Showing posts with label GLOBAL PUBLISHERS. Show all posts
Showing posts with label GLOBAL PUBLISHERS. Show all posts

31 Jul 2013

WARAKA MZITO WA PAPII KOCHA KWA JK

Na Mwandishi Wetu
ULE waraka wa mwanamuziki aliyefungwa gerezani kifungo cha maisha sambamba na baba yake mzazi, Nguza Viking ‘Babu Seya’, Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ umeibua mjadala tena huku Naibu Waziri wa Mali Asili na Utalii, Lazaro Nyalandu akiombwa na kukubali kuufikisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.
Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ (kushoto) akiwa na baba yake Nguza Viking ‘Babu Seya’.
MIAKA 10 GEREZANI
Hivi karibuni wasanii hao walitimiza miaka kumi tangu walipofungwa katika Gereza la Ukonga, Dar mwaka 2003 hivyo kusababisha waraka huo aliouandika Papii Kocha Februari mwaka 2010 kusababisha mjadala upya.
Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, Julai 21, mwaka huu waraka huo ulikuwa gumzo kubwa juu ya ombi la Papii Kocha kwa Rais Kikwete kuwa amhurumie atoke gerezani kwa kuwa bado ni kijana mdogo huku nyuma yake watu wakituhumiana bila ushahidi.
Waraka alioandika Papii Kocha kwa Mhe rais Kikwete.
OMBI KWA WAZIRI NYALANDU
Mwandishi Mtanzania aishie Uskochi, Evarist Chahali aliutundika waraka huo katika ukurasa wake wa Twitter na kusababisha msigano wa kimawazo.
Chahali aliusindikiza waraka huo na maneno akimuomba Waziri Nyalandu kwa kuwa ni mmoja wa ‘memba’ wake mtandaoni aufikishe kwa Rais Kikwete kwa kuwa ulimlenga yeye moja kwa zote.
Alimwandikia Waziri Nyalandu: “Nina imani sana kwako, mheshimiwa waziri na kwa vile Rais Kikwete yupo katika swaumu, natumaini kilio hicho kitasikilizwa.”
Kukawa mchana, kukawa usiku, siku hiyo ikaisha.
Waziri Nyalandu.
WAZIRI NYALANDU AKUBALI
Kesho yake, yaani Julai 22, mwaka huu, Waziri Nyalandu alimjibu Chahali kwa kumwandikia: “Chahali copy that (nimepokea), asante kaka.”

SEHEMU YA MANENO YA KUCHOMA YA WARAKA WA PAPII KOCHA
Baada ya salamu kwa mkuu huyo wa nchi, Papii Kocha aliyekuwa nyota wa Bendi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’ aliandika: “Naanguka na kushika miguu yako mitukufu mheshimiwa rais.
“Nakuomba msaada (msamaha) kwako mheshimiwa rais kwa njia hii ya maandishi kusudi niweze kuondolewa adhabu ya kifungo cha maisha gerezani, niliyohukumiwa na mahakama tajwa hapo juu (Kisutu).
“Mhe. Rais mimi nimefungwa nikiwa bado kijana mwenye umri mdogo. Mpaka sasa natambua wazi hatima pamoja na dhamana ya maisha yangu ipo katika mikono yako mitukufu Mhe. Rais.
“Naomba huruma yako mheshimiwa Rais maana mimi ni mtoto wako ninayehitaji huruma yako wewe mzazi.
“Natumaini kauli yako ya mwisho ndiyo itakayoleta pumzi ya uhai nafsini mwangu.
“Nakutakia kazi njema, afya njema na maisha marefu. Mungu akubariki.”
Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
WAKIKUBALIWA WATAREJEA URAIANI?
Baada ya Waziri Nyalandu kukubali kuupeleka waraka huo ikulu na habari hiyo ikasambaa mitandaoni, baadhi ya watoa maoni walikwenda mbele zaidi wakidai huenda ombi lake litakubaliwa na kumfanya Papii Kocha na baba yake kurudi kula bata uraiani.
Wanamuziki hao walifungwa gerezani kwa tuhuma za kunajisi watoto 10 wa Shule ya Msingi Mashujaa, Sinza jijini Dar.
Mbali na kuachiwa kwa baadhi ya watoto wa familia ya Babu Seya waliokuwa wakitumikia kifungo cha maisha, Papii na baba yake bado wanaendelea kutumikia kifungo hicho hadi sasa.

14 Oct 2008


Wanasema maisha ya jela,popote pale duniani,ni balaa.Lakini maisha ya jela katika nchi masikini kama Tanzania ni zaidi ya balaa.Hebu fikiri,iwapo baadhi ya watu wasio na hatia,na ambao wanalipa kodi kupata huduma stahili,wanateseka kupata HAKI hizo (mifano hai ni kwenye huduma muhimu kama afya,maji,barabara,nk) unatarajia nini kitokee kwa WAHALIFU!Yaani kwa mfano mfupi,kama ndugu wa wanandoa wanawekewa vikwazo kuingia kwenye harusi,what would you expect kwa wazamiaji?

Kuna mantiki zilizojengeka katika jamii kuhusiana na hali flani.Ugonjwa wa ukimwi,mathalan,unahusishwa moja kwa moja na ngono,japo kuna njia nyingine za maambukizi.Kuwa mfungwa nako kunahusishwa moja kwa moja na uhalifu,japo inafahamika wazi kwamba katika baadhi ya sehemu ambapo kuna sheria kwa wenye uwezo na nyingine kwa wasio na uwezo,mtu anaweza kujikuta jela akiwa hana kosa lolote:kasingiziwa kesi,kashindwa kumpata mwanasheria mzuri,nk.Kwahiyo wakati tunahitimisha kwamba wafungwa wote ni wahalifu ni muhimu pia kukumbuka kwamba baadhi yao wapo huko kutokana na haki zao kufinyangwa.Lakini hata kama wote ni wahalifu,hiyo haiondoi umuhimu wa kuwapatia baadhi ya haki za msingi as long as haziwafanyi watamani kuishi jela milele.

Kampuni ya Global Publishers leo imeandaa tamasha la kihistoria huko nyumbani ambapo mwanamuziki mahiri (ambaye kwa sasa anatumikia kifungo cha maisha) Nguza Viking,maarufu kama Babu Seya,na wanae watatumbuiza wafungwa wenzao katika shughuli hiyo itakayofanyika kwenye gereza la Ukonga.Hili ni tukio la kihistoria na Global Publishers wanastahili pongezi nyingi kwa kuja na wazo kama hili.Wakati umefika sasa kuonyesha kwa vitendo kwamba wafungwa ni sehemu ya jamii,hasa ikizingatiwa kwamba status yao ya ufungwa,kwa namna moja au nyingine,ni matokeo ya interaction zao na wanajamii wenzao.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.