kuelezea maana ya vipindi vya namna hiyo kwani nilishawahi kuviongelea katika makala yangu moja huko nyuma.Ila kwa kukumbushia tu,katika makala hiyo nilizungumzia mbinde iliyojitokeza kwenye kipindi cha “celebrity big brother”,yaani “Big Brother” kama hiyo aloshinda Richard lakini wahusika wake wanakuwa “watu wenye majina” (celebrities).Hiyo ni “version” (aina) tofauti ya “Big Brother” ya kawaida ambayo kwa mwaka huu iliweka historia ya kupata mshindi Mweusi,Brian,Mwingereza mwenye asili ya Nigeria.Katika “Celebrity Big Brother” iliyopita kulizuka migogoro wa ubaguzi wa rangi dhidi ya stta wa filamu za Kihindi,Shilpa Shetty,ambapo washiriki watatu wakiongozwa na mshindi wa zamani wa “Big Brother” (ya kawaida) Jade Goody,walitoa matamshi kadhaa yaliyoashiria ubaguzi wa rangi.Zilipigwa kelele nyingi sana na nusura mashindano hayo yavunjike kabla ya muda wake,lakini yalifanikiwa kumalizika salama ambapo Shilpa aliibuka mshindi.Sokomoko hilo lilifika hadi bungeni na wakati flani Gordon Brown (Waziri Mkuu wa sasa) akiwa ziarani nchini India alilazimika “kuwaomba radhi” Wahindi kwamba yaliyomkuta Shilpa katika jumba la “Big Brother” sio taswira halisi ya jamii ya Waingereza.

Sokomoko la ubaguzi wa rangi katika kipindi hicho lilipelekea baadhi ya watu kuhoji umuhimu wa vipindi vya namna hiyo na faida yake kwa jamii.Lakini pia lilizua swali moja la msingi,je panapojitokeza vipindi vya kipuuzi namna hiyo wa kulaumiwa ni nani?Waandaaji au watazamaji?Kwamba kama waandaaji watakuwa makini basi ni dhahiri hakutakuwa na upuuzi katika vipindi wanavyoandaa.Lakini pia iwapo kipindi kitaonekana cha kipuuzi basi watazamaji wanaweza kukisusia hivyo kuwalazimisha waandaaji kukirekebisha au kukiondoa kabisa hewani.Ikumbukwe kwamba kwa nchi za Magharibi,vyombo vya habari vinahangaika sana kupata “ratings” nzuri,yaani idadi kubwa ya watazamaji au wasomaji.Wapo wanaodhani kuwa “ratings” zimekuwa zikichochea sana vyombo vya habari kukurupuka na habari zenye utata au za kusababisha mgongano kwani sote twafahamu kuwa “mbwa kung’ata mtu sio habari lakini mtu kung’ata mbwa ni zaidi ya habari”.Yaani kwa kifupi,utata “unalipa sana” kwenye habari.

Nije kwenye “Big Brother” ya akina Richard.Binafsi sikuwa nafuatilia kwa karibu japo ilipokuwa inaelekea ukiongoni nilijikuta natamani Mtanzania mwenzetu Richard ashinde.Lakini tukiwa wakweli na waadilifu,tunaweza kweli kujibu kwa uhakika nini cha msingi tulichojifunza kutokana na mashindano hayo?Hivi kuna lolote la maana la kujifunza pale mshiriki mmoja anapolewa chakari na kuishia kufanya tendo la ndoa huku anafahamu bayana kuwa kamera zinarekodi tukio hilo laivu?Naamini kuna wenzangu wengi tu ambao “Big Brother” kwao ina umuhimu mdogo kuliko hata vichekesho vya kikundi cha “Ze Comedy” ambavyo kwa kiasi flani vinafikisha ujumbe muhimu katika namna ya kuvunja mbavu.Sina tatizo na ushindi wa Richard,ila tatizo langu ni mantiki nzima ya “Big Brother”.

Lakini kama nilivyosema awali kuwa “mtu akimng’ata mbwa inakuwa zaidi ya habari”.Pengine laiti “Big Brother” ikiondoa “manjonjo” ya ngono za hadharani na uchafu mwingine inaweza kupoteza umaarufu na si ajabu ikafutiliwa mbali baada ya muda mfupi.Nadhani vimbwanga vinavofanyika kwenye jumba hilo vinachangia sana kuongeza umaarufu wa kipindi hicho.Kwa bahati mbaya,vimbwanga hivyo havina umuhimu wowote,sio kwa washiriki pekee bali hata kwa watazamaji.Pia nadhani ngono ndani ya jumba la “Big Brother” inaweza kufunua unafiki wa namna flani wa wenye majukumu ya kulinda maadili ya jamii yetu.Nilisoma mahala flani habari kwamba video ya wimbo “Simama Tucheze” wa Q-Chief imepigwa stop kuonyeshwa katika vituo vya runinga kwa vile imejaa vitendo vya ngono.Japo siungi mkono video zenye kuonyesha vitendo vya ngono lakini kinachonifanya niwatolee mimacho “askari wetu wa maadili” ni namna wanavyoweza kufumbia macho matendo ya ngono kwenye jumba la “Big Brother” lakini wanadiriki kumkalia kooni Q-Chief.Na si hapo tu,kama msomaji mpendwa utakuwa msikilizaji wa vipindi vya miziki (hususan vile vya mchana) nadhani utakuwa umeshasikia baadhi ya tungo za muziki wa kufokafoka (hasa wa Marekani) ambazo “hazijachujwa” na hivyo kujumuisha maneno yasiyofaa katika maadili ya jamii yetu.Kwa kawaida na kwa kuzingatia ujumbe uliomo,nyimbo za kufokafoka hutolewa katika “versions” mbalimbali lakini nazozungumzia hapa ni “radio version” (ambapo “maneno machafu” huwa yamefutwa,yamehaririwa-edited-au yameminywa) na “dirty version” (ambapo kila neno linasikika bila kujali “makali” yake).Inawezekana watangazaji wanaopiga “dirty versions” radioni huwa hawajui kinachoongelewa katika nyimbo hizo au wanajua lakini hawajali kwa vile “askari wa maadili” hawana muda wa kufuatilia.

Kabla ya kuandika makala hii nilisoma Sera ya Taifa ya Utamaduni ambayo inaharamisha waziwazi burudani zinazoendana kinyume na maadili ya jamii yetu.Lakini nadhani ufuatiliaji ni mdogo kwani hata video za baadhi ya nyimbo za wakongomani (Wazaire) ni “chafu” mno kuzionyesha kwenye runinga.Na kama unadhani hiyo ni ndogo basi nenda kajionee “ubunifu” wa bendi zetu katika suala zima la unenguaji.Amin nakuambia,namna baadhi ya wanenguaji wanavyocheza ni mithili ya kuangalia filamu ya “X”.Ukilogwa kwenda na mama mkwe kwenye shughuli kama hizo basi unaweza kujikuta unamtaka radhi kwa namna wanenguaji “wanavyojituma”.

“Askari wa maadili” wanakabiliwa na changamoto nyingine kubwa ya kudhibiti watazamaji wenye umri mdogo kwenye shughuli “za watu wazima”.Kwa hapa Uingereza,ili kijana aweze kuingia kwenye ukumbi wa disko ni lazima awe na kitambulisho kinachoonyesha kuwa umri wake unamruhusu kuingia humo.Na hilo ni hata kwenye kununua pombe na sigara.Sheria iko wazi na inasomeka kwenye kila duka kwamba ili mteja anayeonekana kuwa na umri mdogo aweze kuuziwa bidhaa anapaswa kuthibitisha umri wake.Lakini kwa huko nyumbani ni suala la kawaida kumwona mtoto mdogo kabisa akiwa na “michupa kadhaa ya bia” akielekea grosari au baa kwenda kununua bia.Hivi lile zoezi la kuanzisha vitambulisho vya taifa limefikia wapi?Je vitambulisho hivyo vitaonyesha umri wa mwenye kitambulisho?Nadhani mpango huo utakapokamilika basi inaweza kuwa rahisi kwa “askari wa maadili” kuanza kudhibiti watoto na vijana wenye umri mdogo wasiruhusiwe kuingia sehemu zinazoweza “kuwazibua akili” au kuwabana kununua bidhaa kama bia au sigara.

Pengine kabla sijamalizia makala hii utakuwa unajiuliza tangu lini jeshi la polisi limekuwa na kitengo cha “askari wa maadili”.Well, “askari wa maadili” ni pamoja na mamlaka zinahusika na kuhakikisha maadili ya jamii hayavunjwi,kuupuuzwa au kupindwa.Wahusika wengine ni wazazi,kaka,dada,mabaunsa wanaoruhusu watu kuingia disko,wauza maduka na baa,bila kusahau mimi na wewe.

Alamsiki




Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.