17 Nov 2010

• RIPOTI MPYA YA UNDP YAANIKA KILA KITU

na Tutindaga Mwakalonge

SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limetoa ripoti yake ya hali ya maendeleo duniani inayoichambua Tanzania kuwa moja ya nchi zilizo nyuma sana kimaendeleo kwa kuwa na watu wengi wanaokabiliwa na umaskini.

Ripoti hiyo inayopima maendeleo ya nchi husika kwa kutazama maendeleo ya watu wake ilizinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam jana na kuitaja Tanzania kuwa nchi ya 148 kati ya nchi 169.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, katika kila Watanzania mia moja, 36 wanaishi katika hali mbaya sana ya umaskini, sawa na asilimia 36 ya watu wote, milioni 41.3.

Pia ripoti hiyo ya kimataifa imeonyesha kuwa katika kila Watanzania mia moja, 97 wanaishi kwenye umaskini wa kipato wa chini ya dola 2 za Marekani kwa siku, sawa na chini ya takriban sh 2,000 za Kitanzania kwa siku.

Aidha, ripoti hiyo iliyobeba kauli ya ‘Utajiri halisi wa mataifa’, imeonyesha kuwa katika kila Watanzania mia moja, 89 wametajwa kuishi chini ya dola moja ya Marekani kwa siku.

“Kwa takwimu hizo, Watanzania wengi wako katika umaskini wa kutisha kwa sababu ya kuwa na uwezo duni wa kifedha wa kumudu maisha yao ya kila siku”, alifafanua mtaalamu mmoja aliyehudhuria uzinduzi huo.

Hata hivyo, pamoja na takwimu hizo, Wizara ya Fedha na Uchumi, kupitia kwa Katibu wake, Ramadhani Khijjah, iliendelea kusifia mwenendo wa ukuaji wa uchumi nchini huku ikidai kuwa sekta za elimu na afya zimekuwa zikichochea ukuaji wa uchumi.



You can't access the internet. And it doesn't have a camera or games you can play.In fact, this new mobile phone doesn't even let you send text messages.The designers of 'John's Phone' have created a device that has only one function: it lets you make calls.Hailed as the world's simplest phone, it is designed to be a tongue-in-cheek 'basic backlash' by targeting users who do not want the flashy features of next-generation models.

Dubbed the 'anti iPhone', the £67 device with a brightly coloured facade and big buttons resembles a toy.
The phone's Dutch makers, advertising agency John Doe, are hoping it will be a hit with technophobes and children buying their first phone.The manual is only one page long and, unlike its battery-hungry smartphone counterparts, the makers of 'John's Phone' claim that a single charge will provide users with three weeks' battery life.Even the phone's 'built-in' address book is old-fashioned - concealed behind a flap at the rear of the phone, it's a physical pen-and-paper notepad used to store your contacts.
For those in a rush, the device does have the ability to record ten speed dial numbers.The phone's designers wanted the phone to have 'no frills and no unnecessary features such as a camera, text messaging and an endless number of ringtones'.

Designer Diedriekje Bok said: 'At a time when there is an abundance of choices and oppressive channels, we wanted to develop a simple gadget.

'It is also a useful phone while travelling, exercising or weekend sailing.

'You always reach for your close family and friends, so John's Phone is for when the rest of the world does not matter.'

It remains to be seen whether all mobile phone users will be rushing to swap their hi-tech phones for this new, pared-down model just yet.

Customer Ben Reed, 24, from Preston, said 'I think it looks quite cool. The design is stylish and I like the simplicity of it.

'But I don't know if I could use it instead of my current phone. I rely on it to coordinate my social life, keep an eye on my work e-mails and to follow news updates online.

'I can see how this phone might be good for old people or very young kids, though


TANGAZO MAALUM



Utawala na wafanyakazi wa URBAN PULSE wakishirikiana na Tanzania Community Europe wanapenda kuwatangazia washabiki wote wa Diamond UK na watu wote wanao support kampeni ya vita na Malaria ya kuwa kuna mabadiliko ya lazima yaliyotokea kuhusu show ya Diamond ya tarehe 27 November Birmingham. Kwamba kutokana na idadi kubwa ya watu wanaotegemea kujitokeza siku hiyo imebidi ukumbi ubadilishwe ili uweze kukidhi idadi yao,Kwa hiyo jambo hili limepelekea ulazimu wa kubadilisha kumbi kwenda

27 November 2010
116 GAR GOSFORD STREET
PALMS BAR
COVENTRY
CV1 5 EA


Mabadiliko haya ni ya lazima na tunaomba radhi kwa ufumbufu wowote utakojitokeza

WOTE MNAKARIBISHWA

Utawala
URBAN PULSE


16 Nov 2010


Springburn, Glasgow
Tillydrone,Aberdeen
Gallowgate, Glasgow



BONUS TRACKS FROM UK'S FINEST (BELOW)

Griminal -Supa Dupa


Marvell- We Know


I really like music,hip-hop to be specific.One of my teenage dreams was to become a music producer (inspired by Dr Dre and old pal Profesa Ludigo), had I not indulged myself into academics.A day late and a dollar short,I suppose!

Talking of Dr Dre (above), HERE is some good news about the eagerly-awaited Detox album.Click HERE to listen to a leaked track "KUSH" featuring Snoop Dogg and Akon.


Enjoy Dre's old tune "Been there Done that"





Jadden and his Dad Will in The Pursuit of Happyness



Jada as Stoney in Set It Off




Willow's hit song Whip My Hair


Husband and Dad Will Smith the actor


...and Will Smith the rapper




Last year it was Rage Against The Machine - this year a rap song selling milk is set to challenge The X Factor winner for the coveted Christmas No 1 slot.

The music from the Yeo Valley advert - which features four rustic rappers 'bigging up' the West Country dairy's products - has become hugely popular since it was first shown during the show's commercial breaks.

The Sunday after it was first aired it went on to be featured as a 'top trend' on You Tube's home page - and since then has been watched online 1.5million times.

Unlikely rappers: The rustic foursome from the Yeo Valley adverts could soon be enjoying chart success
The advert sees the unlikely rap stars dressed in flat caps and wellies, and features the lyrics 'rollin' with my Massey on a summer's day' - in reference to the quartet's tractor.

It was made by Los Angeles based director Julien Lutz, who has made music videos for a host of stars including R Kelly, Usher, Kanye West and Nelly Furtado.

Among the 'rappers' in the advert is 21-year-old Alexandra Evans, who was the winner of the fourth series of Britain's Next Top Model.

Model rapper: Former Britain's Next Top Model winner Alexandra Evans features in the commercial
'I'm really surprised so many people like it,' she said of the song. 'Getting the Christmas No 1 is a long shot but who knows?'

Yeo Valley, which is based in Somerset, has committed to showing the commercial exclusive during breaks in The X Factor, at a cost of £5million.

The track was released for download via iTunes due to public demand, after Facebook groups calling for its release were set up and fans took to Twitter to air their views.

The Massey massive: The rappers pay tribute to their tractor in the tongue-in-cheek track
Among those who have shown their support for the track are Radio 1 DJ Zane Lowe, who is known as a champion of new music.

'Must be intimidating for The X Factor finalists to have to compete with the infinitely better Yeo valley crew each week,' he recently said on his Twitter page.

A spokeperson for the dairy added, 'It's not your usual chart topper but the positive response from the public suggests people want to hear it in the top 40.'

Dairy good: The track could pose an unusual threat to The X Factor winner for the Christmas No 1 spot
However the song is not the only one which is being championed to reach the top spot in the Christmas chart, with a number of campaigns popping up on Facebook.

Several pages have emerged to push the Sixties hit Surfin' Bird by The Trashmen, which was made famous by the film Full Metal Jacket, while there are growing campaigns to see Rick Astley's Eighties hit Never Gonna Give You Up and Meat Loaf's Bat Out Of Hell at number one for Christmas.

Also gathering momentum is the four and a half minute silent track by John Cage, which some Facebook fans have dubbed 'Cage Against The Machine' in reference to last year's Christmas campaign on the social networking site.

That one saw Rage Against The Machine's Killing In The Name deprive 2009 X Factor champion Joe McElderry of the festive chart-topper with his winner's single The Climb.

14 Nov 2010

Image and video hosting by TinyPic
The man himself.The Haymaker.A professional KO (Knock Out) Artist.A handsome assassin

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic
David Haye akitoa kichapo cha nguvu

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic
Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Machampioni wa zamani.Lennox Lewis (kushoto) na Frank Bruno.Wote ni Waingereza
Picha kwa hisani ya magazeti ya The Guardian na The Daily Mail

12 Nov 2010


Raymond Kaminyoge
TANGU Machi mwaka jana alipostaafishwa kazi na Rais Jakaya Kikwete, akiwa Mkuu wa Wilaya ya Mbalali, Mbeya, Hawa Ngulume amekuwa haonekani hadharani wala kusikika kwenye vyombo vya habari kama tulivyomzoea.

Tunakumbuka jinsi alivyoendesha operesheni ya kuwaondoa wafugaji katika Bonde la Ihefu wilayani humo na kusababisha habari zake kutawala kwenye vyombo vya habari na kusababisha malumbano makali kati ya wafugaji na wanamazingira.

Tunakumbuka pia alivyoendesha operesheni hiyo kwa yeye mwenyewe kutembea kwa miguu akisindikiza ng’ombe kuondoka kwenye bonde hilo hali iliyomfanya achukiwe na wafugaji hao lakini akapendwa na wanamazingira.

Tunashuhudia hivi sasa baada ya kuondoka kwa wafugaji kwenye bonde hilo, hali mazingira ni shwali kwani ukijani na uoto wa asili umeanza kurejea katika bonde hilo.

Hayo aliyafanya akiwa mkuu wa wilaya ya Mbalali kabla hajastaafishwa na kumpisha mwenzake Luteni Cosmas Kayombo.

Hayo yote yanakumbukwa na Ngulume, ambaye hivi sasa yuko katika hali mbaya kiafya nyumbani kwake Goba Kinzudi, jijini Dar es Salaam akisumbuliwa na maradhi ya vichomi na mapafu.

Hata hivyo, bado madaktari hawajathibitisha ni nini hasa kinachomsumbua kutokana na kukosekana kwa kipimo mbadala cha kupima kansa ya mapafu.

Mwananchi lilifika nyumbani kwake na aliamua kueleza yaliyokuwa moyoni mwake: “Nimeona bora nitumie chombo cha habari kufikisha ujumbe wa ugonjwa kabla sijafa.”

Anaongeza: “Kwa miezi mitatu sasa niko hoi kitandani, siwezi kutembea bila kusaidiwa, naiomba serikali inisaidie niweze kwenda India ambako kuna vipimo na tiba ya maradhi yanayonisumbua.”

Anasema ameamua kutumia gazeti hili ili kufikisha ujumbe kwa serikali na CCM kuhusu maradhi yanayomsumbua baada ya njia nyingine kushindikana.

“Nilipeleka taarifa kwenye chama changu kwamba naumwa nahitaji msaada, lakini sikujibiwa, pia nimefanya juhudi za kutaka kumwona Waziri Mkuu ili anisaidie lakini juhudi zangu hazikuzaa matunda, nimeamua nitumie chombo cha habari kabla sijafikwa na mauti,” anasema.

Ngulume ambaye ni kada maarufu wa CCM aliyetumikia nafasi ya ukuu wa wilaya kwa miaka 18, anasema maradhi yanayomsumbua yalianza baada ya kumalizika kwa mchakato wa kura za maoni za chama hicho.

Anasema aliomba ridhaa ya chama hicho kimsimamishe kuwa mgombea ubunge katika Jimbo la Singida Mjini lakini hakufanikiwa.

“Katika mchakato ule, Mohammed Dewji alishinda na mimi nikawa mshindi wa pili, niliporudi Dar es Salaam nikaanza kujiandaa kwenda kumpigia debe Dewji, kama ulivyo utaratibu wa chama chetu, ndipo nikaanza kuumwa ghafla,” anasema na kuongeza:

“Nilipenda kushiriki kwenye kampeni ili kuwasaidia wagombea mbalimbali wa chama changu lakini anadhani Mungu hakupenda nifanye hivyo.”

Ngulume ambaye amewahi kuwa mkuu wa wilaya mbalimbali zikiwemo za Kinondoni, Bagamoyo na Kibaha anasema baada ya kuumwa amekuwa akipata tiba za aina tofauti lakini hazijamsaidia.

“Nasikia maumivu makali tumboni, utadhani kuna msumeno unakata viungo vyangu, usiku kucha sipati usingizi ni maumivu tu ndiyo yanayotawala mwili wangu,” anasema.

Anasema amekwishatibiwa kwenye Hospitali za Lugalo, Ocean Road na Imtu zote za Dar es Salaam lakini mbali ya kutopata nafuu, hali yake inazidi kuwa mbaya siku hadi siku.

“Katika hospitali ya Ocean Road nilitakiwa kupima kama mapafu yana maji ili kuthibitisha kama ni kansa ya mapafu lakini kipimo kilichopo kinatakiwa kukaa katika kinywa nami sina pumzi, hivyo ikashindikana kupima,” anasema.

Anaongeza kuwa hadi sasa hawezi kuweka wazi kuhusu maradhi yanayomsumbua kwa vile vipimo mbadala ya vile vya kuwekwa katika kinywa vinapatikana nje ya nchi.

“Ndiyo maana naomba msaada wa kwenda kutibiwa nje kwani nikipimwa ndipo naweza kupata tiba ya uhakika,” anasema kwa taabu.

Anasema katika kuhangaika kutafuta tiba aliwahi kwenda katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili lakini cha kushangaza alikaa kuanzia saa 8.00 mchana hadi saa 11.00 jioni bila kuhudumiwa.

“Ndipo mtu mmoja anayenifahamu alipopita nilipoketi akanisalimia kwa kuniita mheshimiwa. Muuguzi mmoja jina ninalihifadhi akaja kutaka kunihudumia, nikamwambia ina maana siwezi kuhudumiwa hadi niwe mheshimiwa? Nikaondoka kwa hasira nikakataa kuhudumiwa,” anasema.

Siku moja baada ya kuzungumza na gazeti hilo, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (Tamisemi) aliyokuwa akifanya kazi chini yake ilitoa tamko la kusimamia matibabu yake nje ya nchi.

Ujumbe wa maofisa wa Tamisemi ulifika nyumbani kwa mkuu huyo wa zamani wa wilaya kumjulia hali. Hatua hiyo imekuwa faraja kwa Ngulume ambaye anasema ingawa bado ana maumivu makali, amefurahi kwani kuna maofisa kutoka Tamisemi waliomtembelea na kumpa matumaini kwamba huenda akaenda nje kutibiwa.

“Baada ya gazeti lenu kuandika habari zangu, ujumbe wa Tamisemi umefika nyumbani kwangu kuniangalia na kuniahidi kwamba utafanya mipango kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ili niweze kwenda nje kutibiwa,” alisema.

Alisema mbali na ujumbe huo, watu wengi ambao hawakuwa na taarifa zake, wameanza kumtembelea na wengine kumpigia simu wakimuombea kwa Mungu ili aweze kupona maradhi yanayomsumbua.

“Nawashukuru waandishi wa mwananchi, kwani nyie ndiyo mlioujulisha umma kuhusu hali ya afya yangu, ninaomba kwa Mungu usiku kucha ili niweze kufanikiwa kutibiwa kwani maumivu ninayoyapata ni makali.

CHANZO: Mwananchi


UPDATE: Soma "utetezi" wa serikali HAPA

10 Nov 2010


Muungwana mmoja amenitumia comment ambayo kwa hakika imenigusa sana.Naomba niinukuu
Mbona umekatisha mijadala ya kuendeleza nchi ghafla mno. nilitegemea utakuwa na tasmini ya matokeo ya uchaguzi lakini umezimika ghafla. Vipi au jamani inakuwaje uchungu na nchi unakuwa kwa muda tu? Au wameshakutishia na wewe?
Naelewa kwanini mzalendo huyu anataka tufanye tathmini ya uchaguzi mkuu ambao wengi wetu tuliupa umuhimu wa kipekee kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo huko nyumbani.Baada ya kushuhudia taifa likienda mrama kwa kugubikwa na ufisadi ilionekana ni lazima Watanzania wenye uchungu wa dhati kwa nchi yao wachukue hatua zinazostahili.Na hatua mwafaka ilionekana kuwa ni kuing'oa CCM madarakani.

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dkt Wilbroad Slaa,ameweka bayana msimamo wake kuwa uchaguzi huo ulichakachuliwa.Baadhi ya taasisi zilizotuhumiwa kufanya uchakachuaji huo zimejitokeza hadharani na kukanusha tuhuma hizo.Haihitaji hata cheti cha kozi ya siku 1 ya uchambuzi wa siasa kumaizi kuwa hakuna hata mmoja kati ya wanaotuhumiwa atakiri mchango wake katika kuirejesha CCM madarakani.Wakubali ili waadhibiwe?

Kadhalika,kuna dhana iliyojengeka kuwa katika uhalisia barani Afrika na katika baadhi ya nchi "za dunia ya tatu" sio rahisi kwa chama tawala kushindwa uchaguzi,na ikitokea kimeshindwa basi yayumkinika kuhitimisha kuwa hayo ni matokeo ya uzembe wa chama husika au migogoro ndani ya chama hicho.Hebu chukulia mfano mazingira ya uchaguzi wetu.Vyombo vya dola vilionyesha waziwazi kuipendelea CCM huku watendaji wa taasisi zinazopaswa kuwa huru wakijibidiisha kumlinda mgombea wa chama tawala.Ndio maana haikumtia hofu Mhariri wa Daily News,gazeti linaloendeshwa kwa kodi za walalahoi,kutamka bayana kuwa Dkt Slaa asingeweza kuwa rais hata baada ya miaka mitano.Kujiamini huko hakukutokana na uimara wa CCM bali ndoa ya kifisadi kati ya taasisi za umma na chama hicho tawala.

Tulisikia taarifa kadhaa kuhusu watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutowatendea haki wagombea wa vyama vya upinzani.Kadhalika,ilifika mahala Msajili wa Vyama vya Siasa akaamua kuweka wazi mahaba yake kwa CCM na kujipachika jukumubla kuitetea hata pale ilipokosea waziwazi.

Sasa unaweza kujiuliza,"kama tulishaona mwenendo wa aina hiyo ie wa kuitengenezea CCM mazingira ya ushindi,kwanini tulijipa matumaini kuwa Dkt Slaa angeibuka mshindi?".Jibu rahisi kwa mtizamo wangu ni kwamba kulikuwa na matumaini kuwa sauti kubwa ya umma ingeweza kukwaza jitihada zozote za uchakachuaji.Au hata kama jitihada hizo zingefanyika basi zingezidiwa nguvu na sauti hiyo ya umma.

Naomba kukiri hadharani kuwa hofu yangu kubwa haikuwa kwenye mikakati ya kundi dogo lakini lenye nguvu kubwa la mafisadi bali MTAJI MKUU WA CCM yaani umasikini wa Watanzania walio wengi.CCM inategemea sana masikini na hata matokeo "halali" yanathibitisha hilo ambapo maeneo yaliyogubikwa na umasikini ndio yaliyoipa CCM kura nyingi.Huu ni uhusiano ambao kitaaluma unaweza kuelezwa kama wa mnyanyasaji na mnyanywasaji (abuser-abused relationship).Mnyanyasaji anawekeza nguvu nyingi kumwaminisha mnyanyaswaji kuwa pasipo uwepo wake (mnyanyasaji) basi mnyanyaswaji hatakuwa na maisha.Ndio hadithi za amani na utulivu,umoja wa kitaifa,mshikamano,na madude mengine kama hayo.

Kitaaluma,mnyanyaswaji anaweza kufikia mahala akawa anaskia raha kunyanyaswa (punch drunk).Ni kama hali ya kuzowea makonde kwa bondia.Hakuna maelezo mengine mwafaka ya kuelezea namna watu wanaoamka wakiwa hawajui siku iyaisha vipi,wanaotembea maili kadhaa kusaka maji safi japo wafadhili wanamwaga fedha za miradi ya maji,wanaoshinda juani kutwa nzima na kulala vibambazani wakiuza peremende lakini bado wanaandamwa na jeshi la mgambo huku polisi wakiwawinda wawabambikizie kesi,wanaokwenda mahospitalini na kuambulia matibabu hewa kwa vile hakuna madawa,watu wenye watoto ambao makalio yanaota sugu kwa kukaa sakafuni mashuleni,watu ambao haki zao hazipatikani bila kutoa "kitu kidogo" kisha watu haohao wakipigie kura chama kinachostawisha mateso yao.

Na kwa waliodhani akina sie tuliokuwa tukipiga kelele za nguvu kutaka CCM iondoke tulikuwa na chuki binafsi basi matukio mawili yaliyojiri hata masaa 72 hayajapita baada ya CCM kurejea madarakani yanapaswa kuwafumbua macho.Tukio la kwanza ni la mtuhumiwa wa ufisadi wa rada,Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge kuchukua fomu ya kugombea Uspika kisha kufanya press conference iliyojaa ngebe,nyodo na dharau kwa wote wanaokerwa na ufisadi.Binafsi,naamini kuwa Chenge katumwa na kundi flani linalotaka kuifakamia keki ya taifa kwa kasi ya marathon hasa kwa vile wanaelewa kuwa Awamu hii ya Tano inaweza kuwa ni lala salama.Chenge ameonyesha bayana kuwa anataka kuwa Spika ili kusafisha majina ya "waliosingiziwa kuwa mafisadi".

Lakini kubwa zaidi ni hisia zangu kuwa Chenge ana baraka kamili za uongozi wa juu wa CCM ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti Jakaya Kikwete.Si bado tunakumbuka jinsi Kikwete alivyokwenda jimboni kwa Chenge kumpigia debe na kisha akatetea uamuzi wake wa kuwapigia debe watuhumiwa wa ufisadi kwa kudai kuwa kinachowakabili ni tuhuma tu.Kama tuhuma si tatizo mbona Bashe aliondolewa kwenye mchakato wa mchujo wa kupata wagombea ubunge kwa tiketi ya CCM kwa tuhuma kuwa sio raia wa Tanzania?Kwahiyo tuhuma kwa Chenge,Mramba,nk zinapaswa kubaki tuhuma tu lakini kwa wengine tuhuma ni sawa na hukumu!

Na kwa wanaidhani Chenge anafanya utani mbaya ( a bad joke) basi labda hawaielewi CCM vizuri.Chenge anaweza kabisa kupitishwa katika mfumo wa "kidemokrasia" wa CCM.Yea,kama ameendelea kuongoza kamati ya maadili ya chama hicho na kupitishwa kugombea ubunge (na kushinda) iweje basi kuukwaa uspika liwe suala gumu?Nguvu anayo,sababu anazo,sapoti anayo na VIJISENTI anavyo.Kipi cha kumzuwia kumrithi Samuel Sitta?

Tukio la pili linahisiana na hilo la kwanza ambapo Taasisi ya Kuzuwia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imekurupuka na kudai kuwa Chenge alishasafishwa katika tuhuma za ufisadi wa rada.Yaleyale ya kuisafisha Richmond japo angalau katika ishu ya Richmond serikali ya Kikwete ilikuwa na umri wa zaidi ya mwaka madarakani.Safari hii vimbwanga vimeanza hata kabla ya wiki kumalizika tangu iingie madarakani!Maumivu ya kichwa huanza polepole...

Na kwa kuthibitisha kuwa kura za kuirejesha CCM madarakani zilikuwa kura za kuubariki ufisadi,Ubalozi wa Uingereza umeishushua TAKUKURU kwa kutoa ufafanuzi kuhusu suala la ufisadi wa rada.Sijui nani ameipa TAKUKURU madaraka ya kusafisha watuhumiwa lakini hata sie tusio na uelewa mkubwa wa masuala ya sheria tunafahamu kuwa jukumu la kuhukumu ni la mahakama.Badala ya taasisi hiyo kumpeleka Chenge mahakamani ili kama kusafishwa asafishwe huku,yenyewe imekurupuka na utetezi wake wa kifisadi pasipo hoja za msingi.Hii yote ni katika kuandaa mazingira mazuri kwa Chenge kuwa Spika wa Bunge jipya.

Nitaendelea na tathmini yangu kadri siku zinavyosonga mbele.Najua kuna mengi tu ya kuyazungumzia hasa tukizingatia mazingaombwe yaliyotawala Awamu iliyopita hivyo ni suala la muda tu kabla hayajajiri mengine mengi ya kuwasuta wale wote waliotarajia miujiza kutoka kwa CCM.

6 Nov 2010


Urban Pulse Inawaletea video fupi kuhusu ziara ya Diamond hapa UK kwa ajili ya kuchangia vita dhidi ya Malaria. Tarehe 03.11.2010 Timu nzima Ya Urban Puse ikiwa na Diamond walipata fursa ya Kutembelea Ubalozi wa Tanzania kwa ajili ya kumtambulisha Diamond na kutoa shukrani.



Urban Tour itaanza Rasmi jumamosi tarehe 6.11.10 Milton keynes Club Opus ikifuatana na Croydon London tarehe 12.11.10


Asante sana,

Urban Pulse

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.