Showing posts with label USAGAJI. Show all posts
Showing posts with label USAGAJI. Show all posts

22 May 2016



Taarifa mbalimbali zinaonyesha kuwa kuna ongezeko kubwa la Watanzania wanaojihusisha na ushoga na usagaji japokuwa vitendo hivyo ni kinyume na sheria za nchi na haviendani na mila na desturi zetu.

Hata hivyo, yawezekana kushamiri kwa vitendo hivyo kunaendana na taarifa za kitafiti kuwa sie Watanzania twaongoza kwa unafiki. Wiki chache zilizopita niliweka bandiko hapa bloguni lililohusu ripoti ya utafiti wa kundi la wasomi katika chuo kikuu cha Nottingham, hapa Uingereza, ulivyobainisha kuwa Tanzania yaongoza duniani kwa unafiki.

Binafsi sikushangazwa na ripoti hiyo hasa kwa vile kuna maeneo mawili yanayothibitisha bayana unafiki wetu. La kwanza ni uhusiano kati ya ucha-Mungu wetu na maovu.

Asilimia kubwa ya Watanzania ni wacha-Mungu. Takwimu zaashiria kuwa takriban asilimia 70 ya Watanzania ni aidha Wakristo au Waislam. Wengi kati ya hao ni watu wasiokosekana kanisani au misikitini. Swali: kama wengi wetu ni waumini kiasi hicho, ni akina nani basi wanaojihusisha na ufisadi, rushwa, biashara ya madawa ya kulevya, ushirikina, na maovu mengine katika jamii?

Tofauti na huko nyumbani, ucha-Mungu hapa Uingereza ni wa kusuasua mno. Watu wengi hapa hawamtambui Mungu na wanajitambulisha kuwa hawana dini. Makanisa mengi yanageuzwa kuwa baa au kumbi za starehe kutokana na uhaba wa waumini.



Lakini licha ya udhaifu katika mahusiano kati yao na Mungu, wenzetu hawa kwa kiasi kikubwa sio wanafiki. Asilimia kubwa kabisa ya watu hawa wanaishi kwa kipato halali, wanaamini katika ukweli, kwa maana ya kusema ukweli na sio wadanganyifu, wanafuata sheria na taratibu mbalimbali, kwa mfano moja ya dhambi kuu hapa ni ukwepaji kodi, kitu ambacho ni kama hobby ya wengi wa wafanyabiashara huko nyumbani.

Eneo la pili ni suala la ushoga na usagaji. Kwa huko nyumbani, suala hili ni mwiko mkubwa, ni laana, ni kinyume na maadili yetu. Lakini kuthibitisha unafiki wetu, sio tu ushoga na usagaji upo bali pia unakua kwa kasi kubwa.

Nenda katika kitchen parties za watu maarufu na 'wakata viuno' ni mashoga huku wengi wa 'makungwi' wakituhumiwa kuwa wasagaji. Inaelezwa kuwa njia moja maarufu ya kusambaa kwa usagaji huko nyumbani ni 'makungwi' wanaofundisha mabinti (kwa malipo) jinsi ya kufanya tendo la ndoa. Hawa wametapakaa jijini Dar na baadhi wanahamia mikoani. Kimsingi, 'darasa la tendo la ndoa' wanalofundisha ni kwa kusagana na 'wanafunzi' wao.

Shughuli za 'madada wa mujini' hazijakamilika kama hakuna akina 'anti naniliu au anti nanihino.' Lakini watu haohao ndio wanaohubiri kwa sauti kubwa kuwa "habari za ushoga na usagaji huko huko kwao (wazungu)."

Kuna kitu kingine 'kichafu' ambacho Watanzania twasifika mno, nacho ni umahiri katika tendo la ndoa kinyume cha maumbile. Kwa kifupi, hii ndio sababu ya kushamiri kwa biashara ya "dawa za makalio feki ya Mchina." Tendo la ndoa kinyume cha maumbile limekuwa kama 'fasheni' kwa wengi wetu huko nyumbani na huku ugenini tunakoishi. 

Sasa, japo tendo la ndoa kinyume cha maumbile sio ushoga per se, kuna hisia kuwa wazoefu wa tabia hiyo "wakikosa nyama wanaweza kula majani." Yaani wanaume wanaopenda tabia hiyo wakikosa mwanamke wanaweza kufanya hivyo na mwanaume shoga.

UTHIBITISHO wa unafiki wetu: Well, sehemu mwafaka zaidi ya kutambua unafiki wetu kuhusu ushoga na usagaji ni INSTAGRAM. Huko, kuna mashoga wanaojinadi waziwazi. Lakini tatizo sio wao kujinadi tu bali ni idadi ya 'followers' wao. Ni wazi kuwa laiti ingekuwa watu wanachukia ushoga 'kihivyo' basi mashoga huko Insta wasingekuwa maarufu kiasi cha kupata followers hadi laki na zaidi.

Profiles hizi pichani chini ni za baadhi tu ya mashoga wa Kitanzania huko Instagram.  Je kama sie sio wanafiki na laiti tungekuwa tunauchukia ushoga 'kihivyo' hao maelfu kwa malaki ya followers kwa hao mashoga wangetaka wapi?


Ukitaka kuchimba zaidi kuhusu 'unafiki' wetu, geukia suala jingine maarufu huko nyumbani: USHIRIKINA. Kwa mujibu wa utafiti wa hivi karibuni wa taasisi moja ya kimataifa inayoheshimika kwa utafiti ya PEW ya Marekani, Tanzania ipo 'matawi ya juu' katika masuala ya juju, ndumba na ngai, tunguri, kamati ya ufundi, wanga...USHIRIKINA... kama inavyoonyeshwa kwenye chati na ramani hapo chini.




Kwa vile lawama pekee hazijengi, ni muhimu kujaribu kuangalia njia zinazoweza kutuondoa katika lindi hilo la unafiki. Binafsi, ninashauri tuwekeze zaidi katika dua na sala za dhati na sio za kinafiki. Au wewe msomaji mpendwa una maoni gani?



31 Mar 2010

Picha kwa Hisani ya Blogu ya Dina Marios
Mie kama Mkatoliki,siafikiani na ushoga au usagaji.Lakini kutoafikiana na kitu ni jambo moja na kukizuia ni jambo jingine.Ni ukweli usiofichika kuwa vitendo vya ushoga na usagaji vinaanza kuonekana kuwa vya kawaida katika jamii ya Kitanzania,hususan jijini Dar es Salaam.Je wakati umefika sasa kuhalalisha ushoga na usagaji?Na je kwa sheria za nchi ku-criminalise homosexuality inakiuka haki za binadamu?Na pengine swali la ziada,kuufanya ushoga na usagaji kuwa mithili ya laana kumesaidia chochote kuukomesha? Ni mjadala wa miaka nenda miaka rudi,karne baada ya karne.Je ushoga na usagaji ni tabia tu ya mwanadamu au ni asili?Ukitafuta jibu la mkato,unaweza kutotenda haki kwa upande mwingine wa mjadala.Kwa ufahamu wangu mdogo,kuna maelezo ya takriban aina mbili.Hoja ya kwanza,ushoga na usagaji ni suala la kimaumbile/kibaiolojia zaidi kuliko ridhaa ya mwanadamu.Maelezo haya yanazingatia wingi wa homini za jinsia tofauti kwatika mwili.Kwa maana kwamba mwanamke mwenye homoni nyingi za kiume ana uwezekano wa kuwa msagaji,na mwanaume mwenye homoni nyingi za kike anaweza kuwa shoga.Ni ishu complicated lakini nimejaribu kuieleza kwa kifupi.

Hoja ya Pili,ushoga na usagaji ni tabia tu ya mwanadamu kama zilivyo tabia nyingine.Yaani ni kama mtu anapoamua kuwa mvuta sigara au mtumia kilevi.Namna mhusika anavyoangukia kwenye tabia ya ushoga au usagaji nayo inaweza kuangalia kwa namna kadhaa.Kwa mfano,mwanadamu anaweza kuangukia kwenye ushoga au usagaji kwa tamaa.Au anaweza kuingia kwenye vitu hivyo kutokana na kuiga.Au pia anaweza kuwa 'majeruhi wa mchezo mchafu' i.e. alilawitiwa jela akaishia kupenda,alijaribu akanogewa,nk.La muhimu hapa ni kwamba uamuzi wa kuwa shoga au msagaji ni katika kile wanasosholojia wanakiita rational choice.Mtu anapima faida na hasara (cost and benefit analysis) kisha anachukua uamuzi anaoona unafaa.Pia hapa kuna suala la makuzi (socialisation) ambapo zawadi na adhabu (rewards and punishment),au tuseme sanctions,zinachangia kukua au kusinyaa kwa tabia husika.Kama familia,kwa mfano,haikemei tabia flani basi kuna uwezekano wa tabia hiyo kuonekana inakubalika.Lakini pia kuna vitu kama fedha ambapo mtoto analawitiwa kisha anapewa fedha inayoweza kumwaminisha kuwa alichofanya ni sahihi.Again,ni maelezo complicated sana na ni ya kitaaluma zaidi kuliko kimtaani.

Yote katika yote,ushoga na usagaji unazidi kushamiri katika jamii yetu licha ya 'jicho kali' la jamii.Je hiyo inamaanisha kuwa ukali huo dhidi ya tabia hiyo umeshindwa kuleta ufanisi?Tukiangalia suala hilo kwa mtazamo wa kisosholojia,inawezekana jibu lisiwe kuwa jamii imeshindwa bali ni ukweli kwamba katika jamii yoyote kuna uwezekano wa kuwepo tabia zisizokubalika.Hiyo ni katika kile wanasosholojia wanakiita deviance.Kila jamii ina walevi,wazinzi,vibaka,mafisadi,nk.Ni makundi yanayokwenda kinyume na kanuni na taratibu zinazoiongoza jamii husika.

Kwa huku nchi za Magharibi,ushoga na usagaji unazidi kuwa jambo la kawaida katika jamii.Lakini sio kirahisi hivyo kwani bado mashoga na wasagaji wanaangaliwa kwa 'jicho la shaka'.Na wao ni miongoni mwa makundi yanayolalamikia kubaguliwa.Hata hivyo,sheria zinawalinda na katika baadhi ya nchi hata ndoa zao zinatambulika kuwa ni ndoa halali.Lakini tena,kuwa na sheria ni kitu kimoja,na jamii kuiheshimu ni kitu kingine.Ni katika minajili hiyo,mashambulizi au uonevu dhidi ya mashoga na wasagaji si jambo geni katika nchi hizo.

Hawa wenzetu wanaamini kuwa mashoga na wasagaji hawastahili kubaguliwa,pasipo kujali kwanini mtu amekuwa shoga au msagaji.Na kinachoangaliwa hapo ni haki za binadamu.Wanasema ushoga au usagaji haumuondolei mtu haki zake kama mwanadamu.Je,kwa mtizamo huo wa Kimagharibi,ina maana jamii yetu huko nyumbani inawanyima haki wanajamii wenzao wanaojihusisha na ushoga na usagaji?Well,kuna wanaosema mila na desturi zetu zinapinga vitendo kama hivyo.Je mila hizo ziendelee kudumu hata kama zinawabagua baadhi ya wanajamii?Binafsi sina jibu sahihi bali nadhani swali hilo linabaki mikononi mwa jamii yetu.

Sijui wewe msomaji unaonaje lakini mie binafsi,nikiweka kando imani yangu ya Kikatoliki,sijali sana namna gani mtu anatumia uhuru wake wa kijinsia alimradi hanikwazi kwa namna yoyote.Naweza kutamka bayana kuwa namchukia zaidi fisadi anayekwaza maendeleo ya nchi yangu kuliko shoga au msagaji anayefanya anachoamini ni sahihi kwake.Lakini hiyo sio kusema naunga mkono vitendo hivyo hasa kwa vile imani yangu kiroho haiafiki.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.