6 Apr 2009

MIMI SI MWANASIASA JAPO MALENGO YANGU YA BAADAYE NI KUWA MCHAMBUZI WA SIASA (POLITICAL ANALYST).BINAFSI SIICHUKII CCM ILA NAKERWA NA BAADHI YA KASUMBA ZILIZOOTA MIZIZI NDANI YA CHAMA HICHO KIKONGWE.NA KASUMBA KUU INAYONITATIZA KUHUSIANA NA CHAMA HICHO NI UNAFIKI.

JUZI JUZI TUMESIKIA KAULI ZA MMOJA WA WAKONGWE WA CCM,MZEE JOHN MALECELA,AMBAPO PAMOJA NA MAMBO MENGINE ALIAMUA "KUSIGINA DEMOKRASIA" KWA KUWATAKA BAADHI YA VIONGOZI WA CHAMA HICHO WANAOLUMBANA WAKOME MARA MOJA.>
SWALI LA MSINGI HAPA NI JE KWA KUKOMESHA MALUMBANO HAYO NDIO UFUMBUZI WA "KINACHOLUMBANIWA" UTAKUWA UMEPATIKANA?BUSARA NDOGO TU INAWEZA KUTUELEZA KWAMBA MTOTO ANAPOLIA INAWEZA KUASHIRIA KUWA ANA TATIZO (NJAA,KIU,ANAUMWA,NK).KUMFINYA MTOTO HUYO ANYAMAZE BADALA YA KUCHUNGUZA KINACHOMLIZA HAIWEZI KUWA SOLUTION YA TATIZO.

HUHITAJI KUWA MCHAMBUZI WA SIASA KUBAINI KUWA MALUMBANO YANAOENDELEA NDANI YA CCM NI MKINZANO WA WATETEZI WA UFISADI vs WAPINZANI WA UFISADI,WABINAFSI vs WANAOJUA JUKUMU LAO KWA TANZANIA,WANAFIKI vs WASEMA KWELI,NA MAKUNDI KAMA HAYO.KITU PEKEE KINACHOWEZA KUYAPATANISHA MAKUNDI HAYO NI KWA CCM KUWA WAZI-SI KWA MANENO PEKEE BALI KWA VITENDO-INASIMAMIA UPANDE UPI KATIKA MIKINZANO HIYO.IWAPO CCM IKISEMA INAPINGANA NA UFISADI HALAFU IKACHUKUA HATUA ZINAZOSTAHILI DHIDI YA BAADHI YA VIONGOZI WAKE WANAOTUHUMIWA KWA UFISADINI DHAHIRI BASI MALUMBANO YANAYOENDELEA YATAKOMA.LAKINI TUSITEGEMEE "UKIMYA" KWA HALI ILIVYO SASA AMBAPO,KWA MFANO, MTU KAMA MZEE WA VIJISENTI PAMOJA NA TUHUMA ALIZONAZO ANAENDELEA KUWA MJUMBE WA KAMATI YA MAADILI NDANI YA CHAMA HICHO.

KAULI YA MZEE MALECELA IMEANZA KUPATA SAPOTI KUTOKA KONA MBALIMBALI NDANI YA CHAMA HICHO.JANA,WAKONGWE FLANI WA CCM WAMEITISHA MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI AMBAPO PAMOJA NA MAMBO MENGINE WAMEKEMEA MALUMBANO HUKU WAKIONEKANA KUKEMEA BAADHI YA VIONGOZI WA CCM WALIOSHIKILIA BANGO VITA DHIDI YA UFISADI.KWA BUSARA ZA WAZEE HAWA,WANATAKA SUALA HILO LIACHWE MIKONONI MWA CCM.HIVI LAITI CCM INGEKUWA IMEMUDU KUFANYA HIVYO,AKINA MWAKYEMBE,KILANGO NA SELELII (KWA MFANO) WANGEKUWA WANAPIGA KELELE KUHUSU UFISADI?

WANACHOJARIBU KUFANYA WAZEE HAWA (PAMOJA NA MALECELA) NI KUJIAMINISHA KUWA HAKUNA TATIZO NDANI YA CHAMA HICHO,NA KELELE ZINAZOPIGWA NA BAADHI YA VIONGOZI WAKE NI SAWA TU NA UTOVU WA NIDHAMU.YALEYALE YA KUMFINYA MTOTO ANYAMAZE PASIPO KUFANYA JITIHADA ZA KUJUA KINACHOMLIZA.

KUNA WENZETU AMBAO KWA MTIZAMO WAO UKIZUNGUMZIA MABAYA YA CCM BASI UMETENDA KOSA LA JINAI.TATIZO LA WATU WA AINA HII NI KUPUUZA NAFASI YA CCM KATIKA ULINZI WA AMANI NA HATMA YA TAIFA LETU KWA UJUMLA.DHAMANA YA NCHI IKO MIKONONI MWA CHAMA HICHO KWA VILE NDICHO KILICHO MADARAKANI KWA SASA.SOTE TUNAWEZA KUBASHIRI KILICHO MBELE YETU IWAPO TUKIIRUHUSU CCM IENDESHE MAMBO INAVYOTAKA-HATA KAMA INATUPELEKA PABAYA-NA SIE TUENDELEE KUKAA KIMYA!

ANYWAY,HEBU SOMA BUSARA ZA WAZEE WETU HAWA HAPO CHINI:

Wenyeviti wastaafu wa CCM waonya

Wenyeviti wastaafu wa mikoa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamevunja ukimya na kuwataka viongozi wa chama hicho wanaotaka kuyatumia mapambano dhidi ya rushwa kama mtaji wa kisiasa na kujipatia umaarufu, kuacha mara moja. Sambamba na hilo, wazee hao wametaka mapambano dhidi ya rushwa yasiwe kichaka cha kuficha ubovu wa uongozi na kushindwa kuwajibika. Akizungumza kwa niaba ya wenyeviti wastaafu wa chama hicho Dar es Salaam jana, Mwenyekiti mstaafu wa Mkoa wa Dodoma, Pancras Ndejembi alisema mapambano dhidi ya rushwa ni ya CCM na si mwanachama binafsi au kikundi cha wanachama wachache.

“Tunashuhudia baadhi ya viongozi wa CCM kurushiana maneno wenyewe kwa wenyewe kwa kutaka kuonyeshana nani zaidi na nani ni vinara kuliko wengine katika mapambano dhidi ya rushwa, hii si sawa,” alisema Ndejembi aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Tanzania. “Tusingependa kuona mapambano haya yanatumiwa kama njia ya kujipatia umaarufu binafsi, mwenyekiti wetu Rais Kikwete ambaye ndiye jemedari wa mapambano haya humsikii anafanya hivyo na sisi wengine tusifanye hivyo…. kama wewe ni kiongozi na hutekelezi wajibu wako kwa wapiga kura wako wakikuuliza uko wapi, usisingizie kupigwa vita na mafisadi,” walionya.

Ndejembi aliyeambatana na wenyeviti wastaafu Hemed Mkali (Dar es Salaam), Tasil Mgoda (Iringa) na Jumanne Mangara (Pwani), alisema wazee hao wamesikitishwa na malumbano ya hadharani baina ya viongozi wa CCM ambao wengine wa ngazi ya juu ya uongozi ndani ya chama. Alisema tabia inayoonyeshwa na viongozi hao ya kushutumiana, kunyoosheana vidole, kuwekeana visasi, kuonyeshana ubabe na kuwekeana nadhiri ya kupambana baina ya viongozi, kunadhoofisha na kukipunguzia heshima chama hicho.

“Lakini pia kufanya hivyo hadharani, kwa nia ya kutaka kuungwa mkono katika shutuma na visasi hivyo kunajenga chuki, uhasama na migawanyiko katika jamii, viongozi hatupaswi kuwajaza watu chuki na uhasama ndani ya mioyo yao,” alisema Ndejembi kwa niaba ya wenzake na kutaka neno ufisadi lisitumiwe kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwakani. Alisema kumuita mtu fisadi kwenye vyombo vya habari haitoshi katika kushinda mapambano dhidi ya rushwa, bali watu waipigie kelele serikali iimarishe taasisi na vyombo vya kupambana na rushwa kama Polisi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Mahakama ambako watuhumiwa wanafikishwa.

Licha ya kuwapo malumbano baina ya viongozi hao wa CCM, wastaafu hao walisema kuhitilafiana ni kitu cha kawaida na kamwe watu wasitarajie chama hicho kitameguka. Wastaafu hao walieleza kumuunga mkono Rais Jakaya Kikwete iwapo atagombea tena urais mwakani na kutaka watu wengine wamuunge mkono, kwa maelezo kuwa anafaa kuongoza nchi. Walitoa sababu za kumuunga mkono kuwa ni kukubalika na anaowaongoza, anawapenda watu wote, mvumilivu, mkereketwa wa maendeleo ya wananchi na hana jazba.

Wazee hao walisema wameamua kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo hayo ili ujumbe uwafikie viongozi, wanachama na mashabiki wa CCM, lakini yote hayo waliyoyaeleza wameshayawasilisha kwenye vikao wanavyoshiriki vya matawi na mashina na wamezungumza na viongozi wa sasa wa chamahicho. Ingawa wastaafu hao hawakuwataja kwa majina viongozi wa CCM waliolumbana hadharani, lakini hivi karibuni Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe ambaye ni mwanahisa wa Kampuni ya kuzalisha umeme wa upepo ya East Africa Power Pool, amelumbana na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.

Dk. Mwakyembe anadai Rostam anatumia vyombo vyake vya habari kumchafua huku Rostam akitaka mbunge huyo ambaye kitaaluma ni mwanasheria na mwandishi wa habari, kuelezea mgongano wa maslahi wakati alipochaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini. Mbali na wazee hao, pia Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM Tanzania Bara ambaye ni Mbunge wa Mtera, John Malecela alitaka malumbano hayo yakome, kwani hayana faida kwa mwananchi na wahusika watumie vyombo husika vya chama kufikisha malalamiko yao.
CHANZO:
HabariLeo

WITH ALL DUE RESPECT,BAADHI YA HAWA WAZEE NDIO WAMETUFIKISHA HAPA TULIPO KUTOKANA NA ITIKADI HIZIHIZI ZA "KUJENGA UMOJA NA MSHIKAMANO NDANI YA CHAMA" PASIPO KUANGALIA ATHARI ZAKE KWA JAMII KWA UJUMLA (AFTERALL,SIO KILA MTANZANIA NI MWANA-CCM).

HATUJACHELEWA.INAWEZEKANA IWAPO UZALENDO NA MASLAHI YA TAIFA YATAWEKWA MBELE YA (in front of) KUJIPENDEKEZA NA UNAFIKI.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.