Showing posts with label MIGOMO. Show all posts
Showing posts with label MIGOMO. Show all posts

2 Feb 2012


Tumeuona wa madaktari, lakini mingi yaja

NI sababu zipi zinazomsukuma mwanafunzi kuchagua mchepuo fulani wa masomo anapopewa nafasi ya kufanya hivyo?
Pengine kwa wanafunzi wengi sababu ya msingi ni jinsi mchepuo huo unavyoweza kupelekea kufikia malengo ya taaluma au ajira tarajiwa.
Lakini kwa wengine, sababu inaweza kuwa uwezo wao kimasomo, yaani kama wanaweza kumudu mchepuo husika au la. Binafsi, nilikuwa na ndoto za kuwa tabibu (daktari). Nilipokuwa kidato cha kwanza hadi cha nne niliwekeza nguvu kubwa kwenye masomo ya elimu ya viumbe na kemia. Na niliyamudu vema masomo hayo ambayo niliamini yangeweza kufanikisha dhamira yangu ya kuwa tabibu.
Hata hivyo, ndoto yangu ilipata pigo kubwa baada ya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne, ambapo japo nilipata alama A katika kemia na C katika baiolojia, nilifeli katika fizikia kwa kupata alama F, huku nikaambulia D kwenye hisabati.
Kwa maana hiyo, japo nilipata daraja la kwanza na kuchaguliwa kuingia kidato cha tano, uwezekano wa kusoma mchepuo “wa udaktari” wa PCB (Fizikia, Kemia na Baiolojia) ulikuwa hafifu.
Kabla ya kuanza masomo ya kidato cha tano nilipewa ushauri kuwa licha ya kushindikana kuchukua mchepuo wa PCB kuna uwezekano wa kuchukua mchepuo mwingine (unaoikwepa fizikia) wa CBG unaojumuisha Kemia, Baiolojia na Jiografia.
Lakini katika kile nilichokitafsiri kama haikuwa majaliwa yangu kuwa tabibu, licha ya shule kuwa na uhaba wa mwalimu wa jiografia nilipoangalia mtaala wa kemia niligundua ina mada kadhaa zilizojumuisha hisabati na maeneo mengine yenye ugumu kama wa fizikia, hususan katika physical chemistry.
Kufupisha maelezo, nilifikia uamuzi wa kuchukua mchepuo wa HGL (Historia, Jiografia na Lugha ya Kiingereza), ambao niliumudu na miaka kadhaa baadaye ulinisaidia kuchukua michepuo ya Elimu ya Jamii (Sosholojia) na Stadi za Siasa katika ngazi ya chuo kikuu.
Miongoni mwa mada za mwanzo kabisa za Elimu ya Jamii kuna mada ya kanuni za sosholojia (sociological theories).Na moja ya kanuni hizo ni ile inayoiangalia jamii kama mfumo kulingana na kazi za kanuni, desturi, mila na vikundi katika jamii. Kanuni hiyo ijulikanayo kama functionalism inaviangalia vipengele hivyo kama namna mwili unavyofanya kazi kwa ushirikiano wa viungo mbalimbali. Katika miili yetu, moyo unaletewa damu na mapafu na mapafu yanategemea damu inayosukumwa kwake na moyo.
Kadhalika, mfumo wa fahamu unaletewa ujumbe na viungo kama macho, ngozi, pua, nk lakini ili viungo hivyo viweze kupelekea ujumbe husika vinategemea ufanisi wa ubongo.
Kwa kifupi, ni vigumu-na pengine haiwezekani kabisa-kudai kiungo fulani katika mwili ni muhimu zaidi ya kingine. Vyote ni muhimu na kila kimoja kinakitegemea kingine katika utendaji kazi wake. Ni ushirikiano wa viungo mbalimbali ulikuwezesha wewe msomaji kuwa unasoma makala hii muda huu. Macho yaliona gazeti kwa muuzaji na kupelekea ujumbe kwenye ubongo ambako maamuzi yalifanyika ulinunue. Ubongo pia ulitumia maelekezo kwa mkono kutoa fedha mahali ilipowekwa (baada ya kukumbuka mahali husika), sambamba na kutofautisha kati ya fedha (ya kunulia gazeti) na funguo za ofisini au nyumbani.
Na pengine muda huu unatabasamu kwa ‘kukumbushwa jinsi mwili unavyofanya kazi na ufanisi wa ushirikiano wa viungo mbalimbali’, tabasamu hilo ni ushirikiano wa viungo mbalimbali mwilini.
Pengine hadi kufikia hapa nimekuchanganya na huelewi makala hii inaelekea wapi. Lengo la makala hii ni kuzungumzia mgogoro unaoendelea kati ya madaktari na serikali huko nyumbani.
Hadi wakati ninaandika makala hii, kulikuwa na taarifa kwamba mgomo huo unaelekea kusambaa katika hospitali mbalimbali. Kadhalika, kuna taarifa kwamba manesi nao wametoa tishio la kugoma iwapo serikali haitayapatia ufumbuzi matatizo ya madaktari yaliyosababisha mgomo huo.
Inawezekana wakati unasoma makala hii mgomo huo utakuwa umeshamalizika lakini kuna kila dalili kuwa hata kama madaktari watamaliza mgomo wao au/na manesi hawatogoma, kitakachokuwa kimemalizwa ni dalili tu za tatizo na wala si kupatikana kwa tiba yake.
Nilipotoa maelezo ya kanuni ya functionalism kwenye Sosholojia nililenga kuonyesha jinsi taaluma/ajira mbalimbali katika jamii zilivyo na umuhimu sawa na jinsi ushirikiano kati ya fani ya taaluma/ajira hizo unavyoleta ufanisi kwa manufaa ya jamii husika.
Je, wabunge ambao taarifa zinaeleza kuwa wameongezewa posho kutoka shilingi 75,000 kwa siku ni muhimu zaidi kuliko madaktari? Jibu la wazi ni hapana, kama ambavyo madaktari si muhimu zaidi ya walimu au viongozi wa dini si muhimu zaidi ya wanausalama.
Wote hawa ni muhimu kwa jamii na kwa namna moja au nyingine, ushirikiano wao (wa moja kwa moja au vinginevyo) ndio unaotuwezesha Watanzania kuwa hai.
Labda nifafanue. Ili tuwe salama, tunawategemea wanausalama. Lakini ili wanausalama waweze kutimiza majukumu yao ipasavyo wanapaswa kuwa na afya salama pia, na hapo unaona umuhimu wa watumishi wa afya (madaktari, manesi, nk).
Lakini ili mtu awe daktari au nesi ni lazima afundishwe, na hapo tunaona umuhimu wa walimu. Lakini mwalimu nae akiugua ni lazima aende kwa daktari. Hata hivyo, ili daktari aweze kufanya kazi zake ipasavyo ni lazima mazingira ya hospitali (na nchi kwa ujumla) yawe salama, na hapo tunarejea kwenye umuhimu wa wanausalama wetu.
Kadhalika, ingekuwa vurugu isiyoelezeka kama kila daktari, mwalimu, mwanausalama, nk angeenda bungeni kuwakilisha maslahi ya jamii yake au kuwa waziri au kiongozi serikalini. Na ndiyo maana licha ya kuepusha vurugu ya aina hiyo na pengine kuepusha uhaba wa wanataaluma kwenye fani husika, unakuwa na mtu mmoja kama waziri au mbunge mwenye jukumu la kuongoza na kuwakilisha makundi mbalimbali katika jamii.
Lakini viongozi au wawakilishi hao si muhimu zaidi ya wanaowaongoza au kuwawakilisha. Waziri hawezi kabisa kutimiza wajibu wake iwapo yeye mwenyewe ni mgonjwa na hakuna daktari wa kumtibu, au kuwa na wasaidizi ambao hawajatia mguu shuleni kwa vile hakuna walimu. Kadhalika, ili waziri atie mguu ofisini sharti nchi iwe salama, na hapo anatambua umuhimu wa wanausalama.
Kwa wabunge wetu pia, kuwa kwao bungeni kunategemea sana taaluma na nyanja nyingine katika jamii, achilia mbali nani waliowapigia kura kuingia bungeni. Japo picha inayojengeka baada ya ongezeko la posho za wabunge ni kama wapo kwa maslahi yao binafsi, ukweli unabaki kuwa hawawezi kuwa wawakilishi wa hewa. Wanawakilisha wananchi ambao wanaojumuisha watu wenye taaluma na majukumu mbalimbali katika jamii.
Kama daktari ni muhimu kama mbunge, kwanini basi kundi hili dogo (lakini linalosaka kila aina ya nguvu katika jamii ikiwa ni pamoja na kuitwa ‘waheshimiwa’) lipendelewe kwa marupurupu yasiyoendana kabisa na hali ngumu ya uchumi wetu? Kama waheshimiwa wabunge ni muhimu kama madaktari, manesi, walimu na watumishi wengine, kwanini basi wapewe shilingi 200,000 kwa siku huku watumishi wengine wakiwa na mahitaji lukuki ambayo yamekuwa yakipuuzwa na serikali?
Hivi kuwaongezea posho wabunge kutasaidiaje afya za Watanzania? Je, ongezeko hilo la posho litasaidiaje kuinusuru sekta ya elimu inayokwazwa na mishahara kiduchu ya walimu, uhaba wa nyumba na vitendea kazi huku wanafunzi wakisoma katika mazingira magumu?
Je, ni vipi ongezeko hilo la posho za wabunge litawasaidia askari polisi kuepuka vishawishi vya rushwa ambavyo kwa kiasi kikubwa vinachangiwa na maslahi duni?
Lakini tatizo kubwa zaidi linalosababishwa na ongezeko la posho za wabunge ni hili: kama serikali ina uwezo wa kutoa nyongeza ya posho kwa wabunge inamaanisha kuwa fedha si tatizo kwake.
Ninaandika hivi kwa sababu sidhani kama kuna mtu yeyote (ukiondoa wabunge wetu) anaamini kuwa maslahi ya wabunge wetu ni duni. Hatujawahi kusikia kuna mbunge ametishia kujiuzulu au kugoma kwa vile kipato chake cha mamilioni hakitoshelezi mahitaji yake, na wala hakuna mbunge aliyekonda kwa vile mshahara wake haumwezeshi kumudu gharama za chakula. Sana sana tunashuhudia vitambi vya baadhi ya waheshimiwa wetu vikizidi kuongezeka sambamba na kasi ileile ya malalamiko kuwa “maslahi ya wabunge ni duni.”
Hakuna anayependa kuona madaktari wakigoma hasa kwa vile wahanga wakubwa wa migomo ya aina hiyo ni walalahoi wasioweza kwenda India (au kwingineko) kupata matibabu. Na tungependa sana kuiunga mkono serikali katika maelezo yake ya kila siku kuwa haina fedha za kuboresha maslahi ya watumishi wake lakini tutaonekana wendawazimu tukifanya hivyo wakati serikali hiyohiyo inayodai iko hoi kifedha inamudu matumizi makubwa yasiyo ya lazima kwa kuwaongezea posho wabunge.
Sipendi kubashiri hili lakini kuna uwezekano mgomo wa madaktari ni mwanzo tu wa mlolongo wa migomo mingine ya watumishi katika sekta mbalimbali za umma huko mbele. Japo sina hakika serikali itamudu vipi mzigo wa posho za wabunge, kilicho wazi ni kwamba kelele za makundi mbalimbali ya jamii pamoja na wananchi kwa ujumla kupinga ongezeko hilo la posho kimepuuzwa na serikali, na kwa kuzingatia uzoefu itakuwa miujiza kama serikali itabadilisha uamuzi huo usiozingatia hali halisi ya nchi yetu (hasa kwa vile ilikuwa na fursa ya kukataa maombi ya wabunge lakini ikaamua kuyaendekeza).
Nihitimishe makala hii kwa kuitahadharisha serikali kuwa ‘imefungua kopo la minyoo’ kwa kutoa nyongeza ya posho kwa wabunge katika kipindi ambacho watumishi wa sekta mbalimbali za umma wanaelekea kuishiwa na uvumilivu wa kusubiri ahadi hewa za kuboreshewa maslahi yao.
Wakati nyongeza hiyo ya posho kwa wabunge inaweza kuwaongezea nguvu ya kuiunga mkono serikali (hata pale maslahi ya wanaowakilishwa na wabunge hao yanapowekwa shakani) hali itakuwa mbaya pindi harakati za watumishi wa umma kudai maslahi bora zinatakapomaanisha migomo zaidi.



21 Nov 2008


Asema viongozi wanakumbatia matajiri, nchi inahitaji maadili mapya ya viongozi

Na Ramadhan Semtawa

WAZIRI MKUU mstaafu, Jaji Joseph Warioba, ameonya kuwa iwapo hali ilivyo sasa nchini ikiachiwa iendelee kama ilivyo, amani, umoja na utulivu vitatoweka.

Kauli ya Jaji Warioba ambaye anaheshimika kutokana na maono yake ya mara kwa mara kuhusu mwelekeo wa nchi, imekuja wakati nchi inakabiliwa na tatizo la ufisadi na migomo kutoka kwa makundi mbalimbali ya jamii.

Huku akichambua nchi ilikotoka, ilipo na inakoelekea, Jaji Warioba alionya jijini Dar es Salaam jana kwamba, hakuna tena sera ya kujitegemea bali msingi wa maendeleo ni fedha, huku utu ukitoweka kwa kasi kubwa na kwamba, hali hiyo imeibuka zaidi baada ya kuvunjwa Azimio la Arusha visiwani Zanzibar mwaka 1990.

Jaji Warioba alisema kuvunjwa kwa Azimio la Arusha kumeivuruga nchi na kutaka ifanyike tathimini ya kuunda azimio jipya ambalo litaweka miiko ya uongozi, kwani sasa nchi iko katika hali ngumu.

Akionyesha jinsi mfumo wa uongozi wa nchi ulivyovurugika baada ya kuvunjwa azimio hilo la mwaka 1967 na kuundwa Azimio la Zanzibar, alisema viongozi badala ya kuangalia wananchi wa kawaida, huamua kukumbatia matajiri na wafadhili ili waendelee kuwepo madarakani.

"Hata ukiangalia huo mfumo wa uwakilishi wa uwiano, badala ya watu kukaa na kujadili namna bora ya kufanikisha mfumo huo, kinachoonekana ni watu kutaka kuzidi kukaa katika madaraka wakifikiri majimbo ni yao," alionya.

Waziri Mkuu huyo mstaafu, alisema mbali ya kukumbatia matajiri, lakini hata maisha ya baadhi ya viongozi wa sasa na watumishi wa umma yako juu yakilinganishwa na viongozi wa zamani ambao walifanya kazi chini ya misingi na miiko ya uongozi ikiwemo ya Azimio la Arusha.

Huku akionyesha msisitizo wa hilo, Jaji Warioba ambaye alizungumza mbele ya viongozi wa vyama 17 vya siasa nchini na wawakilishi wa serikali kutoka Idara ya Utawala Bora Ikulu, katika kongamano hilo lililoandaliwa na Kituo cha Demokrasia (TCD), alimtolea mfano mzee Rashid Kawawa, ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 15 kutoka mwaka 1962 hadi 1977, lakini maisha yake ni ya kawaida.

"Mzee Kawawa alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 15, kutoka 1962 hadi 1977, tena Waziri Mkuu Mtendaji mwenye madaraka kweli si kama Waziri Mkuu wa sasa hivi, lakini hebu nenda katafute mali zake, kaangalie nyumba yake ya Madale ni ya kawaida tu, utajiuliza hivi yale ni maisha ya mtu aliyekuwa Waziri Mkuu kwa miaka 15?" alihoji na kuongeza:

"Leo hii nyumba za serikali zilizouzwa kwetu sisi viongozi, zimekarabatiwa na zinapendeza kweli, wengine wamezivunja na kujenga upya, angalia haya maisha, hata tupige kelele za ufisadi bado haya ni matokeo madogo, tuko katika hali ngumu sana."

Akichambua kipengele kimoja baada ya kingine katika Azimio la Arusha na athari zake kwa sasa baada ya kuvunjwa, alisema wakati siku za nyuma ilikuwa ni mwiko watumishi wa umma kuwa na mishahara miwili, leo hii baadhi yao wanapokea mishahara zaidi ya mmoja na pia ilikuwa ni mwiko kwa watumishi kuwa wakurugenzi au kuwa na hisa, leo wapo wanaomiliki makampuni.

Kwa msisitizo, alisema watu wanapata mishahara miwili, wapo baadhi ya watendaji serikalini wakiwemo mawaziri hawaendi kufungua semina kama hazina maslahi ya posho kubwa.

Alisema posho hizo wakati mwingine ni kubwa kuliko mishahara na kibaya zaidi ni kwamba, haikatwi kodi kama inavyofanyika katika mshahara.

Licha ya kumulika baadhi ya viongozi walio katika utumishi wa umma, Jaji Warioba alisema hata baadhi ya wabunge hupenda kuhudhuria semina ambazo zina posho huku wakilalamikia maslahi duni wakijilinganisha na wenzao wa Kenya.

"Wakati mwingine hata baadhi ya wabunge hutaka kwenda sehemu zenye posho, pia hulalamikia maslahi duni, ni kweli mkijiangalia na wenzenu wa Kenya wao wako juu sana, lakini nanyi msiangalie wale angalieni watu wa chini," alisisitiza.

Huku akiangalia zaidi athari za kuvunjwa azimio hilo kwa nchi, alisema sasa wakati kipindi cha nyuma uongozi wa nchi ulikuwa ni kwa wakulima na wafanyakazi, leo hii hakuna tena nafasi kwa watu wa kada hiyo kushika nafasi.

Alisema hata mfanyakazi au mkulima awe na uwezo mkubwa kiasi gani bado ni nadra kuweza kupata nafasi ya kuongoza kutokana na kuwepo tabaka la wafanyabiashara wenye pesa, ambalo limewatenga na kuwafanya duni watu wa chini.

Jaji Warioba alisema ni kujidanganya kufikiri kunaweza kuwepo Sheria ya Maadili, akitoa mfano kwamba Azimio la Arusha halikuwa sheria, lakini watu waliheshimu na ambao walishindwa kutii walijiondoa wenyewe kabla ya kufikishwa mahakamani.

Alisema sasa hivi maisha ya tabaka la chini yanazidi kuwa magumu hasa kwa wafanyakazi katika sekta ya umma kuwa na mishahara midogo, lakini wakubwa wakizidi kujiongezea posho na mishahara huku tabaka hilo la chini likiona, kitu alichoonya kwamba ni cha hatari.

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema uamuzi wa kuandaa kongamano lenye mada hiyo linalenga kukumbusha maadili katika utumishi wa umma.

Profesa Lipumba ambaye ni msomi mwenye kuheshimika katika taaluma ya uchumi, alisema utumishi wa umma unapaswa kuegemea katika msingi wa kuangalia maslahi ya umma.

"Tumeamua kuangalia hili ili kukumbusha maadili katika utumishi wa umma, hali ni mbaya na nchi inaweza kuvurugika kama hali itakwenda kama ilivyo sasa," alionya.

Profesa Lipumba alisisitiza kwamba, kama matabaka yataendelea kwa watumishi wa chini kuishi kwa mishahara midogo huku viongozi wa juu wakijiongezea posho na mishahara mikubwa, hali itakuwa mbaya.

Kongamano hilo ambalo linamalizika leo, pamoja na mambo mengine limejikita katika kujadili maadili katika utumishi wa umma na namna bora ya kupata viongozi wa dola.

CHANZO: Mwananchi

18 Nov 2008

Picha hii inayoonyesha adha ya usafiri wa wanafunzi Dar (haihusiani na habari ifuatayo) kwa hisani ya Zenjidar
Wakati Gazeti la Serikali HABARI LEO linaripoti  

WALIMU kote nchini jana walianza mgomo usio na kikomo wa kuishinikiza serikali kuwalipa madai yao ya zaidi ya Sh16 bilioni, katika siku ambayo ilijaa matukio mbalimbali, yakiwemo ya kuchapwa viboko kwa walimu waliokataa kugoma, jitihada za serikali kukwamisha mgomo, walimu kuripoti kazini na kuanza kupiga soga na wengine kuanza kulipwa madai yao.

Waandishi wetu kutoka mikoa mbalimbali wanaripoti kuwa mgomo huo, uliotakiwa kuanza Oktoba 15 lakini ukakwamishwa, ulifanikiwa kwa asilimia 70 ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanafunzi kushindwa kuanza mitihani ya kumaliza mwaka, lakini katika baadhi ya shule walimu walifundisha kama kawaida.

Katika ufuatiliaji uliofanywa na Mwananchi katika sehemu kadhaa, walimu ama hawakwenda kabisa kazini ama walienda na kufanya vikao, vilivyoonekana kuwa vya kupoteza muda. Walimu wakuu, wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya wengi walidai kuwa hali ilikuwa shwari kwenye maeneo yao, lakini waandishi wetu walipoenda kwenye shule walikuta migomo ikiendelea kwa mikutano hiyo ya soga maofisini, huku wengine wakipata kinywaji kwenye baa jirani.

Mgomo huo ni matokeo ya serikali kushindwa kuwatimizia walimu madai yao nane tangu walipotangaza mgomo na kutoa siku 60 kwa serikali kuhakikisha inatatua matatizo hayo. Madai hayo ni pamoja na malimbikizo ya Sh6.6 bilioni, masomo (Sh1.01 bilioni), likizo (Sh1.07 bilioni), matibabu (589.9 milioni), posho za kujikimu (Sh565.8 milioni) na mirathi (72.9 milioni), kwa mujibu wa serikali.

Pia walimu wanadai kupandishwa daraja na kuundwa kwa baraza la maridhiano.

Serikali imekuwa ikidai kila mara kuwa inaendelea na zoezi la uhakiki na kuwataka walimu kuvuta subira, lakini baada ya Mahakama ya Rufaa kubatilisha amri ya muda ya kuzuia mgomo, kasi ya kushughulikia madai hayo ilionekana kuongezeka na jana baadhi ya walimu walianza kulipwa madai yao, huku Chama cha Walimu (CWT) kikisitiza kuwa mgomo utaisha baada ya walimu kulipwa senti ya mwisho.

Mwandishi wetu, Shija Felician anaripoti kutoka Kahama, Shinyanga kuwa walimu waliotii uamuzi wa kugoma, jana walitembeza viboko kwa wenzao walioingia darasani kufundisha.

Katibu wa CWT Kahama, Said Mselem alisema asilimia 70 ya walimu wote walioko wilayani hapa waligoma, lakini wale wachache ambao waliandikisha majina kuonyesha wamehudhuria kazini, walijikuta kwenye hali ngumu baada ya kuondolewa madarasani kwa viboko na wenzao waliogoma.

Sakata hilo lilitokea kwenye shule za msingi za Kilima "A" na "B", Nyashimbi na Mbulu, ambako walimu wachache walioamua kuingia darasani waliondolewa kwa viboko.

Baadhi ya shule zilizotembelewa na waandishi wa habari jana zilikuwa zimefungwa wanafunzi walikuwa wamezagaa nje wakicheza. Viongozi wa serikali ngazi ya wilaya, tarafa, kata na vijiji walikuwa wakizunguka kila shule kufuatilia walimu waliogoma baada ya Wizara ya Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuagiza hivyo juzi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kahama, Theresia Mahango alisema amepokea Sh34,300,000 kwa ajili ya kulipa madai ya walimu. Walimu wilayani Kahama wanadai zaidi ya Sh300 milioni, lakini Mahango alisema fedha hizo ni kwa ajili ya malipo yaliyoonekana kuwa ni halali tu.

Awali jana, Katibu Tawala wa Kahama, Bulla Gwandu alisema walimu walikuwa darasani wakifundisha, lakini mashuleni hali haikuwa hivyo.

Jijini Dar es salaam, Hussein Kauli anaripoti kuwa walimu walianza mgomo wao wakifananisha ahadi za serikali na ahadi za kuku kwa vifaranga kuwa atavinyonyesha wakati ni jambo lisilowezekana.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Pwani, Method Rugambarala alisema walimu wake walianza mgomo asubuhi na walimueleza kuwa wanafanya hivyo kuunga mkono tamko la CWT, lakini akasema watafika maeneo ya kazi kuhofia vitisho vya serikali.

Naye mmoja wa walimu wakuu wa shule za msingi Temeke ambaye hakutaka kutajwa gazetini, aliilalamikia serikali kuwa inatafuta ugomvi na walimu kwa kuwa haina sababu ya kutowalipa madai yao.

"Serikali haina sababu inayowafanya wasitulipe madai yetu kwa kipindi kirefu kiasi hiki. Upole wetu kwa watu hawa umefikia kikomo na tutashindwa kufanya kazi hali ambayo itawaathiri watoto wetu," alisema.

Walimu wengi wa shule za msingi za Kunduchi na Pius Msekwa hawakuhudhuria shuleni jana, hatua iliyofanya kushindwa kuanza kwa mitihani ya mwisho wa mwaka.

Walimu wengine waliounga mkono mgomo huo ni wa shule za msingi za Bunge, Uhuru Mchanganyiko, Boma na Diamond za Wilaya ya Ilala, hali iliyowafanya baadhi yao kuandamana kwenda kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Kandoro kufikisha kilio chao.

Naye, Patricia Kimelemeta anaripoti kuwa, zaidi ya asilimia 75 ya walimu wa Manispaa ya Kinondoni walifika shuleni kama kawaida, lakini hawakufundisha.

Mkuu wa Wilaya ya Kindondoni, Kanali Fabian Massawe alisema kuwa alipata taarifa kuwa baadhi ya walimu hawakufika shuleni na kuelezea kitendo hicho kuwa ni kiburi kwa serikali ambayo tayari imeanza kutoa fedha kulingana na madai yao nchi nzima.

Naye Aziza Nangwa, anaripoti kuwa shule za msingi za Ubungo Kibangu na Ubungo Kisiwani hakukuwepo na mgomo.

"Sisi bwana tunaendelea na kazi kama kawaida na suala la kugoma kwetu halipo. Si unaona tunavyochapa kazi au huoni watoto wanaingia madarasani kama kawaida kwahiyo tunafuata selikali inasemaje," alisema Mwalimu Kilimba.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ubungo, Kibangu Juma Abdallah alisema kuwa suala la kugoma ni la mtu binafsi kwa hiyo wanaendelea na kazi.

Mwandishi wetu, Angela Mwakilasa anaripoti kuwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Air Wing, Devota Stambuli alisema kuwa, taarifa za mgomo alizisikia kwenye vyombo vya habari na kwamba ataendelea kufundisha hadi apate barua ya CWT.

Kutoka Morogoro, Samuel Msuya anaripoti kuwa asilimia 70 ya walimu waliitikia wito wa kugoma.

Katibu Mkuu wa CWT Morogoro, Issa Ngayama alisema walimu katika wilaya za Ulanga, Kilombero, Kilosa na Mvomero hawakuingia darasani, lakini wa Manispaa ya Morogoro waliendelea kufundisha.

Ngayama alidai kuwa walipata taarifa kutoka Ulanga na Kilombero kuwa, polisi walikuwa wakipita sehemu kadhaa kuhakikisha kuwa mgomo unadhibitiwa.

"Lakini sisi tunaona kuwa mgomo umefanikiwa kutokana na viongozi wa serikali kuacha kazi zao na kuzunguka katika shule kuhakikisha wanauzima mgomo huu," alisema.

Hata hivyo, uchunguzi katika shule mbalimbali za Manispaa ya Morogoro na Ulanga unaonyesha kuwa walimu waliripoti kwenye vituo vya kazi, lakini hawakuingia darasani kwa madai ya kuandaa ripoti za mwaka.

Katibu wa CWT Kilombero, Maswi Mudani alisema walimu wamefuata maelekezo ya chama chao ya kugoma hadi walipwe haki zao, wakati wilayani Kilombero, Mkurugenzi Mtendaji, Alferd Luanda alisema wamepokea Sh63 milioni kwa ajili ya malipo hayo.

Naye Juddy Ngonyani wa Sumbawanga anaripoti kuwa, walimu wa shule za sekondari na msingi walianza mgomo na kufanya wanafunzi wa shule nyingi kupata fursa ya kucheza nje tangu asubuhi.

Mwananchi ilishuhudia hali hiyo katika shule za msingi Mwenge A na B, Chanji, Kizwite, Chemechem, Majengo, Jangwani, Kanda, Mazwi na Shule ya Kutwa Sumbawanga, wakati walimu wengi wa shule za sekondari hawakwenda kabisa kazini .

Katika Shule ya Msingi ya Jangwani, Mwalimu Mkuu Morris Kibona alisema kuwa walimu wameripoti kazini kama kawaida asubuhi, lakini hawakuingia darasani isipokuwa wale wa darasa la kwanza.

Mmoja wa walimu hao, Mary Kameme alisema: "Hatufurahishwi na kitendo cha kugoma kwa kuwa kinawaathiri wanafunzi, lakini ni lazima serikali itambue kuwa kama walimu wamefikia hatua ya kugoma, inamaanisha wamechoshwa na hali iliyopo."

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwenge "A", Gilbert Mwangosi alisema: "Leo nimechelewa kwa sababu nimekuja kwa mguu... sikuona sababu ya kuchoma mafuta yangu ya pikipiki ili kuwahi shule wakati leo walimu tunaanza mgomo nchi nzima."

Kutoka Arusha, Hemed Kivuyo anaripoti kuwa kulikuwa na walimu waliogoma na walioamua kuingia darasani.

Uchunguzi uliofanywa jana katika shule za msingi na sekondari umebaini kuwa pamoja na walimu wengi kukataa kushiriki mgomo, wengi walikaa kwenye vikundi kujadili hatima yao.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Uhuru ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema hakukuwepo na mgomo isipokuwa baadhi ya walimu wapo katika majadiliano na kwamba, anawasubiri ili waweze kusimamia mitihani.

"Hakuna mgomo kama unavyoona walimu wapo ofisini na wengine wale kule nje wapo katika majadiliano na ninawasubiri waje kusimamia mitihani," alisema mwalimu huyo.

Lakini walimu walioongea na Mwananchi walisema hawawezi kuingia madarasani kwa kuwa, kufanya hivyo ni kusaliti msimamo wa wenzao.

"Hatuingii darasani; huyo mwalimu aliyekueleza hakuna mgomo yeye ndiye hayupo katika mgomo, lakini sisi tunagoma," alisema mmoja wa walimu hao ambao hawakutaka kuandikwa majina yao gazetini.

Katika shule ya msingi Ungalimited, baadhi ya walimu waliingia madarasani kama kawaida huku baadhi yao wakiwa katika baa ya jirani iliyoandikwa `NARA` wakinywa bia, wakidai kuwa wameamua kujiburudisha kwa kuwa kwa sasa wanasimamia mitihani.

Katibu wa CWT Arusha, Nuru Shenkalwa alisema mpaka sasa chama hicho hakina tamko lolote na kwamba wanasubiri maelekezo toka juu, wakati Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Evance Balama alisema kuwa amefanya ziara ya ghafla katika baadhi ya shule na hapakuwepo na mgomo wowote kwa walimu.

Mwandishi wetu wa Mbeya, Brandy Nelson anaripoti kuwa baadhi ya walimu waliamua kuendelea na kazi, ikiwa ni pamoja na kusimamia mitihani ya kumaliza mwaka, wakidai kuwa hawajapata taarifa ya maandishi ya kuwataka wagome.

"Taarifa za mgomo tumezisikia kwenye vyombo vya habari, lakini hatujapata barua yoyote kutuarifu kuhusu mgomo kutoka CWT mkoa," alisema Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Sisimba, Ephata Mbisemmoja.

Naye Afisa Elimu wa Mbeya, Juma Kaponda alisema kuwa tayari Sh 636,507,743 zimeshafika kwa ajili ya kulipa walimu madai yao na kwamba zimeanza kufanyiwa utaratibu wa kuingizwa katika akaunti za halmshauri kwa ajili ya kuanza kuwalipa walimu.

Katibu wa CWT Mbeya, Tweedsmur Zambi alikiri kupata taarifa kuwa katika baadhi ya shule walimu waliamua kuendelea na kazi.

"Lakini si kweli kwamba hawana taarifa ya mgomo. Naomba uelewe kuwa mgomo kwa Mkoa wa Mbeya upo kama ulivyo mikoa mingine,"alisema.

Jijini Tanga walimu waliochelewa vituoni walitumiwa ujumbe mfupi wa simu (sms) kubembelezwa wafike vituoni, anaripoti Burhani Yakub.

Walimu kadhaa walitumiwa ujumbe kwenye simu zao wakiombwa kufika shule na kuhakikishiwa kuwa fedha zao zimeshawasilishwa na kwamba, ziko kwenye akaunti ya halmashauri.

Mwananchi ilionyeshwa ujumbe uliokuwa kwenye simu ya mwalimu mmoja wa shule ya msingi iliyo katikati ya Jiji la Tanga ikisema: “Unoambwa kufika shuleni kwako, usifanye mgomo fedha zimeshaingia na mtaanza kulipwa leo.”

“Hata wenzangu wa shule mbalimbali wametumiwa ujumbe kama huu hivyo tukaamua kuja shuleni baada ya kuhakikishiwa kuwa, fedha zetu zimeshawasilishwa,” alisema mwalimu huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Mwajuma.

Kutoka mkoani Mwanza, Frederick Katulanda anaripoti kuwa walimu waliendesha mgomo baridi, baadhi wakiripoti kazini na wengine kutoripoti kabisa huku wakisubiri taarifa za malipo yao.

Karibu katika shule zote za msingi kulikuwa na walimu wachache na hivyo kushindwa kufundisha na kuachia wanafunzi waendelee na michezo nje.

Katika shule za Nyamagana, Buhongwa, Kitangiri, Mirongo, Mbugani na Nyamanoro, walimu walikuwepo, lakini hawakuweza kufundisha.

Mmoja wa wanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya Kitangiri, Zelaida Filbert alisema ingawa baadhi ya walimu wamefika shuleni hapo, hakuna aliyefundisha na kuongeza: “Tumekaa darasani kwa muda mrefu sasa nimeamua kuondoka tu kwenda nyumbani, walimu hawafundishi wapo tu. Alikuja mwalimu wa Hisabati na kutupatia mitihani yetu halafu akaondoka.”

Mwanafunzi mwingine, Charles James wa shule ya Nyanza alisema leo hatahudhuria shule kutokana na ukweli kuwa, walimu wanaendelea na mgomo.

Mwenyekiti wa CWT Mwanza, Benedicto Raphael alisema jana walikuwa na mgomo baridi kutokana na taarifa kuchelewa kuwafikia walimu wengi na kutangaza kuwa mgomo rasmi ni leo.

“Serikali imetimiza madai mawili kati ya nane, tunaendelea na mgomo wetu. Tunaiomba serikali kutekeleza madai yetu badala ya kututolea vitisho na napenda itambue hatutaogopa vitisho... tutaendelea kudai haki yetu mpaka ilipwe,” alisema na kubainisha kuwa walimu wa Mwanza wanadai Sh1.1 bilioni.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya jiji alisema wamelipa jumla ya madai 67 kiasi cha Sh 37 ml. kuanzia majira ya saa 3:00 asubuhi. Kuna madai 195 ya walimu, lakini madai 128 yamebainika kuwa na kasoro.

Julieth Ngarabali anaripoti kutoka mkoani Pwani kuwa, wanafunzi walishindwa kufanya mitihani ya kumaliza mwaka kutokana na mgomo wa walimu.

Habari ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa shule nyingi za msingi katika wilaya za Kibaha Vijijini, Bagamoyo, Kisarawe na Kibaha Mjini mitihani haikuanza kama ilivyopangwa.

Katika shule kadhaa ikiwemo Msangani, Nyumbu, Umoja, Mwendapole na Chalinze walimu walikiri kuwa mitihani haikufanyika, lakini wakasema kuwa hiyo ilitokana na kutokamilika kuchapishwa na kwa sababu ya mgomo, lakini katika shule za Mkuza, Mkoani, Maili Moja, Nyumbui na Soga wanafunzi waliendelea na mitihani.

Baadhi ya walimu walisema mitihani itaanza Jumatano.

Mwenyekiti wa CWT, Pwani Kelvin Mahundi alisema walimu waliingia darasani kutokana na kuogopa vitisho vya serikali, lakini si kwamba hawana nia ya kugoma, wakati mwenyekiti wa Kibaha, Donald Machapula alikiri kuwepo kwa shule ambazo walimu waligoma kusimamia mitihani.

"Sidhani hapa kuna la maana linaloendelea; naishauri Serikali iharakishe malipo ya walimu maana hakuna kitakachokuwa kinafanyika huko kwa watoto mashuleni," alisema Mahundi.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Kibaha, Festo Kang'ombe alisema wamepokea hundi ya Sh55 milioni kwa Wilaya ya Kibaha Vijijini na Sh51,818,107 kwa Kibaha Mjini na kwamba wahasibu jana walikuwa wakihaha kuandika malipo kwa walimu.

Hali ya mgawanyiko pia ilionekana mkoani Singida, ambako baadhi ya walimu waliingia darasani na wengine kutoenda kabisa kazini, anaripoti Jumbe Ismaily.

Katika Shule ya Msingi ya Kindai, wanafunzi wake walihudhuria shuleni, lakini hawakuweza kusoma kutokana na mgomo huo, hali iliyokuwa pia katika shule za msingi za Bomani, Sabasaba, Ukombozi na Chief Senge Sekondari ambako wanafunzi walitakiwa kurudi nyumbani.

Katika shule za Utemini na Singidani, walimu wote walihudhuria kazini na kusimamia mitihani ya mwisho wa mwaka.

Waandishi wetu walio Babati, Iringa na Handeni wanaripoti kuwa hakukuwepo na mgomo na zoezi lililotawala jana lilikuwa ni malipo.


Gazeti la MWANANCHI kwa upande wake linahabarisha kwamba

WALIMU kote nchini jana walianza mgomo usio na kikomo wa kuishinikiza serikali kuwalipa madai yao ya zaidi ya Sh16 bilioni, katika siku ambayo ilijaa matukio mbalimbali, yakiwemo ya kuchapwa viboko kwa walimu waliokataa kugoma, jitihada za serikali kukwamisha mgomo, walimu kuripoti kazini na kuanza kupiga soga na wengine kuanza kulipwa madai yao.

Waandishi wetu kutoka mikoa mbalimbali wanaripoti kuwa mgomo huo, uliotakiwa kuanza Oktoba 15 lakini ukakwamishwa, ulifanikiwa kwa asilimia 70 ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanafunzi kushindwa kuanza mitihani ya kumaliza mwaka, lakini katika baadhi ya shule walimu walifundisha kama kawaida.

Katika ufuatiliaji uliofanywa na Mwananchi katika sehemu kadhaa, walimu ama hawakwenda kabisa kazini ama walienda na kufanya vikao, vilivyoonekana kuwa vya kupoteza muda. Walimu wakuu, wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya wengi walidai kuwa hali ilikuwa shwari kwenye maeneo yao, lakini waandishi wetu walipoenda kwenye shule walikuta migomo ikiendelea kwa mikutano hiyo ya soga maofisini, huku wengine wakipata kinywaji kwenye baa jirani.

Mgomo huo ni matokeo ya serikali kushindwa kuwatimizia walimu madai yao nane tangu walipotangaza mgomo na kutoa siku 60 kwa serikali kuhakikisha inatatua matatizo hayo. Madai hayo ni pamoja na malimbikizo ya Sh6.6 bilioni, masomo (Sh1.01 bilioni), likizo (Sh1.07 bilioni), matibabu (589.9 milioni), posho za kujikimu (Sh565.8 milioni) na mirathi (72.9 milioni), kwa mujibu wa serikali.

Pia walimu wanadai kupandishwa daraja na kuundwa kwa baraza la maridhiano.

Serikali imekuwa ikidai kila mara kuwa inaendelea na zoezi la uhakiki na kuwataka walimu kuvuta subira, lakini baada ya Mahakama ya Rufaa kubatilisha amri ya muda ya kuzuia mgomo, kasi ya kushughulikia madai hayo ilionekana kuongezeka na jana baadhi ya walimu walianza kulipwa madai yao, huku Chama cha Walimu (CWT) kikisitiza kuwa mgomo utaisha baada ya walimu kulipwa senti ya mwisho.

Mwandishi wetu, Shija Felician anaripoti kutoka Kahama, Shinyanga kuwa walimu waliotii uamuzi wa kugoma, jana walitembeza viboko kwa wenzao walioingia darasani kufundisha.

Katibu wa CWT Kahama, Said Mselem alisema asilimia 70 ya walimu wote walioko wilayani hapa waligoma, lakini wale wachache ambao waliandikisha majina kuonyesha wamehudhuria kazini, walijikuta kwenye hali ngumu baada ya kuondolewa madarasani kwa viboko na wenzao waliogoma.

Sakata hilo lilitokea kwenye shule za msingi za Kilima "A" na "B", Nyashimbi na Mbulu, ambako walimu wachache walioamua kuingia darasani waliondolewa kwa viboko.

Baadhi ya shule zilizotembelewa na waandishi wa habari jana zilikuwa zimefungwa wanafunzi walikuwa wamezagaa nje wakicheza. Viongozi wa serikali ngazi ya wilaya, tarafa, kata na vijiji walikuwa wakizunguka kila shule kufuatilia walimu waliogoma baada ya Wizara ya Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuagiza hivyo juzi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kahama, Theresia Mahango alisema amepokea Sh34,300,000 kwa ajili ya kulipa madai ya walimu. Walimu wilayani Kahama wanadai zaidi ya Sh300 milioni, lakini Mahango alisema fedha hizo ni kwa ajili ya malipo yaliyoonekana kuwa ni halali tu.

Awali jana, Katibu Tawala wa Kahama, Bulla Gwandu alisema walimu walikuwa darasani wakifundisha, lakini mashuleni hali haikuwa hivyo.

Jijini Dar es salaam, Hussein Kauli anaripoti kuwa walimu walianza mgomo wao wakifananisha ahadi za serikali na ahadi za kuku kwa vifaranga kuwa atavinyonyesha wakati ni jambo lisilowezekana.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Pwani, Method Rugambarala alisema walimu wake walianza mgomo asubuhi na walimueleza kuwa wanafanya hivyo kuunga mkono tamko la CWT, lakini akasema watafika maeneo ya kazi kuhofia vitisho vya serikali.

Naye mmoja wa walimu wakuu wa shule za msingi Temeke ambaye hakutaka kutajwa gazetini, aliilalamikia serikali kuwa inatafuta ugomvi na walimu kwa kuwa haina sababu ya kutowalipa madai yao.

"Serikali haina sababu inayowafanya wasitulipe madai yetu kwa kipindi kirefu kiasi hiki. Upole wetu kwa watu hawa umefikia kikomo na tutashindwa kufanya kazi hali ambayo itawaathiri watoto wetu," alisema.

Walimu wengi wa shule za msingi za Kunduchi na Pius Msekwa hawakuhudhuria shuleni jana, hatua iliyofanya kushindwa kuanza kwa mitihani ya mwisho wa mwaka.

Walimu wengine waliounga mkono mgomo huo ni wa shule za msingi za Bunge, Uhuru Mchanganyiko, Boma na Diamond za Wilaya ya Ilala, hali iliyowafanya baadhi yao kuandamana kwenda kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Kandoro kufikisha kilio chao.

Naye, Patricia Kimelemeta anaripoti kuwa, zaidi ya asilimia 75 ya walimu wa Manispaa ya Kinondoni walifika shuleni kama kawaida, lakini hawakufundisha.

Mkuu wa Wilaya ya Kindondoni, Kanali Fabian Massawe alisema kuwa alipata taarifa kuwa baadhi ya walimu hawakufika shuleni na kuelezea kitendo hicho kuwa ni kiburi kwa serikali ambayo tayari imeanza kutoa fedha kulingana na madai yao nchi nzima.

Naye Aziza Nangwa, anaripoti kuwa shule za msingi za Ubungo Kibangu na Ubungo Kisiwani hakukuwepo na mgomo.

"Sisi bwana tunaendelea na kazi kama kawaida na suala la kugoma kwetu halipo. Si unaona tunavyochapa kazi au huoni watoto wanaingia madarasani kama kawaida kwahiyo tunafuata selikali inasemaje," alisema Mwalimu Kilimba.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ubungo, Kibangu Juma Abdallah alisema kuwa suala la kugoma ni la mtu binafsi kwa hiyo wanaendelea na kazi.

Mwandishi wetu, Angela Mwakilasa anaripoti kuwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Air Wing, Devota Stambuli alisema kuwa, taarifa za mgomo alizisikia kwenye vyombo vya habari na kwamba ataendelea kufundisha hadi apate barua ya CWT.

Kutoka Morogoro, Samuel Msuya anaripoti kuwa asilimia 70 ya walimu waliitikia wito wa kugoma.

Katibu Mkuu wa CWT Morogoro, Issa Ngayama alisema walimu katika wilaya za Ulanga, Kilombero, Kilosa na Mvomero hawakuingia darasani, lakini wa Manispaa ya Morogoro waliendelea kufundisha.

Ngayama alidai kuwa walipata taarifa kutoka Ulanga na Kilombero kuwa, polisi walikuwa wakipita sehemu kadhaa kuhakikisha kuwa mgomo unadhibitiwa.

"Lakini sisi tunaona kuwa mgomo umefanikiwa kutokana na viongozi wa serikali kuacha kazi zao na kuzunguka katika shule kuhakikisha wanauzima mgomo huu," alisema.

Hata hivyo, uchunguzi katika shule mbalimbali za Manispaa ya Morogoro na Ulanga unaonyesha kuwa walimu waliripoti kwenye vituo vya kazi, lakini hawakuingia darasani kwa madai ya kuandaa ripoti za mwaka.

Katibu wa CWT Kilombero, Maswi Mudani alisema walimu wamefuata maelekezo ya chama chao ya kugoma hadi walipwe haki zao, wakati wilayani Kilombero, Mkurugenzi Mtendaji, Alferd Luanda alisema wamepokea Sh63 milioni kwa ajili ya malipo hayo.

Naye Juddy Ngonyani wa Sumbawanga anaripoti kuwa, walimu wa shule za sekondari na msingi walianza mgomo na kufanya wanafunzi wa shule nyingi kupata fursa ya kucheza nje tangu asubuhi.

Mwananchi ilishuhudia hali hiyo katika shule za msingi Mwenge A na B, Chanji, Kizwite, Chemechem, Majengo, Jangwani, Kanda, Mazwi na Shule ya Kutwa Sumbawanga, wakati walimu wengi wa shule za sekondari hawakwenda kabisa kazini .

Katika Shule ya Msingi ya Jangwani, Mwalimu Mkuu Morris Kibona alisema kuwa walimu wameripoti kazini kama kawaida asubuhi, lakini hawakuingia darasani isipokuwa wale wa darasa la kwanza.

Mmoja wa walimu hao, Mary Kameme alisema: "Hatufurahishwi na kitendo cha kugoma kwa kuwa kinawaathiri wanafunzi, lakini ni lazima serikali itambue kuwa kama walimu wamefikia hatua ya kugoma, inamaanisha wamechoshwa na hali iliyopo."

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwenge "A", Gilbert Mwangosi alisema: "Leo nimechelewa kwa sababu nimekuja kwa mguu... sikuona sababu ya kuchoma mafuta yangu ya pikipiki ili kuwahi shule wakati leo walimu tunaanza mgomo nchi nzima."

Kutoka Arusha, Hemed Kivuyo anaripoti kuwa kulikuwa na walimu waliogoma na walioamua kuingia darasani.

Uchunguzi uliofanywa jana katika shule za msingi na sekondari umebaini kuwa pamoja na walimu wengi kukataa kushiriki mgomo, wengi walikaa kwenye vikundi kujadili hatima yao.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Uhuru ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema hakukuwepo na mgomo isipokuwa baadhi ya walimu wapo katika majadiliano na kwamba, anawasubiri ili waweze kusimamia mitihani.

"Hakuna mgomo kama unavyoona walimu wapo ofisini na wengine wale kule nje wapo katika majadiliano na ninawasubiri waje kusimamia mitihani," alisema mwalimu huyo.

Lakini walimu walioongea na Mwananchi walisema hawawezi kuingia madarasani kwa kuwa, kufanya hivyo ni kusaliti msimamo wa wenzao.

"Hatuingii darasani; huyo mwalimu aliyekueleza hakuna mgomo yeye ndiye hayupo katika mgomo, lakini sisi tunagoma," alisema mmoja wa walimu hao ambao hawakutaka kuandikwa majina yao gazetini.

Katika shule ya msingi Ungalimited, baadhi ya walimu waliingia madarasani kama kawaida huku baadhi yao wakiwa katika baa ya jirani iliyoandikwa `NARA` wakinywa bia, wakidai kuwa wameamua kujiburudisha kwa kuwa kwa sasa wanasimamia mitihani.

Katibu wa CWT Arusha, Nuru Shenkalwa alisema mpaka sasa chama hicho hakina tamko lolote na kwamba wanasubiri maelekezo toka juu, wakati Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Evance Balama alisema kuwa amefanya ziara ya ghafla katika baadhi ya shule na hapakuwepo na mgomo wowote kwa walimu.

Mwandishi wetu wa Mbeya, Brandy Nelson anaripoti kuwa baadhi ya walimu waliamua kuendelea na kazi, ikiwa ni pamoja na kusimamia mitihani ya kumaliza mwaka, wakidai kuwa hawajapata taarifa ya maandishi ya kuwataka wagome.

"Taarifa za mgomo tumezisikia kwenye vyombo vya habari, lakini hatujapata barua yoyote kutuarifu kuhusu mgomo kutoka CWT mkoa," alisema Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Sisimba, Ephata Mbisemmoja.

Naye Afisa Elimu wa Mbeya, Juma Kaponda alisema kuwa tayari Sh 636,507,743 zimeshafika kwa ajili ya kulipa walimu madai yao na kwamba zimeanza kufanyiwa utaratibu wa kuingizwa katika akaunti za halmshauri kwa ajili ya kuanza kuwalipa walimu.

Katibu wa CWT Mbeya, Tweedsmur Zambi alikiri kupata taarifa kuwa katika baadhi ya shule walimu waliamua kuendelea na kazi.

"Lakini si kweli kwamba hawana taarifa ya mgomo. Naomba uelewe kuwa mgomo kwa Mkoa wa Mbeya upo kama ulivyo mikoa mingine,"alisema.

Jijini Tanga walimu waliochelewa vituoni walitumiwa ujumbe mfupi wa simu (sms) kubembelezwa wafike vituoni, anaripoti Burhani Yakub.

Walimu kadhaa walitumiwa ujumbe kwenye simu zao wakiombwa kufika shule na kuhakikishiwa kuwa fedha zao zimeshawasilishwa na kwamba, ziko kwenye akaunti ya halmashauri.

Mwananchi ilionyeshwa ujumbe uliokuwa kwenye simu ya mwalimu mmoja wa shule ya msingi iliyo katikati ya Jiji la Tanga ikisema: “Unoambwa kufika shuleni kwako, usifanye mgomo fedha zimeshaingia na mtaanza kulipwa leo.”

“Hata wenzangu wa shule mbalimbali wametumiwa ujumbe kama huu hivyo tukaamua kuja shuleni baada ya kuhakikishiwa kuwa, fedha zetu zimeshawasilishwa,” alisema mwalimu huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Mwajuma.

Kutoka mkoani Mwanza, Frederick Katulanda anaripoti kuwa walimu waliendesha mgomo baridi, baadhi wakiripoti kazini na wengine kutoripoti kabisa huku wakisubiri taarifa za malipo yao.

Karibu katika shule zote za msingi kulikuwa na walimu wachache na hivyo kushindwa kufundisha na kuachia wanafunzi waendelee na michezo nje.

Katika shule za Nyamagana, Buhongwa, Kitangiri, Mirongo, Mbugani na Nyamanoro, walimu walikuwepo, lakini hawakuweza kufundisha.

Mmoja wa wanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya Kitangiri, Zelaida Filbert alisema ingawa baadhi ya walimu wamefika shuleni hapo, hakuna aliyefundisha na kuongeza: “Tumekaa darasani kwa muda mrefu sasa nimeamua kuondoka tu kwenda nyumbani, walimu hawafundishi wapo tu. Alikuja mwalimu wa Hisabati na kutupatia mitihani yetu halafu akaondoka.”

Mwanafunzi mwingine, Charles James wa shule ya Nyanza alisema leo hatahudhuria shule kutokana na ukweli kuwa, walimu wanaendelea na mgomo.

Mwenyekiti wa CWT Mwanza, Benedicto Raphael alisema jana walikuwa na mgomo baridi kutokana na taarifa kuchelewa kuwafikia walimu wengi na kutangaza kuwa mgomo rasmi ni leo.

“Serikali imetimiza madai mawili kati ya nane, tunaendelea na mgomo wetu. Tunaiomba serikali kutekeleza madai yetu badala ya kututolea vitisho na napenda itambue hatutaogopa vitisho... tutaendelea kudai haki yetu mpaka ilipwe,” alisema na kubainisha kuwa walimu wa Mwanza wanadai Sh1.1 bilioni.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya jiji alisema wamelipa jumla ya madai 67 kiasi cha Sh 37 ml. kuanzia majira ya saa 3:00 asubuhi. Kuna madai 195 ya walimu, lakini madai 128 yamebainika kuwa na kasoro.

Julieth Ngarabali anaripoti kutoka mkoani Pwani kuwa, wanafunzi walishindwa kufanya mitihani ya kumaliza mwaka kutokana na mgomo wa walimu.

Habari ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa shule nyingi za msingi katika wilaya za Kibaha Vijijini, Bagamoyo, Kisarawe na Kibaha Mjini mitihani haikuanza kama ilivyopangwa.

Katika shule kadhaa ikiwemo Msangani, Nyumbu, Umoja, Mwendapole na Chalinze walimu walikiri kuwa mitihani haikufanyika, lakini wakasema kuwa hiyo ilitokana na kutokamilika kuchapishwa na kwa sababu ya mgomo, lakini katika shule za Mkuza, Mkoani, Maili Moja, Nyumbui na Soga wanafunzi waliendelea na mitihani.

Baadhi ya walimu walisema mitihani itaanza Jumatano.

Mwenyekiti wa CWT, Pwani Kelvin Mahundi alisema walimu waliingia darasani kutokana na kuogopa vitisho vya serikali, lakini si kwamba hawana nia ya kugoma, wakati mwenyekiti wa Kibaha, Donald Machapula alikiri kuwepo kwa shule ambazo walimu waligoma kusimamia mitihani.

"Sidhani hapa kuna la maana linaloendelea; naishauri Serikali iharakishe malipo ya walimu maana hakuna kitakachokuwa kinafanyika huko kwa watoto mashuleni," alisema Mahundi.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Kibaha, Festo Kang'ombe alisema wamepokea hundi ya Sh55 milioni kwa Wilaya ya Kibaha Vijijini na Sh51,818,107 kwa Kibaha Mjini na kwamba wahasibu jana walikuwa wakihaha kuandika malipo kwa walimu.

Hali ya mgawanyiko pia ilionekana mkoani Singida, ambako baadhi ya walimu waliingia darasani na wengine kutoenda kabisa kazini, anaripoti Jumbe Ismaily.

Katika Shule ya Msingi ya Kindai, wanafunzi wake walihudhuria shuleni, lakini hawakuweza kusoma kutokana na mgomo huo, hali iliyokuwa pia katika shule za msingi za Bomani, Sabasaba, Ukombozi na Chief Senge Sekondari ambako wanafunzi walitakiwa kurudi nyumbani.

Katika shule za Utemini na Singidani, walimu wote walihudhuria kazini na kusimamia mitihani ya mwisho wa mwaka.

Waandishi wetu walio Babati, Iringa na Handeni wanaripoti kuwa hakukuwepo na mgomo na zoezi lililotawala jana lilikuwa ni malipo.


HABARI LEO LIMEFANYA KAZI YAKE KAMA YALIVYOKUWA YANAFANYA MAGAZETI YA SERIKALI YA KIKOMUNISTI YA MUUNGANO WA KISOVIETI (USSR),KUTOA TAARIFA ZINAZOASHIRIA UDOGO AU KUTOKUWEPO KABISA KWA TATIZO (KATIKA HABARI HII,MGOMO WA WALIMU UMEDORORA,HAIJALETA ATHARI ZILIZOKUSUDIWA,MAMBO YOTE "POA",NK).UKISOMA MWANANCHI UTAGUNDUA KUWA HALI NI TOFAUTI NA INAYOZUNGUMZIWA NA HABARI LEO.IFAHAMIKE KWAMBA HAKUNA ANAYENUFAIKA KWA KUPEWA TAARIFA ZA KUPENDEZESHA MACHO.SUALA HAPA SIO UKUBWA AU UDOGO WA MGOMO HUO BALI ATHARI ZAKE KWA WADOGO,WATOTO NA WAJUKUU ZETU.IKUMBUKWE PIA KWAMBA TUKIO HILI LINATOKEA WAKATI SUALA LA MIGOMO LINAANZA KUWA KAMA "FASHENI" FLANI.

HILI TATIZO LINGEWEZA KUEPUKWA ZAMANI HIZO LAITI WAHUSIKA WASINGEENDEKEZA PRIORITIES ZAO BADALA YA ZA WALE WANAOPASWA KUWATUMIKIA.UTARATIBU WA KUTATUA MATATIZO KWA NJIA YA ZIMAMOTO NI HATARI SANA,YAANI MPAKA TATIZO LITOKEE NDIO ZIANZE JITIHADA ZA KUTAFUTA UFUMBUZI.HIVI SIKU ZOTE HIZI WALIKUWA WAPI HAO WANAOPASWA KUHAKIKI MADENI YA WALIMU?HIVI HAKUNA WATU WANAOLIPWA MISHAHARA KWA AJILI YA KAZI HIYO YA KUHAKIKI NA KUHAKIKISHA MASLAHI YA WALIMU NA WATUMISHI WENGINE WA UMMA?

KUKIMBILIA MAHAKAMANI KUZUIA MIGOMO NI SULUHISHO LA MUDA TU,UFUMBUZI WA KUDUMU NI KUWAJIBIKA IPASAVYO KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU (UWAJIBIKAJI).TATIZO LA WALIMU NI SEHEMU NDOGO TU YA MATATIZO KADHAA AMBAYO KWA HAKIKA YANGEWEZA KUEPUKIKA LAITI WAHUSIKA WANGEWAJIBIKA IPASAVYO.WALIMU WATALIPWA KWA ZIMAMOTO,INAWEZA KUZIMA MGOMO LAKINI KESHO TRL NAO WATAGUNDUA KUWA WAKIGOMA WATAFANYIWA MALIPO YA ZIMAMOTO,KESHOKUTWA MADAKTARI,MANESI,NK NK NK.

WAHUSIKA WATEKELEZE WAJIBU WAO.PIA,SISI NI MASIKINI NA TUNAPASWA KUISHI KIMASIKINI KAMA TUNATAKA KUMUDU GHARAMA ZA MAISHA YETU.UNUNUZI WA VITU VYA FAHARI NA MATUMIZI MENGINE YASIYO YA LAZIMA YANAATHIRI KWA KIWANGO KIKUBWA UWEZO WETU WA  KUJIHUDUMIA NA KUJIENDESHA WENYEWE.HIVI NI LAZIMA KILA MHESHIMIWA ATUMIE "SHANGINGI" LA MAMILIONI KADHAA?JE GHARAMA ZA GARI HILO ZINGEKATWA JAPO ROBO ZISINGEWEZA KUWALIPA WATUMISHI WENZETU WANAODAI MALIMBIKIZO YAO?



15 Nov 2008

HILI JINAMIZI LA MIGOMO NA KUFUNGA VYUO VIKUU LINAONEKANA KAMA LINATAKA KUSAMBAA KILA MAHALI.ILIANZIA MLIMANI,IKAJA DUCE,IKAJA MKWAWA NA SASA SUA (as extracted from Mwananchi)

Mjini Morogoro, SUA ilitangaza kufunga chuo kwa wanafunzi wote wa shahada ya kwanza kutokana na mgomo uliodumu siku mbili wa kushinikiza serikali iwape mkono kwa asilimia 100.

Taarifa iliyotolewa na mshauri wa wanafunzi wa chuo hicho, Jonas Bisheko iliwataka wanafunzi wote kuondoka maeneo ya chuoni kabla ya saa 9:00 alasiri jana.

Mara baada ya tangazo hilo kutolewa, wanachuo wa chuo hicho walionekana kufungasha mizigo na kuondoka kwa amani kutoka katika mazingira ya chuo hicho.

Wanafunzi walio katika eneo la Solomon Mahlangu Mazimbu walionekana na mizigo yao wakiondoka kuelekea katika maeneo mbalimbali ya mji huku wengine wakielekea kituo cha mabasi.

Awali, kaimu makamu mkuu wa chuo hicho, Profesa Dominic Kambarage alisema kuwa chuo kilitoa muda wa siku tatu wanafunzi kurudi darasani lakini hawakukubali.

Makamu wa rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo hicho, SUASA, Yulian Mizola aliwaambia wanafunzi wenzake kwenye mkutano kuwa uongozi wao ulikutana na kaimu makamu mkuu wa chuo, Profesa Kambarage ambaye aliagiza kuwa wanafunzi wote warejee madarasani mara moja kabla ya uamuzi mwingine kuchukuliwa.

Wakati huo huo, Bodi ya Mikopo imesema kuwa ili wanafunzi wote waliodahiliwa waweze kukopeshwa fedha kwa asilimia 100, serikali inatakiwa kutumia Sh160 bilioni kwa mwaka.

Kaimu mkurugenzi wa bodi hiyo, Lubambula Machunda, alisema kuwa idadi ya wanafunzi wanaotakiwa kukopeshwa ni 60,000 na kwamba wanafunzi hao walipatiwa jumla ya Sh140 bilioni, lakini akasema iwapo wanafunzi wote watatakiwa kupata mkopo kwa asilimia 100, basi Sh163 bilioni zitahitajika.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.