Showing posts with label RUSHWA TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label RUSHWA TANZANIA. Show all posts

1 Aug 2011


Rushwa Inavyoua Elimu ya Watoto Wetu

CHANZO: Haki Elimu

10 Mar 2010

TAkukuru
Katika toleo jana la gazeti la Mwananchi kuna habari kwamba Mbunge wa Nyang’hwale,James Musalika, alilazimika ‘kuingia mitini’ kuwakwepa makachero wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) waliokwenda katika ‘hafla’ kati ya mbunge huyo na wapiga kura.Kwa mujibu wa Mwananchi,hatua hiyo ya wanadola wa TAKUKURU ni katika utekelezaji wa ‘ruhusa’ waliyopewa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete ‘kudhibiti wanasiasa wanaotoa rushwa kwenye chaguzi’.

17 Apr 2009

KWA MUJIBU WA GAZETI LA Uhuru,KATIBU MKUU WA CCM,YUSUPH MAKAMBA,AMEAGIZA UONGOZI WA CCM NA JUMUIYA ZAKE NGAZI ZA MIKOA KUANDAA MAPAMBANO YA KUMPONGEZA JK NA SERIKALI KWA KAZI NZURI KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA.....
Nadhani muda si mrefu kutakuwa na tangazo jingine la kuagiza maandamano ya kupongeza mafanikio ya kutimizwa kwa ahadi ya MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA sambamba na pongezi za kuwabainisha wamiliki wa Kagoda.
CCM HOYEEEE!!!!!

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!!!!

That's all I can say!

Habari nyingine ndani ya gazeti hilo ni pamoja na "UFISADI MALIASILI:Sh Bil 2.4 zayeyuka kiutatanishi;Mil 790 zatumika kununua pikipiki hewa;Watumishi watimuliwa,wachunguzwa"





2 Mar 2009

UAMUZI WA SERIKALI KUHUSU KURA YA MAONI DHIDI YA WAUAJI WA ALBINO-ULIOTANGAZWA NA RAIS JK KWENYE HOTUBA YAKE YA MWISHO WA MWEZI FEBRUARI- UMEPOKELEWA KWA HISIA TOFAUTI NA BAADHI YA WANANCHI KAMA INAVYOELEZWA KATIKA HABARI NAMBARI 2 HAPO CHINI.KWA MTAZAMO WANGU,NADHANI WANANCHI WANA KILA SABABU YA KUHOJI UAMUZI HUO WA SERIKALI HASA KWA VILE IMEKUWA NI KAMA DESTURI KWA NCHI YETU KUTANGAZA HATUA KALI ZA KISIASA AMBAZO HUISHIA KUBAKI HISTORIA TU PASIPO MAFANIKIO.WENGI TUNAKUMBUKA KUHUSU DEADLINE WALIYOPEWA WALA RUSHWA MWANZONI MWA MWAKA 2006 NA ORODHA YA MAJINA YA WANAOJIHUSISHWA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA ILIYOKABIDHIWA KWA (ALIYEKUWA )WAZIRI BAKARI MWAPACHU....LAKINI HADI LEO HAKUNA HATUA YOYOTE ILIYOCHUKULIWA.KWANZA SOMA HABARI HUSIKA KISHA TUJADILI ZAIDI:

Kikwete:Wanaoua albinokuanza kutajwa kwa kura
mwezi huu

Claud Mshana

RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa, maandalizi ya zoezi la upigaji kura za maoni za kung'amua wauaji wa albino na vikongwe, limekamilika na litazinduliwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Akizungumza jana kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa Februari, Rais Kikwete alisema kuwa maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu.

Alisema kuwa alitoa maagizo ya kufanyika kwa zoezi hilo mwezi Desemba mwaka jana kwamba wananchi wapige kura kutaja majina ya waovu hao, akiwa na dhamira ya kuwapa nafasi wananchi kushiriki kikamilifu.

"Maandalizi ya kutekeleza uamuzi wangu huo yanaelekea kukamilika, mheshimiwa waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi Machi, 2009 na zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."

Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa. Alitaja utaratibu wa kuendesha zoezi hilo utakuwa ni kufuata kanda na kwamba mikoa imegawanywa katika kanda saba ambazo ni Kanda ya Ziwa inayojumuisha mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na Shinyanga.

Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa na Ruvuma; Kanda ya Kati (Dodoma na Singida), Kanda ya Kusini (Lindi na Mtwara), Kanda ya Magharibi (Kigoma na Tabora), Kanda ya Kaskazini (Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara), na Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro).
Wakuu wa mikoa yote nchini wameshapewa mwongozo wa jinsi ya kutekeleza zoezi hilo na kutaja miongoni mwa mambo watakayotakiwa kuzingatia ni pamoja na kuelimisha na kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi hilo, upigaji kura ufanyike mwezi Machi kwa tarehe zitakazopangwa kwa kuzingatia kanda hizo.

"Kamati za ulinzi na usalama za mikoa zikiongozwa na wakuu wa mikoa zisimamie zoezi hili kwa makini. Kadhalika, kamati za ulinzi na usalama za wilaya zikiongozwa na wakuu wa wilaya zitaongoza utekelezaji katika wilaya zao na kushirikisha serikali za vijiji na mitaa," alisema Rais Kikwete.

"Napenda kuitumia fursa hii kuwasihi Watanzania; wake kwa waume; vijana na wazee tujitokeze kwa wingi kuwataja watu wanaojihusisha na maovu hayo katika jamii. Kura ni siri, hakuna atakayejua umemtaja nani. Hata msimamizi wa kituo hawezi kujua," alisema......
CHANZO: Mwananchi

NA IFUATAYO NI HABARI KUHUSU REACTION YA BAADHI YA WANANCHI JIJINI DAR ES AALAAM KUHUSIANA NA UAMUZI HUO WA KURA YA MAONI KUWATAMBUA WAUAJI WA MAALBINO.


Dar wataka serikali iweke wazi chanzo cha mauaji ya
albino


Na Boniface Meena

WANANCHI wa Mkoa wa Dar es Salaam wameiomba serikali itafute na kuewaleza chanzo cha mauaji ya albino, badala ya kuendelea kutoa kauli za kisiasa wakati hali inaendelea kuwa mbaya.

Pia wamesema hawadhani kama upigaji kura kuhusu mauaji hayo kama utasaidia kwa kuwa hata kesi za waliokamatwa kwa kuhusishwa na mauaji hayo hazijasikika. Mbali na hilo wameitaka serikali kuanzisha mahakama maalum kwaajili ya kusikiliza kesi za mauaji hayo ili waweze kujua maamuzi yanayotolewa na mahakama. Wakizungumza mbele ya Mkuu wa wilaya ya Temeke ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Kihato wananchi hao walidai serikali inaoneka kutokuwa makini na suala hilo kwa kuwa hakuna hata kesi moja ya mauaji ya albino iliyotolewa hukumu hadi hivi sasa.

Mbunge wa kuteuliwa, Al-Shaimar Kweiger alidai kuwa kuna mtandao mkubwa wa matajiri unaohusika na mauaji hayo ambao alisema hadhani kama unaweza kuishinda serikali katika kupambana nao. "Hili suala limeshazungumziwa sana, tumezunguka na Waziri Mkuu sehemu nyingi, lakini hawakomi nadhani kuna mtandao mkubwa wa watu wenye fedha uko nyuma ya jambo hili," alisema Kweiger.

Josephat Torner ambaye ni mwanaharkati wa kupinga mauaji ya albino alisema suala hilo linaonekana kuwa la kisiasa kwa kuwa hakuna hatua za haraka zilizochukuliwa kuwasaisdia wahanga wa mauaji hayo. "Tunataka kujua serikali imefikia wapi tangu suala hili lilipotangazwa kuwa ni la kitaifa," alihoji Torner. Torner ambaye ni albino alisema hawadhani kama upigaji kura utasaidia, kwani wanaona kama ni mchezo wa kisiasa hivyop wangependa kujua wako katika hali gani hivi sasa kuhusu mauaji hayo.

Christopher Andendekisye ambaye ni Mkurugenzi wa Shirikisho la Vyama vya Walemavu Tanzania (Shivyawata) alisema, kama serikali haitakuwa makini na mauaji hayo yanaweza kuendelea kwa muda mrefu kwa kuwa chanzo chake bado hakijajulikana. "Itabidi tuwe na wiki maalum au mahakama maalumu kwaajili ya kusikiliza kesi za mauaji haya na kama haiwezekani tuambiwe chanzo ni nini," alisema Andendekisye. Maria Chale ambaye ni albino alidai kuwa inaonekana serikali mpaka sasa haijui chanzo kitu ambacho kinatia wasiwasi kama zoezi hilo litafanikiwa.

Steven pascal ambaye ni katibu wa Albino muungano Investiment Trust(Amit), alisema ni bora jeshi (JWTZ) watumike kuwaska wanaohusika na mauaji hayo. "Ni bora Jeshi lihusishwe kwani hawa jamaa (wanajeshi) akipigwa mwenzao mmoja kijiji kizima kinazingira mpaka wapatikane wahusuka," alisema Pascal. Wananchi hao walisemas hayo jana wakitoa maoni yao mbele ya DC Kihato ambaye alikutana nao kuwaeleza juu ya uzinduzi wa upigaji kura za maoni dhidi ya mauaji ya albino utakaofanyika jijini Dar es Salaam Machi 5, mwaka huu.

Akijibu baadhi ya maoni yaliyotolewa na wananchi hao, Kihato ni kweli serikali haijatatua tatizo hilo kama wananchi wanavyotaka lakini inajitahidi kuhakikisha mauaji hayo yanatokomezwa, ndiyo maana wameitisha kura ya maoni.


CHANZO: Mwananchi

KATIKA HABARI YA KWANZA,KUNA MANENO NIMEYAONYESHA KWA RANGI NYEKUNDU KWA SABABU MAALUMU.PAMOJA NA NIA NZURI YA SERIKALI KUTAFUTA UFUMBUZI WA KUDUMU WA MAUAJI YA MAALBINO,WAZO LA KURA YA MAONI LINAWEZA LISIWE NA MAFANIKO YANAYOKUSUDIWA.KWANZA,KAMA MANENO YENYE RANGI NYEKUNDU YANAVYOONYESHA "...Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa..." KUTANUA WIGO WA WALENGWA KUNALIFANYA ZOEZI HILO KUWA PANA ZAIDI ILHALI MAANDALIZI YAKIWA DUNI.ZAIDI,IWAPO KWELI DHAMIRA NI KUWASAKA WAUAJI WA MAALBINO,KUNA HAJA GANI KUINGIZA HABARI ZA WAUZA MADAYA YA KULEVYA,KWA MFANO,AMBAO HUKO NYUMA TULISHAAMBIWA KUWA ORODHA YAO ILIKABIDHIWA KWA WAZIRI MWAPACHU NAE AKADAI KUWA AMEIKABIDHI KWA RAIS?

JINGINE AMBALO LINAHITAJI TAFAKURI NI UTATA KATIKA KAULI ZA VIONGOZI WETU.RAIS ANASEMA ALITOA AGIZO MWEZI DESEMBA,LAKINI TUNAKUMBUKA KAULI ZA WAZIRI MKUU HAPO KATIKATI KWAMBA WAUAJI WA MAALBINO NAO WAUAWE (JAPO BAADAYE ALIOMBA MSAMAHA KWA MACHOZI HUKO BUNGENI)....INA MAANA AGIZO LA DESEMBA LILIPUUZWA NA KUBADILISHWA KUWA "JINO KWA JINO" KABLA HALIJAFUTWA KUFUATIA KELELE ZA WADAU KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA WA SHERIA?

NA KAMA AGIZO LILITOLEWA DISEMBA,KWANINI BASI ICHUKUE MIEZI MITATU MIZIMA KUTOA UAMUZI HUU AMBAO KWA HAKIKA UNAHITAJI MAANDALIZI MAZURI NA YA KUTOSHA (HUSUSAN UHAMASISHAJI)?JE WIKI MBILI ZINATOSHA ?RAIS ANASEMA "...maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu...zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."ARE WE ARE WE REALLY SERIOUS?KURA YA MAONI WIKI MOJA BAADA YA UZINDUZI!?JE MAANDALIZI YANAYODAIWA KUKAMILIKA HAYAKUPASWA KUJUMUISHA UHAMASISHAJI WA WANANCHI?PASIPO UMAKINI,ZOEZI HILI LITAISHIA KUTUNISHA POSHO ZA WAHUSIKA NA WAUAJI WA MAALBINO,WAUZA UNGA NA MAJAMBAZI WAKAENDELEA "KUPETA."

SWALI JINGINE LA MSINGI NI KUHUSU MATOKEO YA KURA HIYO YA MAONI.HIVI KWA MFANO BLOGU HII IKIPIGIWA KURA NYINGI KUWA NDIO SPONSOR WA WAUAJI WA MAALBINO (GOD FORBID),NINI KINAFUATA?MHUSIKA ATAKAMATWA NA KUHOJIWA KWA VILE KURA NYINGI ZIMESEMA HIVYO?MHUSIKA ATATAKIWA AJIELEZE KWANINI WANANCHI WENGI WAMEMPIGIA KURA "ZA CHUKI"?AU WAPELELEZI WATAINGIA UWANJANI KUANZA UCHUNGUZI?VIPI ILE TASK FORCE ILIYOUNDWA HUKO NYUMA?

KWA NCHI INAYOHESHIMU UTAWALA WA SHERIA INATARAJIWA KUWA MATOKEO YA KURA HIYO HAYATACHUKULIWA KUWA NDIO HUKUMU DHIDI YA WATAJWA.HIYO ITAMAANISHA KUFANYIA UCHUNGUZI MAJINA YA WALIOPATA KURA NYINGI.KISHA UCHUNGUZI UTAPOKAMILIKA NA USHAHIDI WA KUTOSHA KUPATIKANA NDIPO ZIANZE HATUA ZA KISHERIA KWA VILE,KWA MUJIBU WA SHERIA, NI MAHAKAMA PEKEE (NA SIO MATOKEO YA KURA YA MAONI) INAYOWEZA KUMTIA MTUHUMIWA HATIANI AU KUMWACHIA HURU.

MWISHO,NI MUHIMU PIA KUKUMBUKA NAMNA UTAMADUNI WA RUSHWA UNAVYOATHIRI MWENENDO WA MAISHA YA MTANZANIA KILA SIKU.HIVI KAMA BAADHI YA WAHESHIMIWA WANAWEZA KUNUNUA KURA ILI WATUWAKILISHE HUKO BUNGENI,KWA MFANO,ITASHINDIKANA VIPI KWA MATAJIRI WANAOFADHILI MAUAJI YA MAALBINO KUNUNUA KURA "ZA KUPENDWA" NA WAPIGA KURA?VIPI IWAPO MATOKEO YA KURA YATAONYESHA MAJINA YA BAADHI YA WAHUSIKA WA KAMPUNI YA KAGODA?HAKUTAKUWA NA KIGUGUGMIZI KAMA KILICHOPO KWENYE UFISADI WA KAMPUNI HIYO KWENYE FEDHA ZA EPA?

NA VIPI IWAPO WANYONGE WATAPIGIWA KURA ZA CHUKI?

MASWALI NI MENGI KULIKO MAJIBU.KWA HAKIKA DHAMIRA KUHUSU KURA YA MAONI NI NZURI LAKINI WASIWASI WANGU MKUBWA NI KATIKA UTEKELEZAJI WAKE.NA KAMA WALIVYOSEMA BAADHI YA WAKAZI WA DAR KATIKA STORI NAMBA 2,MAFANIKIO KATIKA HARAKATI ZA KUKOMESHA MAUAJI YA ALBINO YANAHITAJI JITIHADA ZA ZAIDI YA KAULI ZA KISIASA.

5 Oct 2008


JAJI Kiongozi, Salum Massati, amesema kuanzia sasa madereva watakaosababisha vifo katika ajali za barabarani watanyang’anywa leseni na hata kufungwa miaka miwili jela ili kupunguza matukio hayo.

Akizungumza mjini hapa, Jaji Massati alisema ili kufanikisha mkakati huo, Mahakama ya Tanzania imewaagiza mahakimu wake kutafsiri vizuri na kwa usahihi sheria ya makosa ya barabarani ili kuwabana madereva wazembe. 

Agizo hilo lilitolewa alipokuwa akizungumza na watumishi wa mahakama hiyo Kanda ya Iringa. 

Alisema kwa kipindi kirefu madereva wanaopatikana na hatia za kuua kutokana na makosa ya barabarani wamekuwa wakipata adhabu ndogo, jambo linalolalamikiwa kuchochea matukio ya ajali. 

“Hivi sasa mahakama zimebebeshwa mzigo huu wa lawama kana kwamba sisi ndio chanzo cha kuendelea kwa ajali nyingi barabarani kwa kuwa adhabu tunazotoa haziwiani na makosa yanayofanywa yakiwamo ya kusababisha vifo,” alisema. 

“Sheria inataka anayesababisha kifo kwa makosa ya barabarani ahukumiwe miaka miwili jela na anyang’anywe leseni yake, lakini mahakimu wetu hawatoi hukumu hiyo,” alisema. 

Alisema badala yake madereva wengi wanaokutwa na hatia za makosa hayo hupigwa faini ndogo na kuachiwa. 

Jaji Massati alisema mianya iliyopo katika sheria ya Usalama Barabarani imesababisha wakati mwingine dereva aliyesababisha ajali ambayo hata kama imeua watu 20 apigwe faini na kurudishiwa leseni yake. 

“Pale Kibaha, Pwani aliwahi kukamatwa dereva mwenye leseni feki aliyesababisha ajali na kuua, hata hivyo alipofikishwa mahakamani alihukumiwa kwa faini ya Sh 10,000 na kurudishiwa leseni yake. 

“Sidhani kama hukumu hiyo ilikuwa sahihi na inatoa fundisho kwa madereva wengine kuzingatia sheria zote za barabarani,” alitoa mfano.


Kwa mujibu wa sheria,kila mvunja sheria anapaswa kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria (kifungo ikiwa ni mojawapo ya adhabu hizo).Ajali za barabarani zinapoteza maisha ya Watanzania wenzetu kila kukicha,lakini ufisadi nao unaathiri (na pengine hata kupoteza) maisha ya mamilioni ya Watanzania kila dakika.Madereva wanaosababisha ajali na mafisadi wote ni wavunja sheria na wanapaswa kudhibitiwa kwa kuchukuliwa hatua kali ili,kwa upande mmoja,iwe fundisho kwa wengine,na kwa upande mwingine,wavunja sheria wavune wanachopanda.

Lakini pamoja na kuunga mkono mtazamo wa Jaji Kiongozi,nadhani kuna umuhimu wa kwenda mbali zaidi kuangalia vyanzo vya ajali mbali ya uzembe wa madereva.Tuchukulie madereva wa daladala kwa mfano.Mazingira yao ya kazi yanafanywa kuwa magumu na wamiliki wa daladala wenye uchu wa faida pasipo kujali sana mazingira ya kazi ya wanaowaletea faida hiyo.Na hapo tumewaweka kando askari trafiki wenye kudai rushwa waziwazi kana kwamba ni haki yao.

Hivi anayeamua kuweka chasis ya lori kwenye basi la abiria ni dereva au mmiliki wa basi hilo?Je linapopata ajali kutokana na mechanical corruption hiyo wa kulaumiwa ni dereva au mmiliki wa basi hilo?Na vipi kuhusu trafiki wanaokagua mabasi ya abiria?Au vipi kuhusu wiki ya usalama barabarani ambayo inaadhimishwa kila mwaka?Kwa mmiliki wa basi bovu kulikabidhi kwa dereva kwa ajili ya biashara inamaanisha kwamba ametoa baraka kwa lolote litakalotokea,ikiwa ni pamoja na ajali.Same could be concluded about mamlaka zinazoruhusu gari bovu kuwepo barabarani.

Hapa tunarudi kwenye tatizo lilelile la kila mara la kuangalia matokeo badala ya chanzo.Au kwa mtazamo mpana zaidi,kuhukumu vidagaa badala ya papa.Madereva wengi wa mabasi ya abiria wanalazimika kuyakubali mazingira magumu ya kazi hiyo sio kwa vile wanaipenda sana bali kutokana na tatizo zima la ajira huko nyumbani.Hakuna mtu mwenye akili timamu aliye tayari kuendesha "jeneza linalotembea" (a walking coffin),yaani magari ambayo yako barabarani kwa kudra za Mwenyezi Mungu pekee.

Sawa,madereva wanaosababisha ajali wanapaswa kuchukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kifungo.Lakini pasipo kukomesha tatizo la kuwepo kwa magari mabovu barabarani,vifungo vitaendelea na ajali zitaendelea pia.By the way,kama vifungo pekee vingekuwa kizuizi cha kuvunja sheria,idadi ya wafungwa waliopo magerezani (na mazingira ya kutisha wanayoishi huko) ingetosha kukomesha uvunjifu wa sheria unaoweza kupelekea mtu kwenda gerezani.Pasipo kuangalia upande wa pili wa tatizo,yaani wamiliki wa vyombo vya usafiri wanaoweka mbele faida kuliko uhai wa abiria wao,na trafiki wanaothamini rushwa kuliko maisha ya Watanzania wenzao,basi ajali zitaendelea hata kama adhabu kwa kosa la kusababisha ajali itakuwa hukumu ya kifo.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.