25 Apr 2012

Barcelona 2 Chelsea 2 (agg 2-3): Salute the incredibles! Terry off, 2-0 down but brave Blues hit back to reach final


Amid the chaos created by a captain’s insane indiscipline, Chelsea’s Incredibles emerged on Tuesday night.
This was a group of players who somehow survived for 54 minutes in the absence of the dismissed John Terry and secured their passage to the Champions League final; a team who stopped a Barcelona side that had already scored 102 goals at home this season before this semi-final began.
In doing so, they joined the ranks of the European greats.
Magic moment: Torres celebrates after bagging the goal which confirmed Chelsea's position in the final
Magic moment: Torres celebrates after bagging the goal which confirmed Chelsea's position in the final

MATCH FACTS

Barcelona: Valdes, Puyol, Pique (Dani Alves 26), Mascherano, Xavi, Busquets, Iniesta, Cuenca (Tello 58), Messi, Sanchez, Fabregas (Keita 74).
Subs not used: Pinto, Thiago, Pedro, Adriano. 
Booked: Iniesta, Messi.
Goals: Busquets 35, Iniesta 43.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Cahill (Bosingwa 12), Terry, Cole, Obi, Meireles, Mata (Kalou 58), Lampard, Ramires, Drogba (Torres 80).
Subs not used: Turnbull, Essien, Malouda, Sturridge.
Booked: Cech, Ivanovic, Ramires, Lampard Mikel.
Sent off: Terry.
Goals: Ramires 45+1, Torres 90+2
Referee: Cuneyt Cakir (Turkey)
It was not just the loss of Terry that presented them with a problem. It was not just that, with only 10 men, they were facing the finest team the world has ever seen. It was the fact they triumphed  without a single centre half on the pitch, having already lost Gary Cahill to injury.
Manager Roberto Di Matteo was whistling when he walked through the media zone shortly after the final whistle, cool as you like.
But an Italian — who might just lose the ‘interim’ part of his job title before long — had masterminded an astonishing victory. 
It was a performance that might have superseded Manchester United’s display on this same Nou Camp pitch in 1999, when they beat Bayern Munich in the final. It  might even have been the most extraordinary contest witnessed in this competition.
By the end Di Matteo had organised his side in a 6-3 formation, with Salomon Kalou doubling up alongside Ramires at right back and Fernando Torres sitting outside Ashley Cole at left back. Want to know how to cope with Barcelona’s big pitch? Just play four full backs.
Opener: Busquets opens the scoring on the night - sliding the ball home from seven yards out and celebrates (below)
Opener: Busquets opens the scoring on the night - sliding the ball home from seven yards out and celebrates (below)
Opener: Busquets opens the scoring on the night - sliding the ball home from seven yards out and celebrates (below)
That Ramires and Torres also scored Chelsea’s goals made it all the more memorable and that bit more special. The first came from the Brazilian just before the interval when it seemed Barcelona were on the road to Bavaria, while Torres added the coup de grace in second-half stoppage time.
Together with Terry, Branislav Ivanovic and Raul Meireles, Ramires will miss the final because of the booking he received here last night. But that did not stop him sprinting the full length of the  field, from his new position in the makeshift back-four, to run on to a pass from Frank Lampard before sending a quite brilliant chip over the advancing Victor Valdes and into the net.
Double your money: Iniesta rounds off a wonderful move to extend Barca's lead on the night
Double your money: Iniesta rounds off a wonderful move to extend Barca's lead on the night
Double your money: Iniesta rounds off a wonderful move to extend Barca's lead on the night
It was amazing. It was Roy Keane — who missed that 1999 final — in a Chelsea shirt. It was enough to make grown men cry.
When Chelsea fans who were here share their recollections of the night, they will reflect on that moment in the  context of the 10 or so  dramatic minutes that came before.  
Chelsea had done well to limit Barcelona to one decent chance in the opening half an hour, with Petr Cech denying Lionel Messi after the best player on the planet had executed a marvellous one-two with Cesc Fabregas. 
Smash and grab: Chelsea found themselves back in charge via Ramires' delicate strike on the stroke of half-time
Smash and grab: Chelsea found themselves back in charge via Ramires' delicate strike on the stroke of half-time
Smash and grab: Chelsea found themselves back in charge via Ramires' delicate strike on the stroke of half-time

But it was looking ominous for the visitors the moment they lost Cahill to injury after only 12 minutes, forcing  Di Matteo to deploy Jose Bosingwa on the flank and move Ivanovic to centre half.
In those 10 first-half minutes, though, Chelsea appeared to  collapse and capitulate.
It started when Sergio Busquets met a neat cross from Isaac Cuenca to score, continued two minutes later when Terry mindlessly drove his knee into the leg of Alexis Sanchez and concluded with Andres Iniesta dropping off the right shoulder of Ramires — now at right back thanks to the need to switch Bosingwa to centre-half — to collect a wonderful pass from Messi before slipping his shot beyond the reach of Cech. 
Seeing red: Chelsea were right up against it after being reduced to ten men when captain Terry was sent off
Seeing red: Chelsea were right up against it after being reduced to ten men when captain Terry was sent off
Seeing red: Chelsea were right up against it after being reduced to ten men when captain Terry was sent off

Surely it was game over. Surely Barcelona would succeed only in building on their lead and leave Terry to reflect on yet more Champions League misery — a penalty for his madness to add to the  penalty he missed in Moscow.
But then came the comeback of comebacks — a defiant fight for survival that will strike fear into whichever side they meet in Munich on May 19. 
Taking a tumble: Valdes, Drogba and Pique collide, leaving the Barca defender out for the count
Taking a tumble: Valdes, Drogba and Pique collide, leaving the Barca defender out for the count
Taking a tumble: Valdes, Drogba and Pique collide, leaving the Barca defender out for the count

The goal from Ramires nearly counted for nothing when, two minutes after the break, Fabregas appeared to dive after a challenge from Didier Drogba in the penalty area and Messi was invited by referee Cuneyt Cakir to score from the spot. But Messi had never scored in seven previous meetings with Chelsea and that record was extended to eight when his effort crashed off Cech’s bar and bounced to safety.
Flashpoint: The players lost their composure briefly in the second-half after the the Barca bench celebrate the opener (below)
Flashpoint: The players lost their composure briefly in the second-half after the the Barca bench celebrate the opener (below)
Flashpoint: The players lost their composure briefly in the second-half after the the Barca bench celebrate the opener (below)

Even then, it only seemed a  matter of time before the Catalans would score again. 
Sanchez had one goal ruled out for offside, while Messi was denied by the brilliance of Cech when the Chelsea goalkeeper diverted another shot against a post.
That Di Matteo’s makeshift side survived a further 43 minutes after Messi’s penalty miss was remarkable, but it was the product of  serious hard graft and intense concentration — defending at its finest.
Blue is the colour! Chelsea celebrate after Torres' late goal rounded off a memorable night for the west Londoners
Blue is the colour! Chelsea celebrate after Torres' late goal rounded off a memorable night for the west Londoners
Blue is the colour! Chelsea celebrate after Torres' late goal rounded off a memorable night for the west Londoners

In front of the defensive line stood three midfielders in Frank Lampard, Meireles and John Mikel Obi who battled every bit as courageously, demonstrating exactly why this Barcelona team do not like playing against them.
That Chelsea scored a second goal was irrelevant in the end, even if it did add to the joy for the visitors and the despair for the hosts. 
All smiles: Di Matteo celebrates the most unlikely of victories after Torres rounded Valdes to score the second
All smiles: Di Matteo celebrates the most unlikely of victories after Torres rounded Valdes to score the second
All smiles: Di Matteo celebrates the most unlikely of victories after Torres rounded Valdes to score the second

Torres must have loved it, though, racing clear in pursuit of a ball forward from Ivanovic before casually taking it around Valdes and scoring into an empty net.
Pure delight: Chelsea players and staff race onto the pitch on the full time whistle
Pure delight: Chelsea players and staff race onto the pitch on the full time whistle
Pure delight: Chelsea players and staff race onto the pitch on the full time whistle

Di Matteo had said his side would need to produce ‘two perfect  performances’ to win this semi-final, but not even he would have envisaged this.
Take a bow, Chelsea’s Incredibles.
Roll on Munich: Chelsea will face Real Madrid or Bayern in the final
Roll on Munich: Chelsea will face Real Madrid or Bayern in the final

SOURCE: Daily Mail

Inawezekana kitendawili cha vazi la taifa kinaweza kuwa kimepata mwanzo mzuri,kama si ufumbuzi kabisa.Wazo hilo limenijia baada ya kuangalia picha hii ya Rais Kikwete na huyo mwanamama wa tatu kushoto,ambapo mitindo ya  mavazi yao ni yameshabihiana kwa kiasi flani hususan ukosi wa mikono.WAMEPENDEZA

22 Apr 2012




JK alinda mawaziri
•  ASISITIZA WAACHWE, UPEPO HUU UTAPITA

na Mwandishi wetu

WAKATI taarifa ya Kamati ya wabunge wa CCM chini ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, juzi iliridhia mawaziri wote wanaokabiliwa na tuhuma za ubadhirifu kwenye wizara zao wajiuzulu, jana Rais Jakaya Kikwete aliwasili nchini akitokea Brazil akiwa na msimamo tofauti.

Taarifa zinasema kumekuwa na mazungumzo baina ya Rais Kikwete na Pinda yaliyolenga kunusuru serikali yao lakini walitofautiana kuhusu hatua inayopaswa kuchukuliwa dhidi ya mawaziri waliotakiwa kujiuzulu.

Msimamo wa Pinda inadaiwa kuwa anataka mawaziri wanaokabiliwa na tuhuma waondoke ili kuleta uwajibikaji serikalini, lakini Rais Kikwete amesema mawaziri hao waachwe waendelee na kazi zao, kwa kuwa suala hili ni la upepo tu, liachwe litapita.

Tanzania Daima Jumapili limeelezwa kuwa rais anakataa shinikizo hilo kwa madai serikali haipaswi kuyumbishwa yumbishwa.

Miongoni mwa mawaziri wanaopaswa kuondoka ni Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo; Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Cyril Chami na naibu wake, Lazaro Nyalandu; Waziri wa Tawala wa Mikoa na Serikali za Mitaa, George Mkuchika na naibu wake, Aggrey Mwanri; Waziri wa Afya, Dk. Haji Mponda na naibu wake, Lucy Nkya na Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu.
Wengine ni Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja na Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.

Habari zinasema Rais Kikwete na Pinda walitofautiana juu ya hatua dhidi ya mawaziri hao, hivyo kuwafanya baadhi ya mawaziri kutamba mitaani kuwa hawang’oki madarakani kwa sababu tayari bosi wao ameonyesha kutounga mkono tuhuma zinazoelekezwa kwao na wabunge wa upinzani na CCM.

Habari hizi zinasema pia kwamba Pinda amekuwa hafurahishwi na msimamo wa ‘bosi’ wake, hasa katika kushindwa kutoa uamuzi mgumu.

Zinadai kuwa rais amekuwa na tabia ya kuacha upepo uchukue nafasi yake wakati Pinda anataka baadhi ya watu wawajibike bila kujali nyadhifa zao au ukaribu na kiongozi mkuu wa nchi ili kurejesha imani ya serikali kwa wananchi.

Pinda inadaiwa amekuwa akitaka maamuzi magumu yafanyike, kwakuwa yeye ndiye anayesulubiwa na maswali pamoja na hoja za wabunge wawapo bungeni.
Baadhi ya wabunge waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili, wameweka wazi kuwa kama Rais Kikwete ataamua kuwalinda na kuwatetea mawaziri wake basi watawaondoa kwa mkakati tofauti utakaomlazimisha rais kukubaliana na hoja za wabunge.

Baadhi ya wajumbe waliozungumza na gazeti hili waliweka wazi hatua hiyo inahitaji muda na mipango madhubuti na wao wapo tayari kufanya hivyo, kwani nchi inazidi kudidimia kwenye umaskini huku watu wake wakikosa huduma muhimu za kijamii.

Walisema kwa muda mrefu wamekuwa wakiwalalamikia watendaji wa serikali na chama tawala lakini rais amekuwa mgumu wa kuyashughulikia matatizo hayo.

Wanasema rais ndiye kikwazo kikubwa cha maendeleo ya chama chao na serikali, hasa kwa kuwateua mawaziri, wakurugenzi na maofisa wengine bila kuangalia uwezo wao wa kiutendaji.

“Kaka kwenye Bunge la Februari kuna mbunge alitoa kauli kuwa kama tunaona mambo hayaendi serikalini tupige kura ya kutokuwa na imani na rais, watu walimshambulia. Sasa tunaona umuhimu wa kauli yake ile,” alisema mbunge mmoja.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa makada wa CCM wameanza kuingiwa na hofu ya kubomoka kwa chama chao hasa baada ya makada wenzao kuanza kujiunga na vyama vya upinzani.
Wanasema wakati makada wa chama hicho wakiendelea kukihama uongozi wa CCM hauonekani kuchukua hatua zinazostahiki dhidi ya viongozi wanaochangia wananchi wakose imani na chama tawala.

Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe, aliweka wazi kuwa wabunge wa CCM ni lazima wakemee ubadhirifu kwakuwa Tanzania si mali ya CCM.

Mbunge huyo alikwenda mbali kwa kumtaja Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo, kuwa ni mwizi, mwongo na mbadhirifu wa mali za umma.

Mawaziri wasuasua kuwasilisha barua
Hadi jana Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema hajapokea barua ya kujiuzulu kutoka kwa waziri yeyote huku akiweka wazi kuwa kesho atatoa taarifa kamili juu ya jambo hilo.

Juzi vyombo vya habari vilipata taarifa kutoka kwenye kikao cha wabunge wa CCM kuwa baada ya wabunge kuzituhumu baadhi ya wizara kukithiri kwa ubadhirifu mawaziri wake wameamua kujiuzulu.

Taarifa hizo zilidokeza kuwa mawaziri hao walishinikizwa kuachia nyadhifa zao ili kukinusuru chama na serikali dhidi ya hasira za wananchi wanaokerwa na ufisadi.

Chami atoboa siri
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami, amejitetea kuwa wizara yake haimlindi Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Charles Ekelege, kama alivyotuhumiwa na baadhi ya wabunge.
Alisema amesononeshwa na taarifa ya ukaguzi wa CAG juu ya TBS iliyotolewa kwa waheshimiwa wabunge bila yeye mwenyewe au wizara kupewa nakala kwa kipindi cha wiki nzima.

Alisema kuwa baada ya kusikia kuwa waheshimiwa wabunge wengi wanayo taarifa hiyo na hata naibu wake kukiri bungeni kwamba taarifa imetoka wakati yeye hana nakala, alikwenda kwa Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashillilah na kuiomba nakala ya taarifa hiyo.

Alibainisha kuwa baada ya kufanya ufuatiliaji katika ofisi ya CAG ilikiri kuigawa kwa wabunge na kusahau kuipeleka kwa wizara hiyo ambayo ndiyo inayohusika.

“Hapa wasomaji wapime wenyewe. Inawezekanaje taarifa ya CAG iliyoandikwa kutokana na takwimu zilizotolewa na wizara yangu, iwafikie wabunge huku wizara yangu itakayotakiwa kuifanyia kazi taarifa yenyewe haipewi nakala, eti kwa kughafilika?

“Ni ukweli ofisi ya CAG walighafilikiwa, au jambo hili limesukwa ili kuniaibisha mimi mbele ya Watanzania, rais aliyeniteua na hasa wapiga kura wangu wa Moshi Vijijini?” alihoji.

Nundu ajitetea
Naye Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu, alisema tuhuma dhidi yake zilizoelekezwa na baadhi ya wabunge, hazina ukweli na zimelenga kumchafua.

Alisema kilichoelezwa na Kamati ya Miundombinu ni uongo na uzushi, kwani nyaraka walizozitumia kuorodhesha tuhuma dhidi yake si halali.

Kuhusu kuingilia utendaji wa Mamlaka ya Bandari kwa masilahi binafsi,  alisema si kweli, akaongeza kuwa kinachomponza ni kuipinga kampuni inayotetewa na menejimenti isipewe zabuni ya kufanya upembuzi yakinifu peke yake na kwenda kukopa na baadaye iruhusiwe kujenga gati namba 13 na 14.

“Wanasema namtaka mwekezaji  ambaye makubaliano yanaonyesha atamiliki gati hilo kwa miaka 45. Nachelea kusema ni uongo na uzushi,” alisema Nundu.

Mkuchika apata kigugumizi
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika, alipoulizwa juu ya suala hilo alishindwa kukubali wala kukataa iwapo ataandika barua ya kujiuzulu. Alimtaka mwandishi amuulize Katibu wa Kamati ya Uongozi.


CHANZO: Tanzania Daima

UPDATE:


 
Picture

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 

Gazeti la Tanzania Daima la leo Jumapili Aprili 22, 2012 lina habari katika ukurasa wake wa mbele yenye kichwa cha habari ‘JK alinda Mawaziri’, inayodai kumekuwa na mazungumzo baina ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri MkuuMhe Mizengo Pinda kuhusu hatua inayopaswa kuchukuliwa dhidi ya mawaziri waliotakiwa kujiuzulu.

Habari hiyo imedai kuwa Mhe. Pinda anataka mawaziri wanaokabiliwa na tuhuma waondoke ili kuleta uwajibikaji serikalini, lakini, imeendelea  kudai habari hiyo, “Rais Kikwete amesema mawaziri hao waachwe waendelee na kazi zao, kwa kuwa suala hilini la upepo tu, liachwe litapita”.

Tunachukua nafasi hii kuweka bayana kwamba habari katika hilo gazeti la Tanzania Daima Jumapili si za kweli, bali ni za uzushi na upotoshaji mkubwa.

Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi nchini Brazil, amerejea jana Aprili 21, 2012 jioni. Hajaonana wala kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu, Mhe. Pinda.

Hivi sasa Mhe. Rais anasubiri kupata taarifa rasmi  kutoka Bungeni Dodoma.

Mhe Rais anawasihi wananchi wasiamini habari hizo za upotoshaji zilizomo kwenye gazeti hilo la Tanzania Daima Jumapili.

Pia ametoa rai kwa wanahabari wasitoke nje ya mstari wa weledi katika kutekeleza kazi zao ili kuendelea kulinda heshima zao binafsi, vyombo wanavyofanyia kazi pamoja na taaluma yenyewe.

Mwisho

Imetolewana:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
22 Aprili, 2012


Source: SUBI

Fancy something with your cup of tea? How about a cupcake made of insects

Keki (cupacake) iliyotengenezwa kutokana na wadudu katika chuo kikuu cha Weneningen nchini Uholanzi kuongeza protini inayopatikana kwa kula wadudu

Food with a real bite: A visitor eats a fried scorpion at the Longhua temple fair during the MayDay holiday in Shanghai

Mshkaki wa ng'e huko Shanghai,China

What you looking at? A caramelised locust, ready for eating, sitting on top of a cake

Panzi kwenye keki..'.ufund'i mwingine wa kile chuo kikuu cha Uholanzi
Can you save me one? If you are holidaying in Malawi soon you can sample the roadside delight of boiled rat

Mishkaki ya panya waliochemshwa,anyone?Hii ni Malawi (reminds me of Saranda)

Not so fluffy anymore: An Andean woman cooks 'cuy', or guinea pig, during a guinea pig festival in northern Lima, Peru
Samaki nchanga huko Peru

For your dinner tonight? This Brazilian lorry driver passes on the opportunity to buy an armadillo

Wa leo leo: Panya buku huko Brazil

It's probably NOT chicken: Bush meat for sale in the Ivory Coast

It's probably NOT chicken: Bush meat for sale in the Ivory Coast

Nyama choma iliyotokana na nyama ya wanyama wa porini huko Cameroon.Kumbuka wanyama pori sio swala na nyati pekee,inawezekana ni Simba,Tumbili au kwa kukutia kichefuchefu zaidi,kenge,chatu au mbwa-pori

Fresh from the kitchen: Field rats served up in a restaurant in Guangzhou, China

Panya waliopikwa 'kiufundi' huko China.Unaona binzari hiyo?

Medium rare? Filet mignon drenched in ant sauce and topped with fried ants at the Color de Hormiga restaurant in Columbia

Fillet zilizoandaliwa 'kitaalamu' na 'kunyunyiziwa' nyuki.Sikiza,sio kwa vile nyuki wanatengeneza asali ndio imaanishe ni watamu...Anyway,kwa mapishi haya wala huwezi kudhani kuwa ni nyuki

Home made: Human breast milk stored by chef Daniel Angerer to use for cheese at his New York restaurant

Hakuna haja ya kwenda porini ilhali binadamu nao wanaweza 'kuzalisha bidhaa': Pichani ni jibini iliyotengenezwa kutokana na maziwa ya binadamu

CHANZO: Daily Mail

Muamba: I was just running along, I felt dizzy, my vision started to go... and then I felt myself falling

Fabrice Muamba has spoken for the first time about the horrifying moment he collapsed and 'died' on the pitch.
The Bolton midfielder, aged 24, insisted he had not felt unwell before his heart stopped and he crashed to the ground in the 41st minute of a televised FA Cup tie at Tottenham on March 17.
Miracle man: Fabrice Muamba with Dr Andrew Deaner, left, and Dr Sam Mohiddin
Miracle man: Fabrice Muamba with Dr Andrew Deaner, left, and Dr Sam Mohiddin
'I ran upfield to try and get on the end of a cross from Martin Petrov on our left wing and as I ran back into midfield I felt very slightly dizzy. It wasn't a normal dizziness - it was a kind of surreal feeling like I was running along inside someone else's body,' he told The Sun.
'Then I made another burst forward and noticed it again. Then my vision started to go. I had no pain whatsoever. No clutching at my chest.Then I started to see double. It felt almost like a dream. There was no one anywhere near me when I started to feel myself falling
'The last thing I remember was our defender Dedryck Boyata screaming at to get back and help out in defence. I just felt myself falling then I felt two thumps as my head hit the ground in front of me then that was it. Blackness, nothing. I was dead.'
Terrifying: Muamba lies prostrate as players and medics try to help
Terrifying: Muamba lies prostrate as players and medics try to help
Players were in tears as doctors and paramedics battled to save his life at White Hart Lane.
Muamba was effectively dead for 78 minutes and it took 15 defibrillator shocks - two on the pitch and 13 in the ambulance - to get his heart beating again. 
Bolton doctor Jonathan Tobin said: 'It was 48 minutes from the time he collapsed to the time he reached the hospital and it was a further 30 minutes in the hospital they were working on him without his heart having a muscular beat.
Nightmare: Concern is etched on faces of players and Bolton manager Owen Coyle
Nightmare: Concern is etched on faces of players and Bolton manager Owen Coyle
'In effect he was dead in that time. We were fearing the worst.'
Remarkably Muamba started talking two days after his collapse and began walking just over a fortnight later.
Muamba was released from hospital on April 16 after being fitted with a Cardioverter Defibrillator which releases an electrical charge if it detects a heart malfunction similar to the cardiac arrest he suffered against Tottenham.
Muamba is now recovering at home with fiancee Shauna Magunda and his three-year-old son Joshua. 
Emotional: Some players were in tears as Muamba was carried off
Emotional: Some players were in tears as Muamba was carried off


21 Apr 2012

A PICTURE COULD TELL A MILLION WORDS: Dogo anaonekana akitoa alama ya V (for victory over mafisadi) huku Mtoto wa Mkulima akionekana kupigwa na bumbuwazi!


20 Apr 2012




Ray amtia mbaroni Mange Kimambi
•  KUHUSISHWA KIFO CHA KANUMBA

na Irene Mark
JESHI la Polisi Mkoa wa Kinondoni, jijini Dar es Salaam, limekiri kumshikilia kwa saa kadhaa kwa mahojiano mmiliki wa ‘blog ya Uturn’, Mange Kimambi, kwa madai ya kumhusisha muigizaji maarufu nchini, Vicent Kigosi au Ray, na kifo cha nguli wa tasnia hiyo, Steven Kanumba, ‘The Great’.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Kamanda wa Polisi mkoa huo, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Charles Kenyella, alisema Ray alikwenda kulalamika kwenye kituo hicho, kuhusu maneno yaliyoandikwa kwenye mtandao huo akiomba msaada wa jeshi hilo.

“Ninathibitisha kwamba huyo dada tulimshikilia hapa kwetu tangu jana (juzi), tumemwachia leo (jana), kwa sababu dhamana ni haki yake, ila tunaendelea na upelelezi, maana anadaiwa kutuma taarifa kwenye mtandao akimhusisha Ray na kifo cha Kanumba.

“Hiyo blog haijahalalishwa kutoa taarifa za kukashifu na kuwadhalilisha watu… ameandika skandali kwa Ray, tukiiachia hii, maneno hayo yanaweza kuonekana halali na kuleta maafa katika jamii, hasa kwa huyo anayetajwa,” alisema Kamanda Kenyella na kuongeza kwamba kesi iko mahakamani, hivyo si vema kuingilia upelelezi.

Kwa upande wake, Ray aliyekuwa rafiki wa karibu wa marehemu Kanumba, alisema kitendo hicho kinahatarisha maisha yake, hivyo ameapa kulishughulikia suala hilo, huku akisisitiza kwamba suala hilo linamvunjia heshima na kumharibia kazi yake.

“Hiki sio kitu cha kweli, Kanumba ni mdogo wangu na tumetoka mbali kimaisha, huyu dada Mange Kimambi simjui… ameandika uongo, sijajua hizi habari amezipata wapi hii ni kutaka kunishushia heshima katika jamii.

“Uigizaji ndiyo kazi yangu, kwa hiyo anapoandika na kuweka kwenye intaneti inayosomwa dunia nzima, anataka kuniharibia kazi yangu? Anataka kuniharibia maisha? Anataka kunipotezea mashabiki?

“…Unategemea watu wanioneje? Hili sitaliacha, nitalifanyia kazi na kulifikisha mahakamani ili iwe fundisho kwa wanaotumia kalamu zao kutaka kuwaharibia wengine, chochote kitakachonikuta nitadili na huyo mama... haya ni maisha, nitaendelea kuvumilia Mungu yupo,” alisema Ray anayetamba kwenye medani ya filamu ndani na nje ya nchi.

Juhudi za kumpata Mange, aliyewahi kuandaa shindano la urembo la Dar Indian Ocean 2006 na kumwibua Wema Sepetu, hazikufanikiwa baada ya simu yake kutopatikana.
CHANZO: Tanzania Daima

Waziri Mkuu Pinda akifanya usanii wa kulia bungeni katika sakata la maalbino.Je hatorejea tena mbinu hii?

Tusiume maneno.Tanzania hivi sasa inayomba kwa vile Rais tuliye nae,Jakaya Kikwete,ni mithili ya mtu asiyejua kwanini Watanzania walimpa dhamana ya kuongoza nchi yetu-moja ya nchi masikini kabisa duniani licha ya utajiri luluki ilionao.

Kikwete alifanya uzembe kwa kuteua rundo la mawaziri (ambapo ukubwa tu wa Kabineti yake ni mzigo mzito kwa nchi yetu masikini) lakini kana kwamba hiyo haitoshi,akajaza wababaishaji kibao ambao aidha ni maswahiba wake au kwa busara zinazomtosha yeye pekee aliwaona wababaishaji hao kama sehemu muhimu ya timu yake ya kuwaletea Watanzania MAISHA BORA.

Hivi Rais mwenye busara angeweza kumkabidhi Mustafa Mkulo Uwaziri wa Fedha ilhali historia yake huko nyuma inafahamika vyema?Well,Kikwete hakumpa Mkulo nafasi hiyo kimakosa bali kwa sababu maalum.Teuzi za Mawaziri wa Fedha Barani Afrika huzingatia sana ushkaji kati ya Rais na mteuliwa.Kimsingi,wengi wa mawaziri wa fedha wa Afrika ni kama wahasibu binafsi wa Rais.

Si kwamba Kikwete hajui ufisadi wa Mkulo na mawaziri wengine.HAPANA.Anafahamu fika ila hawezi kuchukua hatua kwa vile Mkulo hafanyi hivyo pasipo uelewa wa bosi wake.Hapa ninamaanisha kuwa kwa kiasi kikubwa,kinacholalamikiwa kuhusu Mkulo kina baraka za Kikwete.

Sijui Tanzania itakuwa katika hali gani wakati huyu mtu anamaliza muda wake hapo 2015!Cha kusikitisha zaidi,wakati nchi inazidi kuangamia yeye yuko bize kushindana na Christopher Columbus kwenye 'safari za uvumbuzi.'

Majuzi kapewa ripoti ya ukaguzi wa fedha za serikali na CAG Ludovick Utouh.Kana kwamba kilichomo kwenye ripoti hiyo ni salamu za hepi bethdei,siku chache baadaye Kikwete huyooo safarini Brazil.Hana habari kuwa nchi inaangamia.Yey na safari,safari na yeye.Basi bora amwondoe Waziri wa Mambo ya Nje,Bernard Membe,kisha yeye Kikwete ajiongezee wadhifa wa uwaziri huo ili akisafiri hata kila wiki tujue moja.

Back to the point ya kumwajibisha Pinda na/au mawaziri,well,kama wabunge watafanikiwa kutekeleza hilo itakuwa vema.Waiwasi wangu mkubwa ni unafiki wa wengi wa wabunge wa CCM.Japo Tanzania yetu inaanza kuonyesha dalili za watu kuchoka kuiona nchi ikigeuzwa shamba la bibi,napatwa na wasiwasi kama wabunge wa CCM watakauwa tayari kumtosa Pinda au kushinikiza mawaziri mafisadi wajiuzulu.Pinda ni msanii anayeweza kuwahadaa wabunge wa chama chake kwa kulia tena hadharani....nao wakalainika.

Lakini,hata kama Pinda na mawaziri mafisadi waking'olewa,bado tutaendelea kuwa na tatizo hapo juu kabisa-yaani Kikwete na urais wake wa sandakalawe (wa kubahatisha).Ameshauthibitishia umma wa Watanzania kuwa sio tu yeye ni dhaifu wa uongozi bali pia hana nia ya kurekebisha chochote dhidi ya kansa inayoitafuna nchi yetu.

Anyway,kama kura ya kutokuwa na imani na Pinda itafanikiwa nadhani hatua itakayofuata ni kura ya kutokuwa na imani na Kikwete mwenyewe.Actually,ni kwa sababu tu ya hizi taratibu za kirasimu za kupiga kura.Sidhani kama kuna Mtanzania yeyote mwenye akili timamu ana imani na Kikwete-hasa baada ya kushindwa kutekeleza hata ahadi alizojiwekea mwenyewe pasipo shinikizo lolote lile.Kitu pekee ambacho amefanikiwa kukitekeleza kwa ufanisi mkubwa ni mashidano yake dhidi ya Vasco da Gama na Christopher Columbus.

MUNGU INUSURU TANZANIA (kwa namna yoyote ile...hata kama ni kwa majonzi) 


Pinda kumfuata Lowassa

• HATMA YA MAWAZIRI WATANO MIKONONI MWA JK

na Mwandishi wetu

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, sasa yuko katika hatari ya kuondolewa madarakani kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kufuatia tuhuma nzito za ubadhirifu wa fedha za umma unaodaiwa kuwahusisha mawaziri watano wakiongozwa na Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo.

Akiwasilisha majumuisho ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, mwenyekiti wa kamati hiyo, Zitto Kabwe, aliliambia Bunge kuwa kuanzia leo wataanza kukusanya saini za wabunge wenye nia ya kupiga kura hiyo na kwamba uamuzi wake utawasilishwa bungeni Jumatatu wiki ijayo.

Mwenyekiti huyo alisema ikiwa mawaziri hao ambao hata hivyo hakuwataja majina mmoja baada ya mwingine hawatakuwa wamejiuzulu wenyewe hadi kufikia siku hiyo, basi wabunge watamwondoa Pinda madarakani kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye.

Kwa hali hiyo, Zitto alisema kuwa itakuwa ni jukumu la mawaziri hao kabla ya Jumatatu wiki ijayo kuamua wenyewe kujiuzulu au kumwacha waziri mkuu atimuliwe.

Hatua hiyo ya Zitto ilitokana na hoja iliyokuwa imetolewa mapema na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), ambaye aliwataka wenyeviti wa kamati za Bunge wakati watakapokuwa wanajumuisha hoja zao kupendekeza kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu Pinda ikiwa mawaziri wake hawatakuwa wamejiuzulu wenyewe.

Lissu alisema wakati wa kupiga kelele umekwisha, na sasa wanachotakiwa ni kuchukua hatua, kwani mamlaka hiyo wanayo kwa mujibu wa Katiba.

“Waziri Mkuu wajibika kwa madudu ya serikali. Nitaomba wenyeviti wa kamati hizi wanapomalizia mjadala huu kupendekeza kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu kwa kujenga mfumo wa siasa wa udokozi. Tukifanya hivyo wananchi watatuamini. Ninyi chama tawala ndio mnaosababisha haya kama mtatumia wingi wenu sawasawa tutafanikiwa, sisi tupo wachache.

“Badala ya kupiga makofi, chukua hatua kwa uozo huu. Mkifanya hivyo mtaheshimika na msipofanya hivyo mtaingia kwenye vitabu vya historia,” alisema.

Alisema masuala ya ufisadi yamekuwa yakizungumzwa na zaidi ya miaka 10 sasa, lakini hawajawahi kuona serikali ikichukua hatua.

“Wakati kila mwaka CAG anatuletea taarifa za wizi, hatujawahi kuona serikali ikichukua hatua dhidi ya wahusika. Hatujawahi kuona mtendaji amechukuliwa hatua wala waziri kuwajibika katika hili. Watu wanapata kupata nafasi za uwaziri ili kuhujumu nchi,” alisema na kuongeza mfumo uliopo ni wa kulinda wezi.

Tanzania sio ya CCM

Akichangia mjadala huo, asubuhi na pia jioni, Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM) aliwafyatua mawaziri kadhaa akisema kuwa wanaongoza kwa kutafuna pesa za Watanzania na kumtaja Waziri wa Fedha Mustafa Mkullo kuwa kinara wa wizi huo.

Mbunge huyo alisema baadhi ya mawaziri wamegeuka kuwa mchwa wanaotafuta fedha za Watanzania bila woga na kuongeza kuwa sasa umefika wakati kwa wabunge kuweka tofauti za kisiasa pembeni na kuzungumza kwa umoja masuala yanayoliangamiza taifa, na katika hilo akadai kuwa hatakuwa tayari kuwaachia mawaziri wachache waangamize nchi.

“Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.

“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,” alisema mbunge huyo.

Awali Filikunjombe alisema Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, alikuwa amelidanganya Bunge kwa kudai amefuata maagizo yote ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Alisema kuwa ana ushahidi wa kutosha jinsi mawaziri hao wanavyoitafuna nchi na kuhoji Bunge linachukua hatua gani inapobainika mawaziri wamelidanganya Bunge.

“Waziri Chami amedai kuwa ametekeleza agizo la kamati kuhusu uchunguzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Uchunguzi ulifanywa wakati mkurugenzi alikuwa akiendelea na kazi, wakati kamati ilishauri wakati wa uchunguzi mkurugenzi huyo awekwe pembeni,” alisema.

Kutokana na kauli hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, ambaye pia ni mnadhimu mkuu wa shughuli za serikali bungeni, alimtaka kuthibitisha madai kuwa mawaziri wote ni wezi kwa kukabidhi ushahidi na kama hana uhakika na anachozungumza afute kauli hiyo. Hata hivyo, mbunge huyo alisisitiza kuwa alichosema ni kwamba mawaziri wengi ni wezi na si wote.

Mbunge wa Kasulu, Moses Machari, alisema wabunge wanaotaka mawaziri na wabadhirifu kunyongwa wanafanya hivyo wakiwa na akili timamu kwa sababu wamechoshwa na wizi wa waziwazi unaofanywa na mawaziri na baadhi ya viongozi wa serikali bila kuchukuliwa hatua yoyote.

Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Mjini, Vicent Nyerere (CHADEMA), alitaja waziwazi majina ya vigogo wanaomiliki kampuni za ukaguzi wa magari ambazo zilitajwa bungeni kama ni za nje, hali iliyolifanya Bunge kuzizima kwa muda.

Nyerere alisema kuwa makampuni hayo yalilipwa mamilioni ya dola za Kimarekani kwa udanganyifu, na kibaya zaidi waziri mhusika akalidanganya Bunge akidai kuwa taarifa hizo zilikuwa za uongo. Alionyesha kushangazwa kwake na nguvu kubwa ya kumlinda Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Nchini (TBS) wakati ukweli wa mambo uko wazi.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, alisema kuwa dhana iliyojengeka kuwa wizara hiyo inaibena TBS na mkurugenzi wake, haina ukweli, kwani taarifa ya kamati ndogo ya uchunguzi wa shirika hilo aliipata jana na ameshaiagiza bodi ya shirika hilo kuifanyia kazi.

Hata hivyo, alisema yuko tayari kuweka rehani uwaziri wake iwapo mbunge huyo atathibitisha kuwa kuna kampuni hewa zinazokagua magari nje ya nchi na iwapo kampuni hizo zina uswahiba naye.

“Nimekosea wapi? Kila nilichoagizwa nimetekeleza. Wizara halindi uozo. Tukilazimishwa kufanya maamuzi bila kufuata taratibu tutakuwa tunakiuka sheria,” alisema.

Ujasiri huo hata hivyo, uliyeyuka kama nta jioni, baada ya Nyerere kumuumbua kwa kutaja majina ya wamiliki wa kampuni hizo, hali iliyompa wakati mgumu waziri huyo.

Mbunge wa Nkasi, Ali Kessy (CCM), alishauri Rais Kikwete kuacha upole na kuwashughulia wote wanaotafuna mali za umma.

“Mawaziri walioshindwa kazi waondolewe na wawekwe wengine. Hakuna aliyesomea uwaziri kila mtu anaweza kuwa waziri. Unakuta kiongozi anatembea na msafara wa magari 40 unamtisha nani. Wakati watu hawana dawa wala chakula,” alisema.

Alisema kutokana na ubadhirifu huo, hata watendaji wa chini wa halmashauri wanakuwa na fedha nyingi kuliko halmashauri yenyewe, hali inayochangia kuiendesha serikali.

“Mafisadi wote tuwanyonge. Tukishanyonga 10 wataogopa. Leteni muswada mtu yeyote mwizi wa mali za umma anyongwe na mali itaifishwe. Tutaokoa nchi yetu. Wabunge tuwe wakali, lisiwe Bunge la mchezo mchezo,” alisema.

Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba, alisema kila wizara kuna mambo ya hivyo na kusema kinachoonekana mawziri hawajali suala hilo.

“Wabunge wa CCM twende kwenye Party Cacus tukafanye kazi tuliyotumwa. Kama kuna mtu atatulaumu basi, tuondoe waziri asiyefaa. Mbilinyi, Iddi Simba na Ngasongwa waliondolewa humu ndani. Tufanye kazi ya kibunge jamani. Nawaomba wabunge tufanye jukumu letu na tukifanya hakuna waziri atakayefanya mchezo,” alisema.

Wabunge waridhia vikao bila posho

Kutokana na uzito wa suala hilo, wabunge wameunga mkono hoja ya kuendelea na mjadala huo kwa kuongeza siku mbili zaidi hata kama vikao hivyo havitakuwa na posho.

Hoja hiyo ilitolewa na mbunge wa Buchosa, Dk. Charles Tizeba (CCM), ambaye alisema siku zilizotengwa kwa ajili ya kuchangia mjadala huo ni chache, hivyo wabunge wote walioomba kuchangia wanaweza wasipate nafasi.

“Mjadala huu ni muhimu sana, tunaomba kuongezewa siku mbili au tatu za kujadili suala hili hata kama hakuna posho tutafanya hivyo,” alisema Tizeba na hoja hiyo kuungwa mkono na nusu ya wabunge waliokuwapo ukumbini hapo.

Naibu Spika, Job Ndugai, alieleza kuwa hajawahi kuona hoja iliyoungwa mkono kama hiyo na kusema suala hilo atalifikisha kwa Spika, Anne Makinda, ambaye naye atajadiliana nayo na kamati ya uongozi na ndipo atakapotoa majibu kuhusiana na hoja hiyo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalum, Christowaja Mtinda (CHADEMA), alisema suala la mishahara hewa limekuwa sugu katika elimu ya juu na kwamba imefikia hatua jina lake limetumika katika suala hilo.

“Pale Open University kuna mtumishi anaitwa Christowanja Mtinda. Sijawahi kuomba kazi hapo wala kufanya kazi hata siku moja,” alisema.

Aidha, alisema makatibu wakuu hawakai katika nyumba zao zilizoko Dodoma na kusema kuwa wanazitumia wakati wa bikao vya Bunge na kuhoji kwa nini nyumba hizo wasipewe wabunge ambao wanapokuwa wanahudhuria vikao vya Bunge wanapata shida kupata nyumba za kuishi.

Naye Mbunge wa Kibiti, Abdul Marombwa, alishauri wabunge wapitishe sheria ya kuwapo kwa kamati kwa ajili mawaziri wanaoshindwa kuwajibika.

“Wenzetu wa Kenya wameanzisha sheria kwa ajili ya mawaziri wanaotoa ahadi zisizotekelezeka. Baada ya miezi miwili anaulizwa ametekeleza ahadi kwa kiwango gani, akishindwa anatimuliwa. Kenya wameshafukuza mawaziri. Tukianzisha hiyo mawaziri watahakikisha ahadi zao zinatekelezeka. Ni lazima tuwe na mahali pa kuanzia,” alisema.

Aidha, alihoji wizara kutumia fedha nyingi katika maonesho mbalimbali kama Sabasaba, Nanenane na utumishi na kuhoji yameleta manufaa gani nchini. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imetumia sh bilioni 1.9 kwa ajili ya maonesho kama hayo katika kipindi cha mwaka 2009/2010.

Mapema asubuhi, Zitto alikuwa ameliomba Bunge kutoa kumbukumbu za mwaka jana kutokana na Waziri Aggrey Mwanri kuendelea kutoa ahadi bila kuwapo kwa utekelezaji.

“Ukichukua ‘hansard’ ya mwaka jana ukasoma maelezo ya majibu ya hoja hayana tofauti na haya anayotaka kutuaminisha leo. Mheshimiwa Naibu Spika naomba kupata mwongozo wako tupate hansard ya mwaka jana ya maelezo ya Mheshimiwa Waziri ili tulinganishe na maelezo ya sasa na aliyotolewa mwaka jana na tuone kama ametekeleza,” alisema Zitto.

Zitto alitoa kauli hiyo, baada ya Waziri Mwanri kueleza serikali imekuwa ikiingilia kati maeneo ambayo yanaona hayaendi na kusema kuwa watakapoanza kushughulikia masuala yanayolalamikiwa na wabunge wasianze kushikwa mikono.

“Tunaomba wabunge tusaidiane; tuseme hakuna kumhamisha mtumishi yeyote aliyekwenda kinyume na tutamchukulia hatua hapo hapo,” alisema.

Aidha, alisema baraza la madiwani limepewa nguvu kushughulikia matatizo yote ya halmashauri husika na kuongeza kwamba hiyo ni vita iliyopangwa na isiyopangwa.

“Hilo rungu tumeshapewa. Tuachieni. Mrema naomba tuamini. Tukitoka hapa kazi ni moja kashi kashi tu...lugha hii inatokana na mazungumzo ya hapa ndani. Halmashauri zilizopata hati chafu, zimeshakabidhiwa barua, haiwezekani sh bilioni 6 zinaondoka halafu mkurugenzi anaendelea kuwapo,” alisema.

Hatma ya mawaziri kwa JK

HATMA ya mawaziri watano wanaotuhumiwa kwa ubadhirifu wa mali ya umma sasa iko mikononi mwa Rais Jakaya Kikwete, kufuatia hatua ya wabunge wa Chama cha Mapinduzi kutaka watendaji hao wajiuzulu.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya kikao cha wabunge wa CCM kilichofanyika jana mchana mjini hapa zimesema kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ameamua kulifikisha suala hilo mikononi mwa Rais Kikwete kwa uamuzi zaidi.

Chanzo chetu cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho, kimewataja wabunge wanaotakiwa kujiuzulu kuwa ni pamoja na waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, na Naibu wake, Lazaro Nyalandu, Waziri wa Fedha, Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),George Mkuchika, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu na Waziri wa Afya, Dk. Haji Mponda.

Katika kikao hicho cha dharura kilichokuwa chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu Pinda, wabunge hao walisema mawaziri hao wameiaibisha serikali kwa kiwango kikubwa, hali iliyosababisha wananchi kukosa imani na serikali yao na kuichukia.

Kikao hicho kilichoanza saa 7 mchana na kumalizika saa 11 jioni kilikuwa na mvutano mkali kati ya wabunge hao na mawaziri.


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.