Showing posts with label JAY-Z. Show all posts
Showing posts with label JAY-Z. Show all posts

7 Jun 2009

Although his Blueprint 3 album is not due until later this year, he's still a power player, according to The Source magazine's annual "Power 30" list.

The long-running hip-hop magazine will land atop their annual list this year, when the magazine drops its new issue later this month.
He's the frontrunner, said the mag, because he's an industry leader and a top businessman, boasting a portfolio that includes ventures with Live Nation, Rocawear, and a small stake ownership -- along with a group of investors -- in the NBA franchise, the New Jersey Nets.

Other names on the list include Lil Wayne, Diddy, 50 Cent, Snoop Dogg, Kimora Lee Simmons, and T-Pain, among others.

Barack Obama (because of his influence on the new hip-hop generation) and the Black Eyed Peas' Will.i.an are also named as "Power 30" honorees.

"The Black Eyed Peas is like one of the biggest groups on the planet. We go out to Brazil, you know, a million, two hundred thousand people is at our concert," Will explained to the mag.

The "Power 30" issue features a coverstory from T.I. and his Grand Hustle crew, and what the rapper's hustle will be post-incarceration.


50 CENT




P DIDDY




KIMORA LEE-SIMMONS




LIL WAYNE




SNOOP DOGG



T-PAIN



WILL.I.AM


27 Feb 2008

Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inazungumzia UNAFIKI: Ule wa Profesa Mwandosya kuitaka Dawasco isiwataje hadharani mawaziri wanaodaiwa maji na Mamlaka hiyo;ule wa Askofu Thomas Laizer wa KKKT Dayosisi ya Arusha kutumia neno la Bwana kuwapiga vijembe wanamwandama Lowassa,na ule wa "mabilioni ya EPA yanayorejeshwa kwa kasi."Makala hiyo imeanza kwa stori za hapa na pale,mambo ya muziki wa kufokafoka na albamu ya Jay-Z ya American Gangster ilivyosahau matatizo ya Black Americans.Stori hizo ni zinaunganishwa katika namna ile ile ya conversational style,napenda sana makala iwe mithili ya kupiga stori na msomaji,iwe kijiweni,kwenye pub,au hata barazani.Pamoja na habari na makala zilizokwenda shule,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA

19 Feb 2008

HABARI ZILIZOJIRI HIVI PUNDE NI KWAMBA FIDEL CASTRO AMEJIUZULU URAIS WA CUBA PAMOJA NA U-AMIRI JESHI MKUU.BREAKING NEWS HIYO KUTOKA SKY NEWS NI KWA MUJIBU WA AFP
PICHANI JUU NI CASTRO (KULIA) AKIWA NA RAPA JAY-Z

19 Jan 2008

Siku chache zilizopita nilizungumzia kuhusu "afya" ya muziki wa Bongofleva.Dhamira ya makala hiyo ilikuwa ni kuwaamsha wahusika na kuwakumbusha kwamba japo ni vizuri kula matunda ya jasho lao,wanapaswa kuwa makini wasije kujikuta wanakata kabisa na mimea inayotoa matunda hayo.

Leo napenda kuzungumzia nafasi ya muziki huo katika kuleta mabadiliko kwenye jamii.Nilisoma mahala flani kuhusu lawama dhidi ya rapa maarufu huko Marekani,Jay-Z,baada ya kutoa albam yake mpya ya American Gangster.Katika makala hiyo,mwandishi alimlaumu Jay-Z kwamba sehemu kubwa ya albam hiyo ilikuwa imetawaliwa na "meseji za kawaida za marapa"...kujisifia kwingi,blings,warembo,nk.Mwandishi huyo alidai kwamba alitegemea,katika nafasi yake kama mmoja ya majina makubwa ya Weusi nchini Marekani, Jay-Z angeelekeza jitihada katika "kuzisaidia 'hoods katika mapambano ya ukombozi wa kweli wa mtu Mweusi".Anyway,sijapata fursa ya kusikia nyimbo zote zilizo katika albam hiyo,kwahiyo siwezi ku-comment lolote katika hoja ya mwandishi huyo.Hata hivyo,alichokisema kina mantiki kuhusiana na muziki wetu huko nyumbani.

Wasanii wa bongofleva na wale wa aina nyingie za muziki (kama taarabu na muziki wa dansi) ni miongoni mwa waathirika wakubwa wa ufisadi.Wengi wao hugeuzwa,ashakum si matusi,mithili ya "kondom za kisiasa".Hapo namaanisha kwamba baadhi ya wanasiasa huwatumia wasanii hawa wakati wa kampeni zao za kusaka uheshimiwa lakini wakishapata madaraka huwapuuza kabisa wasanii hao waliowapigia debe.Ni mithili ya kondom,ambayo kwa kawaida huonekana yenye umuhimu mkubwa (kwa wale wanaojali) kabla ya tendo la ndoa,lakini hugeuka takataka baada ya kutumika.

Wapo watakaodai kwamba wanasiasa wana haki ya "kukatisha" mahusiano na wasanii hao kwa vile huwaalika kwenye kampeni baada ya kuwalipa.Hoja hiyo inaweza kupingwa na ukweli kwamba fedha au malipo sio kila kitu (money isn't everything).Chukulia mfano wa mwalimu.Anapokufundisha anafanya hivyo kwa vile ni mwajiriwa wa taasisi ya elimu,na analipwa kila mwezi kukupatia elimu,achilia mbali uwezekano kwamba unalipia (ada) elimu hiyo.Lakini (pamoja na kupuuzwa kwao) walimu wanaendelea kushikilia nafasi muhimu katika jamii kwani ndio wafunguzi muhimu wa jitihada za binadamu katika kukabiliana na mazingira yake.Mfano mwingine ni wazazi.Wametuzaa,kutulea na kutusapoti katika makuzi yetu.Wapo wanaoweza kudai kuwa huo ni wajibu wao.Lakini tunafahamu kwamba wangetaka,wangeweza kabisa kzuia ujio wetu duniani (kwa baba na mama kuamua kutokuwa na watoto zaidi,kabla sie hatujazaliwa,au hata kutoa mimba zilizosababisha tuzaliwe).Tunaendelea kuwajali wazazi licha ya ukweli kwamba uzazi ulikuwa ni jukumu lao.Mifano hiyo miwili inaweza kulinganishwa na hoja yangu kwamba malipo yoyote yanayofanywa baada ya kutendewa kitu kikubwa hayawezi kulinganishwa na thamani ya matendo hayo.For that matter,fedha yoyote inayotolewa kama malipo kwa wapiga debe kwenye kampeni ya mwanasiasa haiwezi kulingana na mchango wa wapiga debe hao.

Nirejee kwenye kichwa cha habari cha post hii.Wengi wetu tunamfahamu Masudi Kipanya,mchora katuni maarufu huko nyumbani.Katuni zake nyingi huzungumzia matatizo yanayoikabili jamii ya Watanzania,na kwa hakika amekuwa mwiba mkali kwa wanasiasa wababaishaji na mafisadi.Anafanya kazi halisi ya sanaa kwani sanaa ni kioo cha jamii.Kwa bahati mbaya,wasanii wa muziki (hususan bongofleva) wamekuwa "wapole" sana katika mapambano dhidi ya maovu katika jamii yetu.Unakumbuka tungo kama Wauguzi ya Wagosi wa Kaya,au Ndio Mzee ya Profesa Jay?Hizi zilikuwa zina ujumbe mzito ambao kwa hakika ulikuwa unawakilisha kilio cha jamii.Tatizo kubwa la muziki wetu ni kwamba umetawaliwa sana na mada ya mapenzi.Hakuna ubaya kuzungumzia mapenzi,lakini yayumkinika kusema kwamba ili mapenzi yaende vema,shurti kuwe na kitu tumboni,barabara ya kufika kwa mpenzio iwe inafikika kirahisi,ukifika kwao usiku kuwe na mwanga (kwa maana ya upatikanaji wa umeme)....yaani hoja hapa ni kwamba mapenzi yanastawi vema pale huduma muhimu kwa maisha ya binadamu zinapopatikana kwa ufanisi.Ufisadi ni moja ya sababu kuu zinazokwamisha upatikanaji wa huduma hizo,na kwa sababu hiyo,wasanii wenye mahaba na dhima ya mapenzi kwenye tungo zao wana kila sababu ya kupambana nao (ufisadi) kwani vinginevyo wanachokiongelea kitaendelea kuwa ndoto za kujiliwaza tu.

Wapo wasanii ambao wana sababu za ziada za kupambana na mafisadi.Hawa ni pamoja na wale walioporwa wapenzi wao ambao walirubuniwa na nguvu ya fedha za mafisadi.Na kila msanii ana sababu nyingine ya kukabiliana na mafisadi (wadosi) wanaowalipa ujira mdogo ilhali wao (wadosi) wanatengeneza mamilioni ya bure.Ununuzi wa kazi za wasanii zinategemea hali ya kipato cha wateja wao (ikizingatiwa kwamba wengi wenye uwezo wa kiuchumi wako bize sana na masuala yao mengine kuliko kusikiliza tungo za nyumbani,na mafisadi wako bize zaidi na kuimarisha mikakati yao ya kulikamua taifa,kuangalia maendeleo ya miradi yao na kuboresha nyumba zao ndogo),kwa hiyo wasanii wana wajibu wa kushiriki mapambano ya kuboresha maisha ya wateja wao wakuu (wengi wao wakiwa waathirika wakuu wa ufisadi).

Tunahitaji akina (Masudi) Kipanya wengine kwenye bongofleva na miziki mingine kushirikiana na wale wote walio katika mapambano dhidi ya ufisadi huko nyumbani.Kelele za aina yoyote dhidi ya wahalifu (mafisadi) hao zitasaidia angalau kuwakumbusha kwamba tamaa na furaha zao ni kilio kwetu.

Hebu msikie Skinnyman anavyolalamika katika clip hii ya Council Estate of Minds kuhusu hali halisi ya maisha kwenye maghorofa (yaliyosahaulika,na makazi maarufu ya watu wa kipato duni) ya manispaa (Council estates)


15 Jan 2008

Hivi msomaji wangu mpendwa ulishaota ndoto ngapi za "ningependa kuwa flani" kabla hujafika hapo ulipo?Kwangu ni 3,moja naendelea kuhangaika nayo,na kwa Mapenzi yake Mola+jitihada zangu,natarajia kuitimiza miezi michache ijayo.Naomba niihifadhi ndoto hiyo kwa sasa.Ndoto yangu kwanza utotoni ilikuwa kuwa daktari.Sehemu ya elimu yangu ya msingi na O'level ilipatikana katika shule zilizokuwa karibu na hospitali flani yenye CV ya kuridhisha (imezaa madaktari wengi kupitia chuo cha udaktari kilichopo hapo).Kutokana na ukaribu kati ya shule na hospitali hiyo,wanafunzi walikuwa wakipendelea kwenda hapo wakati wa mapumziko ya asubuhi na mchana.Taratibu nikajikuta natamani kwamba siku moja nami niwe katika majoho meupe nikiokoa maisha ya binadamu wenzangu.Nadhani kilichonivutia zaidi kuhusu taaluma ya utatibu ni role yao katika maisha ya binadamu (well,at least sio kama wale wazembe "waliochanganya madawa" huko Muhimbili kwa kumpasua mtu kichwa badala ya mguu na vice versa).Ndoto hiyo iliyeyuka kama pande barafu kwenye maji ya moto baada ya kufeli somo la Fizikia (sioni haya kusema nilipata F japo nilikuwa na A ya Kemia).PCB ikawa imegoma hapo (nilikuwa na C ya Baiolojia).Nikapiga mahesabu ya CBG-Kemia,Baiolojia na Jiografia (ambapo "combi" ingekubali kwani nilikuwa nina A,C na B,consecutively).Ndoto ilifutika kabisa baada ya kuwasili shule nilopangiwa kusoma A'level.CBG ilikwepo lakini,kwanza shule ilikuwa haina mwalimu wa Jiografia (hivyo wanafunzi walikuwa wanalazimika kwenda shule jirani kupata mihadhara ya somo hilo).Lakini,to make matter even worse,nikaja kugundua kwamba Kemia ya A'level ni "hadithi tofauti" na ile ya O'level niliyoimudu.Did I mention kwamba niliibuka na D ya kichovu kwenye Hisabati huko O'level?Yeah I did,na Kemia ya A level imejaa "namba" (nadhani Physical Chemistry ndio balaa zaidi).Enewei,nikaamua kukimbilia kwenye HGL-Historia,Jiografia na Lugha ya Mama..Kimombo (ambayo ilikuwa na msingi mzuri wa A,B na A,consecutively huko O'level).Kilichonisaidia kuwa na options mbalimbali ni mchanganyiko wa masomo huko O'level (sayansi,sanaa na biashara) lakini ndoto ya udaktari ndio ikafa kifo cha asili.

Ndoto ya pili ilinijia nilipokuwa jeshi la kujenga taifa (JKT).Did I mention kwamba shule niliyosoma A'level nayo ilikuwa ya mchepuo wa kijeshi?Sorry if I didn't,lakini "jeshi linininoma" kisawasawa kwa miaka miwili ya A'level kijeshi na mmoja wa JKT kijeshi.Let's leave it there.Huko JKT nilikutana na jamaa flani mahiri sana kwa kufokafoka (rapping).Sijui yuko wapi sasa.Yeye alikuwa rafiki na jamaa mmoja ambaye aliwahi kuibuka mshindi wa mashindano ya Yo!Rap Bonanza miaka ileeee...anaitwa Frank Mtui a.k.a Fresh XE (kama sijakosea,maana ni muda mrefu sasa).Urafiki wao ndio uliopelekea jamaa yangu huyo ambaye jina limenitoka kidogo kuwa mahiri kwenye ku-rap.Tofauti na yeye,mie nikagundua mapema kwamba ulimi wangu mzito,hivyo to become a rapper was out of question.Ndoto yangu ikaegemea kwenye u-producer.Baada ya ngarambe na fatiki za kambini,jamaa yangu huyo alikuwa akinisimulia stori mbalimbali kuhusu maprodyuza maarufu wa muziki wakufokafoka,kama vile Dr Dre,Jermaine Dupri,Pete Rock,et cetera (Dre became my most favourite).Baadaye nikakutana na watu wawili waliozidi kuipa uhai ndoto yangu ya uprodyuza,mmoja anaitwa Profesa Ludigo (alikuwa akitajwatajwa sana kwenye bongoflava kadhaa,ila sijui kwa sasa yuko wapi),mwingine anaitwa Sajo (sio wa Daz Nundaz) ambaye aliwa karibu na Saigon wa Diplomatz,moja ya makundi ya awali ya rap huko nyumbani.Mara ya mwisho nilisikia huyu jamaa (Sajo) yuko Wichita.Prof Ludigo ni "kichwa" kwenye music production na Sajo anaijua fani hiyo nje-ndani.Ndoto ya uprodyuza ikapata nguvu za ziada.How I ended not being a producer I,for some time, dreamt of becoming ,only my God and I know...here I am,not "book-worming" a certain medical journal or searching for some new beat producing softwares,but SIASA...yeah,that's what I'm studying.

Let's go to the point.Nimesoma na kusikia habari kwamba "hali ya afya ya Bongoflava sio ya kuridhisha",na kama ni mgonjwa basi yuko chumba cha wagonjwa mahututi.May be hiyo ni kile ambacho kwenye sarufi ya Kiingereza wanaita "hyperbole" au kuzidisha chumvi.Lakini,kwa a producer that never became one (mimi huyo),nadhani mwelekeo wa muziki huo sio wa kuleta matumaini sana.Frankly speaking,baadhi ya nyimbo za bongofleva zinaweza kukupa hisia kwamba mwanamuziki na prodyuza wake waliurekodi wimbo husika wakiwa usingizini.Ladha (flava) duni,ujumbe (message) ni dhaifu au haueleweki,na wakikurupuka na video ndio inakuwa kana kwamba ililengwa kwa ajili ya "youtube" na sio kuonyeshwa kwenye runinga.Of course,kuna exceptions lakini ni chache.

Nadhani tatizo kubwa liko kwa mwanamuziki kuhakikisha anakuwa bora zaidi ya alipotoa single au album iliyompatia umaarufu.Shughuli imekuwa "kujirusha" sana na kuwekeza "chini" (you surely know what I mean.If you dont,namaanisha "ngono").Wengine wakakimbilia kununua vitu vya thamani ambavyo kwa bahati mbaya hawana uwezo wa kuvimudu.Wengine wakajilinganisha na "wazungu wa unga" ambao hutumia fedha kwa kasi wakijua "shamba" lipo pindi "wakichoka" (wakifilisika).Wengine wakawaiga watu wa Mbughuni na Mererani ambao nao,kama "wazungu wa unga" hutumia kwa fujo wakijua "jiwe" bado lipo mgodini.

Hakuna dhambi kula matunda ya jasho lako lakini ni muhimu kuepuka kung'oa kabisa mmea unaotoa matunda hayo.Lakini vijana wengi waliotokea kupata umaarufu kwenye bongofleva wanakabiliwa na tatizo jingine kubwa zaidi ya hilo la kubweteka au kula jasho lao pasipo kufikiria kesho itakuwaje.Hili ni matumizi ya majani haramu yajulikanayo kama bangi.Kuna idadi kubwa ya wasanii wanaoendekeza bangi kupita vipaji vyao.Najua wapo wanaodai wakivuta "weed" ndio wanawezesha verse kushuka kwa kasi ya tsunami,lakini hizo ni crazy excuses.Bangi sio kitu kizuri.Na mbaya zaidi ni kwa wale wanaotengeneza cocktail ya bangi,unga na laga.

Nini kifanyike?Well,nchi ina matatizo makubwa na ya muhimu zaidi kuliko "hali ya afya ya bongoflava".Na kwa vile suala la kulinda au kutelekeza ajira au kipaji ni la mtu binafsi,inaweza kuwa sio rahisi kuwashauri baadhi ya nyota wetu wanaoelekea kufifia.Wanaopenda majibu mepesi kwenye maswali magumu wanahitimisha kwamba "taarabu ilivuma wee baadaye ikafifia,na sasa ni zamu ya bongoflava...".Mie naona chanzo ni kipana zaidi ya suala la kuvuma na kufifia:kubweteka na mafanikio,kuendekeza anasa na kusahau kazi,maprodyuza wanaoigana wanaopelekea msikilizaji kushindwa kutofautisha wimbo wa msanii mpya na wa zamani-sambamba na productions nyingi "zisizokwenda shule" ni mlolongo wa sababu zinazowakwaza vijana hawa.You have been warned....

Talking of Dr Dre,he cautions in Been There Done That, that "...a fool and his dough soon split..." in the 3rd line of the 2nd verse.Here is the video (caution: explicit lyrics).


Na hapa ni Jay-Z katika Girls,Girls,Girls (dedicated kwa "wanaoendekeza vimwana")


And finally,nadhani utakubaliana nami kwamba some flavaz seem to last forever in your ears,kwa mfano hii I Got 5 on It ya Luniz (japo wenyewe "wamepotea")





Au hii soundtrack ya Friday, You Can Do It ya Ice Cube (Caution: explicit lyrics)


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.