20 Oct 2014

Wakati Mbunge wa jimbo la Kawe, Dar es Salaam (Chadema), Halima Mdee akiahidi kuvalia njuga utata unaogubika mradi wa uwekezaji wa treni za kisasa jijini Dar, utata zaidi umeibuka kufuatia uchunguzi uliofanywa na mtaalam mmoja kutoka hapa Uingereza anayeishi nchini Tanzania (siwezi kutaja jina lake kwa vile sijapata idhini yake). 

Hapa chini ni tafsiri ya sehemu ya maelezo/ushauri alionipatia kwa barua-pepe:

Ni vigumu kujua wapi pa kuanzia kuhusu Shumake kwani anaonyesha kuwa ni mtu mwenye utata. Nyenzo zake za kibiashara zipo tupu na majibu yake kwa maswali uliyomtumia hayaridhishi.Pia ameonyesha dalili za jeuri pale aliposema  'do your research (fanya utafiti).

Unaweza kumkamata katika udanganyifu wake. Anadai kuwa kitabu chake cha 'Climbing Your Inner Mountain' ni 'number one seller' (kinaongoza kwa mauzo). Katika Amazon Kindle edition kinashika nafasi ya 472,476 kwa mauzo. Kwenye orodha ya vitabu vyenye 'jalada' (paperback), kitabu hicho kinashika nafasi ya 3,374, 824.

Hivi kweli (kiwa takwimu hizo) kitabu hicho kinaweza kweli kuitwa 'Number One Bestseller'? Huyu mtu si wa kuaminika, kinyume kabisa na anavyodai.

Kuhusu Shumoja na Shumake Global Partners: Kati ya maelezo yake aliyokutumia kwa email na tovuti yake, ni utata mtupu. Anasema Shumake Global Partners ni 'kampuni ya kibenki ya uwekezaji' (investment banking firm). Nneo 'banking' lipo bayana. Je kuna mahala popote Shumake Global Partners imeandikishwa kama benki? Nina hofu kuhusu hilo, lakini ni yeye pekee anayeweza kujibu. Je anaweza kutaja miradi yoyote ambayo imegharamiwa na Shumake Global Partners?

Kuhusu Shumoja Rails, lini ilianzishwa? Je yupo tayari kuwataja wawekezaji katika kampuni hiyo japo kama ni kampuni binafsi anaweza kupata sababu ya kutfanya hivyo)? Lini Shumoja Industries LLC ilianzishwa? Kuna uhusiano gani kati ya Shumoja Rails na Shumoja Industries LLC?

Je mtaji wa uwekezaji unatoka wapi (tukiamini kuwa kweli anao)? Je katika hilo, kuna fedha zozote zinazotoka kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo amehusishwa nayo huko nyuma kama ilivyo kwenye taarifa hii ya Bloomberg?




0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.