12 Sept 2010












Sijui ndio dalili kuwa mwenendo wa kampeni unakwenda ovyo au ni ubabaishaji tu,lakini "mkwara" uliochimbwa na mnajimu mahiri,Sheikh Yahya Hussein,kwamba anampatia Rais Jakaya Kikwete ulinzi wa majini ni suala linalopaswa kukemewa kwa nguvu zote.Na ukweli kwamba mtajwa-i.e. Kikwete- amekaa kimya ni ushahidi tosha kuwa ananufaishwa na majini hayo.

Kwa baadhi yetu tunaofahamu yanayofanyika "nyuma ya pazia" (behind the scene) hatushtushwi kihivyo na habari hizo kwa vile siasa za Tanzania na ushirikina ni kama samaki na maji.Hakuna msimu mzuri kwa waganga wa kienyeji kama huu wa uchaguzi ambapo wanasiasa wababaishaji wanajaribu kupata msaada wa nguvu za giza ili wapate ushindi.

Awali,Sheikh Yahya alitoa tishio kuwa atakayejitokeza kuwania nafasi ya urais na Kikwete atakutwa na mauti.Well,so far tukio pekee la kutishia uhai wa mwanasiasa katika harakati za uchaguzi wa mwaka huu ni kudondoka jukwaani kwa Kikwete wakati anazindua kampeni zake kwenye viwanja vya Jangwani.Whether majini yaligoma kutumikishwa au Kikwete alikiuka masharti ya mganga wake Sheikh Yahya leaves a lot to be desired.

Binafsi natafsiri tishio hili jipya la Sheikh Yahya kama mkakati mufilisi wa Kikwete na CCM yake kuwatisha wapiga kura.Yea,kwani kama si hivyo kwanini basi mhusika asikanushe hadharani na kusema "ulinzi pekee nilionao ni huu unaotolewa na Idara ya Usalama wa Taifa".Hawa ni wataalam wa ulinzi wa viongozi na wanalipwa kwa ajili ya kazi hiyo.Sasa kama kuna ulinzi mwingine wa nguvu za giza,na ambao Kikwete anauamini,basi pengine ni muhimu kuokoa fedha za walipa kodi kwa kusitisha ulinzi anapotatiwa na "walinzi binadamu" na abaki na hayo majini ya Sheikh Yahya.

Samahani kama nitakuudhi lakini nashawishika kueleza kuwa napatab tabu sana kuelewa kwani pamoja na madudu yote haya-from sera to ushirikina,from afya mgogoro to kurudia ahadi za 2005 as if hii ndio mara ya kwanza kwa JK kuwania urais-bado kuna Watanzania wenzetu wanatamani mwanasiasa huyu na chama chake warejee madarakani.Jamani,hivi Kikwete na CCM wafanye nini zaidi ili mfikie hatua ya kusema "aah sasa basi,just go away!"?

Hivi mkiweka kando ushabiki,hizi "ahadi za fotokopi" anazotoa Kikwete zilishindikana vipi kutekelezwa katika miaka yake mitano aliyokuwa madarakani?Hata kama angejitetea kuwa muda mwingi alikuwa nje ya nchi kutalii bado alikuwa na baraza kubwa la mawaziri ambalo lingeweza kabisa kutekeleza maagizo yake.

Kama mnampenda kwa dhati basi bora msimpe kura ili aweze kupumzika kwa amani kwani kumrejesha tena Ikulu hapo Oktoba ni kumbebesha mzigo ule ule uliomshinda katika miaka mitano tunayomaliza.Hii ni kwa faida yake na yenu.Na anazidi kuwaonyesha kuwa badala ya kutegemea mambo halisi kufikia malengo yaliyokusudiwa,sasa kageukia majini.Nchi haiwezi kuongozwa kwa msaada wa majini.Na kamwe Tanzania haiwezi kupiga hatua kama miongoni mwa wasaidizi wa Rais ni majini.

MPIGA KURA,SHEIKH YAHYA AMEKUPA SABABU NYINGINE KATI YA NYINGI ZILIZOPO ZA KUMNYIMA KURA YAKO KIKWETE.KURA KWA KIKWETE ITAKUGHARIMU MIAKA MITANO IJAYO AMBAPO LICHA YA UFISADI,FEDHA ZA WALIPAKODI ZITATUMIKA KULIPA FADHILA KWA MAJINI WANAOMPATIA ULINZI WAKATI HUU WA KAMPENI.

KUMBUKA JINI LIKITOKA KWENYE CHUPA HALIRUDI.IN CASE YOU FORGET,VIDEO IFUATAYO ITAKUKUMBUSHA(GENIE IN A BOTTLE)




Yesterday,the world joined Americans in remembering the 9/11 terrorist attacks which left scores dead and many others injured.The aftermath of the attacks has completely transformed global politics and rekindled hostile relations between the West and the Muslim world.Is the US,and the world in general,safer from further terrorist attacks?Is there a possibility of another 9/11 in the future (God forbid)?

Despite varying opinions on the subject,it is fair to conclude that terrorism remains the main threat to mankind to-date.Unfortunately,some of the actions taken by the Americans after the 9/11 attacks have somehow served as recruitment tools for future terrorists.The Iraq invasion,for instance,had little to do with 9/11 although George Bush and his fellow neo-cons tried their best to sell the idea,and eventually failed.Of course,it was necessary to bring an end to Saddam Hussein's evil rule,but, arguarbly,not at the cost the world is likely to pay.The invasion has most likely acted as a huge recruitment tool for terrorist in the Gulf region.Presence of the US troops in the country became an instant pull factor for terrorists from different parts of the world.

Although the US invasion of Afghanistan could be justified,mainly due to the fact that the Taliban offered a safe haven for Osama bin Laden,the alleged mastermind of the 9/11 attacks,there are growing signs that the war would ultimately be concluded without a clear victory,just as the case has been in Iraq.Worse still,Osama is still at large,and his capture-if it ever happens-would probably be by sheer luck than the US military and intelligence might.

The 9/11 terrorist attacks escalated the West-Muslim world relations, already uneasy,to  more confrontational stance.The US and other Western countries were willing to sacrifice civil liberties in the name of national security.As a result,the minority Muslim population in these countries became even more alienated as they became the prime targets of some draconian anti-terror legislations.Scores have since then been arrested and put into detention with most denied access to legal representation.The mere existence of the Guantanamo facility is a clear evidence as to how a nation many tend to turn to for global  leadership of the free world is in fact abusing civil liberties.

However,intelligence and security matters are quite complex.Actually,speaking from a professional point of view,the fact that there has never been another terrorist attack in the US should certainly be perceived as quite a success for the various organisations entrusted by the Americans to keep them safe.While such organisations are required to be vigilant 24/7,a terrorist needs only a minute if not seconds to succeed in their evil mission.

All in all,for the world to be such a nice place to live,the threat from terrorism needs to be eliminated at least to a maximum level.Unfortunately,the future does not look so promising.In some way,the West is still not doing enough to address what some objective observers regards to be the pull factors in Islamic radicalisation.I will mention a few with Tanzania being a specific case.

Many studies on Islamic radicalism have shown that poverty plays a crucial role in attracting secular Muslims to turn into Islamic extremists.My own research has so far pointed out that one of the major factor for the rise of Islamism in Tanzania is,putting it bluntly,poverty.During my fieldwork,some respondents who supported the Islamist cause in the country confirmed that their participation in various Islamist groups in Tanzania was a way to protest against the State.Such groups offered them a platform to address social and economic problems facing the country.

Tanzania has emerged as "darling of the West" despite rampant corruption and inherent social injustices.The current regime under President Jakaya Kikwete who is vying for a second term in the coming elections in October has wrecked the fragile economy while trading in dangerous grounds by promising unrealistic solutions to the grievances by the disgruntled Muslim population e.g. promising re-establishing Kadhi courts and joining the OIC.Five years later,such promises which were given during the 2005 General Election campaigns are yet to be realised,putting the country in a compromising position for possible troubles in the future.

Ironically,Kikwete has been showered with praises for his leadership,with the latest coming from the UN Secretary General,Ban Ki-Moon wishing him victory in the forthcoming election.He was also the first leader from Africa to meet President Barack Obama since he got into the White House.It is widely known in the security circles that the American interest on Tanzania is in their effort to contain a growing terrorist threats posed by various Islamist groups in Somalia.The West has turned a blind eye to what is currently happening in Tanzania just because their strategic interest in the country are far more important than the welfare of the majority of Tanzanians.Undoubtedly,Kikwete and his party will portray themselves to voters as being trusted by the West,and therefore try to win some cheap votes.

It is fair to say that the huge share of Africa's stolen wealth is in some Western financial institutions.It also makes no sense at all to see the West pouring aid to African countries when some part of such aid is either used to oppress democracy at a local level or strengthening corrupt regimes such as Tanzania's.As a result,the majority poor would readily fall victim to religious fanatics who promise heaven to them while doing their best to fill the vacuum caused by the State in provision of basic social and economic needs.

I am not calling for suspension of aid but what Africans need is transparent and responsible aid.For such aid to be effective,donor countries have to make sure that the money they offer benefit the whole population and not just a clique of corrupt politicians.The same strictness that some Western governments have shown towards recipients of stimulus packages in their countries should be applied to recipients of their aid.

Finally,as this year's 9/11 commemoration was overshadowed by  the crazy threat  by a Florida-based "twisted pastor" Terry Jones that he would burn the Holy Koran,it is worth reminding all peace-loving people of the world that replicating what the terrorists are doing will only give them further excuses to continue with their evil acts.A blank hate towards all Muslims would only encourage even those who are totally opposed to religious extremism to join forces with terrorists.

Let's work together,regardless of our faiths, to keep the world a better place to live.

9 Sept 2010

Image and video hosting by TinyPic
Waandishi Wetu
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewazuia wagombea wake wa ubunge kushiriki katika mdahalo unaoendeshwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwa kuhusisha wagombea wa vyama vyote katika kila jimbo.
Kipindi hicho kinarushwa kila Jumanne kupitia Kituo cha Televisheni cha TBC1 kwa lengo la kuwasikiliza wagombea wakijinadi pamoja na kunadi sera za vyama vyao.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa wagombea wa CCM wamezuiwa kushiriki mdahalo huo kwa barua iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa chama hicho,Yusuf Makamba kwenda kwa makatibu wa chama wa wilaya na mikoa yote nchini.

"Ninawaandikia kuwajulisha kwamba, wagombea wetu wasishiriki katika aina hiyo ya mdahalo, mpaka hapo mtakapoelezwa vinginevyo.” imesema sehemu ya barua hiyo ambayo nakala yake imepelekwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania, TBC.

Hata hivyo tayari wagombea kadhaa wa ubunge wa CCM wameshiriki kipindi hicho kilichoanza kurushwa hewani mbili zilizopita kwa kuwakutanisha wagombea ubunge wa vyama mbalimbali vya siasa nchini.

Baadhi ya wagombea ubunge wa CCM waliokwisha shiriki mdahalo huo ni pamoja na Hawa Ngh’umbi wa Jimbo la Ubungo na Chrispin Meela anayegombea ubunge katika jimbo la Vunjo.
"Kipindi hicho kimerushwa hewani kwa mara ya kwanza katika Jimbo la Ubungo Dar es Salaam na mgombea wa CCM alishiriki, sijui kwa maelekezo ya nani. Sina tatizo na kipindi. Nina tatizo na ushiriki wetu," ainasema sehemu ya barua hiyo ya Katibu Mkuu.

Katika kipindi hicho wagombea ubunge wa vyama mbalimbali huulizwa maswali na wasikilizaji na watazamaji wanahudhuria katika mdahalo huo.

Kipindi hicho kiliporushwa kwa mara ya kwanza katika Jimbo la Ubungo, mgombea wa CCM (Hawa Ngh’umbi )alipata wakati mgumu kujibu maswali ya watazamaji wa kipindi hicho na kuishia kupandwa na jazba nakutishia kumshitaki, mtu aliyemuliza swali gumu.

Katika barua yake hiyo ya Agosti 31, mwaka huu, Makamba licha ya kukitilia mashaka kipindi hicho na alihoji mgombea wao wa Ubungo alishiriki kwenye mdhahalo huo kwa maelekezo ya nani.
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa kwamba agizo hilo la Makamba limeanza kutekelezwa, juzi mgombea ubunge wa CCM katika Jimbo la Arusha Mjini, Batilda Buriania hakushiriki kipindi hicho.

Hata hivyo, Batilda alisema hakuhudhuria mdahalo wa Arusha kutokana na chama chake kutopewa taarifa na yeye ni mgombea wa CCM sio mgombea binafsi.


“Nimekuwa nikitumiwa ujumbe wa simu kuwa nimeingia mitini katika mdahalo…mimi siwezi kuingia mitini nimedhuria midahalo mikubwa tena ya kimataifa ndani na nje ya nchi siwezi kukimbia hivi sasa,”alisema Dk Batilda.

Barua hiyo yenye kumbukumbu namba CCM/OND/SG/194/9 ya Agosti 31 ambayo Mwananchi imefanikiwa kuiona, Makamba aliwaambia makatibu hao wa CCM kuwa wagombea wote wa chama hich wasishiriki kipindi hicho hadi CCM itakapotafakari kwa kina manufaa itakayopata kwa kushiriki kwao
Alisisitiza kuwa CCM ina utaratibu wake wa kujinadi na kunadi sera zake kwa wananchi ambao anaamini kuwa bado unakidhi haja.

“Tuna utaratibu mzuri wa kijinadi na kunadi sera zetu kwa wananchi; utaratibu wa mikutano ya hadhara na mikutano ya ndani. Utaratibu huo bado unakidhi haja. Tunaendelea nao,” alisema Makamba.

Akizungumza na gazeti hili jana, Makamba alisisitiza akisema: "Hatutaki. Tumekataa ndio. Sisi yetu ni mikutamo ya hadhara. Tutaeleza huko malengo, ilani yetu na sera zetu kwa wananchi. Hatuoni sababu ya kukaa katika chumba kidogo na kuwapa nafasi ya ushiriki watu wachache."

Aliendelea: "Hatuoni sababu ya kwenda kwenye huo mjadala kwa kuwa mikutano yetu ya hadhara inajitosheleza."

Alipotakiwa kueleza kama chama kitawachukulia hatua wagombea wake waliokwishashiriki kipindi hicho, Makamba alijibu: "Hakuna adhabu watakayochukuliwa kwa sababu chama kilikuwa hakijatoa maagizo."

Taarifa zilizopatikana baadaye jana zilieleza kwamba, agizo hilo la Makamba pia limepokelewa katika jimboni Karatu ambako mgombea ubunge wa CCM aliamua kujitoa kwenye mdahalo huo juzi.

Mdahalo wa wagombea wa jimbo hilo, ulipangwa kufanyika juzi katika ukumbi wa maendeleo Karatu, lakini wakati wagombea wengine wakiwa wanajiandaa, taarifa zilitolewa kuwa mgombea wa CCM, Dk Wilbard Lorry hawezi kuhudhuria.

Viongozi wa vyama vya Chadema na CUF, katika wilaya hiyo, walilalamikia kuahirishwa ghafla kwa mdahalo huo wakati walikuwa wamesitisha kampeni vijijini na kurudi Karatu.

Katibu wa CUF Wilaya ya Karatu, Stivin Siay alisema chama chao kilikuwa kimemwandaa mgombea wake kwa mdahalo huo.

“Tunashangaa kujiondoa kwa CCM katika mdahalo huu kumesababisha mdahalo kuahirishwa…,” alisema Siay.

Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Karatu, Moshi Darabe alisema walipata taarifa za kuahirishwa mdahalo huo dakika za mwisho kwa maelezo kuwa mgombea wa CCM hatahudhuria.

Alisema taarifa hizo kwanza zilipatikana ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, ambao ndio awali walitoa taarifa za kuwepo maombi ya TBC kuandaa mdahalo huo.

Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Karatu, Clemence Berege akizungumzia kuahirishwa kwa mdahalo huo alisema kwamba, ofisi yake haihusiki kwani waliotaka kuendesha mdahalo huo ni TBC.

Habari hii imeandaliwa na Mussa Juma, Arusha na Exuper Kachenje

Chanzo: Mwananchi


8 Sept 2010

Image and video hosting by TinyPic
Josephine Mushumbusi, amezungumza kupitia Mwanasheria Mkuu wa Chadema, ambaye pia ni wakili wa Dk Willibrod Slaa, Tundu Lissu, akaviambia vyombo vya habari kuhusu tuhuma zinazowakabili yeye na Dk. Slaa kuwa kwa mara nyingine, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimerejesha mfumo wa uchaguzi unaobadilishwa kuwa mfumo ya kijinga (a silly season). Akasema kwamba CCM wamekuwa wakikishambulia Chadema kuwa ni chama Wachagga; kwamba baadhi ya viongozi wake ndio walimuua Chacha Wangwe; na kwamba Dk Slaa ametumwa na kanisa Katoliki kugombea urais; lakini baada ya kuona hadithi hizo zimepuuzwa, sasa wameibuka na suala jipya na “ndoa za Dk. Slaa” wakidhani zitawasaidia kugeuza macho ya umma kutoka kwenye masuala muhimu ya wakati huu.

Akasema CCM hawataki Dk. Slaa na Chadema wajadili wizi, ubadhirifu wa fedha na mali za umma; hawataki wajadili wizi wa Sh. bilioni 772 zilizoibwa katika mwaka 2008/9 tu, kwa mujibu wa ripoti ya Mkaguzi na mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali; hawataki Chadema itaje majina ya wezi wa Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT); hataki Chadema wajadili jinsi JK na rafiki zake, akina Edward Lowasaa, Nazir Karamagi, Andrew Chenge na Rostam Azizi walivyofilisi taifa hili; hawataki Chadema ijadili madai halali ya wafanyakazi wa Tanzania na ahadi za ‘maisha bora kwa kila Mtanzania.’ CCM hawataki Chadema kijadili sera mbadala ambazo zinalenga kuwakomboa Watanzania kutoka lindi la umaskini.

Wanataka kulielekeza taifa zima katika kujadili masuala ya ‘chumbani’ kwa Dk. Slaa; analala na nani, ana wake wangapi, kawapata wapi na kadhalika; ili kwa kufanya hivyo mgombea wao awarubuni wananchi kwa ziara mikoani na ahadi kemkem zisizotekelezeka.

Tundu Lissu amesisitiza kuwa kila wanapoona wamebanwa, CCM huwa wanabuni njama za kukomoa washindani wao, kama walivyofanya huko nyuma. Alitoa mifano ya kilichotokea miaka ya 1995 na 2005.

Mwaka 1995: Kwa kumwogopa Mrema aliyekuwa tishio kwa CCM, walimtumia mwanamke mmoja, aitwaye Angelina, wakidai ni kimada aliyezaa na Mrema; akawa analala getini kwa Mrema, Masaki, Dar es Salaam. Wakamdhalilisha. Baada ya uchaguzi, Mrema akashindwa, na suala la Angelina halikujadiliwa tena.

Mwaka 2005 tishio la CCM ilikuwa Chama cha Wananchi (CUF), hasa Zanzibar. CCM wakamtumia Inspekta Jenerali wa Polisi, Omar Mahita, siku chache kabla ya uchaguzi, kudai kuwa amekamata lori lenye mapanga, majambia, visu na silaha nyingine zenye nembo ya CUF. Wakakipaka chama matope. Baada ya uchaguzi, hatukuelezwa lolote kuhusu visu hivyo.

Mwaka huo huo, katika uchaguzi wa ndani ya chama, baada ya kundi la JK kuona limezidiwa mno, likaamua kumzushia Dk. Salim Ahmed Salim likidai ni Mwarabu, na muuaji wa Rais Abeid Amani Karume. Wakamhujumu, Na baada ya uchaguzi hawakuzungumzia tena uarabu wa Dk. Salim.

Mwaka 2010: Tishio la CCM ni Chadema na Dk. Slaa. Baada ya kuona upepo unawaendea vibaya, CCM wameamua kufanya siasa za mtaro wa maji taka; hizi wanazotumia watu kumwandama Dk Slaa.

Tundu Lissu alisema kuwa Chadema hawako tayari kufanya siasa za majitaka; na kwamba Watanzania hawako katika kujadili mambo hayo, kama hali ya afya za wagombea, ambao baadhi wanadaiwa kuwa na virusi vya ukimwi kiasi cha kubadili damu kila baada ya miezi, na kwamba kwa sababu ya unyonge huo, baadhi yao waanguka mara kadhaa jukwaani.

Akasema wao hawatazungumzia baadhi ya wagombea urais wana wake wangapi, mahawara wangapi, na wamewaweka katika ofisi gani za umma, wapi wamepewa mikataba minono ya fedha kwa upendeleo, na kadhalika. Akasisitiza kwamba Chadema haitajibu uchafu unaosambazwa na vyombo vya habari, lakini akasema, “sauti yetu itasikika iwapo wataenda mahakamani.”
Akasema Chadema itazungumzia umaskini wa Watanzania na namna ya kuupunguza au kuuondoa; jinsi Tanzania ilivyo nchi ya tatu katika Afrika lakini wanakijiji wanalazimishwa kujenga shule za kata huku serikali ikifuja mabilioni ya pesa (kama hizo bilioni 772/- zilizotafunwa ndani ya mwaka mmoja.

Akasema Chadema itajadili malipo ya anasa kwa mawaziri, maisha duni ya polisi, walimu, wauguzi na makundi mengine yanayonyonywa katika jamii. Akasema Chadema itajadili jinsi ya kuboresha afya za wananchi.

Akasema, “hatutaki siasa za chumbani, bali za hadharani.”

Kwanini wamshambulie Dk Slaa? Kwa sababu ni Dk. Slaa.

- Ana rekodi ya kuwashinda CCM mara tatu, kwa miaka 15 mfululizo
- Amekuwa sauti kuu ya wananchi Bungeni, inayotetea masilahi ya umma
- Kuliko kiongozi yeyote aliyewahi kuwapo Tanzania ndani ya miaka 50, ni Dk Slaa pekee aliyetaja hadharani mafisadi 11 bla woga wowote. Walioathirika kwa ujasiri wake ndio hao wanaomsakama sasa kwa mambo ya chumbani badala ya mambo ya hadharani.


7 Sept 2010


Picha na Habari: Daily Mail

6 Sept 2010



Balozi Mpya wa Tanzania nchini Uingereza Mh Peter Kallaghe aliwaalika Watanzania na kuftari pamoja nyumbani kwake jumamosi tarehe 04.09.10. Baada ya kuftari Mh Kallaghe alijitambulisha na kuwashukuru Watanzania wote waliofika nyumbani kwake. Pia aliahidi kuwa karibu na Watanzania.
Urban Pulse Creative Imewaletea video ya tukio hili. 


From:
Mr. Ban Ki-Moon
To: [email protected]
Eco Bank Compensation unit, maro militaire Boulevard
St Michel face Fedas Building Plot 433, YAYI BONI
Crescent Asokoro District Cotonou Benin republic
P.O. Box 280, Cotonou.
In affiliation with the United Nations
Send a copy of your response to official

Contact person Mr. Traval Cheick
Email: [email protected]
Director Eco Bank Benin plc
Direct Line: +22998717333 Fax: +22998717337

ATTN: Sir / Madam,

How are you today, Hope all is well with you and family? You may not understand why this mail came to you. In regards to the recent meeting between the United Nations and the Present United States Government to restore the dignity and Economy of the Nations Base on the Agreement with the World Bank Assistance to help and make the world a better place for all with the sole aim of abolishing poverty.

We have been having a meeting for the passed 7 months which ended 2 days ago with the then secretary to the UNITED NATIONS.


This email is to all the people that have been scammed in any part of the world, the UNITED NATIONS have agreed to compensate them with the sum of $1.500.000.00 {One Million Five Hundred Thousand United States Dollars} This includes every foreign contractors that may have not received their contract sum, and people that have had an unfinished transaction or international businesses that failed due to Government problems etc.


Your name and email was in the list submitted by our Monitoring Team of Economic and Financial Crime Commission observers and this is why we are contacting you, this have been agreed upon and have been signed.

You are advised to contact Mr. Traval Cheick of Eco BANK BENIN PLC, as he is our representative in Benin, contact him immediately for your ATM master card of {$1.5Million} This funds are in a ATM Master Card for security purpose ok? So he will send it to you through Courier Company of your choice.

This meeting was first held on the 8th of April 2003. You can view this page for your perusal: 

http://www.un.org/News/Press/docs/2003/ik344.doc.htm

Therefore, you should send him your full Name and telephone number/your correct mailing address where you want him to send your ATM Master Card immediately:

Contact: Mr. Traval Cheick 
Director Eco Bank Benin plc
Phone: +22998717333 Fax: +22998717337

Good luck and kind regards,
Making the world a better place


Mr. Ban Ki-Moon

Secretary (UNITED NATIONS)

http://www.un.org/sg/

5 Sept 2010


Courtesy of NGURUMO


Kuna msemo wa Kiingereza usemao "unchallenged,a lie often assumes a status of truth",yaani uongo usipokabiliwa unaweza kupata hadhi ya ukweli. Msemo huu unaweza kuwa na umuhimu wa kipekee kwa mgombea wa tiketi ya urais kupitia Chadema,Dokta Wilbroad Slaa.Tangu atangazwe kuwa mgombea wa chama hicho,kumekuwa na mashambuli lukuki yanayoelekezwa kwake katika jitihada za kuifanya jamii imwone kuwa mchafu na asiyefaa kumrithi Jakaya Kikwete,mgombea kwa tiketi ya chama tawala CCM.

Ni dhahiri kuwa wanaoeneza sumu hiyo dhidi ya Dkt Slaa wanafanya hivyo kwa malengo makuu mawili.Kwanza,kama nilivyobainisha hapo juu,ni kumfanya aonekane hafai kuwa rais wa Tanzania.Aonekane hafai,kisha akose kura za kutosha kumwingiza Ikulu,na mafisadi waendelee kuvuna wasichopanda katika nchi yetu iliyogeuzwa shamba la bibi.

Lakini la pili ni kupoteza malengo au kwa ufasaha ku-divert attention.Yaani wanachotaka ni Dkt Slaa na Chadema waanze kuhangaika kujibu shutuma,jambo ambalo litawapunguzia muda na focus ya kampeni.Yaani badala ya mgombea huyo kuwashawishi Watanzania atawafanyia nini,mafisadi wanataka aanze jukumu la kujitetea kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwake.

Wapo wanaoshauri kuwa dawa ya kudili na tuhuma ni kuzipuuza.Kuna wakati mkakati huo ni mzuri lakini hilo linawezekana katika aina flani ya jamii.Katika jamii yetu ambapo bado asilimia kubwa ya watu wananyimwa uhuru wa kujua ukweli na kuchanganua mambo,uongo usiokanushwa unaweza kabisa kuchukua nafasi ya ukweli.Na ukidhani nachoandika hapa ni hisia zangu tu basi rejea zengwe aliloundiwa Dokta Salim Ahmed Salim alipotangaza dhamira yake ya kugombea urais mwaka 2005.Kikwete na wanamtandao wenzake walimwaga sumu kubwa dhidi ya Dkt Salim hadi wakafanikiwa kumdhibiti.Jitihada zake za kujisafisha hazikuweza kufua dafu kwa character assassination strategy ya wanamtandao.

Ikumbukwe kuwa tunaishi katika jamii iliyolazimika kutegemea umbea na tetesi kubashiri ukweli.Haya ni baadhi ya matokeo ya mfumo dhalimu wa chama kimoja ambapo mambo pekee yaliyopaswa kufahamika kwa umma ni yale yaliyoonekana mazuri kwa watawala.

Kadhalika,kinachotokea kwa Dokta Slaa ni sehemu ya uchafu unaoambatana na fani ya siasa (politics is a dirty game).Huko Marekani,baada ya Barack Obama kuonekana ana nguvu za kumpeleka Ikulu,zilianza kampeni chafu kuhusu imani yake ya dini ikidaiwa alikuwa Muislam (kana kwamba Uislam ni sawa na uhaini nchini humo).Baadaye wakamzushia kuwa sio raia wa Marekani.Timu ya Obama haikukaa kimya bali ilipambana kwa nguvu dhidi ya kampeni hizo chafu na hatimaye Obama akafanikiwa kuingia Ikulu.

Chadema na Dokta Slaa wanaweza kuamua kuwapuuza wanaoeneza sumu kali dhidi yao.Lakini kwa namna hali ilivyo ambapo vyombo vya serikali (vinavyoendeshwa kwa fedha za walipa kodi) kama gazeti la Habari Leo vinapojiunga na kampeni hizo za siasa za maji taka basi ni muhimu kukabiliana nao mapema.

Na kwa kuanzia,nadhani kuna umuhimu wa kulichukulia hatua gazeti la Habari Leo hususan pale lilipoandika "Dokta Slaa padri msomi".Sentensi hiyo ilikuwa na lengo la kumkosesha mgombea huyo kura za wasio Wakatoliki.Ni dhahiri sentensi hiyo ililenga kuendeleza kashfa kuwa Dokta Slaa ni kiongozi wa dini na anataka kuingia Ikulu kuwatumikia Wakatoliki/Wakristo na sio Watanzania wote kwa ujumla.Kulipeleka gazeti hilo kwa Baraza la Habari ni kupoteza muda kwa vile sana sana wataishia kupewa onyo tu.Wanachostahili sio onyo bali adhabu kali ya kuwakumbusha kuwa wanatumia vibaya fedha za walipa kodi kwa maslahi ya watu binafsi.Ni mafisadi kama wale wa Kagoda au Richmond.

Sijui sheri za Tanzania zinasemaje kuhusu super injunctions zinazokataza kuzungumzia maisha ya mtu binafsi.Hapa Uingereza baadhi ya watu maarufu wamekuwa wakizitumia taratibu hizo za kisheria kuwabana vimbelembele wanaoishi kwa kuchokonoa maisha ya wenzao.Naamini Chadema wana wanasheria mahiri wanaoweza kuangalia namna ya kukabiliana na wazushi hawa wanaofadhiliwa na mafisadi.

Blogu hii inatoa wito kwa Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla kutokalia kimya uhuni huu ambao pasipo kudhibitiwa unaweza kabisa kuathiri matokeo ya uchaguzi.Hatuhitaji kujiuliza kwanini wamwandame Dkt Slaa pekee na sio wagombea wengine kwani rekodi yake dhidi ya mafisadi ni siri iliyo wazi,na hofu kubwa ya wanaoeneza sumu dhidi yake ni kuwa akiingia Ikulu itawalazimu watafute mahala pa kujificha.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.