Showing posts with label HUDUMA. Show all posts
Showing posts with label HUDUMA. Show all posts

16 Apr 2008

Katika makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema,nazungumzia suala zima la huduma bora.Makala inaanza kwa kuondoa fikra za "u-tambarare" wa maisha ya ughaibuni,zinazochochewa na taswira za runinga na magazeti ya kimataifa.Ni rahisi baadhi ya wenzetu walioko nyumbani kuhisi kwamba mambo huko "majuu" ni asali na maziwa (land of honey and milk).Kilicho sahihi zaidi kuhusu maisha ya sehemu nyingi za dunia ya kwanza ni huduma inayoendana na matarajio ya mteja.Yaani mteja sio tu mfalme au malkia,bali sehemu ya familia ya watoa huduma (of course kuna exceptions...na kwa UK,tuna wahuni kama British Telecoms-BT,na wababaishaji wengine lakini ni wachache).Maudhui ya makala ni hiyo kwenye title ya post hii:TANZANIA YENYE HUDUMA BORA INAWEZEKANA.Pamoja na habari na makala nyingine za daraja la juu kabisa,binjuka na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.

10 Apr 2008

Huduma za afya hapa nyumbani ni duni na hazileti matumaini ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania (by the way,tangu nifike hapa sijaona ile hamasa niliyoikuta 2005 kuhusiana na kauli-mbiu hiyo.Sijui imekufa kifo cha asili au imepotea kama Gavana Daudi Ballali!).Hospitali za umma zinaweza kujitetea kuhusu huduma zao mbovu,na utetezi unaweza kuwa ule uliozoeleka:serikali haitengi fungu la kutosha kwenye sekta ya afya,mishahara ya watumishi ni midogo,na mlolongo wa sababu ambapo mlengwa mkuu ni serikali.Lakini haitarajiwi hospitali binafsi,ambazo gharama zake ni za juu sana,zitoe huduma ya chini ya kiwango.Nimeelezea kwa kirefu kuhusu suala hilo katika makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema.Pamoja na makala nyingine na habari motomoto,bingirika na vyote hivyo kwa KUBONYEZA HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.