24 Aug 2014

Leaving: Brown is seen walking to his Lamborghini after the drama at 1Oak in Los Angeles
Chris Brown akielekea kwenye Lamborghini lake kuondoka katika klabu ya usiku palipotokea shambulio la risasi
Prodyuza Marion Suge Knight (pichani chini) amejeruhiwa kwa risasi amejeruhiwa kwa risasi katika shambuli lililotokea katika pati iliyokuwa ikiendeshwa na msanii Chris Brown.
Music producer Suge Knight has been injured during a shooting at an awards show party at a Los Angeles nightclub hosted by singer Chris Brown, it has been reported
Mashuhuda wanaeleza kuwa msanii huyo ambaye bado yupo katika msamaha wa uchungu (parole) baada ya kutoka jela hivi karibuni ndiye alikuwa mlengwa wa shambulio hilo, ambapo alikuwa MC wa pati ya utangulizi wa Tuzo za Video za Muziki (MVA) zitakazofanyika leo usiku (kwa saa za Marekani).
OK now: Brown smiled as he left the nightclub where he was reportedly targeted by a gunman
Inadhaniwa kuwa Chris hakuumia katika shambulio hilo, lakini watu wengine watatu, akiwemo Suge Knight, mwanzilishi wa lebo ya muziki ya Death Row Records iliyokuwa ikitumiwa na msanii mwingine maarufu wa nchi hiyo, Marehemu Tupac Shakur, walijeruhiwa na kupelekwa hospitali ya Cedar's Sinai. Inaelezwa kuwa mmoja wa majeruhi hao yupo taabani.
Witnesses: Partygoers talk to emergency personnel after the shooting 
Mwanamitindo na mcheza filamu Tyson Beckford na memba wa kundi la Black Eyees Peas Apple De Ap walikuwa miongoni mwa waliohudhuria pati hiyo, na walieleza kuwa walisikia sauti nne za risasi mida ya saa 7.30 alfajiri ya kuamkia leo.
Treatment: Another victim is fitted with a neck brace following the dramatic shooting
Majeruhi akitibiwa
Suge Knight ambaye kwa sasa anamiliki kampuni ya muziki ya Black Kapital Records alionekana na polisi  nje ya ukumbi baada ya shambulio hilo na akachukuliwa katika gari la kubeba wagonjwa. Inaelezwa kuwa alipigwa risasi mbili, na kujeruhiwa tumboni na mkononi na sasa anafanyiwa upasuaji.
Host: Brown enjoys the party before the alleged shooting took place
Chris Brown 'akijirusha' kabla ya shambulio
Waliofanya shambulio hilo walikamatwa na polisi ambao sasa wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Mastaa wengine waliokuwa kwenye pati hiyo ni pamoja na Justin Beiber na rapa The Game.
Guests: Justin Bieber (right) was among the guests at the VMA Pre-Party hosted by  Brown
Justin Beiber alikuwa miongoni mwa waliohudhuria pati hiyo, kama ilivyokuwa kwa rapa The Game (pichani chini)

Jayceon Terrell Taylor, aka The Game attends a VMA Pre-Party hosted by Chris Brown and Pia Mia
Iliposikika milio ya risasi hizo, Chris Brown alionekana akiruka kuelekea kwenye eneo la baa katika klabu hiyo ya usiku (nightclub), huku kwa hasira akiwaagiza watu wengine kujikinga.
Aftermath: Brown jumped on a table after the shooting, apparently furious at what had taken place
Chrsi Brown akiruka kuelekea eneo la baa baada ya milio ya risasi
Saa 12 kasorobo asubuhi ya leo, msanii huyo alitwiti


Akimaanisha 'Jamii haiwezi kustarehe au kuburudika pasipo mikwaruzo.'
Injured: Another victim is transferred into an ambulance in a stretcher
Majeruhi wakiingizwa kwenye gari la kubebea wagonjwa
Angry: Brown at first appeared to still be furious when he made his way from the West Hollywood club
Chris Brown akiwa ametahayari baada ya shambulio hilo



CHANZO : The Mail Online




Smart mannequins that ¿talk¿ to shoppers through their smartphones will go live today in branches of House of Fraser, Hawes & Curtis and the Bentalls department store

Tafsiri: 1. Duka la nguo linaingiza mtandaoni taarifa kuhusu bidhaa husika.

2. Mteja anapaswa ku-download app iitwayo Icneme katika simu yake ili kuwezesha connection ya Bluetooth.

3. Mteja akipita futi 150 karibu ya duka husika, anapata ujumbe katika simu yake, na sasa anaweza kupata taarifa kamili ya nguo husika ilivyovaliwa na mdoli (mannequin) wa maonyesho ya nguo dukani.

4. App iliyomo kwenye simu ya mteja itamwonyesha malili ilipo nguo husika ndani ya duka husika. Pia itampa kiungo (link) ya tovuti ya duka hilo kumwezesha kuinunua nguo hiyo katika muda wowote ule, iwe mchana au usiku.


Kaleem, a keen cricketer, said the teachers at his school have told him other children are 'scared' of his hands

Doctors in India have been left baffled by his growing hands and many are at a loss as to what the condition is

The youngster has difficulty eating, tying his shoelaces and carrying out other basic tasks due to his  hands

Kaleem's father Shamim, 45, (pictured together above) is worried his son will never become independent

Kaleem, from India, was born with hands twice the size of an average baby and they have continued to grow

Mtoto wa miaka minne nchini India, Kaleem (pichani) amewachanganya madaktari kufuatia mikono yake kuvimba kupita kiasi na sasa imefikia uzito wa kilo 12. Mtoto huyo kwa sasa anashindwa kutekeleza japo majukumu madogo tu kama kufunga 'kamba' (laces) za viatu vyake baada ya kuzaliwa akiwa na mikono mikubwa mno.

Kaleem anadai amekuwa akibughudhiwa mno na watoto wenzie wanaomcheka kutokana na maumbile hayo ya ajabu. "Napata mguu kuvaa nguo zangu, kufunga vifungo hata kuvaa nguo ya ndani, anasema mtoto huyo ambaye mama yake alibaini maradhi yake tangu akiwa mdogo lakini hakuwa na cha kufanya kutokana na kutokuwa na uwezo wa kifedha. Wazazi wa Kaleem wana kipato kisichozidi Paundi za Kiingereza 15 (takriban Tsh 42,000) kwa mwezi.

Baba yake, Shamim, anahofu mwanae hatoweza kujitegemea maishani, na anajilaumu kwa kushindwa kumhudumia kutokana na uwezo duni wa kifedha. Dr Ratani, mkurugenzi wa kituo cha afya kilichomfanyia uchunguzi mtoto huyo anakiri kuwa maradhi hayo ni ya ajabu na magumu kutibika. 

CHANZO: The Mail Online



 Only men who suffered impotence as a side effect of illness or those evaluated by a specialist could be given the pills on the NHS
Mamia kwa maelfu ya wanaume hapa Uingereza wanatarajiwa kunufaika na uamuzi wa Taasisi ya Huduma za Afya (NHS) kulegeza masharti ya upatikanaji wa vidonge vya kuboresha nguvu za kiume, Viagra.

Hadi mwezi huu, watu pekee walioruhusiwa kupewa Viagra hospitalini ni wale ambao pungufu wa nguvu zao za kiume ulitokana na athari za matibabu ya maradhi mengine (side effects).

Lakini tangu taratibu za usajili na upatikanaji (patent) ya Viagra ilipoisha muda wake mwaka jana, bei ya vidonge hivyo imeshuka kwa asilimia 93 kwa vile makampuni mengine ya madawa yameruhusiwa kutengeneza aina zisizo asili (generic) za vidonge hivyo.

Kutokana na hali hiyo, NHS imeeleza kuwa watu wote wenye matatizo ya nguvu za kiume wanaruhusiwa kupata Viagra. Madaktari wengi wamefurahishwa na uamuzi huo wakiamini kuwa utasaidia kuboresha mahusiano ya kinyumba na hata kuokoa ndoa.

Hadi 'patent' ya Viagra inakwisha muda wake, Viagra ilikuwa ikiuzwa kwa Paundi za Kiingereza 21.27 (Tsh 58,567.39) kwa pakti ya vidonge vinne lakini bei hiyo sasa imeshuka hadi Paundi .1.45 (Tsh 3,992.61)kwa pakti moja ya vidonge vinne.



22 Aug 2014

Ijumaa ya leo imekuwa siku ngumu sana kwangu. Rafiki yangu mmoja wa karibu, mhamiaji kutoka Ireland ya Kaskazini aliyehamia hapa Uskochi, anajiandaa kwa ajili ya upasuaji wa moyo hapo Jumatatu. Leo tumeonana 'kwa mara ya mwisho' kwa vile atatumia wikiendi hii kujaindaa na upasuaji huo, na wiki Ijayo ndo shughuli yenyewe.

Nimepata wakati mgumu sana kuagana nae jioni hii wakati anaelekea nyumbani kwake nami narudi kwangu. Japo aliniaga kwa kujiamini kuwa tutaonana Jummatano ijayo, lakini hali ya uoga iligubika ujasiri wake, na kwa hakika almanusra niangushe chozi. 

Huyu bwana alipatwa na mshtuko wa moyo miezi kadhaa iliyopita. Naikumbuka vema siku hiyo. Tulipokutana asubuhi baada ya kuwasili kazini alionekana anatoka jasho japo siku hiyo ilikuwa ya baridi kali. Muda mfupi baadae alionekana anapumua kama mtu aliyekimbia umbali mrefu, na muda mfupi baadaye akaanguka na kupoteza fahamu. Tuliita gari ya kuhumia wagonjwa, na akakimbizwa hospitalini haraka. Kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe, alikuwa kama amekufa kwa masaa kadhaa. Lakini kubwa lililosaidia kuokoa uhai wake ni huduma ya kwanza tuliyompatia wakati tunasubiri gari la wagonjwa, vinginevyo moyo wake ungezimika moja kwa moja.

Alikaa hospitalini kwa wiki kadhaa na huko walimwekea mashine inayousaidia moyo wake kufanya kazi zake kwa ufanisi. 

Sasa upasuaji atakaofanyiwa Jumatatu ijayo ni kwa ajili ya uchunguzi mkubwa wa jinsi mashine hiyo inavyofanya kazi.Ikumbukwe kuwa mashine hiyo inafanya kazi kuusaidia moyo, na kwahiyo moyo wake bado unafanya kazi japo ni kwa msaada wa mashine hiyo iliyowekwa juu kidogo ya moyo wake, kifuani.

Kitakachofanyika Jumatatu ni kilekile walichomfanyia wakati wanaweka mashine hiyo, yaani watatumia kompyuta kufanya kazi ya moyo, na kisha kuusimamisha moyo, na kwa wakati huo uhai wake utakuwa unategemea kompyuta hiyo. Wataitoa mashine waliomwekea mwilini na kuisafisha, sambamba na kuichunguza. Kadhalika, moyo wake nao utafanyiwa uchunguzi wa kina. Yote hayo yatatokea wakati uhai wake unategemea kompyuta inayofanya kazi ya moyo.

Japo upasuaji huo haumaanishi kifo lakini kuna uwezekano-japo si mkubwa- wa moyo kurejeshwa mwilini na ukagoma kufanya kazi kama awali. Kadhalika, ile mashine inayousaidia moyo nayo inaweza kugoma 'kuwajibika ipasavyo.' Lakini cha kutisha ni ukweli kwamba wakati upasuaji huo unafanyika, rafiki yangu huyo atakuwa kama amekufa- kwa maana ya kazi zinazofanywa na moyo wa asili kutegemea msaada wa kitu cha nje- in this case ni hiyo kompyuta. Yaani kwa lugha nyingine ni kama mtu anayepumulia mashine, ikizimwa, yaweza kuwa ndio mwisho wa uhai wake.

Wakati tunaondoka eneo la kazi, rafiki yangu huyo alisema waziwazi kuwa muda huo ndo unaweza kuwa wa mwisho kwa yeye kuwepo hapo. Japo aliongea kwa utani lakini uwezekano huo upo japo si mkubwa. Teknolojia ya matibabu ya moyo imepiga hatua kubwa sana lakini si ya uhakika wa asilimia 100.

Kwangu, nabaki kumfanyia sala, upasuaji huo ufanyie salama, na tukutane tena Jumatano kama alivyoahidi mwenyewe. Nina imani na teknolojia ya matibabu ya hawa wenzetu lakini ukweli kwamba kiungo muhimu kama moyo kitasimamishwa na kazi yake kufanywa na kompyuta inanipa msisimko wa uoga. Na hilo limeonekana hata kwa 'mgonjwa' mweyewe.'

I thought si vibaya ku-share stori hii ya kuogofya ambayo inanigusa kwa kiasi kikubwa. Kwa nman flani yanikumbusha jinsi nilivyompoteza mama yangu mpendwa, ambaye nae kama ilivyo huyo rafiki yangu alipatwa na mshtuko wa moyo, akapoteza fahamu, na fahamu hazikumrejea tena hadi anafariki Mei 29, 2008.

Natumaini msomaji mpendwa utaungana nami kumwombea rafiki yangu huyo upasuaji atakaofanyiwa uwe wa mafanikio na aendelee kuishi salama. Nitawafahamisha kilichojiri Jumatano ijayo.

Asanteni

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.