29 Apr 2010

British National Party (BNP),chama cha kibaguzi cha hapa Uingereza,kimetangaza kwamba kitatoa paundi 50,000 kwa kila atakayeafiki kuhama Uingereza.Akiongea katika kipindi cha 'Today' cha kituo cha redio cha BBC4,mwenyekiti wa chama hicho,Nick Griffin (pichani) alisema kuwa mpango huo ni mahsusi kwa Waingereza wasio Weupe (non-White British) na wahamiaji wengine wasio weupe (non-White migrants).

Griffin alieleza kuwa kwa mujibu wa sera ya uhamiaji ya chama chake 'milango ya Uingereza itafungwa' kwa wageni isipokuwa tu kwa wale wenye ujuzi au taaluma maalum."Aidha unazungumzia fundi bomba wa ki-Polish au mkimbizi kutoka Afghanistan,milango ya Uingereza itafungwa kwa sababu nchi hii imejaa",aliongeza kiongozi huyo mbaguzi wa rangi.

Kiongozi huyo wa BNP alitanabaisha kuwa "Idadi ya watakaozuiwa kuingia nchi hii itakuwa yoyote na kutoka popote.Milango itafunguliwa tu pale itapokidhi mahitaji wa Waingereza na Uingereza".Akitolea mfano wa utekelezaji wa sera hiyo,Griffin alisema laiti Uingereza ikiwa na mahitaji ya wataalam wa nyukia basi chama hicho kitaruhusu,kwa mfano,mwanafikizia kutoka Japan.

Alipoulizwa kama sera hiyo itaambatana na kuvunja mikataba ya kimataifa,mbaguzi huyo alijibu: "Kabisa.Mikataba ya kimataifa haikidhi mahitaji ya Uingereza na watu wake.U-kimataifa (internationalism) ni miradi ya tabaka la wanasiasa".

Kuhusu kuwataka wasio weupe kuondoka Uingereza,Griffin alisema:"Tunasema tutatoa posho ya kuhama makazi (resettlement grants) na hili ni suala la hiari .Tunazungumzia takriban pauni 50,000 kwa kwa mtu".Alipoulizwa ni watu wangapi wanaotarajiwa kuhama Uingereza kwa mujibu wa sera hiyo alisema: "180,000 kwa mwaka,kama wataondoka katika nchi hii iliyojaa kupindukia".

Imetafsiriwa kutoka Yahoo! News


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.