6 Aug 2011



Juu ni taswira mbali mbali zinazo onesha jinsi ujenzi wa soko kuu la Mwanjelwa ulivyo simama, ulianza kwa kasi lakini kwa sasa hakuna kinacho endelea na miezi kadhaa iliyo pita jengo hilo lilibomoka wakati wanaendelea na ujenzi. Tutaendelea kuwafahamisha zaidi juu ya swala hili 

HUU NDIO UBUNIFU WA DARAJA LA JUU KWA WATEMBEA KWA MIGUU WA JIJI LA MBEYA ENEO LA MWANJELWA MIAKA MIWILI IJAYO KAMA ULIVYOBUNIWA NA TAASISI YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA MBEYA

Taswira ya karibu inayo onesha Soko la Mwanjelwa jijini Mbeya 

SWALI NI JE ITAWEZEKANA? IKIWA SOKO TUU LINASUA SUA NA LIPO BARABARANI ENEO WANALO TAKA KUWEKA KIVUKO HICHO.

Imetumwa na Mbeya Yetu Blog

5 Aug 2011


4 Aug 2011





Raia Mwema Ughaibuni
Spika wetu na wauchapao usingizi bungeni!
Evarist Chahali
Uskochi
3 Aug 2011
Toleo na 197
MATUKIO ya kutia aibu yanayozidi kutokea katika kikao kinachoendelea cha Bunge la Bajeti huko Dodoma yanatoa picha moja ya msingi kuwa Spika Anne Makinda anaelekea kushindwa kumudu wajibu wake.
Haihitaji kuwa mchambuzi mahiri wa siasa kutambua hilo. Japo tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi Bunge letu limeshindwa kumudu uwepo wa wabunge wa vyama vya Upinzani, lakini kwa jinsi hali ilivyo sasa; chombo hicho muhimu kwa taifa kimegeuka kuwa uwanja wa vurugu.
Ninamshutumu Spika Makinda kwa sababu tangu apate wadhifa huo, amekuwa akijitahidi kadri awezavyo kuendesha Bunge kibabe; huku akitaka kuuthibitishia umma kuwa anakimudu kiti cha uspika ipaswavyo.
Lakini inawezekana kabisa kuwa chanzo cha matatizo yanayozidi kushamiri Bungeni ni madaraka makubwa anayopewa Spika dhidi ya wabunge. Sio siri kwamba madaraka ya Spika yanampa nguvu kubwa mno ndani ya chombo hicho cha kutunga sheria; huku kukiwa hakuna namna nzuri ya mwafaka ya kumdhibiti.
Kibaya zaidi, kwa makusudi, chama tawala kimeshikilia msimamo wa kuwa na Spika anayetoka moja ya vyama vyenye wabunge bungeni. Busara nyepesi tu inaweza kueleza kuwa katika mazingira ya uchanga wetu kwenye siasa za vyama vingi, Spika lazima atapendelea chama anachotoka.
Tukubali tusikubali, upendeleo ni moja ya vikwazo vikubwa vya maendeleo sio ya Tanzania pekee; bali sehemu kubwa ya nchi za Dunia ya Tatu. Ukimpa mtu madaraka pasipo kutengeneza mazingira bora ya kumdhibiti kuyatumia madaraka hayo isivyofaa, moja ya mambo ya mwanzo kabisa yanayoweza kutokea ni upendeleo.
Na laiti mtu huyo akitambua kuwa ana uhuru wa kufanya apendavyo, basi, atafanya upendeleo wa waziwazi akijua fika kuwa kufanya hivyo hakutoathiri nafasi yake.
Ni rahisi kuhitimisha kuwa Spika Makinda kazi inamshinda iwapo hatutorejea nyuma kidogo na kuangalia utendaji kazi wa waliomtangulia. Lakini kumbukumbu ndogo tu inaweza kutupa mwanga kuwa vitendo vya maspika wote baada ya kuruhusiwa mfumo wa vyama vingi, vimekuwa sio tu vya kidikteta dhidi ya wabunge wa vyama vya Upinzani; bali pia vinaweza kabisa kutafsiriwa kuwa matumizi mabaya ya nafasi hiyo muhimu.
Jingine ambalo linaweza kupoteza kabisa sio tu heshima ya nafasi ya cheo cha Spika bali pia umuhimu mzima wa kuwa na Bunge, ni mtindo wa ku-kasimu madaraka ya kuongoza vikao vya bunge kwa wabunge mbalimbali.
Hilo lisingekuwa tatizo laiti wabunge wote tulionao wangekuwa wa ina moja; yaani wanatambua kwa nini wanalipwa mamilioni ya shilingi kila mwezi kuwatumikia Watanzania.
Lakini sote tunajua kwamba asilimia kubwa tu ya wabunge wetu ni watu wasiojali kabisa jukumu la kuwatumikia wananchi waliowachagua kuwa wabunge, na badala yake wanaendekeza maslahi binafsi; huku picha zikiwaonyesha baadhi yao wakichapa usingizi kwenye vikao.
Na suala hilo la wabunge kulala linaweza kuibua mjadala mwingine kwenye maeneo mawili ya msingi. Kwanza, hivi ni haki kweli kwa mbunge kulipwa mamilioni ya shilingi kama posho; kisha akaishia kulala bungeni? Hivi huo kama sio ukupe ni nini?
Huo si uungwana hata kidogo, kwa sababu wakati mbunge anakoroma bungeni na kulipwa fedha kibao, walalahoi huko mitaani wanadamka alfajiri kusaka fedha ambazo kila kukicha zinazidi kuwa ngumu kupatikana kutokana na hali ngumu ya maisha.
Pili, kama maamuzi ya kuwatimua wabunge yanazingatia haki, kwanini basi wabunge wanaolala bungeni nao wasikumbane na “hasira za Spika” kwa kutolewa nje? Japo kusinzia au kulala si kosa, lakini katika mazingira ya kawaida tu mtumishi anayelala kazini anapaswa kuadhibiwa.
Jingine ambalo mara nyingi hujitokeza nje ya bunge, ni tabia za baadhi ya wabunge baada ya vikao vya chombo hicho kinachopaswa kuwa kitukufu kutokana na dhamana yake kwa umma.
Unaweza kudhani huu ni uzushi kwa vile hakuna chombo cha habari kinachoweza kuthubutu kuripoti hili, lakini ukweli ni kwamba tabia za baadhi ya wabunge wetu nyakati za jioni au wakati wa mapumziko ya mwisho wa wiki sio tu hayaendani na nyadhifa zao; bali pia zinakinzana na wajibu walionao kwenye familia zao.
Sote tunafahamu kwanini akina dada wanaofanya biashara za kuuza miili yao hukimbilia Dodoma kila kunapokuwa na vikao vya bunge. Jibu ni kwamba huo ni msimu wa ‘kuchuma’. Hivi kweli tunawalipa watu hawa mamilioni ya shilingi kwa ajili ya kufanya mambo kinyume na maadili?
Unaweza kutetea kuwa hiyo ni tabia ya mtu binafsi, lakini hoja hiyo inakosa uzito kutokana na ukweli kwamba, kwanza watu hao binafsi wanatumia fedha za walipakodi kufanya anasa zisizostahili, na pili, anasa hizo zinaweza kabisa kuathiri uwezo wao wa kutumikia umma kwa uadilifu.
Unadhani Mheshimiwa mbunge mwenye miadi na “dada poa” anaweza kweli kuelekeza akili yake kutuliza maswali ya msingi kuhusu matatizo yanayowakabili wapigakura wake?
Hili linaweza kuonekana kama tatizo dogo, lakini lina uzito mkubwa; kwani mtu asiye mwadilifu kwa familia yake hawezi kuwa mwadilifu kwa wapiga kura wake au taifa kwa ujumla.
Uhuni wa baadhi ya wabunge wetu umevuka mipaka hadi kufikia hatua ya kumfanya Waziri Mkuu kama mtu wa kumtania. Sikuamini macho yangu niliposoma habari kwamba baadhi ya wabunge wanafoji sahihi ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuandika vimemo feki kwamba mbunge fulani anahitajiwa kukutana na Pinda wakati si kweli.
Taarifa zilizopo ni kwamba mmoja wa wabunge wenye tabia hiyo ya kitoto ameshafahamika, lakini katika kuashiria kuwa bunge hili limekithiri mizaha, hakuna hatua itakayochukuliwa dhidi ya mbunge huyo. Kwa lugha nyingine ni sawa na kuhalalisha upuuzi aliofanya mbunge huyo.
Kuna picha kubwa zaidi kuhusu mapungufu ya bunge letu ambalo katika msimu uliopita lilipata kujigamba na kutunga kitabu chenye jina “Bunge Lenye Meno” (nami nikaandika makala bloguni kwangu nikaliita “Bunge Lenye Meno ya Plastiki”).
Wingi wa wabunge wa CCM ndani ya Bunge hilo umeshindwa kabisa kumsaidia Mtanzania wa kawaida, kwa sababu, kwa CCM na viongozi wake (pamoja na wabunge), maslahi ya chama yana umuhimu mkubwa zaidi kuliko maslahi ya nchi.
Kila mara tunashuhudia wingi wa wabunge wa CCM unavyosababisha sheria mbovu kupita baada ya wabunge hao “kupewa somo la kuwekana sawa.”
Japo tunaweza kujidanganya kuwa demokrasia inakua kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wabunge wa vyama vya Upinzani, ukweli unabaki kuwa tangu vyama vingi viruhusiwe; bunge letu limeendelea kuwa la chama kimoja. Hapa ninamaanisha kuwa wingi wa wabunge wa chama tawala unafunika kabisa uwezekano wa uwepo wa wapinzani kuleta mabadiliko yanayotarajiwa.
Kulaumu tu bila kutoa ushauri hakuwezi kusaidia kutatua tatizo lililopo. Spika Makinda na wasaidizi wake wanapaswa kutambua kuwa kuwatimua nje ya bunge wabunge wa CHADEMA na wengine wa vyama vya Upinzani pekee kunatoa picha moja tu ya uonevu kwa upande mmoja na upendeleo kwa upande mwingine.
Lakini hilo si la msingi zaidi kulinganisha na ukweli kwamba kuwatimua wabunge kwa “makosa” yanayoweza kurekebishika kwa maonyo tu kuna madhara makubwa kwa wapigakura wanaowakilishwa na wabunge hao.
Adhabu kwa mbunge ni adhabu kwa maelfu kama sio malaki ya wapiga kura wanaowakilishwa na mbunge husika. Spika anaweza kujitetea kwamba hawezi kulea tabia mbovu bungeni. Sasa iweje tabia hiyo mbaya iwe ni kwa wabunge wa Upinzani pekee?
Vipi kuhusu baadhi ya wabunge wa CCM tunaowaona kwenye picha wakiwa wamelala; huku bunge linaendelea? Na vipi kuhusu baadhi ya wabunge watoro wasiohudhuria vikao wakati tayari wameshachota malipo ya posho zao?
Nimalizie kwa kusisitiza kuwa Tanzania yetu ni muhimu kuliko maslahi ya mtu au chama binafsi. Kila mbunge, ikiwa ni pamoja na Spika, ni waajiriwa wa Watanzania. Wananchi ndio wanaowalipa mishahara yao monono na posho zao zisizoendana kabisa na umasikini wetu. Ni dhahiri wananchi hawaridhishwi na mwenendo huu wa sasa wa bunge letu.


Tanzania yetu sijui inaelekea wapi!Yaani ufisadi unasambaa kila kona.Wengi mnakumbuka usanii waliofanya kampuni ya utafiti ya Synovate wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.Kwa kifupi,waliamua kuweka kando professionalism na hadhi ya kampuni yao ili wawaridhishe watu wa CCM.Nilikerwa sana na uhuni wao hadi nikafikia hatua ya kumwandikia bosi wao.Kama ilivyo kawaida ya wababaishaji,aliruka kimanga na kudai hawapendelei chama chochote.

Sasa leo nimekumbana na habari iliyonikera kupita maelezo.Eti kampuni hiyo imefanya utafiti wa kura ya maoni kuhusu nafasi ya urais.Hadi hapo hakuna tatizo kwani tunashuhudia takriban kila wiki taasisi za kura za maoni kama Gallup zikiendesha kura za maoni kupima utendaji kazi wa Rais Obama,Congress,nk.Tatizo la kura ya maoni ya Synovate lipo kwenye ukweli kwamba wamekwepa kumweka Rais Jakaya Kikwete kwenye opinion poll hiyo,na badala yake wameweka wanasiasa wengine,ambapo Dkt Willibroad Slaa ameibuka kidedea.

Synovate wamefanya makusudi kukwepa kupima utendaji kazi wa Kikwete.Wangeweza kabisa kuangalia approval rating yake pasipo kumpambanisha na Dkt Slaa.Lakini wamekwepa kwa vile wanajua bayana kuwa  wengi wa Watanzania wenye akili timamu wamechoshwa na ubabaishaji wa rais wao.

Lakini hata kama Synovate wameamua kuendelea kujipendekeza kwa Kikwete na CCM,hiyo haitoondoa ukweli kuwa wengi wa Watanzania wamemchoka Kikwete,na kwa hakika wanasubiri kwa hamu afungashe virago vyake hapo 2015 (huku kukiwa na hofu kuwa by then nchi itakuwa imeharibika beyond repair).

Sidhani kama Synovate wangeamua kuchapisha approval rating ya Kikwete wangelazimishwa kuondoka Tanzania.Lakini naamini kabisa kuwa kampuni hii inafahamu fika kuwa kuficha kukubalika/kuchukiwa kwa Kikwete hakumsaidii kiongozi huyo dhaifu.Ni sawa na mgonjwa wa ukimwi kufichwa matokeo ya vipimo vya damu yake.Kamwe virusi vya ugonjwa huo havitoondoka mwilini kwa vile tu mwathirika hajajulishwa.

Anyway,habari husia ni hii hapa chini
Dk Slaa ang’ara urais 
Wednesday, 03 August 2011 23:11
0
digg

NI IWAPO UCHAGUZI MKUU UNGEFANYIKA SASA ANGESHINDA.

Leon Bahati
MATOKEO ya utafiti uliofanywa na Taasisi ya Synovate yanaonyesha kwamba iwapo Rais Jakaya Kikwete angeamua kujiweka kando na ukaitishwa Uchaguzi Mkuu sasa, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa angeibuka mshindi wa nafasi hiyo.Ripoti ya Synovate iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana ambayo inawapa wapinzani fursa ya ushindi kwa mara ya kwanza, wagombea kutoka vyama vya upinzani wana uwezo wa kupata asilimia 67 iwapo uchaguzi ungefanyika sasa.

Dk Slaa anaongoza kwa kupata asilimia 42, akifuatiwa na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (asilimia 14), Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (asilimia 12) na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe asilimia tisa.

Synovate inaeleza kwenye ripoti hiyo kwamba matokeo ya utafiti huo yanatokana na watu mbalimbali wenye umri zaidi ya kuanzia miaka 18 walioulizwa maswali ya ana kwa ana vijijini na mijini.

Katika kupata maoni juu ya mtu ambaye wangependa awe rais waliuliza: “Mbali na Rais Jakaya Kiwete, ni mtu gani ungeweza kumchagua kuwa Rais iwapo atakuwa miongoni mwa wagombea?”
Kwa mujibu wa matokeo hayo, iwapo uchaguzi ungefanyika sasa, Pinda angeambulia nafasi ya tatu licha ya kwamba CCM ndicho chama kinachoongoza kwa kuaminika mbele ya umma ikilinganishwa na vyama vingine vya siasa.Katika utafiti wake huo uliofanywa kati ya Mei 2 hadi 29, mwaka huu, jumla ya watu 1,994 walihojiwa.

CCM wamtaka Dk Slaa
Utafiti huo unaonyesha kuwa wanachama wengi wa CCM walionyesha kuvutiwa na Dk Slaa ikilinganishwa na viongozi wengine ndani ya chama hicho tawala.Hii inatokana na takwimu kuonyesha kuwa kati ya waliohojiwa katika utafiti huo, wengi wanatokana na CCM, lakini wakamchagua Dk Slaa.

Takwimu za ripoti hiyo zinaonyesha kuwa kati ya waliohojiwa, walipoulizwa kuhusu vyama vyao asilimia 51 walisema ni CCM, asilimia 35 wakasema Chadema, 10, CUF na TLP asilimia moja.

Mbali na Dk Slaa, Profesa Lipumba, Pinda na Zitto wanasiasa wengine wanne wanaofuatia ambao asilimia walizopata zimo kwenye mabano ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli (4), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (2) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (2).

Kadhalika, vigogo tisa waliofungana kwa kupata asilimia moja ya kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo ni Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal, Spika wa Bunge, Anne Makinda, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe na Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya.

Katika utafiti huo, Synovate iliegemea nyanja tatu za utafiti ambazo ni siasa, uchumi na masuala ya kijamii na utamaduni.

Mgombea urais CCM 2015
Ndani ya CCM, anayepewa nafasi ya kwanza kuwa mgombea urais kwa mwaka 2015 ni Pinda aliyepata asilimia 35 akifuatiwa na Dk Magufuli asilimia 14.

Wanaofuatia kwa mvuto pamoja na asilimia walizopata kwenye mabano ni Membe (8), Sitta (3), Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye (3), Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa (3) na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi (2).

Vigogo tisa ndani ya CCM walifungana kwa kupata asilimia moja nao ni Makinda, Dk Mwakyembe, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Magembe na Waziri Mkuu wa zamani, Dk Salim Ahmed Salim.
Wengine ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk Asha-Rose Migiro, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba.

Uvuaji gamba CCM
Utafiti huo wa Synovate unaonyesha kuwa Watanzania wengi wanatofautiana juu ya uelewa wa mpango wa CCM wa kujivua gamba.

Katika mpango huo ripoti hiyo inasema asilimia 41 walisema ni mpango wa kuwataka watu kujiuzulu kwenye uongozi wakati asilimia 29 walisema ni mpango wa kutaka kukisafisha chama.

Inaonyesha kuwa asilimia 15 ya waliohojiwa walielezea kujivua gamba kuwa ni mabadiliko ya uongozi kwa kuondoa viongozi wabovu na asilimia tano wakasema ni mpango wa kuondoa viongozi wote watuhumiwa wa ufisadi.

Asilimia mbili walisema ni mpango wa kukifanya chama hicho cha siasa kiwe na mfumo wa wazi na unaoeleweka wakati asilimia moja walisema ni suala la kujizuzulu, kutafuta viongozi wachapakazi na wenye tija. Kuna wanaouchukulia kuwa ni mkakati wa kisanii wa kuwadanganya wananchi.

Kwa ujumla, taarifa hiyo ilisema ni asilimia 45 tu ambao wana taarifa kuwa kuna Sekretarieti ya CCM ilijiuzulu na Mwenyekiti wake, Rais Kikwete amekwishateua wengine kushika nafasi hizo.

Kero kubwa nchini
Asilimia 56 walisema tatizo kubwa linalowakumba ni kupanda kwa bei ya vyakula, gharama za maisha na umaskini na asilimia 46 walisema njaa na tatizo kwenye kilimo.Tatizo la ufisadi nchini lilichukua nafasi ya tatu kwa kupata asilimia 36, ukosefu wa ajira (31), tatizo la nyumba, barabara na umeme (27), elimu (23), afya (21), maji (16), uharibifu wa mazingira (12), taasisi za siasa (10), haki za binadamu, uhalifu (6) ubeberu na usafirishaji wa dawa za kulevya (3).

Katiba Mpya
Miongoni mwa mambo ambayo yanatajwa kuwa ni vikwazo kwa Tanzania kupata Katiba Mpya ni rushwa (26), kukosekana kwa umoja (19), maslahi ya kisiasa (18), ufahamu mdogo (11) na kukosekana kwa msukumo wa kisiasa (9).

Hata hivyo, asilimia 78 walisema wanataka yawepo mabadiliko ya katiba nchini wakati asilimia 21 hawaoni umuhimu wake.Lakini asilimia 42 walisema wana uhakika kwamba mpango wa Katiba Mpya utafanikiwa.
Lakini pia makosa ya Katiba iliyopo yalielezwa kuwa ni kupitwa na wakati, kuandikwa kwa Kiingereza zaidi kuliko Kiswahili, kukosekana kwa utawala bora, kutokuwepo kwa sheria za haki za binadamu na uhuru wa vyombo vya habari.

CHANZO: Mwananchi

3 Aug 2011

Chuwit kama kuwadi kubwa lao (master pimp)

Wanaposema siasa ni mchezo mchafu hawaongopi: Bango la  Chuwit wakati wa kampeni za uchaguzi

Pengine ushasikia msemo wa Kiingereza usemao "in the long run it is experience that counts." Kwa tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili ni kwamba uzoefu unalipa.Kadhalika,naamini utakuwa umeshasikia matukio ambapo mwizi mstaafu anatumika kukamata wezi waliopo.Hii ni moja ya mbinu muhimu sana kwa polisi na watumishi wengine wa taasisi za usalama.

Lakini ishu hii imechukua sura mpya huko Thailand baada ya tajiri mstaafu wa biashara za umalaya,Chuwit Kamolvisit,kujiingiza kwenye siasa na hatimaye kufanikiwa kuwa mbunge.Mbunge huyo ambaye anadai angependa zaidi kuitwa kuwadi (pimp)kuliko mwanasiasa ameingia kwa kasi ya kipekee kwenye siasa akidhamiria kupambana na tatizo la rushwa katika nchi hiyo inayosifika kwa utalii wa ngono (sex tourism).

Chuwit alikuwa tajiri anayemiliki massage parlour (sijui neno la Kiswahili ni lipi) na vyombo kadhaa vya habari vinamtaja kama kuwadi kubwa lao (super pimp) mstaafu.Anadai kuwa ili kumudu biashara chafu kama yake ilimlazimu kuwahonga polisi mara kwa mara kwa minajili ya kukwepa mkono mrefu wa sheria (si mrefu kihivyo,anyway).Sasa baada ya kuingia kwenye siasa anataka kutumia uzoefu huo wa kukwepa sheria kwa kutumia rushwa kupambana na rushwa.

Awali,mwanasiasa huyo alichapisha kitabu alichokipa jina lenye utata la Dogstyle Politics (yaani,ashakum si matusi,"Siasa za Chuma Mboga".Katika kitabu hicho,Chuwit anatoa mwanga kuhusu mwenendo wa siasa za nchi hiyo kulingana na uzoefu alioupta wakati wa uchaguzi,Anazilinganisha tabia za wanasiasa na mbwa.Lakini anadai baadhi ya vyama vya siasa vinapaswa kufananishwa na nyoka mwenye sumu kali Cobra,kwani havina itikali wala msimamo na ni hatari zaidi ya mbwa.Katika kitabu hicho,mwanasiasa huyo mwenye vituko ameandika shairi lisemalo, "Kuna tofauti gani kati ya binadamu na mbwa?Hawezi kuongea-mbwa hadanganyi,na mapenzi ya kweli ya mbwa ni kwa mmiliki wake"

Binafsi nadhani watu kama Chuwit wanahitajika sana katika Tanzania yetu iliyogubikwa na ufisadi.Hebu pata picha mtu kama Rostam Aziz aamue kwa dhati kuanzisha vita dhidi ya mafisadi.Kwa mfano aanze na namna mtandao uliomwingiza madarakani Rais Jakaya Kikwete ulivyoundwa,fitna walizofanya kusafisha njia ya Ikulu,madili kama ya EPA,Richmond na Dowans yalivyofanikishwa na michezo mingine michafu inayoipa uhai CCM na serikali yake!

Au chukulia mfano Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge aamue "liwalo na liwe" na kumwaga "chenga hadharani" kwa kuufahamisha umma jinsi mikataba ya kijambazi inavyofanikishwa na kurutubisha ufisadi.Au pengine Edward Lowassa baada ya kuona "anazinguliwa" aamue kuwa "bora tufe wote" na kuweka hadharani kila baya analojua linalosababisha Tanzania kuendelea kuwa kichaka cha ufisadi huku maisha ya Mtanzania wa kawaida yakizidi kuwa duni tofauti na danganya toto za Kikwete za "maishabora kwa kila Mtanzania (nadhani alimaanisha 'kwa kila fisadi')

1 Aug 2011


Show ya "Growing Up African" inayo onesha familia kutoka Tanzania na maisha yao Marekani imeanza kutoa video online. Kutoka mwezi wa tatu hadi saa hivi show ilikua inayonekana East Africa TV. Kwenye mwezi huu wa August kila Episode ya Season ya Kwanza itakua kwenye website yao. Kwenye hizi episodes utakutana na ndugu wote kwenye familia kutoka kwa Bea, Eliza, Jesca, Johnson hadi Andrew ambapo huwa maisha yao ni tufauti kwa kila mtu. Episode zitakuwa na familia nzima ambao utaona hile "family dynamic" ya ndungu. Hii show kwanza, niyasisi Watanzania na tunabidi tuwasikie mnavyosema kabla ya kuwa kwenye International Spotlight na kuja na Season ya pili September. Watu hizo episode wanaweza kwenda kwenye youtube.com, au kwenye website www.growingupafrican.com kuona hayo mambo. Website saa hivi hiko tayari na yenyewe ina mambo mengi kama mawazo ya familia kwenye issues kama musiki, fashion, urembo, na vinginevyo vingi kwenye blog zao.

Asanteni Sana, na ninaomba ushauri na mawazo kutoka kwenu kama watanzania wenzetu.

"Growing Up African" since it's inception through our supportive blogs in October 2010 has grown to become a household name in the East African Community. Currently the show is available only on East Africa TV that broadcasts to Uganda, Burundi, Kenya, Rwanda and lastly Tanzania. It is our deep honor to present the first Season of the show to those viewers outside the viewing area of these five countries. We have received numerous requests through mail and phone calls to let people from abroad into this well formed hype machine. In it's first Season, we did experience several setbacks but like any successful business development comes with time. The show is now available on our website at WWW.GROWINGUPAFRICAN.com and Youtube Channel at 

As we prepare to launch the Second Season in September on East Africa Television, we would like to give an opportunity to everyone to catch up on the show.










Qatar-based broadcaster has struck a deal with US network Time Warner Cable, taking it to around 2m homes in the region

The English-language arm of Arabic news channel Al Jazeera has launched on a US cable network in New York.

At midnight last night, Al Jazeera English (AJE) began broadcasting on US network Time Warner Cable, taking it to around 2 million homes in the region.

Six months on from the eruption of widespread protest across the Middle East, the agreement follows the most high-profile period in the history of the Qatar-based news channel.

In the immediate aftermath of the uprisings, some US media commentators – including Jeff Jarvis – called for US cable networks to add Al Jazeera, claiming that it was "downright un-American not to". AJE was at that point only available online to viewers in the US.

AJE's Arabic sister channel has been viewed with suspicion by the US, and was criticised by George Bush during his presidency after airing video messages from Osama Bin Laden. Its newsrooms were also bombed by the US in both Afghanistan and Iraq, although US authorities claimed the strikes were mistakes.

AJE, on the other hand, won praise from the US administration for its coverage of the uprisings in the Arab world, with secretary of state Hilary Clinton saying that the channel was airing "real news".

"Viewership of Al Jazeera is going up in the United States because it's real news. You may not agree with it, but you feel like you're getting real news around the clock instead of a million commercials and arguments between talking heads and the kind of stuff that we do on our news, which is not particularly informative to us, let alone foreigners."

Al Anstey, managing director of AJE, told the New York Times that early meetings with US networks had been about trying to correct "myths and misconceptions" about the AJE, but that now they don't come up.

Anstey added that the channel, which receives some funding from the Qatari finance ministry, will not be seeking the per-subscriber fee common to most US cable channels. "Revenue is not our priority," he said. "It’s being seen."

SOURCE:Journalism.co.uk


Familia yenye furaha: Kushoto ni Baba mtoto Jordan (15),akifuatiwa na  mama mtoto Tia (14) na kichanga  Gracie,na nyuma ni babu kijana  Shem (29) na kulia ni bibi kijana  Kelly (30)

Kwa namna ilivyozoeleka,unaposikia "babu" au "bibi" unadhani pasi wasi kuwa mtajwa ni aliyekula chumvi nyingi,na huenda umri wake upo kwenye miaka ya 50 na kuendelea.Na sia ajbu ana mvi lukuki.

Hali si hivyo kwa Shem Davies,kijana mwenye umri wa miaka 29 ambaye wiki hii amekuwa "Babu Kijana Zaidi nchini Uingereza."Davies,ambaye hana kazi (unemployed),amefanikiwa kupata mjukuu baada ya bintiye wa kike aitwaye Tia (umri miaka 14!!) kujifungua mtoto aitwaye Gracie.
Baba na mwana:  Shem na mwanaye Tia na kijukuu Gracie

Kuzaliwa kwa Tia (miaka 14 iliyopita) ni matokeo ya uhusiano wa kimapenzi kati ya Shem na mwandani wake wa zamani aitwaye Kelly John mwenye umri wa miaka 30 sasa.

Kuchanganya madawa zaidi,kijana aliyezaa na Tia (mama mtoto mwenye miaka 14) naye ni serengeri boy wa miaka 15 tu!Kwa jina anaitwa Jordan Williams (pichani chini akiwa na mzazi mwenzie na kichanga chao)

Kwahiyo mjukuu amepatikana kwa mama mwenye miaka 14 na baba mwenye miaka 15,na ana babu wa miaka 29 na bibi wa miaka 30!

Lakini ukiangalia kwenye picha zinazoambatana na habari hii itakuwia vigumu kutambua umri wa wahusika wa Isidingo hii.Tatizo ni kwamba ni vigumu sana kukadiria umri wa hawa "wazungu."

Uingereza ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mabinti wanaojifungua kabla ya kutimiza miaka 18.

CHANZO: Daily Mail


Rushwa Inavyoua Elimu ya Watoto Wetu

CHANZO: Haki Elimu


MAPENDEKEZO YA MASHIRIKA YA KIRAIA JUU YA MUSWADA WA SHERIA YA MAPITIO YA KATIBA, 2011.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.