Showing posts with label Shumake Rails. Show all posts
Showing posts with label Shumake Rails. Show all posts

20 Oct 2014

Wakati Mbunge wa jimbo la Kawe, Dar es Salaam (Chadema), Halima Mdee akiahidi kuvalia njuga utata unaogubika mradi wa uwekezaji wa treni za kisasa jijini Dar, utata zaidi umeibuka kufuatia uchunguzi uliofanywa na mtaalam mmoja kutoka hapa Uingereza anayeishi nchini Tanzania (siwezi kutaja jina lake kwa vile sijapata idhini yake). 

Hapa chini ni tafsiri ya sehemu ya maelezo/ushauri alionipatia kwa barua-pepe:

Ni vigumu kujua wapi pa kuanzia kuhusu Shumake kwani anaonyesha kuwa ni mtu mwenye utata. Nyenzo zake za kibiashara zipo tupu na majibu yake kwa maswali uliyomtumia hayaridhishi.Pia ameonyesha dalili za jeuri pale aliposema  'do your research (fanya utafiti).

Unaweza kumkamata katika udanganyifu wake. Anadai kuwa kitabu chake cha 'Climbing Your Inner Mountain' ni 'number one seller' (kinaongoza kwa mauzo). Katika Amazon Kindle edition kinashika nafasi ya 472,476 kwa mauzo. Kwenye orodha ya vitabu vyenye 'jalada' (paperback), kitabu hicho kinashika nafasi ya 3,374, 824.

Hivi kweli (kiwa takwimu hizo) kitabu hicho kinaweza kweli kuitwa 'Number One Bestseller'? Huyu mtu si wa kuaminika, kinyume kabisa na anavyodai.

Kuhusu Shumoja na Shumake Global Partners: Kati ya maelezo yake aliyokutumia kwa email na tovuti yake, ni utata mtupu. Anasema Shumake Global Partners ni 'kampuni ya kibenki ya uwekezaji' (investment banking firm). Nneo 'banking' lipo bayana. Je kuna mahala popote Shumake Global Partners imeandikishwa kama benki? Nina hofu kuhusu hilo, lakini ni yeye pekee anayeweza kujibu. Je anaweza kutaja miradi yoyote ambayo imegharamiwa na Shumake Global Partners?

Kuhusu Shumoja Rails, lini ilianzishwa? Je yupo tayari kuwataja wawekezaji katika kampuni hiyo japo kama ni kampuni binafsi anaweza kupata sababu ya kutfanya hivyo)? Lini Shumoja Industries LLC ilianzishwa? Kuna uhusiano gani kati ya Shumoja Rails na Shumoja Industries LLC?

Je mtaji wa uwekezaji unatoka wapi (tukiamini kuwa kweli anao)? Je katika hilo, kuna fedha zozote zinazotoka kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo amehusishwa nayo huko nyuma kama ilivyo kwenye taarifa hii ya Bloomberg?




14 Oct 2014

These were the questions I put forward to Mr Robert Shumake (haya ndiyo maswali niliyomuuliza Robert Shumake)
And below are series of Shumake's responses, click photo to enlarge (na chini ni mlolongo wa majibu ya Shumake, bonyeza picha kuikuza)






My final request to Shumake was advising he publishes the provisionary Memorandum of Understanding between his company M/S Shumoja a.k.a Shumake Rails (he has so far failed to concisely clarify on this) and the Government of Tanzania. While he is yet to respond, I will continue with my investigation, and will definitely keep you posted. As for now, I leave to you wananchi to pass a verdict whether this guy a genuine investor or not? (Ombi langu la mwisho kwa Shumake ni kumshauri aweke wazi kataba wa awali kati ya kampuni yake ya M/S Shumoja au Shumake Rails (kwa ujumla ameshindwa kufafanua kuhusu hili) na serikali ya Tanzania. Wakati bado hajanijibu kuhusu ombi hilo, mie ninaendelea na uchunguzi wangu na nitawajuza maendeleo yake.Kwa sasa nawaachia ninyi wananchi kutoa hukumu iwapo mtu huyu ni mwekezaji kweli au la)





8 Oct 2014

Jana usiku, mwekezaji wa mradi wa treni za kisasa Dar, Bwana Robert Shumake, aliomba kutumiwa maswali kuhusiana na mradi huo. Kufuatia baadhi ya mapendekezo ya wanaharakati wanaofuatilia suala hilo, niliamua kumtumia Bwana Shumake maswali yafuatayo kama inavyoonekana kwenye nyaraka hapo chini.

Iwapo utakuwa na maswali zaidi basi tuwasiliane ili niyaongeze kama nyongeza ya hayo niliyokwishamtumia.

Tusubiri matokeo



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.