Showing posts with label DR MWINYI. Show all posts
Showing posts with label DR MWINYI. Show all posts

30 Apr 2009

Wingu la moshi jijini Dar kufuatia mlipuko wa mabomu maeneo ya Mbagala.Picha kwa hisani ya MICHUZI
Na Mussa Juma, Arusha

WIZARA ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, imeunda Tume ya Wataalam wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kuchunguza chanzo cha kulipuka silaha za aina mbali mbali katika ghala la kambi ya jeshi iliyopo eneo la Mbagala, jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Emanuel Nchimbi alitangaza uamuzi huo jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Ngurdoto, jijini Arusha.

Nchimbi alisema Baraza hilo, litafanya kazi ya kuchunguza chanzo cha ajali hiyo na athari zote ambazo zimetokana na mlipuko huo.

Alisema vilivyokuwepo katika ghala hilo ni mabomu na risasi za aina mbali mbali na silaha nyingine ndogo.

Naibu Waziri huyo, alitoa wito kwa wakazi wote wanaoishi jirani na kambi hiyo kutookota kitu chochote cha chuma na wanapokiona watoe taarifa katika kambi ya JWTZ iliyokaribu nao.

"Endapo wataona au kutilia shaka aina yoyote ya chuma , watoe taarifa haraka katika kambi ya jeshi iliyo karibu nao au katika timu ya wataalam wa jeshi hilo ambayo imeanza uchunguzi," alisema Nchimbi.

Hata hivyo, kwa niaba ya Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi, alitoa pole kwa wote walioathirika na tukio hilo.

"Amiri jeshi mkuu anawapa pole wananchi wote wa Dar es Salaam na Pwani kwa usumbufu ambao wameupata kutokana na tukio hilo," alisema Nchimbi.

Alifahamisha bado chanzo cha ajali hakijajulikana na pia kutokana na sababu za kiusalama haitakuwa rahisi kutangaza athari za kijeshi zilizopatikana kutokana na tukio hilo.
CHANZO: Mwananchi
HIZI TUME HADI LINI?ILE YA AJALI YA CHENGE HAIJATOA TAARIFA YAKE JAPO TUKIO LENYEWE LILIHUSISHA WATU WANNE TU!JE TUKIO KUBWA KAMA HILI TAARIFA SI ITAKUWA MWAKA 2050!?
HIYO WIZARA YA NCHIMBI INA REKODI ISIYOPENDEZA KUHUSIANA NA TUME.HIVI IMESHATUAMBIA MATOKEO YA TUME ILIYOUNDWA KUCHUNGUZA AJALI YA HELIKOPTA YA JWTZ?
LAITI TUNGEKUWA NA UTAMADUNI WA KUWAJIBIKA,BASI MUDA HUU NCHIMBI NA WAZIRI WAKE DR MWINYI WANGEKUWA WAMESHAJIUZULU.LAKINI KWA VILE UWAJIBIKAJI NI MSAMIATI UNAOELEKEA KUTOLETA MAAN KWETU,BASI TUTARAJIE TUME MOJA BAADA YA NYINGINE...NA KWA VILE WATANZANIA WANAONGOZA KWA REKODI YA USAHAULIFU,AT THE END OF THE DAY WAHUSIKA WATAISHIA "KUUCHUNA" TU.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.