Showing posts with label FOOTBALL IN TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label FOOTBALL IN TANZANIA. Show all posts

11 May 2011




Africa here we come! Birmingham set to tour Tanzania ahead of new season

By Sportsmail Reporter

Last updated at 11:11 AM on 11th May 2011

Birmingham are planning a pre-season trip to Tanzania in July.

The details have not yet been finalised but first-team coach Andy Watson and chief medical officer Ian McGuinness have travelled to Africa to inspect facilities

Birmingham are expected to undertake a four-day trip, with Tanzanian top-flight sides Simba or Yanga, or possibly both, providing the opposition at the National Stadium in Dar-es-Salaam.

Watson told the club's website: 'The people of Tanzania that we have met have been very hospitable and kind, and from what we've seen of the country so far it looks an amazing place.
'We have been made aware of just how much the Tanzanian people love their football - especially the Barclays Premier League - and when everything is fully in place we look forward to coming back in July and playing.'

SOURCE: The Daily Mail

2 Jun 2010

Kwa mujibu wa imani zetu za Kiswahili,aliyekuroga akifariki basi uwezekano wa kupona nao unakuwa kama umefariki.Na msemo huu unaonekana kurandana na hali halisi ya baadhi ya matendo yetu viumbe tunaojulikana kama Watanzania.Nafahamu kuwa si wote "tuliorogwa" lakini hiyo si sababu ya "kutowatolea macho" wenzetu "waliorogwa kisha aliyewaroga akafariki".

Mwishoni mwa wiki hii,timu yetu ya taifa inakabiliwa na mpambano muhimu dhidi ya timu ya taifa ya Rwanda katika kusaka nafasi ya kushiriki kwenye michuano ya CHAN.Taifa Stars inatarajiwa kucheza siku ya Jumapili kisha Jumatatu wanatarajiwa kuingia tena uwanjani kupambana na timu ya Taifa ya Brazil katika pambano lililonunuliwa kwa mamilioni ya dola na chama chetu cha soka.

Na kwa takriban wiki nzima sasa,uongozi wa FA umekuwa bize zaidi na maandalizi ya pambano hilo walilonunua kuliko kuelekeza akili zao kwa mpambano dhidi ya Rwanda.Japo natambua kuwa kila mpenzi wa soka duniani angependa kuiona Brazil ikicheza uwanjani lakini sio kwa kununua mechi ya mamilioni ya fedha ambazo hakuna uhakika kama zitarudi.FA hawajaweka bayana gharama za kununua mechi hiyo lakini taarifa zinasema wamelipa dola za kimarekani milioni mbili unusu  (zaidi ya shilingi bilioni 3 unusu).Na hiyo ni ada (fee) tu lakini kuna uwezekano wa kiwango hicho kuwa kikubwa zaidi tukichanganya na gharama za kumudu ziara hiyo.

Kuna hoja kuwa ziara hiyo itasaidia kutangaza utalii.Well,lakini tuwe wakweli,yaani kutangaza utalii kwa dakika tisini kwa gharama ya shilingi bilioni tatu!?Na kama tujuavyo tatizo sugu la wizi wa mapato kuanzia TRA hadi kwa watendaji ngazi ya kata,si ajabu muda huu mafisadi wameshapiga mahesabu ya pasenti ngapi watakwiba kwenye chochote kitakachpatikana kwenye mechi hiyo.

Na kuna hoja ya rankings za FIFA.Hivi mechi moja ya kununua kwa mabilioni itatupandisha kwa kiwango gani ukilinganisha na menchi dhidi ya Rwanda ambayo kama "tukikaza misuli" na kufanikiwa kucheza CHAN tutapata nafasi kubwa zaidi ya kupandisha ranking yetu huko FIFA?

Ukitaka kufahamu namna ubabaishaji na ufisadi unavyozidi kutafuna mfumo wa jamii yetu subiri mechi iishe kisha vianze visingizio vya namna FA walivyoshindwa kufikia lengo la mapato.Binafsi nisingekuwa na tatizo laiti FA wangeafikiana na wenzao wa Brazil kisha kuuza tiketi kabla ya mechi na hivyo kufahamu faida au hasara itakayopatikana.Lakini kwa hali yasasa ni sawa na kucheza bahati nasibu.Na si ajabu visingizio vimeshaandaliwa as to kwanini "mechi hiyo haikuweza kurejesha faida iliyotarajiwa".

Ndio maana nashawishika kusema kuwa inawezekana ALIYETUROGA KESHAFARIKI.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.