Showing posts with label KILOMBERO. Show all posts
Showing posts with label KILOMBERO. Show all posts

14 Jan 2012


Habari za kusikitisha zilizopatikana kwenye mtandao wa jamii wa Twitter na ukumbi wa mijadala ya mtandaoni wa Jamii Forums zinaeleza kuwa Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chadema,Regia Mtema,amefariki kwa ajali ya gari iliyotokea daraja la mto Ruvu.

Licha ya kifo cha Regia kuwa pigo na pengo kubwa kwa Chadema pia ni msiba mkubwa kwa sie wazawa wa wilaya ya Kilombero,mahali alipozaliwa marehemu na ambapo alipatumikia kwa nguvu zake zote.

Tutawaletea taarifa zaidi kadri zinavyopatikana.

Bwana Ametoa Bwana Ametwaa,Jina lake lihimidiwe Milele.Amen.





9 Oct 2011



Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete,

Kwanza naomba kukupa salamu za heri kwa siku yako ya kuzaliwa uliyoadhimisha jana.Mungu akuzidishie uhai,afya njema na nguvu ya kuendelea kututumikia Watanzania wenzako.

Baada ya salamu hizo,naomba niende kwenye mjadala usio rasmi ulioanzia juzi huko Twitter.Katika majibu yako kwa swali langu tunawezaje kuuelezea umasikini unaowakabili wakazi wa wilaya Kilombero (ambapo ulizuru majuzi) licha ya utajiri mkubwa wa raslimali-hususan ardhi yenye rutuba ambayo imelifanya eneo hilo kuwa maarufu kwa kilimo cha mpunga na nafaka ya mchele-ulieleza, naomba nikunukuu, "In Kilombero we've extension officers,SACCOS,market facilitation and mechanization initiatives.Some are using these opportunities" (kwa Kiswahili,Kilombero tuna maafisa ugani,vyama vya ushirika wa kuweka na kukopa,uwezeshaji masoko,jitihada za matumizi ya mashine.Baadhi ya watu wanatumia fursa hizi."

Labda nikuulize,Mheshimiwa Rais,je uliona umasikini usiofichika unaowagubika wakazi wengi wa wilaya ya Kilombero?Ninatumai uliouna japo watendaji wengi wana tabia ya kuificha taswira zisizopendeza ili waonekane wanatekeleza wajibu wao ipasavyo.Hapa ninamaanisha si ajabu iwapo watendaji wa serikali wilayani Kilombero wangeamua kukupa picha ya "kila kitu ni shwari" ili uridhishwe na utendaji kazi wao.

Tuje kwenye jibu lako with an assumption kwamba uliona umasikini unaowakabili "matajiri" wa Kilombero (in the sense of kuwa wakazi kwenye sehemu yenye utajiri lukuki).Mheshimiwa Rais,tatizo la Tanzainia yetu halipo kwenye uwepo wa maafisa wenye majukumu fulani bali ni iwapo maafisa hao wanatekeleza majukumu yao ipasavyo.Mara kadhaa,Mheshimiwa Rais,umelazimika kutumia madaraka yako kuwasaidia wananchi licha ya uwepo wa waziri husika,naibu wake,katibu mkuu,naibu katibu mkuu,mkurugenzi wa idara husika,mkuu wa mkoa,mkuu wa wilaya na pengine diwani kama si mwenyekiti wa serikali ya mtaa.

Mheshimiwa Rais,kama ilivyo kwenye sheria zetu nzuri na ambazo kwa hakika zingesimamiwa ipasavyo tungemedu kukabiliana na matatizo kama ufisadi kwa ufanisi (kwa mfano kwa kiutumia ipasavyo Sheria ya Uhujumu Uchumi) ni wazi pia kuwa laiti wengi wa watendaji unaoamini kuwa wanaweza kuwasaidia wananchi kufikia malengo yao ya kimaendeleo wangetimiza wajibu wao ipasavyo basi tusingeendelea kuwa moja ya nchi masikini kabisa duniani licha ya utajiri lukuki wa raslimali tulionao.

Ni wazi,Mheshimiwa Rais,kuwa laiti maofisa ugani unaowazungumzia huko Kilombero wangekuwa wanatimiza wajibu wao ipasavyo sio tu baadhi ya wakazi au wazawa wa neo hilo kama mie tusingekuwa na cha kulalamikia bali pia eneo hilo lingeweza kabisa kuwa mithili ya Saudi Arabia ya Tanzania (kwa kulinganisha uzalishaji mafuta wa Saudi na mchele wa wilaya ya Kilombero).Wnachofanya maofisa ugani unaosifia uwepo wao ni kukupatia ripoti nzuri zenye kutia matumaini lakini kimsingi wao ni miongoni mwa vikwazo vinavyokwamisha maendeleo ya eneo hilo.

Mheshimiwa Rais,ninaomba kuafikiana nawe kuwa uwepo wa SACCOs umelta ukombozi mkubwa kwa wananchi hususan wa vijijini.Masikini hawa ambao hawana amana za kuwawezesha kukupa benki wamepata ukombozi mkubwa kupitia SACCOs.Hata hivyo,nyingi ya taasisi hizo zimekuwa zikikabiliwa na na tatizo sugu la mtaji mdogo ambao unapelekea kuhudumia wananchi wachache kuliko ilivyopaswa.

Mhehimiwa Rais,utakumbuka jinsi wajanja (polite word for mafisadi) walivyo-misuse "Mamilioni ya Kikwete" na sehemu ya fedha hizo kuishia mifukoni mwao badala ya kuwafikia walengwa.Moja ya taasisi ambazo zingenufaika sana na mpango huo ni SACCOs mbalimbali nchini.

Lakini pia,Mheshimiwa Rais,katika kuonyesha namna serikali yako isivyotoa kipaumbele cha kutosha kwa wakulima waodogo wadogo,fedha za stimulus package zilielekezwa zaidi kwa viwanda na kampuni (ikiwa pamoja na zilizo hewa) badala ya kuwatupia macho wakulima hawa.

Kwa hakika inapendeza kumwona mwekezaji wa kigeni akiwekeza katika kilimo cha mpunga.Lakini ni wazi,Mheshimiwa Rais,ingependeza zaidi iwapo uwekezaji huo ungefanywa na wakulima hao masikini.Sio tu uwekezaji huo ungeinua hali za maisha za walalahoi hawa lakini pia ungeweza kutoa ajira za kutosha na kusaidia harakati za maendeleo ya eneo hilo na nchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Rais,kuhusu kuwezesha upatikanaji wa soko,ninaamini kuwa laiti ungepeata wasaa wa kusikia kilio cha wakazi wa eneo hilo (na pengine maeneo mengine ya uzalishaji) ungebaini kuwa licha ya utajiri wa mpunga/mchele,wakazi wa eneo hilo wanakabiliwa na tatizo sugu la masoko.Kimbilio kubwa limekuwa kwa walanguzi ambao hujazana huko kila unapojiri msimu wa mavuno.

Cha kusikitisha zaidi ni kwamba wakati tunaadhimisha mika 50 ya uhuru wetu,baadhi ya wakazi wa Kilombero hullazimika kurejea njia za kale za uuzaji wa mazao yao ambapo barter trade hutumika kuwawezesha baadhi ya wakulima kumudu kupata bidhaa kama mitumba ya nguo,sukari na hata chumvi.Hivi Waziri husika ana mpango gani mahsusi ya kusaidia wakulima wa aina hii?Tumesikia kuhusu Kilimo Kwanza na Mapinduzi ya Kijani lakini kama ilivyokuwa katika zama za Ujamaa na Kujitegemea kauli mbiu hizo zimesihia kuwa matamko tu yenye malengo mazuri lakini utekelezaji sio wa kuridhisha.

Kuhusu sapoti katika matumizi ya teknolojia kwa maana ya mashine za kilimo,laiti Mheshimiwa Rais ungeongea na wananchi wa eneo hilo wangekufahamisha kuwa wanakabiliwa na tatizo sugu la uhaba wa matrekta.Machache yaliyopo ni mabovu na gharama zake ni kubwa mno kiasi kwamba wakulima wanalazimika kutegemea jembe la kono.Miaka 50 ya uhuru lakini mkulima wa Kitanzania bado anategemea zaidi jembe la mkono badala ya mashine za kisasa.

Mheshimiwa Rais,moja ya sababu zilizowashawishi Watanzania kukupa kura nyingi mwaka 2005 (na baadaye mwaka 2010) ni dhamira uliyoonyesha mwanzoni kuwa unataka kupunguza (kama si kumaliza kabisa) matatiao yanayowakabili Watanzania.Kihistoria,unafahamika kama miongoni mwa viongozi wachache walio karibu sana na wananchi (hata kabla hujaingia Ikulu).Uelewa wako kuhusu matatizo ya Watanzania ulitarajiwa kutoa suluhisho la tatizo la umasikini wa kutupa unaowakabili Watanzania wengi.

Binafsi siamini kuwa wewe binafsi ndio pekee wa kulaumiwa bali baadhi ya watendaji wako.Sasa,Mheshimiwa Rais,mwaka 2006 ulionya watendaji wabovu wasitafsiri vibaya upole wako kwani usingesita kuwawajibisha.Lakini ukweli ni kwamba wengi wa watendaji wako hao wameendela kuwa kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya wananchi.

Mheshimiwa Rais,mwezi huu wa Oktoba utakuwa unatimiza mwaka mmoja mzima tangu uingie madarakani kwa awamu nyingine ya Urais.Lakini kama unakumbuka vyema,nyingi ya hadi ulizotoa mwaka 2005 hazijatekelezwa,na ukichanganya na za mwaka 2010 utaona kuwa una kazi ya ziada kumaliza utekelezaji wa ahadi hizo kabla hujang;atuka rasmi mwaka 2015.

Mwalimu Nyerere alitufundisha kuwa ili tuendelee tunahitaji WATU,ARDHI,SIASA SAFI na UONGOZI BORA.Sasa Mheshimiwa Rais,sio tu kwamba watu wapo bali pia   wana nia na kiu ya maendekleo yao binafsi na ya jamii zao.Ardhi ipo ya kutosha ikama ulivyoona huko Kilombero.Nadhani kinachokosekana na SIASA SAFI na UONGOZI BORA.

Mheshimiwa Rais,umebakiwa na miaka minne tu kabla hujamaliza muda wako kwa mujibu wa sheria.Hivi  ungependa umalize muda wako ukiwa na legacy isiyopendeza kuhusu masikini wa kutupa ambao hawana mbele wala nyuma.

Mwaka 2005 uliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania lakini baadhi yetu sasa tumekuwa tukitafsiri kama Mauisha Bora kwa kila fisadi.Ninaamini kabisa,Mheshimiwa Rais uliota ahadi hizo ukiamini kuwa zinatekelezeka.Lakini kwa bahati mbaya-au makusudi- hali yetu ni mbaya sana.Maendeleo tunayodaiwa kuyafikia yameendelea kubaki ndoto ya mbali.

Sasa Mheshimiwa kwa vile umebakiwa na miaka minne tu na rundo la ahadi zinazosubiri utekelezaji basi ninaomba utumie muda huu ulisailia kufanya jtihada za makusudi kuhakikisha unakumbukwa kwa jambo moja au jingine la msingi.

Basi Mheshimiwa Rais naomba nisikuchoshe sana na makala hii ndefu.Ninaamini una kila SABABU,na UWEZO lakini kiachokosekana ni NIA ya kuifikisha Tanzania mahala inapostahili kuwepo kimaendeleo.Kama Rwanda wamemudu kupiga hatua licha ya mauaji ya kimbari huko nyuma kuathri umoja wao kitaifa,na kama Botswana na Sychelles zinamudu kuwa majabali ya uchumi barani japo tunaweza kuwa na utajiri mkubwa wa raslimali kuliko nchi hizo,hivi tuna sababu gani ya kuendelea kusuasua kiuchumi na kimaendeleo kiujumla?

UKIAMUA,INAWEZEKANA

27 Apr 2009

MOJA YA MAENEO KOROFI KATIKA BARABARA KUU WILAYANI KILOMBERO.UNGETEGEMEA VIONGOZI WA WILAYA HIYO WAELEKEZE NGUVU ZAO KWENYE KU-ADDRESS SHIDA ZA WANANCHI (KAMA HIYO YA BARABARA) BADALA YA KUTAKA KUUZA ARDHI YAO.HUU NI UNYAMA USIOKUBALIKA HATA CHEMBE.ANYWAY,2010 IS COMING.I HOPE UKATILI HUU WA VIONGOZI WABABAISHAJI UTAKUWA SABABU TOSHA YA KUWAPIGA CHINI KWENYE UCHAGUZI.

na Mwandishi Wetu, Kilombero

KIJIJI cha Namwawala, kilichopo Kata ya Idete, Tarafa ya Ifakara, Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, kiko hatarini kuuzwa kwa mwekezaji, huku viongozi wanaosimamia mpango huo wakidai ni agizo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka katika kijiji hicho, zilidai kuwa baadhi ya viongozi wa wilaya na mkoa, wanasimamia uuzaji wa ekari zaidi ya 3,384, sawa na asilimia 95 ya ardhi ya kijiji chote, kwa ajili ya mwekezaji anayetarajia kuanzisha mashamba ya miwa na kiwanda cha sukari.

Hivi sasa, kijiji hicho kimeunda kamati kufuatilia mambo manne ya msingi ambayo ni kuthibitisha kauli ya viongozi wao kwamba Rais Kikwete ameamuakuchukua ardhi hiyo, na kama ardhi inayochukuliwa ni asilimia 95 ya eneo lote la
kijiji.

Mambo mengine ni, Mkurugenzi Mtendaji Kilombero kuanza kuthaminisha mali zao bila taarifa rasmi na kutaka wasomewe waraka unaoelekeza Rais Kikwete kutoa agizo la kuchukua ardhi na kumpa mwekezaji.

Kamati hiyo ambayo inadaiwa kuishi kwa kutishiwa na baadhi ya viongozi wilayani humo, inaundwa na Mwenyekiti Zuberi Kapindijega, Kenani Haule (Katibu), wakati wajumbe ni Johson Msuya na Godfrey Lwema.

Akizungumza na Tanzania Daima kutoka mjini Ifakara jana, Kapindijega, alisema baada ya viongozi wa wilaya na kata kupita kwa wananchi na kuwataka waanze kufanya tathimini ya mali zao na kujiandaa kuhama, walifikisha barua yao kwa Rais Kikwete jijini Dar es Salaam wakitaka ufafanuzi wa mpango huo.

“Januari 31 kwenye mkutano wa mapato na matumizi ya kijiji, iliibuka hoja ya wanakijiji kutaka kujua hatma ya ardhi yetu, ndipo mwenyekiti wa kijiji alitusomea waraka aliodai wa rais, ambao umetumika katika kuchukua asilimi 95 ya ardhi hiyo. Kutokana na mazingira na mfumo uliotumika kufikisha waraka huo wa rais kwetu, tunahisi kuna mchezo
mchafu.

“Kwa hofu hiyo na kwa kuwa kila tunaloliuliza jibu ni moja tu la rais kaamua kuchukua ardhi yake, ndiyo maana tumeamua kuja kuonana na wewe mwenyewe Mheshimiwa Rais,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo kwenda kwa rais iliyoandikwa Februari 13 na Tanzania Daima kupata nakala yake.

Hata hivyo, katika majibu ya rais kwa viongozi hao wa tume yalitolewa kwa barua iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, F. Mwaipaja, Februari 16, viongozi hao walitakiwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, na Mkuu wa Mkoa na kama hawataridhishwa, wanaweza kuonana na rais.

Kutokana na barua hiyo kutoka kwa rais, viongozi wa tume hiyo walibisha hodi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero kwa barua waliyoiandika Februari 20 nakufuatiwa na nyingine ya Februari 27, ambazo pia Tanzania Daima nakala zake inazo.

Hata hivyo, ofisi hiyo ya mkuu wa wilaya, ilijibu barua hiyo kupitia kwa Katibu Tawala, E Mmbaga, akidai kuwa ameagizwa na DC Evarist Evarist Ndikilo awajulishe wajumbe hao wa tume kwamba amepokea barua hizo.

“Aidha mnafahamishwa kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itawasiliana na SUDECO, Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Serikali ya Kijiji (Namwawala) pamoja na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), wanafanya tathmini ya fidia. Mnaombwa mvute subira kwani matokeo ya mawasiliano hayo, mtajulishwa,” ilisema barua hiyo.

Baada ya majibu hayo, tume hiyo pia ilifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, na kuwasilisha barua yao Machi 6, mwaka huu kutaka kupata ufafanuzi wa kuuzwa kwa ardhi ya kijiji chao.

Ofisi ya mkoa kupitia kwa Kaimu Katibu Tawala, L. Msuya, iliahidi katika barua yenye kumb namba CD/148/06/87, kwamba italishughulikia suala hili kwa makini.

“Kumbukeni kwamba mmeshafikisha malalamiko yenu kwenye ofisi ya rais na sasa mmerudishwa kwa Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo suala hili linatakiwa lishughulikiwe kwa umakini sana.
Mnatakiwa mvute subira wakati mkuu wa mkoa anafanya uchunguzi wa kina ili kupata ufumbuzi wa kudumu,” ilisema barua hiyo.

Hata hivyo, akizungumzia malalamiko ya tume hiyo, DC wa Kilombero, jana alikaririwa na moja ya vyombo vya habari vya kila siku kwamba wajumbe wa tume hiyo ni wachochezi na kutoa amri wakamatwe mara moja.

Uchunguzi wa Tanzania Daima umebaini kuwa, hali ya kijiji hicho si shwari kwani wananchi wanashindwa kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kwa hofu ya kuhamishwa, huku baadhi ya viongozi wakitofautiana kuhusu mpango huo unaodaiwa kuendeshwa kiujanja ujanja kwa kutumia jina la rais.


THIS IS BECOMING PERSONAL!TATIZO LA WILAYA YETU (NA JIMBO LA KILOMBERO KWA UJUMLA) NI KAMA HATUNA MBUNGE.KUNA JAMAA ANAITWA LIGALAMA.I JUST CANT UNDERSTAND WHAT THIS GUY HAS BEEN DOING!BADALA YA VIONGOZI KUWEKEZA NGUVU ZAO KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO WAO WANAENDEKEZA USHKAJI NA WAWEKEZAJI....NA HAIHITAJI UTAFITI KUFAHAMU KUWA KICHOCHEO KIKUBWA HAPO NI RUSHWA NA UFISADI KWA UJUMLA.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.