Showing posts with label USALAMA WA TAIFA. Show all posts
Showing posts with label USALAMA WA TAIFA. Show all posts

12 Oct 2010


Nimekumbana na post ifuatayo hapo Jamii Forums.Naiwasilisha kama ilivyo kisha tujiulize kwa pamoja (kama tuhuma hizo ni za kweli) wanafanya hivyo kwa faida ya nani?

Taarifa ya Siri - Mikakati ya Kuiba Kura Inavyoendelea USALAMA WA TAIFA
Napenda kuwajulisha mikakati michafu ya kupora na kuzuia maamuzi ya umma yanayofanywa na ccm kwa uratibu wa usalama wa taifa. Baada ya kubaini dalili za kuanguka vibaya katika uchaguzi wa mwaka huu idara ya usalama wa taifa imeandaa mikakati ya kuiba kura ili kuzuia chadema msiingie ikulu. Mikakati hii inaeleweka vizuri kwa tume ya taifa ya uchaguzi ambayo inashirikiana bega kwa bega na idara ya usalama wa taifa kumtengenezea jk ushindi bandia wa 80%. Wana hakika watanzania watagundua wizi huo na watakataa matokeo ndiyo maana kwanza waliwatumia viongozi wa dini waliotembelea makao makuu ya chadema wawasihi chadema wakubali matokeo yatakapotangazwa na juzi wamelitumia jeshi kutisha wananchi watakaoamua kupinga matokeo ya kupikwa yanayoandaliwa na nec/usalama wa taifa. Majid Kikula ambaye ni government security officer ndiye mratibu wa zoezi la kuiba kura, ni mtaalamu aliyebobea katika kazi za aina hii aliratibu vizuri zoezi kama hilo mwaka 2005. Pia mwaka 2007 alitumwa kenya kwenda kumsaidia kibaki kupora ushindi wa odinga.
Kikula anatumia muda wake mwingi hivi sasa ofisi za tume ya uchaguzi kwa ajili ya uratibu wa uvurugaji daftari la kudumu la wapiga kura akiifanya kazi hiyo kwa karibu na baadhi ya watendaji wa nec na maafisa kadhaa wa usalama wa taifa kutoka kurugenzi ya IT ya idara ya usalama (DITA) ambao wako ndani ya nec kwa zaidi ya miezi sita sasa, nitawapatia majina yao. Pia kuna vijana wataalamu wa IT waliochukuliwa kutoka maeneo mbalimbali wamepewa nyumba upanga mtaa wa undali shughuli kubwa wanayofanya ni kuandaa utaratibu wa ku-access remotely daftari la kudumu la wapiga kura. Hawa wanafanya kazi chini ya Salva Rweyemamu na Mindi Kasiga kutoka kurugenzi ya mawasiliano ikulu. Wapo vijana kadhaa leo nawapa majina ya wawili; Maharage Chande na Edgar Masatu wanafanya kazi kwa karibu na Nzowa wa idara ya usalama ambaye ndiye aliyeratibu shambulio la kumwagiwa tindikali Kubenea. Pia kuna kundi linalojumuisha wataalamu wa printing wa kiwanda cha uchapaji cha usalama wa taifa kilichopo MALINDI ambao hivi karibuni walikuwa mjini tanga kwa semina fupi ya jinsi ya kughushi kura kupitia fake ballot paper, timu hii inaongozwa na ndg SINYAU.
Kwa hiyo utaona kwamba imeandaliwa mikakati mingi kuufanikisha uovu huo ili mmoja ukikwama basi mwingine utatumika ila wameamua ni lazima jk ashinde kwa 80%. Ndani ya idara ya usalama wa taifa maafisa wengi wamechoshwa na uongozi mbovu wa ccm hivyo wanataka mabadiliko ya uongozi idara imechukua hatua kadhaa kuhakikisha maafisa wote wa idara wanampigia kura jk, wote wameagizwa kuwasilisha vitambulisho vyao vya kupigia kura ili vinakiliwe namba ili atakayepigia upinzani afukuzwe kazi baada ya uchaguzi. Fuatilieni kwa karibu haya niliyowaeleza nimeyapata kwa nafasi yangu ndani ya tiss. Huyu KIKULA mfuatilieni kwa  karibu ni hatari. HAKIKISHENI DUNIA NA WATANZANIA WOTE WANAJUA MAPEMA HILA HIZI. Jambo la kujiuliza maafisa usalama wa taifa wanafanya nini ndani ya tume ya uchaguzi wakati huu.



29 Sept 2010


CHADEMA: Synovate wahini mahakamani
*Slaa asema wanazo nyaraka za utafiti wao.
*Adai kuna mbinu za 'kuchakachua' matokeo.

Na Tumaini Makene

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeivaa kampuni utafiti ya Synovate kikisisitiza kuwa kina matokeo ya utafiti uliofanywa na kampuni hiyo ya kupata matokeo yaliyotoa ushindi wa asilimia 45 kwa chama hicho na mgombea wake wa urais, Dkt. Willibrod Slaa.

Synovate hivi karibuni ilikanusha habari kuwa haijawahi kufanya utafiti wala kuficha matokeo hayo yaliyodaiwa kuipa CCM na mgombea wake Rais Jakaya Kikwete asilimia 41, huku ikitishia kulishtaki gazeti moja liliwakariri viongozi wa CHADEMA wakieleza utafiti huo.

Akizungumzia matokeo hayo jana, Dkt. Slaa alisema "Synovate wakimbie haraka mahakamani, tunazo document (nyaraka), hata gazeti lililotishiwa kushtakiwa lisiwe na wasiwasi, huu ni wakati wa kuvunja heshima ya Synovate kitaifa na kimataifa.

"Walifanya utafiti na katika swali namba GP 06 waliuliza, 'uchaguzi ukifanyika sasa hivi nani utampigia kura kuwa rais wa Tanzania?' na majina yote yaliweka pale ya wagombea, sasa wanakanusha nini, waende haraka sana mahakamani, vinginevyo credibility (heshima) yao tutaivuruga nchi nzima na kimataifa, alisema huku akionesha nyaraka hizo kwa mbali.

Dkt. Slaa alisema katika nchi nyingine taasisi za maoni zinakuwa huru, hazipendelei chama chochote kile.

Katika hatua nyingine, CHADEMA kimemshutumu serikali ya CCM inanyoongozwa na Rais Jakaya Kikwete kikidai kuwa imepanga kutumia mbinu chafu ili kuhujumu Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

Kimesema kuwa kinazo taarifa za uhakika kuwa kati ya mbinu hizo chafu ambazo zinatumiwa au zinataka kutumiwa na serikali kukibeba Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi wa mwaka huu ni kutoa maelekezo kwa Usalama wa Taifa na kujipanga kuchapisha karatasi bandia za kupigia kura nje ya nchi.

CHADEMA kimesema kuwa njama hizo ni aina ya ufisadi kwa kuwa zinahusisha matumizi mabaya ya madaraka na raslimali za nchi kukisaidia chama kimoja cha siasa-CCM, hivyo hazipaswi kuvumiliwa kwani zina lengo la kuingilia maamuzi ya wapiga kura na kuvuruga amani ya nchi.

Kimesema kuwa iwapo mbinu hizo chafu zitafanikiwa kwa kuharibu uchaguzi na kupanga matokeo ya kuipendelea CCM na mgombea wake wa urais, "Rais Kikwete ndiye atabeba lawama na laana zote juu ya yale yatakayotokea. Usalama wa Taifa wakanushe kama hawajapewa maelekezo na kama sasa hawazunguki mikoani."

Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibroad Slaa alipokuwa akizungumza na waandishi ambapo alisisitiza kuwa siku zote chama hicho kimekuwa kikisema kuwa amani ya nchi wakati wa uchaguzi imekuwa ikivurugwa na chama tawala kwa nia ya kutaka kung'ang'ania madaraka, kinyume na maamuzi ya Watanzania.

"Leo tumewaita kuzungumzia juu ya mambo matatu, maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA hasa juu ya ubunge wa viti maalumu, uchaguzi mkuu wa mwaka huu na suala la Synovate (kampuni inayojihusisha na kura za maoni ya watu)...juu ya uchaguzi mkuu tunazo taarifa za uhakika kuwa Serikali imetoa instructions (maelekezo) kwa Usalama wa Taifa na sasa wako mikoani wakizunguka nchi nzima, kuhakikisha Kikwete anashinda kwa hali yoyote ile.

"Tunajua mikoa ambayo wamekwisha kwenda mpaka sasa hivi na wanachofanya huko tunakijua...hii ni sawa na ile barua tuliyoikamata hivi karibuni ikiwaelekeza watendaji wa Serikali kuhakikisha CCM inashinda uchaguzi wa mwaka huu kwa hali na mali. Tunatoa angalizo mapema lolote litakalotokea mwaka huu Rais Kikwete atabeba lawama na laana zote za Watanzania.

"Kwa hali wanayoionesha ya kuhangaika mpaka sasa Kikwete ameshashindwa. Ni kigezo tosha kuwa mpaka sasa wameshashindwa uchaguzi. Tunapenda kumwambia kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni uchaguzi wa wananchi, hakuna cha Usalama wa Taifa, hakuna cha JWTZ wala FFU, waache wananchi wafanye maamuzi juu ya nchi yao," alisema Dkt. Slaa.

Dkt. Slaa ambaye pia ni Mgombea urais wa CHADEMA katika uchaguzi wa mwaka huu, lakini jana akitumia kofia yake ya ukatibu mkuu wa chama alisema kuwa wanazo pia taarifa za kina na za uhakika kuwa kuna karatasi za bandia zinachapishwa katika moja ya nchi za nje, ili zije zitumike wakati wa uchaguzi, akidai ni mwendelezo wa mbinu chafu za kuiba kura.

Alisema chama chake na Watanzania wengi wapenda haki hawatakubali mbinu hizo chafu, akisema matumizi mabaya ya madaraka na raslimali za nchi ni aina ya ufisadi ambao CHADEMA kimekuwa kikiupiga vita tangu kilipotangaza orodha ya aibu ya watu mafisadi wapato 11 nchini.

"Wanaonesha dhahiri kuelemewa...sasa wanafanya vitendo vya kuhatarisha amani ya nchi, hawaitakii mema nchi. Tunasema amani ikivunjika Kikwete atabeba lawama, hatuwezi kukubali udikteta na ubabe huu. Kutumia raslimali za serikali na matumizi mabaya ya madaraka ni aina ya ufisadi, ndiyo maana Kikwete tulimweka katika orodha ya mafisadi."

Akiongezea katika suala hilo, Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Bw. Freeman Mbowe alisema kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka huu ukivurugika, Rais Kikwete, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini watapaswa kuwajibika mbele ya Watanzania.

Bw. Mbowe alisema kuwa kuna vitendo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi hao kwa nia ya kubeba ushindi wa CCM vinaiweka matatani dhana nzima ya demokrasia na kuonekana kiini macho, hali ambayo haiwezi kukubalika.

"Tunapenda kutoa tahadhari kwa Rais Kikwete, kwa NEC na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, yaani kwa Makame (Jaji Lewis, Mwenyekiti wa NEC) na Tendwa (John, Msajili), watu hawa watatu ndiyo wenye mamlaka ya umma na wajibu wa kutoa haki, utulivu na amani katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

"Bahati mbaya sana watu hawa watatu wana mikakati ya kuchakachua kura badala ya kutenda haki, wanaliandaa taifa kuchakachua kura...tunatoa angalizo kwa jamii nzima na jumuiya ya kimataifa demokrasia nchi hii ni kiinimacho. Msajili kwa makusudi anabadilisha na kuvunja sheria iliyotungwa na bunge ili kumsaidia Kikwete, halafu hakuna mtu yeyote anayejali wala kuchukuliwa hatua...huu ni uwendawazimu.

"Jana Shinyanga Kikwete kahutubia mpaka saa 1, karibu kila mahali anazidisha muda...tunataka jamii nzima na jumuiya ya kimataifa ituelewe, hawa watu wameshindwa siasa za hoja, wameshindwa siasa za aina zote za maana sasa wanajiandaa kwa siasa za uchakachuaji...mwaka huu kitaeleweka, hapatatosha pale wananchi watakapoamua kulinda maamuzi na kura zao," alisema Bw. Mbowe.

Aliongeza kuwa chama hicho kitaandaa malalamiko ya kuwayawasilisha kwa NEC na Tendwa juu ya vitendo vya kuzidisha muda.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Bw. Salvatory Rweyemamu alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo jana, alisema hizi ni tuhuma za kisiasa na zinamhusu mgombea wa CCM, kwa hiyo aulizwe Meneja wa Kampeni wa chama hicho, Bw. Abdulrahaman Kinana.

Bw. Kinana hakupatikana kwenye simu yake ya mkononi ambayo mara kadhaa ilikuwa ikiita bila kupokewa.

Kuhusu suala la uteuzi wa majina ya wabunge wa viti maalumu wanawake ndani ya CHADEMA, Dkt. Slaa alijigamba kuwa chama chake kimeweka historia nchini kwa kuwa chama cha kwanza kutumia njia ya kisiasa na kisayansi kupata wabunge hao, huku akisema sheria ya uchaguzi inayolazimisha vyama vya siasa kuwasilisha majina hayo siku 30 kabla ya uchaguzi ni chanzo cha zoezi hilo kutofanyika kwa ufanisi mapema, hivyo watairekebisha wakipewa ridhaa ya kuongoza nchi.

"Njia ambayo consultant (mshauri) wetu atawaeleza vizuri imeondoa kabisa yale mawazo ya wabunge kutoka upande mmoja wa nchi, dhana ya mchezo mchafu mtu kumweka girlfriend wake, uswahiba na unafiki mwingine, hii ni kwa sababu CHADEMA tumedhamiria kuchukua dola na tunaenda kuchukua dola. Hivyo ilikuwa lazima tujipange vizuri kupata wabunge kutoka nchi nzima, maana hata katika majimbo tumesimamisha wabunge 185," alisema Dkt. Slaa.

Kwa upande wake mtaalamu mshauri aliyepewa kazi ya kuratibu utaratibu wa kuwapata wabunge wa viti maalumu, Dkt. Kitila Mkumbo alisema kuwa kwa uchanganuzi aliofanya kwa kutumia vigezo vya jumla kama vile umahiri, bidii, dhana ya uwakilishi wa wananchi kupitia wabunge wa viti maalumu na kila kanda kupata nafasi, itasaidia CHADEMA kupata wabunge makini kama ilivyokuwa katika bunge lililopita.

"Mbali ya vigezo hivyo vya jumla nilitumia vigezo vingine kwa sayansi ya takwimu ambavyo vilikuwa ni elimu, uzoefu wa uongozi kisiasa, uzoefu wa uongozi nje ya siasa, ugombea ubunge jimboni, mchango wa hali na mali katika shughuli za chama na kampeni zinazoendelea, umri katika chama, ambapo kila kigezo kilikuwa na sehemu ndogondogo tofauti ambavyo ndivyo tulitolea maksi.

"Kwa kweli kwa ukokotoaji wa vigezo hivyo CHADEMA imepata wabunge mchanganyiko wenye sifa mbalimbali kutoka karibu kila eneo la nchi katika kanda mbalimbali, kwa kweli ilikuwa lazima kuzingatia vigezo vingi kwani CHADEMA kinajiandaa kuunda serikali.

30 Aug 2010

Nimekutana na habari hii huko Jamii Forums,nami naiwasilisha kama ilivyo:

Dola kuishughulikia CHADEMA
DAWATI LA HATUDANGANYIKI limepokea taarifa za kuaminika kutoka vyanzo vyake kuwa kuwa mara tu baada ya mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, siku ya Jumamosi tarehe 28 Agosti 2010 wakuu wa Idara ya intelejensia walikutana na timu ya Kampeni ya CCM kwa ajili ya kutoa mlisho nyuma, na kupanga mikakati ya kuikabili CHADEMA, na yafuatayo yalijiri:-
a)Idara ililazimika kutolea ufafanuzi sababu zilizopelekea shauri wake wa kutaka matangazo ya TBC ya mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za CHADEMA kurejeshwa mara moja baada ya kukatizwa. Walieleza kuwa ilitokana na maelfu ya wananchi waliohudhuruia mkutano huo kuwa wa kwanza kugundua kukatishwa kwa matangazo hayo na kuamua wenyewe, bila ya kushawishiwa na kiongozi yeyote kuchukua hatua kali sana dhidi ya TBC. Viongozi wa CHADEMA walistukia tuu mkutano ukitaka kuvurugika kwa wananchi kudai vikali kurejeshwa kwa matangazo hayo. Ilielezwa kuwa kuvurugika kwa mkutano ikwa sababu ya kukatishwa kwa matangazo ya chombo cha umaa kama TBC iimeelezwa kuwa ingekuwa ni aibu kubwa kwa Serikali na TBC.
b)Idara ilitoa taarifa kuwa licha ya umati wa watu waliohudhuria kutofikia ule wa mkutano wa uzinduzi wa CCM, lakini kwa kuwa umati huo kila mtu alijinyanyua kutoka atokako na kuja Jangwani kwa ajili ya CHADEMA tofauti na maandalizi makubwa ya usafiri, fedha, burudani za kila aina, viburudisho n.k yaliyofanywa na CCM kuwafikisha watu kwa maelfu Jangwani. Hizo ni dalili mabaya na ni tishio kubwa kwa CCM. Na ikaamuliwa kuwa iandaliwe mikakati ya kuwakatisha tamma wananchi wenye mapenzi na CHADEMA.
Mkakati :- Ilamuliwa kuwa upandikizwe mgogoro baina ya viongozi wa CHADEMA na mgombea wake Dr W. Slaa; na kuwachonganisha na wapiga debe wao akina Marando, Shibuda, Mpendazoe n.k kwa nia ya kuwakatisha tamaa wenye mapenzi na CHADEMA na wote wanaotarajia kuwapigia kura wagombea wa CHADEMA.
Iliamualiwa kwa kuwa wananchi wanampenda sana Dr W Slaa, zisambazwe habari kuwa aelewani na Mwenyekiti wake Ndg Freeman Mbowe kwa sababu Dr Slaa sio kutoka kabila la wachagga. Ilikubaliwa kuwa taarifa hizo zianze kusambazwa wiki inayoanzia Jumatatu ya tarehe 30 Agosti 2010. Na tathmini ifanyike kujua mafanikio yake wakati zinatungwa mbinu mpya.
Iliamuliwa kuwa magazeti ya New Habari Corporation ikiwemo Mtanzania, Rai n.k yaanze kutumika kwa kazi hiyo wakati waandishi zaidi wa kufanya kzai hiyo wakitafutwa.
Ili wananchi wenye mapenzi mema na CHADEMA waweze kusadiki taarifa zitakazosambazwa ilikubaliwa kuwa magazeti yatakayotumika yaanze kwanza kwa kipindi kifupi kuandika habari njema kuhusu CHADEMA na wagombea wake; na baada ya mashabiki wake kuyaamini magazeti na vyombo hivyo vya habari ndipo kazi ya kuisamabaratisha CHADEMA ianze rasmi.
Ili kutekeleza mipango hiyo waandishi wa gazeti la Mtanzania walipatiwa maelekezo ya kurekebisha kichwa cha habari na maudhui ya habari za uzinduzi wa CHADEMA zilizochapishwa tarehe 29/8/2010, kwa lengo hilo.
Vyombo vya habari vya Serikali ya ikiwemo magazeti ya Daily News na Habari Leo na TBC na redio za TBC vilielekezwa kuanza mara moja kazi ya kuipamba CHADEMA kama chama na watu wa fujo mbele ya jamii makakati amabo unadaiwa kufanikiwa sana kuisambaratisha CUF mwaka 2005, wakati Mkuu wa chombo kimoja cha dola alipodai siku moja kabla ya upigaji kura wamekamata shehena ya majambia yenye rangi za bendera za CUF
c)Pingamzi la CHADEMA dhidi ya Jakaya Kikwete mkutano ulikubaliana kuwa kuaniza sasa idara ihakikishe kuwa inamgeuzia kibao Dr Slaa na kusambaza habari kwa wafanyakazi na umma kuwa DR Slaa anapinga wafanyakazi kuongezwa mishahara ndio maana CHADEMA inamuwekea pingamizi mgombe wa CCM Jakaya Kikwete kwa kitendo cha kuwaongezea mishahara watumishi wa umma katika kipindi hiki cha kampeni.
Dawati litaendelea kuwahabarisha!!!!!!!

If it's true,hivi hii sio local version yetu ya Watergate?

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.