8 Aug 2012


JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALI ASILI NA UTALII
 
 





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI – (PRESS RELEASE) ILIYOTOLEWA NA WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, MHE. BALOZI KHAMIS .S. KAGASHEKI LIWALE
TAREHE 8/8/2012


NDUGU WAANDISHI WA VYOMBO VYA  HABARI:

1.0    SALAMU ZA JUMLA:
NACHUKUA NAFASI HII KUWAKARIBISHA NA KUWAPONGEZA KWA JINSI MNAVYOSHIRIKIANA NA WIZARA HII KUPIGA VITA UHALIFU / UJANGILI WA RASILIMALI ZA TAIFA. AIDHA NATAMBUA JINSI MLIVYOTENGA MUDA WENU  NA KUFIKA HAPA ILI TUPEANE TAARIFA ZA KIUTENDAJI HUSUSANI OPERESHENI INAYOENDELEA KATIKA WILAYA YA LIWALE MKOA WA  LINDI.

NDUGU WANAHABARI:
2.0           UTEKELEZAJI WA  OPERESHENI:
KUMEKUWA NA ONGEZEKO LA VITENDO / WIMBI LA UHALIFU / UJANGILI WA NYARA ZA SERIKALI AMBAO UNAATHIRI RASILIMALI ZA TAIFA HUSUSANI WANYAPORI TEMBO, VIBOKO, SIMBA, MAMBA, TWIGA, NYATI NA WANYAMA WENGINE PAMOJA NA UVUNAJI HARAMU WA MAZAO YA MISITU. KUTOKANA NA HALI HIYO, WIZARA YA MALI ASILI NA UTALII ILIOMBA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI KUPITIA WIZARA YA MAMBO NDANI YA NCHI KUANDAA OPERESHENI MAALUM WILAYANI LIWALE KUDHIBITI HALI HIYO. JESHI LA POLISI LILIKIAGIZA KITENGO CHA KUPAMBANA NA UHALIFU MKUBWA NCHINI (NATIONAL AND TRANSNATIONAL SERIOUS CRIME INVESTIGATION UNIT – NATIONAL TASK FORCE) AMBACHO KINAVISHIRIKISHA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYA (POLISI, JWTZ, TISS, MAGEREZA, UHAMIAJI NA OFISI YA DPP) KUTEKELEZA MAJUKUMU YA OPERESHENI MAALUM KAMA ILIVYOELEKEZWA. OPERESHENI HII ILIANZA TAREHE 22/07/2012  NA NI ENDELEVU. KATIKA OPERESHENI HIYO MAOFISA WAKUU WAANDAMIZI, MAOFISA WA KATI, WAKAGUZI NA ASKARI WA KAWAIDA KUTOKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA TAJWA HAPO JUU WANASHIRIKI UTEKELEZAJI WA OPERESHENI HIYO.  

MATOKEO YA AWALI YA UTEKELEZAJI WA OPERESHENI HII NI KAMA IFUATAVYO;
v WATUHUMIWA 101 NA KESI 101 ZIMEFUNGULIWA KITUO CHA POLISI LIWALE KATI YA HIZO:

i.                     KESI  15 ZIMEFIKISHWA MAHAKAMANI NA MIONGONI MWAKE KESI MOJA (1) IMETOLEWA HUKUMU NA ZILIZOBAKI ZIKO KWENYE HATUA MBALIMBALI MAHAKAMANI,

ii.                  KESI 20 ZIMESIKILIZWA NA KUPATA HUKUMU YA “BINDING OVER”, MIONGONI MWAKE KESI 7 ZIMEPATA MAAMUZI NA 13 ZINASUBIRI MAAMUZI YA MAHAKAMA. MASHARTI YA “BINDING OVER” YALIYOTOLEWA YAMETOLEWA DHIDI YA WATUHUMIWA;
a.                 KUTOTOKA NJE YA WILAYA YA LIWALE BILA KIBALI CHA HAKIMU MKAZI WA WILAYA

b.                KURIPOTI KWA OC CID KITUO CHA POLISI LIWALE  KILA MWISHO WA MWEZI

c.                 KUITWA KUHOJIWA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA WAKATI WOWOTE KADRI ITAKAVYOONA INAFAA
d.                KUTOFANYA KOSA LOLOTE NDANI YA MIAKA MIWILI YA MATAZAMIO

e.                 KWA WALIOKUWA WAMILIKI WA SILAHA, SILAHA ZAO ZIMEHODHIWA POLISI LIWALE KWA MUDA WA MIAKA MIWILI NA MMILIKI ATAWAJIBIKA KUANZA TARATIBU ZA MAOMBI YA KUMILIKI SILAHA HIYO / HIZO UPYA PINDI UTEKELEZAJI WA HUKUMU HIYO ITAKAPOMALIZIKA

f.                  KUWEKA DHAMANA YA MALI ISIYOHAMISHIKA YENYE THAMANI YA TSH. 5,000, 000.00 NA MALI HIZO ZIWE NDANI YA WILAYA YA LIWALE


II.        KESI 66 ZINAENDELEA KUFANYIWA UCHUNGUZI ILI WAHUSIKA WAFIKISHWE MAHAKAMANI
v AIDHA KATIKA OPERESHENI HII VIJIJI 27 VYA WILAYA YA LIWALE VINGI VIKIWA VIMEPAKANA NA HIFADHI YA SELOUS VIMEHUSIKA. MATOKEO YAKE NI KUPATIKANA KWA SILAHA 80, RISASI 674 NA MAGANDA YA RISASI 289 KAMA IFUATAVYO;
v BUNDUKI 79 ZILIZOKAMATWA NI;
i.                    SAR - 1,
ii.                RIFLE - 16
iii.             SHOT GUN  - 63

v JUMLA YA RISASI 645 ZIMEKAMATWA NI;
i.                    SAR - 20,
ii.                RIFLE - 8
iii.             SHOT GUN – 647

v MAGANDA YA RISASI 289 YALIYOKAMATWA NI  ;
i.                   RIFLE - 99
ii.                 SHOT GUN – 190

v NYARA ZA SERIKALI;
SN
AINA YA NYARA ZILIZOKAMATWA
KIASI
THAMANI TSH
1
MENO YA KIBOKO,
80
18,892,500.00
3
MENO YA TEMBO
14
164,075,000.00
5
BANGILI MOJA YA USINGA WA MKIA WA TEMBO
1
23, 625, 000.00, 
6
NGOZI  ZA SIMBA,
2
15,435,000.00
7
NGOZI YA CHUI,
1
5,505,500.00
9
MIKIA MIWILI YA NGEDERE
2
378,000.00
10
KICHWA CHA NYATI CHENYE PEMBE 2,
1
2,992,500.00
11
NYAMA YA  NYATI ,
KG
2,988,700.00
12
KICHWA CHA POFU CHENYE PEMBE 2,
1
2,677,500.00
JUMLA KUU
212,944,700.00

v VIELELEZO VINGINEVYO
o       GARI NDOGO AINA YA  TOYOTA CORONA NO. T. 836 ADV 

o       PIKIPIKI MBILI ZA SANLG T. 901 BXQ NA T. 772 BSD

o       MSUMENO WA MBAO NA MBAO 149



3.0    LENGO LA OPERESHENI;
OPERESHENI HII MAALUM INALENGA KUZUIA, KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA UHALIFU / UJANGILI KATIKA MAENEO MBALIMBALI NCHINI WILAYA YA LIWALE IKIWA KAMA ‘ROLE MODEL’.

4.0           MAFANIKIO;
I.                  KWA KUWA OPERESHENI HII IMEPANGWA NA KUENDESHWA KITAALAM NA KISAYANSI (INTELLIGENCE LED OPERATIONS), MAFANIKIO YAFUATAYO YAMEJIDHIHIRISHA;

a.                 IMEUNGWA MKONO NA KUSIFIWA NA RAIA NA WANANCHI KWA UJUMLA KWA MAELEZO KUWA HAKUNA MTUHUMIWA ALIYEKAMATWA KWA KUONEWA.

b.                 KUMEKUWEPO NA MAPOKEO CHANYA (POSITIVE IMPACT) KUTOKANA NA WANANCHI KUTAMBUA KUWA MWENENDO WA OPERESHENI HII UNAIPA HESHIMA KUBWA SERIKALI

c.                 HAKUKUWA NA RAIA MWEMA ALIYEBUGHUDHIWA AU KULALAMIKIA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA OPERESHENI HII

ii.                MTANDAO WA UHALIFU WA UJANGILI UNAVUNJWA NA WAHUSIKA WOTE SASA WANAFAHAMIKA NA UCHUNGUZI MAKINI NA WA KINA UNAENDELEA DHIDI YAO NA WATAFIKISHWA MBELE YA MAHAKAMA NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE

iii.             BAADHI YA WAZEE WENYE UMRI MKUBWA NA AMBAO AFYA ZAO ZILIONEKANA KUTOMUDU MASHARTI YA KUENDELEA KUMILIKI SILAHA WALIZISALIMISHA WENYEWE NA KUOMBA ZIHIFADHIWE KATIKA KITUO CHA POLISI LIWALE MPAKA MAAMUZI YATAKAPOTOLEWA NA MAHAKAMA DHIDI YA SILAHA HIZO.

iv.             WALE AMBAO MAHAKAMA ITAONA WAMEPOTEZA SIFA ZA KUMILIKI SILAHA ZITAHODHIWA KITUO CHA POLISI KUSUBIRI UTEKELEZAJI WA MAAMUZI YA MAHAKAMA


5.0           CHANGAMOTO:
i.                   BAADHI YA WAMILIKI WA SILAHA SIO WAAMINIFU    KWA KUWA WANATUMIA SILAHA ZAO KUFANYA UJANGILI AU KUZIAZIMISHA KWA MAJANGILI. 

ii.                BAADHI YA WAMILIKI WA SILAHA WAMEPOTEZA SIFA ZA UMILIKI KUTOKANA NA MATATIZO YA KIAFYA; MFANO KUKABILIWA NA UPOFU, UGONJWA WA KIHARUSI N.K JAMBO AMBALO LINACHANGIA WAO KUSHINDWA KUZINGATIA NA KUTEKELEZA TARATIBU ZA UMILIKI WA SILAHA

6.0           MUONO WA MBELE (WAY FORWARD);
i.                   WIZARA YA MALI ASILI NA UTALII ITAENDELEA KUTOA ELIMU KWA JAMII ZINAZOISHI KANDOKANDO YA MAPORI YA AKIBA /  HIFADHI KUHUSU UMUHIMU WAO WA KUTOJIHUSISHA NA UJANGILI NA WAWE VYANZO VYA TAARIFA ZA KIINTELIJENSIA KUFUATIA MKAKATI MADHUBUTI WA KUDHIBITI MTANDAO WA UJANGILI NCHINI.

ii.                UTAKUWEPO MWENDELEZO WA KUBORESHA NA KUIMARISHA DORIA, MISAKO NA HATUA NYINGINE ZA KIOPERESHENI KWENYE MAPORI YA AKIBA NA HIFADHI ZA TAIFA MARA KWA MARA KUFUATIA MUONGOZO WA TAARIFA ZA KIINTELIJENSIA KADRI ITAKAVYOONEKANA INAFAA KATIKA KUFANYA OPERESHENI ZA PAMOJA (JOINT OPERATIONS INVESTIGATIONS & INTELIGENCE –JOII)  KWA KUTUMIA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUPITIA “TASK FORCE” YA KITAIFA .

7.0    MWISHO
NAWAPONGEZA MAOFISA WAANDAMIZI, MAOFISA WA KATI, WAKAGUZI NA ASKARI WA VYEO MBALIMBALI WANAOSHIRIKI UTEKELEZAJI WA OPERESHENI HII INAYOENDELEA. KWA UJUMLA NAMALIZIA KWA KUWASHUKURU TENA NYINYI WANAHABARI MLIOFIKA HAPA KWA USHIRIKIANO MNAOUTOA KATIKA KUPAMBANA NA UHALIFU HUU.


ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA
//////////////////////////////////////////MWISHO///////////////////////////////////////

IMETOLEWA TAREHE  08/08/2012  NA

MHE. BALOZI KHAMIS .S. KAGASHEKI (MB)
WAZIRI


NAKALA KWA:
VYOMBO VYA HABARI

6 Aug 2012

Champion again: Jamaica's Usain Bolt crosses the finish line to win gold in the men's 100-metre final in the Olympic Stadium in London
BOLT AKIVUKA MSTARI NA KUSHINDA


Outright winner: Usain Bolt streaks clear of the field to claim gold from lane seven in one of the most eagerly awaited Olympic events ever
USAIN BOLT AKIMALIZA MBIO NA KUSHINDA 



Showman: Usain Bolt celebrates his victory by striking his customary lightning bolt pose in the Olympic Stadium in London
USAIN BOLT AKIONYESHA POZI YAKE MAARUFU YA 'RADI' (LIGHTNING BOLT) BAADA YA KUSHINDA


Points ahead: Usain Bolt proved his doubters wrong and retained the Olympic 100m title he first won in Beijing in 2008
USAIN BOLT AKIWEKA POZI YAKE BAADA YA KUSHINDA


Taking a bow: Jamaica's Usain Bolt kneels and rests his head against the track in the Olympic Stadium after recording the second-fastest time ever
USAIN BOLT AKIINAMISHA KICHWA ARHDINI BAADA YA KUSHINDA


Star attractions: Jamaican sprinters Usain Bolt (right) and Yohan Blake (left) are mobbed by fans after winning gold and silver in the race
USAIN BOLT NA YOHAN BLAKE WAKISHANGILIA NA MASHABIKI


Golden boy: The Olympic champion in typical pose with the Olympic mascot
USAIN BOLT AKIWA NA MDOLI (MASCOT) WA OLIMPIKI


They're off: Usain Bolt (third left) did not start well in lane seven but he was comfortably leading the field as the athletes entered the final 20 metres
USAIN BOLT HAKUANZA VIZURI SANA KWENYE MSTARI (LANE) WA SABA LAKINI AKAMUDU KUSHINDA KWA KISHINDO


Effort: The world's fastest men - Usain Bolt (second left), Justin Gatlin (left), Yohan Blake (second right) and Tyson Gay (right) - strive to reach the line first
BINADAMU WENYE KASI KULIKO WOTE DUNIANI


Storming in front: Bolt (second left) crosses the finish line first, ahead of fellow Jamaican Yohan Blake (second right) and bronze medallist Justin Gatlin (centre)
NI USAIN BOLT TENA


Global appeal: Some 80,000 spectators in the Olympic Stadium watched the 100-metre race, as well as an estimated worldwide television audience of up to two billion
USAIN BOLT AKIMALIZA MBIO KWA KISHINDO


Picture perfect: Cameras flash as spectators capture the moment that Usain Bolt left his competitors in his wake
BINADAMU MWENYE KASI ZAIDI USAIN BOLT AKIWEKA REKODI MPYA YA OLIMPIKI HUKU PATNA WAKE  WA MAZOEZI ,MJAMAIKA YOHAN BLAKE (WA TATU KULIA) AKISHIKA NAFASI YA PILI NA MMAREKANI JUSTIN GATLIN (WA TATU KUSHOTO) AKISHIKA NAFASI YA TATU


Number one: Usain Bolt raises a finger after clinching victory, with the time reading 9.64 seconds on the electronic board behind. The time was later officially rounded down to 9.63 seconds
USAIN BOLT AKIWEKA REKODI MPYA 


Rapid results: Bolt ran the second-fastest time ever - an Olympic record of 9.63 seconds. Yohan Blake won silver with a time of 9.75 and Justin Gatlin took bronze in 9.79. Seven men clocked a time below 10 seconds
MATOKEO


World order: American bronze medallist Justin Gatlin (left) can only look on with envy as Jamaica's Usain Bolt (right) rewrites Olympic history once again
MWANARIADHA WA MAREKANI JUSTIN GATLIN ALIYESHIKA NAFASI YA TATU AKIMWANGALIA USAIN BOLT



On fire: Usain Bolt runs past the Olympic flame after winning the sprint final for Jamaica in scintillating fashion
USAIN BOLT AKIPITA PEMBENI YA 'MWENGE WA OLIMPIKI'  BAADA YA KUSHINDA MBIO ZA MITA 1OO WANAUME


Out of contention: Usain Bolt's Jamaican team-mate Asafa Powell, who pulled up injured during the race, looks forlorn after finishing eighth
MWANARIADHA WA JAMAIKA ASAFA POWEEL AKIWA AMESHIKA TAMA BAADA YA KUMALIZA WA MWISHO KUFUATIA MATATIZO YA MISULI


Bolt's our boy: Fans in Brixton watch Usain storm to victory in the 100m
MASHABIKI KATIKA KITONGOJI CHA BRIXTON JIJINI LONDON WAKISHANGILIA USHINDI WA USAIN BOLT


Fans who watched the race at the O2 Arena salute their hero with his 'Lightning Bolt' pose
MASHABIKI WAKISHANGILIA KWENYE UWANJA WA O2 HUKU WAKIONYESHA POZI YA USAIN BOLT


By Royal appointment: The Duke and Duchess of Cambridge and Prince Harry, sitting in front of the Culture Secretary Jeremy Hunt, were among the 80,000 spectators inside the Olympic Stadium
DUKE NA DUCHESS WA CAMBRIDGE NA PRINCE HARRY WAKIWA NA 'WAZIRI' WA UTAMADUNI JEREMY HUNT (NYUMA YA DUKE)



Behind Bolt: Prince Harry wore Jamaican colours as he accompanied his brother and sister-in-law at the athletics
DUKE NA DUCHESS WA CAMBRIDGE (PRINCE WILLIAM NA MKEWE KATE MIDDLETON-WA KWANZA NA WA PILI KUSHOTO) WAKIFUATILIA KASI YA USAIN BOLT HUKU PRINCE HARRY AKIWA AMEJITUNDIKA BENDERA YA JAMAIKA


Psyched: Jamaica's Yohan Blake, pictured gesturing prior to competing in his semi-final, was one of the favourites for the Olympic title as he came into the race in excellent form
YOHAN BLAKE, PATNA WA MAZOEZI WA USAIN BOLT ALIKUWA AKITARAJIA KUTOA UPINZANI MKALI LAKINI AKAISHIA KUWA WA PILI


Fighting fit: Usain Bolt, who had been troubled by a hamstring injury, claimed he was only 95 per cent fit but he looked in fine condition before the eagerly awaited final
USAIN BOLT AKIFANYWA MBWEMBWE KABLA YA MCHUANO


Fervour: Spectators from the Jamaican community in Brixton, south London, watch their heroes in action on television on the 50th anniversary of the Caribbean island's independence from Britain
JUMUIYA YA WAJAMAIKA KATIKA KITONGOJI CHA BRIXTON,JIJINI LONDON WAKIFUATILIA USHIRIKI WA WANARIADHA WAO 


CHANZO: Daily Mail

5 Aug 2012


Makada wa CCM wakiwa na kadi za  uwanachama kwa wanachama wapya  katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akipata picha na tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha CCM, katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha Mapenduzi CCM

  
Baadhi ya waTanzania mbali mbali waliohudhuria kwenye futari hiyo ilioandaliwa na tawi la CCM DMV

Baadhi ya waTanzania waliovalia rangi za chama cha CCM wakiwa kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

  Makada wa CCM Tawi la DMV shoto Mbunifu wa Ma Winny Casey Khanga Wrap Designer, pamoja na Peter Ligate (Picha ya kulia) wakiwa katika mpango mzima wa futari ya pamoja ilioandaliwa na wanatawi la CCM DMV

Watanzania  waliojumuika  kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

  
Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akiwakaribisha rasmi  wageni walikwa  kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.


Baadhi ya wanachama wa  CCM Tawi la DMV wakipata picha ya pamoja baada ya futari walioiyanda 


Wanachama wa  CCM Tawi la DMV na baadhi ya wageni wawili kutoka Londan Uingereza

Wageni wawili majirani wapendanao kutoka jijini London pia walihudhuria katika futari hiyo ilioandaliwa na  ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani


Katibu wa CCM DMV Jacob Kinyemi, kushoto akipata picha ya pamoja na  Halima baada ya kumkabidhi rasmi kadi ya uwanachama wa CCM, Jana Ijumaa  na kuwa mwanachama rasmi wa CCM



Chanzo: SWAHILIVILLA

4 Aug 2012


The Arab Spring has changed the landscape in North Africa, not only politically but also culturally and musically. Spreading throughout the region alongside demands for political freedom, rap music has become a popular way for people to express their desire for change.

The Arab Spring: Dawn of a musical revolution 
Across North Africa and the Middle East people have risen up and demanded a voice. And while the calls may have been political in nature, protestors have used various cultural means to express their desire for change, including music and, specifically, rap.

Media has been at the very heart of the demands for change, with the young using tools such as the internet to spread their message. Music has been another weapon. So often a voice for the disenfranchised, rap music has political defiance and revolutionary ideals at its very core. So it is hardly surprising that the genre has taken off in North Africa in the past 18 months, providing people with the means to express themselves.

The changing voice of rap music
Coming out of the U.S. in the 70s, rap became a global phenomenon in the 80s and has had a presence in North Africa since the 90s. But it is only with the demise of dictatorships in Tunisia, Egypt and Libya that the genre was able to free itself from censorship.

Previously, few had dared to speak out against their governments, fearful of retribution. But the Arab Spring has given young musicians the confidence to speak out. Some of the biggest artists in this musical groundswell are Tunisia's El General, DJ Costa and Psyco-M; Egypt's Ahmed Mekky, Ramy Donjewan and Arabian Knightz; and Libya's Emad Abbar and Hamza Sisi. The popularity of these and other artists continues to grow by the day.

The revolution will be televised… online
The internet has made it easier than ever to share music and in the face of state censorship artists relied on the Web to spread their message enabling their songs to spread from city to city and cross national boundaries.

Traditional media channels such as newspapers and television may have been muted by state control, but crumbling regimes were powerless to contain Twitter and Facebook. These social tools gave young people across North Africa a way to connect with others who felt the same and unite behind the revolutionary ideals expressed in the lyrics of their songs. 


SOURCE: Yahoo! News


KUNA msemo mmoja ninaopenda sana kuutumia kusisitiza hoja katika maongezi, ambao unasema, “Ili uweze kulielewa giza inabidi utoke au uende katika mwanga, na kinyume chake (vice versa).”
Huwa ninautumia msemo huu kubainisha ‘faida’ tuliyonayo baadhi yetu (Watanzania) tulio nje ya nchi yetu. Kwamba, kuwa kwetu huku kwa namna fulani kunatusaidia kuwa kama kile kinachofahamika katika tafiti kuwa ni “participant as an observer,” yaani kwa tafsiri isiyo rasmi ‘mshiriki ambaye pia ni kama mwangalizi.’
Kwa kuwa huku ughaibuni sio tu tunapata fursa ya kulinganisha tofauti ya mambo kati ya hapa na huko nyumbani bali pia tunaweza kuiangalia jamii yetu inayotuhusu lakini tukabaki watazamaji.
Hata hivyo, kuna wakati baadhi yetu tulio nje hukumbanana wakati mgumu kuzungumzia mambo ya huko nyumbani, hususan, kutokana na madai kuwa yanayotokea huku hayatugusi moja kwa moja.
Baadhi ya ‘wapinzani wetu’ hudiriki kwenda mbali zaidi na kutulinganisha na Watanzania ‘tusio kamili’ kwa maana ya kwamba shida au raha za huku  hazitukabili katika namna zinavyowakabili wao.
Huu ni mtizamo potofu hasa ikizingatiwa kuwa wengi wetu, kama si sote, bado tuna ndugu, jamaa na marafiki huko nyumbani. Kimsingi, kuwa nje ya Tanzania hakumpunguzii mtu Utanzania wake, isipokuwa tu kwa wenzetu wachache ambao kuwa kwao huku kunamaanisha ‘talaka’ kati yao na asili yao.
Ni katika kuiangalia nchi yetu kwa mtizamo huo wa ‘mshiriki ambaye ni kama mwangalizi’ ndipo nimejikuta nikifikia hitimisho kwamba mwenendo wa mambo huko nyumbani una mushkeli.
Kati ya wiki iliyopita na muda huu ninapoandaa makala hii kumejitokeza matukio kadhaa yanayoweza kuashiria kuwa nchi yetu inakwenda ‘ndivyo sivyo.’
Nitatoa mifano machache. Habari ambayo imetawala katika vyombo vingi vya habari kwa sasa kuhusu mambo yalivyo huko nyumbani ni hili suala la baadhi ya wabunge kutuhumiwa kupokea rushwa.
Habari hiyo inapata uzito mkubwa zaidi pale inapotanabahisha kuwa licha ya baadhi ya wabunge kuandamwa na tuhuma hizo, baadhi ya Kamati za Bunge pia zinatuhumiwa kujihusisha na rushwa, hali iliyopelekea Spika wa Bunge kuamua kuivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.
Lakini tuhuma hizi za rushwa zimefichua kitu ambacho binafsi ninakiona kama tatizo la msingi katika jamii yetu. Katika siku chache zilizopita, nimekuwa nikitumia muda wangu mwingi katika mtandao wa kijamii wa twitter kuzungumzia tuhuma hizo dhidi ya wabunge, hususan, wale wanaodaiwa kupokea mlungula ili kulifisadi Shirika la Umeme (TANESCO).
Jumapili iliyopita mmoja wa tunaoweza kuwaita watu maarufu (celebrities) alionekana kuchukizwa na twiti zangu ambazo kimsingi zilikuwa zinaelekezwa kwa mbunge mmoja wa chama cha upinzani ambaye ametangaza dhahiri kuwa ana nia ya kuwa rais wetu huko mbele.
Katika mazingira ya kawaida tu, mwanasiasa anayetamka hadharani kuwa anataka kuwa rais ni lazima aangaliwe kwa makini ili wapiga kura wapate fursa nzuri ya kumuelewa.
Kwa sababu anazozijua yeye binafsi, celebrity huyo wa kike alinivurumishia maneno makali akidai kuwa tuhuma nilizotoa dhidi ya mwanasiasa huyo zina dalili za chuki binafsi, hasa kwa ile haijathibitishwa kuwa mwanasiasa huyo ni fisadi.
Lakini kabla sijatulia,      mwanamama mwingine msomi na mwenye wadhifa kwenye taasisi moja ya umma naye akanihoji ni mahali gani mwanasiasa huyo ametajwa kuwa ni mwizi. Labda hadi hapa msomaji unaweza kujiuliza kwanini ‘utetezi’ dhidi ya mwanasiasa huyo unaonekana kwa jinsia moja tu.
Huyu mtu wa pili kukerwa natwiti zangu kuhusu mwanasiasa huyo ndiye aliyenigusa zaidi, kwa sababu kimsingi, elimu na madaraka yake yanamweka katika kundi la kijamii linalofahamika kama tabaka la kati.
Nilishawahi kuandika katika makala moja huko nyuma kuhusu jinsi tabaka hili la kati linavyoshindwa kuwa kiunganishi cha kupigania maslahi ya tabaka la chini la walalahoi.
Nilieleza katika makala hiyo kwamba tabaka la kati lingeweza kuwa nguvu muhimu ya kupigania maslahi ya tabaka la chini kutambuliwa, na hatimaye kufanyiwa kazi na tabaka la juu (ambalo hujumuisha tabaka tawala).
Nikinukuu maneno ya binti huyo wa pili, alinieleza kuwa “wanamchukia mwanasiasa huyo wajinyonge, kwani njia yake kuelekea Ikulu ipo wazi.” Niliguswa sana na maneno haya kwa sababu wakati mwanasiasa huyo anaonekana kupata utetezi katika tuhuma zinazomkabili kuhusu kuifisadi TANESCO, sio tu kuna watuhumiwa wengine wasiotetewa bali pia hata huko nyuma baadhi ya wanasiasa waliotuhumiwa kuwa mafisadi hawakuwahi kutetewa kiasi hicho.
Japo ninatambua na kuheshimu haki ya kila Mtanzania kumtetea mwanasiasa anayempenda, ukweli ni kwamba licha ya utetezi huo kuwa wa ‘upendeleo’ (kile kinachoitwa na Waingereza kuwa ni haki ya upendeleo-selective justice), kwa maana ya kuwa watuhumiwa wengine kwenye kashfa hiyo hawapati utetezi kama ilivyo kwa mwanasiasa huyo, tunapotetea tuhuma za ufisadi kwa vile tu ‘tuna mahaba’ na tunaowateta, tunaweza kuwafahamasisha mafisadi wengine waendelee kuitafuna nchi yetu wakijua watatetewa.
Moja ya mambo yanayokwaza sana maendeleo yetu ni kile ninachokiita ‘siasa za mahaba.’ Kwamba mgombea uongozi hapimwi kutokana na sifa na/au uwezo wa kutumikia umma bali kinachoangaliwa ni urafiki, haiba na vitu kama hivyo visivyoweza kuwa vigezo vya uongozi bora
Bado ni mapema kutoa hitimisho kuhusu wabunge wanaotuhumiwa kujihusisha na rushwa, hususan hiyo ya kuihujumu TANESCO, ukweli kwamba tuhuma hizo zimewekwa hadharani unaeleza bayana kuwa ufisadi umeingia katika hatua mpya na ya hatari zaidi ambapo baadhi ya watu tuliowakabidhi dhamana ya kutunga sheria (ikiwa ni pamoja na zile za dhidi ya ufisadi) nao ni sehemu ya tatizo la ufisadi.
Nimebainisha hapo mwanzoni kuwa matukio ya hivi karibuni yanaashiria kwamba hali ya mambo si shwari. Jingine lililonigusa ni suala la mgomo wa walimu ambapo japo kumekuwa na taarifa za kukanganya, kuna dalili kuwa mgomo huo unaendelea.
Lakini tukio lililotokea katika shule ya msingi ya Maili Moja, Kibaha, linaweza kutufumbua macho zaidi kuhusu mwenendo wa nchi yetu. Inaelezwa kuwa katika tukio hilo, wanafunzi wenye hasira waliamua kuvurumisha mawe shule yao. Sina hakika kama walifanya hivyo kama ishara ya kupinga mgomo wa walimu wao au kuwaunga mkono, lakini kilicho wazi ni kuwa pindi inapofika mahala wanafunzi wa shule ya msingi wanachukua ‘sheria mkononi’ basi ni wazi kuwa Taifa letu limefika mahali pabaya.
Wanafunzi hawa ndio kizazi cha kesho, ndio mawaziri na wabunge wetu, ndio viongozi wa kesho. Sasa inapofika mahala nao wanaingia katika utamaduni mpya wa ‘vurugu kama ufumbuzi wa matatizo’ sijui huko mbele itakuwaje.
Majuzi tu tulishuhudia mgomo wa madaktari ambao bado unaelekea kuwa haujaisha kwa utimilifu (taarifa kwenye mtandao mmoja wa jamii inaeleza kuwa baadhi ya madaktari wameonyesha dhamira ya kutaka kurejea tena kwenye mgomo). Kabla hatujasahau kuhusu mgomo huo tunasikia jinsi baadhi ya wabunge wanavyoshiriki kuihujumu TANESCO.
Wakati huohuo tunashuhudia baadhi ya walimu wakiamua kutimiza azma yao ya siku nyingi ya kugoma. Lakini pengine kubwa na la kutisha zaidi ni taarifa kuwa mmoja wa viongozi maarufu wa dini amekumbwa na kashfa ya shule yake kuiba uniti za umeme wa TANESCO. Haya yote (na mengine ambayo nafasi hairuhusu kuyataja) yanaashiria kuwa hali si shwari huko nyumbani.
Je, viongozi wetu wanafanya nini kukabiliana na hali hii? Usidhani hiki ni kichekesho lakini siku moja kabla sijaandaa makala hii kulikuwa na taarifa kuwa Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai alionekana anaongea na simu wakati kikao cha Bunge kinaendelea.
Labda ilikuwa ni simu muhimu kutoka kwa Spika au pengine Rais, lakini taswira ilivyotokana na tukio hilo inaweza kutanabaisha ni jinsi mtizamo wangu kuwa hali ya mambo si shwari huko nyumbani ilivyotofautina baadhi ya viongozi wetu, ambapo hata kwenye majukumu muhimu ya kuogoza Bunge wanamudu kuongea na selula zao.
Funga kazi ni uamuzi wa Serikali kulifungia jarida la Mwanahalisi kwa muda usiojulikana kwa madai kuwa jarida hilo limekuwa likiandika habari za uchochezi.
Katika toleo lililopita jarida hilo kulikuwa na habari kuhusu suala la Dk. Steven Ulimboka na mtumishi wa taasisi nyeti ya serikali alihusishwa nayo. Je, serikali haidhani kuwa uamuzi wake kulifungia jarida hilo unaweza kutafsiriwa kama unalenga kulizuia kuibua ‘makubwa zaidi’ kuhusu sakata hiyo?
Hivi isingewezekana kulifikisha jarida hilo mahakamani ili haki si tu itendeke bali ionekane imetendeka? Na je, uamuzi wa kulifungia unasaidiaje kuzifanya habari zilizoandikwa nalo zionekane ni uchochezi tu.
Nimalizie kwa kutoa rai ya haja ya mjadala wa kitaifa kuhusu hatma ya Taifa letu. Tunakoelekea si kizuri. Na hili la mjadala si kuhusu tabaka tawala (walio katika bunge, serikali, nk) bali pia kuna haja ya mjadala wa kitaifa kuhusu nafasi ya tabaka la kati katika kuhamasisha, kutetea na hata kupigania maslahi ya tabaka la chini la walalahoi linaloelekea kuachwa bila mtetezi wala msomaji.
Tanzania ni yetu sote. Tuweke kando siasa za mahaba, tuepuke kutanguliza maslahi binafsi badala ya maslahi ya Taifa, tutatue tofauti zetu (migomo, nk) kwa njia za kidiplomasia, na kubwa zaidi tuungane kwa pamoja kuhangaikia kuipeleka nchi yetu katika mwelekeo sahihi.
Inawezekana, timiza wajibu wako.


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.