22 Oct 2008


Viongozi wa dini waonya nchi inaelekaa pabaya
*Washauri Rais apunguze safari za nje

Na Waandishi Wetu

VIONGOZI wa dini wamesema kukithiri kwa migomo, maandamano, vitendo vya kikatili, na migogoro kati ya serikali na watumishi wa umma ni ishara tosha kwamba, mambo hayako sawa nchini.

Wakizungumza na Mwananchi nyakati tofauti jana, viongozi hao walisema hali hiyo inaipeleka nchi pabaya na kuitaka serikali kutafuta suluhisho la matatizo hayo haraka iwezekanavyo.

Walisema kuwa kinachotokea sasa ni matokeo ya ahadi zisizotekelezeka na kwamba njia pekee ni kuyashughulikia madai hayo ya wananchi.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Kanisa la Katoliki jijini Dar es Salaam, Mhashamu Methodius Kilaini alisema, iwapo hali hiyo haitashughulikiwa mapema itasababisha hali kuwa mbaya zaidi nchini.

Kauli hiyo imeungwa mkono na Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ramadhan Sanze aliyesema kuwa, ili kuondoa mitafaruku iliyopo nchini serikali lazima iwe tayari kuwajibika kwa jamii kisheria, kisiasa.

Aliishauri serikali kuyashirikisha makundi mbalimbali ya kijamii na kisiasa katika kupanga na kubuni sera mbalimbali kiutawala na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Sanze alimwomba Rais Jakaya Kikwete kupunguza safari za nje na hasa Marekani, akidai kuwa nchi hiyo si marafiki wazuri kwa ustawi wa taifa la Tanzania.

“Sidhani kama rais safari hizi za Marekani anapanga mwenyewe au anapangiwa, kama anapangiwa basi itifaki hii sio nzuri, hivyo tunamwomba apunguze safari za huko,” alisema Sheikh Sanze.

Alifafanua kuwa, ni vema kwa sasa rais akabakia nchini kuwatumikia Watanzania na kutuliza mitafaruku iliyopo badala ya kusafiri safiri tu huku nchi ikiwa inateketea kwa kuzongwa na migogoro ya kijamii.

Sheikh Sanze alionya kuwa, ikiwa hali itaendelea kama ilivyo sasa bila hatua madhubuti kuchukuliwa, basi kwa mara ya kwanza historia inaweza kubadilika kwa kuwa na rais wa kipindi kimoja.

Awali, Askofu Kilaini alisema ingawa tatizo la migomo linaonekana kuwa ni la miaka mingi, lakini ishara ya sasa inatia mashaka kwani serikali imekuwa ikitoa ahadi nyingi kwa wananchi na mambo machache tu ndiyo yanatekelezwa

“Hatuwezi tukasema kuwa mambo haya yanayoendelea kujiri ni ishara ya kukua kwa demokrasia, bali inatubidi tufahamu kuwa, serikali isipotekeleza ahadi zake kwa wananchi tutaendelea kushuhudia vitendo hivi kila mara.

Alisema uchumi wa dunia unapotikiswa, nchi zinazoendela ndizo zinazoathirika zaidi, hivyo ni vema serikali kupitia wizara zake ikatafuta mbinu zaidi za kuhakikisha kuwa suala la mfumuko wa bei unadhibitiwa ili mwananchi wa kawaida aweze kumudu maisha.

Alisema watu wanapochoka, na kukata tamaa na serikali yao, hutafuta njia nyingine kujinasua na matatizo yanayowakabili.

“ Ukizingatia kuwa suala la maandamano au migomo ni haki za msingi za wafanyakazi, hivyo kama serikali inataka kupunguza masuala haya ni vema ikabeba gharama na siyo kukwepa,” alisema Askofu Kilaini na kuongeza:

“Ninawaomba wananchi wenzangu watafute madai yao kwa kufanya mazungumzo na si kushiriki kwenye vurugu na migomo na pia serikali inapaswa kuwajibika kwa ahadi zake na si kuwayumbisha Watanzania.”

Hata hivyo, Askofu Kilaini alipoulizwa kwamba alishawahi kutamka kuwa Rais Jakaya Kikwete ni chaguo la Mungu na hivi sasa ana maoni gani, alisema kuwa kiongozi yeyote anayechaguliwa kwa ridhaa ya wananchi ni chaguo la Mungu.

“Ni vema nikaeleweka kuwa maandiko ya Mungu yanasema uongozi na mamlaka yote hutoka kwa Mungu, hivyo basi rais aliyechaguliwa kwa ridhaa ya wananchi wenyewe ndilo chaguo la Mungu na sisi tutaendelea kuwa na msimamo huo,” alisema Askofu Kilaini.

Alisema pamoja na kwamba Rais Kikwete ni chaguo la Mungu, anahitaji kusaidiwa katika kutekeleza sera na kutimiza ahadi zote zilizoahidiwa katika serikali yake, kwa sababu viongozi wengine wakimwachia na kushughulikia zaidi maisha yao binafsi, hakuna jambo litakalotekelezeka.

Aliwataka mawaziri na watendaji wengine serikalini wakawa mstari wa mbele kumshauri Rais mambo mema na si kumpotosha ili aweze kutekeleza.

Naye Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Salum Fereji na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT), Padri Charles Kitima walisema jana kwenye semina ya waandishi wa habari toka mikoa mbalimbali nchini inaendelea katika Hoteli ya Isamo mkoani hapa kuwa sera na sheria na madini vimetungwa kwa masilahi ya watu wachache walafi ambao wanajali masilahi yao na hivyo lazima vibadilishwe sambamba na mikataba yote ambayo makampuni ya wawekezaji yameingia katika uchimbaji wa madini hapa nchini.

Sheikh Ferej alisema ni lazima serikali kuamka kwa kuwa sasa nchi inaelekea pabaya kutokana na rasilimali muhimu kama madini kuachiwa watu toka nje ya nchi kuwaacha Watanzania kuendelea kuisha katika umaskini uliotopea.

"Ndugu zangu, sisi kama viongozi wa dini tulitembelea maeneo ya migodi yote, kule hali ni mbaya Watanzania wanaishi maisha ya dhiki, wamefukuzwa katika maeneo yao na watu toka nje ya nchi ndio wananufaika na madini haya kwa kupeleka kwao," alisema Sheikh Fereji.

Alisema wao kama viongozi wa dini wamebaini serikali imefanya makosa katika kuingia mikataba na wawekezaji toka nje ya nchi kwa sababu Watanzania hawanufaiki na madini hayo ambayo miaka michache ijayo yatakuwa yamekwisha na kuacha mashimo.

Naye Padri Kitima alisema bila serikali kufanyika marekebisho sheria na sera za madini Tanzania itaendelea kuwa maskini na siku zijazo yanaweza kukatokea mapigano kama ilivyo katika nchi nyingine barani Afrika ambapo kulikuwa na madini.

Alisema mikataba mingi ya wawekezaji ni mibaya na inatakiwa irekebishwe, lakini inavyoonekana hakuna wa kubadilisha hadi vyombo vya habari na wananchi washikamane na kudai mikataba hiyo ivunjwe au kurekebishwa.

Padri Kitima alisema katika mazingira ya sasa angependa yafanyike mabadiliko makubwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake kabla ya mwaka 2010 na kuwa na kundi la wafuasi wa Nyerere ambao watatetea rasilimali za nchi hii.

"Mimi binafsi kwa hali ilivyo ningependa CCM igawanyike najua kuna watu wazuri ndani ya CCM, lakini wanashindwa kuifanya nchi hii kuwa mikononi mwa Watanzania badala yake kundi la watu wabinafsi ndilo lina nguvu na hata katika kambi ya upinzani kuna matatizo makubwa ya ubinafsi na kuwepo viongozi wasio na sifa," alisema Padri Kitima.

Alisema nchi imepoteza agenda muhimu alizoziacha hayati Mwalimu Julius Nyerere alipounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sasa ubinafsi umetawala hadi kutishia kuvunja Muungano.

CHANZO: Mwananchi


Na Hilary Komba 

WATANZANIA Bara hawawezi kulazimika kuingia Zanzibar kwa pasipoti kutokana na sheria ya uraia kukataza utaratibu huo ndani ya Jamhuri moja. 

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Naibu Kamishina wa Uhamiaji, Wizara ya Mambo ya Ndani Bw. Abdi Ijimbo, wakati akizungumza na Majira kuhusu hoja zilizoripotiwa na vyombo vya habari hivi karibuni, vikiwanukuu baadhi ya watu wakisema ni vyema Watanzania Bara waingie Zanzibar kwa pasipoti. 

Bw. Ijimbo alisema sheria za Uhamiaji zinaruhusu Mtanzania anayetaka kutoka nje ya nchi kuwa na pasipoti, ili ajulikane kuwa ni Mtanzania aliyefuata taratibu ambazo zipo duniani kote. 

"Hadi sasa Serikali haina sababu ya kuanzisha pasipoti kuingia Zanzibar, kwa vile hakuna sheria inayosema hivyo na Zanzibar ipo katika Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, ndiyo maana hata huko nyuma hati ya kuingilia Zanzibar ilifutwa," alisema. 

Bw. Ijimbo aliongeza kuwa katika Serikali ya Awamu ya Pili, Watanzania Bara walikuwa wanaingia Zanzibar kwa hati ambayo ilikuwa pia haina hadhi ya pasipoti, bali ulikuwa ni utaratibu fulani tu uliowekwa na baadaye kuonekana hauna sababu ya kuendelea kuwapo. 

Alisema anashangaa kuona baadhi ya Watanzania wanazungumzia jambo hilo ndani ya nchi zilizoungana na kuwa kwenye Jamhuri ya Muungano. 

Nayo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imesisitiza kwamba vitambulisho vinavyotolewa vya Mzanzibari mkazi ni kwa wale tu wanaoishi visiwani humo, anaripoti Ali Suleiman. 

SMZ imesema Watanzania kutoka Bara wataweza kutambuliwa kwa vitambulisho hivyo, baada ya kutimiza masharti yaliyopo. 

Imesema vitambulisho hivyo havina malengo ya kisiasa kama inavyodaiwa na baadhi ya watu kwamba ni mikakati ya CCM kushinda katika uchaguzi mkuu ujao. 

Akitoa juzi majumuisho ya mjadala wa sera ya vitambulisho vya Mzanzibari, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya Serikali Zanzibar, Bw. Suleiman Othman Nyanga, alisema Zanzibar haiwezi kutoa vitambulisho vya uraia kwani yenye mamlaka ya kufanya hivyo ni Serikali ya Muungano. 

Alisema sera iliyoandaliwa ni ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi na si ya vitambulisho vya Mzanzibari. 

“Mheshimiwa Spika ni vyema kutambua kuwa hii sera ni ya vitambulisho vya Mzanzibari kwa sababu michango mingi iliyotolewa, imezungumzia suala la Mzanzibari, lakini hapa tunasema ni sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi kwa sababu Mzanzibari tunayetaka kumpa kitambulisho ni yule ambaye anakaa Zanzibar,” alisema Waziri huyo. 

Waziri Nyanga alisisitiza, kwamba vitambulisho hivyo hatapewa Mzanzibari anayekaa nje ya visiwa hata kama anakaa Dar es Salaam, lakini ikiwa si mkazi, hatakuwa na halali ya kupata kitambulisho hicho, ambacho ni kwa ajili ya Wazanzibari wanaoishi Unguja na Pemba. 

“Tunayemsema sisi hapa ni Mzanzibari mkazi ndiye tutakayempa kitambulisho, kama anakaa Dar es Salaam maadam si mkazi yeye hahusiki na kitambulisho hiki cha sera hii, ambayo tunataka kuipitisha,” alisema. 

Waziri huyo alisema SMZ haitatoa vitambulisho vya uraia kwa sababu suala hilo ni la Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hata Rais wa kwanza wa Zanzibar, marehemu Abeid Amaan Karume alitoa vitambulisho vya uraia kwa Zanzibar. 

“Wakati huo vitambulisho kweli vilitolewa na viliitwa pasi ya uraia iliyotolewa wakati huo na kwa kuwa kuna neno uraia, na uraia kwa Tanzania ni mmoja, kwa hivyo vitambulisho hivyo kama utavitazama vitakuwa vimeandikwa pasi ya uraia na vimeandikwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Zanzibar ... haikuwa pasi ya uraia ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,” alisema. 

Alisema watakaopaswa kupewa vitambulisho ni wale walioamua kuwa wakazi wa Zanzibar, ambao watakuwa na makazi yao ya kudumu na watakuwa wanahitaji huduma za kila siku za Serikali ambao takwimu zao zitasaidia kupanga mipango ya maendeleo ya visiwa vya Unguja na Pemba. 

Hata hivyo, Waziri Nyanga alisema Mzanzibari yeyote anayeishi nje ya Zanzibar anapoamua kurudi Zanzibar, basi ana haki ya kuomba kitambulisho na atapewa baada ya kuthibitisha kuwa na sifa zinazohitajika. 

“Kwa hiyo akiweza kuthibitisha sifa zilizotajwa, atapewa vitambulisho ingawa wengine walitoa maoni kwamba vielezwe kuwa ni vitambulisho vya uraia kwa kuwa suala la uraia ni la Jamhuri ya Muungano na hakuna raia wa Zanzibar, kwa hiyo vitambulisho hivi vitakuwa bado ni vya Mzanzibari mkazi na si vitambulisho vya uraia wa Zanzibar," alisema. 

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walipitisha sera ya vitambulisho vya ukazi vya Zanzibar, hatua ambayo itasaidia kuweka kumbukumbu na kusaidia takwimu za nchi katika maendeleo.

CHANZO: Majira

21 Oct 2008

Albino Girl Killed For Witchcraft
Tuesday, October 21 02:52 pm
Sky News
A gang murdered and mutilated a 10-year-old albino girl in Tanzania - because they wanted to sell her body parts to witch doctors. Skip related content

Esther Charles was killed in Shilela in the western region of the African country on Sunday.

She died just hours after President Jakaya Kikwete called for a crackdown on gangs, saying the killing of albinos has "stained the country's good image".

At least 26 other albinos, mostly women and children, have been killed in different parts of the east African country over the past year.

Albinos lack melanin pigment in the skin, eyes and hair, which protects from the sun's ultraviolet rays.

But witch doctors believe they have magical powers to bring fortune, and discrimination against albinos is rife across sub-Saharan Africa.

In 2007, police in Tanzania reported several cases of people digging up the bodies of children to remove organs, in many cases the genitals and eyes, to make potions used in rituals.

Shilela councillor Joseph Manyara told a rally organised by the Tanzania Albino Society (TAS): "It is utterly stupid for some people to believe that albinos have magic powers and their parts can make them rich.

"People should be provided with education to understand that it is only through hard working that they can prosper in life and not through selling albinos' body parts."

Police said they have arrested 47 people suspected to be involved in the killings this year.

But TAS chairman Ernest Kimaya blasted authorities over the speed at which the murders were solved.

He said: "We are yet to witness any convictions and incidents of the murder of albinos are on the rise."

There are about 150,000 albinos in the country, and more than 8,000 of them are registered with the TAS.

Some families kill albino babies upon birth, Tanzanian authorities say.

And authorities in Kenya and Burundi, where albino killings have also been reported in recent months, have started to give added protection.

Some reports say albino skin is prized in the Democratic Republic of Congo, another troubled African nation where superstition is high.

SOURCE: Sky News


BAADHI ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamepinga sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi na kusema suala hilo linafanywa zaidi kisiasa na kutaka kurudishwa kwa hati ya kusafiri kati ya Tanzania Bara na Zanzibar ambayo iliondoshwa mwaka 1995. 

Hayo yalisemwa jana na Waziri Kivuli Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Bw. Abdalla Juma, wakati akisoma maoni ya kambi ya upinzani katika suala la sera ya vitambulisho vya Mzanzibari mkazi. 

Alisema haiwezekani Wazanzibari kuitwa wakazi katika nchi yao na kuongeza kwamba vitambulisho hivyo havifai. 

"Vitambulisho hivi kwa kweli havifai, sera hii haifai isipitishwe, kwa sababu inaonekana wazi kuwadhalilisha Wazanzibari katika nchi yao," alisema Bw. Abdalla. 

Wajumbe wengine wa Baraza walitaka kurudishwa kwa utaratibu wa zamani wa kuwapo hati za usafiri wakati wa kuingia katika visiwa vya Unguja na Pemba. 

Mwakilishi wa Magomeni, Bw. Salmin Awadh, alitaka kurudishwa kwa hati za usafiri na kusema kuondoshwa kwake kwa kiasi kikubwa kumesababisha kasi ya ujambazi na uhalifu. 

"Tunataka kurudishwa kwa hati za usafiri kati ya Zanzibar na Tanzania Bara...tunataka kuwepo kwa udhibiti katika eneo la bandari pamoja na uwanja wa ndege'alisema Awadh. 

awadh alisema sera ya vitambulisho vya uzanzibari ukazi lengo lake ni ulinzi kwa wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba na kuweza kuwatambuwa hasa Wazanzibari na wageni. 

mwakilishi wa viti maalumu kutoka katika chama cha wananchi CUF Zakia Omar naye alitaka kurudishwa kwa utaratibu huo ambao alisema ulisaidia sana kudhibiti vitendo vya uhalifu. 

alisema kuondoshwa kwa hati za kusafiria kati ya Tanzania Bara na Zanzibar kwa kiasi kikubwa kumerudisha wimbi la vitendo vya uhalifu. 

hati ya kusafiri kati ya Tazania Bara na Zanzibar pasipoti iliondolewa katika miaka ya 1995,baada ya kubainika kuwepo kwa vikwazo vya usafiri katika nchi moja ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na kuonekana kwenda kinyume na katiba
.

CHANZO: Majira

20 Oct 2008


Now you will need a passport to buy a mobile phone under 'Big Brother' style scheme

Anyone buying a mobile phone could be forced to produce their passport as part of the plan for a huge surveillance database. 

Security chiefs want a national register of all 72million mobile phone users in the UK to help track terror plots or crime networks. 

Customers can currently buy prepaid mobile phones with cash, without providing personal details. 

There are some 40 million prepaid and unregistered mobile phones in Britain. 

Opponents claim determined terrorists or criminals will find it easy to sidestep the database by using foreign-registered mobile or satellite phones. 

The phone database will form part of a surveillance system proposed in the Communications Data Bill, unveiled by Home Secretary Jacqui Smith last week. 

It includes plans to log and store details of every phone call, email, text message and internet visit in Britain - including websites such as Facebook and eBay. 

A spokesman for Information Commissioner Richard Thomas said: 'We would expect that this information would be included in the database proposed in the draft Bill.'

SOURCE: Daily Mail

19 Oct 2008






CLICK HERE to read the story

18 Oct 2008

Wanafunzi 5,300 na wahadhiri wao zaidi ya 100 wa Chuo Kikuu cha Dodoma, wameanza mgomo usio na ukomo wakishinikiza uongozi wa chuo hicho kuwalipa stahili zao mbalimbali.Wanafunzi hao walikuwa wamebeba mabango mbalimbali yenye ujumbe wa kumtaka Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Shabani Mlacha, kujiuzulu kwa madai kuwa ndiye kikwazo. 

Pia walikuwa wakiimba nyimbo za kuhamasisha mshikamano huku wakimtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwenda chuoni hapo kuwasikiliza. 

Askari Polisi wakiwa kwenye magari walikuwa pembeni ya wanafunzi hao wakiwa tayari kupambana na wanafunzi hao kama wangefanya fujo hivyo kusababisha uvunjifu wa amani chuoni hapo. 

Hata hivyo, polisi hao walijikuta hawana kazi ya kufanya kwani hakukuwa na hali yoyote ya uvunjifu wa amani na wanafunzi hao walionekana kuwa watulivu wakati wote wa kuimba nyimbo zao. 

Katika mgomo huo ulioanza jana, wanafunzi hao wanalalamikia uhaba wa malazi kwa madai kuwa wanachangia Sh. 500 kila siku, lakini baadhi yao wanalala kwenye nyumba za kulala wageni na wengine wakilazimika kulala kwenye chumba kimoja watu wanne. 

Akizungumzia mgomo huo, Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo hicho, Malimi Joramu, alisema sababu nyingine ni uongozi wa chuo hicho kuwatoza wanafunzi Sh. 100,000 kama gharama za matibabu kwa miaka mitatu. 

Alisema malalamiko yao yapo upande wa wanafunzi ambao ni watumishi wa umma ambao hulazimika kuchangia gharama hizo kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, lakini uongozi wa chuo umewataka wote kulipia gharama hizo bila kujali ni mtumishi wa umma au la. 

``Tulishakubaliana na Uongozi wa Chuo mwaka jana kuwa wanafunzi hao wasichangie gharama hizo na wale waliokwisha changia warudishiwe gharama zao, lakini tumeshangaa kwa wanafunzi wa mwaka huu, gharama hizo zimerudishwa tena na wale waliorudishiwa fedha zao, wametakiwa kurudisha gharama hizo,`` alisema Rais huyo. 

Madai mengine alisema ni pamoja na Uongozi wa Chuo kuweka muda mfupi wa usajili wa wanafunzi, ambapo chuo hicho kimetangaza kwamba jana ndiyo mwisho na wale ambao watakuwa hawajajisajiliwa, Chuo hicho hakitawatambua. 

Rais huyo anadai kuwa, muda huo ni mfupi mno ukilinganisha kuwa wanafunzi wengi wanaosoma chuoni hapo wanatoka katika familia maskini na hata walipouomba uongozi wa chuo kuwaongezea muda, ulikataa kufanya hivyo na kushikilia msimamo wake wa kuwafukuza. 

``Tunajiuliza hivi iweje mafisadi wa EPA ambao ni wezi wameongezewa muda wa kulipa fedha walizoiba, sisi ambao ni wanafunzi na tunatoka kwenye familia maskini tunakataliwa kuongezewa muda hata wa mwezi mmoja tu, hii sio haki kabisa,`` alilalamika Joramu. 

Kwa upande wa wahadhiri wa chuo hicho, wao wanadai kutolipwa posho ya kujikimu ya wiki moja ya kuripoti chuoni hapo pamoja na fedha za uhamisho kwa baadhi ya wahadhiri. 

Wengine wamedai hawajalipwa mishahara yao ya mwezi uliopita hali inayowafanya waishi maisha ya kuombaomba, hasa kutokana makali ya maisha kupanda. 

Wahadhiri hao wanaokadiriwa kupita 100, wamegoma kuingia madarasani wakishinikiza kulipwa posho hizo, pamoja na mishahara yao na ikiwa ni vinginevyo, mgomo huo hautakuwa na ukomo. 

Akijibu tuhuma za wanafunzi, Profesa Mlacha alisema gharama za malazi wanazolipia wanafunzi hao, zimepunguzwa kutoka shilingi 700 kwa siku mwaka jana, hadi kufikia Sh. 500 mwaka huu. 

Alisema sababu za kupunguza gharama hizo ni malalamiko ya wanafunzi hao wakidai kuwa ni kubwa na wazazi wao wanashindwa kumudu kulipa. 

``Kutoka na hali halisi ya maisha, tuliwaelewa na tukaamua kushusha hadi kufikia Sh. 500, lakini pamoja na kushusha huko, bado baadhi yao wanaendelea kulalamika kuwa gharama hizo ni kubwa,`` alisema. 

Hata hivyo, Profesa Mlacha alisema chuo hicho kina malazi ya kutosha na kila chumba wanalala wanafunzi wanne kutokana na ukubwa wa vyumba hivyo, kwa kuwa kila mwanafunzi ana kitanda chake. 

Alisema hivi sasa kuna vitanda na magodoro zaidi ya 1,000 ambayo hayajalaliwa na wanafunzi kutokana na wengi wao kuwa hawajaripoti chuoni hapo hadi sasa na kushangazwa na malalamiko ya wanafunzi ambayo aliyaita kuwa ni ya uzushi. 

Kwa upande wa malipo ya matibabu alisema, chuo hicho kilikutana na watendaji wa Mfuko wa Bima ya Afya na kuzungumza nao kuangalia utaratibu wa matibabu ambapo walibaini kuwa, kuna baadhi ya magonjwa ambayo mfuko huo hauyalipii. 

Kuhusu madai ya usajili alisema, hizo ni sheria za chuo kwamba mwanafunzi ambaye hajasajiliwa na chuo, hatambuliki kama ni mwanafunzi. 

``Tangu siku ya kwanza ya mwanafunzi kupata barua ya kuitwa chuoni, anaorodhoshwewa mahitaji yote anayotakiwa kuja nayo, sasa iweje mwanafunzi aje shuleni akiwa hana fedha hata nusu ya gharama hizo, chuo hakitakubali hata kidogo kumsajili mwanafunzi ambaye hajalipa hata nusu ya gharama zinazohitajika,`` alisisitiza. 

Akijibu malalamiko ya wahadhiri, Profesa Mlacha alisema sheria iliyokuwa ikitaka wahadhari hao kulipwa posho hiyo imefutwa, lakini hata hivyo, chuo hicho kimetumia busara ya kuwaombea fedha hizo serikalini na taratibu hizo zilikuwa zinaendelea. 

Hata hivyo, alisema pamoja na kwamba asilimia 80 ya walimu hao hawana sifa za kulipiwa gharama za malazi na chuo, chuo hicho kimejitahidi kuwapatia nyumba ambazo zina kila kitu na kwamba hakuna mhadhiri anayekaa kwenye nyumba za kulala wageni. 

``Wahadhiri hao nao wametufikisha mahali ambapo tunashangaa, mwaka jana tuliwalipa, lakini kutokana na sheria hiyo kufutwa bado tukatumia ubinadamu wa kuwaombea fedha hizo serikalini, lakini wakati suala hilo likishughulikiwa tunashangaa nao wanagoma, chuo hakielewi nia yao ni nini,`` alihoji Prof. Mlacha. 

Aidha, Profesa Mlacha alisema, uchunguzi wa chuo hicho umebaini kuwa, wapo wahadhiri wachache wanaojifanya wanazijua siasa au wanataka kutumia chuo hicho kujifunza siasa. 

``Tumebaini wahadhiri hao ndiyo walioshinikiza mgomo huu, inawezekana wanajifunza siasa ndani ya chuo hiki, lakini tunawaeleza kuwa, hiki sio chuo cha siasa na kama wanataka siasa waende kwenye vyama vya siasa kuonyesha uwezo wao wa kujua siasa,`` alisema Profesa Mlacha. 

Hadi mwandishi wa habari hizi anaondoka eneo la chuo hicho bado wanafunzi hao walikuwa wakiendelea na mgomo wao.

CHANZO: Nipashe









Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.