9 Apr 2010

JK alisaini sheria hiyo kwa mbwembe kama alivyoahidi.Siku chache baadaye,Dkt Wilboard Slaa akaibua hoja kuhusu 'usanii' uliofanyika kuongeza vipengere katika Sheria hiyo.Spika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakatetea 'usanii' huo.Licha ya mlolongo wa matukio hayo kuashiria kuwa sheria hii yenye nia njema itabaki kuwa maandishi tu,walengwa wakuu wa sheria hiyo wameamua kuipuuza na 'misaada' inatolewa kama kawaida katika kujitengenezea mazingira ya ushindi kwenye uchaguzi. Dk. Nkya kujitosa ubunge Morogoro Kusini Mashariki

na Joseph Malembeka, Morogoro

NAIBU Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Lucy Nkya, ametangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Morogoro Kusini Mashariki.
Dk. Nkya alitangaza nia hiyo akiwa katika ziara ya kukagua maenndeleo na utekelezaji wa ahadi alizotoa baada ya kuchanguliwa kuwa mbunge wa Viti Maalum.

“Nawatakeni wanachama wenzangu ndani ya CCM muelewe kuwa na mimi nakuja huku mbali na kuwa kuna wenzangu waliotangaza nia hii,” alisema Dk.Nkya.

Dk. Nkya ambaye kwa nyakati tofauti alikabidhi vitu mbalimbali yakiwemo mabati, vipaza sauti, saruji, vyerehani, misumari, baiskeli na fedha taslimu sh 1,500,000 kwa wananchi na wana CCM katika kata mbalimbali aliwataka wana CCM kukiimarisha chama na wao kiuchumi.

“Sasa hivi tunakwenda kwenye hekaheka za uchaguzi ila nawatakeni mbali na siasa jiimarisheni kiuchumi kwa kulima mazao yanayokomaa kwa muda mfupi na yanayostahimili ukame tuepukane na janga la njaa,” alitahadharisha Dk. Nkya.

Dk. Lucy Nkya anakuwa miongoni mwa watu saba walioonyesha nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo. Wengine ni mbunge wa sasa wa jimbo hilo (Samir Lotto), Jamira Mohamed, Amani Mwenigoha, Gabriel Mkwawe, Semindu Pawa na Salumu Salum Mkangala.

CHANZO: Tanzania Daima.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.