Showing posts with label DOKTA WILBROAD SLAA. Show all posts
Showing posts with label DOKTA WILBROAD SLAA. Show all posts

23 Sept 2010



Ukichanganya "nyomi" kama hilo la kampeni za Dokta Slaa mjini Moshi na matokeo "yaliyominywa" ya Synovate,ni dhahiri Kikwete na mafisadi wako tumbo joto na sasa wanahangaika namna ya kuchakachua matokeo ya Uchaguzi Mkuu ujao.Washindwe na walegee.HATUDANGANYIKI!

Slaa anasa waraka mzito
• NI ULE WA SERIKALI KUIMALIZA CHADEMA
na Janet Josiah na Charles Ndagula, Moshi
MGOMBEA urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ametangaza kunasa waraka wa siri ulioandikwa siku nne zilizopita, ambao pamoja na mambo mengine unawaagiza watendaji wakuu wa serikali kufanya kila wawezalo kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinashinda uchaguzi.
Dk. Slaa mwanasiasa mwenye rekodi ya kunasa taarifa mbalimbali nyeti za serikali, alitangaza kuhusu kuuona waraka huo wakati akihutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza kumsikiliza katika Manispaa ya Moshi.
Akizungumzia suala hilo, Dk. Slaa alimtahadharisha mgombea wa urais wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kuhakikisha anachukua hatua ya kuvidhibiti vyombo vyake vya usalama ili visimwage damu isiyo na hatia kwa sababu tu ya kutaka kushinda urais kwa gharama zozote zile.
Dk. Slaa aliyekuwa akihutubia katika Uwanja wa Mashujaa mjini hapa, alisema dalili zimeanza kujitokeza katika mikoa mbalimbali aliyopita, ambako kumekuwapo na matukio ya watu kuonewa na viongozi wa serikali.
Akifafanua, alisema waraka huo unaokwenda kwa vyombo vya usalama, wakiwemo wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya, unawataka wafanye lolote ili kuhakikisha CCM inashinda.
“Ninao waraka ulioandikwa Septemba 19 (Jumapili iliyopita), mwaka huu na leo ni siku ya tatu, unakamilishwa na kusambazwa kwa viongozi hao kuwakumbusha kuwa lazima wahakikishe CCM inashinda, sikuupata hapa hapa, ila tayari umesambazwa nchi nzima,” alisema Dk. Slaa.
Dk. Slaa ambaye ni Katibu Mkuu wa chama hicho, kwa nafasi yake anatoa tamko hilo ili kumtahadharisha Rais Kikwete kuacha mara moja hujuma hiyo, na kuwa dalili zinaonyesha kwamba Watanzania wameamka na wanahitaji mabadiliko.
Alisema pamoja na kupata hujuma hizo, chama chake kimejipanga vyema kukabiliana na mashambulizi ya CCM na serikali yake, kwa kuweka mfumo imara wa ulinzi kwa viongozi wao na wapiga kura wao.
Alivitaka vyombo vya usalama kuacha kuhujumu msafara wake pamoja na watendaji wake, ambao wanatangulia katika vituo ambavyo anafanyia mikutano ya kampeni, kwa kuwa leo serikali ni ya CCM na kesho serikali itakuwa ya CHADEMA.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo baada ya kupata taarifa za polisi kutaka kuwakamata vijana wa chama hicho, ambao wanapima viwanja vya kufanyia mikutano yao, ambavyo helikopta itaweza kutua kwa urahisi (GPS).
Akizungumza na Tanzania Daima, mmoja wa vijana hao, Gwakisa Gwakisa, alikiri kutaka kukamatwa na polisi hao na kudai kuwa alipowaona alifungua mlango wa gari na kukimbia pamoja na wenzake wachache na kuacha gari la chama hicho, ambalo lilichukuliwa na polisi.
Hata hivyo, Tanzania Daima ilipomuuliza Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC) wa Kilimanjaro, Lucas Ng’hoboko, alikiri kuwa wanalishikilia gari la CHADEMA na kwamba wanamsaka mpima ramani ili wamkamate.
“Bado tunamtafuta mpima ramani wa chama hicho ili baadaye tutoe taarifa kwenu nyinyi waandishi wa habari,” alisema RPC Ng’hoboko.
Akizungumzia tukio hilo, Dk. Slaa amewataka polisi kuwaacha Watanzania wanaotimiza mapenzi yao bila kuwabughudhi na kwamba kero hizo mwisho ni Oktoba 31.

Akiwahutubia wananchi hao mara baada ya kutoa tamko la chama chake, Dk. Slaa aliwaomba wawachague wagombea wa chama chao ili waweze kufufua viwanda ambavyo vimekufa kutokana na sera mbovu za CCM.
“Ndugu zangu wana Moshi, ichagueni CHADEMA kwa kuwa CCM imeshindwa kuwaletea maendeleo, kwa kushindwa kufufua viwanda vyenu kama vile kiwanda cha ngozi, magunia, vyuma na viwanda vingine,” alisema Dk. Slaa.
Mapema akimnadi mgombea huyo, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, aliwataka Watanzania kuufanya mwaka huu kuwa wa maamuzi na si wa utani, kwa kuwachagua wagombea makini wa chama hicho.
“Mwaka 2010 hatudanganyiki ndugu zangu wa Moshi…kwa kuwa tutaingia Ikulu na watu makini kama Dk. Slaa, kwa kuwa na nyie ni makini, hivyo mtatuchagua.
“Kwa kuwa CCM ilitumia woga wenu Watanzania kuwatawala na kuwanyanyasa, lakini sasa Watanzania mmeondokana na woga…lakini imani kubwa ipo kwenu wana Moshi, kwa kuwa mmechangia mafanikio ya wana CHADEMA,” alisema Mbowe.
Mkutano huo ulitanguliwa na maandamano makubwa yaliyoanzia katika ofisi za wilaya za chama hicho zilizopo katika Kata ya Majengo na kupita katika barabara za Ghala na Mawenzi, maarufu kama Double Road, Florida hadi katika viwanja vya Mashujaa, huku waandamanaji wakisindikizwa na helikopta iliyokuwa ikiyahamasisha kwa saa nzima.
CHANZO: Tanzania Daima
PICHA KWA HISANI YA Jamii Forums


NAMNA MWAFAKA YA KUMWADHIBU KIKWETE NA MAFISADI NI KWA KUMPIGIA KURA DOKTA WILBROAD SLAA SIKU YA UCHAGUZI HAPO TAREHE 31 OKTOBA.KIKWETE NA CCM YAKE WATAJARIBU KUCHAKACHUA MATOKEO LAKINI HILO LITAWEZEKANA TU KAMA TOFAUTI YA KURA ZA DKT SLAA NA KIKWETE ITAKUWA NDOGO.LA MUHIMU NI KUMPATIA KURA NYINGI MKOMBOZI WETU DOKTA SLAA ILI KIKWETE NA MAFISADI WASHINDWE KUBADILI MATOKEO.KAMA KENYA WALIWEZA KUMG'OA MOI NA KANU BASI HATA SISI PIA TUNAWEZA KUING'OA CCM.


TIMIZA WAJIBU WAKO

13 Sept 2010


Hii ndiyo Bunda ya Dk. Slaa

Leo tuko Bunda. Acha picha hizi ziseme zenyewe. Maelezo mengine
baadaye. Itoshe tu kusema kwamba miongoni mwa maelfu ya wana Bunda waliofurika kumsikiliza Dk. Slaa katika viwanja vya Sabasaba ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Francis Isack. Alikaa jukwaa moja na Dk. Slaa, naye alimsifu kwa ukomavu wa kisiasa, lakini akamuonya kwamba kama alikuwa amekwenda pale kwa nia tofauti, atazame umma, apime nguvu yake na apeleke taarifa za kile anachosikia na kuona. Alimsimamisha DC huyo akawasalimia wananchi kwa kunyosha mikono juu.

Picha na Habari kwa Hisani ya NGURUMO

5 Sept 2010

Kuna msemo wa Kiingereza usemao "unchallenged,a lie often assumes a status of truth",yaani uongo usipokabiliwa unaweza kupata hadhi ya ukweli.Msemo huu unaweza kuwa na umuhimu wa kipekee kwa mgombea wa tiketi ya urais kupitia Chadema,Dokta Wilbroad Slaa.Tangu atangazwe kuwa mgombea wa chama hicho,kumekuwa na mashambuli lukuki yanayoelekezwa kwake katika jitihada za kuifanya jamii imwone kuwa mchafu na asiyefaa kumrithi Jakaya Kikwete,mgombea kwa tiketi ya chama tawala CCM.

Ni dhahiri kuwa wanaoeneza sumu hiyo dhidi ya Dkt Slaa wanafanya hivyo kwa malengo makuu mawili.Kwanza,kama nilivyobainisha hapo juu,ni kumfanya aonekane hafai kuwa rais wa Tanzania.Aonekane hafai,kisha akose kura za kutosha kumwingiza Ikulu,na mafisadi waendelee kuvuna wasichopanda katika nchi yetu iliyogeuzwa shamba la bibi.

Lakini la pili ni kupoteza malengo au kwa ufasaha ku-divert attention.Yaani wanachotaka ni Dkt Slaa na Chadema waanze kuhangaika kujibu shutuma,jambo ambalo litawapunguzia muda na focus ya kampeni.Yaani badala ya mgombea huyo kuwashawishi Watanzania atawafanyia nini,mafisadi wanataka aanze jukumu la kujitetea kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwake.

Wapo wanaoshauri kuwa dawa ya kudili na tuhuma ni kuzipuuza.Kuna wakati mkakati huo ni mzuri lakini hilo linawezekana katika aina flani ya jamii.Katika jamii yetu ambapo bado asilimia kubwa ya watu wananyimwa uhuru wa kujua ukweli na kuchanganua mambo,uongo usiokanushwa unaweza kabisa kuchukua nafasi ya ukweli.Na ukidhani nachoandika hapa ni hisia zangu tu basi rejea zengwe aliloundiwa Dokta Salim Ahmed Salim alipotangaza dhamira yake ya kugombea urais mwaka 2005.Kikwete na wanamtandao wenzake walimwaga sumu kubwa dhidi ya Dkt Salim hadi wakafanikiwa kumdhibiti.Jitihada zake za kujisafisha hazikuweza kufua dafu kwa character assassination strategy ya wanamtandao.

Ikumbukwe kuwa tunaishi katika jamii iliyolazimika kutegemea umbea na tetesi kubashiri ukweli.Haya ni baadhi ya matokeo ya mfumo dhalimu wa chama kimoja ambapo mambo pekee yaliyopaswa kufahamika kwa umma ni yale yaliyoonekana mazuri kwa watawala.

Kadhalika,kinachotokea kwa Dokta Slaa ni sehemu ya uchafu unaoambatana na fani ya siasa (politics is a dirty game).Huko Marekani,baada ya Barack Obama kuonekana ana nguvu za kumpeleka Ikulu,zilianza kampeni chafu kuhusu imani yake ya dini ikidaiwa alikuwa Muislam (kana kwamba Uislam ni sawa na uhaini nchini humo).Baadaye wakamzushia kuwa sio raia wa Marekani.Timu ya Obama haikukaa kimya bali ilipambana kwa nguvu dhidi ya kampeni hizo chafu na hatimaye Obama akafanikiwa kuingia Ikulu.

Chadema na Dokta Slaa wanaweza kuamua kuwapuuza wanaoeneza sumu kali dhidi yao.Lakini kwa namna hali ilivyo ambapo vyombo vya serikali (vinavyoendeshwa kwa fedha za walipa kodi) kama gazeti la Habari Leo vinapojiunga na kampeni hizo za siasa za maji taka basi ni muhimu kukabiliana nao mapema.

Na kwa kuanzia,nadhani kuna umuhimu wa kulichukulia hatua gazeti la Habari Leo hususan pale lilipoandika "Dokta Slaa padri msomi".Sentensi hiyo ilikuwa na lengo la kumkosesha mgombea huyo kura za wasio Wakatoliki.Ni dhahiri sentensi hiyo ililenga kuendeleza kashfa kuwa Dokta Slaa ni kiongozi wa dini na anataka kuingia Ikulu kuwatumikia Wakatoliki/Wakristo na sio Watanzania wote kwa ujumla.Kulipeleka gazeti hilo kwa Baraza la Habari ni kupoteza muda kwa vile sana sana wataishia kupewa onyo tu.Wanachostahili sio onyo bali adhabu kali ya kuwakumbusha kuwa wanatumia vibaya fedha za walipa kodi kwa maslahi ya watu binafsi.Ni mafisadi kama wale wa Kagoda au Richmond.

Sijui sheri za Tanzania zinasemaje kuhusu super injunctions zinazokataza kuzungumzia maisha ya mtu binafsi.Hapa Uingereza baadhi ya watu maarufu wamekuwa wakizitumia taratibu hizo za kisheria kuwabana vimbelembele wanaoishi kwa kuchokonoa maisha ya wenzao.Naamini Chadema wana wanasheria mahiri wanaoweza kuangalia namna ya kukabiliana na wazushi hawa wanaofadhiliwa na mafisadi.

Blogu hii inatoa wito kwa Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla kutokalia kimya uhuni huu ambao pasipo kudhibitiwa unaweza kabisa kuathiri matokeo ya uchaguzi.Hatuhitaji kujiuliza kwanini wamwandame Dkt Slaa pekee na sio wagombea wengine kwani rekodi yake dhidi ya mafisadi ni siri iliyo wazi,na hofu kubwa ya wanaoeneza sumu dhidi yake ni kuwa akiingia Ikulu itawalazimu watafute mahala pa kujificha.


Inaudhi na kukasirisha kuona gazeti la serikali,Habari Leo,likijipachika jukumu la kumuua kisiasa mgombea wa Chadema Dokta Wilbroad Slaa kama ambavyo imekuwa ikifanywa na magazeti ya Habari Corporation na Changamoto,na mengineyo yanayofadhiliwa na mafisadi.

Gazeti hilo limeandika kwa kirefu kuhusu anayedaiwa kuwa mume wa mwenza wa sasa wa Dkt Slaa,Josephine Mushumbusi.Ungetegemea gazeti hilo linaloendeshwa kwa fedha za walipa kodi wa Kitanzania pasipo kujali itikadi zao za kisiasa,lingetafakari kwa makini madhara ya habari hiyo.Wanajua sana wanachofanya,na yayumkinika kuamini kuwa serikali inayoongozwa na mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,imeridhia uchapishaji wa habari za aina hiyo.

Kuna msemo wa busara unaoasa "WANAOISHI KWENYE NYUMBA ZA VIOO WASIRUSHE MAWE".Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una wasifu wenye mawaa ya aina moja au nyingine then si wazo jema kuwachafua watu wengine.Wengi wetu tunafahamu "ishu binafsi" za viongozi wa CCM ikiwa ni pamoja na Kikwete mwenyewe.Hazizungumzwi hadharani kwa kuwatunzia heshima viongozi hao lakini inaelekea katika kutapatapa kwao baada ya kugundua hawamwezi Dokta Slaa kwa hoja,wameamua kuhamia kwenye character assassination.

Majukwaani,Kikwete na CCM yake wanajifanya kuhubiri umuhimu wa kampeni za kistaarabu lakini pembeni wanaruhusu raslimali za umma zitumike kumchafua Dokta Slaa.Kikwete alichukua hatua za haraka pale mtandao maarufu wa Ze Utamu ulipochapisha picha zinazomhusu lakini anaruhusu gazeti la serikali litumike kumwandama Dkt Slaa.

Na kwa kuonyesha unazi,kuna mahala katika habari hiyo ambapo pasi aibu wameandika (nanukuu) "Na wakati Mahimbo akiwa njia panda akishindwa kujua hatima ya ndoa yake, Dk. Slaa, Padri msomi `amelitangazia’ taifa mbele ya mikutano ya kampeni ya chama chake cha Chadema kuwa Josephine ndiye mke wake mtarajiwa..." 

Hivi Mhariri wa Habari Leo hafahamu kuwa Dkt Slaa sio Padri bali aliwahi kushika nafasi hiyo na kuiacha?

Blogu hii inamshauri Kikwete akemee mkakati huu mufilisi wa character assassination.Wengi wanafahamu kwa undani maisha ya Kikwete tangu akiwa Waziri,na wanajua vema maisha yake binafsi ndani na nje ya nchi.Asijivunie vyombo vya dola kumlinda pindi kibao kitapogeuzwa upande wake.Ni bora Dokta Slaa anayetangaza hadharani kuhusu uhusiano wake na Josephine kuliko kashfa lukuki zinazohifadhiwa kuhusu viongozi wa CCM kwa vile tu tunawaheshimu na tuna mambo muhimu zaidi ya kuzungumzia kuliko maisha binafsi ya viongozi wetu.

I repeat: Those who live in glass houses shouldn't throw stones!!!



4 Sept 2010

Dr_Slaa

TAFADHALI UKISHASOMA SAMBAZA KWA MWENZIO.BONYEZA HAPO JUU KULIA PALIPOANDIKWA "<>SHARE" KISHA CHAGUA NJIA YA KUSAMBAZA.

3 Sept 2010

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.