Showing posts with label Intelijensia. Show all posts
Showing posts with label Intelijensia. Show all posts

5 Aug 2014

Nianze sehemu hii ya pili ya mfululizo huu kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa wote waliowasiliana nami kuhusiana na mada hii. Kutokana na mawasiliano hayo, nimetambua kuwa mada hii ina umuhimu wa aina yake. Nami ninaahidi kuwaletea kitu kilicho bora kabisa, kwa maana ya 'darasa' kamili lakini pasipo kukiuka wala kukizana na sheria au taratibu zinazolinda fani hii nyeti.

Katika sehemu hii ya pili, tutaangalia jinsi afisa usalama wa taifa anavyopatikana, au kwa kimombo ni recruitment process. Ni muhimu kueleza kwamba taratibu za kujiunga na taasisi za usalama wa taifa duniani kote hupaswa kufanywa kwa umakini mkubwa hasa kwa vile majukumu na wajibu wa shushushu kwa taifa yana umuhimu mkubwa sana.

Kwa nchi 'za wenzetu' kama Marekani na Uingereza, zoezi la uajiri hufanyika kwa uwazi kidogo, kwa maana kwamba matangazo ya nafasi za kazi huwekwa hadharani. Mifano hai ni matangazo ya ajira za ushushushu katika tovuti ya Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) na Shirika la Ujasusi la Uingereza (MI6)




Kwa huko nyumbani Tanzania, zoezi la uajiri wa mashushushu hufanyika kwa usiri mkubwa (angalau taratibu zinapaswa kuwa hivyo). Na hata kwa mashirika ya kishushushu ya nchi nyingine, ajira za wazi kama nilivyoonyesha hapo juu hazimaanishi kuwa waajiriwa wote wa mashirika hayo hupatikana kwa uwazi. 

Kimsingi, na pengine tukitumia mfano 'mwafaka' wa Idara yetu ya Usalama wa Taifa huko nyumbani, kinachoangaliwa kwa mtu anayetakiwa kuajiriwa ni 'vitu vya ziada' pengine tofauti na watu wengine. Katika mazingira stahili (ideal situation) shushushu mtarajiwa anatarajiwa kuwa na uwezo mkubwa wa akili, yaani kama nilivyoeleza katika makala iliyopita kwamba kazi yenyewe ni ya matumizi makubwa ya akili, kwahiyo mtarajiwa anapaswa kuwa intelligent kweli kweli.

Tukiendelea na mazingira hayo stahili, taasisi ya ushushushu huanza kitambo 'kumwinda' wanayetaka kumwajiri. Sehemu mwafaka zaidi za kusaka mashushushu watarajiwa ni katika taasisi za elimu. Sababu kuu za msingi za kutumia taasisi za elimu kama 'soko' la 'kuchagua mashushushu watarajiwa' ni, kwanza, umri wa wanafunzi wengi huwa mwafaka kuonyesha tabia zao halisi, na pili, taasisi ya elimu hutoa ushahidi mzuri wa kiwango cha akili cha shushushu mtarajiwa.

Sehemu nyingine iliyokuwa mwafaka kuwasaka mashushushu watarajiwa ilikuwa kwenye kambi za jeshi la kujenga taifa. Wakati taasisi za elimu zinatoa fursa nzuri kutambua uwezo wa akili wa shushushu mtarajiwa, kambi za JKT zilikuwa zikitoa fursa nzuri ya kuangalia uwezo wa kimwili, hususan uvumilivu (indurance). Kwa waliobahatika kupitia JKT wanafahamu bayana kuwa mafunzo ya awali (takriban miezi 6 ya mwanzo) yalikuwa yanaufikisha mwili katika kiwango cha juu kabisa cha uvumilivu. Ni katika mazingira kama hayo ndipo taasisi za kishushushu zinaweza kupata fursa ya kuona 'uwezo wa ziara' au 'usio wa kawaida' wa shushushu mtarajiwa.

Kadhalika, zamani kulikuwa na shule mbili-katika-moja iliyokuwa na mchepuo wa kijeshi. Shulke hiyo ni Tabora School, ambayo kimsingi ni Shule ya Sekondari ya Tabora Wavulana (Tabora Boys) na Tabora Wasichana (Tabora Girls). Shule hizi ambazo kimfumo zilikusanya wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo yao kutoka takriban kila wilaya ya Tanzania zilitoa fursa nzuri kwa Idara ya Usalama wa Taifa kupata maafisa wake watarajiwa. Uzuri wa shule hizo ni kwamba zilitoa fursa mbili kwa mpigo: fursa kwa mashushushu kupima uwezo wa kiakili wa mtarajiwa na pia kuona uwezo wake kimwili kupitia mazoezi na mafunzi ya kijeshi katika shule hizo. Vilevile, shule hizo ambazo pia zilikuwa na maafisa wa jeshi kama walimu, na wanafunzi wanaovaa sara zinazofanana na za kijeshi , zilitawaliwa na nidhamu ya hali ya juu, sambamba na kuhimiza uzalendo.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora wakiwa katika mafunzo ya kivita

Lakini kwa vile ajira katika taasisi za kishushushu inazingatia zaidi mahitaji ya kimazingira, nyakati nyingine walengwa huwa watu waliopo makazini, kwa mfano wahadhiri, maafisa wa vyombo vingine vya dola - kwa mfano jeshi au polisi- na maeneo mengineyo. Ila ajira za namna hii ni za nadra kwa sababu mara nyingi watu wa aina hiyo 'huajiriwa' kama 'watoa habari' au sources kama wanavyofahamika kiintelijensia. Kinachoweza kuiskumua taasisi ya kishushushu kulazimika kumwajiri mtu ambaye tayari ana ajira nyingine au yupo katika fani tofauti ni unyeti wa nafasi yake na umuhimuwa wake wa muda mrefu. 

Njia hii ni kama ya dharura au ya katika mazingira maalumu kwani kuna ugumu wa kumshawishi mhusika akubali kuajiriwa, na pengine mtu huyo anaweza kuwa na mtandao mkubwa wa kijamii - kwa maana ya familia au marafiki - na hilo linafanya sharti kuu la ajira kwenye taasisi yoyote ya usalama wa taifa, yaani USIRI, kuwa mashakani. Ni rahisi kumkanya mwanafunzi wa sekondari, kwa mfano, kwamba asimwambie mtu yeyote kuhusu jukumu atakalokabidhiwa mbeleni, na akalihifadhi - pengine kwa vitisho- kuliko mtu mzima ambaye inaweza kumwia vigumu kumficha mkewe au marafiki wa karibu. Na kama tujuavyo, ajira katika sehemu hizo zina 'ujiko' wa namna flani, kwahiyo si ajabu mtu mzima akiambiwa 'kuna dili' sehemu akaanza kutangaza kabla hata hajapewa mafunzo.

Kimsingi hakuna muda maalumu wa kumfuatilia mtu anayetakiwa kujiunga na taasisi ya kishushushu. Panapo dharura, zoezi la ufuatiliaji laweza kudumu kwa muda mfupi, lakini pasipo haraka yaweza kuchukua miaka kadhaa. 

Baada ya kuwatambua 'waajiriwa watarajiwa' - process inayofahamika kama spotting - hatua inayoweza kufuata ni kuwa kuwaendeleza watarajiwa hao (yaani kuwaandaa kwa ajili ya utumishi kwa taasisi husika). Neno mwafaka ni development. Katika hatua hii, mashushushu HALISI wanakutana na mashushushu watarajiwa. Hatua hii inaweza kuchukua muda mfupi kutegemea mabo kahdaa au yaweza kuchukua muda mrefu pia. Hadi hapo, taasisi husika huwa haijafikia uamuzi wa kumwajiri mtarajiwa au la, bali inafanya marejeo ya ufuatiliaji wa awali na maendeleo ya mhusika katika kipindi hicho.

Sambamba na hatua hiyo, ni uamuzi kwa taasisi ya ushushushu kuanza kufanya ufuatiliaji wa kina kuhusu mtarajiwa. Ufuatiliaji huo hujulikana kama VETTING. Hata hivyo, uamuzi wa kufanya vetting hutarajia 'potential' ya mtarajiwa, hasa ikizngatiwa kuwa vetting ni process ndefu na inayoweza kuwa na gharama kubwa. Kwa kifupi, process hiyo inalenga kumfahamu mtarajia 'nje ndani' yaani kila kitu kumhusu yeye. Na hapo ndipo utabaini urahisi wa kutafuta mashushushu wapya wakiwa wadogo mashuleni- kwa vile hufanya vetting kutokuwa ndefu sana kutokana na kutokuwa na mtandao mkubwa wa mahusiano kijamii au kimaisha, ilhali kwa mtu mzima kazini itamaanisha kuwafuatilia watu wengi na pengine kutembelea sehemu nyingi pia. Na pindi vetting isipofanywa kwa umakini, dhamira nzima ya kufanya suala hilo kwa usiri linaweza kuathiriwa. Athari hizo si kwa taasisi ya kishushushu pekee bali pia yaweza kuyaweka maisha ya mtarajiwa hatarini.

Matokeo ya jumla ya vetting ndiyo yatakayoamua hatma ya ajira ya shushushu mtarajiwa. Nimesema 'matokeo ya jumla' kwa sababu hata baada ya kuajiriwa, shushushu huendelea kufanyiwa ufuatiliaji na mwajiri wake katika muda wake wote wa utumishi wake, na pengine hadi atakapoaga dunia. Kadhalika, vetting hujitkeza pia pindi shushushu anapotaka kuoa au kuolewa, ambapo mwenza wake hufanyiwa uchunguzi ili kuthibitika kuwa hatokuwa na madhara kwa utendaji wa kazi wa shushushu husika.

Kwa leo niishie hapa. Makala ijayo itaangalia hatua ya kutoka kuajiriwa hadi mafunzo, na itaelemea zaidi kwenye mafunzo. Endelea kufuatilia makala hii pamoja na habari nyingine mbalimbali, na zinazohusu intelijensia kwa kubonyeza hapo juu ya blogu  kwenye kipengele cha  INTELIJENSIA




31 Jul 2014

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Marekani CIA na shushushu mzoefu, John Brennan, akiwa amezungukwa na walinzi wakati akitoa maelezo yake katika 'bunge' la Seneti la nchi hiyo.
Kwa Watanzania wengi, bila shaka mara yetu ya kwanza kufahamu kuhusu mashushushu ilikuwa kupitia vitabu vya Willy Gamba.Unakumbuka 'KIKOMO'? Au 'KIKOSI CHA KISASI?' Au vipi kuhusu 'NJAMA'? Sio siri, kusoma vitabu vya Willy Gamba vya marehemu Aristablus Elvis Musiba kulimfanya kila msomaji atamani kuwa kama Willy Gamba...yaani shushushu. Lakini kwa vile zama za Willy Gamba zilikuwa kipindi ambacho Tanzania ilikuwa kama 'kisiwa' kisichofahamu yanayojiri nje yake, riwaya hizo zilikuwa na mengi yaliyoshabihiana na shushushu wa kimataifa James Bond wa Uingereza.

Lakini baada ya Tanzania kufungua milango yake kwa dunia, wengi walibahatika kumwona James Bond kupitia filamu zake mbalimbali.Lengo la makala hii sio kujadili vitabu hivyo bali kujenga picha halisi, na penine tofauti kati ya ushushushu wa vitabuni au kwenye filamu na uhalisia wa taaluma hiyo. Lakini kabla ya kwenda mbali ni vema pia kukumbushia kuhusu 'Mashushushu wa zama hizi' kwa mfano Jack Bauer wa 'series' ya 24. Wakati Willy Gamba ameendelea kubaki vitabuni tu-kwa maana kwamba hakuna filamu iliyotengenezwa (bado nina fikra za kuyarejesha maisha ya shushushu huyu kwa njia ya filamu), James Bond amekaa 'kizamani' kwa maana ya uwepo wake kwa miaka mingi.Lakini Bauer anaonekana kama 'shushushu wa kizazi kipya' kama ilivyo kwa Nicholas Brody na Carrie wa Homeland, ambao katika filamu zao zina baadhi ya mabo ya kisasa kama matumizi ya mitandao ya kijamii (kwa mfano Facebook na Twitter) na mambo mengine ya 'kwenda na wakati.'

Hata hivyo, japo ushushushu wa kwenye vitabu vya Willy Gamba na filamu za James Bond au series kama 24 na Homeland zinatoa picha ya karibu kabisa na taaluma halisi ya ushushushu, kuna tofauti kubwa kati ya ndadharia na vitendo. Makala hii inazungumzia maisha halisi ya shushushu mstaafu wa shirika la ujasusi la Marekani (CIA), Robert Baer

Kwenye filamu ya hivi karibuni ya James Bond, SKYFALL, 'kubwa la maadui' ni gaidi la mtandaoni (cyberterrorist),Raoul Silva, shushushu wa Kiingereza aliyeasi na mwenye dhamira ya kusababisha 'kiama' kwa ulimwengu wa komputa (digital universe).Ukiangalia filamu hiyo unapata picha ya jinsi janga hilo linavyoweza kuwa na madhara makubwa. 
Lakini kitu pekee cha karibu kati ya ushushushu wa kwenye filamu na ushushushu halisia ni ukaribu na ukweli wa tishio la ugaidi wa kompyuta. Yaani, iwe ni kwenye filamu au katika dunia halisi, kilichomo kwenye filamu hiyo kitakuwa janga kubwa laiti kikitokea. 
Usinielewe vibaya, mie ni shabiki wa filamu za James Bond.Huenda kuziangalia kwa sababu zilezile ambazo kila mwendaji filamu anazo: wanawake warembo, sehemu nzuri za kuvutia, na 'kimuhemuhe' kinachoambatana na stori zinazobeba filamu za Bond.
Lakini kama shushushu mstaafu, kinachonivutia zaidi katika filamu za Bond ni kila mara mema kushinda maovu.Katika filamu zote za Bond, kubwa la maadui huangamia na dunia ya watu wema husalimika. 
Lakini katika ushushushu halisia, mambo hayaendi 'kiuzuri' kama iavyooneshwa katika filamu za Bond, na kwa hakika kuna 'mbinde' kadhaa. 
Tofauti na busara za muda mrefu mrefu kuwa adui wa adui yetu ni rafiki yetu, kwenye ushushushu halisia hali yaweza kuwa tofauti. Wakati flani, kwenye miaka ya 1980,nilipewa kabrasha la viongozi flani wa upinzani nchini Libya, miongoni mwa wengi waliokuwa wakifanya shughuli zao jijini Khartoum,nchini Sudan. Awali, nilkuwa na upeo mdogo tu kuhusu wasifu wa wapinzani wa kingozi wa Libya wa wakati huo,Kanali Muamar Gahddafi. Kitu pekee nilichokuwa na uhakika nao ni kwamba Rais wa Marekani wakati huo,Ronald Reagan, alikuwa anataka Gaddafi aangamie. 
Usiku mmoja, nilishtushwa na sauti za vitako vya bunduki vilivyokuwa vikibamiza mlango wa chumba changu.Watoa habari wangu wawili wa Kilibya walikuwa wakihangaika kulinda maisha yao dhidi ya wauaji wa Ghaddafi na walitegemea mie ndio niwapatie ulinzi.Tulfanya maongezi takriban usiku mzima kuhusu Libya, historia ya nchi hiyo na Allah. Ulipotimu muda salama kwa wao kuondoka, nilikuja kubaini kuwa watu tuliowaamini kuwa wangetusaidia kumwondoa Ghaddafi ni Waislam wenye msimamo mkali ambao lengo lao kuu ni kuifanya Libya kuwa taifa la msimamo mkali wa Kiislam. 
Wakati flani,katika kumfuatilia mtoa habari 'mpotevu,' mwajiri wangu (CIA) alinituma Monaco. Matatizo yalianza hata kabla sijapanda ndege. CIA walikataa kuninulia suti ya tuxedo (ili kuendana na mazingira ya casino za huko) na mhasibu wetu alikataa kunipa fedha za kuchezea kamari.Nilipofika,na kuingia kwenye casino hiyo, walinzi walinihoji kirefu, na mwishowe operesheni hiyo haikufanikiwa kwani sikuweza kumpa mtoa habari niliyekuwa nikimsaka. Kwa hakika nilitambua urahisi alionao James Bond kwenye filamu ni mgumu katik halisi halisi. 
Mtu yeyote aliyepitia chuo cha mafunzo ya mashushushu wa CIA Langley atakwambia maisha ya shushushu yanahitaji uvumilivu mkubwa. Ni muda mrefu wa kuwa peke yako katika kijichumba kidogo, kupitia mafaili kwa undani, mafaili ambayo watu kibao wameshayapitia, matarajio yakiwa wewe utagundua kitu ambacho wenzio hawakukiona. Au kugandishwa kwenye kibanda cha simu kwa muda mrefu ukisubiri labda mtoa habari atakupigia simu. Au kufanya dua kwa matumaini kwamba operesheni yako ijayo sio katika eneo la kutishia uhai.  
Hata hivyo, pamoja na yote hayo sio kusema kwamba katika ushushushu hakuna matukio kama tunayoyaona katika filamu za James Bond.Mashushushu walimwinda Osama bin Laden na hatimaye kufanikiwa kumuua watakueleza kwamba mara kadhaa walikuwa kama wanaishi kwenye filamu ya James Bond. 
Hata hivyo, ukweli unabaki kuwa maadui wanaowindwa na mashushushu huwa wanajificha katika mazingira ambayo kwa hakika ni vigumu mno kuwagundua. 
Kama ilivyo kwa CIA, maafisa wa shirika la ujasusi la Uingereza MI6 pia wanatumia mjuda mwingi maofisini badala ya unachokiona kwenye filamu za James Bond au Jack Bauer wakifanya mambo ya miujiza kama kuruka kutoka kwenye ndege na kusalimika. Na kama walivyo wenzao wa CIA, kwa muda mwingi mashushushu wa MI6  ni watu wa kupekua mafaili ofisini kuliko watu wa action kwenye mapambano ya 'kuchemsha damu' kama inavyoonyeshwa kwenye filamu za kipelelezi. 
Katika zama tunazoishi sasa, mashushushu wengi ni watu wa kupekua data na kujaribu 'kuhujumu' kompyuta. Hawa ndio watu waliomudu kuhujumu mfumo wa kompyuta wa kijasusi na nyuklia wa Iran unaofahamika kama Stuxnet. Huenda kabla ya kufanikisha operesheni hiyo, mashushushu hao walikaa kwenye kompyuta zao miezi kadhaa kusaka mafanikio walioyapata.
Angalau filamu nyingine ya kishushushu kutoka Hollywood, Argo, inatoa picha ya karibu ya maisha halisi  ya shushushu- kukaa ofisini muda mrefu kurudia 'somo' lileile hadi 'siku ya siku ya balaa' inapowadia. Operesheni za 'hatari' hutmia muda mwingi wa maandalizi ofisini kuliko katika 'uwanja wa mapambano' au 'eneo la tukio,' tofauti na inavyoonyeshwa katika filamu nyingi za aina hiyo. 
Lakini japo mwisho wa filamu hiyo ya 'Argo' ni mtamu ambapo 'mateka' wote waliokolewa, hali haikuwa hivyo kiuhalisia kwani si mateka wote waliookolewa na mwishowe Marekani iliishia kuumbuka badala ya kuonekana shujaa anayeonyeshwa katika filamu ya Argo.

Sote tuliinjoi kusoma stori za Willy Gamba au kuburudika na stori za James Bond, Jack Bauer au Carrie na Nicholas Brody ambazo kwa kiasi flani zinarahisisha operesheni za kishushushu kwa minajili ya ileile ya 'stering hauwawi.' Hata hivyo, kwenye uhalisi wa operesheni za kishushushu ni vigumu mno kubashiri matokeo, na hata kama mambo yakionekana kwenda sawia kama ilivyapangwa, surprise ni jambo la kawaida. 

Na wakati mwingine ugumu wa operesheni unachangiwa na funzo muhimu kwa mashushushu kwamba 'ukiona kila kitu kinakwenda sawia basi ujue kuna hatari huko mbeleni.' Katika mafunzo ya taaluma hiyo, inakumbushwa mara kwa mara kwamba kamwe usiamini unachokiona bali jaribu kwenda ndani zaidi na kutafuta kisichoonekana.

Nimalizie makala hii na stori moja ya kusisimua (hainihusu): jamaa flani alikuwa ajifanikiwa kujipenyeza kwenye genge flani la wauza noti bandia katika mtaa mmoja maarufu jijini Dar. Kwa umahiri wake alifanikiwa kuaminika mno hadi akaweza kuwa karibu na bosi wa genge hilo. Kwa vile mashushushu ndio wanaowataarifu polisi kabla ya kuvamia makundi kama hayo, siku ya tukio kulijitokeza mgogoro wa kimawasiliano kati ya mashushushu na polisi, na matokeo yake polisi walivamia genge hilo wakati yule jamaa akiwa kazini-kaka shushushu na kama membe wa lile genge. Naomba uelewe kuwa katika matukio ya aina hiyo kuna uwezekano wa kupoteza maisha kwa vile polisi wanadhani wote waliomo katika genge husika ni wahalifu halisi bila kujua kuwa kuna mashushushu wapo kazini pia. 

Katika dakika ya kuamua kifo au kubaki hai, jamaa huyo alipatwa na mtihani wa aidha ajitambulishe kwa polisi na kuwasihi wawasiliane na viongozi wa operesheni hiyo (na kwa kufanya hivyo angekuwa anaweka roho yake rehani kwani genge lingebaini kuwa yeye ndo aliwachoma) au 'afe kizungu na tai shingoni' kwa kuendelea kujifanya mhalifu na kuomba dua zake pilisi wasimtoe roho...

No, hiyo sio hadithi ya kutunga. Ni tukio la kweli kabisa, na japo nisingependa kueleza hatma yake kwa undani (jamaa huyo alisalimika na yupo hai hadi leo licha ya baadhi ya wahalifu 'wenzie kuuawa au kujeruhiwa kwa risasi za polisi katika tukio hilo) nadhani tukio hilo laweza kukuonyesha jisni ushushushu wa vitendo unavyoambatana na hatari ambazo pengine kwenye vitabu vya Willy Gamba au filamu za James Bond, 24 au Homeland zinajengwa katika amzingira ya 'stering hauwawi.'

Endelea kutembelea blogu hii kwa ajili ya kupata habari na matukio mbalimbali yanayohusiana na taaluma ya intelijensia, hasa kwa kubonyeza hapo juu ya blogu kwenye maneno INTELIJENSIA




29 Jul 2014

An armed pro-Russia militant stands guard at the MH17 crash site.
Katika jitihada za kubaini chanzo-nani na kitu gani-cha kudunguliwa ndege ya Shirika la Ndege la Malaysia MH17,kundi la waandishi wa habari wa kijamii (citizen journalism) wakitumia mtandao wa intanet na hisia zao tu wamekuwa wakikusanya habari pengine zaidi ya mashushushu wa Kimarekani.

Jumanne iliyopita, maafisa usalama wa Marekani walikiri kwamba japo ni kweli kwamba Russia imekuwa ikiwasaidia waasi wanaoiunga mkono, huko Ukraine, kwa miezi kadhaa, hakuna uthibitisho wowote kuonyesha kuwa kifaru cha kurusha makombora ya kutoka ardhini kwenda angani (surface -to-air missile) aina ya Buk SA-11, ambacho Marekani inadai ndio kilitungua ndege hiyo, kilikuwa cha Russia. Hata hivyo, waasi hao wa Ukraine walijigamba awali kuwa wana makombora ya aina hiyo.

Msemaji wa serikali ya Marekani alikiri kwamba kuna uhaba mkubwa wa maelezo kuhusu silaha iliyotumika kudungua ndege hiyo, na kuthibitisha kuwa ni vigumu kuja na ushahidi mpya wa kuthibitisha uhusika wa Russia katika tukio hilo.

Lakini kundi la waandishi wa habari wa kijamii likiongozwa na Ellliot Higgins, anayefahamika zaidi kwa jina lake la mtandaoni kama "Brown Moses," ameonyesha ushahidi mwingi kuhusiana na tukio hilo. Kwa msaada wa wafuasi wake (followers) katika mtandao wa kijamii wa Twitter, ameweza kuonyesha sehemu kilipokuwa kifaru cha kurusha makombora (launcher) ya Buk wakati kinasafirishwa katika eneo la Snizhne, lililopo chini ya milki ya waasi wanaoungwa mkono na Russia, kulingana na video inayosambaa kwenye mtandao wa video wa Yout Tube

Siku iliyofuata, Aric Toler, mfuasi wa muda mrefu wa Higgins, alionyesha eneo sahihi la kifaru cha kurushia makombora ya Buk katika mji uliopo Mashariki kwa Ukraine wa Torez, akitumia taarifa alizozikusanya kwa vyanzo vya wazi (open source information) na video nyingine za YouTube zilizorekodiwa eneo hilo.

Toler na Higgins waliweza kuthibitisha kuwa picha hiyo ilipigwa saa 5.40 asubuhi, kwa kutumia nyenzo ya mtandaoni iitwayo Suncalc, ambayo inawezesha kukokotoa nafasi (position) ya jua kwa kuzingatia muda na sehemu husika. Hiyo iliwawezesha kuthibitisha kuwa kifaru hicho kilikuwa eneo ilipodunguliwa ndege ya MH17.

Uchambuzi mwingine wa kutumia watu wengi (crowdsourced analysis) ambao Higgins aliukusanya Jumanne iliyopita unatoa ushahidi mkubwa kuhusu video iliyotolewa hadharani na serikali ya Ukraine ikionyesha kifaru husika kikihamishwa kutoka eneo linaloshikiliwa na waasi kuelekea Russia. Katika video husika, mtambo wa kurushia makombora (launcher) hauonekani 

Serikali ya Russia ilikanusha usahihi wa video hiyo, ikidai kwamba ilirekodiwa katika mji wa Krasnoarmeisk, ambao upo chini ya himaya ya majeshi ya Ukraine. Hata hivyo, shukrani kwa uchambuzi wa habari kwa kutumia vyanzo vya wazi, ilikuja kufahamika kuwa mji huo wala sio uliotajwa bali mwingine ulio chini ya himaya  ya waasi wanaoungwa mkono na Ruassia wa Luhansk, kilomita 30 kutoka mpaka wa Russia na Ukraine.

"Russia imeongopa," aliandika Higgins katika tovuti yake ya Bellingcat, anayoitumia kuhamasisha kazi za waandishi wengine wa wa kijamii wanaoandika habari za uchunguzi na kufundiha kuhusu nyenzo mbalimbali kwa ajili ya kazi hiyo. 

Matokeo ya uchunguzi huo hayathibitishi kwa hakika uhusika wa Russia katika kuidungua ndege hiyo ya Malaysia, kama anavyokiri Higgins mwenyewe, lakini yanathibitisha kuwa waasi wanaoungwa mkono na Russia wanamiliki kifaru cha kurushia makombora ya Buk,.na kilikuwa karibu na eneo ilipodunguliwa ndege hiyo.

Kwa Higgins, kazi yao ni sawa na ushushushu lakini kwa kutumia njia rahisi,na unaweza kuwasaidia wachunguzi wa ajali hiyo. Baada ya yeye na mwenzie Toler kuonyesha eneo na muda picha ya kifaru hicho lipopigwa, waandishi wa habari walikwenda huko na kukutana na mashuhuda waliothibitisha maelezo ya Higgins na mwenzake.

Uchunguzi wa aina hii ni mfano mzuri wa anachotaka kufanya Higgins kupitia tovuti yake ya Bellingcat: kujenga jamii ya waandishi wa kijamii mtandaoni wanaojuhusisha na uchunguzi ambao waweza kuibua ukweli mbalimbali. Higgins amekuwa akifanya hivyo kwa miaka kadhaa, akibandika mtandaoni video mbalimbali kutoka Syria ili kbainisha zipi ni za kweli au la.

Yeye alikuwa mmoja wa waangalizi huru wa mwanzo kuthibitisha kuwa utawala wa Rais Bashir al-Assad wa Syria ulitumia silaha za sumu katika kitongoji cha Ghouta Agosti mwaka jana,a aliibua biashara ya kuingiza silaha nchini humo, akiwa nyumbani kwake, Leicester, Uingereza.  Sasa anataka kuwaunga mkono watu wengine wanaofanya kazi kama yake na kuwafundisha jinsi ya kupata ujuzi husika.

"Ni muhimu kufahamu kuwa uchunguzi huu ulifanywa na na watu wa aina mbalimbali, na hiyo inaonyesha umuhimu wa kufanya nyenzo na mbinu za kukusanya habari kwa vyanzo vya wazi kuwa za wazi kwa yeyeote yule."

Chanzo: Imetafsiriwa kutoka mtandao wa WAtoday.com.au



28 Jul 2014

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Rashid Othman 
Wakati idadi kubwa ya Watanzania inapinga vikali taasisi za intelijensia kuwafanyia ushushushu viongozi wa siasa na raia wa kawaida, Tanzania inashika nafasi ya pili duniani-nyuma ya Italia-kwa kudaka mawasiliano ya wananchi wake kwa siri.

Asilimia 71 ya Watanzania waliohojiwa katika utafiti uliofanywa na taasisi ya Pew Research Centre ya Marekani walipinga vitendo vya serikali kuingilia mawasiliano ya simu na email ya viongozi wa kisiasa. Asilimia 25 waliafiki vitendo hivyo.

Utafiti huo ulionyesha kuwa Watanzania wanaongoza barani Afrika katika upinzani wao dhidi ya uvamizi wa faragha yao unaofanywa na taasisi za intelijensia.

Hata hivyo vitendo vya kishushushu kufanya ufuatiliaji kwa kuingilia au kunasa mawasiliano vimeshamiri mno nchini Tanzania kiasi kwamba nchi hiyo inashika nafasi ya pili duniani nyuma ya Italia katika vitendo hivyo.

Mwezi uliopita, kampuni ya kimataifa ya simu za mkononi ya Vodafone, ilitoa taarifa inayoonyesha kuwa kampuni yake tanzu ya Vodacom Tanzania ilitoa mawasiliano 98,765 ya wateja wake kwa mashushushu.

Katika ripoti hiyo, Tanzania inatajwa kuwa ni nchi ya pili duniani - katika nchi 29 ambapo Vodafone inatoa huduma - nyuma ya Italia kwa kufuatilia, kuingilia au kunasa mawasiliano ya simu. Italia inashika nafasi ya kwanza kwa mawasiliano 605,601 yaliyoombwa na taasisi za usalama.

Vodafone ilibainisha uwepo wa nyenzo za siri zinazowawezesha mashushushu kusikiliza mawasiliano ya wateja wa kampuni hiyo.

Kampuni hiyo imevunja ukimya kuhusu vitendo vya serikali kuwafuatilia raia wake kwa ushushushu katika mitandao ya simu na intaneti.

Wakati hali ikiwa hivyo kwa Tanzania, utafiti huo umeonyesha kuwa asilimia 49 ya Wakenya wanaafiki mashushushu kunasa mawasiliano ya simu na email ilhali asilimia 44 hawaafiki.

Utafiti huo unaonyesha kuwa Kenya inaongoza miongoni mwa nchi za Afrika kuhusu ridhaa kwa serikali/mashushushu kuwapeleleza raia.

Chanzo: imetafsiriwa kutoka gazeti la The Citizen (Tanzania)



27 Jul 2014

Spy central: The MI5 headquarters near Vauxhall Cross on the River Thames
Jengo la makao makuu ya Idara ya ushushushu ya Uingereza,jijini London
Kuna ukweli mmoja usiofichika wala kupingika kwamba watu wengi sana wanapenda kazi ya ushushushu, yaani Uafisa Usalama wa Taifa.Hiyo sio kwa Tanzania pekee bali sehemu nyingi duniani. Ukiingia mtandaoni utakutana na watu wengi wanaozungumzia taaluma ya intelijensia au/na wahusika katika hali ya kutamani kuifahamu taaluma hiyo nyeti  au kuwa mhusika.

Leo nitaanza mlolongo (series) wa makala kuhusu taaluma hiyo adimu. Hata hivyo ni vema nikatahadharisha mapema kwamba nitakachoandika ni kile tu kinachoruhusiwa kuandikwa hadharani. Kimsingi,taaluma ya ushushushu inatawaliwa na usiri,na mengi ya yanayohusiana na taaluma hayo yanabaki kuwa siri. Hata hivyo,kuna maelezo ambayo yapo wazi japo inahitaji uelewa wa aina flani kuchora mstari kati ya kipi ni siri na kipi ni ruksa kuwa hadharani.

Kwa tafsiri rahisi, ushushushu ni taaluma inayohusu ukusanyaji wa taarifa za kiusalama kwa njia za siri (clandestine methods). Japo kwa kiswahili ushushushu ni intelijensia, kiundani kuna tofauti kati ya ushushushu unaofanyika ndani ya nchi na unaofanyika nje ya nchi.Kwa hapa Uingereza, Idara ya ushushushu inayoshughulika na masuala ya ndani inajulikana kama MI5 na inayohusiska na ushushus nje ya nchi ni MI6.Kwa huko nyumbani, tofauti hizo zipo ndani ya muundo wa taasisi husika, kwa maana kwamba kuna taasisi moja tu lakini ndani yake kuna mgawanyo wa kimajukumu ya ndani na ya nje.

Kadhalika, japo mashushushu wamekuwa wakifahamika pia kama spies, ukweli ni kwamba spy ni shushushu anayefanya kazi nje ya nchi yake,kitu kinachojulikana kiusalama kama ujasusi au espionage kwa Kiingireza.

Japo mataifa mbalimbali yana miundo tofauti ya Idara zao za Usalama wa Taifa,lengo na kazi kuu ni ukusanyaji wa taarifa hizo.Kwa minajili ya makala hizi, nitazungumzia zaidi mazingira ya huko nyumbani Tanzania. Kwa mujibu wa Sheria ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1996, Idara yetu ya Usalama wa Taifa ni idara ya serikali iliyo chini  ya Ofisi ya Rais,ambayo ina jukumu la kukusanya na kuchambua taarifa za usalama na kuziwasilisha 'mahala kunakohusika' katika namna ambayo Mkurugenzi Mkuu wa Idara hiyo ataona inafaa.

Kimsingi, mkuu'halisi' wa Idara hiyo ni Rais mwenyewe,ambaye kwa lugha ya kiusalama anafahamika kama 'sponsor.' Wakuu wa Idara za usalama popote pale duniani hufahamika kama spymaster.

Maeneo makuu ya kazi za Idara ya Usalama wa Taifa ni kukusanya na kuchambua habari za kiusalama zinazohusiana na ujasusi (espionage),uzandiki (subversion),uhujumu (sabotage) na ugaidi (terrorism). Lakini jukumu la Idara hiyo si kukusanya taarifa hizo na kuzichambua tu bali pia kuzuwia matukio hayo yanayofahamika kama matishio ya usalama wa taifa.

Ni kwa vile utendaji wa kazi wa Idara yoyote ile ya Usalama wa Taifa unaegemea katika usiri mkubwa ndio maana kwa 'mtaani' kuna hisia tofauti kuhusu umuhimu wa taasisi hiyo. Ukweli ni kwamba laiti umma ungefahamu nini kinafanywa (au kinapaswa kufanywa) na Idara hiyo basi kwa hakika ingethaminiwa zaidi ya kuogopwa tu. Ni muhimu hapa nisisitize kuwa ninazungumzia 'hali mwafaka' yaani kwa Kiingereza ideal situation. Hivi karibuni kumekuwa na malalamiko mengi miongoni mwa wananchi wakiishutumu Idara yetu ya Usalama wa Taifa kuwa imeleemea mno kwenye siasa hasa kuibeba CCM,imezembea mno kiasi cha kuruhusu ufisadi kushamiri, na imekuwa ikilaumiwa pia kutokana na matukio mbalimbali yanayotishia usalama wa Taifa kama vile ugaidi.

Wanaotoa lawama hizo wapo sahihi kwa kiasi flani,kwani  kushamiri kwa maovu katika jamii sambamba na mwendelezo wa matukio yanayotishia usalama wa taifa ni viashiria kuwa Idara ya Usalama ya nchi husika ina mapungufu kiutendaji.

Hata hivyo,ni muhimu kutambua kanuni moja muhimu ya ufanisi au kushindwa kimajukumu kwa Idara ya Usalama wa Taifa popote pale.Ni kwamba wakati Idara husika inapaswa kuwa macho katika kila sekunde kuzuwia matendo ya kidhalimu, wanaopanga kufanya matendo hayo wanahitaji mara moja tu kufanikisha azma yao.Mfano halisi ni kwenye matukio ya ugaidi. Wakati gaidi anahitaji fursa moja tu kufanikisha tukio la kigaidi, Idara ya Usalama inahitaji kila fursa- kila sekunde,dakika,saa,siku,wiki,mwezi,mwaka-kuhakikisha gaidi hafanikiwi.

Kadhalika, wakati inaweza kuwa rahisi kuilaumu Idara ya Usalama wa Taifa inaposhindwa kuzuwia tukio flani, kwa mfano shambulio la kigaidi nchini Kenya, kiuhalisi suala zima la ukusanyaji wa taarifa za kiusalama ni gumu mno. Hebu pata picha: unaletewa tetesi kuwa kuna mtu anataka kulipua bomu kanisa au msikiti. Mara nyingi tetesi hizo huwa hazibainishi jinsia ya mtu huyo,wajihi wake,ni mwenyeji au mgeni na vitu vingine muhimu vya kuweza kumtambua japo kwa ugumu. 

Kutokana na ugumu wa zoezi la kukusanya taarifa za kiusalama,ndio maana wahusika-mashushushu/maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa-wanapaswa kuwa watu wenye akili isiyo ya kawaida, au angalau wenye uwezo mkubwa wa kutumia akili.Neno lenyewe intelijensia linahusiana na matumizi ya akili.Lakini si akili tu, bali pia maafisa usalama wa taifa hupaswa kujifunza na kuendeleza hisia ya sita (6th sense). Mwanadamu wa kawaida ana hisia 5: HARUFU  kwa kutumia pua; LADHA kwa kutumiamdomo/ulimi, KUGUSWA (touch) kwa kutumia ngozi, KUONA kwa kutumia macho, KUSIKIA kwa kutumia masikio. Lakini kwa mashushushu wanapaswa kuwa na hisia ya ziada ya kutambua kitu zaidi ya kutumia hisia hizo 5 kuu. Si kazi rahisi hata kidogo.

Basi kwa leo niishie hapa.Nitaendelea na mfululizo wa makala hizi angalau kila wiki. Usikose kutembea blogu hii kupata habari na makala zaidi kuhusu taaluma hii nyeti ya ushushushu kwa kubonyeza hapo juu ya blogu kwenye seksheni ya INTELIJENSIA 



20 Jul 2014

Oscars zero dark thirty jessica chastain
It's not often we get a look inside the secret world of spies.
While intelligence officers continue to operate in the shadows, a fantastic article by Josef Hufelschulte of Focus Magazine gives a rare look inside their secret training regimen.
We picked out the five most interesting skills new recruits learn at Germany's version of the CIA, the Bundesnachrichtendienst (BND).

Spies need to learn their most important skill: how to recruit sources to give up secrets.

The bread and butter of a spy is acquiring secret information from sources. In the Focus report, one intelligence officer was given the location of a visiting lord and after 90 minutes, the young woman had learned the lord's marital status, occupation, career, hobbies, and daughter's college exam grades. By the end of the rendezvous, the officer had accomplished her mission while the lord had fallen in love.
"You also have to figure out what motivates people, and what their vulnerabilities are," former CIA officer Lindsay Moran revealed in an interview with Pursuit Magazine. "Because this is the information you will use to manipulate them to get what you want — which is secret information."

They need to know how to lie — and to tell when someone else is lying.

The world of secrecy includes a lot of lying and officers better be good at it. Not only do they have to be good at lying, but they must be able to spot when someone else is. This starts from day one, as friends and family are kept in the dark.
Officers even create elaborate stories to use to practice lying when their fellow officers ask them personal questions. In examples of how to spot a liar, former U.S. President Bill Clinton is presented as a textbook example, and students pored over the tells the former president made during the Lewinsky scandal. 

Spies are taught advanced driving skills, like how to lose someone who may be following them.

All aspects of driving are covered. Officers are taught how to avoid being followed, how to tell if someone's on their tail, and how to shake them.
"They teach you tricks, such as making left-hand turns so you can see if there are cars behind you," former CIA officer Lindsay Moran revealed of her CIA vehicle training.
BND officers are taught not only how to avoid suspicion but also how to handle high-speed and violent chases. Three officers credit their survival of a gunshot-filled chase through the streets of Saudi Arabia to the skills learned in driving classes.  

Spies must be able to conduct espionage operations in crisis regions.

For six weeks, students are relocated to a hidden compound to complete operations training. The training includes explosions and realistic scenarios that mirror conditions in countries with high levels of terrorist activity.
Everything from how to handle an attack on an embassy, to first aid and helicopter evacuations is covered. Weapons proficiency is also taught but from a defensive mindset: If you have to engage with a weapon, something has gone terribly wrong.

Classwork is an all-day event and covers everything from languages to psychology.

20% of classroom curriculum includes law classes with practical applications like how to respond to a kidnapping in a foreign country — a situation particularly dicey for a spy. Their classwork stretches deep into the evening and covers subjects as diverse as international politics, Islam, geography, psychology, observation, photographic technology and foreign languages. English proficiency is required and other language skills are developed. 
According to the class subject to the Focus report, of 800 men and women who applied to the BND, only 40 made it to graduation

Seven internet service providers have filed a legal complaint against the UK's intelligence agency GCHQ.

ISPs from the US, UK, Netherlands and South Korea have joined forces with campaigners Privacy International to take the agency to task over alleged attacks on network infrastructure. 

It is the first time that GCHQ has faced such action.

The move follows allegations about government snooping made by US whistleblower Edward Snowden. 'Infected with malware' The ISPs claim that alleged network attacks, outlined in a series of articles in Der Spiegel and the Intercept, were illegal and "undermine the goodwill the organisations rely on".

 The allegations that the legal actions are based on include:

  •  claims that employees of Belgian telecommunications company Belgacom were targeted by GCHQ and infected with malware to gain access to network infrastructure
  •  GCHQ and the US National Security Agency, where Mr Snowden worked, had a range of network exploitation and intrusion capabilities, including a "man-on-the-side" technique that covertly injects data into existing data streams to create connections that will enable the targeted infection of users
  •  the intelligence agencies used an automated system, codenamed Turbine, that allowed them to scale up network implants 
  • German internet exchange points were targeted, allowing agencies to spy on all internet traffic coming through those nodes 
While the ISPs taking the action were not directly named in the leaked Snowden documents, Privacy International claims that "the type of surveillance being carried out allows them to challenge the practices... because they and their users are at threat of being targeted". 


Privacy International has previously filed two other cases - the first against alleged mass surveillance programmes Tempora, Prism and Upstream, and the second against the deployment by GCHQ of computer intrusion capabilities and spyware.

'Strict framework' Eric King, deputy director of Privacy International, said "These widespread attacks on providers and collectives undermine the trust we all place on the internet and greatly endangers the world's most powerful tool for democracy and free expression." 

The ISPs involved in the action are UK-based GreenNet, Riseup (US), Greenhost (Netherlands), Mango (Zimbabwe), Jinbonet (South Korea), May First/People Link (US)and the Chaos Computer Club (Germany). 

Cedric Knight, of ISP GreenNet, added: "Snowden's revelations have exposed GCHQ's view that independent operators like GreenNet are legitimate targets for internet surveillance, so we could be unknowingly used to collect data on our users. We say this is unlawful and utterly unacceptable in a democracy." 

GCHQ maintains that all its work is conducted "in accordance with a strict legal and policy framework which ensures that our activities are authorised, necessary and proportionate".

SOURCE: BBC



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.