11 May 2011

Mwangalie huyo kijana (well,may be mzee.You can't tell the difference,can you?) wa kwanza kulia.Sidhani kama anayoongea Nape yanamwingia akilini.Na wa tatu kutoka kulia,mwanamama aliyeshika tama,ni kama aliamrishwa kuhudhuria mkutano huo.Sio kashfa au dharau,lakini ni wazi kuwa sura za wahudhuriaji zinatia huzuni.Zimejaa mawazo,hazionyeshi matumaini....yet wamehudhuria.Ukiwaangalia akinamama hao hapo chini,japo kuna kijitabasabu cha kujipa matumaini,lakini hizo flana za njano na khanga zimeficha mengi...ngozi zao zinaonyesha waziwazi namna maisha yao ya kila siku yalivyo magumu katika harakati za kupeleka mkono kinywani.


Lakini bado wanahudhuria mikutano ya porojo.Wanajua wanadanganywa,kwani huhitaji kwenda shule kujua una njaa ilhali anayepiga porojo ameshiba.Mng'aro tu wa ngozi ya Nape as opposed to msinyao wa ngozi za wasikilizaji wake unaelezea mengi.Wanaambiwa kuwa CCM imejivua magamba,sasa itaendeshwa kisayansi,sijui imekuwa mpya...lakini hawaambiwi ni kwa namna gani ugumu wa maisha ya walalahoi hao utapungua...ni lini nao watapata fursa ya kunawiri kama akina Nape....

Lakini bado wanahudhuria mikutano hii ya porojo.Ndio maana katika kichwa cha habari nimehoji: WAMEROGWA?

Picha kwa hisani ya Jamii Forums

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.