14 Jan 2012


Habari za kusikitisha zilizopatikana kwenye mtandao wa jamii wa Twitter na ukumbi wa mijadala ya mtandaoni wa Jamii Forums zinaeleza kuwa Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chadema,Regia Mtema,amefariki kwa ajali ya gari iliyotokea daraja la mto Ruvu.

Licha ya kifo cha Regia kuwa pigo na pengo kubwa kwa Chadema pia ni msiba mkubwa kwa sie wazawa wa wilaya ya Kilombero,mahali alipozaliwa marehemu na ambapo alipatumikia kwa nguvu zake zote.

Tutawaletea taarifa zaidi kadri zinavyopatikana.

Bwana Ametoa Bwana Ametwaa,Jina lake lihimidiwe Milele.Amen.





0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.