Fanya kusapoti kazi hii ya sanaa yenye ujumbe muhimu kwa mustakabali wa taifa letu kwa kununua wimbo huu kwa bei nafuu katika tovuti ya MDUNDO http://mdundo.com/a/2788
20 May 2015
17 May 2015
8 May 2015

Jana Uingereza ilipiga kura katika Uchaguzi wake Mkuu, na matokeo yalianza kupatikana jana usiku muda sio mrefu baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa majira ya saa nne usiku.
Hadi muda huu, chama cha Conservatives kinazidi kufanya vizuri, na hadi muda huu ninapoandika makala yhii, wameshajikusanyia viti 250, chama cha Labour kina viti 212 na Liberal Democrats viti 6. Chama cha kibaguzi cha UKIP kimepata kiti kimoja tu hadi muda huu, na ubashiri unaonyesha kitapata viti viwili tu, huku kiongozi wake Nigel Farage akiwa katika hatihati ya kushindwa.
CChama tawala hapa Uskochi, Scottish National Party (SNP) kimepata mafaniuko makubwa mno, ambapo katika viti 59 kimeshapata viti 55 na kimepoteza kiti kimoja tu.
Kuna kila dalili kuwa Waziri Mkuu David Cameron ataendelea kuwa Waziri Mkuu lakini ni mapema mno kufahamu iwapo ataunda serikali kwa kushirikiana na chama gani. Kuhusu kiongozi wa Labour, Ed Miliband, tayari kuna tetesi kuwa huenda akalazimika kujiuzulu kabla ya mwisho wa siku hii ya leo baada ya chama chake kufanya vibaya. Kuhusu chama cha Liberal Democrast, huenda kiongozi wake, Naibu Waziri Mkuu, Nick Clegg, nae akalazimika kujiuzulu kufuatia matokeo mabaya mno kwa chama hicho.
Matokeo kamili yatafahamika hapo baadaye.
Kwa coverage ya usiku mzima kuhusu uchaguzi huo, tembelea ukurasa wangu wa Twitter hapa @chahali
7 May 2015

Leo hapa Uingereza tunafanya uchaguzi Mkuu kuchagua chama kitachotuongoza miaka mitano ijayo.Kwa kifupi, tofauti na huko nyumbani, katika uchaguzi mkuu huu wa leo tunawapigia kura wabunge.Hapa hatuna Rais, Mkuu wa nchi ni Malkia japo mkuu wa serikali ni Waziri Mkuu anayetokana na chama kitakachoshinda viti vingi vya ubunge.
Hata hivyo, mchuano ni mkali sana na hadi muda huu ni dhahiri kuwa hakuna chama kitakachopata viti vya kutosha kuunda serikali peke yake bila kushirikiana na chama kingine. Sasa iwapo hali itakuwa hivyo katika matokeo - ni vigumu kubashiri kwa uhakika kuwa hakuna uwezekano wa chama kimoja kuibuka na ushindi wa kukitosheleza kuunda serikali peke yake, kwa sababu lolote laweza kutokea katika masaa machache yajayo kabla ya kuanza kwa uchaguzi na likabadili mwelekeo.
Serikali inayomaliza muda wake inaundwa na chama cha Conservatives ambacho ndicho cha Waziri Mkuu wa sasa David Cameron, kwa kushirikiana na chama cha Liberal Democrats ambacho ndio cha Naibu Waziri Mkuu Nick Clegg.
Ili chama kiweze kuunda serikali peke yake bila kuhitaji ushirikiano na chama kingine, kinahitajika kushinda viti 326.Iwapo hakuna chama kitachofikia idadi hiyo ya vitu, kunapatikana kitu kinachoitwa 'hung parliament' kama ilivyotokea katika uchaguzi mkuu uliopita (mwaka 2010) ambapo Conservatives walipata viti 307,Labour 258 na Liberal Democrats 57, na kwa vile hakuna aliyefikia idadi ya viti 326, Conservative na Liberal Democrats wakakubaliana kuunda serikali ya ushirikiano.
Nimeandika swali hapo juu, nani kuibuka mshindi? Well, njia kuu inayotumika katika chaguzi kubashiri ushindi wa chama kama uchaguzi ni kura za maoni (opinion polls).Kwahiyo, ili kupata mwangaza wa nani anaweza kupata nini, hapa chini ninaorodhesha matokeo ya kura za maoni kutoka makampuni mbalimbali yanayojihusisha na shughuli hiyo:










Utabiri wa matokeo na uwezekano wa ushirikiano wa vyma kuunda serikali ya pamoja



Subscribe to:
Posts (Atom)