Showing posts with label DOWANS. Show all posts
Showing posts with label DOWANS. Show all posts

26 Apr 2011


Wakati habari kuhusu chama tawala CCM "kujivua magamba" zinaendelea kukamata nafasi ya juu,ni vema tukakumbushana magamba halisi yanayopaswa sio kuvuliwa tu bali kutekeketezwa kwa moto wa gesi.CCM wanaweza kutuchezea shere kwa usanii wao lakini ukweli unabaki kuwa ni migongano ya kimaslahi miongoni mwao ndio inayopelekea hizi ngonjera za kujivua magamba.Ufisadi katika taasisi za umma na serikalini kwa ujumla ndio magamba halisi yanayopaswa kuchunwa kwa nguvu badala ya kuwaruhusu wenye magamba hayo wajivue kwa hiari.By the way,tangu lini uchafu ukajiondoa wenyewe pasipo kutumika nguvu ya sabuni na mkono aumashine ya kufulia?

Soma habari hii ujionee mwenyewe namna Tanzania yetu inavyozidi kuwa shmba la bibi

Kashfa mpya ya Ufisadi Tanesco
Tuesday, 26 April 2011 10:14

CAG ADAI IMEILIPA DOWANS BILIONI MOJA ISIVYO HALALI
Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limeingia katika kashfa nyingine ya ufisadi baada ya kubainika kuwa limeilipa Kampuni ya kufua umeme ya Dowans dola za Marekani 1.2 milioni ikiwa ni gharama ya kusafirisha mitambo ya kampuni hiyo kuja nchini kwa ndege badala ya dola 120,000.

Matumizi hayo ya ziada yanayokadiriwa kufikia Sh1.4 bilioni za Tanzania yanaelezwa kwamba yaliingizwa katika akaunti ya Dowans kimakosa.

Hata hivyo, mpaka sasa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amesema Tanesco imeshindwa kumpelekea ripoti ya matumizi ya fedha hizo alizoziita kuwa ni ufisadi.

Mbali na hivyo CAG amelitaka shirika hilo limpelekee mchanganuo wa matumizi ya dola za Marekani 4,865,000 sawa na Sh6.8 bilioni.

Jana, alipotakiwa kufafanua kuhusu ripoti hiyo, CAG Ludovic Utoh alisema: “Nashukuru kwa kunipigia, lakini nyie si mnazo ripoti hizo, mnaweza mkasoma na kuendelea kuripoti.”

Kwa mujibu wa gazeti la The East African, toleo la Aprili 25, mwaka huu, ripoti ya CAG iliyoishia Juni 30, 2010 inaonyesha kuwa Tanesco ilifanya malipo hayo kupitia akaunti ya gharama za mikutano.

Taarifa hiyo imeonyesha kuwa Tanesco ilishindwa kutoa maelezo kuhusu malipo hayo kwa ajili ya kukodisha ndege maalumu ya kusafirishia mitambo hiyo. Pia inaonyesha kuwa kiasi cha Sh13,000,000 ziliripotiwa kimakosa kama Sh1,300,000,000 kwenye kifungu cha matumizi ya vikao na pia kiasi cha Sh11.0 bilioni kinachohusu malipo kupitia barua ya mkopo (letter of credit) na kuingizwa katika akaunti ya makusanyo ya shirika kupitia benki ya NBC.
CAG pia alibaini kuingizwa mara mbili kwa Sh101 milioni katika akaunti ya mitambo ya Tanesco kinyume na taratibu.

CAG alisema kuwa ndani ya Tanesco hakufanyiki usuluhishi wa mapato yatokanayo na mauzo katika matawi yake kukiwemo pia jumla ya Sh103,000,000 za masurufu ambazo hazijarejeshwa. Pia umeme unaozalishwa na ule unaouzwa unaonyesha kwamba shirika hilo linapata hasara kutokana na sababu za kiufundi.

Ripoti hiyo inasema, Tanesco ilionyesha hasara za uniti 1,188 KwH’m kutoka katika uniti 4,831 KwH’m inazozalisha ikionyesha kwamba kuna hasara katika mapato. Hasara hizo zinachangiwa na kuwepo kwa wateja wasio waaminifu, bili za uongo na uunganishaji haramu wa umeme.

Imeeleza kwamba hata wateja waliokatiwa umeme, wanaendelea kutumia huduma hiyo kama kawaida licha ya kudaiwa wastani wa dola za Marekani 65,000.CAG, Utouh alikaririwa akisema manunuzi katika shirika la Tanesco yalirekodiwa kimakosa na kwa udanganyifu.

Utouh alisema wakati wa ukaguzi, iligundulika kwamba Tanesco, hawakuwa wakifanya ‘reconciliation’ (upatanisho) ya mwezi kati ya mauzo na mapato.Kwa mujibu wa CAG, kuna hasara katika idara za uzalishaji na usambazaji wa umeme kwenda wateja.

“ Kuna mapendekezo niliyoyatoa yanayotakiwa kuchukuliwa hatua na Serikali, Bunge, Kamati ya Hesabu za Serikali, Bodi ya Wakurugenzi na maofisa watendaji wakuu kupitia ripoti ya fedha iliyoishia Juni 30,2009,” ilisema ripoti hiyo.

Katika ripoti hiyo, CAG alisema katika ripoti ya mwaka uliopita ya ukaguzi katika mamlaka za umma na bodi nyingine kuna mapendekezo 15 yaliyotolewa kwa utekelezaji: “Lakini hadi sasa mapendekezo hayo hayajatekelezwa kikamilifu.”

Alisema mapendekezo hayo ambayo hayajatekezwa yanahitaji ufumbuzi wa Serikali ili kuyawezesha mashirika mengine ya umma kufanya vizuri.

Badra Masoud, Meneja mahusiano wa Tanesco hakuweza kupatikana jana kuzungumzia suala hiyo baada ya simu yake kuita muda wote bila kupokelewa huku simu ya Mkurugenzi wa Tanesco William Mhando ikiwa haipatikani.

CHANZO: Mwananchi

22 Feb 2011


Kuna taarifa kwamba mtu aliyetambulishwa kama mmiliki wa kampuni ya Dowans, Brigedia Jenerali (Mstaafu) Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi ni kiini macho.

Chanzo cha kuaminika kinaeleza kuwa tukio zima la "mmiliki wa Dowans kuzungumza na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari" ni sehemu tu ya mkakati mahsusi na endelevu kuughilibu umma wa Watanzania katika sakata la malipo ya fidia kwa kampuni hiyo.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo,sababu iliyopelekea "Bilionea huyo wa Dowans" kukataa kupigwa picha mgando wala kurekodiwa na kamera za televisheni ni hofu kuwa "danganya toto" hiyo ingebainika kirahisi pindi Watanzania wangekwenda mbali zaidi kuchimba undani na ukweli.

Lakini hata katika mazingira ya kawaida tu,haiyumkiniki mfanyabiashara anayejitambulisha kuwa amewekeza zaidi ya dola bilioni moja (USD 1,000,000,000,000) nchini India akwepe kupigwa picha kwa madai dhaifu kuwa anaendesha biashara zake kwa "low profile".

Na kama hiyo haitoshi,itakumbukwa kuwa Waziri wa Nishati William Ngeleja aliwahi kutangaza wamiliki wa kampuni ya Dowans (ambao bosi wa Ngeleja,Rasi Jakaya Kikwete,alidai hawajui) ni Brigedia Jenerali Sulaiman Mohamed Yahya Al Adawi ambaye ni raia wa Oman, Guy Arthur Picard raia wa Canada, Stanley Munai raia wa Kenya. Wengine ni Andrew James Tice raia wa Canada, Gopala Krishnan Balachandran kutoka India na Hon Sun Woo kutoka Singapore.Lakini katika mkutano wake na wahariri hao,'Bilionea huyo wa Dowans' alidai kuwa yeye pekee ndio mmiliki wa kampuni hiyo.


Na kama hiyo haitoshi, 'Bilionea huyo wa Dowans' alishawahi "kuruka kimanga" huko nyuma akidai yeye si mmiliki wa kampuni hiyo LAKINI SASA ANADAI SI TU MMILIKI BALI MMILIKI PEKEE.Hizi ni dalili za wazi za ubabaishaji wa "Bilionea" huyu! (And shame on you gazeti la Tanzania Daima kwa habari iliyoonyesha bayana mnalamba miguu ya mtu huyu ambaye laiti ikibainika ni yeye basi mahala panapomfaa ni Segerea kama sio Keko au Ukonga).

Tovuti hii inaendelea na uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo na inaahidi kuwafahamisha maendeleo (ya uchunguzi huo).Kwa wakati huu,tunatoa wito kwa waandishi wetu wa habari kuacha uzembe wa kuripoti kinachotamkwa tu badala ya kwenda mbali zaidi na kufukua data mbalimbali.Kadhalika,wahariri walioalikwa na Brigedia huyo walipaswa kuwa na msimamo wa kuhoji kwanini hataki picha zake zionekane kwenye vyombo vya habari.

10 Feb 2011



Mlolongo wa ushahidi kuwa Kikwete ni sehemu muhimu ya ustawi na mafanikio ya ujambazi wa Dowans,na uthibitisho kuwa nchi imemshinda.

www-freemedia-co-tz

www-mwananchi-co-tz

www-freemedia-co-tz (1)

www-mwananchi-co-tz (1)

www-freemedia-co-tz (2)

Www Uhurupublications Com

24 Jan 2011



Kwa hakika inachosha kila unapoingia mtandanoni na kukutana na episode mpya ya sakata la Dowans.Tangu mwanzo ilishabainika Rais Jakaya Kikwete yuko upande gani katika ishu ya ujambazi wa waziwazi (daylight robberies) ulioshamiri kwenye sekta ya nishati.Lakini si vibaya kujikumbusha tumetoka wapi na uhusika wa Kikwete katika ufisadi unaokaribia kuadhimishwa kitaifa kwa tuzo kubwa ya mabilioni ya shilingi kwa kampuni ya kijambazi ya Dowans.


Muda si mrefu baada ya Kikwete kuingia madarakani,aliendeleza mlolongo wa porojo zake za kuwaletea Watanzania maisha bora kwa kulipatia ufumbuzi tatizo sugu la nishati ya umeme.Na hapo tunaweka kando uhusika wa Kikwete katika mkataba mwingine wa kitapeli unaoiwezesha kampuni ya IPTL kulipwa mamilioni ya shilingi hata wasipoipatia Tanesco mchango wa umeme katika gridi zake.

Huku baadhi ya Watanzania wakiendelea kuamini kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu,aliwaahidi kuwa tatizo la umeme litakuwa historia pindi itapowasili mitambo ya umeme kutoka nchini Marekani.Na hatimaye mitambo hiyo ikawasili kwa mbwembwe ikiwa imekodiwa dege kubwa la mizigo.Picha zikapigwa,wahusika katika radio,runinga, magazeti na blogu wakaripoti.

Lakini kama wasemavyo waswahili kuwa za mwizi arobaini,mitambo hiyo ikabaki kuwa mitambo tu.Kumbe sio tu ilikuwa bomu bali hata kampuni iliyopewa dili na Kikwete-RICHMOND HIYO- nayo ilikuwa bomu.Actually,ilikuwa ni kampuni yenye ofisi kwenye brifukesi.

Kikwete akaufyata kana kwamba si yeye aliyeutangazia umma kuwa mitambo feki ya richmond ingekuja kumaliza tatizo la upatikanaji wa nishati ya umeme.Lakini kwa vile Kikwete hakuwa peke yake kwenye dili hilo,swahiba wake wa karibu,na Waziri wake Mkuu kwa wakati huo,Edward Lowassa,akaamua kulivalia njuga suala hilo na kuanzisha jitiahada za makusudi kuzuwia mjadala wowote kuhusu utapeli huo.Katika harakati hizo,blogu hii ilikumbwa na zahma pale mwandishi wa habari wa Lowassa,Said Nguba alodiriki kuandika comments kali hapa bloguni akinishambulia Truly Yours baada ya mie kumkemea Lowassa kuhusu jitihada zake za kuzuwia mjadala wa Richmond Bungeni. 

Kadhalika,msimamo wangu na wa blogu hii kuhusu suala hilo ilipelekea kupewa karipio kali kutoka kwa aliyekuwa mwajiri wangu wakati huo huku bosi aliyenipigia simu kuwasilisha karipio hilo akihoji nimekuja Uingereza kusoma au kuandika habari za uchochezi.Kichwa maji huyu alijifanya haelewi kuwa mie nilikuwa najinyima muda wangu wa masomo ili kufanya kile mwajiri wangu alipaswa kukifanya in first place,na laiti angefanya basi leo hii tusingekuwa tunajadili malipo kwa mrithi wa Richmond,yaani kampuni ya kiharamia ya Dowans.Kwa sababu za kimaadili,siwezi kumtaja mwajiri huyo. 

Ofkoz,Nguba na bosi huyo walikuwa wanatekeleza tu wajibu wao uliokuwa unawawezesha kupeleka mikono yao kinywani.Hata hivyo,kile kile nilichokiasa kwenye makala iliwasukuma wazushi hao kunikaripia,kilitokea miaka miwili baadaye: Lowassa alilazimika kujiuzulu baada ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dr Harrison Mwakyembe kuchunguza sakata hilo la Richmond kukamilisha kazi yake.

Kufupisha habari,baadaye Richmond ikarithishwa kwa jambazi mwingine Dowans.Na muda wote huo Kikwete akaendelea kuuchuna kana kwamba kinachotokea hakihusiani na maamuzi yake finyu.Baadaye mjadala wa Richmond ukarejeshwa tena bungeni lakini kwa vile wahusika walishajipanga vyema kuukabili,na kwa vile CCM ilishajitambulisha kuwa ni kichaka cha mafisadi,mjadala huo ukamalizwa kishkaji.Hakuna aliyewajibishwa,na Watanzania kama kawaida yao wakaendelea na maisha yao kana kwamba hakuna fedha zilizoibiwa.

Kelele za hapa na pale zilikuwepo,lakini kimsingi zilikuwa kama kelele za kutimiza wajibu tu (talking for sake of hearing own voice).Ni katika kipindi hicho pia kukazuka mjadala nini kifanyike kuhusu mitambo feki ya Dowans.Baadhi ya wenzetu,kwa mfano Mbunge Zitto Kabwe,walishauri mitambo hiyo itaifishwe.Wengine wakasisitiza kuwa kutaifisha pekee hakutoshi pasipo kuwawajibisha waliotuingiza mkenge katika suala hilo.Wakati wote huo Kikwete aliendelea kujifanya bubu na kiziwi kuhusu ishu hiyo.

Lakini kabla kidonda hakijapona,zikasikika habari kuwa Mahakama moja ya Kimataifa imeipa ushindi Dowans na serikali kuamuriwa ilipe mabilioni kama fidia.Kichekesho,or rather matusi,ni ukweli kwamba habari kuwa serikali imeshtakiwa na Dowans zilifanywa siri.Na kama kuongeza uzito wa matusi,viumbe waliopaswa kuwa watetezi wa umma kupinga malipo kwa majambazi wa Dowans-hapa namaanisha Waziri wa Nishati William Ngeleja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Werema- wakaibuka kuwa watetezi wa Dowans.Uchizi,kulewa madaraka,sintofahamu au sheer ufisadi!!!???Yani mshtakiwa anakuwa bize kuhalalisha hukumu dhidi yake?Kwanini basi nguvu wanayotumia mafisadi hawa baada ya hukumu kutolewa haikutumika kuhakikisha wanashinda kesi husika (assuming kulikuwa na kesi kweli,maana kuna tetesi kuwa mahakama yenyewe ilikuwa katika mfumo wa mlo wa jioni hapo Movenpick).

Back to Rais wetu Kikwete.Ameendelea kuuchuna hadi majuzi.Awali,alipotuhumiwa kuwa ndio mmiliki wa Dowans,mpambe wake Salva Rweyemamu akakurupuka na kauli chafu kabisa dhidi ya mwakilishi wa umma,Dkt Willibrod Slaa,aliyeamua to call a spade a spade kwa kubainisha kwamba Kikwete ndiye Dowans.Siku chache baadaye Kikwete akamjibu Dkt Slaa kwa vitendo: akaagiza askari wake (through IGP Said Mwema) wapige hadi kuua wananchi wasio na hatia huko Arusha.

Lakini,again za mwizi arobaini.Juzi tumefahamishwa bayana kuwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichokaa chini ya uenyekiti wa Kikwete kimeridhia malipo kwa Dowans.Huhitaji japo short course ya uchambuzi wa siasa kutambua kuwa laiti Kikwete angekuwa upande wa wananchi na hivyo kupinga malipo kwa kampuni hiyo ya kifisadi,Kamati Kuu isingethubutu kuridhia malipo hayo.Kwa hiyo at last Kikwete ameweza kuibua sura yake aliyoficha mchangani kwa ukimya wa kuzungumzia suala la Dowans,na ametujulisha bayana kuwa kamwe hawezi kukata mkono unaomlisha.Hawezi kuamuru Dowans isilipwe ilhali yeye ni mhusika mkuu katika ujio wa Richmond iliyorithiwa na Dowans.


Nihitimishe kwa kutoa wito kwa Kikwete na washirika wake wa Dowans kuwa sasa tumechoshwa na drama hii.Wameshaamua kujilipa,wajilipe.Hakuna haja ya kuendeleza mchezo huu mchafu wa kuigiza.In fact,hakukuwa na haja kwa CCM kutoa tamko la kuridhia malipo hayo kwani walishaamua mapema kuwa watailipa Dowans.Kwanini wasiilipe wakati inawadai fadhila?Actually,kwanini wasijilipe wakati wao ndio wamiliki wa kampuni hiyo?Wanasaini mikataba fyongo kwa makusudi ili baadaye waivunjue kisha wajishtaki mahakamani na kudai fidia,na hatimaye wajilipe.Yaleyale ya kununua bima ya moto kisha mnunuzi wa bima hiyo anachoma moto alichokiwekea bima,na kuishia kulipwa mara 1000 ya gharama halisi bima husika.

Sio kama nimechoka kupiga kelele dhidi ya ufisadi bali katika ishu hii ya Dowans naona kama kelele zetu zinamaliza sauti bure.Kwenda Mahakama Kuu kuzuwia malipo kwa Dowans ni wazo zuri,only if we forget nani anayewateua majaji tunaowapelekea kesi hiyo.Mnadhani kasi ya Kikwete kuteaua majaji ni coincidence tu?Anaweza kuwa dhaifu katika kuitumikia Tanzania ipasavyo lakini yuko makini sana katika kuhakikisha maslahi yake binafsi na ya washkaji zake hayaathiriwi kwa namna yoyote ile.

18 Jan 2011









SAKATA LA DOWANS: Sitta afungwa mdomo

BARAZA LA MAWAZIRI CHINI YA JK LAMSHAMBULIA YEYE NA MWAKYEMBE

na Mwandishi wetu

RAIS Jakaya Kikwete amemfunga mdomo Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samuel Sitta aliyeingia katika mzozo na waziri mwenzake wa Nishati na Madini, William Ngeleja.

Mzozo huo uliibuka baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi (ICC), kuamua Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) iilipe Dowans fidia ya sh bilioni 94 kutokana na TANESCO kuvunja mkataba nayo.

Uamuzi wa kumziba mdomo Sitta, ulifikiwa jana katika kikao cha Baraza la Mawaziri, kilichofanyika Ikulu, jijini Dar es Salaam, chini ya Rais Kikwete, ambapo pamoja na mambo mengine, mjadala wa malipo ya Dowans ulitawala kikao hicho.

Mwingine aliyepigwa kufuli katika kikao hicho ni Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk. Harrisson Mwakyembe, ambaye naye aliungana na Sitta kumpinga Ngeleja kuilipa Dowans.

Vyanzo vyetu vya habari vilisema Sitta na Mwakyembe walikuwa na wakati mgumu kutetea hoja ya kutaka serikali isiilipe Dowans na kwamba hata Rais alisema hafurahishwi na hukumu ya malipo hayo.

“Kikao bado kinaendelea, lakini Sitta na Mwakyembe walibanwa sana na mawaziri na hata Bwana mkubwa (Rais) aliungana na mawaziri wengine kuwalaumu kwa kupeleka mjadala huo hadharani,” kilisema chanzo chetu cha habari.

Kwa mujibu wa habari hizo, kuanzia sasa Sitta na Dk. Mwakyembe, wamefungwa mdomo kuzungumzia suala la malipo ya Dowans hadharani na kwamba wanapaswa kuwa kitu kimoja kuhakikisha mipango ya serikali inatekelezwa kama ilivyopangwa.

Kabla ya kibano hicho jana, wiki iliyopita katika kikao cha kamati ndogo ya mawaziri uliibuka msuguano wa hoja kati ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema na Waziri Sitta.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho ambacho kilifanyika chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, zinaeleza kuwa Jaji Werema alieleza kusikitishwa na matamshi ya Sitta katika vyombo vya habari.

Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho zimemkariri Werema akieleza kushangazwa na hatua ya Sitta kuwashambulia yeye na Ngeleja huku akijua kuwa walichokifanya na kuamua kilikuwa kinagusa moja kwa moja mamlaka yao ya kiwajibu na kimamlaka.

Jaji Werema amekaririwa akimweleza Waziri Sitta kwamba iwapo kweli alikuwa ana uchungu na suala la Dowans, basi wakati kesi ikiendelea alipaswa kuisaidia serikali katika kuwasilisha utetezi dhidi ya malalamiko 17 yaliyokuwa yamewasilishwa na kampuni hiyo.

Habari zinaeleza kwamba hatua ya Sitta ambaye alikuwa akitambua fika namna kesi hiyo ilivyokuwa ikiendelea kutochangia jambo lolote wakati shauri hilo likiwa ICC na badala yake kusubiri hadi serikali ishindwe ndipo aanze kutoa matamshi katika vyombo vya habari ilikuwa ni ya kuchochea hasira za wananchi dhidi ya viongozi pasipo sababu zozote.

Wakati Jaji Werema akimshushia lawama Sitta kwa muda usiopungua dakika 15, Waziri Mkuu Pinda alikuwa kimya muda wote.

Baada ya kumaliza hoja yake, Waziri Mkuu aliwataka wajumbe wa kamati hiyo ya mawaziri iliyokuwa ikijadili kuhusu Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Manunuzi unaotarajiwa kuwasilishwa katika Bunge lijalo kuendelea na mjadala.

Awali kabla ya Werema kuzungumza, Sitta alichangia kuhusu muswada huo na akaeleza haja ya kuwekwa kwa masharti magumu zaidi ili kuzuia uwezekano wa makampuni ya kitapeli kujipenyeza nchini na kuigharimu serikali mamilioni ya fedha kauli ambayo ilionekana kumkera Werema.

Awali hofu ilitawala kwamba Sitta na Mwakyembe, wangeweza kupoteza nafasi zao za uwaziri kutokana na hatua yao ya kuibua mjadala dhidi ya mawaziri wenzao nje ya Baraza la Mawaziri kuhusu uamuzi wa serikali kukubali kuilipa Kampuni ya Dowans Holdings SA.

Mkanganyiko wa kauli ya Sitta na Mwakyembe, ulisababisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe, kutoa matamshi makali ya karipio kwa mawaziri hao wawili.

Ukali wa matamshi hayo ya Chikawe ambaye anadaiwa kupata baraka za Rais Kikwete, uliongezwa na tamko lake la kuwataka Sitta na Mwakyembe iwapo wanataka kuendeleza malumbano hayo nje ya utaratibu wa kawaida wa mawasiliano wa mawaziri, wajiondoe serikalini.

Chikawe amekaririwa akisema kitendo cha Sitta kumtuhumu Ngeleja kwamba alitangaza kulipwa kwa Dowans kabla suala hilo halijafikishwa katika Baraza la Mawaziri kinakwenda kinyume cha miiko ya uwaziri kinachomtaka kutotoa siri za baraza.

Kwa mujibu wa Chikawe, Waziri Ngeleja kwa mamlaka aliyonayo kama waziri mwenye dhamana na masuala ya nishati alikuwa na mamlaka ya kutoa tamko alilotoa baada ya kufanya mashauriano na wataalamu mbalimbali wa masuala ya sheria serikalini.

Chikawe alisema iwapo Sitta na Mwakyembe walikuwa hawajaridhishwa na uamuzi wa Waziri Ngeleja walikuwa na njia za kuwasilisha hoja zao pasipo kutumia vyombo vya habari.

Kwa upande wake, Mwakyembe ameingia matatani kutokana na kunukuliwa na gazeti la Uhuru linalomilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) akieleza kushangazwa na hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICC) iliyoipa ushindi Dowans dhidi ya serikali na kutakiwa kulipwa fidia ya shilingi bilioni 94.

ICC iliamua katika hukumu yake Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) iilipe Dowans fidia ya sh bilioni 94 kutokana na TANESCO kuvunja mkataba nayo.


HAIHITAJI UTAFITI KUBAINI KUWA KIKWETE SIO TU ANASAPOTI DOWANS ILIPWE MABILIONI KAMA ZAWADI KWA KAMPUNI HIYO KUFANIKISHA WIZI HUO MKUBWA WA FEDHA ZA UMMA,BALI PIA YEYE NDIYE ALIYERIDHIA MCHAKATO MZIMA KUANZIA ENZI ZA MAJAMBAZI WA RICHMOND HADI KWA MRITHI WAKE DOWANS.

KWA NAMNA MWENENDO WA MAMBO ULIVYO,WE ARE ALREADY SCREWED (NIKITUMIA SENTENSI YA KISWAHILI ITAKUWA MATUSI).DOWANS WATALIPWA KWA VILE MWENYE NCHI (YES,WAMEIBINAFSISHA TANZANIA NA KUWA KAMA MALI YAO BINAFSI).

LAKINI WAKATI KIKWETE ANAFANYA BIDII KUHAKIKISHA MABILIONI HAYO YANALIPWA KWA MASWAHIBA ZAKE,ASIJIFANYE HAONI KINACHOJIRI HUKO TUNISIA.NA KAMA WASHAURI WAKE WANAMDANGANYA KUWA WATANZANIA WA 2011 NI WALEWALE WA 2005 WAKATI ANAINGIA MADARAKANI BASI HAWAMTAKII MEMA.

ASITOKEE MPUUZI WA KUSEMA TUNAHAMASISHA VURUGU WAKATI WANATUFANYA WATANZANIA KAMA MAHAYAWANI.HAIWEZEKANI KABISA KUWALIPA WEZI NA MAJAMBAZI HATA KAMA TUNGEKUWA NA UTAJIRI WA KUPINDUKIA.

KIKWETE,YOU HAVE BEEN WARNED.JUST REMEMBER THAT ALTHOUGH YOUR SWAHIBAs DID ALL IT TOOK TO MAKE SURE YOU BECAME OUR PRESIDENT (SO THAT YOU WOULD REMAIN INDEBTED TO THEM THROUGHOUT YOUR TERMS OF LEADERSHIP), THEY CERTAINLY WONT BE ABLE TO STOP A TUNISIA-LIKE PEOPLE'S POWER MOVEMENT NOR WOULD THEY CARE ABOUT YOU WHEN THE MASSES SAY "NO MORE SCREWING,ENOUGH IS ENOUGH"

8 Jan 2011







Mbunge wa zamani kutoka chama cha Labour hapa Uingereza,David Chaytor (pichani juu),leo amelala usiku wa kwanza akiwa jela kama mfungwa baada ya kuhukumiwa kifungo cha miezi 18 kutokana na kukutwa na hatia ya ubadhirifu wa fedha za umma takriban pauni 20,000 (takriban shilingi 45 milioni za Tanzania).Ubadhirifu wa fedha hizo za umma ni kutokana na matumizi mabaya ya fedha za posho kwa wabunge.


Wakati hayo yakijiri hapa,huko nyumbani Waziri wa Nishati na Madini,William Ngeleja alivunja mzizi wa fitina kwa kutangaza hadharani kuwa hatimaye serikali italipa shilingi 95,000,000,000 (bilioni tisini na tano) kwa kampuni ya kifisadi ya Dowans kufuatia hukumu ya kiini macho iliyotoa ushindi kwa kampuni hiyo licha ya rundo la utata linaloendelea kuizunguka.



Ngeleja,bila haya wala uoga,alieleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Frederick Werema) ameridhia hukumu hiyo ya miujiza kabisa na ushauri wake wa kitaalam (ya sheria) ni kuilipa kampuni hiyo.

Wote,Ngeleja na Werema ni wateuliwa wa Rais Jakaya Kikwete,ambaye kwa makusudi kabisa aliepuka kuzungumzia suala la Dowans katika hotuba yake ya kukaribisha mwaka mpya 2011.Ni dhahiri kuwa Kikwete ameridhia Dowans ilipwe na ndio maana Ngeleja na Werema wanatoa maamuzi yao bila hofu wala aibu. Na kama umesahau,ni Kikwete huyuhuyu aliyeahidi wakati wa kampeni zake kuwa ana dhamira ya kuboresha maisha ya Watanzania.Nadhani labda alichomaanisha ni kuboresha akaunti za mafisadi kwa mgongo wa walalahoi.

Napata shida kutumia lugha ya kistaarabu kushangazwa na uwendawazimu huu!Hivi hawa viongozi wetu wamerogwa na mafisadi au ni matokeo ya kupokea fadhila za mafisadi kupita kiasi kwamba sasa wanalazimika kulipa fadhila hizo kwa gharama yoyote ile?Hizi sio tamaa za kawaida tulizozowea kuziona kwa watawala wetu.Hiki ni kichaa hatari ambacho pasipo hatua za haraka kinaweza kupelekea nchi nzima kuuzwa,kisha akina Werema wakaja kutuambia gharama za kuzuia kuuzwa kwa nchi yetu ni kubwa kuliko uamuzi wa kukubali nchi iuzwe.

Blogu hii ilifanya kila ilichoweza kuhamasisha wapiga kura waiepuke CCM na mgombea wake Kikwete.Sio kwamba blogu hii ilifanya utafiti wa kina kubaini athari za kuirejesha CCM madarakani bali taarifa kuhusu uhuni wa chama hicho,sambamba na kilivyojipa jukumu la kuwa kichaka cha kuhifadhi mafisadi,zilikuwa bayana kwa kila mwenye macho.Hivi kuna Mtanzania asiyefahamu kuwa ujio wa kampuni ya kijambazi ya Richmond (iliyopelekea ujambazi mwingine wa Dowans) ulikuwa na baraka za Kikwete pamoja na swahiba wake Lowassa na "kubwa la maadui" Rostam Aziz?





Ndio maana majuzi baada ya aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dkt Wilbroad Slaa,kurejea kauli yake kuwa Kikwete ni mmiliki wa Dowans,hasira za mkuu huyo zikaishia kwa kuamuru polisi wake kutoa kipigo kwa raia wasio na hatia huko Arusha na kupelekea vifo kadhaa (Polisi wanadai wameua watu watatu tu lakini tangu lini wauaji wakaaminika?).


Na kama adhabu ya Kikwete kwa Chadema na wana-Arusha haijatosha,kaamua kuwadhihaki Watanzania wote kwa kuidhinisha Dowans ilipwe mabilioni hayo,huku swahiba wake Rostam akidhihaki Watanzania kwa kudai hizo bilioni kadhaa ni fedha kiduchu tu kwake.Huwezi kumlaumu kwani kaiweka serikali mfukoni na anaendesha nchi kwa remote control.

Blogu hii iliwaasa wapiga kura kuhusu madhara ya kumpatia Kikwete miaka mitano mingine baada ya awamu yake ya kwanza kugubikwa na ufisadi wa kutisha.Lakini hata kwa viwango vilivyozoeleka vya ufisadi hakuna aliyetarajia kuwa hata kabla miezi mitatu haijapita tangu arejee madarakani,Kikwete angediriki kuruhusu Watanzania wenzie wabakwe kiuchumi kwa mtindo huu wa Dowans.Lakini kwa vile Katiba tuliyonayo inampa madaraka mithili ya mungu-mtu,na kwa vile anafahamu fika kuwa Watanzania ni wepesi wa kusahau na ndio maana wengi wao wakampigia kura licha ya maumivu aliyowasababishia tangu aingie madarakani Desemba 2005,ameruhusu ujambazi huu wa mabilioni ya fedha za walipa kodi pasi soni.

Tusipochukua hatua za haraka tutashtukia tumefikishwa mahala ambapo hatutokuwa na namna ya kurekebisha mambo.Kama less than three months tangu Kikwete arejee madarakani tumeshashuhudia Dowans ikizawadiwa mabilioni kama asante ya kututapeli,na tumeona hasira za Kikwete kwa ukatili na mauaji yaliyofanywa na polisi wake (kisa kasutwa kuwa analea ufisadi),ni wazi kuwa hali itazidi kuwa mbaya na yawezekana ikawa ya kutisha kabla Kikwete hajamaliza muda wake hapo 2015 (assuming hatachakachua Katiba kutaka aongezewe muda).

Moja ya hatua inayoweza kuzaa matunda ni kufikisha kilio chetu kwa nchi wahisani.In addition to malezi anayotoa Kikwete kwa mafisadi,sasa tuna jambo jingine zito ambalo linaweza kuvuta hisia za wahisani,nalo ni ukiukwaji wa haki za binadamu kama ilivyodhihirika huko Arusha.



Kwa kuanzia,blogu hii inamwomba kila mzalendo anayeishi katika nchi mfadhili kwa Tanzania,kuwasiliana na mbunge wake na kumwomba afikishe kilio cha wanyonge wa Tanzania.Toa chapa ya picha za matukio ya Arusha pamoja na habari zinazobainisha ukiukwaji wa haki za binadamu,na ufisadi,kisha mfahamishe mbunge huyo kuwa hii ndio hali halisi ya Tanzania chini ya utawala wa Kikwete.Kama utahitaji maelezo zaidi ya namna ya kuwasilisha ujumbe wako kwa mbunge wa sehemu unayoishi,usisite kuwasiliana nami.

KWA USHIRIKIANO WETU,TUNAWEZA KUPAMBANA NA UTAWALA DHALIMU AMBAO LICHA YA KUUA RAIA WASIO NA HATIA HUKO ARUSHA,UNATOA ZAWADI YA SHILINGI BILIONI 95 KWA DOWANS KANA KWAMBA HIYO NDIO RAMBIRAMBI KWA WALIOUAWA NA POLISI HUKO ARUSHA.

5 Jan 2011

Picha Hii Inatoa Maelezo Alfu Kidogo.Ukiangalia kwa Makini Utamwona Rostam Kama Kalizimishwa Kuinua Mkono,huku Kikwete Akiwa as if Anampigia Debe Bosi Wake...na Tabasamu Juu!Lol,Ama Kweli Rais Tunaye,Si Mchezo

Dk. Slaa: Kikwete ajiuzulu
• Asisitiza anahusika na Dowans, aahidi kutoboa siri
na Janet Josiah

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa, sasa amekuja na hoja mpya ya kumtaka Rais Jakaya Kikwete ajiuzulu kutokana na kuhusika moja kwa moja na sakata la Dowans iliyorithi mikoba ya Richmond.

Dk. Slaa ametoa kauli hiyo nzito jana katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima Jumatano, ikiwa ni siku moja baada ya Ikulu kutoa taarifa ya kejeli na vijembe vya mitaani dhidi yake kuhusu sakata hilo.

Akizungumza kwa utulivu na umakini mkubwa, Dk. Slaa alisema Rais Kikwete alipaswa kujiuzulu kabla ya aliyekuwa Waziri Mkuu na swahiba wake mkubwa, Edward Lowasa, kuchukua hatua hiyo Februari 7, mwaka 2008, mjini Dodoma.

Yaani Kikwete Mpaka Kaikamata Mic Kuhakikisha Kuwa Debe Analompigia Swahiba Wake ni La Nguvu Kweli Kweli!Kama Alivyowahi Kusema Lowassa,Wawili Hawa Hawakufahamiana Mtaani.Wametoka Mbali.BIRDS OF A FEATHER..
Mawaziri wengine waliojiuzulu kutokana na sakata la Richmond lililozua mjadala mkali nchini ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati huo, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha ambaye alikuwa waziri wa wizara hiyo kabla ya kuhamishiwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC).

Akitoa ufafanuzi wa taarifa ya Ikulu iliyotolewa juzi na Kurugenzi ya Mawasiliano, Dk. Slaa alisema mkuu huyo wa nchi hawezi kukwepa kuhusishwa na sakata la Dowans, kwani alilijua hata kabla mitambo yake haijaingizwa nchini.

"Nataka niwatoe Watanzania wasiwasi kwamba ingawa kurugenzi ya mawasiliano imetoa taarifa ya kumsafisha Rais Kikwete na kunikashifu mimi kwa lugha ya mtaani, nawaambia alipaswa kujiuzulu kabla na anatakiwa ajiuzulu sasa, kwani anahusika moja kwa moja na uingiaji wa mkataba wa Kampuni ya Richmond na baadaye na Dowans" alisema Dk. Slaa.

Alimtaka Rais Kikwete kutambua kuwa hawezi kukaa kimya kwa kisingizio cha kuhatarisha amani na utulivu wakati wananchi wanaibiwa mabilioni ya fedha na mafisadi wachache kupitia kampuni feki ya Dowans.

Akirejea historia ya vita dhidi ya ufisadi aliyoiasisi bungeni, Dk. Slaa aliwataka wananchi wakumbuke kuwa taifa lilipokumbwa na tatizo la umeme kabla ya mitambo ya Richmond kuingia nchini, Rais Kikwete alikwenda Marekani kwa ziara ya kikazi.

Alisema aliporejea nchini, alizungumza na waandishi wa habari kuhusu tatizo hilo na kuahidi kuwa serikali yake inalifanyia kazi na siku chache baadaye, rafiki yake wa karibu, Rostam Azizi, Mbunge wa Igunga (CCM), naye alikwenda Marekani.

"Rostam aliporejea kutoka Marekani baada ya siku chache tukaanza kusikia mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura kutoka Kampuni ya Richmond inatarajiwa kuwasili. Kweli ilitua nchini katika Uwanja wa Mwalimu Nyerere na shughuli nyingine zilifungwa uwanjani hapo kupisha ushushaji wa mitambo ya Richmond" alisema Dk. Slaa.

Kwanini Rostam Asiwe na Furaha?Kuendesha Nchi ya Watu Takriban Milioni 50 kwa Kutumia Remote Control si Jambo Dogo Ati!

Huku akisisitiza kuwa ana ushahidi wa anachokisema, Dk. Slaa alisema hata baada ya Richmond kushindwa kuzalisha umeme na kusababisha mawaziri kujiuzulu, serikali ya Kikwete iliamua kuingia mkataba na Dowans iliyorithi shughuli za Richmond na hatua hiyo Rais Kikwete pia aliijua.

"Dowans nayo ikashindwa kuzalisha umeme, mwisho Bunge katika moja ya maazimio yake liliridhia uamuzi wa kuvunja mkataba huo, lakini leo Serikali inadaiwa fidia ya sh bilioni 185, je, Rais Kikwete anaweza kukwepa kwamba hana mkono wake hapo?" alihoji.

Kutokana na hayo, Dk. Slaa alimtaka Rais Kikwete amtaje mmiliki halali wa Dowans ili kuwatoa kiu Watanzania wanaohitaji kumjua.

"Sitaacha kuzungumzia masuala yanayowagusa Watanzania na mali, hasa katika kipindi hiki ambacho Watanzania wanataka kuibiwa fedha zao, wakati wa kukaa kimya umekwisha" alisema Dk. Slaa.

Alisema hashangazwi na kejeli za Ikulu na kuwataka Watanzania kukumbuka alipoanza kuwalipua mafisadi, Rais Kikwete aliwahi kutamka kwamba kelele za mlango haziwezi kumnyima mwenye nyumba usingizi na kamwe kelele za chura hazimzuii ng ombe kunywa maji.

Kaaazi Kweli Kweli
"Lakini baada ya sisi kuamua kupambana na Richmond, Rais Kikwete alikiri linamnyima usingizi na hili la Dowans litamnyima usingizi zaidi katika kipindi hiki cha mwisho cha uongozi wake" alisema Dk. Slaa.

Ili kumaliza kelele za Dowans, Dk. Slaa alimtaka Rais Kikwete kumtaja mmiliki wake ambaye anataka kuwaibia Watanzania mabilioni ya fedha.


 
Wakati Dk. Slaa akimkaba koo Rais Kikwete, mjadala wa Dowans hivi sasa umewavuruga hata viongozi wa serikali tangu ilipoamriwa ilipwe sh bilioni 185.

Aliyekuwa Spika wa Bunge lililopita, Samuel Sitta, hivi karibuni alikaririwa akiitaka serikali iache kuilipa Dowans kwa madai kuwa ni mradi wa mafisadi watatu.

Kauli hiyo ilipingwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambaye alisema kuwa suala la malipo ya Dowans lipo kisheria na ikithibitika serikali haiwezi kukata rufaa, italazimika kulipa mabilioni hayo.

Juzi Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeelezea kukerwa kwake na hatua ya Dk. Slaa kumtaja Rais Kikwete kuwa alihusika katika uzembe uliosababisha taifa kutakiwa kuilipa Kampuni ya Dowans sh bilioni 185 kama fidia.

Taarifa hiyo kali ya Ikulu iliyobeba ujumbe wenye maneno ya kebehi na ya mitaani ya kumwita Dk. Slaa mtu aliyechanganyikiwa na mzabinazabina ilisainiwa na Salvatory Rweyemamu, ambaye kabla ya kwenda Ikulu alikuwa mmoja wa wahariri watendaji, aliyekuwa akiheshimika kwa kutumia lugha fasaha na ya staha.

Rweyemamu katika taarifa yake hiyo iliyoonyesha waziwazi kuandikwa na mtu mwenye hasira, chuki na dharau ama kwa Dk. Slaa, CHADEMA na Tanzania Daima, alikwenda mbali na kumwita kiongozi huyo wa kisiasa kuwa ni mtu hatari.

Katika mahojiano maalumu na gazeti la Tanzania Daima Jumapili, mwishoni mwa wiki, Dk. Slaa alikaririwa akisema chanzo cha suala la Dowans kutakiwa kulipwa fidia limetokana na uzembe wa serikali na Rais Kikwete mwenyewe anahusika kuileta Kampuni ya Richmond ambayo baada ya kuonekana ya kitapeli iliamua kurithisha kazi zake kwa Dowans.

VYANZO: Habari kwa Mujibu wa Tanzania Daima.Picha Kutoka Vyanzo Mbalimbali Mtandaoni.

29 Dec 2010



Takriban kila jambo kinaweza kutizamwa kwa sura mbili,au zaidi,hasa kwa minajili ya kuangalia faida na hasara.Ni katika mantiki hiyo,baadhi yetu tunaweza kuthubutu kuangalia "upande wa pili wa shilingi" kuhusu umoja wa Watanzania.Naomba nisisitize kuwa hoja hapa sio kudharau jitihada za waasisi wa taifa letu waliofanya kazi kubwa kujenga mshikamano miongoni mwa makabila zaidi ya 120 na kuzaa Utanzania uliogubika ukabila,udini,nk (angalau kwa kipindi kirefu cha uhai wa Tanzania).

Lakini moja ya athari zinazosababishwa na umoja huo ni uwezekano wa watu wasio na damu ya Kitanzania kujificha kwenye kivuli hicho cha "umoja wetu".Na ukichanganya na udhaifu,let alone ufisadi uliokubuhu,wa Idara ya Uhamiaji,yayumkinika kuamini tuna "Watanzania wenzetu" kadhaa tu ambao kimsingi hawapaswi kuwepo nchini mwetu.Kadhalika,kwa vile teuzi zinazofanywa na Rais Jakaya Kikwete (kama ilivyokuwa enzi za Mwinyi na baadaye Mkapa) hazizingatii kujiridhisha kuhusu u-Tanzania halisi ( as opposed to u-Tanzania wa kufoji), baadhi ya viongozi wanaoteuliwa kushika nyadhifa nyeti wanaweza kabisa kuwa sio Watanzania.

Kuongeza ugumu katika suala hilo la u-Tanzania ni makabila ambayo yametapakaa zaidi ya mipaka ya nchi.Hapa nazungumzia makabila ambayo yapo zaidi ya nchi moja.Kwa mfano,Kenya kuna Wamasai,Wameru,Wajaluo,nk kama ilivyo Tanzania.Simaanishi kila Mtanzania anayetoka katika makabila ya aina hiyo anaweza kuwa na utata katika u-Tanzania wake bali kilicho wazi ni ukweli kwamba ni rahisi kwa asiye Mtanzania (lakini anatoka kabila kama la Kitanzania) kujificha nchini ndani ya kivuli cha umoja wetu.

Tutamtambuaje mtu wa aina hiyo?MATENDO YAKE (including KAULI zake).Na ni katika mstari huo wa fikra nimefika mahali nikalazimika kujiuliza iwapo Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Jaji Werema ni Mtanzania kweli au ni walewale wanaotumia umoja wa Tanzania (licha ya wingi wa makabila)+udhaifu na ufisadi Idara ya Uhamiaji,kuwepo Tanzania isivyo halali,na kupewa madaraka makubwa pasipo watoa madaraka hayo kujiridhisha kuhusu u-Tanzania wa mteuliwa.

Simtuhumu Werema kuwa si Mtanzania kwani sina nyaraka za kuthibitisha hilo.Hata hivyo,nalazimika kupata hisia za walakini katika u-Tanzania wake kutokana na mlolongo wa kauli zake za kihuni na zisizoendana na wadhifa mkubwa aliokabidhiwa.Wakati takriban kila Mtanzania halisi anazungumzia umuhimu wa Katiba mpya,mbabaishaji Werema akakurupuka na kudai hakuna haja ya Katiba mpya (kana kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyesema atashughulikia suala hilo ni mdogo kimadaraka kwa Werema).

Mpuuzi huyu ambaye ni dhahiri kuteuliwa kwake tena kuwa Mwanasheria Mkuu kunathibitisha matatizo makubwa ya kimaamuzi yanayomwathiri Rais Kikwete alifikia hatua ya kusifia rushwa ndani ya CCM kuwa ni sehemu ya demokrasia (rejea gazeti la Uhuru,Agosti 6,2010 habari yenye kichwa AG Asifu Demokrasia CCM).Yani kichwa maji huyu mwenye jukumu la usimamizi wa sheria ikiwa ni pamoja na kupambana na rushwa alijifanya kupofu kwenye rushwa za wazi zilizotawala mchakato wa CCM kupata wagombea wake katika uchaguzi mkuu uliopita.Basi bora angekaa kimya,lakini mropokaji huyu akaona ni vme atuthibitishie how good msema ovyo he is.

Tunakumbuka pia ubabaishaji wake kuhusu muswada wa kizushi wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi.Ofisi ya mbabaishaji huyu pasipo aibu iliwasilisha madudu huko Bungeni ambapo haikuchukua muda kwa watu makini kama Dr Wilbroad Slaa kubaini uhuni uliofanyika.Na kwa vile ni rahisi zaidi kwa Kikwete kufanya teuzi kuliko kutimua wababaishaji,Werema hakuguswa.In fact,amezawadiwa tena Uanasheria Mkuu.

Ilikuwa rahisi kwa Werema kupandwa na muku katika kipindi cha kampeni za uchaguzi na kutishia kuishtaki Chadema kwa sababu anazojua yeye lakini sasa badala ya kuungana na Watanzania halisi kuonyesha hasira zao kuhusu hukumu ya Dowans ambapo serikali inatakiwa kuwalipa matapeli hao shilingi BILIONI MIA MOJA THEMANINI NA TANO (Tshs185,000,000,000/=)!!!!Badala ya angalau kuonyesha uchungu kwa nchi yetu na kuelezea suala hilo kistaarabu,jitu hili linakurupuka na kudai "..The matter is as good as closed...let's use our resources on important issues..." (mjadala huo umefungwa,tuangalie mambo mengine ya msingi).Yaani kwa mzembe huyu wa kufikiri,malipo ya shilingi bilioni 185 kwa matapeli wa Dowans sio suala muhimu (ambao laiti Werema na ofisi yake wangewajibika ipasavyo mmiliki wa Dowans angekuwa jela muda huu).Je cha muhimu ni kipi Mista Jaji?

Kwanini Watanzania wabebeshwe mzigo uliosababishwa na ufisadi katika serikali ya Kikwete?Yes,Kikwete anahofia kumuudhi swahiba wake anayemiliki Dowans,na ataendelea kuwa mateka wa fisadi huyo mpaka anamaliza urais wake 2015.Ni katika mazingira haya ya kubebana na kulindana ndipo wababaishaji kama Werema wanapata nafasi za kupewa madaraka (kulinda maslahi ya mafisadi) na kwa vile anafahamu fika kuwa Kikwete hana ubavu wa kumtimua (Werema) anaropoka kadri misgipa ya mdomo wake inapowashwa.Huyu mtu ana kauli chafu na zilizojaa ngebe.Si mlevi wa madaraka (kama walivydai Chadema) bali ni teja la madaraka.Uanasheria wake Mkuu haukamiliki pasipo kuwadharau Watanzania wenye nchi yao.Hajioni mheshimiwa mpaka aongee maneno mawili matatu ya "kutunyooshea kidole cha kati" (middle finger in the air)

Ndio maana nimepatwa na wazo la kujiuliza kuhusu iwapo Werema ni Mtanzania kweli au ndio walewale wanaojificha kwenye umoja wetu licha ya wingi wa makabila yetu?Nimeeleza hapo awali kuwa katika mchanganyiko huu wa makabila ni rahisi kwa wasio Watanzania kujichanganya nasi kana kwamba ni wenzetu.Kuwatamvua si rahisi lakini kwa bahati nzuri baadhi ya watu hawa wanaweza kutambulika,sio kwa mwonekano wao,bali KAULI ZAO ZINAZOONYESHA BAYANA HAWANA UCHUNGU WALA UPENDO KWA TANZANIA.

Nimalize kwa kumlaumu tena Rais Kikwete kwa kuzidi kuipeleka Tanzania shimoni.Teuzi zake za rapid fire na zinazoelemea zaidi kwenye kulindana badala ya sifa na/au uzalendo ndio sababu ya kupata watu wa ajabu kama huyu Werema.Najua Chadema wamemtaka kichwa maji huyu ajiuzulu,lakini hiyo ni ndoto mbaya.Werema ajiuzulu achekwe?Na akishajiuzulu nani atasimamia maslahi ya mafisadi hapo kwa Mwanasheria Mkuu?Nani atasimamia malipo kwa mafisadi kama wa Dowans?Nani atahakikisha mikataba ya kiuendawazimu inaendelea kusainiwa na kulindwa kwa nguvu zote?Werema ajiuzulu ili Kikwete aonekane a total fraud katika uongozi na teuzi zake?

12 Dec 2010



Majuzi kulifanyika uzinduzi wa kitabu kinachoelezea wasifu wa Rais Jakaya Kikwete.Tukio hilo linaelekea kuwa na uzito wa kipekee kwani baadhi ya picha zilionyesha sehemu kubwa ya familia ya mkuu huyo wa nchi ilihudhuria uzinduzi huo.Sina hakika kuhusu kilichomo kwenye kitabu hicho lakini yayumkinika kuamini kuwa laiti wasifu huo ungegusia masuala kama "Wanamtandao na mchango wao katika ushindi wa Kikwete 2005",au "Uswahiba kati ya Kikwete,Lowassa na Rostam Aziz na jinsi unavochangia kufilisika kwa Tanzania", au "wasifu wa wateuliwa mbalimbali wa Kikwete na namna wanavyohusiana nae",nk isingekuwa rahisi kwa Rais Kikwete kujitokeza kwenye uzinduzi huo.

Mwandishi wa kitabu hicho ni Profesa Julius Nyang'oro.Wakati mwingine najiuliza kama baadhi ya maprofesa wa aina hii wameishiwa na mada za muhimu kwa jamii na badala yake wanageukia kujikomba kwa watawala kwa kuandika wasifu mithili ya pambio.Unaweza kunilaumu kwa kutoa tuhuma kabla sijasoma kilichomo katika kitabu hicho.Hata hivyo,huhitaji upeo wa juu kubashiri yaliyomo katika kitabu hicho,maana laiti ingekuwa ni wasifu wa Kikwete huyu ambaye utawala wake umetuzalishia msamiati wa "ufisadi",sambamba na kugubikwa na ishu za Kagoda,EPA,Dowans,Richmond na uzururaji njeya nchi,basi si mkulu huyo wala wanafamilia yake wangetia mguu kwenye uzinduzi huo.

Sasa sijui Profesa Nyang'oro kajaza nini kwenye wasifu huo!Mamia ya ahadi za Kikwete na kisha kuichambua moja baada ya nyingine ( kwa mtizamo chanya usiomuudhi mtawala) au ni hadithi za namna Jakaya alivyozaliwa katika familia ya kawaida,akajiendeleza pasipo makeke,akashika hatamu za uongozi lakini akiendelea kuwa "mtu wa watu" na hatimaye akapata urais ( bila kutaja mchango wa wanamtandao) na ameendelea kuwa mwenye upendo na upole sio kwa walalahoi pekee bali hata mafisadi.

Huenda wasifu huo pia ukagusia udaktari wa falsafa (wa heshima) wa Rais Kikwete.Inawezekana atapomaliza miaka yake 10 hapo 2015 (na kama hatafanya mbinu za kutaka aongezewe muda madarakani) ataweka historia nyingine ( on top ya ile ya kumpiku Vasco da Gama kwa safari) ambapo atakuwa kiongozi pekee aliyezawadiwa shahada nyingi za uzamifu kuliko mwingine duniani.Sijui mpaka sasa ana PhD ngapi,ila nakumbuka ile ya Uturuki,nyingine sijui ya Uganda kama sio Kenya,hii ya juzijuzi Dodoma na Muhimbili nao wamemzawadi shahada ya Afya ya Jamii.


Na kwa vile utawala wa Kikwete umetawaliwa na usanii wa namna flani,yayumkinika kuhisi kuwa hizo PhDs zinatolewa baada ya wahusika "kupigwa somo" au "kupewa kilicho chao".Ungeweza kuhisi kuwa ilikuwa hivyo hata Profesa Nyang'oro,lakini "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni" hapo itakuwa mtu tu kaamua kujikomba.

Na kama ilivyozoeleka,wanahabari wetu (pamoja na baadhi ya mabloga) walichokumbuka ni picha za tukio na maelezo ya picha hizo (captions) tu,utadhani kwa kuangalia picha hizo msomaji atapata summary ya jumla ya kilichomo katika kitabu hicho.Hapa "simpigi mtu dongo" ila natoa changamoto kwa wenzetu mliobobea kwenye picha,mkumbuke kuwa picha pekee si habari kamili.Hivyo,inapowezekana mtupatie habari zaidi ya picha husika.Ni ushauri tu,tena wa bure buleshi.

Nakumbuka mwaka 2005 kulikuwa na kitabu cha wasifu wa Kikwete.Nahisi hapa katikati kuna waliojipendekeza na kuja na wasifu mwingine.Sasa tuna wasifu huu "mpya" kutoka kwa Profesa Nyang'oro na huenda hapo 2015 kutakuwa na wasifu mwingine wa "miaka 10 ya mafanikio ya kihistoria chini ya utawala wa Jakaya Kikwete".Mtu mmoja wasifu kibao!

Enewei,hiyo ndio Tanzania yetu.Na ukiwa na kiongozi mpenda sifa basi wajanja hawachelewi kumpamba kwa sifa hii au ile.Na kwa vile hawagusii yale yatakayomfanya mtawala atambue kuwa "hajafunga zipu" basi kwa upande mmoja watoa sifa hao wanapata wanachotegemea kupata (sifa,hela,kupiga picha na rais,kualikwa ikulu,na pengine kuzawadiwa U-DC) na kiongozi mpenda sifa anaendelea kuamini yeye ni chaguo la Mungu ndio maana sifa zinaendelea kumiminika kumhusu yeye.

27 Mar 2009


KWA MTU YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU,HATA AKIAMSHWA USINGIZINI AU AKIWA BWII KWA ULEVI,HAIINGII KICHWANI KUSIKIA HOJA ZA KIFISADI ZA KUNUNUA MITAMBO ILIYONGIZWA NCHI KITAPELI NA MAJAMBAZI WA RICHMOND NA HATIMAYE KURITHISHWA KISANII KWA WENZAO WA DOWANS.TUKIRUHUSU HILI LITOKEE,KUNA MAHALA ITAFIKA NCHI YETU NAYO ITAUZWA NA KISHA TUTATAKIWA KUINUNUA BACK....


Tausi Mbowe na Elias Msuya

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa ameitaka serikali kuitaifisha mitambo ya Kampuni ya kuzalisha umeme ya Dowans badala ya kujadili manunuzi yake.

Dk Slaa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada yakutopa taarifa ya kamati kuu kilichokutana kwaajili ya kuandaa mkutano wa baraza kuu.

Alisema kuwa mitambo ya Dowans ilirithiwa kutoka kwenye kampuni ya Richmond ambayo ilibainika bungeni kuwa ni ya kifisadi kwahiyo hakuna haja ya kuinunua tena bali kuitaifisha.

“Msimamo wangu siku zote ni kutaifishwa kwa mitambo ile na siyo kuinunua. Naishangaa serikali, kutaka kuinunua mitambo ya Dowans wakati mitambo ile ilishabainishwa Bungeni kuwa ni ya kifisadi. Kama mtu umekamata kitu chako cha wizi utakinunua tena?" alihoji

Akizungumzia malumbano kati ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Dk Slaa alisema,

“Mradi wa kuzalisha umeme nimeushughulikia kwa miezi minane. Nilikwenda hadi kijiji cha Kisesida mkoni Singida ambako ndiko kampuni mbili za Power Pool East Africa ya Dk Mwakyembe na wenzake na Wind East Africa ya Rostam Aziz zimewekeza.

Kampuni ya Power Pool East Afrika ni ya wazalendo na imeshalipa fidia kwa wakazi wa kijiji cha Kisesida lakini ile ya Wind East Africa haijafanya hivyo, badala yake inabebwa na kiongozi wa ngazi za juu mkoani ambaye amekuwa akiwakejeli wanakijiji wa Kisesida. Ndiyo maana kuna kuwa na malumbano kati ya Rostam Aziz na Dk Mwakyembe,” alisema Dk Mwakyembe.

Akizungumzia tatizo la mgawo wa umeme ambalo litangazwa na Tanesco hivi karibuni, Dk Slaa alisema,"Baada ya kubainika kwa kashfa ya Richmond, Rais Kiwete alitangaza kuwa suala la mgawo wa umeme litakuwa historia katika nchi hii, sasa mgawo huu unatoka wapi tena? nendeni mkamwulize,” alisema Dk Slaa.

Aidha alimshangaa Rais Kikwete kwa kuendelea kumwacha madarakani Mkurugenzi wa Tanesco, Idriss Rashid wakati anatuhumiwa kwa ufisadi.

"Dk Rashid (PICHANI JUU) alihusishwa na ufisadi alipokuwa Gavana wa Benki kuu. Tumeshatoa vilelezo vyote kuthibitisha jinsi alivyoshiriki kwenye ununuzi wa rada na ndiyo maana sasa hivi anashirkiana na Dowans ili kununua mitambo yake kiufisadi. Tunashangaa kwanini Rais Kikwete hamchunguzi, wala kumwajibisha. Eti wanasema Serikali ya Uingereza inachunguza, wakati si kweli. Uingereza wanachunguza ushiriki wa BAE system siyo watu wetu,” alisema Dk Slaa.



CHANZO: Mwananchi
IT MAKES A LOT OF SENSE,DOESN'T IT?UNAMKAMATA KIBAKA NA MALI YAKO,BADALA YA KUMKWINDA AKUREJESHEE NA HATIMAYE KUMFIKISHA POLISI ETI UNAKUBALI AKUUZIE ALICHOKUIBIA!IT COULD ONLY HAPPEN IN TANZANIA,I SUPPOSE!

23 Mar 2009


KADA maarufu wa Chama cha Mapinduzi, Nape Nnauye, amesema malumbano yanayoendelea sasa nchini ni ishara kwamba mafisadi wamejipanga kuifanya nchi isitawalike.

Nape alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu hali ya kisiasa nchini, hususani malumbano yanayoendelea sasa kati ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Bila kutaja majina ya watu, Nape alisema chimbuko la malumbano hayo aliyoyaita ya kipuuzi ni kashfa nzima ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, iliyosababisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na aliyekuwa Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha, kujiuzulu.

Huku akiwa makini kuchangua maneno ya kuzungumza, Nape alisema malumbano hayo yanaonyesha kuna baadhi ya watu hawakuridhika na taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Mwakyembe, hivyo kuna ulazima wa hoja hiyo kurudishwa tena bungeni ili kukata mzizi wa fitna.

“Kuna kila dalili kuwa mafisadi wamejipanga kuhakikisha nchi haitawaliki, ndiyo maana mijadala isiyo na kichwa wala miguu inaibuka kila kukicha hata kwa mambo ambayo yamekwishaamuliwa na chombo kikubwa kama Bunge,” alisema.

Katika kuthibitisha kauli yake, Nape alisema ana taarifa za siri kuwa kuna baadhi ya mafisadi wamekuwa wakifanya mikutano ya faragha ambapo pamoja na mambo mengine, wamepanga kuhakikisha nchi haitawaliki kwa kuibua hoja na mijadala kupitia baadhi ya vyombo vyao vya habari.

“Tunakoenda ni kubaya, ila naamini serikali iko imara na CCM kama chama tawala, tutaomba tulizungumze kwenye vikao vyetu kwa nia njema ya kuliokoa taifa linalovurugwa na watu wachache wenye fedha,” alisema Nape.

Nape alisema ili kuhakikisha Tanzania haiyumbishwi, aliwataka wananchi kupuuzia mjadala wa sasa kwa madai kuwa hauna tija na una lengo la kuhatarisha amani na utulivu uliopo nchini.

Kuhusu mjadala wa ununuzi wa mitambo ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans iliyorithi kutoka Kampuni ya Richmond, kada huyo wa CCM alisema anashangazwa na uamuzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kuomba kibali cha Bunge au kamati zake.

“Kwani TANESCO wanapoenda kununua transfoma na vifaa vingine, wanaomba kibali cha Bunge? Kama si hivyo, kwa nini wanataka kuhalalisha ununuzi wa mitambo ya Dowans kupitia kamati za Bunge? Hata hivyo, Bunge lilishatoa msimamo wake juu ya hilo, kama kuna mtu hakuridhika, alirudishe bungeni na si kuwagawa Watanzania kwa mijadala isiyoisha na vitisho,” alisema Nape.

Mwanasiasa huyo machachari aliwataka mafisadi kutambua kuwa hata wakiibua mijadala ya kuwagawa Watanzania kama ilivyo sasa, hakutabadili ukweli kwamba Richmond na hata mrithi wake Dowans, ndio waliolifikisha taifa hapa lilipo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Maswa, John Shibuda, alisema malumbano yanayoendelea sasa kati ya Dk. Mwakyembe na Rostam kumetokana na upepo wa kisiasa ambao wakati mwingine huleta tija katika kukuza demokrasia.

Hata hivyo, Shibuda ambaye hupenda kuzungumza kwa mafumbo, alisema mjadala huo umejikita kwenye hila na visa vya kufunika mema na mazuri ya mtu.

“Mimi naona hayo ni mapepo ya kisiasa na mtenguko wa fikra ambao umeleta mng’atuko dhidi ya dhulma, lakini ni mjadala wa heri kwa maana kuwa unawafanya watu kutoa manung’uniko yao, bila hivyo hali ingekuwa mbaya siku moja, kwa hiyo naona mjadala uendelee,” alisema Shibuda.

Mbunge wa zamani wa Morogoro Vijijini, Semindu Pawa (CCM), aliiambia Tanzania Daima jana kuwa, mjadala huo sasa umechacha na kuwataka waandishi wa habari kuachana nao.

“Mimi sitaki kusema nani yuko sahihi, lakini nasema mjadala huo umechacha, umepitwa na wakati, wanahabari mkiacha tu, hautausikia tena, lakini naweza kusema wanahabari ndio mnaoukuza, waacheni,” alisema Semindu Pawa.

Mwishoni mwa wiki, Dk. Mwakyembe alijibu tuhuma zinazomhusisha na kumiliki kampuni binafsi ya kuzalisha umeme kuwa ni kazi mahususi inayofanywa na majeruhi wa vita ya ufisadi, ambao waliumizwa na matokeo ya kazi ya Kamati Teule ya Bunge ya kuchunguza mkataba wa Kampuni ya Richmond, ambayo yeye alikuwa mwenyekiti wake.


Hatua ya Mwakyembe kujibu tuhuma hizo, ilikuja baada ya magazeti mawili ya kila siku, (si Tanzania Daima) kuchapisha habari zinazomhusisha yeye na umiliki wa hisa 1,000,000 zenye thamani ya jumla ya sh bilioni 1.5 katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd.

Mbali ya habari hizo kuandikwa katika magazeti hayo mawili; moja la binafsi na jingine la serikali, nyaraka kadhaa zinazomhusisha Mwakyembe na kampuni hiyo, zimesambazwa katika mtandao wa intaneti.

Taarifa hizo pia zinamtaja Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya TANESCO, kuwa miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo binafsi ambayo wakati fulani Mwakyembe alipata kuwa mtendaji mkuu wake.

Taarifa hizo zinajaribu kujenga hoja zinazojaribu kumuondolea Mwakyembe uhalali wa kuendelea kudai kupambana na ufisadi ndani na nje ya Bunge ilhali yeye mwenyewe akionekana kuwa na ukwasi mkubwa unaotiliwa shaka.

Pia zinaonyesha kuwa, Mwakyembe licha ya kuwa na hisa nyingi katika kampuni hiyo, ameisaidia katika mambo mbalimbali ambayo hata hivyo hayakufafanuliwa, wakati akiwa katika wadhifa wa mtendaji mkuu.

Kwa mujibu wa uchunguzi wetu, lengo kuu la kusambaza nyaraka hizo ni kujaribu kumnyoshea kidole Mwakyembe na kujaribu kumuondolea uhalali wa kuendelea kupigania sekta ya nishati ilhali yeye mwenyewe akijua kuwa na maslahi.

Mwakyembe ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alisema kuwa katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd, hakuwezi kukamsababishia akaingia katika mgogoro wowote wa kimaslahi kutokana na ukweli kwamba, kampuni hiyo iliyosajiliwa kwa Wakala wa Usajili wa Makampuni (BRELA), bado ipo katika hatua ya awali ya mradi ambao bado haujaanza kuzalisha.

Alipotakiwa kueleza ni kwa nini wakati alipoteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyoichunguza Richmond kuanzia Oktoba mwaka juzi na kuwasilisha ripoti yake mwaka jana, hakueleza lolote kuhusu kuwa na kampuni ya kuzalisha umeme, Mwakyembe alisema asingeweza kufanya hivyo wakati mkakati wao wa kikampuni ukiwa katika hatua ya mradi tu.

‘‘Kwa mujibu wa sheria ya makampuni, majina yanakuwapo mpaka hapo kampuni itakapoanza ‘ku-take off’ (kuanza kazi). Sikuweza kuitaja kuwa ni sehemu ya makampuni yangu, kwa kuwa bado ilikuwa katika hatua ya mradi,” alisema Mwakyembe.

Mwanasiasa huyo alikwenda mbele zaidi na kuwaeleza wanahabari hao ambao miongoni mwao walionekana dhahiri kukabiliana naye kwa njia ya malumbano kuwa, hata wakati akiandikisha mali anazomiliki chini ya sheria ya viongozi kutangaza mali wanazomiliki, hakuitaja kampuni hiyo ya Power Pool kwa sababu hizo hizo za kutoanza kwake kazi.

Akifafanua tuhuma hizo dhidi yake, alimgeukia mbunge mwenzake wa CCM, Rostam Aziz na kumtuhumu kuwa nyuma ya habari zote mbaya zinazoandikwa dhidi yake.

Huku akilitaja jina la Rostam mara kadhaa, Mwakyembe alisema ni jambo ambalo haliingii akilini kwa mtu ambaye amechafuka kuamua kutumia maji taka kujisafisha.


WALA TUSINGEFIKA HAPA TULIPO IWAPO SHERIA INGEFUATA MKONDO WAKE.VINARA WALIOTUINGIZA MKENGE KWENYE UTAPELI WA RICHMOND HAWAJACHUKULIWA HATUA BAADA YA KUJIUZULU,NA SASA WAMEPATA JEURI YA KUTAKA KUTULIZA MARA YA PILI KWA KUTUUZIA MITAMBO MITUMBA ILEILE ILE YA RICHMOND a.k.a DOWANS.HUU MTINDO WA KULINDANA UTALIPELEKA TAIFA MAHALA PABAYA.

HOWEVER,LET IT BE KNOW TO MAFISADI AND THOSE WHO SHIELD THEM THAT IF THEY TURN OUR BELOVED COUNTRY INTO ANOTHER MADAGASCAR THEY TOO WOULDNT BE SAFE!

5 Mar 2009

SAKATA la ununuzi wa mitambo ya ufuaji umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited, jana lilimgusa spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta na kuamua kutoa tamko kali la kuitahadharisha serikali dhidi ya azma yake ya kutaka kuinunua mitambo hiyo yenye utata.

Spika Sitta pia ameonya kuwa mkasa wa kampuni tata ya Richmond Development (RDC) LLC uliotikisa kiasi cha kusababisha Edward Lowassa awajibike kwa kujizulu wadhifa wake wa waziri mkuu, lisifufuliwe upya kwa kutumia Dowans, ambayo ilirithishwa mkataba wa miaka miwili wa kufua umeme wa dharura.


Richmond ilishinda zabuni ya kufua umeme wa dharura kwa njia iliyojaa utata kabla ya matatizo ya usajili wake kuzua maswali mengi na kusababisha Dowans warithishwe mkataba huo mwaka 2006.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Sitta alieleza nafasi ya Bunge katika kuisimamia na kuishauri serikali katika utekelezaji wa majukumu yake, huku akitaka ushauri wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini wa kuizuia serikali isinunue mitambo hiyo uheshimiwe.

Sitta pia alisema Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma haikustahili kufuatwa katika kutaka ushauri kuhusu suala hilo kwa kuwa suala hilo lipo kwenye Kamati ya Nishati na Madini na kwamba kama kuna sababu mbadala, wasi ililazimika kuliwasilisha upya kwa kamati hiyo.

"Naitahadharisha serikali juu ya athari zinazoweza kujitokeza iwapo itaamua kuendelea na mchakato wa ununuzi wa mitambo ya Dowans kwa kupuuza ushauri uliotolewa na Kamati ya Nishati na Madini," alisema Spika Sitta.

Alisema: "Isisahaulike kwamba Dowans ni kampuni iliyopatikana kwa kurithishwa mradi na kampuni ya Richmond katika mazingira yenye utata ambao hadi leo ni kitendawili."

Spika Sitta alifafanua kuwa uhalali wa utaratibu wa Richmond kumkabidhi mradi Dowans ulitiliwa mashaka na kamati teule ya Bunge, na kuongeza kuwa Dowans na Richmond ni kama kitu kimoja.

"Dowans na Richmond ni mtu na binamu yake na si vigumu kukubali kuwa bado wao ni wabia hadi sasa: Pamoja na yote mkasa wa Richmond haufai kufufuliwaaa upya kupitia Dowans," alisisitiza Sitta.

Aliongeza kuwa kama kweli Tanesco na serikali inazo Dola 69 milioni za Kimarekani (sawa na Sh90 bilioni za Kitanzania) ambazo ni bei ya mtambo wa Dowans, ingezitumia fedha hizo kama sehemu ya malipo ya kununua mitambo mipya. Alisema Tanesco ingetafuta ushauri kutoka Mamlaka ya Ununuzi Serikalini (PPRA) ili taratibu za dharula zitumike kununua mitambo mipya kukabiliana na "dharula inayotabiriwa".

Sitta alihoji mantiki itakayotumiwa na Tanesco kutaka kununua mitambo ambayo inamilikiwa na kampuni ambayo imeishtaki kwenye Baraza la Usuluhishi ambalo makao yake makuu yako Paris, Ufaransa.

"Gharama za mitambo na gharama za kuikodi haviwezi kuepukwa kuwa ni sehemu ya shauri lililo Paris," anasema Sitta. "NI kwa mantiki ipi kesi baina yao iendelee na hapo hapo mdaiwa (Tanesco) anunue mitambo kutoka kwa mdai (Dowans.

"Tanzania ilikuwa ikilipa Dowans shilingi za Kitanzania milioni 152 kwa siku (Dola 120,000) sawa na Dola 42 milioni kwa mwaka).

"Pamoja na yote, mkasa wa Richmond haufai kufufuliwa upya kupitia Dowans. Tanesco/serikali waelekeze nguvu zao katika njia mbadala za kulipatia taifa umeme wa dharura, badala ya njia hii ya Dowans iliyojaa utata."

Kuhusu mvutano kati ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Mashirika ya Umma na ile ya Nishati na Madini, Spika Sitta amsema si sahihi kwa kamati yoyote ya Bunge isiyo ya sekta husika, kutoa maoni yake hadharani na kuishawishi jamii kwamba Bunge lina ushauri unaopingana kuhusu suala husika.

"Si sahihi kwa Kamati yoyote ya Bunge isiyo ya sekta kutoa maoni yake hadharani na kujenga taswira kwa umma kwamba, Bunge lina ushauri unaokinzana kuhusu suala lililo mbele yake. Kamati nyingine, haina budi kupitisha ushauri na maoni yake kwenye kamati ya kisekta," alisema Sitta.

Zitto Kabwe, ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, alikaririwa na vyombo vya habari akieleza msimamo wa kamati yake kuunga mkono Shirika la Umeme (Tanesco), kuinunua mitambo ya Dowans kwa maelezo kuwa hatua itasaidia kulinusuru taifa katika janga kubwa la kukosa umeme na kwamba sheria ya manunuzi si msahafu, hivyo inaweza kubadilishwa.

Lakini Kamati ya Nishati na Madini, ambayo mwenyekiti wake ni William Shelukindo, inapinga hatua hiyo ikieleza kuw ainakiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma, inayokataza serikali kununua vitu ambavyo tayari vimetumika.

Alisema ushauri kwa serikali kuhusu Tanesco kununua au kutonunua mitambo ya Dowans ulikwishatolewa kwa Wizara ya Nishati na Madini na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini Desemba 14 mwaka uliopita.

"Huo ndiyo ushauri rasmi na sahihi wa Bunge ninaoutambua. Kwa msingi huo hoja ya kuzikutanisha Kamati hizi mbili (ya Nishati na Madini na ya Hesabu za Mashirika ya Umma) ili kurejea uamuzi au maoni yaliyokwishatolewa na Kamati inayohusika, haina msingi," alisema Sitta.

Alisema mkondo rasmi wa ushauri kwa serikali uliokusudiwa kwenye Ibara ya 63 (2) ya katiba ikisomwa na pamoja na kanuni za Bunge za mwaka 2007 ni kupiti Bunge zima au kamati zake za kisekta kila kamati na sekta yake.

Wakati Spika Sitta akibainisha msimamo wake na wa Bunge, mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba ameunga mkono ununuzi wa mitambo hiyo huku akisema kauli ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa jana inaweza kukwamisha mchakato wa ununuzi wa mitambo hiyo.

Lipumba alisema katika mfumo wa utawala bora wakati kamati za bunge zinazohusika na mambo hayo na bodi za mashirika zipo, rais hapaswi kujiingiza mapema katika mijadala.

“Katika mfumo wa utawala bora ambao una kamati za bunge zinazohusika na sekta ya umeme na manunuzi, kwa rais kujiingiza kunaweza kuwa ni kikwazo cha mchakato mzima wa ununuzi wa mitambo,” alisema Profesa Lipumba.

Alifafanua kuwa, sheria ya manunuzi ya Serikali ina upungufu kwa kuwa inalazimisha ununuzi wa mitambo mipya, jambo ambalo haliwezekani kwa nchi zinazoendelea kama Tanzania.

“Ununuzi wa mitambo ya kibiashara katika sekta ya biashara huwezi kulazimisha ununuzi wa mitambo mipya hususan katika nchi zinazoendelea kama ya kwetu. Jambo la msingi ni kuangalia uwezo wa mitambo katika kufanya kazi na si kwamba ni mipya au mikongwe,” alifafanua Lipumba na kuongeza:

“Sheria yetu ya manunuzi ni nzuri na inafaa sana kwa kununua vitu vya huduma za serikali, kama magari na vifaa vingine.”

Aliitaka Tanesco kuwa wazi kwa kuwa ni wao waliosema mitambo hiyo hawaitaki hivyo kuamuwa kuvunja mkataba na Dowans iweje leo wanageuka na kusema mitambo hiyo ni mizuri na kuitaka serikali iinunuwe.

“Tanesco walituambia kuwa mitambo hiyo hawaitaki na walivunja mkataba na Dowans, sasa inakuaje leo wanageuka na kusema kwamba mitambo hiyo ni mizuri na inunuliwe kwa ajili ya kuzalishia umeme? Tunahitaji uwazi zaidi kutoka Tanesco,” alihoji Profesa Lipumba.

Naye Stephen Menad ambaye ni mshauri wa masuala ya nishati na mazingira, alisema hakuna kitu kipya kwenye mitambo hiyo ya Dowans hivyo isinunuliwe na badala yake itafutwe mipya ili kuondoa mvutano baina ya wananchi na serikali.

Mussa Hassan, mkazi wa jijini Dar es Salaam ambaye ni mfanyabiashara, alisema ni aibu kwa serikali kula matapishi na kwamba viongozi wasisahau yaliyotokea wakati mitambo ya Richmond ilipokuja na mwisho wake kuwaweka pabaya viongozi waliokuwa serikalini.

Anthony Chambi, ambaye ni mfanyabiashara katikati ya jiji la Dar es Salaam, alisema hataki kusikia kuhusu mitambo hiyo kwa kuwa tayari ilishaiabisha serikali. Alisema anasikia kuna kesi Ufaransa kuhusu mitambo hiyo kitu kinachomshangaza kwa nini serikali inataka kununua mitambo ambayo ina kesi.
CHANZO: Mwananchi
BIG UP,MHESHIMIWA SPIKA.
BINAFSI HADI MUDA HUU SIELEWI HAO WANAOTAKA MITAMBO YA DOWANS INUNULIWE WANA AJENDA GANI!NACHANGANYWA ZAIDI NAPOSIKIA WATU KAMA ZITTO KABWA NA PROFESA LIPUMBA NAO WAKIPIGA DEBE MITAMBO YA DOWANS INUNULIWE.HUU NI UNAFIKI WA MCHANA KWEUPE.WHY?BECAUSE KUNUNUA MITAMBO HIYO NI KUHALALALISHA UJAMBAZI WA DOWANS NA KAKA YAKE RICHMOND.HIVI INAINGIA AKILINI KWELI PALE TAPELI ANAPOKUUZIA MALI FEKI KISHA UKAMKALIA KOONI MPAKA AKAKIRI KUWA KWELI ALICHOKUUZIA NI FEKI,HALAFU UKAISHIA KUONGEZA FEDHA KUNUNUA MALI HIYO FEKI!?
I WOULD ONLY SUPPORT MATUMIZI YA MITAMBO YA DOWANS LAITI INGEKUWA IMETAIFISHWA (NA SIJUI KWANINI HADI MUDA HUU HAIJATAIFISHWA...WE MISS YOU BABA WA TAIFA).ETI AKINA KABWE WANASEMA TUWEKE MBELE UTAIFA KWANZA!UTAIFA KWANZA KWA MANUFAA YA AKINA RICHMOND?HAWA WAMEINGIZWA MKENGE NA VITISHO VYA TANESCO KUWA ETI NCHI IKO HATARINI KUINGIA KIZANI!YALEYALE YA RICHMOND!
WIZI MTUPU!

4 Nov 2008

Nadhani unakumbuka wasiwasi nilioonyesha katika POST HII.Inaelekea suspicion yangu haiko mbali na ukweli.Zaidi,soma habari hii:
Serikali imesema itakuwa tayari kununua mitambo ya Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd endapo Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), litaishauri kufanya hivyo. Dowans Tanzania Ltd jana ilitangaza rasmi zabuni ya kuuza mitambo yake ya kuzalisha umeme ikiwa ni miezi mitatu baada ya serikali kukatisha mkataba wake na Tanesco. 

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliiambia HabariLeo jana kuwa kimsingi serikali haitakuwa na tatizo na mitambo hiyo endapo wataalamu wa Tanesco watashauri hivyo. “Tanesco ndiyo wataalamu wetu, tutawauliza wakisema tununue tutanunua, lakini kwa kufuata taratibu na sheria za manunuzi ya mitambo hiyo,” aliongeza Ngeleja. 

Endapo serikali au Tanesco watanunua mitambo hiyo, itasaidia kupunguza uwezekano wa kutokea mgawo wa umeme mara mitambo mingine ikipata hitilafu. Mwezi uliopita, Tanesco ililazimika kutangaza mgawo wa umeme baada ya mashine moja ya Kampuni ya Songas yenye uwezo wa kuzalisha megawati 40 kuharibika. 

Hata hivyo, Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud alisema jana kuwa shirika hilo halijaamua kama watanunua au la. Alisema watatoa taarifa uamuzi ukifikiwa. Dowans Tanzania Limited ilirithi mkataba wa kuiuzia umeme wa megawati 120 Tanesco kutoka kwa Kampuni ya Richmond Development LLC ambayo baadaye iligundulika kuwa ni kampuni hewa. 

Serikali ilifikia uamuzi wa kusitisha mkataba huo Agosti mosi mwaka huu baada ya kuridhika kuwa mkataba huo haukuwa halali wala haukuwa na nguvu kisheria. Tangazo lililotolewa jana na kampuni hiyo lilimtaka mtu yeyote, taasisi, kampuni itakayotaka kununua mitambo hiyo ipange bei inayoona inaweza kutoa kuipata mitambo hiyo.


CHANZO: HabariLeo

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.