Showing posts with label AGENDA 21. Show all posts
Showing posts with label AGENDA 21. Show all posts

5 Mar 2008

Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inatoa lawama kwa wale ambao baada ya kutajwa kwenye Ripoti ya "Tume ya Mwakyembe" wamekuja na ngonjera za ukabila,eti kuna mpango wa ethnic cleaning dhidi ya kabila flani.Pia makala hiyo inatoa changamoto kwa Bunge kutumia kasi ile ile ya "mwewe" (kama iliyomshukia Zitto Kabwe) kuwashukia wale wote wanaoikejeli Ripoti hiyo ilhali hilo ni kosa kisheria.Kadhalika,wito unatolewa katika makala hiyo kuharakisha uchukuzi wa hatua pindi yanapoibuka mambo yanayohitaji actions dhidi ya wahusika.Sambamba na hilo ni changamoto kwa wansheria "kununua kesi" dhidi ya mafisadi na vikundi vya kijamii kutoishia kulalamika tu bali kuchukua hatua dhidi ya mafisadi.Makala inamalizika kwa wito kwa CCM kutodhani taarifa kwamba kuna kundi la "Agenda 21" ni hadithi za kuvuta muda tu.Onyo la makala kwa chama hicho ni kwamba wakizembea,basi itakuwa kilio pindi maji yatakapozidi unga usiku wa manane wakati maduka yote yashafungwa.Pamoja na habari za makala nyingine zilizofanyiwa utafiti wa kina,soma makala yangu hiyo kwa KUBONYEZA HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.