5 May 2011


Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida maridhawa la Raia Mwema inafanya uchambuzi linganifu kuhusu,kwa upande mmoja,tuhuma zilizomwandama Rais Obama kuwa sio raia wa Marekani,na hatimaye uamuzi wake kutoa cheti chake cha kuzaliwa,na kwa upande mwingine ni tuhuma za ufisadi zinazomwandama Rais Kikwete,na jinsi kutochukua hatua kadhaa kunazifanya tuhuma hizo kuwa na uzito.

Kadhalika,makala hiyo inawagusa jamaa zangu wa Usalama wa Taifa,kwa kuangalia wnavyofanikisha upatikanaji wa taarifa zinazowahusu wanasiasa wa CCM wanaotajwa kama magamba.Lakini ninaibua maswali kadhaa huku nikiwatahadharisha kuhusu uwezekano wa kuzua skandali kama ile ya Watergate ya nchini Marekani ambapo Rais Nixon,pamoja na mambo mengine alitumia nafasi yake kuamrisha ukusanyaji wa taarifa za kiintelijensia dhidi ya wapinzani wake wa kisiasa.

Pamoja na makala hiyo unayowaza kuisoma kwa KUBONYEZA HAPA,jarida hili la Raia Mwema limesheheni habari na chambuzi za kiwango cha juu kabisa. 


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.