29 Dec 2010



Takriban kila jambo kinaweza kutizamwa kwa sura mbili,au zaidi,hasa kwa minajili ya kuangalia faida na hasara.Ni katika mantiki hiyo,baadhi yetu tunaweza kuthubutu kuangalia "upande wa pili wa shilingi" kuhusu umoja wa Watanzania.Naomba nisisitize kuwa hoja hapa sio kudharau jitihada za waasisi wa taifa letu waliofanya kazi kubwa kujenga mshikamano miongoni mwa makabila zaidi ya 120 na kuzaa Utanzania uliogubika ukabila,udini,nk (angalau kwa kipindi kirefu cha uhai wa Tanzania).

Lakini moja ya athari zinazosababishwa na umoja huo ni uwezekano wa watu wasio na damu ya Kitanzania kujificha kwenye kivuli hicho cha "umoja wetu".Na ukichanganya na udhaifu,let alone ufisadi uliokubuhu,wa Idara ya Uhamiaji,yayumkinika kuamini tuna "Watanzania wenzetu" kadhaa tu ambao kimsingi hawapaswi kuwepo nchini mwetu.Kadhalika,kwa vile teuzi zinazofanywa na Rais Jakaya Kikwete (kama ilivyokuwa enzi za Mwinyi na baadaye Mkapa) hazizingatii kujiridhisha kuhusu u-Tanzania halisi ( as opposed to u-Tanzania wa kufoji), baadhi ya viongozi wanaoteuliwa kushika nyadhifa nyeti wanaweza kabisa kuwa sio Watanzania.

Kuongeza ugumu katika suala hilo la u-Tanzania ni makabila ambayo yametapakaa zaidi ya mipaka ya nchi.Hapa nazungumzia makabila ambayo yapo zaidi ya nchi moja.Kwa mfano,Kenya kuna Wamasai,Wameru,Wajaluo,nk kama ilivyo Tanzania.Simaanishi kila Mtanzania anayetoka katika makabila ya aina hiyo anaweza kuwa na utata katika u-Tanzania wake bali kilicho wazi ni ukweli kwamba ni rahisi kwa asiye Mtanzania (lakini anatoka kabila kama la Kitanzania) kujificha nchini ndani ya kivuli cha umoja wetu.

Tutamtambuaje mtu wa aina hiyo?MATENDO YAKE (including KAULI zake).Na ni katika mstari huo wa fikra nimefika mahali nikalazimika kujiuliza iwapo Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Jaji Werema ni Mtanzania kweli au ni walewale wanaotumia umoja wa Tanzania (licha ya wingi wa makabila)+udhaifu na ufisadi Idara ya Uhamiaji,kuwepo Tanzania isivyo halali,na kupewa madaraka makubwa pasipo watoa madaraka hayo kujiridhisha kuhusu u-Tanzania wa mteuliwa.

Simtuhumu Werema kuwa si Mtanzania kwani sina nyaraka za kuthibitisha hilo.Hata hivyo,nalazimika kupata hisia za walakini katika u-Tanzania wake kutokana na mlolongo wa kauli zake za kihuni na zisizoendana na wadhifa mkubwa aliokabidhiwa.Wakati takriban kila Mtanzania halisi anazungumzia umuhimu wa Katiba mpya,mbabaishaji Werema akakurupuka na kudai hakuna haja ya Katiba mpya (kana kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyesema atashughulikia suala hilo ni mdogo kimadaraka kwa Werema).

Mpuuzi huyu ambaye ni dhahiri kuteuliwa kwake tena kuwa Mwanasheria Mkuu kunathibitisha matatizo makubwa ya kimaamuzi yanayomwathiri Rais Kikwete alifikia hatua ya kusifia rushwa ndani ya CCM kuwa ni sehemu ya demokrasia (rejea gazeti la Uhuru,Agosti 6,2010 habari yenye kichwa AG Asifu Demokrasia CCM).Yani kichwa maji huyu mwenye jukumu la usimamizi wa sheria ikiwa ni pamoja na kupambana na rushwa alijifanya kupofu kwenye rushwa za wazi zilizotawala mchakato wa CCM kupata wagombea wake katika uchaguzi mkuu uliopita.Basi bora angekaa kimya,lakini mropokaji huyu akaona ni vme atuthibitishie how good msema ovyo he is.

Tunakumbuka pia ubabaishaji wake kuhusu muswada wa kizushi wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi.Ofisi ya mbabaishaji huyu pasipo aibu iliwasilisha madudu huko Bungeni ambapo haikuchukua muda kwa watu makini kama Dr Wilbroad Slaa kubaini uhuni uliofanyika.Na kwa vile ni rahisi zaidi kwa Kikwete kufanya teuzi kuliko kutimua wababaishaji,Werema hakuguswa.In fact,amezawadiwa tena Uanasheria Mkuu.

Ilikuwa rahisi kwa Werema kupandwa na muku katika kipindi cha kampeni za uchaguzi na kutishia kuishtaki Chadema kwa sababu anazojua yeye lakini sasa badala ya kuungana na Watanzania halisi kuonyesha hasira zao kuhusu hukumu ya Dowans ambapo serikali inatakiwa kuwalipa matapeli hao shilingi BILIONI MIA MOJA THEMANINI NA TANO (Tshs185,000,000,000/=)!!!!Badala ya angalau kuonyesha uchungu kwa nchi yetu na kuelezea suala hilo kistaarabu,jitu hili linakurupuka na kudai "..The matter is as good as closed...let's use our resources on important issues..." (mjadala huo umefungwa,tuangalie mambo mengine ya msingi).Yaani kwa mzembe huyu wa kufikiri,malipo ya shilingi bilioni 185 kwa matapeli wa Dowans sio suala muhimu (ambao laiti Werema na ofisi yake wangewajibika ipasavyo mmiliki wa Dowans angekuwa jela muda huu).Je cha muhimu ni kipi Mista Jaji?

Kwanini Watanzania wabebeshwe mzigo uliosababishwa na ufisadi katika serikali ya Kikwete?Yes,Kikwete anahofia kumuudhi swahiba wake anayemiliki Dowans,na ataendelea kuwa mateka wa fisadi huyo mpaka anamaliza urais wake 2015.Ni katika mazingira haya ya kubebana na kulindana ndipo wababaishaji kama Werema wanapata nafasi za kupewa madaraka (kulinda maslahi ya mafisadi) na kwa vile anafahamu fika kuwa Kikwete hana ubavu wa kumtimua (Werema) anaropoka kadri misgipa ya mdomo wake inapowashwa.Huyu mtu ana kauli chafu na zilizojaa ngebe.Si mlevi wa madaraka (kama walivydai Chadema) bali ni teja la madaraka.Uanasheria wake Mkuu haukamiliki pasipo kuwadharau Watanzania wenye nchi yao.Hajioni mheshimiwa mpaka aongee maneno mawili matatu ya "kutunyooshea kidole cha kati" (middle finger in the air)

Ndio maana nimepatwa na wazo la kujiuliza kuhusu iwapo Werema ni Mtanzania kweli au ndio walewale wanaojificha kwenye umoja wetu licha ya wingi wa makabila yetu?Nimeeleza hapo awali kuwa katika mchanganyiko huu wa makabila ni rahisi kwa wasio Watanzania kujichanganya nasi kana kwamba ni wenzetu.Kuwatamvua si rahisi lakini kwa bahati nzuri baadhi ya watu hawa wanaweza kutambulika,sio kwa mwonekano wao,bali KAULI ZAO ZINAZOONYESHA BAYANA HAWANA UCHUNGU WALA UPENDO KWA TANZANIA.

Nimalize kwa kumlaumu tena Rais Kikwete kwa kuzidi kuipeleka Tanzania shimoni.Teuzi zake za rapid fire na zinazoelemea zaidi kwenye kulindana badala ya sifa na/au uzalendo ndio sababu ya kupata watu wa ajabu kama huyu Werema.Najua Chadema wamemtaka kichwa maji huyu ajiuzulu,lakini hiyo ni ndoto mbaya.Werema ajiuzulu achekwe?Na akishajiuzulu nani atasimamia maslahi ya mafisadi hapo kwa Mwanasheria Mkuu?Nani atasimamia malipo kwa mafisadi kama wa Dowans?Nani atahakikisha mikataba ya kiuendawazimu inaendelea kusainiwa na kulindwa kwa nguvu zote?Werema ajiuzulu ili Kikwete aonekane a total fraud katika uongozi na teuzi zake?

3 comments:

  1. Sasa ndiyo mtatufahamu kama sisi ndiyo chama cha Mafisadi(CCM). Kura tumezinunua na pesa zetu lazima zirejeshwe kwa namna yoyote ile....Mpaka hatutaji majina wamiliki wa DOWANS....!!!!!!!!!!!! Kimsingi nazungumzia hii serikali ya kitapeli ya CCM ikiongozwa na Tapeli namba moja JK aliyekosa haya usoni. Tulitegemea kufingiwa kwa blogu ya utamu ingebadlisha kuitendaji na kuwajibika kwa wananchi kwa dhati. Mmefanya juhuudi kuifungia utamu alkini niyi wenyewe mmbaki tabia zilezile....Mzee utamu rudisha ule mtambo wetu wakurekebisha tabia uwajnai tafadhali.

    ReplyDelete
  2. Ninachoshindwa kumuelewa Jaji Werema ni kwamba kama makubaliano ni ya Tanesco na Dowans, Na Tanesco wakili wao walitoka Rex (not sure of sp) yeye anahusikaje huko? Kwanini serikali inaingilia hayo mambo ya payment? Je yeye alihusika toka mwanzo? Tanesco ni mfu already maana ata-umeme wenyewe hauonekani sasa kwanini serikali iisaidie kulipa? Kwanini Tanesco isilipe/filisike yenyewe tu? Kwanini wanamficha mmiliki wa Dowans wanamuita msimamizi? Je kweli hamna hidden ajenda hapa? Inaonyesha kama serikali ni sign za mfa maji haishi kutapa tapa. Jamani nisaidieni kunielewesha kama nakosea.

    ReplyDelete
  3. jamani tunatoa points nyingi na nzuri kuirekebisha hii serikali ya wababaishaji ccm lakini sikio la kufa halisikii dawa. Labda tujaribu kwenye level ya watu binafsi...kuna kababaishaji uchwara kengine ambako hivi karibuni kamekuwa kakitumiwa na ccm na serikali yake kuendesha porojo za kishabiki redioni. si kengine ni haka ka Ephraim Kibonde. na ni kibonde haswaa maana shule hakana eti kanajiita mwanahabari!! Mwanahabari gani huyu? uwezo wa uchambuzi hana(and rightly so), ustaarabu hana, kwenye dini hayumo, kwenye siasa hana guts, amebaki kujikomba tu kwa kupigia debe uoza. kipindi chake cha Jahazi la Clouds FM kama hiki cha jana 5jan 2011 kametumiwa kusafisha akili za watu kwa maji machafu yenye tope.Jana wanathubutu kudai hata Arusha ni shwari hakuna tatizo. Kama hao mafisadi na serikali yao wanakapenda sana wakasomeshe basi kaweze kujua kuchambua mambo na hawawezi hilo maana kakielimika hakatatumika kwa ujinga.hooovyoo! Jahazi mnachefua watu, au mnajikomba mpewe u-DC maana ndio sandakalawe ya CCM kwa wapiga debe. afadhali yake Habash kajiengua kwenda msaidia JD kubeba kipimajoto!!

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.