Showing posts with label PROFESA JAY. Show all posts
Showing posts with label PROFESA JAY. Show all posts

9 Jun 2013


Huiwezi kuuzungumzia muziki wa Bongoflava pasi kumtaja Mike Mhagama. Huyu alikuwa mtangazaji wa kituo cha kwanza binafsi cha redio nchini Tanzania, Radio One. Mike,ambaye kwa sasa anaishi nchini Marekani, alitoa mchango mkubwa sana kuutambulisha muziki wa Bongoflava- na kama sijakosea ni miongoni mwa waasisi wa neno 'Bongoflava' (sina hakika sana).

Ninakumbuka enzi hizo, kukosa kipindi cha DJ Show (kama sijakosea) ilikuwa kama dhambi flani kwa mtu anayependa muziki. Ama kwa hakika zama hizo kulikuwa na raha ya kuskiza redio, burudani iliyokuwa ikitolewa licha ya kuwa na ladha nzuri lakini pia iliendeshwa ki-professional.

Kama ambavyo wengi tumeguswa na kinachoonekana kama 'bifu' (uhasama) wa wasanii wawili nguli wa Bongofleva, Hamisi Mwinjuma a.k.a @MwanaFA na Judith Wambura a.k.a @LadyJaydee, Mike nae ameonyesha kuguswa na suala hilo japo yupo mbali na nyumbani.

Katika 'Timeline' yake huko Twitter, mtangazaji (@MikeMhagama) huyo wa zamani ameandika (ninamnukuu)

Screenshot_2013-06-09-21-09-01-1.png

Mike alikuwa anajibu rai yangu kwa wasanii Fareed Kubanda a.k.a @FidQ Ambwene Yesaya a.k.a AY (@AyTanzania) na Joseph Haule a.k.a @Profesa_Jay wafanye jithada za upatanishi kati ya Mwana FA na Jide. Kadhalika nilipendekza kuwa kikao hicho kinaweza pia kuhudhuriwa na watangazaji walio-present Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2013 Jokate (@JokateM) na Millard Ayo (@MillardAyo)

Hadi wakati ninaandika makala hii raia hiyo ilikuwa haijajibiwa.Hata hivyo,ninapenda kumpongeza Mike Mhagama kwa angalau kuonyesha kuguswa na 'bifu' hiyo na kutamani kuisuluhisha. Si vigumu kuelea kwanini Mike ameguswa. Kama miongoni mwa waasisi na waliopromoti Bongoflava tangu inazaliwa hadi ilipofikia, lazima atakuwa anahuzunishwa na ugomvi huu.

Kwa upande mwingine, mhariri na mmiliki wa tovuti ya Bongo Celebrity, ambayo maarufu zaidi ya burudani kuliko zote za Watanzania,  Jeff Msangi, naye ameandika makala nzuri inayohusu suala hilo la bifu ya FA na JIDE. 

Makala hiyo ni hii hapa chini 

LADY JAYDEE Vs MwanaFA: BEEF,BIASHARA, PERSONAL AU?

Yapo mambo ambayo mara nyingi sisi hapa BC huwa tunayaacha yapite. Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na Beef baina ya watu fulani fulani hususani wale ambao BC inawachukulia kama Celebrities na hivyo kuleta maana halisi ya BongoCelebrity.
Nakumbuka wakati BC inaanza (miaka mingi sasa) nia ilikuwa ni kuyatizama maisha ya watu wetu maarufu (celebrities) katika jicho chanya zaidi. Tulielewa kwamba watu wanapenda zaidi kusikia umbea. Tulifahamu kwamba habari mbaya huenea kwa kasi ya aina yake kulinganisha na habari njema. Pamoja na kuelewa hivyo,tumejikita kwenye nia. To stay positive and ask everyone to stay positive and pay attention to more positives than negatives.
Sasa kama wewe ni mtumiaji au mtembeleaji mzuri wa mitandao ya kijamii kama vile Twitter,Facebook, Instagram etc, bila shaka leo umekumbana na maendeleo ya mpambano wa maneno kati ya Lady Jaydee na MwanaFA.Kuna kashfa, kuna kuitana majina. Kuna ushabiki ambao naamini mwisho wake sio mzuri….
Hawa wote ni wasanii wakongwe. Ni mifano ya kutizamwa na wengi hususani wasanii wachanga ambao wanataka kufikia mafanikio ambayo hawa tayari wameyafikia. Kinachoendelea, ingawa ni kweli kinaleta msisimko fulani (hususani kwa watu wanaofurahia wakati wengine wakiumizana), hakina mantiki yenye mlengo chanya. Ni ushindani wa siku moja (June 14-siku ambayo wote wana show). Tarehe 15 June kutakuwa na nini?
Kuna njia kadhaa za kuangalia kitu kinachoendelea. Ni beef? Ni biashara? Au ni mambo binafsi? Kama ni beef la ukweli,basi kuna haja ya mtu kuingilia kati na kuwapatanisha. Kama wasanii naamini issues zao zinafanana. Matatizo ya kudhulumiwa au kutolipwa ipasavyo, ni matatizo yao wote. Sio tatizo la JayDee au MwanaFA peke yake. Hakuna haja ya beef. Kuna haja ya kuungana na kupigania kitu kimoja; Haki.
Kama malumbano haya ni kibiashara zaidi, basi tutaona tarehe 14 June kama njia inayotumiwa ni sahihi au la. Kuna tofauti kubwa kati ya beef za kupromote biashara katika nchi za wenzetu kama Marekani (50Cent na Kanye West) na Tanzania yetu.Mazingira yanatofautiana…
Kama kinachoendelea ni masuala binafsi…then we don’t have a business to be into other people’s businesses. Wanaweza kuyamaliza…



CHANZO: BONGOCELEBRITY.COM Ni matumaini yangu-na pengine yenu wasomaji- kuwa hatimaye wasanii wetu, Mwana FA na Jide, watakaa pamoja na kufikia mwafaka wa kumaliza tofauti zao.Labda baadhi ya video hizi walioshirikiana zinaweza kuwakumbusha kuwa wamtoka mbali
Katika wimbo huu 'Nangoja Ageuke' wa FA a AY kuna cameo ya Lady Jaydee



21 May 2013

Click image for larger version. 

Name: Prof Jay Ajiunga Na Chadema.jpg 
Views: 0 
Size: 47.5 KB 
ID: 94612
 Profesa Jay akipokea kadi ya unachama wa Chadema kutoka kwa Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) Mh. Joseph Mbilinyi (a.k.a Sugu)
Click image for larger version. 

Name: Prof Jay Na Sugu Na Mnyika.jpg 
Views: 0 
Size: 40.8 KB 
ID: 94613

Profesa Jay akiwa na Mh 'Sugu'  na Mbunge wa Ubungo (Chadema) Mh John Mnyika.

Ni Mtanzania gani kijana (na hata wazee wa kati) asiyemjua Profesa Jay, msanii mahiri wa Bongoflava ambaye jina lake halisi ni Joseph Haule (au Jay wa Mitulinga). Msanii huyo, pengine katika hali ambayo haikutarajiwa kabisa, leo amejiunga na chama cha upinzani cha Chadema.

Uamuzi wa Profesa Jay kujiunga na Chadema unaweza kuwa na manufaa makubwa sana kwa chama hicho hasa kwa vile mabadiliko ya kisiasa huko nyumbani yanategemea zaidi hamasa ya vijana.


Nitaandika zaidi baadaye kuhusu tukio hili muhimu kwa Chadema, muziki wa bongoflava na vijana kwa ujumla, lakini kwa sasa burudika na kibao hiki cha "Nikusaidiaje" cha Profesa Jay akimshirikisha Ferouz

19 Jan 2008

Siku chache zilizopita nilizungumzia kuhusu "afya" ya muziki wa Bongofleva.Dhamira ya makala hiyo ilikuwa ni kuwaamsha wahusika na kuwakumbusha kwamba japo ni vizuri kula matunda ya jasho lao,wanapaswa kuwa makini wasije kujikuta wanakata kabisa na mimea inayotoa matunda hayo.

Leo napenda kuzungumzia nafasi ya muziki huo katika kuleta mabadiliko kwenye jamii.Nilisoma mahala flani kuhusu lawama dhidi ya rapa maarufu huko Marekani,Jay-Z,baada ya kutoa albam yake mpya ya American Gangster.Katika makala hiyo,mwandishi alimlaumu Jay-Z kwamba sehemu kubwa ya albam hiyo ilikuwa imetawaliwa na "meseji za kawaida za marapa"...kujisifia kwingi,blings,warembo,nk.Mwandishi huyo alidai kwamba alitegemea,katika nafasi yake kama mmoja ya majina makubwa ya Weusi nchini Marekani, Jay-Z angeelekeza jitihada katika "kuzisaidia 'hoods katika mapambano ya ukombozi wa kweli wa mtu Mweusi".Anyway,sijapata fursa ya kusikia nyimbo zote zilizo katika albam hiyo,kwahiyo siwezi ku-comment lolote katika hoja ya mwandishi huyo.Hata hivyo,alichokisema kina mantiki kuhusiana na muziki wetu huko nyumbani.

Wasanii wa bongofleva na wale wa aina nyingie za muziki (kama taarabu na muziki wa dansi) ni miongoni mwa waathirika wakubwa wa ufisadi.Wengi wao hugeuzwa,ashakum si matusi,mithili ya "kondom za kisiasa".Hapo namaanisha kwamba baadhi ya wanasiasa huwatumia wasanii hawa wakati wa kampeni zao za kusaka uheshimiwa lakini wakishapata madaraka huwapuuza kabisa wasanii hao waliowapigia debe.Ni mithili ya kondom,ambayo kwa kawaida huonekana yenye umuhimu mkubwa (kwa wale wanaojali) kabla ya tendo la ndoa,lakini hugeuka takataka baada ya kutumika.

Wapo watakaodai kwamba wanasiasa wana haki ya "kukatisha" mahusiano na wasanii hao kwa vile huwaalika kwenye kampeni baada ya kuwalipa.Hoja hiyo inaweza kupingwa na ukweli kwamba fedha au malipo sio kila kitu (money isn't everything).Chukulia mfano wa mwalimu.Anapokufundisha anafanya hivyo kwa vile ni mwajiriwa wa taasisi ya elimu,na analipwa kila mwezi kukupatia elimu,achilia mbali uwezekano kwamba unalipia (ada) elimu hiyo.Lakini (pamoja na kupuuzwa kwao) walimu wanaendelea kushikilia nafasi muhimu katika jamii kwani ndio wafunguzi muhimu wa jitihada za binadamu katika kukabiliana na mazingira yake.Mfano mwingine ni wazazi.Wametuzaa,kutulea na kutusapoti katika makuzi yetu.Wapo wanaoweza kudai kuwa huo ni wajibu wao.Lakini tunafahamu kwamba wangetaka,wangeweza kabisa kzuia ujio wetu duniani (kwa baba na mama kuamua kutokuwa na watoto zaidi,kabla sie hatujazaliwa,au hata kutoa mimba zilizosababisha tuzaliwe).Tunaendelea kuwajali wazazi licha ya ukweli kwamba uzazi ulikuwa ni jukumu lao.Mifano hiyo miwili inaweza kulinganishwa na hoja yangu kwamba malipo yoyote yanayofanywa baada ya kutendewa kitu kikubwa hayawezi kulinganishwa na thamani ya matendo hayo.For that matter,fedha yoyote inayotolewa kama malipo kwa wapiga debe kwenye kampeni ya mwanasiasa haiwezi kulingana na mchango wa wapiga debe hao.

Nirejee kwenye kichwa cha habari cha post hii.Wengi wetu tunamfahamu Masudi Kipanya,mchora katuni maarufu huko nyumbani.Katuni zake nyingi huzungumzia matatizo yanayoikabili jamii ya Watanzania,na kwa hakika amekuwa mwiba mkali kwa wanasiasa wababaishaji na mafisadi.Anafanya kazi halisi ya sanaa kwani sanaa ni kioo cha jamii.Kwa bahati mbaya,wasanii wa muziki (hususan bongofleva) wamekuwa "wapole" sana katika mapambano dhidi ya maovu katika jamii yetu.Unakumbuka tungo kama Wauguzi ya Wagosi wa Kaya,au Ndio Mzee ya Profesa Jay?Hizi zilikuwa zina ujumbe mzito ambao kwa hakika ulikuwa unawakilisha kilio cha jamii.Tatizo kubwa la muziki wetu ni kwamba umetawaliwa sana na mada ya mapenzi.Hakuna ubaya kuzungumzia mapenzi,lakini yayumkinika kusema kwamba ili mapenzi yaende vema,shurti kuwe na kitu tumboni,barabara ya kufika kwa mpenzio iwe inafikika kirahisi,ukifika kwao usiku kuwe na mwanga (kwa maana ya upatikanaji wa umeme)....yaani hoja hapa ni kwamba mapenzi yanastawi vema pale huduma muhimu kwa maisha ya binadamu zinapopatikana kwa ufanisi.Ufisadi ni moja ya sababu kuu zinazokwamisha upatikanaji wa huduma hizo,na kwa sababu hiyo,wasanii wenye mahaba na dhima ya mapenzi kwenye tungo zao wana kila sababu ya kupambana nao (ufisadi) kwani vinginevyo wanachokiongelea kitaendelea kuwa ndoto za kujiliwaza tu.

Wapo wasanii ambao wana sababu za ziada za kupambana na mafisadi.Hawa ni pamoja na wale walioporwa wapenzi wao ambao walirubuniwa na nguvu ya fedha za mafisadi.Na kila msanii ana sababu nyingine ya kukabiliana na mafisadi (wadosi) wanaowalipa ujira mdogo ilhali wao (wadosi) wanatengeneza mamilioni ya bure.Ununuzi wa kazi za wasanii zinategemea hali ya kipato cha wateja wao (ikizingatiwa kwamba wengi wenye uwezo wa kiuchumi wako bize sana na masuala yao mengine kuliko kusikiliza tungo za nyumbani,na mafisadi wako bize zaidi na kuimarisha mikakati yao ya kulikamua taifa,kuangalia maendeleo ya miradi yao na kuboresha nyumba zao ndogo),kwa hiyo wasanii wana wajibu wa kushiriki mapambano ya kuboresha maisha ya wateja wao wakuu (wengi wao wakiwa waathirika wakuu wa ufisadi).

Tunahitaji akina (Masudi) Kipanya wengine kwenye bongofleva na miziki mingine kushirikiana na wale wote walio katika mapambano dhidi ya ufisadi huko nyumbani.Kelele za aina yoyote dhidi ya wahalifu (mafisadi) hao zitasaidia angalau kuwakumbusha kwamba tamaa na furaha zao ni kilio kwetu.

Hebu msikie Skinnyman anavyolalamika katika clip hii ya Council Estate of Minds kuhusu hali halisi ya maisha kwenye maghorofa (yaliyosahaulika,na makazi maarufu ya watu wa kipato duni) ya manispaa (Council estates)


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.