12 Aug 2013


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Picha kwa hisani ya MILLARD AYO






Sijui ilikuwaje, jana nimeshinda Twitter takriban kutwa nzima pasi kutambua kuwa mmoja wa wanaharakati wa haki za jamii, msanii wa Bongoflava, BABU SIKARE a.k.a ALBINO FLANI, yu mgonjwa. Katika maelezo ya picha aliyoweka katika mtandao wa kijamii wa Instagram, msanii huyo ameeleza kuwa anasumbuliwa na kansa ya ngozi, na sasa anapata matibabu.

Katika maelezo hayo, anaeleza (namnukuu), "kWAHIYO, NIMEGUNDULIWA NINA KANSA YA NGOZI. KWA MWEZI SASA NIMEKUWA NIKIFANYIWA OPERESHENI NA MATIBABU MAKUBWA YA KANSA YA NGOZI. SI MUHIMU KUELEZEA MAUMIVU YALIVYO LAKINI NI MUHIMU KUJADILI JINSI MAALBINO WASIOJIWEZA WATAKAVYOWEZA KUPAMBANA NA KANSA PASIPO MATIBABU NCHINI TANZANIA.

Pole sana, mpambanaji. Natambua pole pekee haitoshi, na ndio maana ninatoa wito kwako msomaji wa blogu hii kuungana nami kumwombea ndugu yetu huyo apate uponyaji, si kwa ajili yake tu bali pia kwa jamii nzima ya maalbino ambayo amekuwa mstari wa mbele kuipigania.

Nimefahamiana na ALBINO FULANI huko Twitter, katika mijadala mbalimbali ya mustakabali wa taifa letu. Ni msanii mwenye upeo na uelewa wa hali ya juu. Na katika majadiliano yetu, amejitanabaisha waziwazi kuwa ni mtu mwenye kuguswa sana na haki za jamii (social justice). Na ndio maana namwita MPAMBANAJI.

Basi pamoja na sala zangu kwa Mungu, naamini mpambanaji utashinda mtihani huu wa maisha. Naamini pia maradhi yako yataifungua macho jamii kuhusu wajibu wetu kuwasaidia wenzetu wenye ulemavu wa ngozi (albinism), sambamba na kupigani haki zao, hususan za matibabu stahili.

MUNGU AKULINDE NA KUKUBARIKI. 


11 Aug 2013


Wasanii wawili wakongwe wa Bongoflava, Mwana FA na AY wapo nchini Afrika Kusini kurekodi video kwa ajili ya wimbo wao mpya wa Cheza Bila Kukunja Goti waliomshirikisha msanii mahiri kutoka Nigeria J. Martins.

Kwa mujibu wa taarifa nilizopewa na Mwana FA mwenyewe, wasanii hao pia jana walifanya 'shoo ya kufa mtu' jijini Pretoria.

Kaa mkao wa kula kusubiri video ya kiwango cha kimataifa kutoka kwa wasanii hao bora kabisa nchini Tanzania.

Sikiliza wimbo huo hapa chini



Victims Kirstie Trup and Katie Gee

Gazeti la kila siku la Telegraph la hapa Uingereza linaripoti kuwa baadhi ya viongozi wa dini ya Kiislam visiwani Zanzibar wanaamini kuwa shambulio la tindikali dhidi ya mabinti wawili wa Kiingereza, Kirstie Trup na Katie Gee lilifanywa na wafuasi wa kikundi cha UAMSHO, ambacho kinataka Zanzibar ijitenge na Tanzania Bara na kisha kuanzisha sheria kali za Kiislam.

Huko nyuma kumeshatokea mashambulizi dhidi ya viongozi wa dini ya Kiislam na Kikristo, ikiwa ni pamoja na mashambulio ya tindikali na mauaji.

"Ofkoz, itakuwa kazi ya Uamsho," alinukuliwa Sheikh Fadhil Soraga, aliyeshambuliwa kwa tindikali Novemba mwaka jana, na anaamini wahusika katika tukio hilo dhidi yake walikuwa UAMSHO.

Wiki mbili zilizopita, vipeperushi vya vyenye wito mkali wa uchochezi dhidi ya Wakristo vilisambazwa sehemu mbalimbali huo Zanzibar, tukio linalohusishwa na harakati za UAMSHO.

"Siku 10 tu zilizopita, walikuwa wanasema wanaandaa kitu kikubwa. Tukio hili, ambalo Waislamu wote twapaswa kulilaani, ni kazi ya kundi hilo (UAMSHO)," alisisitiza Sheikh Soraga.

Paroko wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, Zainzibar, Padri Cosmas Shayo naye alikuwa na mtizamo kama huo wa Sheikh Soraga. Mtangulizi wa Padri huyo, Padre Evaristus Mushi, aliuawa kwa kupigwa risasi mwezi Februari, na hisia zimekuwa kwamba UAMSHO walihusika na tukio hilo.

"Hawa watu wamedhamiria kuzusha vurugu  ili kufikia malengo yao," alisema.

"Wanataka kuifanya Zanzibar iwe ya Waislam pekee, na walianza kwa kuwatisha Wakristo na sasa wanataka kuwatisha watalii ambao wanawaona kama Wakristo pia."

Kabla ya shambulio hilo la tindikali, mmoja wa mabinti hao, Katie, alizabwa kibao na mwanamke mmoja mtaani wakati wa mfungo wa  Mwezi wa Ramadhan.

Katie na Kirstie, walikuwa Zanzibar wakifanya kazi kwa kujitolea, baada ya kumaliza masomo yao ya sekondari. Wote wanatoka katika familia zinazojiweza kimaisha. Baba ya Katie ni chartered surveyor,moja ya ajira inayolipa vizuri hapa Uingereza, huku Kirstie alisoma sekondari ambayo ada yake ni pauni 3,375 (zaidi ya Sh milioni 13)  kwa muhula.

Mabinti hao walikuwa Zanzibar kwa mwezi mmoja wakijitolea katika shule ya chekechea ya Mtakatifu Monica, iliyopo Stone Town, kupitia shirika la kujitolea la Art in Tanzania.

Siku moja kabla ya shambulio hilo la tindikali, ali-tweet kwa furaha baada ya kukutana na Rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton, alipozuru Zanzibar hivi karibuni kuhamasisha vita dhidi ya malaria kupitia Clinton Health Access Initiative.

Kwa mujibu wa gazeti la Telegraph, mmoja wa masapota wakubwa wa UAMSHO ni Sheikh Ponda Issa Ponda, anayedaiwa kutumia wiki tatu zilizopita kuhamasisha Waislam Zanzibar 'kuamka kama huko Misri.'

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali Elieza Feleshi alinukuliwa akisema kuwa Serikali itafanya kila jitihadakumkamata Sheikh Ponda.

Wakati huo huo, gazeti la kila Jumapili la Sunday Mirror lina habari ndefu kuhusu Sheikh Ponda, iliyobeba kichwa cha habari: "Shambulio la tindikali Zanzibar: Mhubiri wa chuki Sheikh Ponda Issa Ponda apigwa risasi na polisi, akamatwa"

Gazeti hilo limeeleza kuwa polisi walimpiga Ponda risasi ya machozi begani kabla ya kumkamata, na sasa yupo mahututi hospitalini.

Habari hiyo inaeleza kuwa Ponda alikwenda Zanzibar kuhamasisha maandamano dhidi ya serikali, na kukiunga mkono kikundi cha UAMSHO, kwa malengo ya kutimua wageni Zanzibar na kuanzisha sheria za Kiislam.




.
.

.
.
.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

10 Aug 2013


Horrific: The girls suffered "horrendous" burns

Moja ya magazeti makubwa nchini Israel, Jerusalem Post, limeandika kuwa mabinti wawili wa Kiingereza walioshambuliwa kwa tindikali huko ZANZIBAR walikuwa wanaharakati na wanachama wa Shirikisho la Vijana wa Kiyunani (Federation of Zionist Youth).

Kwa namna flani, ukaribu wao na harakati hizo za Kizayuni unaweza kuwa miongoni mwa sababu zilizopelekea mabinti hao, Kirstie Trup na Katie Gee, kushambuliwa. Hisia iliyopo ni waliofanya shambulio hilo walisukumwa zaidi na 'kuwaadhibu Wayunani na marafiki zao,' kama ambavyo imekuwa ikitokea sehemu mbalimbali duniani. Inafahamika kuwa vikundi vyenye msimamo mkali wa Kiislam kama vile Al-Qaeda vimekuwa na uhasama mkubwa na Wayahudi.
The plane

Wakati huohuo, Shirika la Utangazaji wa Uingereza (BBC) linaripoti kuwa serikali ya Zanzibar imetangaza zawadi ya shilingi milioni 10 kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazopelekea kukamatwa kwa wahusika wa shambulio hilo.

Tukio hilo la kikatili bado linatawala vichwa vya habari kwenye magazeti, TV na radio, hapa Uingereza.

Gazeti la kila siku la Daily Mirror linaelezea jinsi mtalii mmoja kutoka Uingereza,Sam Jones, alivyojitoa mhanga kumwokoa Katie baada ya kumsikia akilia kwa uchungu kutokana na maumivu ya kumwagiwa tindikali.
The two acid attack victims
Sam aliyekuwa visiwani Zanzibar na girlfriend wake, Nadine, alieleza kuwa Katie alikuwa akilia kwa kelele na kuomba amwagiwe maji huku tindikali ikiunguza ngozi yake. Mtalii huyo alifanikiwa kupata maji na kummwagia Katie.

Mhanga mwingine wa tukio hilo, Kirstie, alikutwa na wasamaria wema mtaani akilia kwa uchungu baada ya kumwagiwa tindikali, na walimbeba hadi baharini na kumtumbukiza majini kwa ajili ya kudhibiti madhara zaidi ya tindikali.
Hadi sasa polisi wa Zanzibar wameshawahoji watu saba. Pia wametoa amri ya kukamatwa Sheikh Ponda Issa Ponda, ambaye wanadai alihamasisha shambulio hilo.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.