Showing posts with label UBINAFSISHAJI TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label UBINAFSISHAJI TANZANIA. Show all posts

27 Apr 2009

MOJA YA MAENEO KOROFI KATIKA BARABARA KUU WILAYANI KILOMBERO.UNGETEGEMEA VIONGOZI WA WILAYA HIYO WAELEKEZE NGUVU ZAO KWENYE KU-ADDRESS SHIDA ZA WANANCHI (KAMA HIYO YA BARABARA) BADALA YA KUTAKA KUUZA ARDHI YAO.HUU NI UNYAMA USIOKUBALIKA HATA CHEMBE.ANYWAY,2010 IS COMING.I HOPE UKATILI HUU WA VIONGOZI WABABAISHAJI UTAKUWA SABABU TOSHA YA KUWAPIGA CHINI KWENYE UCHAGUZI.

na Mwandishi Wetu, Kilombero

KIJIJI cha Namwawala, kilichopo Kata ya Idete, Tarafa ya Ifakara, Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, kiko hatarini kuuzwa kwa mwekezaji, huku viongozi wanaosimamia mpango huo wakidai ni agizo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka katika kijiji hicho, zilidai kuwa baadhi ya viongozi wa wilaya na mkoa, wanasimamia uuzaji wa ekari zaidi ya 3,384, sawa na asilimia 95 ya ardhi ya kijiji chote, kwa ajili ya mwekezaji anayetarajia kuanzisha mashamba ya miwa na kiwanda cha sukari.

Hivi sasa, kijiji hicho kimeunda kamati kufuatilia mambo manne ya msingi ambayo ni kuthibitisha kauli ya viongozi wao kwamba Rais Kikwete ameamuakuchukua ardhi hiyo, na kama ardhi inayochukuliwa ni asilimia 95 ya eneo lote la
kijiji.

Mambo mengine ni, Mkurugenzi Mtendaji Kilombero kuanza kuthaminisha mali zao bila taarifa rasmi na kutaka wasomewe waraka unaoelekeza Rais Kikwete kutoa agizo la kuchukua ardhi na kumpa mwekezaji.

Kamati hiyo ambayo inadaiwa kuishi kwa kutishiwa na baadhi ya viongozi wilayani humo, inaundwa na Mwenyekiti Zuberi Kapindijega, Kenani Haule (Katibu), wakati wajumbe ni Johson Msuya na Godfrey Lwema.

Akizungumza na Tanzania Daima kutoka mjini Ifakara jana, Kapindijega, alisema baada ya viongozi wa wilaya na kata kupita kwa wananchi na kuwataka waanze kufanya tathimini ya mali zao na kujiandaa kuhama, walifikisha barua yao kwa Rais Kikwete jijini Dar es Salaam wakitaka ufafanuzi wa mpango huo.

“Januari 31 kwenye mkutano wa mapato na matumizi ya kijiji, iliibuka hoja ya wanakijiji kutaka kujua hatma ya ardhi yetu, ndipo mwenyekiti wa kijiji alitusomea waraka aliodai wa rais, ambao umetumika katika kuchukua asilimi 95 ya ardhi hiyo. Kutokana na mazingira na mfumo uliotumika kufikisha waraka huo wa rais kwetu, tunahisi kuna mchezo
mchafu.

“Kwa hofu hiyo na kwa kuwa kila tunaloliuliza jibu ni moja tu la rais kaamua kuchukua ardhi yake, ndiyo maana tumeamua kuja kuonana na wewe mwenyewe Mheshimiwa Rais,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo kwenda kwa rais iliyoandikwa Februari 13 na Tanzania Daima kupata nakala yake.

Hata hivyo, katika majibu ya rais kwa viongozi hao wa tume yalitolewa kwa barua iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, F. Mwaipaja, Februari 16, viongozi hao walitakiwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, na Mkuu wa Mkoa na kama hawataridhishwa, wanaweza kuonana na rais.

Kutokana na barua hiyo kutoka kwa rais, viongozi wa tume hiyo walibisha hodi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero kwa barua waliyoiandika Februari 20 nakufuatiwa na nyingine ya Februari 27, ambazo pia Tanzania Daima nakala zake inazo.

Hata hivyo, ofisi hiyo ya mkuu wa wilaya, ilijibu barua hiyo kupitia kwa Katibu Tawala, E Mmbaga, akidai kuwa ameagizwa na DC Evarist Evarist Ndikilo awajulishe wajumbe hao wa tume kwamba amepokea barua hizo.

“Aidha mnafahamishwa kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itawasiliana na SUDECO, Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Serikali ya Kijiji (Namwawala) pamoja na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), wanafanya tathmini ya fidia. Mnaombwa mvute subira kwani matokeo ya mawasiliano hayo, mtajulishwa,” ilisema barua hiyo.

Baada ya majibu hayo, tume hiyo pia ilifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, na kuwasilisha barua yao Machi 6, mwaka huu kutaka kupata ufafanuzi wa kuuzwa kwa ardhi ya kijiji chao.

Ofisi ya mkoa kupitia kwa Kaimu Katibu Tawala, L. Msuya, iliahidi katika barua yenye kumb namba CD/148/06/87, kwamba italishughulikia suala hili kwa makini.

“Kumbukeni kwamba mmeshafikisha malalamiko yenu kwenye ofisi ya rais na sasa mmerudishwa kwa Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo suala hili linatakiwa lishughulikiwe kwa umakini sana.
Mnatakiwa mvute subira wakati mkuu wa mkoa anafanya uchunguzi wa kina ili kupata ufumbuzi wa kudumu,” ilisema barua hiyo.

Hata hivyo, akizungumzia malalamiko ya tume hiyo, DC wa Kilombero, jana alikaririwa na moja ya vyombo vya habari vya kila siku kwamba wajumbe wa tume hiyo ni wachochezi na kutoa amri wakamatwe mara moja.

Uchunguzi wa Tanzania Daima umebaini kuwa, hali ya kijiji hicho si shwari kwani wananchi wanashindwa kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kwa hofu ya kuhamishwa, huku baadhi ya viongozi wakitofautiana kuhusu mpango huo unaodaiwa kuendeshwa kiujanja ujanja kwa kutumia jina la rais.


THIS IS BECOMING PERSONAL!TATIZO LA WILAYA YETU (NA JIMBO LA KILOMBERO KWA UJUMLA) NI KAMA HATUNA MBUNGE.KUNA JAMAA ANAITWA LIGALAMA.I JUST CANT UNDERSTAND WHAT THIS GUY HAS BEEN DOING!BADALA YA VIONGOZI KUWEKEZA NGUVU ZAO KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO WAO WANAENDEKEZA USHKAJI NA WAWEKEZAJI....NA HAIHITAJI UTAFITI KUFAHAMU KUWA KICHOCHEO KIKUBWA HAPO NI RUSHWA NA UFISADI KWA UJUMLA.

24 Oct 2008


SERIKALI ipo katika hatua za mwisho za kuingia ubia na Kampuni ya Sonangol kutoka nchini China kwa ajili ya kuendesha Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).

Nia hiyo ya serikali ilitangazwa jana kwenye ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, Mohamed Misanga, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupokea taarifa ya utendaji kazi wa ATCL.

Alisema ATCL, hivi sasa ipo katika hali mbaya kiuchumi kutokana na kuelemewa na madeni sambamba na kutokuwa na mtaji ambao utawezesha kuingia katika soko la ushindani.

Alisema awali serikali ilipozindua upya kampuni hiyo iliahidi kuchukua madeni yote na kutoa mtaji kwa kampuni hiyo, ili iweze kufanya biashara ya ushindani, lakini imeshindwa kutekeleza ahadi yake.

“Hali ya kiuchumi kwa ATCL ni mbaya, serikali imeamua kuinusuru kwa kuingia ubia na Kampuni ya Sonangol International ambayo wakati wowote kuanzia sasa watasaini mkataba,” alisema Misanga.

Alisema wabunge wameionya serikali kuwa makini na mwekezaji huyo, ili ubia huo usije ukawa kama wa kampuni ya SAA ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo iliyosababisha ATCL iwe hoi na kuidai madeni makubwa.

Alisema lengo la wabunge ni kuona serikali haiingi tena katika uingiaji mikataba mibovu ambayo imekuwa isainiwe na wataalamu wa serikali kila kukicha,” alisema Misanga.

Alisema ni jambo la kusikitisha kuwa hivi sasa ATCL imekuwa ikinunua mafuta kwa siku kila ndege inapotaka kufanya safari badala ya kununua mafuta ya muda wa miezi mitatu au minne.

Aliongeza kuwa shirika hilo halikopesheki na kila kinachopatikana hutumika kwa madeni na shughuli za uendeshaji, jambo ambalo hulidhoofisha shirika hilo kununua na kukodisha ndege.

Alibainisha kuwa Serikali tayari imeamua kuiandikia barua Kampuni ya SAA kuitaka iache kuidai ATCL na badala yake iidai serikali ambayo ndiyo iliyoyachukua madeni.

Aidha, alisema ATCL ipo katika mchakato wa kuuza ndege yake aina ya Boeing 737-200 ambayo inadaiwa kutumia mafuta mengi sambamba na kupitwa na wakati.

“Uamuzi huu utasaidia kupunguza gharama zisizo za lazima kwa shirika lakini pia itasidia kupatikana kwa fedha kidogo zitakazotumika kwa mambo mengine,” alisema Misanga.

Aidha, alikanusha kuwa ATCL hakuna ndege mbovu zilizoletwa hivi sasa kwani kuna Mamlaka mbalimbali ambazo huzithibitisha ndege hizo kabla ya kuanza kazi.

CHANZO: Tanzania Daima

Hivi hatuwezi kuwauliza wenzetu Wakenya au Waethiopia kwanini wao wameweza lakini sie tunashindwa?Well,pengine Kenya na Ethiopia ni mbali,if so kwanini tusiwadadisi wazalendo wenzetu wa Precision Air?

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.